Ruge wa Clouds yuko live kumjibu Jide

Inaonekana unajua mengi kuhusu hz bifu ........... waonaje ukitiririka km gt wa jf!?
Topic ambazo watu wametiririka zipo tele hapa JF. We nenda pale kwenye search, tafuta jina la Ruge Mutahaba. Utakuta mada nyingi sana zinazomhusu, hasa ile ya bifu lake na Sugu. Watu wamemwagika mnoooooo! Almost kila kitu kipo pale
Mkuu majibu yake hayakutii kiu ya watu wengi maana kuna waraka alitoa JD kuwa akifa asiguswe na watu wa Clouds, na issue ya OSATA...kuhusu mmoja wa wafanyikazi wa Clouds kuwa na share na hii kampuni ya usambazaji na promo...angejibu haya ningekuwa upande wake..
Sure.
Ruge si mweledi wa kiasi hicho, hawezi kujibu hoja kwa mpangilio kama inavyopaswa. Ungesoma mada ya ugomvi wake na Sugu ungejua huyu juha ni empty upstairs.

Bas huu ugomvi ukiendelea nadhan uhusiano wa Jide na G nao upo hatarini sana, mana mengi yatasemwa na sidhani kama Gadner atavumilia yote.

Unadhani hayo yanayosemwa hayajulikani kwa Gardner? Anayajua yote, ndio sababu aliacha kazi pale sehemu. Pale paone vilevile
 
Habari wanaJf,
Nimebahatika kusikia alichoongea Boss Ruge kama wanavyomuita wafanyakazi wa clouds Fm, eti leo hakuna kupiga bongo flava kwenye redio yao.Swali langu hii kama ni redio ya watu hizo bongo flava ambazo amesema zisipigwe na kwa ajili ya wanyama au viumbe wa sayari nyingine.Angefanya la maana asema kabisa kuanzia leo redio yao haitapiga Bongo fleva au imekua ni redio ya gospel hapo ningemkubali,but the way amesema ni kwa siku ya leo,tena kwa kuamrisha kabisa,"nimesema leo hakuna kupiga bongo fleva mpaka saa sita usiku" mi sielewi kwa kweli ,anafanya hivyo kumkomoa nani.Lady Jay dee au waskilizaji wao.Eti redio ya Watu.ama kweli kuwa mkurugenzi sio tu jina,hata kichwani nako kunahusika.Maneno aliyoongea kwa kweli sio ya kiutendaji.Halafu anailaumu serikali eti imeshindwa kufanya kazi yake kwa kuwakamata wanaowachafua na kuwatukana watu kwenye mitandao.Leo ndio ameona ? Tangu siku zote alikuwa wapi.? na anasema eti hataongea tena kuhusu hili suala la yeye na Lady Jay Dee,..Ningemuona wa busara kama angeenda kuongea naye kabla hajaja kwenye media yao na kuliongelea hili.Haya malumbano ya clouds na wasanii wetu wa hapa nchini yanaelekea kuipeka hii tasnia yetu ya mziki wapi?
 
Habari wanaJf,
Nimebahatika kusikia alichoongea Boss Ruge kama wanavyomuita wafanyakazi wa clouds Fm, eti leo hakuna kupiga bongo flava kwenye redio yao.Swali langu hii kama ni redio ya watu hizo bongo flava ambazo amesema zisipigwe na kwa ajili ya wanyama au viumbe wa sayari nyingine.Angefanya la maana asema kabisa kuanzia leo redio yao haitapiga Bongo fleva au imekua ni redio ya gospel hapo ningemkubali,but the way amesema ni kwa siku ya leo,tena kwa kuamrisha kabisa,"nimesema leo hakuna kupiga bongo fleva mpaka saa sita usiku" mi sielewi kwa kweli ,anafanya hivyo kumkomoa nani.Lady Jay dee au waskilizaji wao.Eti redio ya Watu.ama kweli kuwa mkurugenzi sio tu jina,hata kichwani nako kunahusika.Maneno aliyoongea kwa kweli sio ya kiutendaji.Halafu anailaumu serikali eti imeshindwa kufanya kazi yake kwa kuwakamata wanaowachafua na kuwatukana watu kwenye mitandao.Leo ndio ameona ? Tangu siku zote alikuwa wapi.? na anasema eti hataongea tena kuhusu hili suala la yeye na Lady Jay Dee,..Ningemuona wa busara kama angeenda kuongea naye kabla hajaja kwenye media yao na kuliongelea hili.Haya malumbano ya clouds na wasanii wetu wa hapa nchini yanaelekea kuipeka hii tasnia yetu ya mziki wapi?

Kichaa kachukua nguo za boss, boss katoka mtoni mbio kumfukuzia ...... hahahahahahahahaha
 
Ruge ndio aliyemtoa matongotongo huyo mnaemwita Jide; bila hivyo hata huyo mumewe asingemuona!!! Hiyo wanayocheza ni cinema tu kwani hawa walishalala chumba kimoja walipokwenda kwenye KOLA kule south siku za nyuma na ikaleta SOOOOO!!!

Kama unaamini kwamba Ruge ndio bingwa wa kutoa watu tongotongo, kwanini basi amng'ang'anie Jide tu? anashindwa nini kumtoa mwingine tongotongo hadi afikie mafanikio kama ya Jide?

Kama alivyosema Jide, Kusaga na Ruge wanaweza kuwatoa ama kuwabeba watoto wao ama watoto wa dada zao ama watoto wa kaka zao ili wawafikishe katika mafanikio aliyonayo, lakini badala yake wamejikita katika kumfanyia fitna Jide tu ili watimize lengo lao la kumfanya mtumwa wao.

Mungu ndiye anagawa riziki hata kama waliwahi kumfanyia ukupe miaka ile ya giza, sasa watambue kwamba hizi ni enzi za nuru na hawawezi kuendelea kuishi mjini kwa staili ya kupe kwani mazingira na ufahamu wa wasanii umebadilika sana.
 
Bas huu ugomvi ukiendelea nadhan uhusiano wa Jide na G nao upo hatarini sana, mana mengi yatasemwa na sidhani kama Gadner atavumilia yote.


Gadna anayajua yote haya, anajua mengi zaidi ya haya tunayoyajua sisi. Yuko pale kimaslahi, anachuma na kutumia na wengine.

Jide ana stress nyingi, Mume wake wa ndoa ni kicheche, Mume wake wa kando (Ruge) kamgeuka, pia issue ya Mtoto inamchanganya (alijaribu kujisingizia mimba siku za karibuni).

Timing ya wimbo wa kuchukulia tuzo imechemka (Joto Hasira).

Msameheni bure na mmwombee! Joto hasira!
 
Gadna anayajua yote haya, anajua mengi zaidi ya haya tunayoyajua sisi. Yuko pale kimaslahi, anachuma na kutumia na wengine.

Jide ana stress nyingi, Mume wake wa ndoa ni kicheche, Mume wake wa kando (Ruge) kamgeuka, pia issue ya Mtoto inamchanganya (alijaribu kujisingizia mimba siku za karibun

Timing ya wimbo wa kuchukulia tuzo imechemka (Joto Hasira).

Msameheni bure na mmwombee! Joto hasira!

Aiseeeeee...!!!
 
Baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu,
hatimaye mmoja wa wakurugenzi wa
Clouds Media Group, Ruge Mutahaba
ameamua kujibu shutuma za Lady
Jaydee dhidi yake. Ruge amekitumia
kipindi cha Power Break Fast cha
Clouds FM, kujibu rasmi shutuma hizo.
Amesema anasikitishwa na jinsi Jaydee
anavyoendesha harakati zake na kudai
kuwa anapigana kwenye vita isiyo
sahihi.
"Jaydee akaze buti, anapigana na wrong
war, vita yake ameidirect tofauti na
mizinga yake, bunduki zake
amezielekeza kusiko. Skylight Band
inamsumbua, akubaliane na ukweli
kwamba Skylight ndio iliyoisababishia
Nyumbani Lounge kushuka ilivyoshuka,
sio Lady Jaydee kama msanii. Vita yake
na bunduki zake azielekezee Skylight
Band. Hajazungumza hata mara moja
kwamba ndio kitu kinachosumbua. Mimi
naamini kabisa akifanya hiyo kazi,
Jaydee bado ni msanii mzuri, ana
nguvu, afanye kazi kubwa ya kuweza
kurudisha mapambano yake kisanii,
kufanya kazi na aangalie tatizo
lililotokea Nyumbani Lounge labda
anaweza akatatua matatizo lakini sio
kushambulia watu kwenye mitandao,"
amesema Ruge.
Hata hivyo amesema yupo tayari kukaa
meza moja na Lady Jaydee kuzungumza
na kumaliza tofauti zao.
"Mimi niko tayari, kesho, kesho kutwa,
kama yupo tayari na ana watu wengine
wengi tu ambao wanahisi kuna matatizo
binafsi ya kuongea na Clouds, twende
sehemu nyingine neutral tu, tukodishe,
tukae pale tusikie matatizo. Haisaidii
muziki wetu kuonekana Bongo Flava ni
watu ambao kutwa ni kulalamika, kutwa
ni maneno na matusi tu pale
panapokuwa na matatizo."
Ameongeza kuwa suala la wasanii wa
Bongo Flava kupenda kutukana
limewafanya hata wasambaji wa muziki
nchini kuacha kufanya kazi nao.
"GMC kampuni iliyowapa pesa nyingi
wasanii kwenye biashara sio kuwapa tu
kwa kuwagawia, kwa kufanya nao
biashara, sasa hivi huu ni mwaka wao
wa pili na nusu hawajatoa hata albam
moja ya Bongo Flava. Wasanii wa Bongo
Flava wanafikiria kwa Mamu
pamefungwa lakini Mamu anaendelea
na wasanii wa Gospel na wanauza vile
vile.
Ruge amewaasa wasanii wa Tanzania
akiwemo Lady Jaydee kuzitumia vizuri
fursa za kiuchumi zinazojitokeza na sio
kupenda kulalamika.
"Turudi kwenye mstari wa kuziona
opportunities, turudi kwenye mstari wa
kusema kwamba leo tunataka
kumzungumzia Jaydee akiwa na
perfume, akiwa na lipstick kama jana
iliyozinduliwa na Rihanna ambayo
nikaambiwa kwamba stock ya lipstick
mpya ya Rihanna iliyozinduliwa ilikwisha
baada ya masaa matatu.
That's how bigger brand is supposed to
be, and that's how powerful a brand is
supposed to be katika namna ya
kuunganisha na fursa zilizopo.
Unapokuwa na jina tumia fursa, tumia
opportunities zinazokuijia wewe
kujiendeleza na kujikuza. Lakini suala la
kulaumiana halitatukuza kwasababu sisi
ni radio binafsi, tutafanya kile
tunachokifanya sisi kwa matakwa ya
wasikilizaji wetu wengi zaidi, tukiiangalia
faida kama motivation, tukiiangalia
social responsibility kama motivation
yetu ya pili, in the long run kuangalia
tunakotaka kwenda kufikia strategy
ambayo kampuni yetu inajiwekea."
Ruge pia amewakumbusha wasanii
kutojisahau kwakuwa hakuna msanii
anayeweza kuhit maisha yake yote.
"Tuwaandae wasijisahau, na katika hili
simzungumzii Jaydee peke yake,
nazungumzia wasanii wote wa Tanzania
nawazungumzia kuelewa kwamba
tunajisahau sana. Tunapata hela nyingi
sana, sitashangaa miaka mitatu baada
ya leo, Ommy Dimpoz naye ukamsikia
anaandika hivi hivi, au Diamond naye ni
kwasababu hakujipanga tu."
Kuhusu shutuma kuwa Clouds FM inaua
muziki wa Bongo Flava, Ruge amesema,
"inanishangaza kidogo kwasababu
Clouds inategemea matangazo ya
biashara kwa asilimia 95, ndio biashara
yake hiyo. Lakini inategemea muziki wa
Bongo Flava kama maudhui ya kipindi,
inaanzaje kuuua, inategema wasanii wa
Bongo Flava kama wasanii wa kwenda
kufanya shows mkoani."
Kuhusu msimamo wa kampuni Ruge
amesema:
Msimamo wa kampuni ni kwamba
tunaamini kabisa mwanadada kinara wa
muziki wa Tanzania naamini atakaa na
kutafakari la kufanya. Tunamtakia kila
lakheri kwenye show yake ya tarehe 31
afanye vizuri lakini atakapokuwa tayari
sisi tuko tayari kuendelea kufanya kazi,
anajua cha kufanya. Chanzo cha haabari Bongo 5.
 
Back
Top Bottom