RPC Morogoro alivunja criminal procedure of arrest

Taso

JF-Expert Member
Jun 12, 2010
2,461
2,288
CAP 20 of Laws
Criminal Procedure Act, 1985, RE 2002
SECT 23

PERSON TO BE INFORMED OF GROUNDS OF ARREST

Any person who arrests another person shall, at the time of the arrest, inform the other person the offence of which he is arrested.



Cha ajabu Kamanda wa Jeshi la Polisi, Morogoro, alidai hajui sababu ya yeye kumkamata Ney wa Mitego zaidi ya kufuata maagizo kutoka Kituo cha Kati, Kanda Maalum, Dar es Salaam.

Sheria ilimtaka amwambie Mitego sababu ya kumkamata pale pale alipomuekea pingu.

Jeshi la Polisi, tafadhali jifunzeni kufuata sheria bila shuruti.

Wakati wa vuguvugu la kuchaguliwa Rais mpya wa Marekani ambae alionekana ana maamuzi ya kimhemko, lilitolewa onyo kwenye mijadala ya kitaifa, kwamba mtumishi yeyote, hususan mwana ulinzi na usalama, atakaefuata amri ya Donald Trump ambayo ni kinyume cha sheria anaweza kujikuta yuko peke yake mahakamani. Kufuata amri haramu ni jinai

Sasa Makamanda wetu Jeshi la Polisi, hivi hamkusoma taratibu hizi za kitaaluma kabla ya kupewa mamlaka makubwa makubwa kama ya u-RPC? Waziri mpya wa Habari amesema suala la Nay wa Mitego linahusu mambo muhimu, mazito, ya haki za kikatiba.

Mahakama na Bunge Tukufu, tunawasihi sana simamieni sheria mlizotunga ili kuhakikisha zinaheshimiwa na vyombo vya dola.
 
Back
Top Bottom