Somaiyo
Senior Member
- Jul 1, 2022
- 103
- 187
Denis ni kijana mwerevu mwenye uwezo mkubwa wa kuamua na kutenda mambo mbali mbali kwa hali
ya juu sana. Ni kijana ambaye amelelewa na familia ya Mr John Kapinga waziri mkuu wa nchi ya
KONGOA.
Mnamo mwaka 2011 akiwa na umri wa miaka 25 jijini London alitunukiwa shahada yake ya
kwanza ya masuala ya komputa akiwa kama mwanafunzi wa kwanza mwenye ufaulu mkubwa sana
kupita wote kwa mwaka huo akiwa na G.P.A ya 5.0 na kuweka historia ya kuwa mwanafunzi wa kwanza
kutoka nchi za kiafrika kufanya vizuri zaidi katika masomo hayo ya computa ndani ya chuo hicho kikuu
cha Oxford.
Alisomea maswala ya mtandao yaani (networking), ni mtu hatari na mbobezi aliyekuwa na uwezo wa
kukusanya taarifa mbalimbali za kiusalama kwa kuingia kwenye kifaa chochote cha mawasiliano na
kupakua taarifa zake na kuzitumia atakavyo bila kujulikana.
Aliporudi KONGOA aliendelea kuitumikia
nchi yake ya kongoa kama afisa usalama mbobezi katika maswala ya mtandao. Usoni mwa watu, Denis
alijulikana kama mtumishi wa kampuni ya simu ya AMATEL Kampuni kubwa ya mawasiliano ya simu
nchini Kongoa.
Alikuwa akiamka hasubui kama watumishi wengine na kuelekea kazini kama watumishi
wengine, na alionekana kama akifanya shughuli za kawaida pale AMATEL kama watumishi wengine
kumbe yeye alikuwa pale kama undercover agent ambaye alikuwa na ofisi yake ya siri ndani ya jengo
hilo kwa ajili ya kuratibu taarifa mbalimbali za nchini Kongoa.
Denis hakuwahi kumfahamu baba yake mzazi, alichukuliwa na familia ya Mr John Kapinga akiwa na umri
wa siku moja hapa duniani, alikuja kufahamu kuwa Mr kapinga sio Baba yake mzazi alipofikisha umri wa
miaka 16 akiwa anahitimu elimu yake ya sekondari ya kidato cha nne kwenda kidato cha tano baada ya
Mr Kapinga kuamua kumweleza ukweli kuhusu historia yake.
Siku hiyo Mr Kapinga baada ya kutoka shuleni kwenye mahafali alimuita na kumweleza Denis kuwa,
aliokotwa barabarani siku ya jumapili mwaka 1989 karibu na geti la Mr kapinga na familia yake wakiwa
wanatoka kanisani na alikuwa amewekwa kwenye boksi jeupe ambalo ndani yake palikuwa na
maandishi yaliyoandikwa “AM SORY” (samahani).
Kwa ushahidi zaidi Mr Kapinga alilichukua boksi lile
alilokuwa amelitunza ndani mwake na karatasi ile aliyoikuta kwenye boksi na akampatia Denis aione,
denis ambaye wakati huo alikuwa anatetemeka huku machozi yakimtiririka kwa mshtuko wa taarifa zile
alipokea vitu vile huku akilia akiwa haamini kile alicho kuwa anaambiwa.
Hakuamini kwa kuwa alijua kabisa Mr Kapinga ndiye baba yake, na mrs kapinga “JULIETH” ndiye mama
yake, kwani ni watu waliomlea vizuri toka hajitambui mpaka kufikia umri wa kujitambua, alijua Kenedy
mtoto wa kwanza wa mr Kapinga ni kaka yake na Poul mtoto wa mwisho wa familia ile ni mdogo wake.
Hakuwahi kuwaza wala kufikiria kabisa kuwa yeye si mtoto wa familia ile kutokana na malezi yaliyo
tolewa kwa upendo mkuu na familia ile.
Zilipita dakika kumi za kulia na kutokuamini alichoambiwa, Alikuwa na maswali mengi sana kwa Mr
Kapinga. Mojawapo ni pale alipomuulliza kuhusu familia yake. Aliuliza kama familia yake ya sasa iliwahi
kufuatilia kama wazazi wake walikuwa ni akina nani alitaka kujua kwanini walimtelekeza, neno AMSORY
lililokutwa limeandikwa kwenye karatasi ile ndani ya boksi lilikuwa na maana gani na Alitaka kujua je ni
baba au mama yake ndie aliyemtelekeza pale nje getini na pia kutaka kujua ni kwa nini walimtelekeza.
majibu aliyoyapata yalizidi kumuumiza zaid Denis kwani alielezwa kuwa mpaka wanafanya mazungumzo
yale taarifa walizo kuwa nazo nikuwa Baba na mama yake wanasadikika walisha fariki dunia na chanzo
cha kifo chao hakikuwahi kujulikania na hivyo hawakuwahi kujulikana wanatokea upande gani mwa nchi
ya KONGOA.
Taarifa za uhakika walizozipata nikuwa alizaliwa katika hospitali ya Mtakatifu John na
ilijulikana hivo baada ya Denis kuokotwa, alipelekwa hospitalini kumuangalia kama anatatizo loloe la
kiafya na yupo nesi aliyemfahamu denis akiwa mchanga kwani nguo alizokuwa amevishwa wakati
anaokotwa ni yeye aliyezitoa kwa mama yake na niyeye aliyemfunga bangili yenye jina lake mkononi
kabla ya kuwaruhusu denis kichanga na mama yake kuondoka.
*************************************************************************************************
ya juu sana. Ni kijana ambaye amelelewa na familia ya Mr John Kapinga waziri mkuu wa nchi ya
KONGOA.
Mnamo mwaka 2011 akiwa na umri wa miaka 25 jijini London alitunukiwa shahada yake ya
kwanza ya masuala ya komputa akiwa kama mwanafunzi wa kwanza mwenye ufaulu mkubwa sana
kupita wote kwa mwaka huo akiwa na G.P.A ya 5.0 na kuweka historia ya kuwa mwanafunzi wa kwanza
kutoka nchi za kiafrika kufanya vizuri zaidi katika masomo hayo ya computa ndani ya chuo hicho kikuu
cha Oxford.
Alisomea maswala ya mtandao yaani (networking), ni mtu hatari na mbobezi aliyekuwa na uwezo wa
kukusanya taarifa mbalimbali za kiusalama kwa kuingia kwenye kifaa chochote cha mawasiliano na
kupakua taarifa zake na kuzitumia atakavyo bila kujulikana.
Aliporudi KONGOA aliendelea kuitumikia
nchi yake ya kongoa kama afisa usalama mbobezi katika maswala ya mtandao. Usoni mwa watu, Denis
alijulikana kama mtumishi wa kampuni ya simu ya AMATEL Kampuni kubwa ya mawasiliano ya simu
nchini Kongoa.
Alikuwa akiamka hasubui kama watumishi wengine na kuelekea kazini kama watumishi
wengine, na alionekana kama akifanya shughuli za kawaida pale AMATEL kama watumishi wengine
kumbe yeye alikuwa pale kama undercover agent ambaye alikuwa na ofisi yake ya siri ndani ya jengo
hilo kwa ajili ya kuratibu taarifa mbalimbali za nchini Kongoa.
Denis hakuwahi kumfahamu baba yake mzazi, alichukuliwa na familia ya Mr John Kapinga akiwa na umri
wa siku moja hapa duniani, alikuja kufahamu kuwa Mr kapinga sio Baba yake mzazi alipofikisha umri wa
miaka 16 akiwa anahitimu elimu yake ya sekondari ya kidato cha nne kwenda kidato cha tano baada ya
Mr Kapinga kuamua kumweleza ukweli kuhusu historia yake.
Siku hiyo Mr Kapinga baada ya kutoka shuleni kwenye mahafali alimuita na kumweleza Denis kuwa,
aliokotwa barabarani siku ya jumapili mwaka 1989 karibu na geti la Mr kapinga na familia yake wakiwa
wanatoka kanisani na alikuwa amewekwa kwenye boksi jeupe ambalo ndani yake palikuwa na
maandishi yaliyoandikwa “AM SORY” (samahani).
Kwa ushahidi zaidi Mr Kapinga alilichukua boksi lile
alilokuwa amelitunza ndani mwake na karatasi ile aliyoikuta kwenye boksi na akampatia Denis aione,
denis ambaye wakati huo alikuwa anatetemeka huku machozi yakimtiririka kwa mshtuko wa taarifa zile
alipokea vitu vile huku akilia akiwa haamini kile alicho kuwa anaambiwa.
Hakuamini kwa kuwa alijua kabisa Mr Kapinga ndiye baba yake, na mrs kapinga “JULIETH” ndiye mama
yake, kwani ni watu waliomlea vizuri toka hajitambui mpaka kufikia umri wa kujitambua, alijua Kenedy
mtoto wa kwanza wa mr Kapinga ni kaka yake na Poul mtoto wa mwisho wa familia ile ni mdogo wake.
Hakuwahi kuwaza wala kufikiria kabisa kuwa yeye si mtoto wa familia ile kutokana na malezi yaliyo
tolewa kwa upendo mkuu na familia ile.
Zilipita dakika kumi za kulia na kutokuamini alichoambiwa, Alikuwa na maswali mengi sana kwa Mr
Kapinga. Mojawapo ni pale alipomuulliza kuhusu familia yake. Aliuliza kama familia yake ya sasa iliwahi
kufuatilia kama wazazi wake walikuwa ni akina nani alitaka kujua kwanini walimtelekeza, neno AMSORY
lililokutwa limeandikwa kwenye karatasi ile ndani ya boksi lilikuwa na maana gani na Alitaka kujua je ni
baba au mama yake ndie aliyemtelekeza pale nje getini na pia kutaka kujua ni kwa nini walimtelekeza.
majibu aliyoyapata yalizidi kumuumiza zaid Denis kwani alielezwa kuwa mpaka wanafanya mazungumzo
yale taarifa walizo kuwa nazo nikuwa Baba na mama yake wanasadikika walisha fariki dunia na chanzo
cha kifo chao hakikuwahi kujulikania na hivyo hawakuwahi kujulikana wanatokea upande gani mwa nchi
ya KONGOA.
Taarifa za uhakika walizozipata nikuwa alizaliwa katika hospitali ya Mtakatifu John na
ilijulikana hivo baada ya Denis kuokotwa, alipelekwa hospitalini kumuangalia kama anatatizo loloe la
kiafya na yupo nesi aliyemfahamu denis akiwa mchanga kwani nguo alizokuwa amevishwa wakati
anaokotwa ni yeye aliyezitoa kwa mama yake na niyeye aliyemfunga bangili yenye jina lake mkononi
kabla ya kuwaruhusu denis kichanga na mama yake kuondoka.
*************************************************************************************************