Roho imeniuma sana

Ninampenz wangu tuna muda kama miez 6 hv..
Jana aliniita kwake kua anaumwa ajisikii poa nami nikaenda kwake kama kumuona kufika kumbe mtu mzima tu et nilitaka nijue kama unanipenda
Sababu mda ulikua umeenda nikaamua kulala kwake
Kilichoniuma tumelala asubuh kaamka kaenda kazini mi naamka hajaniachia hata nauli sijakaa kama dakika 20 hv akarudi alisahau kitu mi sikuambia kitu nikafikiria labda alisahau kama binadam au alikua ninayo,,,kumbe aliacha 500 mezan akairudia akaichukua
Nimeamka sina nauli kibaya nikwamba alivyonishtua anaumwa hata poch niliacha nyumban....
Wapendwa nimeumia sana maana nimehangaika nimemtumia msg my sina nauli...kakaa kimya hajajibu mpaka sasa hv nilichokifanya nikamwambia rafik yangu akanitumia...
Moyo umeniuma sana kwel kwa mtu unaempenda kwel unamfanyia hivyo.. Wht if nisingepata mtu wakumitumia

Vumilia bado kidogo utafaulu mtihani wake aliokupangia
1: alitaka kuona kama unamjali, na kweli ukaonyesha sense of urgency, umefika kwenye tukio nila kuchelewa
2: Mtihani wa pili ndio huo, kakuacha bila kitu, anategemea utafika kwako bila kulalamika wala kulaumu na wala upendo wako hautapungua,

Natania tu mama pita ,
 
mkuu jiongeze basi suala liko wazi kabisa Jamaa ako alimiss mgegedo.... pili kwa jamaa ako kushindwa kupokea simu yako inaonesha wazi keshakuchoka na wewe kama mtu mzima anza kuwa na plan B kuanzia sasa.... kila la kheri
 
Ulimuambia unamtegemea nauli?? Yaani ulienda kumuona mgonjwa na ulitegemea akupe nauli yeye? Ungemuambia sina nauli.

Huu utegemezi umezidi kipimo.

Sent using Jamii Forums mobile app


tunawazaga pamoja kwa ishu hizi ! sasa huyu akija olewa nae atateseka kama yupo hai alafu yupo kaburini! na jinsi andika yake inaonekana atamsamehe jamaa!hhhhheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee [HASHTAG]#najipenda[/HASHTAG] nilivyo aisee !yaan ni nusu dk nakusahau hata km unaniskwitisha vipi mfyuuuuuu
 
Kilichoniuma tumelala asubuh kaamka kaenda kazini mi naamka hajaniachia hata nauli sijakaa kama dakika 20 hv akarudi alisahau kitu mi sikuambia kitu nikafikiria labda alisahau kama binadam au alikua ninayo,,,kumbe aliacha 500 mezan akairudia akaichukua
aisee huyo jamaa yako apewe tuzo maana anamiliki upumbafu first grade/pure/uncontaminated stupidity,
 
Ulimuambia unamtegemea nauli?? Yaani ulienda kumuona mgonjwa na ulitegemea akupe nauli yeye? Ungemuambia sina nauli.

Huu utegemezi umezidi kipimo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Best mi sio tegemez hata kidogo ninabiashara yangu inanilipa tu
Nadhan imetokea tu kanipigia sikua nyumban na aliniambia yuko hoi anaumwa kwel sikurud hata nyumban kuchukua hela,,,bht nzur nilikua na hela kwenye manyonyo tena ulikua ya upatu,, ikabidi niende nafika ananiambia nilikumiss nikuone tu,,,,
Asubuh kaamka namwambia unajua sina nauli akaniambia poa
 
1. Unajuaje kama alikua hana hela...??

2. Au roho imekuuma kwakua tu alikutafuna na asubuhi akakuachia manyoya..!?

3. Hivi kweli kama huyo ni mpenzi wako, kwani ni lazima akulipe kila ukilala kwake....!?

4. Mbona sikunyingine haujawahi kuja kuyasema mazuri yake, ama hata kumuanzishia thread kila akikupa pesa...!?

5. Ulitaka akulipe, kwani wewe ni mfanya biashara ya mwili wako....!?

Aggghhhhh......
Nimejikuta napata maswali mengi kabla ya kukushauri aiseee.....
Anyway, huo ni mtazamo wangu tu. Naomba nisirushiwe mawe
 
Aiseee, pole sana, kuna siku na mimi nilienda kumuona mgonjwa(mchepuko) enzi hizo lakini, Nimefika pale tukapiga story akaniambia anataka akanunue maji ya kunywa, nilikua na kama elfu 37 hivi kwenye mfuko wa shati, sasa nazitoa ili nimpe hiyo hela ya maji si akazivuta zote!!!

Halafu sikua na usafiri na ilikua usiku ushaingia, na cm imezima chaji, nilichukia mno, nikamwambia basi nipe hiyo buku mbili nichukue bodaboda mpaka makumbusho then nipande daladala to home akawa anacheka ile kwa dharau.

Akatoka akaenda kununua vya kununua, na mimi nikatoka nikaanza mguu mosi mguu pili huku nikitafakari cha kufanya maana hata umeme ulikua umekatika kote. Ila mpaka leo sijawahi kurudi tena kwake. Alinifanya nimuwazie tofauti sana.
 
Inasikitisa sana aisee!

To accomplish much you must first lose everything..
 
Back
Top Bottom