tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 25,972
- 25,365
Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikifuatilia namna Channel Ten inavyotumika kumpamba Lowassa kwenye taarifa zake za habari, na kufanikiwa kuunganisha dots kama ifuatavyo:
Siku zote Channel Ten wamekuwa wakiripoti taarifa za Lowassa kwa ustadi wa hali ya juu sana na taarifa zake hupewa air time ya kutosha tofauti na wagombea wengine ndani ya CCM.
Huu ni mpango maalumu wa Rostam Aziz (mmiliki wa Channel Ten) kumpigia debe fisadi mwenzake ili pindi akifanikiwa kuingia ikulu ya magogoni washirikiane naye kuiba rasilimali za taifa.
Mtakumbuka kwamba Lowassa, Chenge na Rostam ni mapacha watatu (utatu wa KIFISADI) ndani ya CCM. Hawa watu hawakukutana barabarani. Wamekuwa wakishirikiana katika shughuli zao za kulihujumu Taifa kwa muda mrefu sasa.
Mtakumbuka hata Nape Nnauye alijaribu kuwavua magamba akawashindwa. Endapo EL atafanikiwa kuingia ikulu mwaka huu, basi elewa kwamba ikulu yetu itageuka kuwa pango la wanyang'anyi. Tuwe makini na mafisadi hawa na kamwe tusiwaruhusu kuisogelea ikulu yetu.
:israel:
Siku zote Channel Ten wamekuwa wakiripoti taarifa za Lowassa kwa ustadi wa hali ya juu sana na taarifa zake hupewa air time ya kutosha tofauti na wagombea wengine ndani ya CCM.
Huu ni mpango maalumu wa Rostam Aziz (mmiliki wa Channel Ten) kumpigia debe fisadi mwenzake ili pindi akifanikiwa kuingia ikulu ya magogoni washirikiane naye kuiba rasilimali za taifa.
Mtakumbuka kwamba Lowassa, Chenge na Rostam ni mapacha watatu (utatu wa KIFISADI) ndani ya CCM. Hawa watu hawakukutana barabarani. Wamekuwa wakishirikiana katika shughuli zao za kulihujumu Taifa kwa muda mrefu sasa.
Mtakumbuka hata Nape Nnauye alijaribu kuwavua magamba akawashindwa. Endapo EL atafanikiwa kuingia ikulu mwaka huu, basi elewa kwamba ikulu yetu itageuka kuwa pango la wanyang'anyi. Tuwe makini na mafisadi hawa na kamwe tusiwaruhusu kuisogelea ikulu yetu.
:israel: