Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
Tuliondoka April 16 jioni toka Dar kupitia Nairobi kwa Swiss Air, April 17 baadhi ya tuliotoka East Africa na kuunganisha US airways kwenda kutalii Marekani tulionja joto ya jiwe tulioingia pipa la US airways kwenda Washington DC Dulls International Airport, dege hilo maalum kutuvusha bahari ya Atlantic lilijivuta taratibu kuingia njia ya kurukia, na kabla haijashika kasi rubani alisimamisha ghafla kwenye njia ya kukimbilia na tukasubiri kwa dakika kadhaa. Kisha akatangaza kwamba kumetokea tatizo la kifundi, kama angeamua kuruka tusingekuwa salama wakati wa kuruka au kutua.
Hivyo aliruhusiwa kurudi tena kwa ajili ya matengenezo yaliyochukua takribani masaa mawili na ndipo tuliporuhusiwa kuruka tena. Pamoja na kuchelewa kuunganisha shuttle ya ndege nyingine DC, tunamshukuru rubani kutunusuru isije historia kujirudia mara kwa mara.
Bongo walionisindikiza Airport nimefika salama na punde tu namaliza likizo ya utalii na nitakuwa bongo soon. Thanks a lot Pilot kwa uzoefu wako.