Riwaya: Sala ya Sarah

Riwaya: Sala ya Sarah

Babu kazingua kinoma, amejua kutukera

the Legend☆
Kwa mtazamo wetu sisi wasomaji tunaona babu kazingua lakini ukweli anaujua mtunzi kwa nini tukio hilo likawepo, yawezakuwa kaliweka makusudi uone jinsi gani Sala atapona kwa mara nyingine
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA.

ILIPOISHIA.......................

Safari yao iliishia ndani ya chumba kimoja ambacho ndani yake alikuwepo babu yake Sarah, Sarah alishtuka ila alijikaza,

"kaendelee na kazi" Trigger alimwambia Sarah kisha Trigger akasimama pale mlangoni, Sarah akamsogelea babu yake,

"babu mimi ni Sarah" Sarah aliongea kwa sauti ndogo ila iliyosikika vyema kwa babu yake,

"Sarah??? Kumbe wewe ni Sarah mjukuu wangu?" Babu yake Sarah aliongea kwa sauti kubwa iliyosikiwa vyema na Trigger, Trigger akachomoa bastola na kumuelekezea Sarah......
.

"umeharibu babu" Sarah aliongea katika sauti iliyokata tamaa............

*********ENDELEA*********

Sarah hakua na jinsi, alichomoa kisu kutoka katika koti lake la kidaktari na kukirusha kwa kasi kumuelekea Trigger, Trigger akaruka pembeni na kushuhudia mkasi ukija usawa wa kichwa chake, Trigger akainama, aliponyanyua uso hakukuta mtu mwingine zaidi ya babu yake Sarah ambaye alikuwa akimshuhudia mjukuu wake akipambana.

Trigger akatoka mbio kuelekea nje, koridoni aliweza kuwapita vijana wake wakiwa wamelala chini kutokana na kipigo walichokipata kutoka kwa Sarah.

Trigger alitoka mpaka nje na kukuta gari yake ikiondoka kwa kasi, ilikuwa ikiendeshwa na Sarah, Trigger baada ya kushuhudia ule mwendo, alijikuta akipata uvivu hata kuchukua gari nyingine ili akimbizane na Sarah, na wakati huo vijana wengine walikuwa wakitoka ndani kuungana nae,

"tuchukue gari tumfuate?" kijana mmoja aliuliza lakini Trigger hakujibu, badala yake aliingia ndani mpaka katika kile chumba ambacho alifungwa babu yake Sarah, na kumtazama mzee yule kwa muda, kisha akatoka zake nje na kuufunga ule mlango.

Trigger akaelekea mpaka nje na kuchukua gari nyingine, akaingia ndani ya lile gari na kuliwasha, kisha akamuita kijana mmoja,

"mtu asiingie, wala mtu asitoke ndani ya nyumba hii" Trigger aliongea huku uso wake ukionekana umejaa ghadhabu,

"sawa mkuu" kijana alijibu kisha Trigger akaondoka na ile gari.

Safari Trigger iliishia nyumbani kwa Taita, akaiingiza gari ndani ya geti kisha akatelemka na kuingia moja kwa moja ndani ya nyumba, safari yake iliishia sebuleni kwa Taita, bahati nzuri alimkuta Taita akiwa amekaa na Harry sebuleni, wote walipata mshangao baada ya kumuona Trigger muda huo.

"we vipi, mbona sa hivi upo hapa?" Taita aliuliza huku akiiangalia saa yake ya mkononi,

"huko sio kwema hata kidogo?" Trigger alijibu huku akikaa kwenye kochi na kufanya wenzie waogope,

"kuna nini?" Taita alimuuliza,

"Sarah ametuvamia" Trigger alitoa jibu lililomfanya Taita macho yamtoke,

"kwa hiyo umemkimbia?" Taita aliendelea kuuliza,

"yeye ndio amekimbia" Trigger alijibu,

"ebu tueleze vizuri, mbona kama unatuvuruga" Harry aliongea baada ya kuona hamuelewi Trigger, kisha Trigger akaelezea mwanzo mpaka mwisho,

"kwa hiyo unataka kuniambia kuwa yule Dokta ni Sarah" Taita aliuliza,

"inawezekana" Trigger alijibu,

"Sidhani, kama angekuwa ni Sarah angeshamsaidia babu yake tangu mwanzo" Harry alijibu,

"kwa hiyo wewe unahisi nini?" Taita alimuuliza Harry,

"Mimi nadhani inawezekana Sarah alimteka daktari na kumshurutisha aeleze ana uhusiano gani na sisi" Harry aliongea hisia zake,

"basi kwa namna yoyote ile hata huyo Dokta Pendo anahusika, kwa maana nilimwambia iwe siri, yeye ameshindwa kutunza" Trigger aliongea,

"unapafahamu anapoishi huyo Dokta?" Harry alimuuliza Trigger,

"ndio" Trigger alijibu,

"kwanini usiende nyumbani kwa huyo Dokta Pendo?" Harry aliuliza,

"nadhani hatuwezi kumkuta, atakuwa amekimbia" Trigger alijibu,

"Mimi nadhani yule mzee inahitajika ahamishwe, aondolewe pale" Taita alimwambia Trigger,

"tumpeleke wapi?" Trigger aliuliza,

"nadhani tumpeleke kwa Harry" Taita aliongea,

"kwangu!!!!!?? Hapana mkuu, naomba hayo mambo muyaweke mbali na familia yangu" Harry aliongea kwa jazba,

"nitawapeleka kwangu, ila yule mwanae itabidi tumuachie tu" Trigger aliongea,

"bora iwe hivyo, maana wakiendelea kukaa pale itakuwa hatari" Taita aliongea,

"dah, tujitahidi tumdhibiti sasa hivi, maana tukishindwa kumdhibiti muda huu, wote tutakufa" Harry aliongea kwa sauti tulivu.

"basi acheni mimi nikafanye utaratibu wa kumuamisha yule mzee, alafu nitarudi baadae" Trigger aliongea huku akinyanyuka kwenye kochi,

"hujaniambia hali ya mzee lakini, anaendeleaje?" Taita alimuuliza Trigger,

"mzee anaendelea vizuri" Trigger alijibu,

"anahitaji daktari tena?" Taita aliuliza,

"Sidhani, ngoja nikaangalie hali yake alafu nitakupa jibu" Trigger alijibu huku akiondoka,

"kuwa muangalifu" Taita aliongea wakati Trigger akipotelea mlangoni.

"hii ni hatari sana, yaani adui anaingia mpaka ndani na hawajamtambua? Kwa hiyo bila ya yule mzee kulopoka basi wote wangekufa" Harry aliongea huku hofu ya wazi ikijionesha machoni mwake.

"kweli ni hatari sana, ila Harry kumbuka hii ni vita, hatutakiwi kurudi nyuma wala kuogopa, uzuri ni kwamba adui yetu tumeshamjua" Taita aliongea kwa kujiamini huku akimtazama Harry,

"ubaya ni kuwa yeye anatufahamu vizuri, na ndio maana anaweza kwenda katika nyumba ya yoyote kati yetu, sisi hatujui anapokaa" Harry aliongea kwa sauti tulivu,

"kutudhuru hawezi na ndio maana mpaka sasa hajafanya hivyo" Taita aliendelea kujiamini,

"sawa bwana, ila nilichofanyiwa si unakikumbuka?" Harry aliuliza,

"naona uoga umeshakuingia, ila kumbuka, hakuna mtu yoyote atakayetoka nje ya hii vita, na yoyote atakayesaliti hii kitu ni lazima auawe" Taita aliongea na kusimama kisha akaelekea zake chumbani na kumuacha Harry akiwa katika fikra nzito.

**********************

Sarah alivyoondoka na gari ya Trigger, alienda nalo mpaka mjini na kulitelekeza, akachukua bajaj iliyompeleka mpaka nyumbani kwake, alipofungua mlango tu alishtuka kuona anakabwa shingo, sema kabali yenyewe haikuwa nzito ila ilionesha mkabaji alidhamilia kufanya kitu, Sarah alifanya kama anainamia mbele kisha akamtupa kwa mbele mkabaji, alikuwa ni Dokta Pendo.

Alivyotupwa kwa mbele akainuka na kukunja ngumi, Sarah akajikuta anatabasamu, kwa maana alishaona huyo mtu hawezi chochote,

"ebu Kaa kwenye kochi tuongee, sina ubaya na wewe" Sarah aliongea huku akimuangalia Dokta Pendo,

"sitaki kuongea na wewe, ninachotaka ni kurudi kwangu" Dokta Pendo aliongea kwa ukali,

"kwako utarudi, ila nisikilize kwanza nataka nikwambie nini, upo hatarini wewe" Sarah aliongea kwa upole,

"sema" Dokta Pendo aliongea huku akiwa amesimama,

"yule mzee unaepelekwa kumtibu, ni babu yangu na alitekwa na yule niliyekuona nae kwenye gari jana, na wala sio mume wangu kama nilivyosema hapo hawali" Sarah aliongea kisha akameza mate na kumfanya Dokta Pendo amtolee macho,

"samahani kwa yote niliyokufanyia jana, ila lengo langu halikuwa baya kwako, nilichotaka ni kukuteka na mimi nichukue nafasi yako ili yule bwana anaekufuataga akija anichukue mimi badala ya wewe" Sarah alizungumza na kisha Dokta Pendo akaamua akae kabisa,

"unasema yule aliyetekwa ni babu yako?" Dokta Pendo aliuliza,

"ndio, yule ni babu yangu, na wale wana lengo baya na mimi na wala sio yule babu, na hapa wanachofikiria ni kukudhuru na wewe, wanadhani kuwa umenisaidia kunionesha kambi yao ilipo" Sarah aliongea,

"na kwanini wakufanyie wewe, umewakosea nini?" Dokta Pendo aliuliza,

"nitakuadithia hapo mbele nikishaimaliza kazi yangu, Maana sio hadithi nzuri" Sarah Aliongea huku akiwa ameinamisha kichwa,

"pole sana, je unaweza ukaniruhusu niondoke?" Dokta Pendo aliuliza,

"kuondoka unaweza, ila uko unapotaka kwenda, usalama haupo, watakuwa tayari wameshakuweka kundi moja na mimi" Sarah aliongea,

"Mimi hawatanifanya kitu, nitawaambia uliniteka" Dokta Pendo aliongea,

"umesema makubaliano yako wewe na Trigger ilikuwa ni kutomwambia mtu kuwa mule ndani uwa unaenda kumtibu mtu, je huoni umeshakiuka makubaliano?" Sarah alimuuliza Dokta Pendo,

"Mimi naenda hivyo hivyo, hawawezi kunifanya kitu" Dokta Pendo aliongea kwa kujiamini,

"sawa, usijali shoga yangu, mimi naomba tushinde wote, tule tushibe, alafu nitakurudisha usiku" Sarah alimwambia Dokta Pendo,

"nataka niende muda huu" Dokta Pendo aliongea,

"sasa hivi haiwezekani, naomba uniamini tu, wale watu muda huu watakuwa maeneo yale yale wanakuwinda" Sarah alimuelewesha Dokta Pendo,

"sawa, acha nikuamini" Dokta Pendo aliongea na kuonesha amekubaliana na Sarah.

**************************

Mishale ya saa tatu usiku, Sarah alikuwa nyumbani kwake na dokta Pendo,

"twende mi nimeshajiandaa" Sarah alimwambia Dokta Pendo,

"Mimi mwenyewe nipo tayari, nirudishe kwangu shoga" Dokta Pendo alimjibu Sarah,

"samahani, naomba nikufunge kitambaa cheusi machoni, maana sihitaji mtu apajue ninapoishi" Sarah alimwambia Dokta Pendo,

"kwanini hutaki mtu apajue hapa?" Dokta Pendo alihoji,

"ni sababu tu za kiusalama" Sarah alijibu,

"si uniambie hizo sababu shoga yangu" Dokta Pendo alimsihii Sarah,

"nitakuambia siku nyingine shoga yangu" Sarah alimjibu hivyo huku akitabasamu,

.

"haya Bwana, nifunge" Dokta Pendo aliongea kwa upole na Sarah akachukua Kitambaa na kumfunga, kisha akamshika mkono na kutoka nae mpaka nje, Akamuingiza ndani ya gari na safari ikaanza.

Ndani ya gari walikuwa na maongezi ya hapa na pale, iliwachukua nusu saa kufika nyumbani kwa Dokta Pendo, walipofika Sarah aliegesha gari yake upande wa pili wa barabara.

Ila waliweza kukuta vijana kadhaa wenye silaha wakiwa wameizunguka nyumba ya Dokta Pendo, hapo Sarah alimtoa kile kitambaa cheusi machoni na dokta Pendo akaweza kuwashuhudia wale vijana,

"wale ni polisi?" Dokta Pendo aliuliza, na wakati huo ndani Alikuwa akitoka Taita na Trigger,

"sio polisi wale, ni watu wako hao wanakutafuta" Sarah alijibu,

"ebu ngoja nishuke nikaongee nao" Dokta Pendo aliongea huku akitaka kufungua mlango,

"subiri kwanza, usiwe na pupa" Sarah alimwambia Dokta Pendo na wakati huo Trigger na Taita waliweza kuiona ile gari ambayo alikuwepo Sarah na dokta Pendo, ila hawakuweza kujua mtu aliyekuwepo ndani ya ile gari, ila waliitilia mashaka, Taita akiwa na Trigger waliamua kuisogelea ile gari huku bunduki zikiwa mkononi, walihisi kabisa mule ndani ya gari hakukuwa na watu wazuri.

Sarah aliweza kuona namna Taita na Trigger wanavyokuja, akawasha gari, lakini gari haikuwaka, akajaribu tena na bado gari haikuwaka, na kipindi hicho Taita na Trigger walibakiza hatua mbili tu waifikie gari ya Sarah, hapo Sarah akapata kihoro, tumbo joto.

Akajaribu tena kuwasha ila gari ikagoma,

"Shuka kwenye gari malaya wewe" Taita aliongea huku mtutu ukiwa usawa wa kichwa cha Sarah, kwa maana hiyo walikuwa tayari wameshamfikia Sarah, Sarah akatabasamu, halikuwa tabasamu la furaha, ila ni tabasamu la kukata tamaa na muda huo Taita alitoa tabasamu la ushindi, Sarah akanyoosha Mikono juu ikiwa ni ishara ya kutii amri..................

*********ITAENDELEA**********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA.

ILIPOISHIA...................

Ndani ya gari walikuwa na maongezi ya hapa na pale, iliwachukua nusu saa kufika nyumbani kwa Dokta Pendo, walipofika Sarah aliegesha gari yake upande wa pili wa barabara.

Ila waliweza kukuta vijana kadhaa wenye silaha wakiwa wameizunguka nyumba ya Dokta Pendo, hapo Sarah alimtoa kile kitambaa cheusi machoni na dokta Pendo akaweza kuwashuhudia wale vijana,

"wale ni polisi?" Dokta Pendo aliuliza, na wakati huo ndani Alikuwa akitoka Taita na Trigger,

"sio polisi wale, ni watu wako hao wanakutafuta" Sarah alijibu,

"ebu ngoja nishuke nikaongee nao" Dokta Pendo aliongea huku akitaka kufungua mlango,

"subiri kwanza, usiwe na pupa" Sarah alimwambia Dokta Pendo na wakati huo Trigger na Taita waliweza kuiona ile gari ambayo alikuwepo Sarah na dokta Pendo, ila hawakuweza kujua mtu aliyekuwepo ndani ya ile gari, ila waliitilia mashaka, Taita akiwa na Trigger waliamua kuisogelea ile gari huku bunduki zikiwa mkononi, walihisi kabisa mule ndani ya gari hakukuwa na watu wazuri.

Sarah aliweza kuona namna Taita na Trigger wanavyokuja, akawasha gari, lakini gari haikuwaka, akajaribu tena na bado gari haikuwaka, na kipindi hicho Taita na Trigger walibakiza hatua mbili tu waifikie gari ya Sarah, hapo Sarah akapata kihoro, tumbo joto.

Akajaribu tena kuwasha ila gari ikagoma,

"Shuka kwenye gari malaya wewe" Taita aliongea huku mtutu ukiwa usawa wa kichwa cha Sarah, kwa maana hiyo walikuwa tayari wameshamfikia Sarah, Sarah akatabasamu, halikuwa tabasamu la furaha, ila ni tabasamu la kukata tamaa na muda huo Taita alitoa tabasamu la ushindi, Sarah akanyoosha Mikono juu ikiwa ni ishara ya kutii amri..................

***********ENDELEA**********

Sarah akili ikachemka, na vile hujiamini kwa kasi aliyokuwa nayo, alichofanya ni kuushika mkono wa Taita wenye bastola na kuuvuta kwa nguvu mkono wa Taita wenye bastola na kuuvuta kwa nguvu kisha akaachia ngumi nyepesi iliyompiga Taita kooni, Taita akajikuta akiiangusha ile bastola yake mapajani mwa Sarah, kisha Sarah akaikota ile bastola na kumuwekea Taita usawa wa kichwa huku akiwa amemkaba Taita,

"waambie mbwa wako waweke silaha chini na wasogee nyuma" Sarah aliongea huku mdomo wake ukiwa jirani na sikio la Taita, Taita akaona bora atii amri, akajitahidi na kupaza sauti akiwaamuru vijana wake waweke silaha chini na kurudi nyuma, vijana wakatii amri ya mkuu wao, kisha Sarah akatoka ndani ya gari na kumuamuru Taita aingie katika siti za nyuma za gari, Taita akatii kisha nae akaingia na yeye siti za nyuma,

"Dokta Pendo endesha gari" Sarah alimwambia Dokta Pendo ambaye muda wote alikuwa akitetemeka,

"gari si imekataa kuwaka?" Dokta Pendo aliuliza huku akitetemeka,

"we washa bwana, jaribu huenda itakubali" Sarah aliongea na kufanya Dokta Pendo asogee upande wa dereva na kujaribu kuwasha gari, ikawaka,

"tunaelekea wapi?" Dokta Pendo aliuliza,

"nenda eneo lolote lile ambalo unajua kuna pori" Sarah aliongea na kisha Dokta Pendo akaondoa gari, kuna vijana kama wawili walitaka kuokota silaha ili waishambulie gari, Sarah akawawahi na kuwafyatulia risasi, wakafa palepale. Kipindi hicho chote Taita alikuwa tumbo joto, hakuamini kama ametekwa kizembe hivyo, ila hakuwa na cha kufanya.

********************

Sajenti Minja alikuwa bize na lap top yake, bado alikuwa akifuatilia kuhusu ile nyumba iliyoungua, bahati nzuri aligundua kuwa mwenye ile nyumba pia alimuoa mwanamke aliyeitwa margret ambaye alikuwa ni mfanyakazi wa serikali, baada ya kumfuatilia margret kupitia mtandao akagundua kuwa ana undugu wa karibu na Taita, pia akagundua kuwa hata ile hotel iliyojengwa kwenye ile nyumba iliyoungua zamani, ni hotel ya Taita,

Sajenti Minja akakuna kidevu, akaamua amtafute Sarah yule rafiki yake wa kwenye memory card, alimtafuta kwa njia ya mtandao, aliutumia whatsap kwa kuwa alikuwa na namba yake ya simu,

"upo wapi mrembo?" Sajenti Minja aliuliza baada ya salamu,

"nipo marekani, vipi kwani?" Sarah alihoji,

"hakuna kitu, nimekukumbuka tu" Sajenti Minja aliongea,

"bado wewe ni polisi?" Sarah alimuuliza Sajenti Minja,

"bado ndugu yangu, hizi kazi zetu ngumu kuziacha"Sajenti Minja alijibu huku akitabasamu,

"komaa bwana, endeleza mapambano" Sarah aliongea,

"poa bwana, wacha nikuage" Sajenti Minja aliongea,

"poa afande, nashukuru kwa kunikumbuka" Sarah aliongea huku akitabasamu,

"usijali, nitaendelea kukumbuka" Sajenti Minja aliongea,

"poa" Sarah alijibu kisha akakata mawasiliano.

Sajenti Minja akabaki anawaza, swali alilojiuliza kuwa yule binti aliyepambana nae kule pagaleni ni nani?

Mwisho Sajenti Minja akaamua aende Vin hotel, aliamua akamtafute Taita ili aweze kumuuliza maswali machache kuhusu margret na familia yake, aliamini kufanya hivyo kunaweza kumpa mwanga kidogo juu ya kile anachokitafuta.

Akatoka nje ya jengo la polisi na kuelekea moja kwa moja kwenye gari lake, akaingia na kuliondoa.

*******************

Kwenye kambi ya Taita kulikuwa na majonzi makubwa, walikuwa hawajui kiongozi wao yupo kwenye hali gani?

Muda huo aliyekuwa akiumiza kichwa sana ni Trigger, kwa maana tukio zima lilitokea mbele yake, na muda huo bado alikuwa eneo lile lile la nyumbani kwa Dokta Pendo, alikuwa na vijana wake, akawaamuru vijana wakapumzike majumbani mwao, kisha yeye akaingia kwenye gari lake alilokuja nalo na kuamua kwenda moja kwa moja nyumbani kwa Taita.

Wakati akiwa ndani ya gari alijitahidi sana kuwapa taharifa watu muhimu katika kundi lao, hakutaka kuwaambia ukweli, alichowaambia ni kuwa wote wakutane muda huo nyumbani kwa Taita, kuna tukio lisilo la kawaida limetokea.

Baada ya muda Trigger aliwasili nyumbani kwa Taita, akaingiza gari ndani, akaelekea moja kwa moja sebuleni, akawakuta Tekso na Strategic wakiwa wanamsubiri,

"Harry yupo wapi?" Trigger aliuliza,

"bado hajatimba, ila nadhani tunaweza kuendelea na kikao" Tekso alijibu,

"na bosi naye yuko wapi?" Strategic aliuliza lakini Trigger hakuonekana kuwa tayari kujibu hilo swali, na muda huo Harry alikuwa anaingia huku akionekana hajafurahishwa na kikao hicho cha usiku. Harry akawasalimia wenzake na kisha akakaa kwenye kochi,

"nadhani tunaweza kuanza kikao" Trigger aliongea huku akiangalia chini,

"Taita yuko wapi, maana yeye ndio anatakiwa aongoze kikao na sio wewe" Harry aliongea huku akionekana kumshangaa Trigger,

"lengo la kikao ni hilo, kuwajulisha ni wapi alipo Taita" Trigger aliongea na kufanya wenzake watege vizuri masikio yao,

"ukiwa unaeleza kitu unatakiwa uende direct kwenye jambo husika, sio kukatisha katisha maneno" Harry aliongea kwa ukali baada ya kutofurahishwa na mtindo anaoutumia Trigger katika kuongea,

"ok, ni hivi, Taita ametekwa na Sarah muda mchache uliopita" Trigger aliongea na kufanya miili ya wenzake ipigwe na ganzi,

"bado sijakuelewa, unasema?" Harry aliuliza tena kanakwamba hajasikia kilichozungumzwa na mwenzie huyo,

"ilikuwaje kuwaje yaani?" Tekso nae akapandishia swali jingine.

Mpaka kufikia hapo wote walikuwa wamechanganyikiwa, maana walikuwa wanamjua vyema Sarah katika suala zima la kufanya unyama, na hakuna hata mmoja aliyekuwa na imani ya bosi wao huyo kurudi akiwa hai.

"tueleze basi kilichotokea" Harry aliongea baada ya kumuona Trigger akiwa kimya,

Trigger akaeleza kila kitu, hakuficha chochote.

"tunafanyaje sasa?" Tekso aliuliza ila hakuna aliyemjibu, hali ilikuwa mbaya sana kwenye hii kambi,

"sasa mbona hamjibu?" Tekso aliuliza tena, ila safari hii alitumia sauti kubwa kidogo Baada ya kuona wenzie hawakutilia mkazo swali Lake la hawali,

"taratibu basi, hilo swali ulilouliza halihitaji jibu la kukurupuka, linahitaji nafasi ya kufikiria" Strategic alijibu huku akiwa amefunga macho,

"kweli tunahitaji muda kiasi wa kupata cha kufanya kuhusu hili suala" Harry alionekana kumuunga mkono Strategic,

"ndio tufikirie hapa hapa na tupate jibu" Trigger aliongea,

"na hiyo pia haiwezekani, inaweza kutuchukua siku mbili au tatu kuweza kupata fikra sahihi" Strategic aliongea,

"siku mbili au tatu? Wewe una wazimu nini? Siku hizo zote utakuwa unafikiria nini?" Trigger aliongea kwa jazba huku akionekana amekereka kutokana na majibu ya Strategic,

"Trigger kwani wewe unapajua alipopelekwa Taita?" Harry aliuliza huku akimuangalia Trigger,

"sipajui, ningekuwa napajua si ningeshaenda?" Trigger alijibu,

"unajua ni wapi Sarah anapokaa?" Harry akamtupia swali jingine Trigger,

"hapana" Trigger akajibu,

"sasa kwanini Strategic anaposema hili suala itabidi lichukue siku mbili au tatu kuweza kupata fikra sahihi, Wewe unakuwa unapinga wakati unajua kabisa adui tunaepambana nae hatujui pa kumpata?" Harry aliongea huku akimtazama Trigger,

"Tekso si yupo, anaweza kucheza na technolojia tugundue chochote" Trigger aliongea,

"kwani uko alipo Taita ameenda na simu?" Tekso aliuliza,

"simu ameiacha ndani ya gari" Trigger alijibu,

"dah, basi ni ngumu sana kujua alipo" Tekso alijibu na kufanya Trigger achoke kabisa,

"mi nadhani tutawanyike tu, kesho asubuhi tukutane ili tujue cha kufanya, na kila mtu akalale huku akitafuta njia ya kuweza kumpigania Taita" Harry aliongea huku akiwatizama wenzake,

"nyie nendeni, mimi nitabaki hapa nikilinda nyumba, maana hakuna mtu zaidi ya mlinzi" Trigger aliongea,

"sawa, mimi naenda, ila kesho tukutane hapa asubuhi kama nilivyosema" Harry aliongea huku akiinuka kwenye kochi,

"sawa mkuu, naimani kesho tutakuwa na mbinu zozote" Tekso alijibu huku nae akiinuka katika kochi,



"na wewe uende, mimi nataka nifunge mlango" Trigger alimwambia Strategic aliyekuwa bado amekaa,

"taratibu mkuu, kila kitu kinahitaji mpangilio, nasubiri wenzangu wapite mlangoni na mimi ndio nifuate" Strategic alijibu katika sauti tulivu,

"nyanyuka bwana, unajifanya mtu wa mipango wakati umeshindwa kupanga namna ya kumkomboa Taita" Trigger aliongea huku akimvuta Strategic ainuke, strategic akainuka na kuondoka zake huku wakimuacha Trigger akiwa amesimama mlangoni akiwatazama.

*********************

Usiku huu Sajenti Minja aliingia Vin hotel na kuelekea moja kwa moja mapokezi,

"nahitaji Kuongea na meneja wa hapa" Sajenti Minja aliongea huku akionesha kitambulisho chake, dada wa mapokezi akamuelekeza ofisi ya meneja ilipo, akaenda na kumkuta msichana akiwa ndio meneja wa pale, akamsalimu,

"kama nilivyosema hawali, mimi ni askari na hapa nimekuja nikiwa nataka kuonana na mmiliki wa hii hotel" Sajenti Minja aliongea kwa utulivu,

"Mimi hapo sina cha kukusaidia, labda tu nikupe namba yake" meneja aliongea kinyenyekevu,

"pia huo ni msaada" Sajenti Minja aliongea huku akiitoa simu yake na kisha yule dada Meneja akamtajia namba ya Taita, Sajenti Minja akainakiri katika simu yake.

"usimpigie usiku, mtagombana" Meneja alimtahadharisha Sajenti Minja,

"usijali, nitampigia kesho asubuhi" Sajenti Minja alijibu huku akitabasamu na kutoka zake nje, akaelekea kwenye gari yake na kuingia ndani, alipoiwasha ili aondoke, ndipo alishuhudia gari aina ya range Rover likikatiza mbele yake huku likiwa katika mwendo mkali, akalikumbuka hilo gari kuwa ni la muharifu anayemtafuta.

Sajenti Minja nae akaitoa gari yake kwa kasi kuifuata ile Range Rover, alijitahidi kuifanyia ishara zote ili ile Range Rover isimame, badala yake iliongeza mwendo, alafu eneo ilipokuwa inaelekea ni eneo la porini.

Sajenti Minja akaamua atumie akili ili kuweza kuikamata ile gari, akaendelea kuikimbiza kwa nusu saa, akafanikiwa kuipita kisha akaisimamisha kwa ghafla gari yake katikati ya barabara, ile Range Rover nayo ikaminya breki, Sajenti Minja akawasha tochi yake na kummulika dereva wa ile gari, alikuwa ni Dokta Pendo, tena alikuwa na hofu tele.

Sajenti Minja akachomoa bastola yake na kushuka ndani ya gari,

"telemka chini, Mikono ikiwa juu" Sajenti Minja aliongea huku bastola yake akimuelekezea Dokta Pendo, hapo Dokta Pendo akazidi kuchanganyikiwa, akashuka kwenye gari.

"mpo wangapi kwenye gari na mmebeba nini?" Sajenti Minja aliuliza lakini Dokta Pendo hakujibu, ni machozi tu yalimtoka,

"wewe mwanamke si nakuuliza?" Sajenti Minja aliongea kwa ukali, lakini Dokta Pendo hakujibu, aliendelea kulia kimya kimya, sasa Sajenti Minja akahisi ndani ya gari kuna kitu na ndio maana yule dada analia, Sajenti Minja akalisogelea gari na kufungua mlango wa nyuma kwa nguvu.......

*********ITAENDELEA*********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA.

ILIPOISHIA...................

Ndani ya gari walikuwa na maongezi ya hapa na pale, iliwachukua nusu saa kufika nyumbani kwa Dokta Pendo, walipofika Sarah aliegesha gari yake upande wa pili wa barabara.

Ila waliweza kukuta vijana kadhaa wenye silaha wakiwa wameizunguka nyumba ya Dokta Pendo, hapo Sarah alimtoa kile kitambaa cheusi machoni na dokta Pendo akaweza kuwashuhudia wale vijana,

"wale ni polisi?" Dokta Pendo aliuliza, na wakati huo ndani Alikuwa akitoka Taita na Trigger,

"sio polisi wale, ni watu wako hao wanakutafuta" Sarah alijibu,

"ebu ngoja nishuke nikaongee nao" Dokta Pendo aliongea huku akitaka kufungua mlango,

"subiri kwanza, usiwe na pupa" Sarah alimwambia Dokta Pendo na wakati huo Trigger na Taita waliweza kuiona ile gari ambayo alikuwepo Sarah na dokta Pendo, ila hawakuweza kujua mtu aliyekuwepo ndani ya ile gari, ila waliitilia mashaka, Taita akiwa na Trigger waliamua kuisogelea ile gari huku bunduki zikiwa mkononi, walihisi kabisa mule ndani ya gari hakukuwa na watu wazuri.

Sarah aliweza kuona namna Taita na Trigger wanavyokuja, akawasha gari, lakini gari haikuwaka, akajaribu tena na bado gari haikuwaka, na kipindi hicho Taita na Trigger walibakiza hatua mbili tu waifikie gari ya Sarah, hapo Sarah akapata kihoro, tumbo joto.

Akajaribu tena kuwasha ila gari ikagoma,

"Shuka kwenye gari malaya wewe" Taita aliongea huku mtutu ukiwa usawa wa kichwa cha Sarah, kwa maana hiyo walikuwa tayari wameshamfikia Sarah, Sarah akatabasamu, halikuwa tabasamu la furaha, ila ni tabasamu la kukata tamaa na muda huo Taita alitoa tabasamu la ushindi, Sarah akanyoosha Mikono juu ikiwa ni ishara ya kutii amri..................

***********ENDELEA**********

Sarah akili ikachemka, na vile hujiamini kwa kasi aliyokuwa nayo, alichofanya ni kuushika mkono wa Taita wenye bastola na kuuvuta kwa nguvu mkono wa Taita wenye bastola na kuuvuta kwa nguvu kisha akaachia ngumi nyepesi iliyompiga Taita kooni, Taita akajikuta akiiangusha ile bastola yake mapajani mwa Sarah, kisha Sarah akaikota ile bastola na kumuwekea Taita usawa wa kichwa huku akiwa amemkaba Taita,

"waambie mbwa wako waweke silaha chini na wasogee nyuma" Sarah aliongea huku mdomo wake ukiwa jirani na sikio la Taita, Taita akaona bora atii amri, akajitahidi na kupaza sauti akiwaamuru vijana wake waweke silaha chini na kurudi nyuma, vijana wakatii amri ya mkuu wao, kisha Sarah akatoka ndani ya gari na kumuamuru Taita aingie katika siti za nyuma za gari, Taita akatii kisha nae akaingia na yeye siti za nyuma,

"Dokta Pendo endesha gari" Sarah alimwambia Dokta Pendo ambaye muda wote alikuwa akitetemeka,

"gari si imekataa kuwaka?" Dokta Pendo aliuliza huku akitetemeka,

"we washa bwana, jaribu huenda itakubali" Sarah aliongea na kufanya Dokta Pendo asogee upande wa dereva na kujaribu kuwasha gari, ikawaka,

"tunaelekea wapi?" Dokta Pendo aliuliza,

"nenda eneo lolote lile ambalo unajua kuna pori" Sarah aliongea na kisha Dokta Pendo akaondoa gari, kuna vijana kama wawili walitaka kuokota silaha ili waishambulie gari, Sarah akawawahi na kuwafyatulia risasi, wakafa palepale. Kipindi hicho chote Taita alikuwa tumbo joto, hakuamini kama ametekwa kizembe hivyo, ila hakuwa na cha kufanya.

********************

Sajenti Minja alikuwa bize na lap top yake, bado alikuwa akifuatilia kuhusu ile nyumba iliyoungua, bahati nzuri aligundua kuwa mwenye ile nyumba pia alimuoa mwanamke aliyeitwa margret ambaye alikuwa ni mfanyakazi wa serikali, baada ya kumfuatilia margret kupitia mtandao akagundua kuwa ana undugu wa karibu na Taita, pia akagundua kuwa hata ile hotel iliyojengwa kwenye ile nyumba iliyoungua zamani, ni hotel ya Taita,

Sajenti Minja akakuna kidevu, akaamua amtafute Sarah yule rafiki yake wa kwenye memory card, alimtafuta kwa njia ya mtandao, aliutumia whatsap kwa kuwa alikuwa na namba yake ya simu,

"upo wapi mrembo?" Sajenti Minja aliuliza baada ya salamu,

"nipo marekani, vipi kwani?" Sarah alihoji,

"hakuna kitu, nimekukumbuka tu" Sajenti Minja aliongea,

"bado wewe ni polisi?" Sarah alimuuliza Sajenti Minja,

"bado ndugu yangu, hizi kazi zetu ngumu kuziacha"Sajenti Minja alijibu huku akitabasamu,

"komaa bwana, endeleza mapambano" Sarah aliongea,

"poa bwana, wacha nikuage" Sajenti Minja aliongea,

"poa afande, nashukuru kwa kunikumbuka" Sarah aliongea huku akitabasamu,

"usijali, nitaendelea kukumbuka" Sajenti Minja aliongea,

"poa" Sarah alijibu kisha akakata mawasiliano.

Sajenti Minja akabaki anawaza, swali alilojiuliza kuwa yule binti aliyepambana nae kule pagaleni ni nani?

Mwisho Sajenti Minja akaamua aende Vin hotel, aliamua akamtafute Taita ili aweze kumuuliza maswali machache kuhusu margret na familia yake, aliamini kufanya hivyo kunaweza kumpa mwanga kidogo juu ya kile anachokitafuta.

Akatoka nje ya jengo la polisi na kuelekea moja kwa moja kwenye gari lake, akaingia na kuliondoa.

*******************

Kwenye kambi ya Taita kulikuwa na majonzi makubwa, walikuwa hawajui kiongozi wao yupo kwenye hali gani?

Muda huo aliyekuwa akiumiza kichwa sana ni Trigger, kwa maana tukio zima lilitokea mbele yake, na muda huo bado alikuwa eneo lile lile la nyumbani kwa Dokta Pendo, alikuwa na vijana wake, akawaamuru vijana wakapumzike majumbani mwao, kisha yeye akaingia kwenye gari lake alilokuja nalo na kuamua kwenda moja kwa moja nyumbani kwa Taita.

Wakati akiwa ndani ya gari alijitahidi sana kuwapa taharifa watu muhimu katika kundi lao, hakutaka kuwaambia ukweli, alichowaambia ni kuwa wote wakutane muda huo nyumbani kwa Taita, kuna tukio lisilo la kawaida limetokea.

Baada ya muda Trigger aliwasili nyumbani kwa Taita, akaingiza gari ndani, akaelekea moja kwa moja sebuleni, akawakuta Tekso na Strategic wakiwa wanamsubiri,

"Harry yupo wapi?" Trigger aliuliza,

"bado hajatimba, ila nadhani tunaweza kuendelea na kikao" Tekso alijibu,

"na bosi naye yuko wapi?" Strategic aliuliza lakini Trigger hakuonekana kuwa tayari kujibu hilo swali, na muda huo Harry alikuwa anaingia huku akionekana hajafurahishwa na kikao hicho cha usiku. Harry akawasalimia wenzake na kisha akakaa kwenye kochi,

"nadhani tunaweza kuanza kikao" Trigger aliongea huku akiangalia chini,

"Taita yuko wapi, maana yeye ndio anatakiwa aongoze kikao na sio wewe" Harry aliongea huku akionekana kumshangaa Trigger,

"lengo la kikao ni hilo, kuwajulisha ni wapi alipo Taita" Trigger aliongea na kufanya wenzake watege vizuri masikio yao,

"ukiwa unaeleza kitu unatakiwa uende direct kwenye jambo husika, sio kukatisha katisha maneno" Harry aliongea kwa ukali baada ya kutofurahishwa na mtindo anaoutumia Trigger katika kuongea,

"ok, ni hivi, Taita ametekwa na Sarah muda mchache uliopita" Trigger aliongea na kufanya miili ya wenzake ipigwe na ganzi,

"bado sijakuelewa, unasema?" Harry aliuliza tena kanakwamba hajasikia kilichozungumzwa na mwenzie huyo,

"ilikuwaje kuwaje yaani?" Tekso nae akapandishia swali jingine.

Mpaka kufikia hapo wote walikuwa wamechanganyikiwa, maana walikuwa wanamjua vyema Sarah katika suala zima la kufanya unyama, na hakuna hata mmoja aliyekuwa na imani ya bosi wao huyo kurudi akiwa hai.

"tueleze basi kilichotokea" Harry aliongea baada ya kumuona Trigger akiwa kimya,

Trigger akaeleza kila kitu, hakuficha chochote.

"tunafanyaje sasa?" Tekso aliuliza ila hakuna aliyemjibu, hali ilikuwa mbaya sana kwenye hii kambi,

"sasa mbona hamjibu?" Tekso aliuliza tena, ila safari hii alitumia sauti kubwa kidogo Baada ya kuona wenzie hawakutilia mkazo swali Lake la hawali,

"taratibu basi, hilo swali ulilouliza halihitaji jibu la kukurupuka, linahitaji nafasi ya kufikiria" Strategic alijibu huku akiwa amefunga macho,

"kweli tunahitaji muda kiasi wa kupata cha kufanya kuhusu hili suala" Harry alionekana kumuunga mkono Strategic,

"ndio tufikirie hapa hapa na tupate jibu" Trigger aliongea,

"na hiyo pia haiwezekani, inaweza kutuchukua siku mbili au tatu kuweza kupata fikra sahihi" Strategic aliongea,

"siku mbili au tatu? Wewe una wazimu nini? Siku hizo zote utakuwa unafikiria nini?" Trigger aliongea kwa jazba huku akionekana amekereka kutokana na majibu ya Strategic,

"Trigger kwani wewe unapajua alipopelekwa Taita?" Harry aliuliza huku akimuangalia Trigger,

"sipajui, ningekuwa napajua si ningeshaenda?" Trigger alijibu,

"unajua ni wapi Sarah anapokaa?" Harry akamtupia swali jingine Trigger,

"hapana" Trigger akajibu,

"sasa kwanini Strategic anaposema hili suala itabidi lichukue siku mbili au tatu kuweza kupata fikra sahihi, Wewe unakuwa unapinga wakati unajua kabisa adui tunaepambana nae hatujui pa kumpata?" Harry aliongea huku akimtazama Trigger,

"Tekso si yupo, anaweza kucheza na technolojia tugundue chochote" Trigger aliongea,

"kwani uko alipo Taita ameenda na simu?" Tekso aliuliza,

"simu ameiacha ndani ya gari" Trigger alijibu,

"dah, basi ni ngumu sana kujua alipo" Tekso alijibu na kufanya Trigger achoke kabisa,

"mi nadhani tutawanyike tu, kesho asubuhi tukutane ili tujue cha kufanya, na kila mtu akalale huku akitafuta njia ya kuweza kumpigania Taita" Harry aliongea huku akiwatizama wenzake,

"nyie nendeni, mimi nitabaki hapa nikilinda nyumba, maana hakuna mtu zaidi ya mlinzi" Trigger aliongea,

"sawa, mimi naenda, ila kesho tukutane hapa asubuhi kama nilivyosema" Harry aliongea huku akiinuka kwenye kochi,

"sawa mkuu, naimani kesho tutakuwa na mbinu zozote" Tekso alijibu huku nae akiinuka katika kochi,



"na wewe uende, mimi nataka nifunge mlango" Trigger alimwambia Strategic aliyekuwa bado amekaa,

"taratibu mkuu, kila kitu kinahitaji mpangilio, nasubiri wenzangu wapite mlangoni na mimi ndio nifuate" Strategic alijibu katika sauti tulivu,

"nyanyuka bwana, unajifanya mtu wa mipango wakati umeshindwa kupanga namna ya kumkomboa Taita" Trigger aliongea huku akimvuta Strategic ainuke, strategic akainuka na kuondoka zake huku wakimuacha Trigger akiwa amesimama mlangoni akiwatazama.

*********************

Usiku huu Sajenti Minja aliingia Vin hotel na kuelekea moja kwa moja mapokezi,

"nahitaji Kuongea na meneja wa hapa" Sajenti Minja aliongea huku akionesha kitambulisho chake, dada wa mapokezi akamuelekeza ofisi ya meneja ilipo, akaenda na kumkuta msichana akiwa ndio meneja wa pale, akamsalimu,

"kama nilivyosema hawali, mimi ni askari na hapa nimekuja nikiwa nataka kuonana na mmiliki wa hii hotel" Sajenti Minja aliongea kwa utulivu,

"Mimi hapo sina cha kukusaidia, labda tu nikupe namba yake" meneja aliongea kinyenyekevu,

"pia huo ni msaada" Sajenti Minja aliongea huku akiitoa simu yake na kisha yule dada Meneja akamtajia namba ya Taita, Sajenti Minja akainakiri katika simu yake.

"usimpigie usiku, mtagombana" Meneja alimtahadharisha Sajenti Minja,

"usijali, nitampigia kesho asubuhi" Sajenti Minja alijibu huku akitabasamu na kutoka zake nje, akaelekea kwenye gari yake na kuingia ndani, alipoiwasha ili aondoke, ndipo alishuhudia gari aina ya range Rover likikatiza mbele yake huku likiwa katika mwendo mkali, akalikumbuka hilo gari kuwa ni la muharifu anayemtafuta.

Sajenti Minja nae akaitoa gari yake kwa kasi kuifuata ile Range Rover, alijitahidi kuifanyia ishara zote ili ile Range Rover isimame, badala yake iliongeza mwendo, alafu eneo ilipokuwa inaelekea ni eneo la porini.

Sajenti Minja akaamua atumie akili ili kuweza kuikamata ile gari, akaendelea kuikimbiza kwa nusu saa, akafanikiwa kuipita kisha akaisimamisha kwa ghafla gari yake katikati ya barabara, ile Range Rover nayo ikaminya breki, Sajenti Minja akawasha tochi yake na kummulika dereva wa ile gari, alikuwa ni Dokta Pendo, tena alikuwa na hofu tele.

Sajenti Minja akachomoa bastola yake na kushuka ndani ya gari,

"telemka chini, Mikono ikiwa juu" Sajenti Minja aliongea huku bastola yake akimuelekezea Dokta Pendo, hapo Dokta Pendo akazidi kuchanganyikiwa, akashuka kwenye gari.

"mpo wangapi kwenye gari na mmebeba nini?" Sajenti Minja aliuliza lakini Dokta Pendo hakujibu, ni machozi tu yalimtoka,

"wewe mwanamke si nakuuliza?" Sajenti Minja aliongea kwa ukali, lakini Dokta Pendo hakujibu, aliendelea kulia kimya kimya, sasa Sajenti Minja akahisi ndani ya gari kuna kitu na ndio maana yule dada analia, Sajenti Minja akalisogelea gari na kufungua mlango wa nyuma kwa nguvu.......

*********ITAENDELEA*********

the Legend☆
Babe njoo tuendelee bwana

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom