Rostam Aziz amekuja kumharibia Lowasa badala ya kumjenga

Rostam Aziz amekuja kumharibia Lowasa badala ya kumjenga

Lizaboni

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2013
Posts
33,901
Reaction score
20,410
Wadau, amani iwe kwenu.

Kwa sasa kuna mgogoro mkubwa ambao umeibuka ndani ya Team Lowasa baina ya wale wanaomuunga mkono Apson Mwang'onda na kambi ya Rostam Aziz. Chanzo changu ndani ya Team Lowasa kimebainisha kuwa mara baada ya ujio wa Rostam, hali ndani ya kambi hiyo imeanza kwenda kombo kutokana na kutofautiana kifalsafa na mbinu za kumpeleka Lowasa Magogoni.

Taarifa zinasema kuwa kambi ya Apson inaundwa na watu weledi na wenye uzoefu kwenye mikakati mbalimbali hasa kutokana na wengi wao kuwa wamewahi kulitumikia taifa hili katika maeneo tofauti. Hata hivyo, weledi wao unaonekana kuwa si lolote wala chochote kutokana na kushindwa kufanikisha kuwashawishi baadhi ya wajumbe wa sekretarieti, Kamati Kuu na Halmashauri kuu ambao wamekuwa wakimkemea waziwazi Lowasa pale anaposhindwa kwenda sambamba na kanuni na maadili ya chama. Pia kambi hii ni masikini na walala hoi kwa vile wamekuwa wakinyonya kambi ya Rostam kifedha kupitia kwa Lowasa mwenyewe. Kwa maana nyingine, kambi hii ni ya wanyonyaji na kwamba wapo kwa Lowasa kimaslahi zaidi na si kufanikisha lengo la Lowasa kwenda Ikulu. Hii ni kambi ya 'KUPE'.

Kambi Rostam, nguli wa kashfa mbalimbali za ufisadi nchini inaundwa na watu wenye jeuri ya pesa ambao wamekuwa wakiitwa au kujiita kwa majina yenye kuonesha jeuri ya pesa kama Mzee wa Vijisenti, Nyoka Mwenye Makengeza nk. Kambi hii inaamini kuwa fedha inaweza kufanya kila kitu ikiwa ni pamoja na kununua haki za wana CCM.

Kwamba wapende wasipende ni lazima Lowasa aende Ikulu kwa vile pesa zipo. Kwa maana nyingine Kambi Rostam ndio wafadhili wakuu wa Team Lowasa kifedha.

Kutokana na jeuri ya pesa waliyonayo, wamefanikisha kumshawishi Lowasa kuwatema baadhi ya washauri wake walio chini ya Apson na kwa sasa Rostam ndiye anayeratibu harakati zote za Lowasa huku akiwatumia vijana wake kama Peter Serukamba na Hussein Bashe.

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaona kuwa mwelekeo wa Team Lowasa kwa sasa ni mbaya na kwamba lengo lao la kumpeleka Magogoni halitafanikiwa. Kwamba, watu ambao wameteka kambi hiyo hawana taswira nzuri ndani ya chama na kwenye jamii kutokana na kuhusika kwao na kashfa mbalimbali zinazoibuka nchini ikiwa ni pamoja na EPA, RICHMOND, ESCROW, VODACOM nk.

Kwamba, ujio wa Rostam si kwamba amekuja kuimarisha kambi hilo bali amekuja kuliangamiza na kwamba amekuja kuzidisha uchafu kwenye uchafu. Ni sawa na kutupa kinyesi kwenye jalala.

Rostam hana pesa bali anatumia pesa alizokwapua kwa njia ya kifisadi kumweka fisadi mwenzake madarakani huku akiamini kuwa pindi Lowasa akiwa Rais, fedha zote zitarudi kwa njia ile ile ya kifisadi.
 
Mkuu Lizaboni kinacho fanyika sasahvi kwenye siasa ni biashara kubwa ,urais imekua sio kutumikia tena wananchi bali ni biashara tena biashara isiyo na hasara na yenye uhakika wa faida kubwa. Iwe Rostam, iwe apson, iwe Chenge joka kubwa lenye makengeza ,yoyote atakayejiunga na kambi ya Lowasa itakua kwa ajili ya kuchuma pesa tu.

Hao wote uliowataja wanaongoza magenge makubwa ya wafanya biashaara wa ndani na nje ya nchi wanchotaka wao ni kimoja tu Lowasa ashinde kwa namna yoyote ile hata kwa kumtoa Kikwete kesho wanacho taka wao ni kupora rasilimali za Watanzania. Watanzania na tuombe Mungu kikombe hiki kituepuke.
 
Last edited by a moderator:
Subirini mimi niwe Raisi 2030. Nina vision kali sana. Tutaendelea tu.
 
Watakulaje ilhali hawa mafisadi wameifilisi nchi mpaka tunashindwa kupata mlo wa watoto wetu? Nimejitolea kupambana na hawa mafisadi

Hahahahahahahahahahahahaha! Siamini kama haya maneno yameandikwa na gamba la fisi lilokomaa.
 
Hahahahahahahahahahahahaha! Siamini kama haya maneno yameandikwa na gamba la fisi lilokomaa.

Kuna mtu kahack ac ya lizaboni aiseeee!
Hapana wakuu. Ni mie mwenyewe na nimeandika haya kwa utashi wangu na ndio uhalisia. Watu wanapiga mabilioni ya EPA, RICHMOND ESCROW nk then utegemee wananchi wa kawaida wawe na maisha bora? Haiwezekani na haitakuja kuwa hivyo. Siku zote bepari kama Rostam Aziz na wengineo wanawaza jinsi ya kutunyonya watanzania. Ujinga mtupu. Mbaya zaidi kinapakaziwa chama chetu na serikali yetu kumbe kuna manyang'au machache yamejikusanya na yanapiga deal hizi kinyemela
 
Kweli kabla ya October mafisi yameanza kukimbia zizi kama hili jamaa limefunguka.


swissme
 
Kweli kabla ya October mafisi yameanza kukimbia zizi kama hili jamaa limefunguka.


swissme
Mambo ya msingi yanapaswa kusemwa hadharani. Hatuwezi kuacha chama kinaharibiwa na watu wachache ambao wanafahamika
 

Attachments

  • IMG_20150523_134646.jpg
    IMG_20150523_134646.jpg
    452.3 KB · Views: 903
Regina, mwambie mmeo ni muda wa kukaa na familia! Aliyoyafanya kwa watanzania yanatosha.
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Kwa sasa kuna mgogoro mkubwa ambao umeibuka ndani ya Team Lowasa baina ya wale wanaomuunga mkono Apson Mwang'onda na kambi ya Rostam Aziz. Chanzo changu ndani ya Team Lowasa kimebainisha kuwa mara baada ya ujio wa Rostam, hali ndani ya kambi hiyo imeanza kwenda kombo kutokana na kutofautiana kifalsafa na mbinu za kumpeleka Lowasa Magogoni.

Taarifa zinasema kuwa kambi ya Apson inaundwa na watu weledi na wenye uzoefu kwenye mikakati mbalimbali hasa kutokana na wengi wao kuwa wamewahi kulitumikia taifa hili katika maeneo tofauti. Hata hivyo, weledi wao unaonekana kuwa si lolote wala chochote kutokana na kushindwa kufanikisha kuwashawishi baadhi ya wajumbe wa sekretarieti, Kamati Kuu na Halmashauri kuu ambao wamekuwa wakimkemea waziwazi Lowasa pale anaposhindwa kwenda sambamba na kanuni na maadili ya chama. Pia kambi hii ni masikini na walala hoi kwa vile wamekuwa wakinyonya kambi ya Rostam kifedha kupitia kwa Lowasa mwenyewe. Kwa maana nyingine, kambi hii ni ya wanyonyaji na kwamba wapo kwa Lowasa kimaslahi zaidi na si kufanikisha lengo la Lowasa kwenda Ikulu. Hii ni kambi ya 'KUPE'.

Kambi Rostam, nguli wa kashfa mbalimbali za ufisadi nchini inaundwa na watu wenye jeuri ya pesa ambao wamekuwa wakiitwa au kujiita kwa majina yenye kuonesha jeuri ya pesa kama Mzee wa Vijisenti, Nyoka Mwenye Makengeza nk. Kambi hii inaamini kuwa fedha inaweza kufanya kila kitu ikiwa ni pamoja na kununua haki za wana CCM.

Kwamba wapende wasipende ni lazima Lowasa aende Ikulu kwa vile pesa zipo. Kwa maana nyingine Kambi Rostam ndio wafadhili wakuu wa Team Lowasa kifedha.

Kutokana na jeuri ya pesa waliyonayo, wamefanikisha kumshawishi Lowasa kuwatema baadhi ya washauri wake walio chini ya Apson na kwa sasa Rostam ndiye anayeratibu harakati zote za Lowasa huku akiwatumia vijana wake kama Peter Serukamba na Hussein Bashe.

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaona kuwa mwelekeo wa Team Lowasa kwa sasa ni mbaya na kwamba lengo lao la kumpeleka Magogoni halitafanikiwa. Kwamba, watu ambao wameteka kambi hiyo hawana taswira nzuri ndani ya chama na kwenye jamii kutokana na kuhusika kwao na kashfa mbalimbali zinazoibuka nchini ikiwa ni pamoja na EPA, RICHMOND, ESCROW, VODACOM nk.

Kwamba, ujio wa Rostam si kwamba amekuja kuimarisha kambi hilo bali amekuja kuliangamiza na kwamba amekuja kuzidisha uchafu kwenye uchafu. Ni sawa na kutupa kinyesi kwenye jalala.

Rostam hana pesa bali anatumia pesa alizokwapua kwa njia ya kifisadi kumweka fisadi mwenzake madarakani huku akiamini kuwa pindi Lowasa akiwa Rais, fedha zote zitarudi kwa njia ile ile ya kifisadi.
Inakuwaje kambi ya Apson uiseme kuwa ni ya watu weledi kuliko kambi Rostam wakati wote wanania moja ya kupigana kufa na kupona kuhakikisha fisadi ana ingia Ikulu?.
 
Inakuwaje kambi ya Apson uiseme kuwa ni ya watu weledi kuliko kambi Rostam wakati wote wanania moja ya kupigana kufa na kupona kuhakikisha fisadi ana ingia Ikulu?.
Weledi unaozungumzwa hapa ni wa kupanga mikakati. Si vinginevyo. Kumbuka Apson anampigania Lowasa kwa vile ameahidiwa kupewa kazi maalum ndani ya Idara ya Usalama wa Taifa. Rostam anamsaidia Lowasa kwa lengo la kutunyonya Watanzania. Hizi ni kambi mbili zenye malengo tofauti kwa Lowasa
 
Bora wewe Mkuu. Lakini kusubiri miaka 15 huku tukinyonywa na hawa mafisadi papa hakika ni maumivu makali sana

Wewe subiri Laigwaanan aingie ikulu kama hajakukafin ukiwa hai. Kila ukimsikia jina lazima ukahare kwanza. Mwisho wa ubaya aibu.
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Kwa sasa kuna mgogoro mkubwa ambao umeibuka ndani ya Team Lowasa baina ya wale wanaomuunga mkono Apson Mwang'onda na kambi ya Rostam Aziz. Chanzo changu ndani ya Team Lowasa kimebainisha kuwa mara baada ya ujio wa Rostam, hali ndani ya kambi hiyo imeanza kwenda kombo kutokana na kutofautiana kifalsafa na mbinu za kumpeleka Lowasa Magogoni.

Taarifa zinasema kuwa kambi ya Apson inaundwa na watu weledi na wenye uzoefu kwenye mikakati mbalimbali hasa kutokana na wengi wao kuwa wamewahi kulitumikia taifa hili katika maeneo tofauti. Hata hivyo, weledi wao unaonekana kuwa si lolote wala chochote kutokana na kushindwa kufanikisha kuwashawishi baadhi ya wajumbe wa sekretarieti, Kamati Kuu na Halmashauri kuu ambao wamekuwa wakimkemea waziwazi Lowasa pale anaposhindwa kwenda sambamba na kanuni na maadili ya chama. Pia kambi hii ni masikini na walala hoi kwa vile wamekuwa wakinyonya kambi ya Rostam kifedha kupitia kwa Lowasa mwenyewe. Kwa maana nyingine, kambi hii ni ya wanyonyaji na kwamba wapo kwa Lowasa kimaslahi zaidi na si kufanikisha lengo la Lowasa kwenda Ikulu. Hii ni kambi ya 'KUPE'.

Kambi Rostam, nguli wa kashfa mbalimbali za ufisadi nchini inaundwa na watu wenye jeuri ya pesa ambao wamekuwa wakiitwa au kujiita kwa majina yenye kuonesha jeuri ya pesa kama Mzee wa Vijisenti, Nyoka Mwenye Makengeza nk. Kambi hii inaamini kuwa fedha inaweza kufanya kila kitu ikiwa ni pamoja na kununua haki za wana CCM.

Kwamba wapende wasipende ni lazima Lowasa aende Ikulu kwa vile pesa zipo. Kwa maana nyingine Kambi Rostam ndio wafadhili wakuu wa Team Lowasa kifedha.

Kutokana na jeuri ya pesa waliyonayo, wamefanikisha kumshawishi Lowasa kuwatema baadhi ya washauri wake walio chini ya Apson na kwa sasa Rostam ndiye anayeratibu harakati zote za Lowasa huku akiwatumia vijana wake kama Peter Serukamba na Hussein Bashe.

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaona kuwa mwelekeo wa Team Lowasa kwa sasa ni mbaya na kwamba lengo lao la kumpeleka Magogoni halitafanikiwa. Kwamba, watu ambao wameteka kambi hiyo hawana taswira nzuri ndani ya chama na kwenye jamii kutokana na kuhusika kwao na kashfa mbalimbali zinazoibuka nchini ikiwa ni pamoja na EPA, RICHMOND, ESCROW, VODACOM nk.

Kwamba, ujio wa Rostam si kwamba amekuja kuimarisha kambi hilo bali amekuja kuliangamiza na kwamba amekuja kuzidisha uchafu kwenye uchafu. Ni sawa na kutupa kinyesi kwenye jalala.

Rostam hana pesa bali anatumia pesa alizokwapua kwa njia ya kifisadi kumweka fisadi mwenzake madarakani huku akiamini kuwa pindi Lowasa akiwa Rais, fedha zote zitarudi kwa njia ile ile ya kifisadi.

WTF,sasa wewe kinakuwasha nini ikiwa Lowassa anaharibiwa?Pilipili usokula zakuwashiani
 
Hapana wakuu. Ni mie mwenyewe na nimeandika haya kwa utashi wangu na ndio uhalisia. Watu wanapiga mabilioni ya EPA, RICHMOND ESCROW nk then utegemee wananchi wa kawaida wawe na maisha bora? Haiwezekani na haitakuja kuwa hivyo. Siku zote bepari kama Rostam Aziz na wengineo wanawaza jinsi ya kutunyonya watanzania. Ujinga mtupu. Mbaya zaidi kinapakaziwa chama chetu na serikali yetu kumbe kuna manyang'au machache yamejikusanya na yanapiga deal hizi kinyemela

nitajie huyo ambae sie fisadi ndani ya CCM
 
Back
Top Bottom