Romy Jones ndani ya bifu zito na Lamata!

Kama ndiivyo basi RJ kazingua sababu hali yake kifedha haikuwa nzuri ndio maana akaanza kujiongeza. Anatakiwa akumbuke kwanini aliitafuta hiyo kazi.

Pale kwa kaka Mondi mambo ya fedha si rahisi kwa kila mtu.
Mwenzangu ana madeni na maisha ya wasanii si unayajua tena?

Ila angemshirikisha Lamata wakajua namna ya kupanga ratiba zake za shootings, kazi hafanyi anataka maokoto.

Mondi kumpa kazi ya kuwa DJ wake rasmi ni bonge la mchongo, hana deni.
 
DJ maarufu nchini, Romeo George ‘Romy Jones’ ameingia katika bifu zito na bosi wake katika tasnia ya filamu mwanamama Leah Mwendamseke ’Lamata’ kwa kile kinachodhaniwa kuwa vita ya kimaslahi.

Wawili hao wamefanya kazi kwa mafanikio katika tamthilia maarufu nchini ya Jua Kali, kabla ya kuibuka kwa majukumu mapya yaliyomzidia Romy Jones kutimiza wajibu wake wa kushiriki ktk tamthilia hiyo.

CHANZO NI WASAFI FESTIVAL!
Ikumbukwe kuwa, licha ya Romy Jones kuwa ndugu wa damu wa Diamond Platinumz, ndiye DJ wake rasmi katika kila tamasha la muziki atakaloshiriki.

Hiyo imepelekea Romy Jones kuwa busy kutokana na utitiri wa shows nyingi ndani ya tamasha hilo ambalo Diamond kama muasisi na mmiliki amewekeza nguvu zake nyingi huko kwa kushiriki binafsi katika kila mkoa ambao kuna ratiba ya kufanyika kwa Wasafi Festival.

Romy Jones baada ya kutingwa na matamasha, akakosa kushiriki kwa ukamilifu na pengine kutokushiriki kabisa kwa sehemu kubwa katika tamthilia hiyo.

Kitendo hiki kilimuumiza sana Lamata ambaye ndiye aliyempa nafasi ya kuigiza kwa mara ya kwanza kupitia tamthilia hiyo kubwa na ilikuwa bahati tu kwa mujibu wake mwenyewe Romy Jones kutokana na mahojiano kadhaa aliyowahi kuyafanya juu ya ushiriki wake katika tamthilia hiyo na nyingine za Kiswahili.

Balaa baina yao lilizuka pale Romy Jones alipokwama kwenye mambo yake, huku akitaka kupewa malipo kutoka kwa uongozi wa Jua Kali ambako hakuwa ameonekana katika shooting kadha wa kadha.

Lamata kama bosi wa tamthilia hiyo hivi sasa amepumzika kwa kiasi kikubwa majukumu kutokana na ujauzito wake kufikia ukingoni karibuni na kujifungua, aliingilia kuweka sawa baada ya mzozo mkubwa kuibuka kati ya mhasibu wake na Romy Jones juu ya malipo.

Alimpigia simu RJ na kuzozana nae kwa kumpa ukweli wa mambo jinsi gani anavyokwamisha shooting, na kutoa maagizo RJ atumiwe laki moja katika simu kwa ajili ya mafuta ya gari kwa RJ kisha amfuate Lamata alipo wakajadili kwa kina, na ikiwa ni pamoja na kulipwa stahiki zake zote.

RJ hakukubaliana na hilo, punde laki moja ilipoingia kupitia simu yake na mhasibu kupiga simu kuthibitisha, RJ akagombana na mhasibu kisha akaurudisha muamala.
Yeye RJ alitaka kuongea wayaweke sawa na sivyo Lamata alivyotaka ‘kumalizana’ nae.

Hadi ninavyoandika hapa, kuna uwezekano mkubwa wa Billy Jr. kutokuonekana tena katika tamthilia ya Jua Kali baada ya kuchokwa na kila mmoja hadi wasanii wenzie kwa ‘uzinguaji’ wake.

RJ mwenyewe anahaha huku na huko kuomba kikao na Lamata bila mafanikio…

Ndimi,

Nifah


View attachment 2844179View attachment 2844182
Kwa hili nasimama na RJ..

Lamata Sasa kazidi mara ya kwanza alikuwa Neila..Akabadilishwa sasa Bill Jr hapana aisee
 
DJ maarufu nchini, Romeo George ‘Romy Jones’ ameingia katika bifu zito na bosi wake katika tasnia ya filamu mwanamama Leah Mwendamseke ’Lamata’ kwa kile kinachodhaniwa kuwa vita ya kimaslahi.

Wawili hao wamefanya kazi kwa mafanikio katika tamthilia maarufu nchini ya Jua Kali, kabla ya kuibuka kwa majukumu mapya yaliyomzidia Romy Jones kutimiza wajibu wake wa kushiriki ktk tamthilia hiyo.

CHANZO NI WASAFI FESTIVAL!
Ikumbukwe kuwa, licha ya Romy Jones kuwa ndugu wa damu wa Diamond Platinumz, ndiye DJ wake rasmi katika kila tamasha la muziki atakaloshiriki.

Hiyo imepelekea Romy Jones kuwa busy kutokana na utitiri wa shows nyingi ndani ya tamasha hilo ambalo Diamond kama muasisi na mmiliki amewekeza nguvu zake nyingi huko kwa kushiriki binafsi katika kila mkoa ambao kuna ratiba ya kufanyika kwa Wasafi Festival.

Romy Jones baada ya kutingwa na matamasha, akakosa kushiriki kwa ukamilifu na pengine kutokushiriki kabisa kwa sehemu kubwa katika tamthilia hiyo.

Kitendo hiki kilimuumiza sana Lamata ambaye ndiye aliyempa nafasi ya kuigiza kwa mara ya kwanza kupitia tamthilia hiyo kubwa na ilikuwa bahati tu kwa mujibu wake mwenyewe Romy Jones kutokana na mahojiano kadhaa aliyowahi kuyafanya juu ya ushiriki wake katika tamthilia hiyo na nyingine za Kiswahili.

Balaa baina yao lilizuka pale Romy Jones alipokwama kwenye mambo yake, huku akitaka kupewa malipo kutoka kwa uongozi wa Jua Kali ambako hakuwa ameonekana katika shooting kadha wa kadha.

Lamata kama bosi wa tamthilia hiyo hivi sasa amepumzika kwa kiasi kikubwa majukumu kutokana na ujauzito wake kufikia ukingoni karibuni na kujifungua, aliingilia kuweka sawa baada ya mzozo mkubwa kuibuka kati ya mhasibu wake na Romy Jones juu ya malipo.

Alimpigia simu RJ na kuzozana nae kwa kumpa ukweli wa mambo jinsi gani anavyokwamisha shooting, na kutoa maagizo RJ atumiwe laki moja katika simu kwa ajili ya mafuta ya gari kwa RJ kisha amfuate Lamata alipo wakajadili kwa kina, na ikiwa ni pamoja na kulipwa stahiki zake zote.

RJ hakukubaliana na hilo, punde laki moja ilipoingia kupitia simu yake na mhasibu kupiga simu kuthibitisha, RJ akagombana na mhasibu kisha akaurudisha muamala.
Yeye RJ alitaka kuongea wayaweke sawa na sivyo Lamata alivyotaka ‘kumalizana’ nae.

Hadi ninavyoandika hapa, kuna uwezekano mkubwa wa Billy Jr. kutokuonekana tena katika tamthilia ya Jua Kali baada ya kuchokwa na kila mmoja hadi wasanii wenzie kwa ‘uzinguaji’ wake.

RJ mwenyewe anahaha huku na huko kuomba kikao na Lamata bila mafanikio…

Ndimi,

Nifah


View attachment 2844179View attachment 2844182
Nifah mwaka huu kwenye ubuyu hutaki utani.

Wakianzisha nyuzi za mwisho wa mwaka za wachangiaji walioshinda JF idara ya ubuyu nakupigia kura.
 
Lols!
Asante Mkuu…

Kama umenishawishi kesho niwape ubuyu mwingine hiviiiiii, ninao tele kabatini mwangu.
Ni mimi kuchagua upi wa kuweka na upi wa kusubiri.
Weka weka ubuyu.

Halafu ubiyu wako unauweka newsy newsy hivi.

Ubuyu umepimwa kwa viwango vya TBS 🤣🤣

Hatuwezi kuwa tunaongea ma logical fallacy ya logical non sequitur muda wote.

Kazi na dawa 🤣🤣🤣
 
Kwa lolote lile nasimama upande wa RJ.

RJ ni mtu poa sana.
Ni kweli mkuu. Mwaka 2018 nilimpa kazi ya kunitangazia biashara yangu alinifanyia kwa uaminifu wa hali ya juu kama tulivyokubaliana. Pia aliniunganisha na dogo mmoja wa Graphics ambaye naye ni mtu makini na ninafanya nae kazi hadi leo. Romy Jones ni mtu mwema sana. Katika hili siko upande wowote ila ninawasihi wakae chini na kuliweka hili jambo sawa kwa maslahi mapana ya pande zote.
 
Sasa kosa la Lamata ni nini? Mtu hajatokea kutimiza wajibu wake, anaibuka anataka hela.
Tena kwenye igizo ambalo linaendelea…
Sababu zake zinaelezeka mbona ila lamata sio msikiliza wa Sababu za wenzake anajali kazi kuliko utu..
Nakumbuka Naila (Menina) alifiwa na mumewe na wakati huo kajifungua bado anataka aende kwenye Scene kushoot aangalie utu kwanza mengine baadae
 
Back
Top Bottom