SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 5: EPISODE 4
Saa kumi na mbili za
asubuhi Melanie alipigiwa
simu na Edwin Mbeko
akamjulisha kwamba
amemtumia taarifa za balozi
wa jamhuri ya kidemokrasia
ya Congo hapa nchini katika
barua pepe yake.Melanie
akaamka na kuelekea katika
chumba cha mazoezi ambako
alimkuta Joyce naye
amekwisha amka akifanya
mazoezi.Waliungana pamoja
katika mazoezi kisha kila
mmoja akaelekea chumbani
kwake kujiandaa kwa ajili ya
kuianza siku.Hawakuwa na
mtumishi bado hivyo Joyce
akaandaa kifungua
kinywa.Wakati Joyce
akiandaa kifungua kinywa
Melanie alikuwa chumbani
kwake akijiandaa,siku hii
alivaa suti ya rangi nyeupe
ambayo sketi yake iliishia
juu kidogo ya magoti na
kuwa na mpasuo mdogo kwa
nyuma.Alijiangalia kwenye
kioo akatabasamu
“Walionitengeneza
namna hii wanastahili
pongezi kubwa.Kwa
muonekano huu hakuna
mwanaume anayeweza
kuponyoka kama
nikimuhitaji” akawaza na
kuchukua moja ya simu kati
ya simu tatu zilizokuwa
mezani ambazo alipewa na
Edwin kwa ajili ya
mawasiliano.Akaziandika
namba za simu alizopewa na
Gosu Gosu akampigia
“Hallow” akasema Gosu
Gosu baada ya kupokea simu
akiwa hafahamu namba zile
ni za nani
“Halo mpenzi
wangu.Habari za
asubuhi?akauliza Melanie
“Melanie.Habari yao
malaika wangu.Umeamka
salama?
“Nimeamka salama
mpenzi sijui wewe”
“Hata mimi nimeamka
salama kabisa.Mawazo yote
juu yako” akasema Gosu
Gosu na Melanie
akatabasamu
“Darling hiyo ndiyo
namba yangu nitakayoitumia
hapa Tanzania muda wowote
ukitaka kunitafuta
utanitafuta katika namba
hiyo.Kwa shughuli zote za
kiofisi itatumika namba
hiyo” akasema Melanie
“Ahsante sana
Melanie.Vipi kuhusu ratiba
yako ya siku ya leo?
“Nitakuwa na mizunguko
kadhaa leo lakini kabla ya
mizunguko yangu nataka
kwanza nijitambulishe kwa
wafanyakazi ili wanifahamu
na mimi niwafahamu na kazi
hiyo ya kunitambulisha
utaifanya wewe.Nataka
niifahamu ofisi yako halafu
ndipo nitaendelea na
shughuli nyingine.Nielekeze
tukutane wapi?akauliza
Melanie
“Nielekeze mahala ulipo
nije nikuchukue” akasema
Gosu Gosu
“Usijali Gosu Gosu
ninaye dereva ambaye
anaweza akanileta mahala
ulipo”
“Ouh safi sana.Basi
mwambie akulete ofisi kuu
za MAPEN GROUP CO
LTD.Mimi nitakuwepo pale
nikikusubiri” akasema Gosu
Gosu
“Ahsante sana Gosu Gosu
tutaonana muda si
mrefu.Nakupenda sana”
akasema Melanie
“Nakupenda pia Melanie”
akasema Gosu Gosu na
Melanie akakata simu
Melanie akatoka
chumbani kwake na
kuelekea chini ambako
alimkuta Joyce akiwa tayari
amejiandaa lakini hakuwa
peke yake alikuwa na
mwanamke mmoja mfupi
mwenye weusi wa kung’aa.
“Hello ladies” akasema
Melanie na Yule mwanamke
aliyekuwa anazungumza na
Joyce akastuka baada
kumuona Melanie
“Madam Melanie huyu
anaitwa Frimina Mbozi ndiye
atakayekuwa katibu wako
muhtasi” akasema Joyce
“Hallow Frimina”
akasema Melanie na kumpa
mkono Frimina
“Hallow madam
Melanie.Naamini tayari
taarifa zangu unazo”
“Hutajali nikikuita Mina
badala ya Frimina? Akauliza
Melanie
“Hakuna tatizo Madam
Melanie”
“Good.Mina taarifa zako
tayari ninazo karibu sana”
akasema Melanie na wote
wakaenda kupata kifungua
kinywa na baada ya
kumaliza safari
ikaanza.Kituo cha kwanza
ilikuwa ni katika ofisi kuu za
MAPEN Group .Gosu Gosu
ambaye alikwisha wasili toka
mapema ndiye aliyempokea
Melanie.Siku hii alikuwa
amevalia suti nzuri nyeusi
na kila mmoja alimsifia kwa
muonekano ule.Wengi
hawakuzoea kumuona aiwa
amependeza namna
ile.Baada ya kupokelewa
Melanie akatembezwa katika
ofisi mbali mbali za jengo lile
la ghorofa tatu halafu
akaingizwa katika ofisi yake
kubwa ambayo ilikuwa ni
ofisi ya Mathew Mulumbi
kisha ikatumiwa na Gosu
Gosu na sasa ni Melanie
Davis.
“Ofisi nzuri sana hii
nimeipenda” akasema
Melanie halafu akaenda
kukutana na wafanyakazi
ambao walitaarifiwa kuacha
kila kitu na kukusanyika
katika ukumbi mkubwa wa
mikutano.Walifahamu kuna
ugeni lakini hawakujua
mgeni Yule ni
nani.Aliyefahamu ni Gosu
Gosu pekee
Gosu Gosu akiwa
ameongozana na Melanie na
katiku wake Frimina
waliingia katika ukumbi wa
mikutano.Gosu Gosu
akawasalimu wafanyakazi
wale halafu akatumia nafasi
ile kuwatangazia rasmi
kwamba kuanzia wakati ule
Melanie Davis ndiye mmiliki
mpya wa kampuni ya
MAPEN.Wafanyakazi wote
walipatwa na mshangao
mkubwa Gosu Gosu
akawaeleza sababu za
mmiliki wa kampuni ile
kuamua kuuza biashara zake
kwa mtu mwingine.Melanie
akakaribishwa kuzungumza
na wafanyakazi
akazungumza nao kwa muda
mfupi na kuwahakikishia
hakutakuwa na mabadiliko
yoyote,kila kitu kitaendelea
kuwa kama kilivyokuwa
awali na kuwaomba
wafanyakazi ushirikiano
mkubwa.Baada ya mkutano
ule na wafanyakazi Melanie
akarejea ofisini kwake na
rasmi Gosu Gosu
akamkabidhi ofisi
“Gosu Gosu huna haja ya
kunikabidhi ofisi.Hii
itaendelea kuwa ni ofisi
yako.Mimi nitatafuta ofisi
nyingine.Wewe bado ni
meneja mkuu wa
makampuni haya yote.Kama
alivyokuamini Peniela na
mimi pia ninakuamini vile
vile.Kila kitu kitakuwa chini
yako”akasema Melanie na
kumfuata Gosu Gosu
akambusu
“Japo bado nasubiri jibu
lako kuhusu kufunga ndoa
lakini wewe tayari ni mume
wangu Gosu Gosu.Wewe ni
mfalme wangu na kila kilicho
changu ni cha
kwako”akasema Melanie na
kumbusu
“Ahsante sana Melanie
kwa
kuniamini.Nitahakikisha
hujutii kuniamini” akasema
Gosu Gosu huku Melanie
akichezea tai yake
“Gosu Gosu kulala usiku
mmoja bila uwepo wako
pembeni yangu naona kama
ni miezi mitatu.Jioni ya leo
nitakuja nyumbani kwako
japo sintalala”akasema
Melanie na kumbusu tena
halafu akamuaga kwamba
anakwenda katika
mizunguko yake mingine
wataonana jioni kisha
Melanie akaondoka katika
ofisi kuu za MAPEN GROUP
huku akiacha gumzo watu
wakijadili uzuri wake.
Kutoka ofisi za MAPEN
group Melanie alielekea
katika ubalozi wa jamhuri ya
kidemokrasia ya
Congo.Alipokewa vizuri
akajitambulisha kama yeye
ana asili ya Congo lakini
ametokea Ufaransa na
anahitaji kuonana na balozi
wa DRC nchini
Tanzania.Balozi hakuwa na
mtu yoyote ofisini hivyo
Melanie akakaribishwa
ndani.
“Mheshimiwa balozi”
akasema Melanie akitumia
lugha ya kifaransa huku
akitabasamu na kumpa
mkono balozi
“Hallow habari
yako.Karibu sana”akasema
balozi na kumuelekeza
Melanie katika sofa nzuri
zilizokuwamo mle ofisini.
“Naitwa Melanie Davis
nina asili ya Congo lakni
ninaishi Ufaransa” akasema
Melanie
“Nafurahi kukufahamu
Melanie.Mimi naitwa
Germinus Mapupu balozi wa
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo hapa Tanzania.Karibu
sana katika ubalozi wetu
hapa Dar es salaam”
“Nashukuru sana
mheshimiwa balozi” akasema
Melanie na kukaa vizuri
kwani sketi yake fupi
aliyovaa ilikuwa imepanda
sana juu na kuyaacha
sehemu kubwa ya mapaja
yake wazi
“Niite Mr Mapupu
inatosha” akasema balozi
huku akitabasamu
“Kaona paja tu tayari
amekwisha anza
kujichekesha
chekesha”akawaza Melanie
“Mhehimiwa balozi Mr
Mapupu,kama
nilivyokujulisha mimi nina
asili ya Congo,wazazi wangu
wote wawili ni wazaliwa wa
Congo lakini walihamia
Ufaransa kibiashara.Kwa
sasa wote wawili
wametangulia mbele za haki
na mimi ndiye niliyebaki
nikisimamia mali
walizoziacha.Ninataka
kupanua biashara
walizoacha wazazi wangu
nataka kuogeza uwekezaji
zaidi hasa katika ukanda
huu wa Afrika
Mashariki.Tayari nimenunua
makampuni kadhaa hapa
Tanzania na sasa nataka
nikawekeze pia nyumbani
Congo”akasema Melanie
“Hongera sana Melanie
kwa uamuzi huo mkubwa wa
kuamua kuja kuwekeza
nyumbani.Wapo watu wengi
wa kutoka bara la Afrika
wamepata fedha nyingi huko
ughaibuni na hawakumbuki
tena kurejea kuwekeza
nyumbani na kuwapatia
ajira ndugu zao.Wewe
umefanya maamuzi mazuri
sana.Tunahitaji sana
uwekezaji kutoka nje na kwa
hivi sasa nchi ya Congo
imeweka sera nzuri sana za
kuvuta wawekezaji na wewe
ukiwa kama ni mkongo basi
utapewa kipaumbele
kikubwa.Ni sekta zipi
unataka kuwekeza?akauliza
balozi Mapupu
“Bado sijajua ni sekta ipi
ninaweza kuwekeza na
kupata faida ndiyo maana
nimekuja hapa kwako
nikitaka kupata kibali cha
dharura niweze kuingia
nchini Congo nikaonane na
idara inayohusika na
uwekezaji nizungumze nao
na nikitoka huko ntakuwa
nimepata picha kamili ni
sehemu gani ninaweza
kuwekeza” akasema Melanie.
Balozi Mapupu alielekeza
Melanie aandaliwe nyaraka
za kumuwezesha kuingia
nchini jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo na
ndani ya ya dakika kumi na
tano kila kitu kilikuwa tayari
“Hapa Dar es salaam
unapatikana sehemu gani?
Akauliza balozi
Mapupu.Melanie akatoa
simu na kumpatia balozi
namba zake naye balozi
akampatia za kwake
“Nitakaporejea kutoka
Congo nitakupigia
kukujulisha na kama
utakuwa na nafasi basi
tunaweza kukutana jioni
moja kwa chakula na
kinywaji tukabadilishana
mawazo” akasema Melanie
huku akitabasamu
“Nitafurahi sana
Melanie.Utakaporejea
tafadhali usiache kunipigia
simu” akasisitiza balozi
Mapupu na kumsindikiza
Melanie hadi katika gari lake
wakaagana akaondoka
“Balozi Mapupu tayari
amekwisha ingia katika
kitabu changu
chekundu.Mate yamemtoka
hasa alipoliona paja
linavyong’aa.Sikuwahi kujua
kama wanaume ni wadhaifu
kiasi hiki.Walionitengeneza
nikawa na umbo hili
nitaendelea kuwasifu siku
zote kwa akili kubwa
waliyotuma walijua kabisa
nikiwa na umbo la namna hii
hakuna mwanaume anaweza
akanikatalia jambo lolote.”
Akawaza Melanie na
kutabasamu
RIYADH – SAUDI ARABIA
Dr Abiha aliingia katika
chumba alimo Mathew
Mulumbi,kama kawaida
alikuwa ameongozana na
wale jamaa waliokuwa na
silaha akawataka wamsubiri
nje amuhudumie mgonjwa
“Habari yako Abu
Zalawi” akasema Dr Abiha
“Nzuri kabisa Dr Abiha”
“Vipi maendeleo yako?
“Ninaendelea vizuri
tofauti na jana”
“Nafurahi kusikia hivyo”
akasema Dr Abiha na
kumpima Mathew halafu
akasema
“Unaendelea vizuri Abu
Zalawi”
“Ahsante kwa huduma
nzuri Dr Abiha.Ulifanikiwa
kupata taarifa zozote
kuhusiana na Yule
mwenzangu Nawal? Akauliza
Mathew
“Hapana bado
sijafanikiwa kupata taarifa
zake zozote.Unaweza
ukanielezea zaidi kuhusu
huyo mwenzako?Ni mpenzi
wako?akauliza Dr Abiha
“Hapana si mpenzi
wangu.Ni mke wa kiongozi
wangu” akasema Mathew
“Wewe ni mwanachama
wa kikundi kipi?Abiha
akauliza
“Mimi ni mwanacahama
wa kikundi cha Ammar
Nazari brigades ambacho
kinapambana na Israel kudai
haki ya taifa la Palestina”
akasema Mathew
“Wewe ni Mpalestina?
“Hapana mimi si
mpalestina.Asili yangu ni
Misri baba yangu alijulikana
kama Khalid Al Zalawi na
aliuliwa na majeshi ya
Israel.Baada ya hapo ndipo
nilipoamua kuingia katika
mapambano na
Israel.Nilijiunga na kundi la
Ammar Nazari brigades na
huko tumekuwa tukiendeleza
mapambano dhidi ya Israel
na juzi kiongozi wetu ambaye
ni Ammar Nazari ameualiwa
na vikosi vya Israel.Yule
mwanamke niliyekuwa naye
Nawali alikuwa mke wa
Ammar Nazari na
alinikabidhi nimlinde
nihakikishe anakuwa
salama” akasema Mathew
“Kwa nini unamtafuta
Habiba Jawad?akauliza Dr
Abiha
“Kuna taarifa muhimu
nataka kumpatia”
“Kuhusu nini?akauliza
Dr Abiha
“Kuna mtu wake wa
muhimu ambaye ninafahamu
mahala alipo” akasema
Mathew
“Abu Zalawi utakataa
nikisema kwamba wewe ni
gaidi?akauliza
“Mimi si gaidi” akajibu
Mathew
“Kama si gaidi kwa nini
mnaua watu wasio na hatia?
“Haya ni mapambano Dr
Abiha na ni mapambano ya
kudai haki.Wapalestian
wana haki ya kupigana kwa
ajili ya ardhi yao ambayo
inakaliwa kimabavu na
Israel.Kwa nini Israel
wanapoua wapalestina dunia
inaona sawa lakini
wapalestina wanapoua
waisrael viongozi wa mataifa
wanasimama na kulaani?
Palestina wanapigana kwa
haki ya ardhi yao na Israel
hawana budi kurejesha ardhi
hiyo na kuacha ukandamizaji
inaowafanyia wapalestina”
akasema Mathew
“Abu wewe ni muislamu
na ninaamini unasoma
kitabu chetu
kitukufu.Unaweza
ukaniambia kitabu chetu
kinasemaje kuhusu kuua
watu wasiokuwa na
hatia?akauliza Dr Abiha
“Mwenyezi Mungu
Subhanahu wa ta’ala
ameagiza kwamba tusiue
nafsi ambayo
amekataza”akajibu Mathew
“Kwa nini saa mnaua
watu wasio na
hatia?akauliza Dr Abiha
“Katika Surah Al
Baqarah 2:190 – 192
tunaaambiwa “Na piganeni
katika njia ya Allaah na wale
wanaokupigeni, wala
msipundikie mipaka
(mkawapiga wasiokupigeni).
Kwani Allaah hawapendi
warukao mipaka. Na waueni
popote muwakutapo, na
muwatowe popote
walipokutoweni; kwani
kuwaharibu watu na dini yao
ni kubaya zaidi kuliko kuua.
Wala msipigane nao karibu
na Msikiti Mtakatifu (wa
Makka) mpaka wakupigeni
huko. Wakikupigeni (huko)
basi nanyi pia wapigeni.
Namna hivi ndivyo yalivyo
malipo ya makafiri. Lakini
kama wakikoma, Allaah ni
Mwingi wa kusamehe na
Mwingi wa kurehemu”
akasema Mathew na Dr
Abiha akabaki anamtazama.
“Sina haja ya kueleza
zaidi kwani maelezo hayo
yanajitosheleza”akasema
Mathew
“Kweli
yanajitosheleza”akasema Dr
Abiha
“Lini utanisaidia niweze
kutoka humu ndani? Vipi
kuhusu Habiba Jawad
umepata taarifa zake
zozote?akauliza Mathew
“Ninaendelea
kutengeneza mpango wa
kukutorosha pale
nitakapokuwa tayari
nitakujulisha” akasema Dr
Abiha
“Dr Abiha tafadhali
naomba unisaidie kupata
taarifa za Habiba
Jawad.Ninahitaji sana
kumuona”akasema Mathew
“Sawa nitakusaidia Abu
Zalawi “ akasema Dr Abiha
na kutoka mle ndani
akamauacha Mathew
“Niliwahi kukaa Libya
miaka miwili nikiwa kule
nilipata mafunzo ya lugha ya
kiarabu na kupata mafunzo
kuhusu Uislam.Kama
nisingepata mafunzo yale
swali aliloniuliza Dr Abiha
lingeniumbua.Anaonekana
ana nia ya dhati ya
kunisaidia.Namuomba
afanye haraka anisaidie
kwani wale jamaa wakijua
nimepata nafuu
watanirejesha tena
kuendelea kunitesa.Akinitoa
hapa lazima nifanye juu
chini nimpate Habiba
Jawad.Naamini yuko hapa
Saudi Arabia na siwezi
kuondoka bila kuonana naye”
akawaza Mathew
KINSHASA – JAMHURI YA
KIDEMOKRASIA YA
CONGO
Ndege ndogo iliyokodiwa
kutoka Dar es salaam
Tanzania iliwasili katika
uwanja wa ndege wa
kimataifa jijini
Kinshasa.Ndani ya ndege
hiyo alikuwa amepanda
Melanie Davis na dereva
wake Joyce.Ndege ilipotua
wakashuka na kufuata
taratibu za pale uwanjani
kisha wakaruhusiwa kuingia
jijini Kinshasa.Nje ya uwanja
tayari gari kutoka kampuni
ya kukodisha magari
lilikuwa linawasubiri.Kabla
ya kufika Kinshasa
maandalizi yote yalikwisha
fanyika.Melanie na Joyce
wakaingia katika gari lile la
kukodi wakaelekea mahala
ambako Melanie alielekeza
nje kidogo ya jiji la Kinshasa.
Siku hii Melanie alikuwa
amevaa mavazi meusi na
macho yake aliyafunika kwa
miwani mikubwa myeusi
kwani yalikuwa mekundu
kutokana na kulia sana
usiku kila alipowakumbuka
wazazi wake.Safari ilikuwa
ya kimya kimya hadi
walipofika katika shamba
walilokuwa wanalimiliki
wazazi wake ambako ndiko
walikozikwa.Kulikuwa na
geti lenye walinzi na Melanie
akajitambulisha kwamba
amekuja kutoa heshima za
mwisho kwa Lucy na
Laurent
Muganza.Walimuhoji yeye ni
nani na akawadanganya
kwamba anatokea Ufaransa
na marehemu Lucy Muganza
aliwahi kumsomesha ndiyo
maana amefunga safari
kutoka Paris kuja kutoa
heshima za mwisho.Walinzi
wale wakamjulisha mtu
mmoja ambaye ni mdogo
wake Laurent Muganza naye
akaelekeza watu wale
waruhusiwe kuingia
ndani.Lilikuwa shamba
kubwa na kutoka getini hadi
kufika mahala iliko nyumba
kubwa ni umbali wa kilometa
moja.Shamba lilisheheni
mazao mbali mbali
Walifika katika jumba
lile kubwa na kupokewa na
mdogo wake Laurent
Muganza.Melanie
alipomuona alishindwa
kuyazuia machozi kumtoka
kwani alikuwa amefanana
mno na baba
yake.Walikaribishwa ndani.
“Hii ni nyumba yetu
nilizoea kuja kukaa hapa
mara nyingi nirudipo kutoka
likizo kutokana na utulivu
unaopatikana mahala hapa
lakini leo hii ninakaribishwa
kama mgeni.Hakuna
anayenifahamu tena.Hata
nikiwaeleza mimi ni Theresia
Muganza hakuna
atakayeniamini” akawaza
Melanie
“Karibuni sana jamani”
baba yake mdogo Melanie
akasema
“Tunashukuru
sana.Mimi naitwa Melanie
Davis na huyu mwenzangu
anaitwa Joyce.Ninatokea
Paris Ufaransa na nimekuja
hapa kwa ajili ya kutoa
heshima kwa marehemu
Lucy na Laurent Muganza”
akasema Melanie
“Karibu sana”
“Ahsante baba.Lucy na
mumewe walikuwa watu
wakarimu sana na waliwahi
kunilipia ada ya chuo kikuu
pale nilipofiwa na wazazi
hivyo ni watu wangu wa
muhimu sana.Nilipata
taarifa za kuuawa kwao
nikiwa nchini Urusi hivyo
nikashindwa kuhudhuria
mazishi.Baada ya kupata
nafasi nimeona nije nami
nitoe heshima zangu kwa
watu hawa wema ambao
wamenifikisha hapa
nilipofika” akasema Melanie
na kufuta machozi
“Pole sana Melanie.Kifo
cha Laurent na mke wake
kinaumiza sana.Walikuwa ni
watu wema hawakuwa na
maadui na walipendwa na
kila mtu.Hata sisi
imetuumiza mno.Mimi ni
mdogo wake na Laurent”
akasema Yule jamaa
“Mmefanana
sana”akasema Melanie
halafu ukimya mfupi ukapita
“Vipi kuhusu waliofanya
mauaji haya wamekwisha
kamatwa hadi sasa?Melanie
akauliza
“Kuna utata
mwingi.Serikali ya Tanzania
inadai kwamba waliofanya
mauaji yale ni majambazi
lakini hadi leo hii hawajatoa
tena taarifa nyingine na
hawataki kuruhusu
wachunguzi wa kimataifa
wakalichunguze hili
suala.Kwa upande wa
serikali ya Congo imekuwa
kimya kabisa na hawajahi
kutoa taarifa zozote”
“Unadhani mauaji haya
yanaweza kuwa ni sababu za
kisiasa?Melanie akauliza
“Tunahisi hivyo kwa
sababu siku walipouawa ni
siku ambayo Lucy alikuwa
atangazwe na chama kikuu
cha upinzani kama mgombea
wa urais na Dar es salaam
alipita ili kumchukua
mwanae Theresia ili waje
wote Kinshasa lakini
hawakufika tena Kinshasa”
akasema Yule baba mdogo
wa Melanie
“Vipi kuhusu mtoto wa
marehemu yeye yuko
wapi?akauliza Melanie
“Theresia alinusurika
katika shambulio lile na
alipelekwa nchini Ufaransa
kwa matibabu.Tumekuwa
tunafuatilia kwa ubalozi wa
Ufaransa ili kupata taarifa
za maendeleo ya Theresia
lakini jibu ambalo tumekuwa
tukipewa ni kwamba
hatuwezi kuzungumza naye
kwani amefichwa mahala pa
siri akiendelea kupatiwa
matibabu.Kuna tetesi
kwamba toka alipotolewa
Tanzania akapelekwa
Ufaransa hajawahi
kuzinduka.Amewekwa
katika mashine za kumsaidia
kuishi”
“Mungu amsaidie aweze
kupona”akasema Melanie
“Tunasali usiku na
mchana Theresa aweze
kupona na kurejea.Wazazi
wake wameacha mali nyingi
sana ambazo zinamsubiri
yeye aweze kuziendeleza.Hivi
sasa tunaendelea na
mchakato wa kuorodhesha
mali zote za marehemu
wazazi wake na kuziweka
tayari kumsubiri aje
azisimamie”akasema Yule
jamaa.Melanie akavua
miwani na kufuta machozi
“Ninaweza tafadhali
kupelekwa mahala
walikozikwa wazee
hawa?akasema Melanie na
Yule mzee akawaongoza
kuelekea mahala
walikozikwa Lucy na
Laurent Muganza.Kulikuwa
na nyumba nzuri sana
ambayo ndani yake
kulijengwa makaburi mawili
ya Lucy na Laurent
Muganza.Mlango
ukafunguliwa na Melanie
akaomba apewe
faragha.Alilia machozi mengi
sana juu ya makaburi ya
wazazi wake
“Ninawaahidi wazazi
wangu yeyote ambaye
alishiriki katika kuwakatili
roho zenu hatabaki
salama.Nitawatafuta kokote
waliko na mmoja mmoja
lazima walipe.Damu yenu
haiwezi kupotea
bure.Ninapotoka ndani ya
nyumba hii mlimolala
ninakwenda kuanza kazi ya
kuwasaka wale wote
waliowalaza humu kabla ya
wakati wenu”Melanie
akatamka maneno hayo na
kuzibusu picha za wazazi
wake zilizokuwa katika
makaburi akafuta machozi
kisha akatoka.Hakutaka
tena kukaa eneo lile
wakaagana na Yule baba
yake mdogo kisha
wakaondoka.Hakutaka tena
kupita sehemu yoyote
akarejea uwanja wa ndege
ambako ndege ilikuwa
inawasubiri wakapanda na
kuondoka kurejea Dar es
salaam
“Kidonda changu
kimetoneshwa leo kwa
kuyaona makaburi ya wazazi
wangu.Nimeumia sana”
akawaza Melanie.Hakukuwa
na mazungumzo mengi ndani
ya ndege muda mwingi
Melanie alikuwa
ameinamisha kichwa
akiwaza na kulia.
Hatimaye ndege
ikawasili salama jijini Dar es
salaam tayari ilikuwa ni saa
kumi na mbili za jioni.Mara
tu waliposhuka
ndegeni,Melanie akampigia
simu Gosu Gosu na
kumjulisha kwamba
anakwenda kwake kisha
wakachukua gari lao
walilolicha pale uwanjani
wakaondoka.Walifika
nyumbani kwa Gosu Gosu
ambaye aliwapokea na
kuwakaribisha
sebuleni.Melanie akamtaka
waende chumbani
wakazungumze
faragha.Mara tu walipoingia
chumbani Melanie
akamrukia Gosu Gosu na
kumuangusha kitandani
kisha akaanza kutoa
nguo.Mambo yalikwenda
kimya kimya na Gosu Gosu
alielewa kile anachotakiwa
kukifanya na akashika
usukani.Ulikuwa ni
mtanange mzito sana lakini
Gosu Gosu aliumiliki vilivyo.
“Ahsante sana Gosu
Gosu,ahsante sana mpenzi
wangu” akasema Melanie
huku akimbusu Gosu Gosu
mfululizo na kumkumbatia
kwa nguvu baada ya
kumaliza mtanange ule
“Melanie ulinipania sana
siku ya leo” akasema Gosu
Gosu
“Gosu Gosu ni kweli.Sijui
ningefanya nini kama
ningekukosa.Ahsante
tena”akasema Melanie
“Nimekutafuta siku
nzima ya leo simu yako
haikuwa ikipatikana na hata
ofisini sijakuona” akasema
Gosu Gosu
“Ni kweli.Kutwa nzima
ya leo simu yangu ilikuwa
imezimwa nilikuwa na
mizunguko mingi” akasema
Melanie
“Pole sana.Kila kitu
kimekwenda vyema?akauliza
Gosu Gosu
“Usihofu kila kitu
kimekwenda
vizuri.Nashukuru
nimeimaliza siku nikiwa
kifuani kwako” akasema
Melanie na kuendelea
kukilaza kichwa chake
kifuani kwa Gosu Gosu
“Gosu Gosu nakupenda
sana na niko tayari kufanya
jambo lolote kwa ajili yako.Je
wewe uko tayari kufanya
chochote kwa ajili
yangu?akauliza Melanie
“Melanie nadhani jibu
unalifahamu kwamba niko
tayari kufanya chochote kwa
ajili yako” akasema Gosu
Gosu
“Nashukuru kwa kauli
hiyo”
“Kuna nini
Melanie?Mbona kama leo
hauko hauko sawa?
“Kuna kitu nitakuomba
unisaidie”
“Sema Melanie
nikusaidie nini?
“Kwanza kabla
sijakueleza ninachokitaka
kwako naomba nikueleze siri
yangu.Naomba tafadhali
uitunze siri hii kwani
sijawahi kumueleza mtu
mwingine yeyote”
“Usihofu Melanie.Siri
yako iko salama kwangu”
akasema Gosu Gosu
“Baba yangu na Rais
Patrice Eyenga wa DRC
walikuwa marafiki na kabla
Patrice hajawa Rais
walikuwa wanafanya
biashara pamoja.Walimiliki
kampuni kadhaa kwa
pamoja.Patrice alipotaka
kuwania urais wa Congo
kiasi kikubwa cha fedha za
kuendesha kampeni yake
alitegemea kutoka katika
biashara walizokuwa
wamechanga na
baba.Alitumia fedha nyingi
katika kampeni kwa ahadi
ya kuzirejesha pale
atakapokuwa ameshinda
urais.Baada ya kufanikiwa
kushinda urais baba
alimtaka aanze kurejesha
zile fedha ambazo ni nyingi
ili kunusuru biashara zao
lakini Rais Patrice Eyenga
alitengeneza mpango na
wazazi wangu wakauawa”
akasema Melanie na Gosu
Gosu akastuka na kuinuka
akakaa.Alihisi mwili wote
ukimsisimka kumbu kumbu
ya mauaji ya Lucy na
Laurent ikamjia
“Wazazi wako waliuawa
namna gani? Akauliza kwa
wasi wasi kidogo
“Walifariki katika ajali
ya gari ambayo tunaamini
ilitengenezwa.Gari lao dogo
liligongana na gari kubwa la
mizigo na wote wawili
wakafariki hapo hapo.Ripoti
ya wachunguzi wa
kujitegemea inaonyesha
kwamba ajali ile ilikuwa ya
kutengenezwa.Hakuna
ushahidi wa moja kwa moja
unaomuhusisha Rais Patrice
Eyenga na ajali ile lakini
tunaamini anahusika kwa
sababu kifo cha baba
kilitokea mara tu ulipoanza
mzozo kati yake na Patrice
kuhusu fedha”
“Pole sana Melanie”
akasema Gosu Gosu
“Ahsante
sana.Nimekwisha lia sana
kwa miaka mingi na machozi
yamekauka.Hivi sasa sina
tena machozi.Gosu Gosu
kilichopo katika akili yangu
kwa sasa ni jambo moja
tu.Ninataka kulipa kisasi
kwa Rais Patrice Eyenga
kwa kile alichonifanyia”
akasema Melanie na Gosu
Gosu akabaki
kimya.Alishindwa aseme nini
“Unanisikia Gosu
Gosu?akauliza Melanie
baada ya kumuona Gosu
Gosu amebaki kimya
“Nimekusikia Melanie”
“Naamini utaniunga
mkono katika harakati
zangu.Nataka Patrice
Eyenga naye apate maumivu
makali kwa kumpoteza mtu
wake wa karibu sana kama
mimi nilivyopata maumivu
makali kwa kuwapoteza
wazazi wangu” akasema
Melanie na Gosu Gosu
akahisi kama kuna kitu
kimekwama katika koo lake
akakohoa kidogo
“Gosu Gosu umekuwa
kimya ghafla baada ya
kukueleza jambo langu kuna
tatizo lolote?akauliza
Melanie
“Hapana niko sawa
Melanie”
“Unasemaje kuhusiana
nahiki
nilichokueleza?akauliza
Melanie
“Niko nawe Melanie
katika jambo lolote.Siwezi
kukuacha nyuma.Katika
jambo lolote lile nitatangulia
mbele na wewe utakuwa
nyuma yangu nitakulinda
dhidi ya hatari zozote
zinazoweza kujitokeza.Pole
sana kwa mara nyigine kwa
kifo cha wazazi wako na
Patrice Eyenga anapaswa
kulipa uovu wake
aliokufanyia.Nini unafikiria
kukifanya katika mpango
wako wa kulipiza
kisasi?akauliza Gosu Gosu
“Ahsante kwa kuniunga
mkono.Nitahitaji msaada
wako Gosu Gosu”
“Unahitaji nifanye nini
Melanie?Niambie chochote
nitakifanya” akasema Gosu
Gosu
Melanie akavuta pumzi
ndefu na kusema
“Nahitaji kuonana na
James Kasai”akasema
Melanie na Gosu Gosu
akahisi kama tumbo lake
limekuwa tupu ghafla
“James Kasai
yupi?akauliza Gosu Gosu
“Kwa miaka mingi
umekuwa katika mapigano
msituni.Humfahamu James
Kasai?akauliza Melanie
“James Kasai
ninamfahamu kama kiongozi
wa kundi la waasi walio
furushwa kutoka jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo na na
kukimbilia katika misitu ya
Uganda.Wakati James na
kundi lake wanafurushwa
jeshi la Congo lilivuka mpaka
na kuingia Uganda katika
kuwatafuta waasi hao ambao
walikataa kuweka silaha zao
chini.Uganda iliita kitendo
hicho cha wanajeshi wa
Congo kuvuka mpaka kama
kitendo cha uvamizi na
kuongeza majeshi yake
mpakani.Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo
inailaumu Uganda kuwa
inawahifadhi waasi hao na
Uganda inailaumu Congo
kwa jeshi lake kuvuka
mpaka na kuua raia wake”
“Safi sana kumbe bado
unafuatilia masuala hayo
kwa karibu.Huyo James
Kasai ambaye alikimbilia
Uganda baada ya
kufurushwa Congo ndiye
ambaye ninataka kuonana
naye.Nitakuachia wewe kazi
hiyo ya kutafuta namna ya
mimi kuweza kuonana
naye.Sifahamu utafanyaje
lakini ninachohitaji mimi ni
kupata nafasi ya kuonana na
James Kasai” akasema
Melanie
“Sawa Melanie
nitajitahidi kutafuta namna
ili uweze kuonana na huyo
mtu unayemuhitaji” akasema
Gosu Gosu
“Ndiyo maana
nakupenda sana Gosu Gosu”
akasema Melanie na kuanza
kumwagia mabusu mazito
kisha wakaingia katika
raundi nyingine ya
mtanange.
“Gosu Gosu jambo hili
nililokueleza ni siri kubwa
hivyo asifahamu mtu
yeyote”akasema Melanie
wakati akijiandaa kuondoka
“Mimi ni mwanajeshi
ninafahamu maana ya
kutunza siri hivyo usiwe na
wasiwasi mpenzi wangu”
akasema Gosu Gosu
“Nakupenda sana Gosu
Gosu” akasema Melanie na
kumbusu Gosu Gosu kisha
akaelekea katika gari lake
wakaondoka.Baada ya
Melanie kuondoka Gosu
Gosu akarejea ndani akiwa
ameinamisha kichwa alihisi
kitu kama nyundo inagonga
kichwa chake.Moja kwa moja
akaelekea katka baa yake
ndogo iliyoko mle ndani
akachukua chupa ya pombe
kali akaelekea chumbani
kwake akamimina katika
glasi akanywa yote akaweka
tena mara ya pili akanywa
yote kisha akashusha pumzi
“Melanie ametaka
kunipasua moyo wangu
leo.Mstuko nilioupata pale
aliponitamkia kwamba
Patrice Eyenga anahusika
katika vifo vya wazazi wake
ni mkubwa.Nashukuru
wazazi wake walifariki huko
Ufaransa” akawaza Gosu
Gosu na kunywa funda la
kinywaji kile kikali
akafumba macho
“Kwa nini Melanie
anataka kuonana na James
Kasai?Huyu ni mtu mbaya
na katili sana.Ni mtu
ambaye amekuwa
anatafutwa ili afikishwe
katika mahakama ya uhalifu
wa kivita kutokana na
ukatili mkubwa ambao kundi
lake liliufanya wakati
likipambana na majeshi ya
serikali ya Congo.Hadi leo
bado James ameshindwa
kukamatwa kwa sababu
anakingiwa kifua na nchi ya
Uganda ambao inadaiwa
wamempa hifadhi.Nahisi
kwamba Melanie anataka
kuandaa mipango ya kulipiza
kisasi kwa Rais Patrice
Eyenga na anataka
kumtumia James Kasai”
akawaza na kujiegemeza
sofani
“Sikutaka tena kujiingiza
katika masuala yoyote ya
mauaji,nilitaka niishi maisha
ya amani lakini siwezi
kumuacha Melanie peke
yake katika suala
hili.Lazima nisimame
naye.Ninampenda na huu ni
wakati mzuri wa
kumuonyesha ni namna gani
ninampenda na
kumthamini.Kama ni kuua
niko tayari kuua kwa ajili
yake.Nitatafuta namna ya
kumpata James Kasai”
akawaza Gosu Gosu na
kuchukua simu yake.
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 5: EPISODE 4
Saa kumi na mbili za
asubuhi Melanie alipigiwa
simu na Edwin Mbeko
akamjulisha kwamba
amemtumia taarifa za balozi
wa jamhuri ya kidemokrasia
ya Congo hapa nchini katika
barua pepe yake.Melanie
akaamka na kuelekea katika
chumba cha mazoezi ambako
alimkuta Joyce naye
amekwisha amka akifanya
mazoezi.Waliungana pamoja
katika mazoezi kisha kila
mmoja akaelekea chumbani
kwake kujiandaa kwa ajili ya
kuianza siku.Hawakuwa na
mtumishi bado hivyo Joyce
akaandaa kifungua
kinywa.Wakati Joyce
akiandaa kifungua kinywa
Melanie alikuwa chumbani
kwake akijiandaa,siku hii
alivaa suti ya rangi nyeupe
ambayo sketi yake iliishia
juu kidogo ya magoti na
kuwa na mpasuo mdogo kwa
nyuma.Alijiangalia kwenye
kioo akatabasamu
“Walionitengeneza
namna hii wanastahili
pongezi kubwa.Kwa
muonekano huu hakuna
mwanaume anayeweza
kuponyoka kama
nikimuhitaji” akawaza na
kuchukua moja ya simu kati
ya simu tatu zilizokuwa
mezani ambazo alipewa na
Edwin kwa ajili ya
mawasiliano.Akaziandika
namba za simu alizopewa na
Gosu Gosu akampigia
“Hallow” akasema Gosu
Gosu baada ya kupokea simu
akiwa hafahamu namba zile
ni za nani
“Halo mpenzi
wangu.Habari za
asubuhi?akauliza Melanie
“Melanie.Habari yao
malaika wangu.Umeamka
salama?
“Nimeamka salama
mpenzi sijui wewe”
“Hata mimi nimeamka
salama kabisa.Mawazo yote
juu yako” akasema Gosu
Gosu na Melanie
akatabasamu
“Darling hiyo ndiyo
namba yangu nitakayoitumia
hapa Tanzania muda wowote
ukitaka kunitafuta
utanitafuta katika namba
hiyo.Kwa shughuli zote za
kiofisi itatumika namba
hiyo” akasema Melanie
“Ahsante sana
Melanie.Vipi kuhusu ratiba
yako ya siku ya leo?
“Nitakuwa na mizunguko
kadhaa leo lakini kabla ya
mizunguko yangu nataka
kwanza nijitambulishe kwa
wafanyakazi ili wanifahamu
na mimi niwafahamu na kazi
hiyo ya kunitambulisha
utaifanya wewe.Nataka
niifahamu ofisi yako halafu
ndipo nitaendelea na
shughuli nyingine.Nielekeze
tukutane wapi?akauliza
Melanie
“Nielekeze mahala ulipo
nije nikuchukue” akasema
Gosu Gosu
“Usijali Gosu Gosu
ninaye dereva ambaye
anaweza akanileta mahala
ulipo”
“Ouh safi sana.Basi
mwambie akulete ofisi kuu
za MAPEN GROUP CO
LTD.Mimi nitakuwepo pale
nikikusubiri” akasema Gosu
Gosu
“Ahsante sana Gosu Gosu
tutaonana muda si
mrefu.Nakupenda sana”
akasema Melanie
“Nakupenda pia Melanie”
akasema Gosu Gosu na
Melanie akakata simu
Melanie akatoka
chumbani kwake na
kuelekea chini ambako
alimkuta Joyce akiwa tayari
amejiandaa lakini hakuwa
peke yake alikuwa na
mwanamke mmoja mfupi
mwenye weusi wa kung’aa.
“Hello ladies” akasema
Melanie na Yule mwanamke
aliyekuwa anazungumza na
Joyce akastuka baada
kumuona Melanie
“Madam Melanie huyu
anaitwa Frimina Mbozi ndiye
atakayekuwa katibu wako
muhtasi” akasema Joyce
“Hallow Frimina”
akasema Melanie na kumpa
mkono Frimina
“Hallow madam
Melanie.Naamini tayari
taarifa zangu unazo”
“Hutajali nikikuita Mina
badala ya Frimina? Akauliza
Melanie
“Hakuna tatizo Madam
Melanie”
“Good.Mina taarifa zako
tayari ninazo karibu sana”
akasema Melanie na wote
wakaenda kupata kifungua
kinywa na baada ya
kumaliza safari
ikaanza.Kituo cha kwanza
ilikuwa ni katika ofisi kuu za
MAPEN Group .Gosu Gosu
ambaye alikwisha wasili toka
mapema ndiye aliyempokea
Melanie.Siku hii alikuwa
amevalia suti nzuri nyeusi
na kila mmoja alimsifia kwa
muonekano ule.Wengi
hawakuzoea kumuona aiwa
amependeza namna
ile.Baada ya kupokelewa
Melanie akatembezwa katika
ofisi mbali mbali za jengo lile
la ghorofa tatu halafu
akaingizwa katika ofisi yake
kubwa ambayo ilikuwa ni
ofisi ya Mathew Mulumbi
kisha ikatumiwa na Gosu
Gosu na sasa ni Melanie
Davis.
“Ofisi nzuri sana hii
nimeipenda” akasema
Melanie halafu akaenda
kukutana na wafanyakazi
ambao walitaarifiwa kuacha
kila kitu na kukusanyika
katika ukumbi mkubwa wa
mikutano.Walifahamu kuna
ugeni lakini hawakujua
mgeni Yule ni
nani.Aliyefahamu ni Gosu
Gosu pekee
Gosu Gosu akiwa
ameongozana na Melanie na
katiku wake Frimina
waliingia katika ukumbi wa
mikutano.Gosu Gosu
akawasalimu wafanyakazi
wale halafu akatumia nafasi
ile kuwatangazia rasmi
kwamba kuanzia wakati ule
Melanie Davis ndiye mmiliki
mpya wa kampuni ya
MAPEN.Wafanyakazi wote
walipatwa na mshangao
mkubwa Gosu Gosu
akawaeleza sababu za
mmiliki wa kampuni ile
kuamua kuuza biashara zake
kwa mtu mwingine.Melanie
akakaribishwa kuzungumza
na wafanyakazi
akazungumza nao kwa muda
mfupi na kuwahakikishia
hakutakuwa na mabadiliko
yoyote,kila kitu kitaendelea
kuwa kama kilivyokuwa
awali na kuwaomba
wafanyakazi ushirikiano
mkubwa.Baada ya mkutano
ule na wafanyakazi Melanie
akarejea ofisini kwake na
rasmi Gosu Gosu
akamkabidhi ofisi
“Gosu Gosu huna haja ya
kunikabidhi ofisi.Hii
itaendelea kuwa ni ofisi
yako.Mimi nitatafuta ofisi
nyingine.Wewe bado ni
meneja mkuu wa
makampuni haya yote.Kama
alivyokuamini Peniela na
mimi pia ninakuamini vile
vile.Kila kitu kitakuwa chini
yako”akasema Melanie na
kumfuata Gosu Gosu
akambusu
“Japo bado nasubiri jibu
lako kuhusu kufunga ndoa
lakini wewe tayari ni mume
wangu Gosu Gosu.Wewe ni
mfalme wangu na kila kilicho
changu ni cha
kwako”akasema Melanie na
kumbusu
“Ahsante sana Melanie
kwa
kuniamini.Nitahakikisha
hujutii kuniamini” akasema
Gosu Gosu huku Melanie
akichezea tai yake
“Gosu Gosu kulala usiku
mmoja bila uwepo wako
pembeni yangu naona kama
ni miezi mitatu.Jioni ya leo
nitakuja nyumbani kwako
japo sintalala”akasema
Melanie na kumbusu tena
halafu akamuaga kwamba
anakwenda katika
mizunguko yake mingine
wataonana jioni kisha
Melanie akaondoka katika
ofisi kuu za MAPEN GROUP
huku akiacha gumzo watu
wakijadili uzuri wake.
Kutoka ofisi za MAPEN
group Melanie alielekea
katika ubalozi wa jamhuri ya
kidemokrasia ya
Congo.Alipokewa vizuri
akajitambulisha kama yeye
ana asili ya Congo lakini
ametokea Ufaransa na
anahitaji kuonana na balozi
wa DRC nchini
Tanzania.Balozi hakuwa na
mtu yoyote ofisini hivyo
Melanie akakaribishwa
ndani.
“Mheshimiwa balozi”
akasema Melanie akitumia
lugha ya kifaransa huku
akitabasamu na kumpa
mkono balozi
“Hallow habari
yako.Karibu sana”akasema
balozi na kumuelekeza
Melanie katika sofa nzuri
zilizokuwamo mle ofisini.
“Naitwa Melanie Davis
nina asili ya Congo lakni
ninaishi Ufaransa” akasema
Melanie
“Nafurahi kukufahamu
Melanie.Mimi naitwa
Germinus Mapupu balozi wa
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo hapa Tanzania.Karibu
sana katika ubalozi wetu
hapa Dar es salaam”
“Nashukuru sana
mheshimiwa balozi” akasema
Melanie na kukaa vizuri
kwani sketi yake fupi
aliyovaa ilikuwa imepanda
sana juu na kuyaacha
sehemu kubwa ya mapaja
yake wazi
“Niite Mr Mapupu
inatosha” akasema balozi
huku akitabasamu
“Kaona paja tu tayari
amekwisha anza
kujichekesha
chekesha”akawaza Melanie
“Mhehimiwa balozi Mr
Mapupu,kama
nilivyokujulisha mimi nina
asili ya Congo,wazazi wangu
wote wawili ni wazaliwa wa
Congo lakini walihamia
Ufaransa kibiashara.Kwa
sasa wote wawili
wametangulia mbele za haki
na mimi ndiye niliyebaki
nikisimamia mali
walizoziacha.Ninataka
kupanua biashara
walizoacha wazazi wangu
nataka kuogeza uwekezaji
zaidi hasa katika ukanda
huu wa Afrika
Mashariki.Tayari nimenunua
makampuni kadhaa hapa
Tanzania na sasa nataka
nikawekeze pia nyumbani
Congo”akasema Melanie
“Hongera sana Melanie
kwa uamuzi huo mkubwa wa
kuamua kuja kuwekeza
nyumbani.Wapo watu wengi
wa kutoka bara la Afrika
wamepata fedha nyingi huko
ughaibuni na hawakumbuki
tena kurejea kuwekeza
nyumbani na kuwapatia
ajira ndugu zao.Wewe
umefanya maamuzi mazuri
sana.Tunahitaji sana
uwekezaji kutoka nje na kwa
hivi sasa nchi ya Congo
imeweka sera nzuri sana za
kuvuta wawekezaji na wewe
ukiwa kama ni mkongo basi
utapewa kipaumbele
kikubwa.Ni sekta zipi
unataka kuwekeza?akauliza
balozi Mapupu
“Bado sijajua ni sekta ipi
ninaweza kuwekeza na
kupata faida ndiyo maana
nimekuja hapa kwako
nikitaka kupata kibali cha
dharura niweze kuingia
nchini Congo nikaonane na
idara inayohusika na
uwekezaji nizungumze nao
na nikitoka huko ntakuwa
nimepata picha kamili ni
sehemu gani ninaweza
kuwekeza” akasema Melanie.
Balozi Mapupu alielekeza
Melanie aandaliwe nyaraka
za kumuwezesha kuingia
nchini jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo na
ndani ya ya dakika kumi na
tano kila kitu kilikuwa tayari
“Hapa Dar es salaam
unapatikana sehemu gani?
Akauliza balozi
Mapupu.Melanie akatoa
simu na kumpatia balozi
namba zake naye balozi
akampatia za kwake
“Nitakaporejea kutoka
Congo nitakupigia
kukujulisha na kama
utakuwa na nafasi basi
tunaweza kukutana jioni
moja kwa chakula na
kinywaji tukabadilishana
mawazo” akasema Melanie
huku akitabasamu
“Nitafurahi sana
Melanie.Utakaporejea
tafadhali usiache kunipigia
simu” akasisitiza balozi
Mapupu na kumsindikiza
Melanie hadi katika gari lake
wakaagana akaondoka
“Balozi Mapupu tayari
amekwisha ingia katika
kitabu changu
chekundu.Mate yamemtoka
hasa alipoliona paja
linavyong’aa.Sikuwahi kujua
kama wanaume ni wadhaifu
kiasi hiki.Walionitengeneza
nikawa na umbo hili
nitaendelea kuwasifu siku
zote kwa akili kubwa
waliyotuma walijua kabisa
nikiwa na umbo la namna hii
hakuna mwanaume anaweza
akanikatalia jambo lolote.”
Akawaza Melanie na
kutabasamu
RIYADH – SAUDI ARABIA
Dr Abiha aliingia katika
chumba alimo Mathew
Mulumbi,kama kawaida
alikuwa ameongozana na
wale jamaa waliokuwa na
silaha akawataka wamsubiri
nje amuhudumie mgonjwa
“Habari yako Abu
Zalawi” akasema Dr Abiha
“Nzuri kabisa Dr Abiha”
“Vipi maendeleo yako?
“Ninaendelea vizuri
tofauti na jana”
“Nafurahi kusikia hivyo”
akasema Dr Abiha na
kumpima Mathew halafu
akasema
“Unaendelea vizuri Abu
Zalawi”
“Ahsante kwa huduma
nzuri Dr Abiha.Ulifanikiwa
kupata taarifa zozote
kuhusiana na Yule
mwenzangu Nawal? Akauliza
Mathew
“Hapana bado
sijafanikiwa kupata taarifa
zake zozote.Unaweza
ukanielezea zaidi kuhusu
huyo mwenzako?Ni mpenzi
wako?akauliza Dr Abiha
“Hapana si mpenzi
wangu.Ni mke wa kiongozi
wangu” akasema Mathew
“Wewe ni mwanachama
wa kikundi kipi?Abiha
akauliza
“Mimi ni mwanacahama
wa kikundi cha Ammar
Nazari brigades ambacho
kinapambana na Israel kudai
haki ya taifa la Palestina”
akasema Mathew
“Wewe ni Mpalestina?
“Hapana mimi si
mpalestina.Asili yangu ni
Misri baba yangu alijulikana
kama Khalid Al Zalawi na
aliuliwa na majeshi ya
Israel.Baada ya hapo ndipo
nilipoamua kuingia katika
mapambano na
Israel.Nilijiunga na kundi la
Ammar Nazari brigades na
huko tumekuwa tukiendeleza
mapambano dhidi ya Israel
na juzi kiongozi wetu ambaye
ni Ammar Nazari ameualiwa
na vikosi vya Israel.Yule
mwanamke niliyekuwa naye
Nawali alikuwa mke wa
Ammar Nazari na
alinikabidhi nimlinde
nihakikishe anakuwa
salama” akasema Mathew
“Kwa nini unamtafuta
Habiba Jawad?akauliza Dr
Abiha
“Kuna taarifa muhimu
nataka kumpatia”
“Kuhusu nini?akauliza
Dr Abiha
“Kuna mtu wake wa
muhimu ambaye ninafahamu
mahala alipo” akasema
Mathew
“Abu Zalawi utakataa
nikisema kwamba wewe ni
gaidi?akauliza
“Mimi si gaidi” akajibu
Mathew
“Kama si gaidi kwa nini
mnaua watu wasio na hatia?
“Haya ni mapambano Dr
Abiha na ni mapambano ya
kudai haki.Wapalestian
wana haki ya kupigana kwa
ajili ya ardhi yao ambayo
inakaliwa kimabavu na
Israel.Kwa nini Israel
wanapoua wapalestina dunia
inaona sawa lakini
wapalestina wanapoua
waisrael viongozi wa mataifa
wanasimama na kulaani?
Palestina wanapigana kwa
haki ya ardhi yao na Israel
hawana budi kurejesha ardhi
hiyo na kuacha ukandamizaji
inaowafanyia wapalestina”
akasema Mathew
“Abu wewe ni muislamu
na ninaamini unasoma
kitabu chetu
kitukufu.Unaweza
ukaniambia kitabu chetu
kinasemaje kuhusu kuua
watu wasiokuwa na
hatia?akauliza Dr Abiha
“Mwenyezi Mungu
Subhanahu wa ta’ala
ameagiza kwamba tusiue
nafsi ambayo
amekataza”akajibu Mathew
“Kwa nini saa mnaua
watu wasio na
hatia?akauliza Dr Abiha
“Katika Surah Al
Baqarah 2:190 – 192
tunaaambiwa “Na piganeni
katika njia ya Allaah na wale
wanaokupigeni, wala
msipundikie mipaka
(mkawapiga wasiokupigeni).
Kwani Allaah hawapendi
warukao mipaka. Na waueni
popote muwakutapo, na
muwatowe popote
walipokutoweni; kwani
kuwaharibu watu na dini yao
ni kubaya zaidi kuliko kuua.
Wala msipigane nao karibu
na Msikiti Mtakatifu (wa
Makka) mpaka wakupigeni
huko. Wakikupigeni (huko)
basi nanyi pia wapigeni.
Namna hivi ndivyo yalivyo
malipo ya makafiri. Lakini
kama wakikoma, Allaah ni
Mwingi wa kusamehe na
Mwingi wa kurehemu”
akasema Mathew na Dr
Abiha akabaki anamtazama.
“Sina haja ya kueleza
zaidi kwani maelezo hayo
yanajitosheleza”akasema
Mathew
“Kweli
yanajitosheleza”akasema Dr
Abiha
“Lini utanisaidia niweze
kutoka humu ndani? Vipi
kuhusu Habiba Jawad
umepata taarifa zake
zozote?akauliza Mathew
“Ninaendelea
kutengeneza mpango wa
kukutorosha pale
nitakapokuwa tayari
nitakujulisha” akasema Dr
Abiha
“Dr Abiha tafadhali
naomba unisaidie kupata
taarifa za Habiba
Jawad.Ninahitaji sana
kumuona”akasema Mathew
“Sawa nitakusaidia Abu
Zalawi “ akasema Dr Abiha
na kutoka mle ndani
akamauacha Mathew
“Niliwahi kukaa Libya
miaka miwili nikiwa kule
nilipata mafunzo ya lugha ya
kiarabu na kupata mafunzo
kuhusu Uislam.Kama
nisingepata mafunzo yale
swali aliloniuliza Dr Abiha
lingeniumbua.Anaonekana
ana nia ya dhati ya
kunisaidia.Namuomba
afanye haraka anisaidie
kwani wale jamaa wakijua
nimepata nafuu
watanirejesha tena
kuendelea kunitesa.Akinitoa
hapa lazima nifanye juu
chini nimpate Habiba
Jawad.Naamini yuko hapa
Saudi Arabia na siwezi
kuondoka bila kuonana naye”
akawaza Mathew
KINSHASA – JAMHURI YA
KIDEMOKRASIA YA
CONGO
Ndege ndogo iliyokodiwa
kutoka Dar es salaam
Tanzania iliwasili katika
uwanja wa ndege wa
kimataifa jijini
Kinshasa.Ndani ya ndege
hiyo alikuwa amepanda
Melanie Davis na dereva
wake Joyce.Ndege ilipotua
wakashuka na kufuata
taratibu za pale uwanjani
kisha wakaruhusiwa kuingia
jijini Kinshasa.Nje ya uwanja
tayari gari kutoka kampuni
ya kukodisha magari
lilikuwa linawasubiri.Kabla
ya kufika Kinshasa
maandalizi yote yalikwisha
fanyika.Melanie na Joyce
wakaingia katika gari lile la
kukodi wakaelekea mahala
ambako Melanie alielekeza
nje kidogo ya jiji la Kinshasa.
Siku hii Melanie alikuwa
amevaa mavazi meusi na
macho yake aliyafunika kwa
miwani mikubwa myeusi
kwani yalikuwa mekundu
kutokana na kulia sana
usiku kila alipowakumbuka
wazazi wake.Safari ilikuwa
ya kimya kimya hadi
walipofika katika shamba
walilokuwa wanalimiliki
wazazi wake ambako ndiko
walikozikwa.Kulikuwa na
geti lenye walinzi na Melanie
akajitambulisha kwamba
amekuja kutoa heshima za
mwisho kwa Lucy na
Laurent
Muganza.Walimuhoji yeye ni
nani na akawadanganya
kwamba anatokea Ufaransa
na marehemu Lucy Muganza
aliwahi kumsomesha ndiyo
maana amefunga safari
kutoka Paris kuja kutoa
heshima za mwisho.Walinzi
wale wakamjulisha mtu
mmoja ambaye ni mdogo
wake Laurent Muganza naye
akaelekeza watu wale
waruhusiwe kuingia
ndani.Lilikuwa shamba
kubwa na kutoka getini hadi
kufika mahala iliko nyumba
kubwa ni umbali wa kilometa
moja.Shamba lilisheheni
mazao mbali mbali
Walifika katika jumba
lile kubwa na kupokewa na
mdogo wake Laurent
Muganza.Melanie
alipomuona alishindwa
kuyazuia machozi kumtoka
kwani alikuwa amefanana
mno na baba
yake.Walikaribishwa ndani.
“Hii ni nyumba yetu
nilizoea kuja kukaa hapa
mara nyingi nirudipo kutoka
likizo kutokana na utulivu
unaopatikana mahala hapa
lakini leo hii ninakaribishwa
kama mgeni.Hakuna
anayenifahamu tena.Hata
nikiwaeleza mimi ni Theresia
Muganza hakuna
atakayeniamini” akawaza
Melanie
“Karibuni sana jamani”
baba yake mdogo Melanie
akasema
“Tunashukuru
sana.Mimi naitwa Melanie
Davis na huyu mwenzangu
anaitwa Joyce.Ninatokea
Paris Ufaransa na nimekuja
hapa kwa ajili ya kutoa
heshima kwa marehemu
Lucy na Laurent Muganza”
akasema Melanie
“Karibu sana”
“Ahsante baba.Lucy na
mumewe walikuwa watu
wakarimu sana na waliwahi
kunilipia ada ya chuo kikuu
pale nilipofiwa na wazazi
hivyo ni watu wangu wa
muhimu sana.Nilipata
taarifa za kuuawa kwao
nikiwa nchini Urusi hivyo
nikashindwa kuhudhuria
mazishi.Baada ya kupata
nafasi nimeona nije nami
nitoe heshima zangu kwa
watu hawa wema ambao
wamenifikisha hapa
nilipofika” akasema Melanie
na kufuta machozi
“Pole sana Melanie.Kifo
cha Laurent na mke wake
kinaumiza sana.Walikuwa ni
watu wema hawakuwa na
maadui na walipendwa na
kila mtu.Hata sisi
imetuumiza mno.Mimi ni
mdogo wake na Laurent”
akasema Yule jamaa
“Mmefanana
sana”akasema Melanie
halafu ukimya mfupi ukapita
“Vipi kuhusu waliofanya
mauaji haya wamekwisha
kamatwa hadi sasa?Melanie
akauliza
“Kuna utata
mwingi.Serikali ya Tanzania
inadai kwamba waliofanya
mauaji yale ni majambazi
lakini hadi leo hii hawajatoa
tena taarifa nyingine na
hawataki kuruhusu
wachunguzi wa kimataifa
wakalichunguze hili
suala.Kwa upande wa
serikali ya Congo imekuwa
kimya kabisa na hawajahi
kutoa taarifa zozote”
“Unadhani mauaji haya
yanaweza kuwa ni sababu za
kisiasa?Melanie akauliza
“Tunahisi hivyo kwa
sababu siku walipouawa ni
siku ambayo Lucy alikuwa
atangazwe na chama kikuu
cha upinzani kama mgombea
wa urais na Dar es salaam
alipita ili kumchukua
mwanae Theresia ili waje
wote Kinshasa lakini
hawakufika tena Kinshasa”
akasema Yule baba mdogo
wa Melanie
“Vipi kuhusu mtoto wa
marehemu yeye yuko
wapi?akauliza Melanie
“Theresia alinusurika
katika shambulio lile na
alipelekwa nchini Ufaransa
kwa matibabu.Tumekuwa
tunafuatilia kwa ubalozi wa
Ufaransa ili kupata taarifa
za maendeleo ya Theresia
lakini jibu ambalo tumekuwa
tukipewa ni kwamba
hatuwezi kuzungumza naye
kwani amefichwa mahala pa
siri akiendelea kupatiwa
matibabu.Kuna tetesi
kwamba toka alipotolewa
Tanzania akapelekwa
Ufaransa hajawahi
kuzinduka.Amewekwa
katika mashine za kumsaidia
kuishi”
“Mungu amsaidie aweze
kupona”akasema Melanie
“Tunasali usiku na
mchana Theresa aweze
kupona na kurejea.Wazazi
wake wameacha mali nyingi
sana ambazo zinamsubiri
yeye aweze kuziendeleza.Hivi
sasa tunaendelea na
mchakato wa kuorodhesha
mali zote za marehemu
wazazi wake na kuziweka
tayari kumsubiri aje
azisimamie”akasema Yule
jamaa.Melanie akavua
miwani na kufuta machozi
“Ninaweza tafadhali
kupelekwa mahala
walikozikwa wazee
hawa?akasema Melanie na
Yule mzee akawaongoza
kuelekea mahala
walikozikwa Lucy na
Laurent Muganza.Kulikuwa
na nyumba nzuri sana
ambayo ndani yake
kulijengwa makaburi mawili
ya Lucy na Laurent
Muganza.Mlango
ukafunguliwa na Melanie
akaomba apewe
faragha.Alilia machozi mengi
sana juu ya makaburi ya
wazazi wake
“Ninawaahidi wazazi
wangu yeyote ambaye
alishiriki katika kuwakatili
roho zenu hatabaki
salama.Nitawatafuta kokote
waliko na mmoja mmoja
lazima walipe.Damu yenu
haiwezi kupotea
bure.Ninapotoka ndani ya
nyumba hii mlimolala
ninakwenda kuanza kazi ya
kuwasaka wale wote
waliowalaza humu kabla ya
wakati wenu”Melanie
akatamka maneno hayo na
kuzibusu picha za wazazi
wake zilizokuwa katika
makaburi akafuta machozi
kisha akatoka.Hakutaka
tena kukaa eneo lile
wakaagana na Yule baba
yake mdogo kisha
wakaondoka.Hakutaka tena
kupita sehemu yoyote
akarejea uwanja wa ndege
ambako ndege ilikuwa
inawasubiri wakapanda na
kuondoka kurejea Dar es
salaam
“Kidonda changu
kimetoneshwa leo kwa
kuyaona makaburi ya wazazi
wangu.Nimeumia sana”
akawaza Melanie.Hakukuwa
na mazungumzo mengi ndani
ya ndege muda mwingi
Melanie alikuwa
ameinamisha kichwa
akiwaza na kulia.
Hatimaye ndege
ikawasili salama jijini Dar es
salaam tayari ilikuwa ni saa
kumi na mbili za jioni.Mara
tu waliposhuka
ndegeni,Melanie akampigia
simu Gosu Gosu na
kumjulisha kwamba
anakwenda kwake kisha
wakachukua gari lao
walilolicha pale uwanjani
wakaondoka.Walifika
nyumbani kwa Gosu Gosu
ambaye aliwapokea na
kuwakaribisha
sebuleni.Melanie akamtaka
waende chumbani
wakazungumze
faragha.Mara tu walipoingia
chumbani Melanie
akamrukia Gosu Gosu na
kumuangusha kitandani
kisha akaanza kutoa
nguo.Mambo yalikwenda
kimya kimya na Gosu Gosu
alielewa kile anachotakiwa
kukifanya na akashika
usukani.Ulikuwa ni
mtanange mzito sana lakini
Gosu Gosu aliumiliki vilivyo.
“Ahsante sana Gosu
Gosu,ahsante sana mpenzi
wangu” akasema Melanie
huku akimbusu Gosu Gosu
mfululizo na kumkumbatia
kwa nguvu baada ya
kumaliza mtanange ule
“Melanie ulinipania sana
siku ya leo” akasema Gosu
Gosu
“Gosu Gosu ni kweli.Sijui
ningefanya nini kama
ningekukosa.Ahsante
tena”akasema Melanie
“Nimekutafuta siku
nzima ya leo simu yako
haikuwa ikipatikana na hata
ofisini sijakuona” akasema
Gosu Gosu
“Ni kweli.Kutwa nzima
ya leo simu yangu ilikuwa
imezimwa nilikuwa na
mizunguko mingi” akasema
Melanie
“Pole sana.Kila kitu
kimekwenda vyema?akauliza
Gosu Gosu
“Usihofu kila kitu
kimekwenda
vizuri.Nashukuru
nimeimaliza siku nikiwa
kifuani kwako” akasema
Melanie na kuendelea
kukilaza kichwa chake
kifuani kwa Gosu Gosu
“Gosu Gosu nakupenda
sana na niko tayari kufanya
jambo lolote kwa ajili yako.Je
wewe uko tayari kufanya
chochote kwa ajili
yangu?akauliza Melanie
“Melanie nadhani jibu
unalifahamu kwamba niko
tayari kufanya chochote kwa
ajili yako” akasema Gosu
Gosu
“Nashukuru kwa kauli
hiyo”
“Kuna nini
Melanie?Mbona kama leo
hauko hauko sawa?
“Kuna kitu nitakuomba
unisaidie”
“Sema Melanie
nikusaidie nini?
“Kwanza kabla
sijakueleza ninachokitaka
kwako naomba nikueleze siri
yangu.Naomba tafadhali
uitunze siri hii kwani
sijawahi kumueleza mtu
mwingine yeyote”
“Usihofu Melanie.Siri
yako iko salama kwangu”
akasema Gosu Gosu
“Baba yangu na Rais
Patrice Eyenga wa DRC
walikuwa marafiki na kabla
Patrice hajawa Rais
walikuwa wanafanya
biashara pamoja.Walimiliki
kampuni kadhaa kwa
pamoja.Patrice alipotaka
kuwania urais wa Congo
kiasi kikubwa cha fedha za
kuendesha kampeni yake
alitegemea kutoka katika
biashara walizokuwa
wamechanga na
baba.Alitumia fedha nyingi
katika kampeni kwa ahadi
ya kuzirejesha pale
atakapokuwa ameshinda
urais.Baada ya kufanikiwa
kushinda urais baba
alimtaka aanze kurejesha
zile fedha ambazo ni nyingi
ili kunusuru biashara zao
lakini Rais Patrice Eyenga
alitengeneza mpango na
wazazi wangu wakauawa”
akasema Melanie na Gosu
Gosu akastuka na kuinuka
akakaa.Alihisi mwili wote
ukimsisimka kumbu kumbu
ya mauaji ya Lucy na
Laurent ikamjia
“Wazazi wako waliuawa
namna gani? Akauliza kwa
wasi wasi kidogo
“Walifariki katika ajali
ya gari ambayo tunaamini
ilitengenezwa.Gari lao dogo
liligongana na gari kubwa la
mizigo na wote wawili
wakafariki hapo hapo.Ripoti
ya wachunguzi wa
kujitegemea inaonyesha
kwamba ajali ile ilikuwa ya
kutengenezwa.Hakuna
ushahidi wa moja kwa moja
unaomuhusisha Rais Patrice
Eyenga na ajali ile lakini
tunaamini anahusika kwa
sababu kifo cha baba
kilitokea mara tu ulipoanza
mzozo kati yake na Patrice
kuhusu fedha”
“Pole sana Melanie”
akasema Gosu Gosu
“Ahsante
sana.Nimekwisha lia sana
kwa miaka mingi na machozi
yamekauka.Hivi sasa sina
tena machozi.Gosu Gosu
kilichopo katika akili yangu
kwa sasa ni jambo moja
tu.Ninataka kulipa kisasi
kwa Rais Patrice Eyenga
kwa kile alichonifanyia”
akasema Melanie na Gosu
Gosu akabaki
kimya.Alishindwa aseme nini
“Unanisikia Gosu
Gosu?akauliza Melanie
baada ya kumuona Gosu
Gosu amebaki kimya
“Nimekusikia Melanie”
“Naamini utaniunga
mkono katika harakati
zangu.Nataka Patrice
Eyenga naye apate maumivu
makali kwa kumpoteza mtu
wake wa karibu sana kama
mimi nilivyopata maumivu
makali kwa kuwapoteza
wazazi wangu” akasema
Melanie na Gosu Gosu
akahisi kama kuna kitu
kimekwama katika koo lake
akakohoa kidogo
“Gosu Gosu umekuwa
kimya ghafla baada ya
kukueleza jambo langu kuna
tatizo lolote?akauliza
Melanie
“Hapana niko sawa
Melanie”
“Unasemaje kuhusiana
nahiki
nilichokueleza?akauliza
Melanie
“Niko nawe Melanie
katika jambo lolote.Siwezi
kukuacha nyuma.Katika
jambo lolote lile nitatangulia
mbele na wewe utakuwa
nyuma yangu nitakulinda
dhidi ya hatari zozote
zinazoweza kujitokeza.Pole
sana kwa mara nyigine kwa
kifo cha wazazi wako na
Patrice Eyenga anapaswa
kulipa uovu wake
aliokufanyia.Nini unafikiria
kukifanya katika mpango
wako wa kulipiza
kisasi?akauliza Gosu Gosu
“Ahsante kwa kuniunga
mkono.Nitahitaji msaada
wako Gosu Gosu”
“Unahitaji nifanye nini
Melanie?Niambie chochote
nitakifanya” akasema Gosu
Gosu
Melanie akavuta pumzi
ndefu na kusema
“Nahitaji kuonana na
James Kasai”akasema
Melanie na Gosu Gosu
akahisi kama tumbo lake
limekuwa tupu ghafla
“James Kasai
yupi?akauliza Gosu Gosu
“Kwa miaka mingi
umekuwa katika mapigano
msituni.Humfahamu James
Kasai?akauliza Melanie
“James Kasai
ninamfahamu kama kiongozi
wa kundi la waasi walio
furushwa kutoka jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo na na
kukimbilia katika misitu ya
Uganda.Wakati James na
kundi lake wanafurushwa
jeshi la Congo lilivuka mpaka
na kuingia Uganda katika
kuwatafuta waasi hao ambao
walikataa kuweka silaha zao
chini.Uganda iliita kitendo
hicho cha wanajeshi wa
Congo kuvuka mpaka kama
kitendo cha uvamizi na
kuongeza majeshi yake
mpakani.Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo
inailaumu Uganda kuwa
inawahifadhi waasi hao na
Uganda inailaumu Congo
kwa jeshi lake kuvuka
mpaka na kuua raia wake”
“Safi sana kumbe bado
unafuatilia masuala hayo
kwa karibu.Huyo James
Kasai ambaye alikimbilia
Uganda baada ya
kufurushwa Congo ndiye
ambaye ninataka kuonana
naye.Nitakuachia wewe kazi
hiyo ya kutafuta namna ya
mimi kuweza kuonana
naye.Sifahamu utafanyaje
lakini ninachohitaji mimi ni
kupata nafasi ya kuonana na
James Kasai” akasema
Melanie
“Sawa Melanie
nitajitahidi kutafuta namna
ili uweze kuonana na huyo
mtu unayemuhitaji” akasema
Gosu Gosu
“Ndiyo maana
nakupenda sana Gosu Gosu”
akasema Melanie na kuanza
kumwagia mabusu mazito
kisha wakaingia katika
raundi nyingine ya
mtanange.
“Gosu Gosu jambo hili
nililokueleza ni siri kubwa
hivyo asifahamu mtu
yeyote”akasema Melanie
wakati akijiandaa kuondoka
“Mimi ni mwanajeshi
ninafahamu maana ya
kutunza siri hivyo usiwe na
wasiwasi mpenzi wangu”
akasema Gosu Gosu
“Nakupenda sana Gosu
Gosu” akasema Melanie na
kumbusu Gosu Gosu kisha
akaelekea katika gari lake
wakaondoka.Baada ya
Melanie kuondoka Gosu
Gosu akarejea ndani akiwa
ameinamisha kichwa alihisi
kitu kama nyundo inagonga
kichwa chake.Moja kwa moja
akaelekea katka baa yake
ndogo iliyoko mle ndani
akachukua chupa ya pombe
kali akaelekea chumbani
kwake akamimina katika
glasi akanywa yote akaweka
tena mara ya pili akanywa
yote kisha akashusha pumzi
“Melanie ametaka
kunipasua moyo wangu
leo.Mstuko nilioupata pale
aliponitamkia kwamba
Patrice Eyenga anahusika
katika vifo vya wazazi wake
ni mkubwa.Nashukuru
wazazi wake walifariki huko
Ufaransa” akawaza Gosu
Gosu na kunywa funda la
kinywaji kile kikali
akafumba macho
“Kwa nini Melanie
anataka kuonana na James
Kasai?Huyu ni mtu mbaya
na katili sana.Ni mtu
ambaye amekuwa
anatafutwa ili afikishwe
katika mahakama ya uhalifu
wa kivita kutokana na
ukatili mkubwa ambao kundi
lake liliufanya wakati
likipambana na majeshi ya
serikali ya Congo.Hadi leo
bado James ameshindwa
kukamatwa kwa sababu
anakingiwa kifua na nchi ya
Uganda ambao inadaiwa
wamempa hifadhi.Nahisi
kwamba Melanie anataka
kuandaa mipango ya kulipiza
kisasi kwa Rais Patrice
Eyenga na anataka
kumtumia James Kasai”
akawaza na kujiegemeza
sofani
“Sikutaka tena kujiingiza
katika masuala yoyote ya
mauaji,nilitaka niishi maisha
ya amani lakini siwezi
kumuacha Melanie peke
yake katika suala
hili.Lazima nisimame
naye.Ninampenda na huu ni
wakati mzuri wa
kumuonyesha ni namna gani
ninampenda na
kumthamini.Kama ni kuua
niko tayari kuua kwa ajili
yake.Nitatafuta namna ya
kumpata James Kasai”
akawaza Gosu Gosu na
kuchukua simu yake.