Sehemu ya 5*
Mbena koo lilimkauka na hakuwa na cha kufanya japo hakuwa tayari kuingiliwa kimwili na watu wale asiowajua.
Akaona kupiga kelele hakutomsaidia,njia pekee ni kukubali yeye ndie mhusika katika mauji yale,akapaza sauti kwa nguvu,sauti ile ikamfikia Mchinjiko,akasitisha zoezi la kurekodi,akawaamuru mabaunsa wale wamwache Mbena.
Walimwacha huku wakiwa na uchu wa ngono kwa binti Mbena aliekuwa kanawiri kwa wingi wa uzuri ulioanza kufifia baada ya kukutana dhahama asiojua mwisho wake.
Mchinjiko akawaamuru mabaunsa wale watoke,kisha akambeba mbena na kuingia nae chumba cha pili kilichokuwa maalumu kwa usafi wa mwili wake,akaoga kisha akaamuliwa kujiweka katika muonekano wa mtu ambae yupo huru.
Alipokwisha kuwa tayari akaletwa mbele ya kamera kisha akawekewa ubao mbele yake akaambiwa asome maelezo yale,.
Yote yalikuwa yakiendelea wakati ambao Mchinjiko alikuwa akirekodi kila kitu,na alikuwa mbele yake Mbena na ubao wenye maandishi.
*****
Koplo Mina hakuwa na ujanja mbele yake alisimama mwanaume shababi asie na mzaha na ni mtu anaeonekana kuwa kuua ni jambo jepesi,.
Akamwamuru koplo Mina aweke silaha yake chini,nae akatii,yule bwana alishindwa kuelewa jambo moja,hakuna silaha mbaya duniani kama mwanamke,na ndio yaliomkuta.
Kwa uzuri aliouona kwa Koplo Mina ukampagawisha kabisa akaona asimuue kwanza askari yule,akamletea mzaha,mara amkebehi,mara amtomase maziwa kwa mdomo wa bastola,akaona haitoshi akamsogelea karibu zaidi
Kwa mkono ulioshika bastola akaelekeza kwenye paji la uso,akashuka hadi kifuani kwa Mina,hapo akatulia kidogo akampekenyua blauzi yake,alipoona haimpi ushirikiano wa kuacha matiti wazi akazidi kushuka,hadi alipogusa kitovu.
Wakati yule bwana akifanya udhalilishaji ule hakujua hila za koplo Mina wakati gani atazifanya,yeye akazidi kushuka,akafika eneo la makutano ya maungo ya wanadamu,hapo koplo Mina akatoa mguno hafifu huku akirudisha kiuno nyuma,yule bwana akiwa kazubaishwa na mguno akastukia korodani zikiwaka moto wa pekecha,lilikuwa ni pigo mujarabu kutoka kwa koplo Mina,.
Pigo lile halikumwacha yule bwana na urijali wake,isipokuwa likamfanya awe mdogo kifikira na hakuwa na mbinu mbadala ya kukabiliana na maumivu yake zaidi ya kuweka mikono yote huko angalau azifunde mkononi korodani zake.
Hakujua ni kosa akakutana na mapigo mawili ambayo hakujua ni kutoka katika aina gani ya mapigano,mwili ukaaga roho na roho yake dhalimu ikaenda kukutana na adhabu ya milele.
Koplo akaanza kupekua nyumba ile iliokuwa na maiti mbili,hakukuta cha maana zaidi alikutana na kompyuta mpakato pamoja na simu,akavitia kwenye begi dogo lililokuwa pembeni hapo,hakuwa na la zaidi isipokuwa kupiga simu polisi ili wafike eneo lile kuendelea na utaratibu zaidi.
*****
Saa 11:07 ahsubuh
20/07/2017
Video ya mtoto wa waziri wa Afya Mbena Mnuo kujirekodi na kukiri kuhusika na mauji hayo,kisha kutumia simu yake kurusha mtandaoni ilisambaa kama moto wa kifuu na karibia robo ya watumiaji wa mitandao ya kijamii walikuwa wameiona video hiyo,huku kisa cha yeye kuua akisema Maiga hakuwa mwaminifu na alimfuma akimsaliti na kahaba vyooni.
Watu wengi walionesha kusikitishwa na taarifa ile,huku wanafunzi wengi wa vyuo mbalimbali wakilaani vikali tukio lile,ilifikia hatua hata ndugu wa pande zote mbili kuanza kurumbana kila upande ukimtuhumu mwenzie,.
Wakati hayo yakiendelea IGP alitoa tamko rasimi kwa vijana wake Mbena atafutwe na akamatwe mara moja kwa kuhusika na kifo cha mtoto wa waziri wa kilimo na rais wa serikali ya wanafunzi dar es laam,..
Vijana wakaingia kazini rasimi wakitumia magari na hata mtandao kumsaka binti yule alieaminika amejificha mahali.
*****
Taarifa zote zile kuna mtu alikuwa anazifuatilia kwa makini sana.
Kisha akachukua simu akapiga mahali,punde upande wa pili ukaitikia na yeye akasema
"Imekuwa kama tulivyotaka"
Kisha akasikiliza upande wa pili kidogo akakata simu na kuiweka mfukoni na akatoka nje ya eneo alilokuwa akatokomea anakokujua.
*****
Yote hayo yalipokuwa yakiendelea Koplo Mina yeye alikuwa ndo anarikabia lango la ofisi za Lengo media,akiwa na shauku ya kukutana na mhariri wa gazeti lile akiamini atampa taarifa muhimu anazozihitaji,akapita kwa pupa hadi mlangoni,na bila kufuata utaratibu akazama ofisini kwa mhariri bastola yake mbele,akapigwa na butwaa hakutarajia kukiona alichokiona mbele yake,bwana Mgimba alikuwa amekaa kwenye dimbwi la damu huku ikionesha risasi zaidi ya tatu zikiwa zimezama kifuani pake.....
Nb:Napenda kuwakumbusha kwa mwenye nia ya kuniunga mkono ili nipige zaidi hatua na Mimi basi nakuomba nichangie kupitia no hizi
0758573660
0658564341
0624155629
Asalaam Kudo.