Roho imeniuma sana

Roho imeniuma sana

1. Unajuaje kama alikua hana hela...??

2. Au roho imekuuma kwakua tu alikutafuna na asubuhi akakuachia manyoya..!?

3. Hivi kweli kama huyo ni mpenzi wako, kwani ni lazima akulipe kila ukilala kwake....!?

4. Mbona sikunyingine haujawahi kuja kuyasema mazuri yake, ama hata kumuanzishia thread kila akikupa pesa...!?

5. Ulitaka akulipe, kwani wewe ni mfanya biashara ya mwili wako....!?

Aggghhhhh......
Nimejikuta napata maswali mengi kabla ya kukushauri aiseee.....
Anyway, huo ni mtazamo wangu tu. Naomba nisirushiwe mawe
mama pita mama pita mama pita, ana hatari sana huyu mama pita brooo
 
Ni mapema sana kujudge kwa upande mmoja...
1.Inawezekana jamaa kachunguza cm yako usiku kaona kuna sponser so kachukia why anahudumia while wako wawili au zaidi..

2.Inawezekana jamaa hataki aondoke..

3.Inawezekana kamchoka anamtafutia sababu....

4.Inawezekana jamaa kakuona sio wife material mwanaume akiwa anataka kuoa huwa wanakuwa na vigezo vingi sana labda kaamka morning kajiandalia breakfast au kaondoka na njaa...kajipasia nguo n.k....

5.Lakini pia inawezekana kitendo cha kukuita ghafla na kuamua kulala kwake coz hapo umesema muda umeenda umeamua kulala kwake kimekudisqualify kuwa mke...

kuna sababu zaidi ya mia za upande wa pili bado hatuzijui na hatutazijua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ungekuwa muwazi ulipofika kwake kumueleza. Ila haya ya pesa duh.. kweli unanyanyuka kutoka kwako bila nauli au haukuwa na pesa na ulitegemea mgonjwa ndio akupe!? Wanawake tujitahidi kuwa tunabeba pesa ukizoea hayo hautajitia aibu kama iliyokukuta. Sasa haya hiyo mia tano inaelekea alitaka kukupima kama utaichukua na kuikuta akaichukua.. huyo anakupa nafasi ya kujiondosha kutoka kwake.. na inaelekea umezoea kutaka akupe pesa kila mara.. jibadili pia ukipata mwingine na usionyeshe kuwa upo upo wa kuomba omba. Kama hauna unamwambia sio kusubiri akusome kama vile ni wizard.
 
Hahahahahaaaa jamaa bandidu hadi kero, yaani kairudia jero, duh nimecheka hadi mbavu zinauma. Pole Sana mkuu, usimind maana hukumwambia kuwa utahitaji nauli mbaya zaidi no mgonjwa, huwezi kwenda kwa mginjwa ukitegemea akupe nauli.
 
Hivi alivyokujulisha kuwa anaumwa ulitegemea kwenda kumfanyia nni?

Bahati mzuri umemkuta mzima na kakwambia alitaka ajue kama unampenda.
Kaondoka asubuhi hajaacha nauli ! Kwani VP mambo ya kula pia hayaeleweki.

Yawezekana jamaa kaenda kuhangaika anajua akirudi atakuta umerekebisha kila kitu na akirudi tu anakutamkia uhamie jumla. Unadhani umepoteza bahati yako.
 
Iyo ni tabia ya wanawake wengi.mna tabia mkienda kwa wapenz mnabena pochi kubwa lenye vitu kibao vyakujiremba ila siku zote mnasemaga hamna nauli yakuwarudisha mlikotoka.ata wewe ata kama ungebeba iyo pochi bado naamini ungesema huna nauli yakurudia kwako japo pia siamini kama kweli uliacha pochi vinginevyo sema kweli nauli uliyomaanisha.Ata ivyo ni wajibu kwa mwanaume kutoa huduma kwa mpenzi wake ila pia ni ulimbukeni kwa mwanamke anayejitambua kushindwa kujisaidia kwa vitu vidogo vidogo kama nauli ya daladala pale anapotoka kwa mpenzi wake.Hii tabia yenu yakujiendekeza ata kwa vitu vidogo vidogo ndo vinazidi kukuza tabia ya wanaume wengi kuwachukulia wanawake kama chombo cha starehe.
 
Back
Top Bottom