Rostam nusura ajiumbue

Rostam nusura ajiumbue

Kazi ipo...............................

Dream as if you will live forever,live as you will die tommorow
 
Kazi ipo,ngoja tuone mwisho wake...

Dream as if you will live forever but live as you will die tommorow.
 
Bubu Ataka Kusema said:
Alisema, kampuni zinazodaiwa kugombea eneo awali zilikuwa kampuni moja. “Hizi kampuni awali zilikuwa moja. Zimegawanyika kutokana na sababu zao binafasi,” alisema Kone katika mahojiano na gazeti hili kwa njia ya simu.

Hii habari mbona ni mpya? Kama ni kweli hapo kuna kazi kubwa. Inaelekea kuna mengi ambayo wananchi hatujui kwenye hii saga.

Sasa Mwandishi kwanini asiwaulize wahusika kama hii habari ni kweli?
 
Ni kweli hii ni mpya, hivi tayari amepewa mkataba? Sasa Dr. Rashid atasema nini kuhusu hili, mtu anamkataba na eneo hana hii nchi kweli, mtu kaburunda kwenye Dowans mnampa mkataba mwingine.

Nafikiri alitaka kuchota tena BOT kwa kutumia KAKITI sasa badala ya KAGODA na kuwekeza Singida

Nchi yangu Tanzania
 
Bongo, kwanza unapata tenda(mkataba) ndipo unatafuta eneo. hii picha ilivyo japo Dr. Harry hakusema, mwanzo walikuwa wote, yeye akajitoa, wakaanzisha kampuni yao, wakakimbilia Singida kwa wananchi, wakapata eneo. Wenzao wakamwaga rupia, wakapata mkataba na kuamini watamwaga tena rupia kupata eneo.
Kwa lugha nyingine, Dr. aliwazungunguka wenzake na sasa anapiga kelele kutafuta public symphathy. Mwisho wa movie, wote ni mafisadi, ila atakae cheka kweli, ni atakaecheka mwisho.

- This is incredible, yaani Mkuu Pasco kumbe unajua yote, unaona sasa mimi nilisema haya, sasa tupe basi ukweli wote tujue maana wewe unaonekana unajua sana hii deal, duh! Patamu sana hapa, ndio maana mimi nilisema hawa baadhi ya wawekezaji a decent man kama Mwakyembe, amekutana nao wapi?

- Mkulu Pasco weka vitu hapa maana fumbo hufumbwia mjinga tu, au?

Wazee wa umeme umeme lakini sio Singida FMES!
 
Hii habari mbona ni mpya? Kama ni kweli hapo kuna kazi kubwa. Inaelekea kuna mengi ambayo wananchi hatujui kwenye hii saga.

Sasa Mwandishi kwanini asiwaulize wahusika kama hii habari ni kweli?

- Ndugu yangu Mtanzania, msome vizuri Mkulu Pasco, maana anayajua sana haya ya umeme wa Rostam na Mwakyembe.

FMES!
 
Dk. Slaa anasema akina Rostam wanataka kuzalisha umeme wakati hawana eneo. “Hicho ndicho chanzo cha ugomvi wao na Dk. Mwakyembe (Harrison Mwakyembe, Mbunge wa Kyela).”

Alisema, “Nimekwenda Singida. Naufahamu vema mradi unaodaiwa. Nimeongea na wanakijiji Singida na viongozi wao.

- Pole pole tunaanza kuusogelea ukweli.
 
Hili Riburushi kwa nini mnalionea aibu jamani?
Mnataka atutawale hadi kwenye familia zetu?Jamani inauma sana mi ngoja niende kwa bibi Swanga nampiga na kombora kali afie mbali atatunyanyasa mpaka lini?Kama mmeshindwa mi namloga.

Burushi lilitoa michuzi mingi sana wakati wa Kampeni za 2005 ili kumsaidia Kikwete kuibuka kidedea kama mgombea wa CCM. Hayo mapesa aliyotoa alijifanya ni ya kwake kumbe ni mapesa aliyokupua toka EPA. Sasa njemba lazima amuogope maana mkanda wote wa sinema ya 2005 anao akiamua kuanika hadharani itakuwa patashika nguo kuchanika yale ya Kiwira tutayaona ni cha mtoto. Hivyo njemba lazima iendelee kuwa Bubu kuhusiana na ufisadi wote uliofanywa na Rostam maana akimgusa tu basi utakuwa kama mtego wa panya, huingia waliostahili na hata wale wasiostahili. Ndiyo matatizi ya kuingia madarakani kwa kupitia debe lililopigwa na mafisadi wanakuwa wamejuweka mifukoni mwao huwezi hata kufurukuta.
 
Rostam na apewe kiwanja na ajenge Mitambo halafu mitambo ije ku#&******Pufuuuuuuusss
 
KINACHOTOKEA ni kwamba hivi sasa CCM inatafuta kwa jino na ukucha fedha kwa ajili ya kampeni za kuirudisha tena madarakarni 2010.

Tatizo ni kwamba CCM sasa hivi inatumia WEZI na MAFISASADI wakubwa katika nchi kuitafutia fedha.

Sisi vijana tunaoipenda CCM tuna uhakika kwamba chama kinaweza kuachana na watu hao ambao ajenda yao ni kuishi kama ndio wenye uwezo tu wa kumfanya mtu kuwa Rais nchi hii, kitu ambacho sio kweli.

Mwenyekiti wa CCM akitumia staili kama ile ya Obama na kutuomba vijana kutumia intaneti, barua za kawaida na michango ya anakwaana tunaweza kukusanya mabilioni ya kuirudisha madarakani.

Tunaomba viongozi wetu waachane na watu wenye ajenda zao za siri na ambao wanatumia fursa ya kuitafutia CCM fedha kwa kuwaibia wananchi kile kidogo walichonacho!

Ukweli ni kuwa nchi hii haiwezi kwenda popote kama Chama chochote kinachotawala kitakuwa ni kinara wa wizi, utapeli, ufisadi, ujanja ujanja wa kupata fedha zake za matumizi na zile za kugombania uchaguzi.

Kuna wengi waliokwishasema kuwa hawa Watanzania wasio na asili ya Kiafrika wanaoshirikiana na waswahili wa porini na nyikani wenye uroho na ulafi wa kutisha, ubinafsi wa hali ya juu na uchu wa madaraka ambao huwafanya waone maisha ya wengine sio lolote sio chochote watatrufikisha pabaya tukiwaachia kuhusiana na chama chetu kwa namna yoyote ile.
huduma
 
- This is incredible, yaani Mkuu Pasco kumbe unajua yote, unaona sasa mimi nilisema haya, sasa tupe basi ukweli wote tujue maana wewe unaonekana unajua sana hii deal, duh! Patamu sana hapa, ndio maana mimi nilisema hawa baadhi ya wawekezaji a decent man kama Mwakyembe, amekutana nao wapi?

- Mkulu Pasco weka vitu hapa maana fumbo hufumbwia mjinga tu, au?

Wazee wa umeme umeme lakini sio Singida FMES!
Mkuu FMES, amini usiamini, mimi sijui lolote, na hata wasifu wako naupokea kimachale. nijuacho ni kitendo cha Dr. Harry kushutumiwa ana conflict of interest, yeye katika mkutano wake alimshutumu King Maker, tukajiuliza kwanini asijibu shutuma na badala yake anatoa mashambulizi.
Ni mwanzo wa thread hii ndipo macho yamefunguka kutaka kuona zaidi. kampuni za umeme wa upepo ziko mbili na majina yanafanana. Moja ndio hiyo ya kina Dr. na anaowaita wananchi na ya pili ndio hiyo ya mafisadi.
Data zote zitamwagwa na Dr mwenyewe pale atakapo fyatuka.
 
Haya ndio matatizo ya kuteua maswaiba kwenye uongozi.Kone ni pro EL na EL ni pro RA sasa kesi hapo itapelekwa kwa nani.JK karudia kosa hilo hilo kwenye uteuzi wa ma DCs sasa tusubiri kushuhudia vituko zaidi 2010.
 
Wewe una interest zako binafsi hapa! Sijamsikia Rostam akisema chochote, mbona Dr. tu ndio ana confidence ya kuongea na wananchi? Doesn't that ring a bell? Au ndio amekupigia simu umsemee nini?
Shisye nakuheshimu, naomba tuheshimiane, kwa vile hunijui, sikujui, our common denominator ni jamii forums, hizo interest zangu binafsi hapa ni zipi?
hujamsikia Rostam akisema chochote, jee ushamsikiaga akisema chochote?.
Hakuna ubishi kuhusu makonfo ya Dr, hata alipowasilisha taarifa yake ya December 30 na kujazia mambo yaliyotokea January ni sehemu ya hayo makomfo. Kuongea sana ndio kunakuzuzua?.
Anipigie mimi simu kama nani?. yaani mimi nimuongelee mtu anyeogopwa mpaka na rais wako anamnyenyekea, mimi nitakuwa nani!.
nimesema na nasisitiza "wote ni mafisadi" na atakayecheka mwisho ndiye aliyecheka kweli "he who laugh most is he who laugh last'. kama mlaji tuu, ni mla leo. Chakula kiko jikoni, kitaiva na kitapakuliwa, subiri kujua mlaji ni nani na sio kuleta kumbukumbu ya pilau uliokula siku ya iddi.
 
- Kuna siku wa-Tanzania tutakuja kuamka na ku-figure out how this Rostam man works, naomba mtu mmoja humu anihakikishie kwamba hii kichwa cha topic na habari nzima sio yeye aliyei-plant kwa lengo lake maalum ambalo ndilo hasa tunalifanya sasa hivi hapa na huu mjadala! Hii habari kwangu ni clear kuwa imetengezwa na yeye mwenyewe kwa makusudi maalum.

- Ufike wakati ndugu zangu tuamke usingizini!

William.
 
Last edited:
- Kuna siku wa-Tanzania tutakuja kuamka na ku-figure out how this Rostam man works, naomba mtu mmoja humu anihakikishie kwamba hii kichwa cha topic na habari nzima sio yeye aliyei-plant kwa lengo lake maalum ambalo ndilo hasa tunalifanya sasa hivi hapa na huu mjadala! Hii habari kwangu ni clear kuwa imetengezwa na yeye mwenyewe kwa makusudi maalum.

- Ufike wakati ndugu zangu tuamke usingizini!

William.

Nakuhakikishia siyo King Maker, he is not learned, but bright and smart, anza kuamka wewe, mwamshe baba na mama ili waamshe chama uone moto utakao waka humo ndani. Jamaa ni habari nyingine, kama Mkulu anabow down kwa huyu jamaa, naamini unakokwenda one day, you will too.
 
Mtamfanya Rostam ajione babu kubwa kweli kweli. Kila kitu Rostam, itafika siku wananchi watachoka na hizo kelele za Rostam kila siku.

Kama ana mambo ya ajabu, basi mvizieni na kumkamata kwenye angle ambayo itakuwa ngumu kujinasua.

Magazeti yote haya na wanasiasa wote hawa, wanaimba Rostam Rostam lakini hakuna hata mmoja ambaye ana ushahidi wa kuweza kumfikisha mahakamani?

Watu wanajua hata leo kaenda choo kipi, kakutana na mtu gani lakini hakuna mtu ambaye ana ushahidi wa wazi kumwonyesha Rostam akitenda kosa?

Wakati mwingine njia ya kumkamata mbaya wako ni kukaa kimya.
 
Mtamfanya Rostam ajione babu kubwa kweli kweli. Kila kitu Rostam, itafika siku wananchi watachoka na hizo kelele za Rostam kila siku.

Kama ana mambo ya ajabu, basi mvizieni na kumkamata kwenye angle ambayo itakuwa ngumu kujinasua.

Magazeti yote haya na wanasiasa wote hawa, wanaimba Rostam Rostam lakini hakuna hata mmoja ambaye ana ushahidi wa kuweza kumfikisha mahakamani?

Watu wanajua hata leo kaenda choo kipi, kakutana na mtu gani lakini hakuna mtu ambaye ana ushahidi wa wazi kumwonyesha Rostam akitenda kosa?

Wakati mwingine njia ya kumkamata mbaya wako ni kukaa kimya.



Inawezekana ndiyo jibu lililopatikana huko China, maana nakumbuka mara baada ya Uchaguzi mkuu wa 2005 kuna walioenda China ili kujua teknolojia iliyotumika "kuhamisha" kura za ndiyo kwa wagombea urais wa upinzani na "kuhamia" kwa Kikwete. .... LOL!!!
 
Mtamfanya Rostam ajione babu kubwa kweli kweli. Kila kitu Rostam, itafika siku wananchi watachoka na hizo kelele za Rostam kila siku.

Kama ana mambo ya ajabu, basi mvizieni na kumkamata kwenye angle ambayo itakuwa ngumu kujinasua.

Magazeti yote haya na wanasiasa wote hawa, wanaimba Rostam Rostam lakini hakuna hata mmoja ambaye ana ushahidi wa kuweza kumfikisha mahakamani?

Watu wanajua hata leo kaenda choo kipi, kakutana na mtu gani lakini hakuna mtu ambaye ana ushahidi wa wazi kumwonyesha Rostam akitenda kosa?

Wakati mwingine njia ya kumkamata mbaya wako ni kukaa kimya.

Mkuu Mtanzania, nakubaliana na wewe katika baadhi ya mambo, lakini si suala la ushahidi. Katika Kagoda kuna kila aina ya ushahidi ambao wanao wapelelezi na magazeti yamegusia na kuripoti. Hata hii habari unaona kabisa kuna hati ya kiapo ya wakili, kuna hati ya kiapo ya marehemu Ballali, kuna nyaraka ambazo alitumia BoT kuchukua fedha, kuna mawasiliano na kamera za BoT akifuatilia hizo fedha, kuna watumishi wake waliotumika, kuna EPA nyingine ya mwaka 2000 ambayo kampuni yake ya Afritainer ilihusika na anuani yake ni ile ile ya Kagoda, hayo ni machache lakini anaonekana sehemu nyingi sana lakini hadi leo kina Jeetu Patel wamepelekwa mahakamani yeye bado, pamoja na kujaribu kumtanguliza Manji, lakini ushahidi bado unamgusa.
 
Hili Riburushi kwa nini mnalionea aibu jamani?
Mnataka atutawale hadi kwenye familia zetu?Jamani inauma sana mi ngoja niende kwa bibi Swanga nampiga na kombora kali afie mbali atatunyanyasa mpaka lini?Kama mmeshindwa mi namloga.

Jamani Fidel80. Du naona umechukia sana. Yaani kama kweli unafahamu mchawi bingwa, ruksa. Ila tu uwe makini maana naye amejizindika kisawasawa. Kuna babu mmoja maeneo ya Bagamoyo, anaitwa Simba Kerege. Huyo, ni hatari, nenda huko. Hata kama jamaa ana zindiko, mzee atacheza nalo na atalifuta!!!! E bwana eh, kwenye haya maofisi yetu kuna mastory sana, yaani watu wanajua ndumba ile mbaya. We jifanye tu kuwa na wewe ni mshiriki, kila siri ya uchawi utaipata!!!! Hata kama wewe ni boss sana jitahidi, ujishushe some times ongea na hawa support staff, du utapata mambo mpaka utataka uikimbie ofisi maana unajua for sure na wewe wanakuroga!!! or kukuwekea Limbwata!!!
 
Back
Top Bottom