Rushwa Imekithiri Baraza la Ardhi na Nyumba Arusha

Bukene

Member
May 27, 2016
59
30
Licha ya kuwa Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Jemedari Rais Mhe. John Magufuli kuwa katika mstari wa mbele kupiga vita rushwa, lakini katika hali ya kusikitisha vitendo vya rushwa vimekithiri Baraza la Ardhi na Nyumba Arusha.

Wengi wa wanaohitaji huduma kutoka kwa waheshimiwa Wenyeviti na Makarani wa baraza hilo wamekumbana na matatizo ya kuwekwa katika mazingira ya kulazimishwa kutoa rushwa ili kupata huduma wanayohitaji kutoka kwa serikali yao. Watendaji wa baraza hili wameweka mbele rushwa kama vile hawalipwi mishahara.

Hali ya kutakwa kutoa rushwa iko wazi kiasi kwamba TAKUKURU ikitaka kuwakamata haitachukua uchunguzi wa kina.

Serikali ya awamu ya Tano inafanya kazi nzuri, lakini kuna baadhi ya watendaji wachache kama hawa wa Baraza la Ardhi na Nyumba Arusha wanaotia doa kazi nzuri anayofanya Mheshimiwa Rais John Magufuli na serikali yake.

Vyombo vinavyohusika vinaombwa kufuatilia na kufyekelea mbali wote (kwa sasa majina yamehifadhiwa kwa muda) wanaotia doa kazi nzuri ya Mhe Rais magufuli na Serikali ya awamu ya tano.
 
Wewe ni vipi, mbona unaficha wala rushwa?

Kuna Mwenyekiti anayeitwa Mdachi na Karani anayeitwa Kachenje ni wala rushwa mashuhuri pale Baraza la Ardhi na Nyumba - Arusha.

Mdachi alipata shida ya kupewa mkataba kwa miezi kadhaa, baada ya kupewa mkataba sasa anachukua rushwa kama njia ya kufidia mapengo aliyopata alipokuwa nje ya ofisi.

Kachenje anatumia uzoefu wake wa muda mrefu katika ofisi hiyo na sasa anakula rushwa mchana kweupe. Amekuwa na jeuri na kujibu vibaya wanaotaka huduma katika ofisi ile kama njia ya kutaka kupewa rushwa.

Baraza la Ardhi na Nyumba - Arusha ni kama halina uongozi kwa sababu kila mmoja pale anajifanyia kazi kama anavyotaka.

Ni wakati muafaka sasa kwa Mhe Lukuvi na Mhe Angelina Mabula kufuatilia na kuchukua hatua zinazostahili kwa watendaji hawa wala rushwa walio chini ya Wizara yao na kuharibu taswira nzuri ya Serikali ya awamu ya Tano.
 
Uzi wako hautapata wachangiaji kisa tu umemsifu namba one
Tuache unafiki, namba one anapiga kazi. Jirani zetu walikuwa wanatudharau sana zamani lakini sasa wameanza kutuheshimu.

Nikirudi kwenye hoja ya msingi kuna haja ya vyombo vya uchunguzi kufanyia kazi tuhuma hizi maana watakao kuwa wana athirika na rushwa inayotajwa ni wananchi na wanyonge wasiojua nini cha kufanya.

RUSHWA NI ADUI WA HAKI, haipendezi sisi mawakili tuendeshwe na makarani wa Baraza kama magari mabovu au tushinde kesi kwa sababu tu tumempa mheshimiwa Mwenyekiti Rushwa au Tushindwe kesi tu kwa sababu mheshimiwa Mwenyekiti hakupewa rushwa.
 
Wewe ni vipi, mbona unaficha wala rushwa?

Kuna Mwenyekiti anayeitwa Mdachi na Karani anayeitwa Kachenje ni wala rushwa mashuhuri pale Baraza la Ardhi na Nyumba - Arusha.

Mdachi alipata shida ya kupewa mkataba kwa miezi kadhaa, baada ya kupewa mkataba sasa anachukua rushwa kama njia ya kufidia mapengo aliyopata alipokuwa nje ya ofisi.

Kachenje anatumia uzoefu wake wa muda mrefu katika ofisi hiyo na sasa anakula rushwa mchana kweupe. Amekuwa na jeuri na kujibu vibaya wanaotaka huduma katika ofisi ile kama njia ya kutaka kupewa rushwa.

Baraza la Ardhi na Nyumba - Arusha ni kama halina uongozi kwa sababu kila mmoja pale anajifanyia kazi kama anavyotaka.

Ni wakati muafaka sasa kwa Mhe Lukuvi na Mhe Angelina Mabula kufuatilia na kuchukua hatua zinazostahili kwa watendaji hawa wala rushwa walio chini ya Wizara yao na kuharibu taswira nzuri ya Serikali ya awamu ya Tano.
Matendo yao mabaya yanaonekana, wasifikiri wamejificha sana.
 
Back
Top Bottom