Rostam Aziz amekuja kumharibia Lowasa badala ya kumjenga

Rostam Aziz amekuja kumharibia Lowasa badala ya kumjenga

Jk aliingizwa uraisi kwa rusha hivi hivi na kwa mshikamano wa kambi yake ikiongozwa na Edward Lowasa na Rostam Aziz. Kiasi hata taarifa ya tume ya nidhamu haikusomwa ili mradi tu mlengwa aende magogoni. Leo kila mtu ni shahidi wa wapi taifa lilipo.

Rostam si Mtanzania, kinachomrudisha kuja kuanza kutuletea uharamia wake hapa ni nini kama si maslahi binafisi? Nchi isiyo na mwenyewe. Kama anauchungu na taifa, mbona anapoona mgombea wake anaelekea kukwama anaanza kutoa machozi. Machozi hayo ni ya kuwapenda sana watanzania au machozi ya mamba akikosa mawindo?

Na mfahamu hayo ndiyo yalikuwa makubaliano yao kwamba baada ya huyu wa sasa, eddo aingie ikulu.

Ninashangaa ccm hakuna hata mmoja aliyesalia mwenye maarifa na uzalendo akakakemea huu ugaidi?

Nguvu ya rushwa na udanganyifu unaotumika kwenye mafisadi kwenda ikulu = uzembe wa wana ccm maskini na hohehahe wasiojitambua wanaoimba nyimbo za kusifu maamuzi ya kifisadi ya chama bila kujua wanaua watoto wao na vizazi vyao.

Sasa lililopo ni kila mtanzania mwenye nia njema, kazi iwe moja. Peleka habari kwa mdomo kwa kila Mtanzania maskini, mgonjwa, aliyekoseshwa elimu kwa sababu ya ufisadi, aliyepoteza wazazi na ndugu kwa sababu ya ufisadi, aliyekosa mahala pa kuishi kwa sababu ya ufisadi na yeyote asiyejua kama atakula nini kesha kwa sababu ya ufisadi. Sote tuungane bila kujali vyama, dini wala kabila, tukajiandikishe kwa wingi ili siku ya kura tuikatae Ccm na ufisadi wao wajibebe!.

Ndugu zangu, kumbukeni wana ccm wakawaida hawafaidiki lolote kwenye ufisadi ila wanatumika tu. Misiba inayoletwa na ufisadi inatukumba wote, tunazika kwa wanaccm na kusiko na ccm. Ongezeko la majuha ni watoto wetu sote wana ccm na wasio. Maisha mabaya ni kwa wanaccm na wasio. Wanaofaidi ni mafisadi tu.

Tuungane sote, kwa nguvu zetu zote ccm ifutike kwa sababu ni mkono wa shetani ndani ya Tanzania.

Mwenye kufundisha afundishe.

Mwenye kutunga nyimbo atunge.

Mwenye sanaa za maigizo yatungwe na yaonyeshwe.

Mwenye kutayarisha prints kwenye mavazi afanye hivyo.

Mwenye kuandika vipeperushi atawanye kwa wingi.

Mwenye kuandika kwenye product zinazotumika majumbani kama viberiti, sabuni na mafuta, aweke label.

Mwenye kusimama jukwaana anene.

Mwenye ndugu na uwezo wa nyumba kwa nyumba asichoke.

Mwenye Kumch Mungu, aombe sana.

Mwenye chombo cha usafiri abandike mabandiko.

Ili kwa umoja wetu tukajiandikishe na 25 tukapig kura kinyume na ccm. Tanzania kwanza, vyama vitajengwa ndani ya Tanzania huru.
 
Wako na Karamagi na Chenge pia,hapa ni lazima tupambane watanzania
 
Ngoja wachukue nchi wakufilisi

Hawezi kufulisiwa....WATU KILA SIKU WANASINDA KESI DHIDI YA JAMHURI?......Nikitingwa kidogo tu namwita mheshimiwa sana na mwanasheria ambaye wanasheria wote wa ccm wanamuogopa......TUNDU ANTIPAS LISSU
 
Huwezi kuyaona kwakuwa wewe si mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM Taifa,Halmashauri kuu taifa.Hata kama mabilioni yanamwagwa lazima yamwagwe kwa wahusika si kila mtu eboo hata hili linakushinda kung'amua.
.......kiongozi, mgombea wako yeye nasikia anagawa matrilioni, aliyapata kutoka kwa marehemu Gadaffi, atayagawa kwa nani? orodha ya wajumbe inafanana?
 
Hawa watu wanamagenge ya kupora rasilimali za watanzania na wanatumia wanasiasa kupora hizi rasilimali,ni rostamu huyuhuyu aliejiuzulu kwa kuziita siasa za tanzania ni siasa za maji taka ila chagushanga amerudi kulekule aliko kukimbia kwa kukutukana ,lazima watanzania tuungane kuwashinda watu hawa hapa lazima tuondoe tafauti zetu hakuna cha ukawa wala ccm rostam na kundi lake ni hatari zaidi,anachofanya ni kuja kuchuma mali zetu na kwenda kuwekeza kenya na dubai na nchi nyngine .
 
rostam amerudi kwa kasi kuja kumuunga mkono rafiki yake. inasadikika wamefanikiwa kuiteka ccm kwa 79% na wanaendelea kupambana. watanzania tuamke toka usingizini mafisadi wanapambana kuhakikisha mtu wao anaingia magogoni
wacha waiteke CCM hata 100%. October 25 ndo watajua kuwa hii nchi ina wenyewe na wenyewe watachukua nchi yao!
 
DSC02976.jpg
 
WTF,sasa wewe kinakuwasha nini ikiwa Lowassa anaharibiwa?Pilipili usokula zakuwashiani
Ha ha ha nimelipenda swali lako kwa mtoa mada maana ni kweli yeye ni team membe alafu analalamika team Eddo kujichanganya.
 
Back
Top Bottom