Rufaa Igunga: Kafumu atofautiana na CCM

Ni kwenye rufaa tu!Yule aliyeanzisha kesi au yule aliyeshtakiwa NDIYO TU WANAOTAKIWA KISHERIA WAENDELEE NAYO KWENYE HATUA YA RUFAA!Kwa mfano waliomshtaki LEMA wangeshindwa kesi Mama BATILDA asingeweza KUKATA RUFAA hata kama angependa kufanya hivyo maana HAYUMO KWENYE ORODHA YA WASHTAKI na yy aliitwa kama SHAHIDI TU!

Jaji Rwakabalila aliyemvua LEMA ubunge aliongelea chochote kwenye kipengele"cha haki ya mtu asiyegombea ubunge kushtaki kulalamikia uchaguzi ili hali yeye HAKUWA MGOMBEA?Wakili wa LEMA aliweka pingamizi kuomba mahakama iifute kesi kwani Mama Batilda mwenyewe HAJALALAMIKA KAMA ALITUKANWA?Zilionyeshwa hata DVD zozote za LEMA akitukana?

Tuache mahakama ya rufaa iamue lkn mm tayari NIMENUSA KITU!

Kuna kitu ambacho nimekuwa najiuliza kwa muda sasa. Hivi mtu anayekuwa amekashfiwa si ndiye anayekasirika na anayetakiwa kufungua lalamiko? Sasa iweje mtu mwingine achukue umamuzi wa kufungua mashtaka na hata aliyekashfiwa asifike mahakamani kutoa ushahidi?
Maana hata mwanao akikashfiwa huwezi sema unakwenda fungua mashtaka? Labda kama amepigwa na kuumizwa na kukawa na ushahidi wa daktari.
Ndiyo maana hili la Lema lilinishinda kabisa kuelewa. Ama kwa hakika Mh. Tundu Lisu Taifa linamhitaji sana, tena tunahitaji wawepo wengi zaidi.
Kuna jambo pia hunishangaza sheria ya uchaguzi haiweki wazi kuwa Vyama vya siasa vinatakiwa vipate kibali kwa Polisi ili kufanya maandamano, lakini sheria nyingine inayokinzana nayo inawapa Polisi ruhusa ya kutoa au kutotoa kibali cha maandamano. Ama kwa hakika tabia zetu zinajionyesha wazi hata kwenye sheria za nchi.
 
Wakuu, ninaomba kuelimishwa.
Hivi rufaa ya kupinga hukumu hukatwa na nani? Aliyeshindwa katika kesi (individual) au chama cha mwanachama aliyeshindwa katika kesi?
Mkuu hizi Sheria utekelezaji wake unachanganya sana. Kumbuka Godbless Lema alivuliwa ubunge baada ya raia wawili kukata rufaa(sio wagombea, ni watu baki kabisa).
Kwa mfano huo nalazimika kusema kuwa yeyote tu kiwe chama, mgombea au hata mtu yeyote tu anaweza kukata rufaa.
 
Nashangaa kwa nini Magamba hawakubali ukweli,mambo yamebadilika sana,mijini Magamba hawakubaliki wamebaki kuwadanganya wazee wetu vijijini kwa kanga,fulana na kofia.Mbona hawakukata rufaa sumbawanga mjini?wasubiri kuvuliwa nguo mchana kweupe.
 
Mkuu hizi Sheria utekelezaji wake unachanganya sana. Kumbuka Godbless Lema alivuliwa ubunge baada ya raia wawili kukata rufaa(sio wagombea, ni watu baki kabisa).
Kwa mfano huo nalazimika kusema kuwa yeyote tu kiwe chama, mgombea au hata mtu yeyote tu anaweza kukata rufaa.

Ndibalema;
Wale wailoshtakiana tu(Lema na Nkangaa na wenzake 2 kwenye kesi ya Lema)Ndiyo wanaopaswa kukataa rufaa!Ni Dr Kafumu na Mwl Kashindye tu diyo wenye haki za kukata rufaa Igunga!

Huwezi UKAWA HAUMO kwenye kesi ya awali lkn UKAKATA RUFAA!Igunga wanaopaswa kukata rufaa kupinga hukumu ama ni Kashindye au Kafumu tu na CCM wanajua hilo!
 
Igunga,Arusha,Sumbawanga................... Mungu atupe nini tena? labda Nchemba atagombea badala ya Kafumu,makubwa haya!
 
Wakuu, ninaomba kuelimishwa.
Hivi rufaa ya kupinga hukumu hukatwa na nani? Aliyeshindwa katika kesi (individual) au chama cha mwanachama aliyeshindwa katika kesi?
inapingwa na yoyote anayeamini haki haikutendeka katika hukumu hiyo. silazima wawe mlalamikaji au mlalamikiwa
 
Baada ya Dr Kafumu kugoma kukataa rufaa sasa Tume ya taifa ya uchaguzi inatakiwa kuitisha uchaguzi mdogo wa Igunga. CCM wakiwa hawaamini kinachotokea wamebaki wakishangaa wakitafuta mbinu za kuchelewesha uchaguzi.

M4C, Nguvu ya umma na chama cha wananchi Chadema wamejipanga kuchukua jimbo la Igunga kuwahakikishia CCM hawana ngome tena popote. Igunga inakwenda kutoa mwelekeo wa 2015 na hapo ndipo CCM wanataka kutafuta jinsi ya kujificha.

Dr kafumu ameona siasa zimemyeyusha na alitapeliwa ili aondoke madini kwani ni kati ya watu waliokuwa makini na wazalendo, alijitahidi sana kukataa vi-memo vya wizi ila hakujua mbinu chafu, akajikuta kwenye kampeni za rushwa, maneno machafu, ghiliba na udini, huku matapeli wa ccm wakitoa ahadi za hewa na za utengano baina ya dini na dini na koo na koo, leo hii Dr kafumu anaonekana mgeni ndani ya jimbo alilozaliwa.

Kampeni chafu za CCM zilisababisha uzinzi, wizi wa wake za watu, vifo, uharibifu wa mali za raia na matumizi ya silaha za moto kutishia watu na mali zao. Huku Mbunge wa Tabora mjini akiitumia juu ya jukwaa kutishia wapiga kura bastola yake iliyokuwa ikining'inia kiunoni.

Ahadi hewa za Kuwahadaa wananchi bila kafumu hakuna daraja la mbutu na mengine mengi. Dr Kafumu baada ya kuona kachafuliwa vya kutosha sasa atangaza kujikita kwenye taalauma yake na kuachana na siasa. Kibarua hiki kinawafanya CCM ama kutafuta mgombea mwingine au kumrudia Rostam Azizi arudi kugombea Igunga kwani swala la kuvua gamba limekwisha na wamewaangukia wote waliosema ni magamba na kuwaambia zilikuwa kelele za Nape tu. Kwa kuwahakikishia kwamba hakukuwa na swala la kujivua gamba wamemwakikishia RA kwa kuwarusdisha magamba wenzake kwenye kinyang'anyiro cha NEC mzee wa vijisenti na mamvi.

CDM wanasubiria kauli ya Tue ya uchaguzi ili haki itendeke na kura iwe ndio njia pekee ya kuchagua mgombea. ikumbukwe katiba mpya inatakiwa iweke bayana jinsi ya kuendesha mapingamizi ya ubunge badala ya kusubiria kesi muda mrefu ni heri kuweka pingamizi na kusikiliza kesi kabla ya kutangaza mshindi ili kuweza kutangaza mshindi baada ya kila kesi kufungwa na kutoa mwanya wa kutokuwa na kesi mbeleni, hii itasaidia kuwapa wabunge muda wa kufanya kazi na kuepuka gharama nyingi za chaguzi ndogo.

Chief Mkwawa wa Kalenga
Mungu akipenda huwezi badilisha - CDM 2015 Ikulu hakuna wa kuzuia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom