Rubani wa US Airways afunga break ghafla - abiria matumbo moto

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,898
US_Airways_A320_ground.jpg

Tuliondoka April 16 jioni toka Dar kupitia Nairobi kwa Swiss Air, April 17 baadhi ya tuliotoka East Africa na kuunganisha US airways kwenda kutalii Marekani tulionja joto ya jiwe tulioingia pipa la US airways kwenda Washington DC
Dulls International Airport, dege hilo maalum kutuvusha bahari ya Atlantic lilijivuta taratibu kuingia njia ya kurukia, na kabla haijashika kasi rubani alisimamisha ghafla kwenye njia ya kukimbilia na tukasubiri kwa dakika kadhaa. Kisha akatangaza kwamba kumetokea tatizo la kifundi, kama angeamua kuruka tusingekuwa salama wakati wa kuruka au kutua.

Hivyo aliruhusiwa kurudi tena kwa ajili ya matengenezo yaliyochukua takribani masaa mawili na ndipo tuliporuhusiwa kuruka tena. Pamoja na kuchelewa kuunganisha shuttle ya ndege nyingine DC, tunamshukuru rubani kutunusuru isije historia kujirudia mara kwa mara.

Bongo walionisindikiza Airport nimefika salama na punde tu namaliza likizo ya utalii na nitakuwa bongo soon. Thanks a lot Pilot kwa uzoefu wako.
 
Kuna dalili ndege za hawa jamaa ziko choka ile mbaya. Picha hizi dege lao moja liliposhindwa kuendelea na safari jijini New York na kuishia rubani kulitua ndani ya mkondo wa bahari unaounganishwa na mto Hudson.

crash1630.jpg
Gallery-Hudson-river-plan-002.jpg
Gallery-Hudson-river-plan-007.jpg
 
Kwa hiyo return ticket ushabadilisha usije safiri tena na US Airways, au ndiyo kujiandaa kukaa mkao mwingine wa "matuambo moto"? Lol! :smile-big:
 
Kuna dalili ndege za hawa jamaa ziko choka ile mbaya. Picha hizi dege lao moja liliposhindwa kuendelea na safari jijini New York na kuishia rubani kulitua ndani ya mkondo wa bahari unaounganishwa na mto Hudson.

crash1630.jpg
Gallery-Hudson-river-plan-002.jpg
Gallery-Hudson-river-plan-007.jpg
Hapana. Hii ndege haikutumbukia majini kwa sababu ya hali ya choka mbaya. Kuna ndege waliingia kwenye injini wakati ilipokuwa inaanza kupaa. The accident was unavoidable and the pilot did a commendable job.
 
Kwa hiyo return ticket ushabadilisha usije safiri tena na US Airways, au ndiyo kujiandaa kukaa mkao mwingine wa "matuambo moto"? Lol! :smile-big:

Nakushukuru kunishtua, kesho naenda kubadilisha ndege ya kurudi bongo, pamoja na fees zake bora kuliko kuingia ndege na roho juu juu nini kitatokea.
 
Hapana. Hii ndege haikutumbukia majini kwa sababu ya hali ya choka mbaya. Kuna ndege waliingia kwenye injini wakati ilipokuwa inaanza kupaa. The accident was unavoidable and the pilot did a commendable job.

Utetezi dhaifu huo. Mbona uwanja wa KIA hapa kwetu Tanzania kumelalamikiwa sana tatizo la ndege kuingiliwa na ndege wengi zinaporuka na haijatokea ndege kutua ghafla? Na katika historia hatujapata kusikia ndege nyingine iliyotua ghafla sababu ya ndege kuingia kwenye engine. Kwa vyo vyote hiyo ilikuwa ni dalili wazi ya kujenga utetezi wa kosa la udhaifu wa ndege zao kuwa choka ile mbaya.
 
US_Airways_A320_ground.jpg

Tuliondoka April 16 jioni toka Dar kupitia Nairobi kwa Swiss Air, April 17 baadhi ya tuliotoka East Africa na kuunganisha US airways kwenda kutalii Marekani tulionja joto ya jiwe tulioingia pipa la US airways kwenda Washington DC
Dulls International Airport, dege hilo maalum kutuvusha bahari ya Atlantic lilijivuta taratibu kuingia njia ya kurukia, na kabla haijashika kasi rubani alisimamisha ghafla kwenye njia ya kukimbilia na tukasubiri kwa dakika kadhaa. Kisha akatangaza kwamba kumetokea tatizo la kifundi, kama angeamua kuruka tusingekuwa salama wakati wa kuruka au kutua. Hivyo aliruhusiwa kurudi tena kwa ajili ya matengenezo yaliyochukua takribani masaa mawili na ndipo tuliporuhusiwa kuruka tena. Pamoja na kuchelewa kuunganisha shuttle ya ndege nyingine DC, tunamshukuru rubani kutunusuru isije historia kujirudia mara kwa mara.

Bongo walionisindikiza Airport nimefika salama na punde tu namaliza likizo ya utalii na nitakuwa bongo soon. Thanks a lot Pilot kwa uzoefu wako.

msalimie mkulog mwambie huku home mambo si mambo tena. Wabunge wa ndiyooo nao wanafuata upepo, japo kinafiki.
 
Utetezi dhaifu huo. Mbona uwanja wa KIA hapa kwetu Tanzania kumelalamikiwa sana tatizo la ndege kuingiliwa na ndege wengi zinaporuka na haijatokea ndege kutua ghafla? Na katika historia hatujapata kusikia ndege nyingine iliyotua ghafla sababu ya ndege kuingia kwenye engine. Kwa vyo vyote hiyo ilikuwa ni dalili wazi ya kujenga utetezi wa kosa la udhaifu wa ndege zao kuwa choka ile mbaya.
US airways wapo poa, sema midege yao inayofanya local trips ndiyo ipo mibovu. Locally piga JetBlue!
Hiyo ndege imetokea wapi?.. Zurich?
 
Utetezi dhaifu huo. Mbona uwanja wa KIA hapa kwetu Tanzania kumelalamikiwa sana tatizo la ndege kuingiliwa na ndege wengi zinaporuka na haijatokea ndege kutua ghafla? Na katika historia hatujapata kusikia ndege nyingine iliyotua ghafla sababu ya ndege kuingia kwenye engine. Kwa vyo vyote hiyo ilikuwa ni dalili wazi ya kujenga utetezi wa kosa la udhaifu wa ndege zao kuwa choka ile mbaya.
Subiri utakaposikia ndege (birds) wameingia kwenye injini wakati ndege (airplane) inapaa ndipo uje kutuambia utetezi dhaifu. The pilot of the plane that ditched in the Hudson River is an American hero.
 
Kaka hii ilibidi uwaambie ndugu zako waliokusindikiza, au unataka kusema kuna wa JF walijipanga na kukusindikiza airport? Kama ni ndugu na watu wako wa karibu, hauoni ingkuwa rahisi kuwajulisha tu hao kwa sms or email? au ni ulimbukeni wa kupanda ndege kwenda Washington, mbona hii ni kawaida tu jamani? hemu tuacheni ushamba na ulimbukeni bwana .... najua utapiga picha nyingi sana huko ... haya piga moja na fridge and ingine na video utuwekee hapa JF picha of the century .....


US_Airways_A320_ground.jpg

Tuliondoka April 16 jioni toka Dar kupitia Nairobi kwa Swiss Air, April 17 baadhi ya tuliotoka East Africa na kuunganisha US airways kwenda kutalii Marekani tulionja joto ya jiwe tulioingia pipa la US airways kwenda Washington DC
Dulls International Airport, dege hilo maalum kutuvusha bahari ya Atlantic lilijivuta taratibu kuingia njia ya kurukia, na kabla haijashika kasi rubani alisimamisha ghafla kwenye njia ya kukimbilia na tukasubiri kwa dakika kadhaa. Kisha akatangaza kwamba kumetokea tatizo la kifundi, kama angeamua kuruka tusingekuwa salama wakati wa kuruka au kutua. Hivyo aliruhusiwa kurudi tena kwa ajili ya matengenezo yaliyochukua takribani masaa mawili na ndipo tuliporuhusiwa kuruka tena. Pamoja na kuchelewa kuunganisha shuttle ya ndege nyingine DC, tunamshukuru rubani kutunusuru isije historia kujirudia mara kwa mara.

Bongo walionisindikiza Airport nimefika salama na punde tu namaliza likizo ya utalii na nitakuwa bongo soon. Thanks a lot Pilot kwa uzoefu wako.
 
JF bwana kuna vituko..si ungesema tu ulitaka tujue ulikuja na sasa umerudi huko amerika!! Yote haya mara breki ya ghafla mara sisi wa east africa,mara dull airport ya nini unajijazisha maparagraph wakati issue iko simple tu...
 
Hapa ndipo utaona tofauti kati ya wabongo na wa huko majuu. Sasa ili rubani la Dash 8 ya ATC kwa nini alikuamua kutokuruka baada ya kuona matatizo ambayo abiria waliya-notice? Home
 
Utetezi dhaifu huo. Mbona uwanja wa KIA hapa kwetu Tanzania kumelalamikiwa sana tatizo la ndege kuingiliwa na ndege wengi zinaporuka na haijatokea ndege kutua ghafla? Na katika historia hatujapata kusikia ndege nyingine iliyotua ghafla sababu ya ndege kuingia kwenye engine. Kwa vyo vyote hiyo ilikuwa ni dalili wazi ya kujenga utetezi wa kosa la udhaifu wa ndege zao kuwa choka ile mbaya.

Mkuu hao birds ni hatari sana

Kuna boeing ya ATC karibia ituangushe in 2006 pale KIA, waliingia hao brids kama wawili hivi na ile injini nadhali ilitupwa palepale

BIRDS ARE VERY DANGEROUS HATA KAMA NDEGE IMENUNULIWA JANA
 
Kaka hii ilibidi uwaambie ndugu zako waliokusindikiza, au unataka kusema kuna wa JF walijipanga na kukusindikiza airport? Kama ni ndugu na watu wako wa karibu, hauoni ingkuwa rahisi kuwajulisha tu hao kwa sms or email? au ni ulimbukeni wa kupanda ndege kwenda Washington, mbona hii ni kawaida tu jamani? hemu tuacheni ushamba na ulimbukeni bwana .... najua utapiga picha nyingi sana huko ... haya piga moja na fridge and ingine na video utuwekee hapa JF picha of the century .....

2Mejua kama ulipanda ndege, wasalimie huko ulipo.
 
Back
Top Bottom