RIWAYA: Siku kabla ya leo

RIWAYA: Siku kabla ya leo

Sehemu ya 6*

Koplo Mina aliishiwa ujanja ila hakutaka kuzubaa eneo lile akampigia konstebo Tito akamwelekeza cha kufanya juu ya mwili ule kisha akatoka akamwendea muhudumu wa mapokezi akamweleza habari zile,punde ofisi mzima ikawa na taarifa juu ya tukio lile.
Koplo Mina hakutaka kupoteza muda akatazama kushoto na kulia akaziona kamera za usalama ofisini pale,akaomba apelekwe kilipo chumba cha kuongozea kamera zile.
Akaomba aoneshwe matukio ya tangu ahsubuh,hakuna tukio au nyendo za mtu aliemstukia,isipokuwa tangu ahsubuh ni yeye peke yake aliekuwa ameonekana kuingia ofisini kwa mhariri,na hata aliporudi ni yeye alieonekana kuchomoa bastola na kuingia ndani ya ofisi ya mhariri kwa hiyo kimsingi yeye ndie muuaji.

Hakuwa na jipya alijua kama kuna mtu mkubwa anahusika katika sakata lile basi atakuwa amekwisha na kwa mara ya kwanza akajuta kuwa askari,ila hakutaka kufa kizembe akaondoa pikipiki yake akaelekea kituoni kuna jambo alipaswa kulifanya alihitaji kumtoa pale binti yule aliemkuta masai club siku ya kuuwawa Maiga.

Saa 11:59

Akiwa na haraka ya kufika kituo kikuu cha polisi koplo Mina akaona kuna pikipiki nyuma ikiwa imebeba watu wawili,hakukawia kugundua ni wale waliokimbia wakati yeye akiingia kwa mwandishi wa gazeti la Ahsubuhi yetu.

Akaongeza kasi na kuyapita magari kadhaa yaliokuwa yakisogea taratibu kutokana na foleni ahsubuh ile iliokuwa ikiishia kuelekea mchana.

Ni wakati akikaribia kusimama baada ya kuona taa za barabarani zimeashiria kusimama kwa magari upande wao,kwa kutumia kioo cha nyuma ama sitemirow aliiona ile pikipiki ikija kwa kasi usawa wake akiwa hajawaza cha kufanya ikawa imemfikia na kitendo bila kufikiri akajikuta akiitupa pikipiki yake na kwa wepesi wa hali ya juu akaruka na kuangukia upande wa pili wa barabara kwa uruka gari moja aliokua sambamba nayo huku nyuma akiacha mvua ya risasi ikimwandama.

Baada ya risasi kukoma akatoka alipokuwa amejibanza na kuchungulia hakuona mtu wala pikipiki ile,akapiga hatua kuifuata pikipiki yake iliokuwa imedondoka na kuvunja kioo cha kushoto akainyanyua huku watu wakishangaa na wasijue cha nini kwanini mwanamke yule kashambuliwa.

Wakati wao wakishangaa hilo koplo Mina alikuwa mbali na eneo lile,akafika kituoni na kumtoa binti Nyange alipokuwa kahifadhiwa na kwenda nae nyumbani kwake ila hata yeye hakujua kwanni emewaza vile.

Ni wakati akiwa karibu kabisa kinondoni karibu na duka la Robie One simu yake ikatetema kuonesha kuna mtu anapiga,akapaki pembeni na kuitoa hapo akakutana na jina la mkuu wake wa kazi Sacp Odeni, akaipokea.

"Koplo Mina unaombwa kufika ofisini mara moja,na kuanzia sasa kesi hiyo haitakuwa mikononi mwako na unatakiwa ujisalimishe mara moja kwa mauji ya Mhariri wa gazeti"

Hakutaka koplo Mina ajitetee akakata simu.
Koplo Mina hakuwa na jipya akapumua na kuikubali akili yake inawaza mbali,akamtazama Nyange kisha akamwamuru apande,alipokwisha kupanda akampeleka hadi kwake na kumwacha hapo kisha akanyanyuka na kurudi mtaani hakuwa na mpango wa kuripoti kazini wala kujisalimisha alikuwa anamfuata mtu muhimu kwa wakati huo..
..


Asalaaam Kudo (Bahati Mwamba)
 
Unamaanisha nini labda unamaana hata bila bando itafunguka? Au Mimi ndo sijakuelewa au ulimaanisha nini chief
Ndio bila bando tunapata access ya jf! Ingia kwenye browser yako andika www.freebasic.com unapata access bila gharama za data! Na kwa bahati nzuri Ni kuwa Ni legally kuingia hata max meelo anajua
 
Sehemu ya 7*


Mchinjiko alimtazama Mbena,kisha kwa utaratibu akamfuata akamshika mkono na kumwinua alipokuwa amekaa,akamkokota hadi ilipokuwa gari ikiwa imepaki na watu wengine ndani,
Kisha pasipo kuambiwa kitu akabebwa na kutupwa ndani gari lile aina ya toyota Ford,ndani Mbena alikutana na watu wengine wawili waliompokea na kumfunga uso kisha safari ikaanza na hakujua anapelekwa wapi.

Saa 12:38

Muda huu ilimkuta Mbena akiwa kwenye mchanga laini,akasimama akajipapasa akajikuta kama alivyokuwa wakati akitolewa sehemu asioijua na hakujua hata hapo alipo ni wapi,akakumbuka Mara ya mwisho alikuwa wapi,kumbukumbu zilipo mrudia vizuri akakumbuka punde alipotupwa ndani ya gari akafungwa kitambaa,kisha yakafuatia maumivu makali karibu na mkono wake,maumivu ya kuchomwa kama na sindano.

Ajabu alipojaribu kupiga hatua akashindwa,hapo akajaribu kutazama napo akashindwa akajipapasa usoni akagundua bado amezibwa uso,akanyanyua mkono na kukitoa usoni kitambaa cheusi kilichotumika kumfunga usoni.

Akatazama kushoto na kulia akagundua alikuwa ametupwa kando kando ya fukwe za bahari ama ziwa,alijaribu kuvuta taswira maeneo gani atakuwa,hakupata jibu,akajaribu kupiga tena hatua,miguu ikakataa kumpa ushirikiano,si miguu hata mwili ulikuwa hauna nguvu za kufanya lolote.

Mbena alijulikuta akitetemeka mwili mzima,hofu ikamwingia,
Midomo nayo ikamsaliti ikakataa kufumba,akaanza kutokwa na udenda,kila akijaribu kuzuia akashindwa,mikono haikunyanyuka, miguu nayo ikashindwa kuhimili akajikuta akirudi chini bila kupenda na alipojaribu kupiga kelele haikuwezekana,machozi yakaanza kumtoka,na kwa mbali hakuona msaada wowote.
*****
Koplo Mina alipaki pikipiki yake hatua kadhaa kutoka mlango wa kuingilia Lasi Vegas casino,akatazama kushoto na kulia akavuka kijia kidogo na kukifikia kimlango kidogo cha kuingizia kadi ya kufungulia mlango,akazama mfukoni akatoa kadi ile,akapachika kwenye kijimlango kile,punde mlango ukajifungua nae akazama ndani,hatua kadhaa akakutana na mlinzi wa mlango ule akiwa amevalia suti safi nyeusi,wakatazamana kisha bila kusemeshana koplo Mina akatoa kadi nyingene akamnyooshea,hakusubiri aruhusiwe akapiga hatua na kuingia ndani.

Koplo Mina akatua begi mezani bila kukaa akasema na aliemkuta ndani ya chumba kile.

"Kamba nahitaji Msaada!?"

"upi"

"kuna hii chombo hapa nimepora nataka kupata kilichomo"

Kamba akalipekua lile begi,akatoka na kompyuta mpakato,akaitazama kisha akaifungua na na kuiwasha,akainama kidogo akapekua na kutoka waya mrefu akauweka kwenye kitu mfano wa kihifandi umeme au power bank,akatulia kimya kisha akamtazama Mina,akamuuliza

"email au vihadhio"

Mina akajibu "email"

Kamba akazama kupekua kompyuta ile.
Ndani ya dakika kadhaa hakupata kitu akamtazama Mina na kuzungumza

"email nyingi ila kuna Email moja inaonekana iliingia jana na kufutwa, na alieituma inaonekana alitumia utaalamu maana nikiifuatilia ilikotoka haionekani lakini ngoja....."
.akazama tena kupekua hiki na kile punde akatoka na jibu

"inaonekana ujumbe ulitumwa kwa ems kutoka mwanza na hii ilikuwa ni saa tisa na dakika kumi usiku lakini huu ujumbe kutoka mwanza ulipokelewa kabla ya kutumwa kwenye email hii kutokea Dar es laam na huyu alietuma mwanza alikuwa amesimama au alikuwepo kituo kikubwa cha polisi"

Koplo Mina akaguna na hapo akagundua mchezeshaji wa mchezo ule alikuwepo palepale kituoni,akazama kwenye tafakuri akazama mfukoni akatoka na simu akampa Kamba,kamba akaitazama kisha akapachika kwenye kifaa kidogo,hapo akapakua vitu kadhaa kisha akatoka na jibu

"Simu ya mwisho kuingia kwake ilitoka kwa mtu anaetambulika kwa jina Temba,simu hii ilikuwa na ujumbe wa maneno pia yalioonesha walikuwa na makubaliano ya kulipana nyumbani."
Temba pia alifanya mawasiliano akitokea mtaa wa kawe karibu na kituo cha radio,nyumba namba 14

Saa 12:45

Mina alikuwa ameiacha Vegas kasino alikokwenda kukutana na rafiki yake ambae huwa anamsaidia mambo mengi ya mawasiliano na alitoka kuvikagua vifaa vya mwandishi wa habari alieuawa makumbusho.
Na sasa alikuwa njiani kuelekea kawe.

****
Walikaa wawili tu katika ofisi hii,mazungumzo yao waliyafanya kwa sauti ndogo,hata ungekuwa hatua kadhaa nyuma yao asingelisikia,wote walikuwa wanaume,
Mmoja alikuwa mnene mfupi na mwingine alikuwa mrefu mwembamba,wote walivaa mawani......




Asalaam kudo(Bahati Mwamba)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom