Don san tan
JF-Expert Member
- May 23, 2015
- 562
- 433
RIWAYA: HUJUMA 1
MTUNZI: richard R. MWAMBE
UTANGULIZI
Tanzania inasonga katika nyanja ya sayansi na teknolojia, inapate uwezo wa kutengeneza silaha kubwa na za kisasa, vitu mbalimbali vya thamani na weredi wa hali yajuu.
Meli kubwa ya kivita ya JW inatekwa na maharamia wakiwa na lengo la kupora makombora makubwa yaliyokuwa yakisafirishwa kwenda ng'ambo.
Jw inaingia katika mgogoro mzito na watekaji wa meli hiyo wasio na chembe ya huruma......
Richard Mwambe anakuja tena na riwaya HUJUMA... keti nae jamvini mwanzo mwisho upate kujua nani kahujumu na kwa nini HUJUMA?
CHAPISHO LA 01
1
Bahari ya indi
MANOWARI ya kijeshi kubwa kabisa ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kikosi cha wanamaji cha Kigamboni ilikuwa ikikata maji kwa kasi, ikitokea Tanzania kuelekea Urusi. Ilikuwa ni safari ya kusafirisha makombora kumi na mbili ya kisasa, makubwa yenye nguvu, makombora ya kisasa ambayo Urusi na Tanzania zilishirikiana kuyaunda ndani ya ardhi ya Tanzania. Kiwanda kikubwa kilikuwa kimejengwa maeneo ya pwani ya Mtwara eneo la Msanga mkuu, maalum kwa kazi hiyo.
Baada ya uchunguzi wa muda mrefu uliochukua takribani miaka kumi na tano hatimaye wataalamu wa milipuko wa jeshi la Urusi na wale wa Tanzania walikuwa wamekamilisha kuunda makombora hayo yenye nguvu aina ya R-36 ambayo teknolojia yake ni ya kule Urusi tangu miaka mingi ‘Intercontinental ballistic missile’, yenye urefu wa mita 32.2 (futi 106) na kipenyo cha mita 3.05 (futi 10), linaloweza kusafiri kwa kasi ya kilomita isiyopungua 7.9 kwa sekunde. Ni makombora yanayokwenda kasi ya ajabu na yenye mlipuko usio wa kawaida. Baada ya kuundwa katika kituo hicho maalum huko Msanga mkuu, Mtwara, sasa yalikuwa yakipelekwa kwa majaribio katika jangwa kubwa la Ryn lililoko Kusini Mashariki mwa Urusi, Maghalibi mwa Khazakistan, Kaskazini mwa bahari ya Caspian. Manowari kubwa ya Tanzania Kirov Class yanye urefu wa futi 827 iliyotengenezwakati ya miaka ya 1970 na 1990 huko Urusi na kuiuza kwa serikali ya Tanzania ndiyo ilifanya kazi hiyo ya kubeba makombora hayo makubwa kumi na mbili kuyapeleka huko bahari ya Caspian kwa majaribio.
Wanamaji waliokuwa ndani ya meli hiyo walikuwa wakiendelea kula raha kwa kucheza michezo mbalimbali kama bao, karata, draft na mingineyo mingi huku manaodha nao wakiwa kwenye kebini yao wakabadilishana mawazo. Wengi wa wanamaji hao walikuwa kutoka Tanzania na wacahache walikuwa kutoka Urusi, jumla yao ilikuwa ni kama ishirini na tano hivi. Ilikuwa ni wakati wa pekee wa wapiganaji hawa kubadilishana uzoefu wa kazi yao, ukiachilia wanamaji hao pia kati yao kulikuwa na wataalam wa milipuko nao walikuwamo. Siku hizo kulikuwa na wimbi kubwa la utekeji meli za mizigo, mafuta na nyinginezo katika bahari ya Indi hasa eneo la Somalia.
Usiku wa manane kila mtu akiwa kasinzia katika lile saa la shetani yaani saa nane kwenda saa tisa, kila mmoja alijibwaga ndani ya kitanda chake akiwa kabebwa na usingizi wa ajabu, kwa kuwa chombo hicho kilikuwa kikijiongoza kwa mitambo maalumu ya kompyuta hakikuwapa tabu waongozaji kujipumzisha japo kwenye viti vyao.
Mara ghafla kioo kikubwa katika chumba cha nahodha kilipasuka na kumwagika sakafuni, nahodha mmoja alishtuka kwa kelele za kioo hicho na upepo mkali ulikuwa ukiingia ndani ukipeperusha karatasi huku na kule, wasaidizi wa nahodha huyo nao wakaamka lakini kabla hawajakaa sawa, mmoja alibamizwa ukutani alikuwa amerushwa kwa risasi nzito ya mdunguaji, damu ikaanza kumwagika, kabla nahodha hajaminya ile nobu ya kengele ya hatari, naye alijikuta chali kifua chote kikiwa fumu kwa risasi nyingine ya mdunguaji. Msaidizi mmoja aliyebaki akaona isiwe tabu akaamua kutimua mbio kutoka chumba cha nahodha ili kuwahi mlango wa kuingia ndani ambako wengine walikuwa wamelala, alipotoka tu kwenye deki akajikuta akimulikwa na mwanga mkali sana uliomfanya ajizibe macho asiweze kuuona.
Helkopta kubwa ya kijeshi ilikuwa angani si mbali sana na uwanja wa meli hiyo ambao uliweza kuruhusu helkopta kama hiyo kutua juu yake, alipotaka kukimbia tena la haikuwezekana, alitunguliwa risasi ya mgongo na kujibwaga chini kwa kiwewe kilichomshika akakimbia na kujitumbukiza baharini, lile helkopta likashuka taratibu na kukanyaga sehemu ya juu ya manowari hiyo.
Giza nene likaivamia meli hiyo ghafla, kila mtu akashtuka ndani ya meli hiyo na kukurupuka kujiweka sawa kujua kulikoni, wamechelewa. Kila kona kulikuwa kumetanda watu walioficha nyuso zao wakiwa na silaha nzito za kisasa za kivita, walikuwa ni wengi maana mara tu baada ya ile helkopta kutua zilifuata boti nyingi ziendazo kasi zikaizunguka manowari ile, Maharamia. Kiongozi wa wale maharamia akatoa amri ya kuikagua ile manowari, na kuhakikisha kila binadamu mwenye uhai anateremshwa. Wale wapiganaji wote wakatolewa nje na kuwekwa mstari mmoja huku wakimulikwa na taa kubwa la ile helkopta.
“Karibuni sana Somalia, hii ndiyo Pwani ya Shetani, asikwambie mtu, hapa kila goti litapigwa,” yule Kiongozi alikuwa akiongea kwa kujigamba huku mkononi mwake amekamata bunduki kubwa yenye kilo nyingi, usoni akiwa kijifunika na soksi jeusi ili hasionekane uso wake, akatoa amri myingine na wale wafuasi wake wakawafunga kamba wale wapiganaji na kuwavisha kila mmoja soksi usoni baada ya kuwavua makombati waliovaa juu.
Kishapo wakawapakia kwenye boti zao na kuondoka nao eneo lile. Maharamia wanaojua kuongoza vyombo kama hivyo waka shika usukani wa Manowari hiyo kubwa kabisa na kuigeuza kuipeleka pwani ya Somalia, Mogadishu.
MOGADISHU
Maharamia waliwafikisha mateka wao katika pwani ya Mogadishu na kuwashusha wakiwaswaga mpaka kwenye malori yaliyokwisha andaliwa kisha wakaondoka nao kuelekea kusikojulikana.
Alkadhalika, ile manowari nayo ilifikishwa Mogadishu na mara moja usiku ule ule ilianza kazi ya kupakuwa yale makombora na kuyaficha kwenye ghala kubwa lililojengwa chini ya maji karibu kabisa na bandari kuu ya Mogadishu, yalifichwa hivyo ili kama wakija kuwakomboa wenzao basi waikute meli tupu kisha wale maharamia nao wakaondoka eneo lile.
§§§§§
Jamhuuriyadda Federaalka Soomaaliya, ‘Jamhuri ya Shirikisho la Somalia’, ni nchi iliyoko katika pembe ya Afrika, sehemu kubwa upande wa Mashariki ni bahari ya Indi. Somalia ni nchi iliyokuwa katika mapigano ya wenyewe kwa wenyewe kwa kipindi kirefu na vikundi mbalimbali vya kigaidi kama Al-Shabab walitokea ndani ya nchi hiyo kutokana na tofauti za kisiasa.
Wimbi la utekaji vyombo vya majini liliibuka katika pwani ya nchi hiyo na kulaaniwa na kila taifa, kila serikali, kila taasisi ya kibinadamu duniani zikitoa wito kwa mataifa makubwa kukomesha uharamia huo.
Ilikuwa ni vigumu sana kutimiza lengo hilo la kukomesha wimbi la utekaji vyombo vya majini, haikujulikana sababu ni nini hasa ya kushindikana kwa juhudi hizo. Ilikuwa ni kitendawili kisicho na mteguaji. Hali kwa ujumla ilikuwa ni ya kuogofya katika eneo hilo, maharamia wa Somalia walikuwa hawaogopi hata sheria za maji makubwa, wao walichojua ni kuteka meli ilimradi wapate pesa, ukiwaona maharamia hao wanavovaa utasema ni masikini wakutupwa, lakini majumba hayo wanayomiliki ndani ya mji wa Mogadishu na viunga vyake ni kufuru kwa nchi hiyo isiyo na serikali kwa kipindi kirefu, kila mtu akiwa anajiamulia madaraka yake mkononi.
§§§§§
Jazeera Palace Hotel
Saa 2:10 asubuhi
Pembezoni kabisa mwa barabara ya Uwanja wa ndege ‘Airport road’,gari aina ya Jaguar nyeusi ilikuwa ikikunja kona kuingia katika hoteli ya Jazeera Palace asubuhi hiyo, moja kwa moja ikaingia katika maegesho na kuegeshwa sawasawa kabisa. Bwana mmoja wa makamo akateremka kutoka katika katika gari hiyo ya kifahari na kuuendea mgahawa wa hotel hiyo akachagua siti moja na kuketi. Haikupita hata dakika tano akaja mtu mwingine mnene kiasi mwenye upara unaong’aa ulioonekana wazi baada ya kuvua ile balaghashia yake na kuiweka mezani.
“Nipe habari,” yule bwana mwenye upara akamwambia Yule mwingine.
“Kila kitu tayari mzigo tunao, kilichobaki ni kuhesabiana tu, sisi wenyewe tunajua jinsi ya kuifikisha mahali husika,” alijibu bwana Shalabah, kiongozi wa maharamia. Ilikuwa ni biashara kubwa ya pesa nyingi za kigeni, nah ii ndio hasa waliokuwa wakiifanya maharamia hawa, safari hii walikuwa wamefanya biashara kubwa ya makombora hayo mazito.
“Ok, hatuna muda wa kupoteza, pesa iko tayari lini?” bwana Shalabah alimuuliza Yule mwenye upara.
“Pesa, pesa kitu gani? Kama wewe tayri una mzigo basi pesa utapata,” Yule mwenye upara alijibu.
“Kuna makombora 12, yenye uzito wa hali ya juu, ukipiga New York mpaka Ontario watatetemeka kwa hofu,” bwana Shalabah alimweleza Yule mwenye upara umadhubuti wa makombora hayo.
“Umenishtua sana, usijali nitwasiliana na washika dau ili tuyachukue yote 12 tuyapeleke huko maskani, sasa yako wapi japo niyaone,” Yule mwenye upara akamwambia Shalabah.
”Huwezi kuyaona, na wala hutakiwi kujua yako wapi, unachotakiwa kufanya wewe ni kuwasiliana na watu wako ili tufanye biashara, basi, hakuna kingine,” Shalabah alimueleza. Kisha akavuta mkoba wake na kufungua, akatoka kijitabu Fulani wakaandikiana mawasiliano yao na kisha wakaagana, kila mtu akachukua hamsini zake.
Shalabah akaikunja miguu yake na kuiweka kwa mtindo wa nne na kuagiza kinywaji kikali, alipoletewa alikuwa akinywa taratibu akisubiri miadi mingine, mara hii ya watu wake. Haikupita hata saa moja vijana watatu warefu, wembamba wakaingia na land cruiser pick up, wakateremka na kuungana naye katika kinywaji hicho.
MTUNZI: richard R. MWAMBE
UTANGULIZI
Tanzania inasonga katika nyanja ya sayansi na teknolojia, inapate uwezo wa kutengeneza silaha kubwa na za kisasa, vitu mbalimbali vya thamani na weredi wa hali yajuu.
Meli kubwa ya kivita ya JW inatekwa na maharamia wakiwa na lengo la kupora makombora makubwa yaliyokuwa yakisafirishwa kwenda ng'ambo.
Jw inaingia katika mgogoro mzito na watekaji wa meli hiyo wasio na chembe ya huruma......
Richard Mwambe anakuja tena na riwaya HUJUMA... keti nae jamvini mwanzo mwisho upate kujua nani kahujumu na kwa nini HUJUMA?
CHAPISHO LA 01
1
Bahari ya indi
MANOWARI ya kijeshi kubwa kabisa ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kikosi cha wanamaji cha Kigamboni ilikuwa ikikata maji kwa kasi, ikitokea Tanzania kuelekea Urusi. Ilikuwa ni safari ya kusafirisha makombora kumi na mbili ya kisasa, makubwa yenye nguvu, makombora ya kisasa ambayo Urusi na Tanzania zilishirikiana kuyaunda ndani ya ardhi ya Tanzania. Kiwanda kikubwa kilikuwa kimejengwa maeneo ya pwani ya Mtwara eneo la Msanga mkuu, maalum kwa kazi hiyo.
Baada ya uchunguzi wa muda mrefu uliochukua takribani miaka kumi na tano hatimaye wataalamu wa milipuko wa jeshi la Urusi na wale wa Tanzania walikuwa wamekamilisha kuunda makombora hayo yenye nguvu aina ya R-36 ambayo teknolojia yake ni ya kule Urusi tangu miaka mingi ‘Intercontinental ballistic missile’, yenye urefu wa mita 32.2 (futi 106) na kipenyo cha mita 3.05 (futi 10), linaloweza kusafiri kwa kasi ya kilomita isiyopungua 7.9 kwa sekunde. Ni makombora yanayokwenda kasi ya ajabu na yenye mlipuko usio wa kawaida. Baada ya kuundwa katika kituo hicho maalum huko Msanga mkuu, Mtwara, sasa yalikuwa yakipelekwa kwa majaribio katika jangwa kubwa la Ryn lililoko Kusini Mashariki mwa Urusi, Maghalibi mwa Khazakistan, Kaskazini mwa bahari ya Caspian. Manowari kubwa ya Tanzania Kirov Class yanye urefu wa futi 827 iliyotengenezwakati ya miaka ya 1970 na 1990 huko Urusi na kuiuza kwa serikali ya Tanzania ndiyo ilifanya kazi hiyo ya kubeba makombora hayo makubwa kumi na mbili kuyapeleka huko bahari ya Caspian kwa majaribio.
Wanamaji waliokuwa ndani ya meli hiyo walikuwa wakiendelea kula raha kwa kucheza michezo mbalimbali kama bao, karata, draft na mingineyo mingi huku manaodha nao wakiwa kwenye kebini yao wakabadilishana mawazo. Wengi wa wanamaji hao walikuwa kutoka Tanzania na wacahache walikuwa kutoka Urusi, jumla yao ilikuwa ni kama ishirini na tano hivi. Ilikuwa ni wakati wa pekee wa wapiganaji hawa kubadilishana uzoefu wa kazi yao, ukiachilia wanamaji hao pia kati yao kulikuwa na wataalam wa milipuko nao walikuwamo. Siku hizo kulikuwa na wimbi kubwa la utekeji meli za mizigo, mafuta na nyinginezo katika bahari ya Indi hasa eneo la Somalia.
Usiku wa manane kila mtu akiwa kasinzia katika lile saa la shetani yaani saa nane kwenda saa tisa, kila mmoja alijibwaga ndani ya kitanda chake akiwa kabebwa na usingizi wa ajabu, kwa kuwa chombo hicho kilikuwa kikijiongoza kwa mitambo maalumu ya kompyuta hakikuwapa tabu waongozaji kujipumzisha japo kwenye viti vyao.
Mara ghafla kioo kikubwa katika chumba cha nahodha kilipasuka na kumwagika sakafuni, nahodha mmoja alishtuka kwa kelele za kioo hicho na upepo mkali ulikuwa ukiingia ndani ukipeperusha karatasi huku na kule, wasaidizi wa nahodha huyo nao wakaamka lakini kabla hawajakaa sawa, mmoja alibamizwa ukutani alikuwa amerushwa kwa risasi nzito ya mdunguaji, damu ikaanza kumwagika, kabla nahodha hajaminya ile nobu ya kengele ya hatari, naye alijikuta chali kifua chote kikiwa fumu kwa risasi nyingine ya mdunguaji. Msaidizi mmoja aliyebaki akaona isiwe tabu akaamua kutimua mbio kutoka chumba cha nahodha ili kuwahi mlango wa kuingia ndani ambako wengine walikuwa wamelala, alipotoka tu kwenye deki akajikuta akimulikwa na mwanga mkali sana uliomfanya ajizibe macho asiweze kuuona.
Helkopta kubwa ya kijeshi ilikuwa angani si mbali sana na uwanja wa meli hiyo ambao uliweza kuruhusu helkopta kama hiyo kutua juu yake, alipotaka kukimbia tena la haikuwezekana, alitunguliwa risasi ya mgongo na kujibwaga chini kwa kiwewe kilichomshika akakimbia na kujitumbukiza baharini, lile helkopta likashuka taratibu na kukanyaga sehemu ya juu ya manowari hiyo.
Giza nene likaivamia meli hiyo ghafla, kila mtu akashtuka ndani ya meli hiyo na kukurupuka kujiweka sawa kujua kulikoni, wamechelewa. Kila kona kulikuwa kumetanda watu walioficha nyuso zao wakiwa na silaha nzito za kisasa za kivita, walikuwa ni wengi maana mara tu baada ya ile helkopta kutua zilifuata boti nyingi ziendazo kasi zikaizunguka manowari ile, Maharamia. Kiongozi wa wale maharamia akatoa amri ya kuikagua ile manowari, na kuhakikisha kila binadamu mwenye uhai anateremshwa. Wale wapiganaji wote wakatolewa nje na kuwekwa mstari mmoja huku wakimulikwa na taa kubwa la ile helkopta.
“Karibuni sana Somalia, hii ndiyo Pwani ya Shetani, asikwambie mtu, hapa kila goti litapigwa,” yule Kiongozi alikuwa akiongea kwa kujigamba huku mkononi mwake amekamata bunduki kubwa yenye kilo nyingi, usoni akiwa kijifunika na soksi jeusi ili hasionekane uso wake, akatoa amri myingine na wale wafuasi wake wakawafunga kamba wale wapiganaji na kuwavisha kila mmoja soksi usoni baada ya kuwavua makombati waliovaa juu.
Kishapo wakawapakia kwenye boti zao na kuondoka nao eneo lile. Maharamia wanaojua kuongoza vyombo kama hivyo waka shika usukani wa Manowari hiyo kubwa kabisa na kuigeuza kuipeleka pwani ya Somalia, Mogadishu.
MOGADISHU
Maharamia waliwafikisha mateka wao katika pwani ya Mogadishu na kuwashusha wakiwaswaga mpaka kwenye malori yaliyokwisha andaliwa kisha wakaondoka nao kuelekea kusikojulikana.
Alkadhalika, ile manowari nayo ilifikishwa Mogadishu na mara moja usiku ule ule ilianza kazi ya kupakuwa yale makombora na kuyaficha kwenye ghala kubwa lililojengwa chini ya maji karibu kabisa na bandari kuu ya Mogadishu, yalifichwa hivyo ili kama wakija kuwakomboa wenzao basi waikute meli tupu kisha wale maharamia nao wakaondoka eneo lile.
§§§§§
Jamhuuriyadda Federaalka Soomaaliya, ‘Jamhuri ya Shirikisho la Somalia’, ni nchi iliyoko katika pembe ya Afrika, sehemu kubwa upande wa Mashariki ni bahari ya Indi. Somalia ni nchi iliyokuwa katika mapigano ya wenyewe kwa wenyewe kwa kipindi kirefu na vikundi mbalimbali vya kigaidi kama Al-Shabab walitokea ndani ya nchi hiyo kutokana na tofauti za kisiasa.
Wimbi la utekaji vyombo vya majini liliibuka katika pwani ya nchi hiyo na kulaaniwa na kila taifa, kila serikali, kila taasisi ya kibinadamu duniani zikitoa wito kwa mataifa makubwa kukomesha uharamia huo.
Ilikuwa ni vigumu sana kutimiza lengo hilo la kukomesha wimbi la utekaji vyombo vya majini, haikujulikana sababu ni nini hasa ya kushindikana kwa juhudi hizo. Ilikuwa ni kitendawili kisicho na mteguaji. Hali kwa ujumla ilikuwa ni ya kuogofya katika eneo hilo, maharamia wa Somalia walikuwa hawaogopi hata sheria za maji makubwa, wao walichojua ni kuteka meli ilimradi wapate pesa, ukiwaona maharamia hao wanavovaa utasema ni masikini wakutupwa, lakini majumba hayo wanayomiliki ndani ya mji wa Mogadishu na viunga vyake ni kufuru kwa nchi hiyo isiyo na serikali kwa kipindi kirefu, kila mtu akiwa anajiamulia madaraka yake mkononi.
§§§§§
Jazeera Palace Hotel
Saa 2:10 asubuhi
Pembezoni kabisa mwa barabara ya Uwanja wa ndege ‘Airport road’,gari aina ya Jaguar nyeusi ilikuwa ikikunja kona kuingia katika hoteli ya Jazeera Palace asubuhi hiyo, moja kwa moja ikaingia katika maegesho na kuegeshwa sawasawa kabisa. Bwana mmoja wa makamo akateremka kutoka katika katika gari hiyo ya kifahari na kuuendea mgahawa wa hotel hiyo akachagua siti moja na kuketi. Haikupita hata dakika tano akaja mtu mwingine mnene kiasi mwenye upara unaong’aa ulioonekana wazi baada ya kuvua ile balaghashia yake na kuiweka mezani.
“Nipe habari,” yule bwana mwenye upara akamwambia Yule mwingine.
“Kila kitu tayari mzigo tunao, kilichobaki ni kuhesabiana tu, sisi wenyewe tunajua jinsi ya kuifikisha mahali husika,” alijibu bwana Shalabah, kiongozi wa maharamia. Ilikuwa ni biashara kubwa ya pesa nyingi za kigeni, nah ii ndio hasa waliokuwa wakiifanya maharamia hawa, safari hii walikuwa wamefanya biashara kubwa ya makombora hayo mazito.
“Ok, hatuna muda wa kupoteza, pesa iko tayari lini?” bwana Shalabah alimuuliza Yule mwenye upara.
“Pesa, pesa kitu gani? Kama wewe tayri una mzigo basi pesa utapata,” Yule mwenye upara alijibu.
“Kuna makombora 12, yenye uzito wa hali ya juu, ukipiga New York mpaka Ontario watatetemeka kwa hofu,” bwana Shalabah alimweleza Yule mwenye upara umadhubuti wa makombora hayo.
“Umenishtua sana, usijali nitwasiliana na washika dau ili tuyachukue yote 12 tuyapeleke huko maskani, sasa yako wapi japo niyaone,” Yule mwenye upara akamwambia Shalabah.
”Huwezi kuyaona, na wala hutakiwi kujua yako wapi, unachotakiwa kufanya wewe ni kuwasiliana na watu wako ili tufanye biashara, basi, hakuna kingine,” Shalabah alimueleza. Kisha akavuta mkoba wake na kufungua, akatoka kijitabu Fulani wakaandikiana mawasiliano yao na kisha wakaagana, kila mtu akachukua hamsini zake.
Shalabah akaikunja miguu yake na kuiweka kwa mtindo wa nne na kuagiza kinywaji kikali, alipoletewa alikuwa akinywa taratibu akisubiri miadi mingine, mara hii ya watu wake. Haikupita hata saa moja vijana watatu warefu, wembamba wakaingia na land cruiser pick up, wakateremka na kuungana naye katika kinywaji hicho.