SEHEMU YA 11*
askari polisi wa kituo kikuu cha polisi jijini Mwanza,walikosa majibu ya maana kutoka kwa Mbena.
Kamanda mkuu wa mkoa alikuwepo pia wakati mahojiano yale yasiokuwa na majibu sahihi yakiendelea kwa mtoto yule wa waziri wa Afya.
Ajabu walioiona askari wengine mbali ya kuwa walikuwa wanamhoji mhusika wa kwanza wa mauaji ya Maiga mtoto wa waziri pia,lakini ilikuwa wazi kwao ilihitajika binti yule apelekwe hospitali kwanza maana hali yake haikuwa nzuri.
Mbena alikuwa akitoa udenda kila dakika huku ulimi ukiwa mzito kusema na hata alipoomba kalamu aandika alijikuta anashindwa maana mikono ilikuwa kama mtu aliepooza au kwa lugha nzuri mtu aliugua kiharusi.
Mbena aliwatazama maaskari waliokuwa wamemzunguka,aliwatizama kwa ishara ya kuomba msaada wa matibabu angalau kidogo apate ahueni,lakini hakuna aliemwelewa na hakuna aliejali hasa kamanda yule ambae vijana wake walikuwameshatoa pendekezo la kupelekwa hospitali kwanza ila aligoma kwa sababu anazozijua yeye.
***
Mauna Seko alikuwa akibalizi upepo wa ziwa viktoria ndani ya fukwe za Tunza jijini mwanza.
A
Mawazo yake yalikuwa mbali wakati huo huku kitu pekee kikiwa ni bukta nyepesi iliokuwa mwilini mwake.
Ilikuwa ajabu ahsubuh kabisa kumkuta mtu analipia kwenda fukweni,lakini yeye alikuwa na sababu za kufanya hivyo.
Alikuwa pale kuweka sawa akili yake baada ya kumfumania mpenzi wake akiliwa uroda na mwanaume mwingine ndani ya gari yake alionunua na kumpa mwanamke yule zandiki.
Mawazo yalimjaa pasipo kifani na hakuwa na kuyapunguza zaidi tu aliamua kutafuta pahali tulivu wakati huo na sehemu pekee ilikuwa ni hiyo.
Wakati akijaribu kurusha vimchanga viliwili vitatu ndani ya maji,alihisi harufu katika mwili wake,akageuza shingo ili atizame eneo gani lilikuwa likitoa harufu ile.
Akageuka upande wa bega la kushoto hakuona kitu,akageuka upande wa kulia akajikuta akitoa tusi zito la nguoni huku akifanya jitahada za kujifuta,alikuwa ni ndege aliemwangushia kinyesi chake.
Akiwa kamaliza kujifuta,akili ikamkaa sawa,akakumbuka kitu.
Wakati anageuka upande ule wa kulia, aliona kitu kwa mbali na hapo akageuka tena,ni kweli aliona kitu kikiwa umbali fulani kutoka pale alipo,na bila kutarajia akajikuta miguu ikiwa tayari imeanza kujongea kuelekea kule.
Alistaajabu kumkuta binti akihangaika kusimama,kwa kumtazama alikuwa akipitia mateso makali muda ule.
Haraka akarudi kule hotelini na kuita kiongozi wa Hotel ile akampa taarifa,yule aliepewa taarifa akapiga simu kituo cha polisi.
Kulingana na hali aliokuwa nayo binti Yule, Mauna Seko akaamua kuchukua jukumu la kumwahisha hospitali.
Kama ilivyokawaida ya hospitali zetu na hali aliokuwa nayo ikabidi waombe PF3 kwanza na kweli Mauna akapiga kona kugeuka ili amwahishe kituo cha polisi cha karibu hilo likawa kosa.
Alipofika tu kituoni wakaanza kumhoji huku mgonjwa akizuiliwa kupelekwa hospital.
Mauna hakuwa na namna hasa aliposikia yule aliemsaidia ndie muuaji wa Maiga akagwaya.
***
"Inawezekana vipi hii"Mauna alijiwazia mwenyewe akiwa ndani ya gari akielekea kwa mwanasheria flani ili aende kusimama kumtetea binti yule apewe matibabu.
Licha ya kupeleka mwanasheria lakini bado jitihada zake zikagonga ukuta na akabaki hana la kufanya na imani yake ikamwambia kuna la zaidi katika hayo,akachukua simu yake akzitafuta namba flani kisha muda mfupi alikuwa hewani.
Alikuwa anampigia Temba rafiki yake wa muda wote,usiku na mchana,iwe jua iwe mvua lazima watasaidiana.
Upele ukapata mkunaji,Mauna alipomaliza kuongea na simu akapiga ngumi hewani kama ishara ya ushindi baada ya kuambiwa na Temba nae yupo kwenye harakati hizohizo.
***
Asalaam Kudo.