the_legend
JF-Expert Member
- Jan 14, 2019
- 1,612
- 7,112
- Thread starter
- #161
RIWAYA : SALA YA SARAH.
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI.
ILIPOISHIA....................
Baada ya muda yule bwana aliyekuwa anatoa matangazo alikuwa amemaliza na sasa askofu akachukua kipaza sauti, kisha akawasalimu waumini waliohudhuria ibada, baada ya hapo akairudia ile sala iliyowahi kuombwa na Sarah miaka mingi iliyopita, wakati akiirudia ile sala, Taita alishtuka, tena uzuri alikuwa amekaa kiti cha mbele kabisa pamoja na Harry ambaye nae alipata mshtuko,
Masikio na mwili wa Taita vikapata ubaridi kwa pamoja wakati askofu akiirudia ile sala, Taita akakumbuka na ule ujumbe aliouona kwenye box upande wa chini, box ambalo kiliwekwa kichwa cha Toisa, ila bado Taita alisubiri kusikia ni kipi askofu ataongea baada ya kuirudia sala ile,
"Sasa baada ya kuirudia sala hii iliyowahi kuombwa na mtoto mdogo miaka kumi na Tisa iliyopita, leo hii huyu mtoto yupo hapa, namuomba asogee mbele" Askofu aliongea kisha Sarah akawa anajongea mbele huku waumini wakimpigia makofi. Sarah alipofika mbele akapewa kipaza sauti,
"Naitwa Sarah, Sarah Isack" Sarah aliongea kisha akatupia macho mahali walipokaa Taita na Harry na kuwaona namna walivyopata mshtuko, tena sio kidogo........
************ENDELEA***********
Sarah akatabasamu, halikuwa tabasamu alilolipanga, lilikuwa ni tabasamu lililokuja ghafla baada ya kuwaona maadui zake walivyopata mshtuko baada ya yeye Sarah kujitambulisha.
"Mimi ndiye yule mtoto niliyetoa sala miaka kumi na tisa iliyopita, na niliitoa nikiwa na maanisha kile nilichokiomba, sikuwa nasali tu ili mradi maneno yanitoke, nilitaka niwe mkubwa na niwe moto, tena moto kweli, nashukuru nimekuwa hivyo" Sarah aliongea na kufanya baadhi ya waamini wabaki na maswali, sio hao tu, mpaka askofu mwenyewe sura yake ilionesha ana swali,
"Umekuaje moto sasa?" Askofu alijikuta anauliza bila kutegemea,
"Na ninaposema nimekuwa moto simaanishi nawaka, hapana, maana yangu ni ule uwezo niliokuwa nao wa kushinda kila kikwazo kilichopo mbele yangu, na nadhani hiyo yote ni kutokana na Mungu kusimamia kila nifanyacho. Nawashukuru sana, maana mimi ni muongeaji sana, mnaweza shangaa naongea tu mpaka nachukua muda wa misa zote" Sarah alitania kisha waumini wakacheka, Sarah akarudisha kipaza sauti kwa askofu.
"Pia napenda kuwaambia habari njema kuhusu Sarah, Sarah ametoa ahadi ya kutoa mifuko mia moja ya cement kwa ajili ya kabisa" Askofu aliongea na waumini wakalipuka kwa furaha na huku wengine wakipiga makofi na vigele gele.
"Basi nadhani tutegemee kumuona hapa sarah mara kwa mara kwa maana amekuzwa na imani yetu" Askofu aliongea kisha akaweka kipaza sauti sehemu husika, kisha wakaongea kidogo na Sarah na baada ya hapo Sarah akawapa mikono mapadri na watumishi waliokuwepo mbele ya kanisa, kisha Sarah na askofu wakaanza kutoka kuelekea nje ya kanisa.
Walipokuwa wanatoka ndipo Sarah akayapeleka macho yake sehemu alipokuwa amekaa Taita, wakagongana macho, Sarah akatabasamu kisha akambinyia jicho Taita ambaye muda wote alikuwa amekamatwa na mshangao.
Sarah alitoka moja kwa moja mpaka ofisini kwa askofu,
"Sina muda tena was kukaa hapa, labda unisaidie tu namba ya account ya benk ambayo inatumiwa na kanisa" Sarah aliongea huku akimtupia jicho askofu ambaye alikuwa ameshika pen na akachukua karatasi akaandika namba ambayo Sarah anaihitaji,
"Mbona haraka hivyo" Askofu alimuuliza huku akimpatia ile karatasi,
"Kawaida, nitarudi siku chache zijazo baba askofu, ila pesa nitaiingiza kesho mapema kwenye account ya kanisa, kwa maana leo jumapili benki zimefungwa" Sarah aliongea huku akinyanyuka katika kiti,
"Sawa haina shida" askofu aliongea huku akipeana mkono na Sarah, kisha Sarah akaondoka zake.
Sarah alipotoka kwenye mlango was askofu, alipiga hatua za haraka haraka mpaka nje ya uzio wa kanisa na kwenda kuingia kwenye bajaj ambayo ndiyo ilimleta eneo lile la kanisa,
"Subiri kidogo, kuna mtu namsubiri" Sarah alimwambia dereva bajaj ambaye alitaka aiwashe bajaj yake,
"Sawa bosi" dereva bajaj alijibu na kutulia.
Baada ya dakika chache waumini walianza kutoka katika jengo la ibada kumaanisha kwamba misa imeisha, hapo ndipo Sarah aliweza kumuona Taita na Harry wakitoka, akashuhudia namna wanavyoangaza angaza macho wakiashiria kuwa kuna kitu wanatafuta.
Baada ya muda aliwashuhudia wakiongozana kuelekea ofisi ya askofu, Sarah akatabasamu peke yake,
"Haya washa bajaj tuondoke" Sarah alimwambia dereva Bajaj ambaye alitii na kuiwasha bajaj kisha wakaondoka taratibu na kupotea eneo lile la kanisa.
********************
Taita na Harry walielekea moja kwa moja mpaka mlangoni kwa askofu na kubisha hodi, askofu akaitikia na kisha wakaingia ndani, wakamsalimia askofu na kujikaribisha wenyewe kwenye viti,
"Samahani kwa kukuingilia" Taita aliongea huku akitabasamu,
"Bila samahani" Askofu alijibu,
"Nilikuwa nahitaji kuonana na yule binti, Sarah" Taita aliongea huku akimtazama askofu,
"Una maongezi nae labda, au kuna chochote?" Askofu alimuuliza Taita,
"Yule ni mtoto wa marehemu Dada yangu, baada ya Dada yangu kufariki miaka kumi na Tisa iliyopita, Sarah aliondoka na kwenda kusoma uingereza, sijawahi kubahatika kumuona tena mpaka leo" Taita aliongea,
"Kwa hiyo anakuita Mjomba?" Askofu alimuuliza,
"Ndio" Taita alijibu,
"Sawa, ila kwa bahati mbaya huyo Sarah ameshaondoka" Askofu alitoa jibu lililofanya Harry na Taita watazamane,
"Ameondoka muda mrefu?" Harry aliuliza,
"Sasa hivi tu" Askofu alijibu,
"OK, basi nisaidie namba yake ya simu" Taita aliongea huku akiitoa simu yake mfukoni,
"Bahati mbaya ameniambia kuwa hana simu" Askofu alitoa jibu jingine lenye ukakasi,
"Dah, hajasema hata eneo analoishi?" Taita aliuliza tena,
"Hapana, ila kama shida yako ni kuonana nae tu, mtaonana, maana atakuwa anakuja hapa mara kwa mara" Askofu akajibu,
"Sawa askofu, akirudi basi naomba unifahamishe, maana ni mtu muhimu sana kwangu" Taita aliongea,
"Sawa"'Askofu alijibu kisha Taita na Harry wakaondoka zao na kumuacha Askofu akiendelea na mambo yake.
Taita na Harry walielekea moja kwa moja kwenye gari walilokuja nalo na kumkuta Trigger akiwa anawasubiri ndani ya gari,
"Mbona ibada imeisha muda tu, alafu ninyi mnatoka sasa hivi?" Trigger aliwauliza huku akiwasha gari,
"Trigger moto umewaka sasa, ni jinsi gani tutauzima?" Taita aliuliza huku akijifuta jasho. ila swali alilouliza ni kwamba Trigger hakulielewa,
"Moto umewaka wapi?" Trigger aliuliza huku akimtupia jicho bosi wake huyo,
"Kumbe matukio yote tunayofanyiwa na mtu asiyejulikana, kumbe mtu huyo ni Sarah" Taita aliongea huku macho yakiwa mbele,
"Sarah kale kabinti ka kipindi kile, Dada ake vin?" Trigger aliuliza kwa mshangao,
"Ndio huyo huyo" Taita alijibu kinyonge,
"Yaani kale katoto ndio kamekuwa hatari hivyo?" Trigger aliuliza huku akitoa tabasamu lililoambatana na mshangao,
"Nadhani amekuja kulipa kisasi, sasa basi umakini uongezeke, jambo zuri ni kwamba tumeshamjua adui yetu" Taita aliongea,
"Jioni itabidi tuitishe kikao, lazima tujadili hili jambo" Harry aliongea,
"Ni kweli" Taita alijibu wakati gari ikiingizwa ndani ya uzio wa nyumba yake.
**"****************
Sarah alielekea moja kwa moja mpaka katika sehemu ambapo yanauzwa magari, akaingia ndani na kuwasalimia wahusika,
"Nimekuja kuangalia magari" Sarah aliongea baada ya salamu,
"Karibu, twende upande ule" Kijana aliyekuwa muuzaji aliongea huku akinyooshea kidole upande ambao anatakiwa aende.
Wakaelekea mpaka katika huo upande ambao kulikuwa na gari ndogo nyingi, Sarah akaanza kutafuta gari ambayo alihisi itamfaa. Baada ya dakika ishirini alisimama mbele ya gari ambayo ilionekana ameipenda, ilikuwa ni range rover sports, nyeusi.
"Bei gani hii" Sarah aliuliza huku akiikagua tairi zake, muuzaji akamtajia bei,
"Mnapokea cash au cheque?" Sarah akauliza,
"Tunapokea vyote, ila cash nadhani ndio haina mlolongo mrefu, ukishakabidhi tu unapatiwa gari, ila cheque ukikabidhi hupatiwi gari mpaka benki itoe uhakiki kuwa ni kweli account yako ina fedha hizo" Kijana muuzaji alitoa ufafanuzi,
"Sawa, nitatoa cash" Sarah aliongea huku akitabasamu,
"Ikague kwanza vizuri gari yako, alafu twende ofisini tukakabidhiane pesa" Kijana muuza magari aliongea huku akifungua mlango was ile gari na kisha Sarah akaanza kuikagua upande wa ndani, alipojiridhisha, walienda ofisini na kukabidhiana pesa, kisha Sarah akatoka na gari yake.
*****************
Mida ya saa kumi jioni, Taita na vijana wake walikuwa Vin hotel wakiendelea na kikao kizito kumuhusu Sarah,
"sasa mnaona kipi kifanyike kumdhiti au kummaliza kabisa Sarah?"Taita aliuliza,
"yaani suala la kumdhiti au kummaliza yote hayawezekani, kwa maana yeye anatujua vizuri sisi kuliko sisi tunavyomjua yeye" Tekso alijibu katika sauti ya utulivu,
"nadhani kumdhibiti tunaweza" Trigger aliongea kisha akachukua glass ya maji na kuipeleka kinywani na wenzake wakawa wanangojea kumsikiliza,
"tunamdhibiti vipi sasa?"Harry aliuliza baada ya kumuona Trigger yupo kimya ingali amemaliza kunywa maji,
"babu yake Sarah si yupo? nadhani tunatakiwa tumteke, alafu Sarah ni lazima ajue tu, akishajua ni lazima atatutafuta" Trigger aliongea na wenzake wakampigia makofi,
"hiyo ifanyike lini? " Taita aliuliza huku akitabasamu,
" leo hii, maana tukichelewa yule demu anaweza kutuzidi akili " Trigger alijibu,
"safi, nadhani muda huu Trigger chukua vijana na muende mkafanye hichi tulichopanga" Taita aliongea huku akimtazama Trigger.
********************
Mishale ya saa mbili usiku Sarah alikuwa yupo juu ya sofa ndani ya sebule yake akicheza game, play station, alikuwa akicheza game ya kivita, kitu ambacho hakukijua ni kuwa muda huo Trigger na vijana wake walikuwa wameizunguka nyumba ya babu yake.
Trigger baada ya kuizunguka nyumba ile na kujiridhisha hakuna kitu chochote cha kuwazuia, aliwahamrisha vijana wake na kuusogelea mlango, walipoufikia waligonga hodi, mlango ukafunguliwa na babu yake Sarah, ila cha ajabu alikutana na mdomo wa bunduki,
"eh!!! Shusha bunduki wewe" Babu Sarah alijikuta akitamka hayo maneno Bila kutegemea,
"Trigger akikunyooshea bunduki uwa haishushi chini mpaka risasi itoke" Trigger aliongea huku akitabasamu kisha akafyatua risasi kumuelekea babu yake Sarah................
**********ITAENDELEA***********
the Legend☆
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI.
ILIPOISHIA....................
Baada ya muda yule bwana aliyekuwa anatoa matangazo alikuwa amemaliza na sasa askofu akachukua kipaza sauti, kisha akawasalimu waumini waliohudhuria ibada, baada ya hapo akairudia ile sala iliyowahi kuombwa na Sarah miaka mingi iliyopita, wakati akiirudia ile sala, Taita alishtuka, tena uzuri alikuwa amekaa kiti cha mbele kabisa pamoja na Harry ambaye nae alipata mshtuko,
Masikio na mwili wa Taita vikapata ubaridi kwa pamoja wakati askofu akiirudia ile sala, Taita akakumbuka na ule ujumbe aliouona kwenye box upande wa chini, box ambalo kiliwekwa kichwa cha Toisa, ila bado Taita alisubiri kusikia ni kipi askofu ataongea baada ya kuirudia sala ile,
"Sasa baada ya kuirudia sala hii iliyowahi kuombwa na mtoto mdogo miaka kumi na Tisa iliyopita, leo hii huyu mtoto yupo hapa, namuomba asogee mbele" Askofu aliongea kisha Sarah akawa anajongea mbele huku waumini wakimpigia makofi. Sarah alipofika mbele akapewa kipaza sauti,
"Naitwa Sarah, Sarah Isack" Sarah aliongea kisha akatupia macho mahali walipokaa Taita na Harry na kuwaona namna walivyopata mshtuko, tena sio kidogo........
************ENDELEA***********
Sarah akatabasamu, halikuwa tabasamu alilolipanga, lilikuwa ni tabasamu lililokuja ghafla baada ya kuwaona maadui zake walivyopata mshtuko baada ya yeye Sarah kujitambulisha.
"Mimi ndiye yule mtoto niliyetoa sala miaka kumi na tisa iliyopita, na niliitoa nikiwa na maanisha kile nilichokiomba, sikuwa nasali tu ili mradi maneno yanitoke, nilitaka niwe mkubwa na niwe moto, tena moto kweli, nashukuru nimekuwa hivyo" Sarah aliongea na kufanya baadhi ya waamini wabaki na maswali, sio hao tu, mpaka askofu mwenyewe sura yake ilionesha ana swali,
"Umekuaje moto sasa?" Askofu alijikuta anauliza bila kutegemea,
"Na ninaposema nimekuwa moto simaanishi nawaka, hapana, maana yangu ni ule uwezo niliokuwa nao wa kushinda kila kikwazo kilichopo mbele yangu, na nadhani hiyo yote ni kutokana na Mungu kusimamia kila nifanyacho. Nawashukuru sana, maana mimi ni muongeaji sana, mnaweza shangaa naongea tu mpaka nachukua muda wa misa zote" Sarah alitania kisha waumini wakacheka, Sarah akarudisha kipaza sauti kwa askofu.
"Pia napenda kuwaambia habari njema kuhusu Sarah, Sarah ametoa ahadi ya kutoa mifuko mia moja ya cement kwa ajili ya kabisa" Askofu aliongea na waumini wakalipuka kwa furaha na huku wengine wakipiga makofi na vigele gele.
"Basi nadhani tutegemee kumuona hapa sarah mara kwa mara kwa maana amekuzwa na imani yetu" Askofu aliongea kisha akaweka kipaza sauti sehemu husika, kisha wakaongea kidogo na Sarah na baada ya hapo Sarah akawapa mikono mapadri na watumishi waliokuwepo mbele ya kanisa, kisha Sarah na askofu wakaanza kutoka kuelekea nje ya kanisa.
Walipokuwa wanatoka ndipo Sarah akayapeleka macho yake sehemu alipokuwa amekaa Taita, wakagongana macho, Sarah akatabasamu kisha akambinyia jicho Taita ambaye muda wote alikuwa amekamatwa na mshangao.
Sarah alitoka moja kwa moja mpaka ofisini kwa askofu,
"Sina muda tena was kukaa hapa, labda unisaidie tu namba ya account ya benk ambayo inatumiwa na kanisa" Sarah aliongea huku akimtupia jicho askofu ambaye alikuwa ameshika pen na akachukua karatasi akaandika namba ambayo Sarah anaihitaji,
"Mbona haraka hivyo" Askofu alimuuliza huku akimpatia ile karatasi,
"Kawaida, nitarudi siku chache zijazo baba askofu, ila pesa nitaiingiza kesho mapema kwenye account ya kanisa, kwa maana leo jumapili benki zimefungwa" Sarah aliongea huku akinyanyuka katika kiti,
"Sawa haina shida" askofu aliongea huku akipeana mkono na Sarah, kisha Sarah akaondoka zake.
Sarah alipotoka kwenye mlango was askofu, alipiga hatua za haraka haraka mpaka nje ya uzio wa kanisa na kwenda kuingia kwenye bajaj ambayo ndiyo ilimleta eneo lile la kanisa,
"Subiri kidogo, kuna mtu namsubiri" Sarah alimwambia dereva bajaj ambaye alitaka aiwashe bajaj yake,
"Sawa bosi" dereva bajaj alijibu na kutulia.
Baada ya dakika chache waumini walianza kutoka katika jengo la ibada kumaanisha kwamba misa imeisha, hapo ndipo Sarah aliweza kumuona Taita na Harry wakitoka, akashuhudia namna wanavyoangaza angaza macho wakiashiria kuwa kuna kitu wanatafuta.
Baada ya muda aliwashuhudia wakiongozana kuelekea ofisi ya askofu, Sarah akatabasamu peke yake,
"Haya washa bajaj tuondoke" Sarah alimwambia dereva Bajaj ambaye alitii na kuiwasha bajaj kisha wakaondoka taratibu na kupotea eneo lile la kanisa.
********************
Taita na Harry walielekea moja kwa moja mpaka mlangoni kwa askofu na kubisha hodi, askofu akaitikia na kisha wakaingia ndani, wakamsalimia askofu na kujikaribisha wenyewe kwenye viti,
"Samahani kwa kukuingilia" Taita aliongea huku akitabasamu,
"Bila samahani" Askofu alijibu,
"Nilikuwa nahitaji kuonana na yule binti, Sarah" Taita aliongea huku akimtazama askofu,
"Una maongezi nae labda, au kuna chochote?" Askofu alimuuliza Taita,
"Yule ni mtoto wa marehemu Dada yangu, baada ya Dada yangu kufariki miaka kumi na Tisa iliyopita, Sarah aliondoka na kwenda kusoma uingereza, sijawahi kubahatika kumuona tena mpaka leo" Taita aliongea,
"Kwa hiyo anakuita Mjomba?" Askofu alimuuliza,
"Ndio" Taita alijibu,
"Sawa, ila kwa bahati mbaya huyo Sarah ameshaondoka" Askofu alitoa jibu lililofanya Harry na Taita watazamane,
"Ameondoka muda mrefu?" Harry aliuliza,
"Sasa hivi tu" Askofu alijibu,
"OK, basi nisaidie namba yake ya simu" Taita aliongea huku akiitoa simu yake mfukoni,
"Bahati mbaya ameniambia kuwa hana simu" Askofu alitoa jibu jingine lenye ukakasi,
"Dah, hajasema hata eneo analoishi?" Taita aliuliza tena,
"Hapana, ila kama shida yako ni kuonana nae tu, mtaonana, maana atakuwa anakuja hapa mara kwa mara" Askofu akajibu,
"Sawa askofu, akirudi basi naomba unifahamishe, maana ni mtu muhimu sana kwangu" Taita aliongea,
"Sawa"'Askofu alijibu kisha Taita na Harry wakaondoka zao na kumuacha Askofu akiendelea na mambo yake.
Taita na Harry walielekea moja kwa moja kwenye gari walilokuja nalo na kumkuta Trigger akiwa anawasubiri ndani ya gari,
"Mbona ibada imeisha muda tu, alafu ninyi mnatoka sasa hivi?" Trigger aliwauliza huku akiwasha gari,
"Trigger moto umewaka sasa, ni jinsi gani tutauzima?" Taita aliuliza huku akijifuta jasho. ila swali alilouliza ni kwamba Trigger hakulielewa,
"Moto umewaka wapi?" Trigger aliuliza huku akimtupia jicho bosi wake huyo,
"Kumbe matukio yote tunayofanyiwa na mtu asiyejulikana, kumbe mtu huyo ni Sarah" Taita aliongea huku macho yakiwa mbele,
"Sarah kale kabinti ka kipindi kile, Dada ake vin?" Trigger aliuliza kwa mshangao,
"Ndio huyo huyo" Taita alijibu kinyonge,
"Yaani kale katoto ndio kamekuwa hatari hivyo?" Trigger aliuliza huku akitoa tabasamu lililoambatana na mshangao,
"Nadhani amekuja kulipa kisasi, sasa basi umakini uongezeke, jambo zuri ni kwamba tumeshamjua adui yetu" Taita aliongea,
"Jioni itabidi tuitishe kikao, lazima tujadili hili jambo" Harry aliongea,
"Ni kweli" Taita alijibu wakati gari ikiingizwa ndani ya uzio wa nyumba yake.
**"****************
Sarah alielekea moja kwa moja mpaka katika sehemu ambapo yanauzwa magari, akaingia ndani na kuwasalimia wahusika,
"Nimekuja kuangalia magari" Sarah aliongea baada ya salamu,
"Karibu, twende upande ule" Kijana aliyekuwa muuzaji aliongea huku akinyooshea kidole upande ambao anatakiwa aende.
Wakaelekea mpaka katika huo upande ambao kulikuwa na gari ndogo nyingi, Sarah akaanza kutafuta gari ambayo alihisi itamfaa. Baada ya dakika ishirini alisimama mbele ya gari ambayo ilionekana ameipenda, ilikuwa ni range rover sports, nyeusi.
"Bei gani hii" Sarah aliuliza huku akiikagua tairi zake, muuzaji akamtajia bei,
"Mnapokea cash au cheque?" Sarah akauliza,
"Tunapokea vyote, ila cash nadhani ndio haina mlolongo mrefu, ukishakabidhi tu unapatiwa gari, ila cheque ukikabidhi hupatiwi gari mpaka benki itoe uhakiki kuwa ni kweli account yako ina fedha hizo" Kijana muuzaji alitoa ufafanuzi,
"Sawa, nitatoa cash" Sarah aliongea huku akitabasamu,
"Ikague kwanza vizuri gari yako, alafu twende ofisini tukakabidhiane pesa" Kijana muuza magari aliongea huku akifungua mlango was ile gari na kisha Sarah akaanza kuikagua upande wa ndani, alipojiridhisha, walienda ofisini na kukabidhiana pesa, kisha Sarah akatoka na gari yake.
*****************
Mida ya saa kumi jioni, Taita na vijana wake walikuwa Vin hotel wakiendelea na kikao kizito kumuhusu Sarah,
"sasa mnaona kipi kifanyike kumdhiti au kummaliza kabisa Sarah?"Taita aliuliza,
"yaani suala la kumdhiti au kummaliza yote hayawezekani, kwa maana yeye anatujua vizuri sisi kuliko sisi tunavyomjua yeye" Tekso alijibu katika sauti ya utulivu,
"nadhani kumdhibiti tunaweza" Trigger aliongea kisha akachukua glass ya maji na kuipeleka kinywani na wenzake wakawa wanangojea kumsikiliza,
"tunamdhibiti vipi sasa?"Harry aliuliza baada ya kumuona Trigger yupo kimya ingali amemaliza kunywa maji,
"babu yake Sarah si yupo? nadhani tunatakiwa tumteke, alafu Sarah ni lazima ajue tu, akishajua ni lazima atatutafuta" Trigger aliongea na wenzake wakampigia makofi,
"hiyo ifanyike lini? " Taita aliuliza huku akitabasamu,
" leo hii, maana tukichelewa yule demu anaweza kutuzidi akili " Trigger alijibu,
"safi, nadhani muda huu Trigger chukua vijana na muende mkafanye hichi tulichopanga" Taita aliongea huku akimtazama Trigger.
********************
Mishale ya saa mbili usiku Sarah alikuwa yupo juu ya sofa ndani ya sebule yake akicheza game, play station, alikuwa akicheza game ya kivita, kitu ambacho hakukijua ni kuwa muda huo Trigger na vijana wake walikuwa wameizunguka nyumba ya babu yake.
Trigger baada ya kuizunguka nyumba ile na kujiridhisha hakuna kitu chochote cha kuwazuia, aliwahamrisha vijana wake na kuusogelea mlango, walipoufikia waligonga hodi, mlango ukafunguliwa na babu yake Sarah, ila cha ajabu alikutana na mdomo wa bunduki,
"eh!!! Shusha bunduki wewe" Babu Sarah alijikuta akitamka hayo maneno Bila kutegemea,
"Trigger akikunyooshea bunduki uwa haishushi chini mpaka risasi itoke" Trigger aliongea huku akitabasamu kisha akafyatua risasi kumuelekea babu yake Sarah................
**********ITAENDELEA***********
the Legend☆
