Rostam Aziz anavyompiga tafu rafikiye Lowassa

Rostam Aziz anavyompiga tafu rafikiye Lowassa

Hivi mbona mnadhani kuwa sisi wote ni "mapumbavu" kama walivyo wanachama wa chama chenu? (Chama Cha Mapumbavu aka FISI WENU). Wizi wa rasilimali unaoendelea hamjauona tu mnangojea Lowassa aingie madarakani? Na hao mapacha watatu si ndio wamemwingiza madarakani raisi aliyepo? Au hujui. Ni hujuma gani ambayo wanashindwa kufanya hivi sasa na hata wakati mwingine wowote rais yeyote wa FISI WENU akiwa madarakani? Huu usanii wenu kaufanyieni Lumumba.

Eti ikulu itageuka kuwa pango la wanyang'anyi, igeuke mara ngapi? Madhali FISI WENU wapo madarakani ikulu ni pango la wanyang'anyi, full stop! Au hujui mambo ya Escrow nini? Unadhani kwanini hawakutoa orodha ya waliochukua fedha Stanbic bank mpaka leo? Muulize kiongozi wa Agizo la Chama Tawala. Sasa anadandia walioweka fedha Uswisi wakati zilizochukulia hapahapa kashindwa kusema. Muulize mwenyekiti wa Kamati husika tutajie nani alichukua fedha Stanbic bank, uone atakavyotoka nduki. We acha Manyang'anyi yaliyopo ikulu ni habari nyingine. Tena alipoingiliwa bungeni na mmoja wa hao mapacha kuhusu hoja zake za Escrow, nusura azimie. Hoja zote zikadoda. Mpaka leo kafunga domo.

Halafu unakuja hapa na ujasiri eti ikulu itakuwa pango la wanyang'anyi, liwe mara ngapi ndipo ujue limekuwa?

ni kweli kabisa mkuu....dawa ya hawa mafisadi ni kuwapiga chini wote oktoba ili nchi hii ipate kupona kutoka kansa ya ufisadi. mwaka huu safari ya UKAWA kuelekea magogoni ni nyeupe kama theluji.
 
Hapana shaka sasa Rostam Aziz na Hussein Bashe wanatumia kila aina ya propaganda kupitia vyombo vyao vya habari kama Gazeti la Mtanzania na kituo cha Television cha CHANNEL TEN kujaribu kuuaminisha Umma kuwa Swahiba wao mkubwa, Edward Ngoyayi Lowassa hatendewi haki Katika mchakato unaoendelea wa kumpata Mgombea urais wa CCM atakaepeperusha bendera ya Chama hicho hapo mwezi Oktoba Mwaka huu,. Leo katika taarifa ya habari ya Channel ten saa 12:00 asubuhi, huku mtangazaji akiisoma taarifa bila kujiamini alisema: "Habari zilizotufikia ktoka Dodoma zinasema kucheleweshwa kwa vikao vya mchujo ni mizengwe iliyoandaliwa ili kumkata Lowassa na kwamba ameandaliwa Jaji mmoja(mtangazaji hakumtaja jina) kuandaa waraka mzito kuhusu Maovu ya Lowassa. taarifa hiyo pia ipo katika gazeri la Mtanzania kwa kichwa cha habari, MKAKATI KUMUENGUA LOWASSA WAVUJA. Swali la kujiuliza hapa ni kwanini mizengwe hiyo iibuliwe na vyombo vya habari vya Rostam Aziz pekee kati ya magazeti mengi na vituo kibao vya TV? Propaganda hizi zinaweza kuwa na lengo la kuandaa mazingira yafuatayo:
1. Kupata uhalali wa kuandaa vurugu kwa kisingizio cha Lowassa kutotendewa haki
2. Kuandaa wana CCM kisaikolojia kuwa bendera fuata upepo pale lowassa atakapo amua kuhamia chama kingine kwa kisingizio cha kutotendewa haki.

Tabia hii siyo nzuri kabisa, ni hatari kwa amani ya nchi kwani CCM ni chama kikongwe ambacho kina kanuni zake za kumpata mgombea
Siyo tu anayekubalika kwa wanancni kwa kuwanunua bali anayekubalika kwa wananchi kwa hiari yao.
Sasa kwa matumizi haya ya nguvu ya Rostam Aziz, Rostam ambaye alipokuwa akiwaaga wananchi wa Igunga alisem amechoshwa na siasa uchwara ndani ya CCM, Rostam ambaye amelifilisi taifa kwa biashara haramu, makampuni hewa na uchafu Mwingi, ni wazi taifa linakwenda kuangukia kwenye Mikono isiyo salama.
Ni HERI LOWASSA KULIKO ROSTAMA AZIZ, LAKINI JE INAWEZEKANA LOWASSA BILA ROSTAM?

leo angalau umejaribu kifikiri ki-GT ila unakosea sana unapowabagua baadhi ya mafisadi na kuwaacha wengine. kiukweli ndani ya CCM hakuna asiyekuwa fisadi isipokuwa tu wanaziadiana viwango. huo ndio ukweli ambao hutaki kuuweka wazi hapa.
 
Back
Top Bottom