gilbert35
JF-Expert Member
- Nov 20, 2021
- 247
- 474
SIMULIZI; TAHARURI
Imeandikwa na Halfani Sudy
Whatsapp; 0652212391
Hii ni Sehemu ya Kwanza
Kwa mara ya tatu sasa simu ya Catherine iliyokuwa imelala pweke juu ya kitanda chake ilikuwa inaita. Simu iliita kwa mara nyingine tena mpaka ikakatika, hakukuwa na mpokeaji wa simu ile.
Catherine, alikuwa yupo bafuni mwake, akiipitisha taratibu sabuni yenye manukato mazuri katika mwili wake wa kirembo. Sabuni ilikuwa ikipitishwa na mkono laini maeneo mbalimbali ya mwili huo, huku ikiacha povu lililoambatana na harufu nzuri sana. Hakuwa na haraka, na hii ilikuwa ni kawaida yake siku zote akiingia bafuni.
Alikuwa anatumia zaidi ya dakika arobaini ili kuhakikisha mwili wake mzuri umetakata vilivyo. Baada ya kuhakikisha zoezi lake la kuutakatisha mwili wake kukamilika, alifungulia tena bomba la maji, maji yalikuwa yanatiririka kutokea juu mithili ya mvua za rasharasha, maji yaliyopata bahati ya kudondokea juu ya mwili mzuri sana wa Catherine.
Catherine Simon Madoshi, alikuwa ni msichana mwenye umri wa miaka ishirini na moja. Alikuwa na urefu wa wastani, urefu uliopata bahati ya kuvikwa katika mwili mzuri sana. Alikuwa ni kati ya wasichana wachache tunaoweza kusema kuwa walibarikiwa na Muumba.
Alikuwa na uzuri wa umbo, sura na sauti. Ungelipata bahati ya kumuona ungeliweza sema kuwa kama alipata bahati ya kujichagulia jinsi alivyotaka awe kwa Muumba.
Katika umri huo mdogo, Catherine alikuwa anamiliki maduka matatu makubwa ya nguo za kike, huku brand yake ya Cathy Clothing Line ikiwa inakuwa kwa kasi kubwa sana nchini Tanzania. Catherine, alikuwa ameingia mkataba na msanii maarufu sana wa kike, ambaye alimsaidia sana kuipaisha brand yake ya nguo za kike. Huku Cathirine mwenyewe, akiwa ni mwanamitindo aliyeibuka ghafla na moja kwa moja kukimbilia katika kilele cha uanamitindo.
Wiki moja iliyopita, alikuwa ametoka kukabidhiwa taji kubwa sana la uanamitindo wa Afrika, nchini Afrika ya Kusini. Baada ya kulitwaa taji hilo, jina la Catherine lilipaa mithili ya tiara, na kujaa katika kila mdomo wa mtanzania mpenda mitindo. Catherine ilikuwa ni nyota mpya iliyong’ara katikati ya mzimu wa kushindwa kwa nchi ya Tanzania katika mashindano mbalimbali ya urembo na ulimbwende.
Catherine alitoka bafuni baada ya kumaliza kuoga, akiwa amejifunga kwa taulo jeupe lililopita juu kidogo ya matiti yake madogo. Alifungua mlango wa bafu na kutokea chumbani kwake. Moja kwa moja alielekea mbele ya kabati lake lililokuwa na kioo kikubwa. Macho yake yalikuwa yanautazama mwili wake mzuri kiooni.
Alidumu akijitazama kwa dakika zipatazo tano, kisha alitabasamu mwenyewe, tabasamu ambalo lililoongeza urembo wake maradufu. Alilitoa taulo lake mwilini na kulitupia juu ya sofa pekee lililokuwemo mle ndani. Sasa alibaki mtupu, mwili wake laini usio na doa hata la bahati mbaya ukiwa mbele ya kioo.
Alichukua kopo la mafuta, akalifungua, kisha akatosa kidole chake cha shahada. Kidole kikiwa kinazama taratibu katikati ya mafuta ndipo simu yake iliita tena. Catherine alikitoa kidole katika mafuta na kugeuka nyuma, alielekea mahali kilipo kitanda.
Aliichukua simu yake kwa mkono wa kushoto, alisoma jina la mtu aliyekuwa anapiga,
“Sweetheart..,” alisema kwa sauti ndogo, kisha akaipokea.
“Habari za sahivi mpenzi,” Catherine alisema kwa sauti yake laini ya kudeka baada ya kupokea simu.
“Unaongea na Sauti Simuni, tunamshikilia mpenzi wako, utafuata maelekezo yetu kama unapenda kumwona jamaa yako akiendelea kupumua!”
Sauti kavu, ya kiume ilisema simuni bila ya wasiwasi wowote ule.
Mstuko uliompata Catherine ulikuwa hauna mfano. Alibaki ameganda kama sanamu akiwa mtupu chumbani, mkono wake wa kushoto ukiwa vilevile sikioni, kilichoongezeka ni majimaji laini yakiyoshuka katika mashavu yake, Catherine alikuwa analia.
“Hallo, hallo, bila shaka unanisikia, tutakupa maelelekezo ya nini cha kufanya baada ya dakika tano. Usijaribu kumwambia mtu yeyote juu ya jambo hili, tunaifatilia kila hatua yako.” Simu ikakatwa.
Catherine alibaki kimya, mkono wake wenye simu bado ukiwa sikioni. Lakini ubongo wake ulisafiri mbali sana, aliikumbuka siku ya kwanza aliyokutana na Martin Mbaga.
Sherehe ilikuwa inakaribia kufika tamati. Waalikwa na wageni mbalimbali walikunywa, kula na kusaza, lakini bado vyakula na vinywaji vilibaki vingi sana. Ilikuwa ni katika sherehe ya harusi kubwa sana jijini Dar es salaam. Tajiri namba moja nchini Tanzania, Bilionea Khatibu Zawiya alikuwa anamuoa mtoto wa kike wa waziri wa mambo ya ndani, mheshimiwa Almas Fumbo. Harusi iliyolitikisa jiji la Dar es salaam kwa takribani miezi mitatu leo hii ilikuwa inafikia tamati.
Ndani ya ukumbi kulijaa watu wengi wenye nyadhifa mbalimbali. Kulikuwa na wanasiasa wakubwa sana, wafanyabiashara matajiri na watu maarufu mbalimbali. Miongoni mwa watu maarufu waliopata bahati ya kualikwa katika sherehe hiyo ni Catherine, ikiwa ni wiki moja tu tangu atoke kutunukiwa taji la Mwanamitindo bora wa Afrika.
Catherine alikuwa amekaa upande wa kushoto wa ukumbi wa Mlimani city, sehemu ambayo kulikuwa na watu maarufu mbalimbali, kulikuwa na wanamuziki wakubwa, wachezaji wa mpira wa miguu maarufu na waigizaji mbalimbali wa filamu waliokuwa wanatamba katika kurasa za mbele za magazeti. Ilikuwa ni siku ya furaha sana kwake kukaa karibu na watu ambao hakuwahi hata kuwaza kama ipo siku atakaa karibu nao kwa kiasi hicho. Mmoja wa watu hao, alikuwepo Martin Mbaga....
Catherine aligutushwa kutoka mawazoni baada ya simu yake kuita, simu iliyokuwa bado imeganda katika sikio lake tangu alivyotoka kuongea na mtu aliyejitambulisha kwa jina la Sauti Simuni. Aliangalia mtu aliyekuwa anapiga simu ile, ilikuwa ni namba ileile ya Martin. Hofu ilimpanda marudufu, alishuhudia jinsi vidole vyake mwenyewe vilivyokuwa vinatetemeka, huku vikiwa vimeloa jasho. Hali hii ilikuwa inamtokea mara zote anapopatwa na hali ya uwoga kupitiliza.
Aliipokea,
“Ninashukuru sana kwa kufata maelekezo yetu ya kutomwambia mtu yeyote kuhusu simu yangu. Sasa unachotakiwa kufanya ili kuokoa maisha ya mpenzi wako, kwanza vaa nguo zako..” Kauli hii ilimstua sana Catherine, “Inamaana ananiona?” alijiuliza kwa sauti ndogo iliyosikiwa na sikio la Sauti Simuni.
“Hiyo sio kazi yako kujua, nimekwambia fuata maelekezo yangu. Vaa nguo zako zile ulizovaa katika sherehe ya harusi ya Bilionea Khatibu Zawia. Acha simu juu ya kitanda chako. Utatoka nje ya geti lako, utakuta gari ndogo nyekundu imepaki upande wa pili wa barabara, utaenda kupanda katika mlango wa kati. Ukiingia tu gari itaondoka, hutakiwi kuongea kitu chochote kile na dereva wa gari hilo.
Dereva atakupeleka hadi katika nyumba moja, utashuka na kuingia ndani ya nyumba hiyo, katika eneo la maegesho la magari utamkuta kijana mmoja atakayekuwa amevaa kanzu nyeupe na barghashia, utamwambia,
“ Nimefuata mzigo”.
Huyo kijana ataingia ndani na kutoka na begi jeusi. Utachukua begi hilo na kutoka nalo nje. Utakuta gari ya bluu imepaki upande wa pili wa barabara, utaenda kuingia katika mlango wa kati wa gari hilo. Gari itakupeleka hadi uwanja wa ndege, dereva wa hilo gari atakupa nakala zote unazotakiwa kuwa nazo unaposafiri.
Utapanda ndege inayoelekea jijini Nairobi saa mbili asubuhi. Ukifika katika uwanja wa ndege wa Nairobi, kuna mtu atakupokea, atakuwa amevaa fulana nyeupe, kwa mbele imeandikwa kwa maandishi meusi ‘OCAFONA’, utampa hilo begi baada ya kuingia ndani ya gari lake atakalokuja nalo uwanjani, kisha yeye atakupa nakala zote za kukuwezesha kurudi jijini Dar es salaam.
Ukifika katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere, utapokelewa na mpenzi wako Martin. Na hapo ndipo utakuwa umeokoa maisha ya mpenzi wako. Kumbuka, tutakuwa tunakufatilia katika kila hatua utakayokanyaga. Katika safari hiyo utakuwa karibu na kifo kuliko wakati wowote ule katika maisha yako. Kosa moja tu, liwe la kukusudia ama la bahati mbaya litakupeleka kuzimu! Nakutakia kazi njema mrembo wangu.....” Simu ikakatwa.
Catherine alipumua kwa nguvu, kichwa chake kilikuwa kina mambo mengi sana ya kufikiria, lakini hakukuwa na muda huo wa kufikiria. Ilimpasa kutekeleza maagizo kwa ajili ya maisha yake, kwa ajili ya kumuokoa mpenzi wake.
Je nini kitatokea? Huu ni mwanzo wa TAHARUKI kutoka kwa mwandishi Halfani Sudy. Like na comment
Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app
Imeandikwa na Halfani Sudy
Whatsapp; 0652212391
Hii ni Sehemu ya Kwanza
Kwa mara ya tatu sasa simu ya Catherine iliyokuwa imelala pweke juu ya kitanda chake ilikuwa inaita. Simu iliita kwa mara nyingine tena mpaka ikakatika, hakukuwa na mpokeaji wa simu ile.
Catherine, alikuwa yupo bafuni mwake, akiipitisha taratibu sabuni yenye manukato mazuri katika mwili wake wa kirembo. Sabuni ilikuwa ikipitishwa na mkono laini maeneo mbalimbali ya mwili huo, huku ikiacha povu lililoambatana na harufu nzuri sana. Hakuwa na haraka, na hii ilikuwa ni kawaida yake siku zote akiingia bafuni.
Alikuwa anatumia zaidi ya dakika arobaini ili kuhakikisha mwili wake mzuri umetakata vilivyo. Baada ya kuhakikisha zoezi lake la kuutakatisha mwili wake kukamilika, alifungulia tena bomba la maji, maji yalikuwa yanatiririka kutokea juu mithili ya mvua za rasharasha, maji yaliyopata bahati ya kudondokea juu ya mwili mzuri sana wa Catherine.
Catherine Simon Madoshi, alikuwa ni msichana mwenye umri wa miaka ishirini na moja. Alikuwa na urefu wa wastani, urefu uliopata bahati ya kuvikwa katika mwili mzuri sana. Alikuwa ni kati ya wasichana wachache tunaoweza kusema kuwa walibarikiwa na Muumba.
Alikuwa na uzuri wa umbo, sura na sauti. Ungelipata bahati ya kumuona ungeliweza sema kuwa kama alipata bahati ya kujichagulia jinsi alivyotaka awe kwa Muumba.
Katika umri huo mdogo, Catherine alikuwa anamiliki maduka matatu makubwa ya nguo za kike, huku brand yake ya Cathy Clothing Line ikiwa inakuwa kwa kasi kubwa sana nchini Tanzania. Catherine, alikuwa ameingia mkataba na msanii maarufu sana wa kike, ambaye alimsaidia sana kuipaisha brand yake ya nguo za kike. Huku Cathirine mwenyewe, akiwa ni mwanamitindo aliyeibuka ghafla na moja kwa moja kukimbilia katika kilele cha uanamitindo.
Wiki moja iliyopita, alikuwa ametoka kukabidhiwa taji kubwa sana la uanamitindo wa Afrika, nchini Afrika ya Kusini. Baada ya kulitwaa taji hilo, jina la Catherine lilipaa mithili ya tiara, na kujaa katika kila mdomo wa mtanzania mpenda mitindo. Catherine ilikuwa ni nyota mpya iliyong’ara katikati ya mzimu wa kushindwa kwa nchi ya Tanzania katika mashindano mbalimbali ya urembo na ulimbwende.
Catherine alitoka bafuni baada ya kumaliza kuoga, akiwa amejifunga kwa taulo jeupe lililopita juu kidogo ya matiti yake madogo. Alifungua mlango wa bafu na kutokea chumbani kwake. Moja kwa moja alielekea mbele ya kabati lake lililokuwa na kioo kikubwa. Macho yake yalikuwa yanautazama mwili wake mzuri kiooni.
Alidumu akijitazama kwa dakika zipatazo tano, kisha alitabasamu mwenyewe, tabasamu ambalo lililoongeza urembo wake maradufu. Alilitoa taulo lake mwilini na kulitupia juu ya sofa pekee lililokuwemo mle ndani. Sasa alibaki mtupu, mwili wake laini usio na doa hata la bahati mbaya ukiwa mbele ya kioo.
Alichukua kopo la mafuta, akalifungua, kisha akatosa kidole chake cha shahada. Kidole kikiwa kinazama taratibu katikati ya mafuta ndipo simu yake iliita tena. Catherine alikitoa kidole katika mafuta na kugeuka nyuma, alielekea mahali kilipo kitanda.
Aliichukua simu yake kwa mkono wa kushoto, alisoma jina la mtu aliyekuwa anapiga,
“Sweetheart..,” alisema kwa sauti ndogo, kisha akaipokea.
“Habari za sahivi mpenzi,” Catherine alisema kwa sauti yake laini ya kudeka baada ya kupokea simu.
“Unaongea na Sauti Simuni, tunamshikilia mpenzi wako, utafuata maelekezo yetu kama unapenda kumwona jamaa yako akiendelea kupumua!”
Sauti kavu, ya kiume ilisema simuni bila ya wasiwasi wowote ule.
Mstuko uliompata Catherine ulikuwa hauna mfano. Alibaki ameganda kama sanamu akiwa mtupu chumbani, mkono wake wa kushoto ukiwa vilevile sikioni, kilichoongezeka ni majimaji laini yakiyoshuka katika mashavu yake, Catherine alikuwa analia.
“Hallo, hallo, bila shaka unanisikia, tutakupa maelelekezo ya nini cha kufanya baada ya dakika tano. Usijaribu kumwambia mtu yeyote juu ya jambo hili, tunaifatilia kila hatua yako.” Simu ikakatwa.
Catherine alibaki kimya, mkono wake wenye simu bado ukiwa sikioni. Lakini ubongo wake ulisafiri mbali sana, aliikumbuka siku ya kwanza aliyokutana na Martin Mbaga.
Sherehe ilikuwa inakaribia kufika tamati. Waalikwa na wageni mbalimbali walikunywa, kula na kusaza, lakini bado vyakula na vinywaji vilibaki vingi sana. Ilikuwa ni katika sherehe ya harusi kubwa sana jijini Dar es salaam. Tajiri namba moja nchini Tanzania, Bilionea Khatibu Zawiya alikuwa anamuoa mtoto wa kike wa waziri wa mambo ya ndani, mheshimiwa Almas Fumbo. Harusi iliyolitikisa jiji la Dar es salaam kwa takribani miezi mitatu leo hii ilikuwa inafikia tamati.
Ndani ya ukumbi kulijaa watu wengi wenye nyadhifa mbalimbali. Kulikuwa na wanasiasa wakubwa sana, wafanyabiashara matajiri na watu maarufu mbalimbali. Miongoni mwa watu maarufu waliopata bahati ya kualikwa katika sherehe hiyo ni Catherine, ikiwa ni wiki moja tu tangu atoke kutunukiwa taji la Mwanamitindo bora wa Afrika.
Catherine alikuwa amekaa upande wa kushoto wa ukumbi wa Mlimani city, sehemu ambayo kulikuwa na watu maarufu mbalimbali, kulikuwa na wanamuziki wakubwa, wachezaji wa mpira wa miguu maarufu na waigizaji mbalimbali wa filamu waliokuwa wanatamba katika kurasa za mbele za magazeti. Ilikuwa ni siku ya furaha sana kwake kukaa karibu na watu ambao hakuwahi hata kuwaza kama ipo siku atakaa karibu nao kwa kiasi hicho. Mmoja wa watu hao, alikuwepo Martin Mbaga....
Catherine aligutushwa kutoka mawazoni baada ya simu yake kuita, simu iliyokuwa bado imeganda katika sikio lake tangu alivyotoka kuongea na mtu aliyejitambulisha kwa jina la Sauti Simuni. Aliangalia mtu aliyekuwa anapiga simu ile, ilikuwa ni namba ileile ya Martin. Hofu ilimpanda marudufu, alishuhudia jinsi vidole vyake mwenyewe vilivyokuwa vinatetemeka, huku vikiwa vimeloa jasho. Hali hii ilikuwa inamtokea mara zote anapopatwa na hali ya uwoga kupitiliza.
Aliipokea,
“Ninashukuru sana kwa kufata maelekezo yetu ya kutomwambia mtu yeyote kuhusu simu yangu. Sasa unachotakiwa kufanya ili kuokoa maisha ya mpenzi wako, kwanza vaa nguo zako..” Kauli hii ilimstua sana Catherine, “Inamaana ananiona?” alijiuliza kwa sauti ndogo iliyosikiwa na sikio la Sauti Simuni.
“Hiyo sio kazi yako kujua, nimekwambia fuata maelekezo yangu. Vaa nguo zako zile ulizovaa katika sherehe ya harusi ya Bilionea Khatibu Zawia. Acha simu juu ya kitanda chako. Utatoka nje ya geti lako, utakuta gari ndogo nyekundu imepaki upande wa pili wa barabara, utaenda kupanda katika mlango wa kati. Ukiingia tu gari itaondoka, hutakiwi kuongea kitu chochote kile na dereva wa gari hilo.
Dereva atakupeleka hadi katika nyumba moja, utashuka na kuingia ndani ya nyumba hiyo, katika eneo la maegesho la magari utamkuta kijana mmoja atakayekuwa amevaa kanzu nyeupe na barghashia, utamwambia,
“ Nimefuata mzigo”.
Huyo kijana ataingia ndani na kutoka na begi jeusi. Utachukua begi hilo na kutoka nalo nje. Utakuta gari ya bluu imepaki upande wa pili wa barabara, utaenda kuingia katika mlango wa kati wa gari hilo. Gari itakupeleka hadi uwanja wa ndege, dereva wa hilo gari atakupa nakala zote unazotakiwa kuwa nazo unaposafiri.
Utapanda ndege inayoelekea jijini Nairobi saa mbili asubuhi. Ukifika katika uwanja wa ndege wa Nairobi, kuna mtu atakupokea, atakuwa amevaa fulana nyeupe, kwa mbele imeandikwa kwa maandishi meusi ‘OCAFONA’, utampa hilo begi baada ya kuingia ndani ya gari lake atakalokuja nalo uwanjani, kisha yeye atakupa nakala zote za kukuwezesha kurudi jijini Dar es salaam.
Ukifika katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere, utapokelewa na mpenzi wako Martin. Na hapo ndipo utakuwa umeokoa maisha ya mpenzi wako. Kumbuka, tutakuwa tunakufatilia katika kila hatua utakayokanyaga. Katika safari hiyo utakuwa karibu na kifo kuliko wakati wowote ule katika maisha yako. Kosa moja tu, liwe la kukusudia ama la bahati mbaya litakupeleka kuzimu! Nakutakia kazi njema mrembo wangu.....” Simu ikakatwa.
Catherine alipumua kwa nguvu, kichwa chake kilikuwa kina mambo mengi sana ya kufikiria, lakini hakukuwa na muda huo wa kufikiria. Ilimpasa kutekeleza maagizo kwa ajili ya maisha yake, kwa ajili ya kumuokoa mpenzi wake.
Je nini kitatokea? Huu ni mwanzo wa TAHARUKI kutoka kwa mwandishi Halfani Sudy. Like na comment
Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app