Ya kwangu iliisha 2008 na mpaka leo nadunda na corolla yangu kama kawaida...! Road Licence ni sawa sawa na ile iliyokuwa inaitwa "kodi ya kichwa"...! Ni wizi tu...!
Mkuu Kiriku siku hizi utawakuta traffic wakiwa pamoja na mijamaa ya TRA na ile mijamaa mingine ya fire yaani Tanzania kuna kodi nyingi hadi kichwa kinauma.
Kuna dalili ya kuingia mjini kwa kibali cha jiji kama bodaboda! Serikali inatafuta mbinu zote kuingiza mapato ya nchi.
haya bana...Nimesha ku-tick kwenye attendance.
Hawa wahuni wanatafuta mapato ili waweze kwenda kustarehe huko New-York wakati wake na dada zetu wanazalia sakafuni!!!
Mhhh..ngoja nichanganye na zangu......Gari yangu hailipiwi hzo kodi ndogondogo na hata plate namba natumia fake na sijawahi kuulizwa na nmeingia nalo hadi posta mara kibao tu nadhani hua wanaangalia na mtu mwenyewe lkn mm hua ukinisimamisha napiga lugha ya malkia mwanzo mwisho na hv wengi wao vilaza tena naminya ulimi mwisho nasiki MR AROVERA GO!
Mkuu hii ndio tutalia zaidi.......kupitia mafuta ndio tutaumia zaidi........wanatujua watanzania....hatujali....kama PAYE tunakatwa lakini haituumi utadhani tunalipiwa na mwajiri.......
Fikiria waongeze hata 300 kwa lita.....kama unatumia lita 5 kwa siku utalipia 1500 then kwa mwaka Approx 540,000
Halafu "wakimnjunjia" vimada wake utaona reaction yake yenye true vengeance na mateso kwa wasio na hatia kama ilivyomtokea mzee wa watu Nguza.
Mie 2009, na nipo nipo sana.
Ni kama ule mkopo wa chuo, silipi hata kwa upinde.
Nimemshangaa sana, mie fees hizi nalipa nikiamua.
Kuvunja sheria ni hobby na haifundishiki, kuna raha yake. Hasa kama kosa lenyewe dogo kama hili.
Na ukitaka kujipima, jiulize, shuleni ulikuwa kati ya watiifu au watukutu? Kama ni mtukutu, ulikuwa mtukutu kwa hiari au kwa kulazimishwa na mazingira. Kama ulikuwa mtukutu wa hiari, trafiki hakushiki kwa road licence tu.