Riwaya: Sala ya Sarah

Riwaya: Sala ya Sarah

Haya Mambo ya kuwekeana vipande vipande yamenichosha, Sasa ivi nishajua na mute Kama wiki 2 ndio nakuja Soma ikiwa imekamilika mnanipandisha vibes af nianze subir kesho Tena mambo ya watchout part two, bongo movie...........

Kazi nzuri ila huu usambazaji umenichosha nimeacha riwaya nyingi sana kwa huu utaratibu



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya Mambo ya kuwekeana vipande vipande yamenichosha, Sasa ivi nishajua na mute Kama wiki 2 ndio nakuja Soma ikiwa imekamilika mnanipandisha vibes af nianze subir kesho Tena mambo ya watchout part two, bongo movie...........

Kazi nzuri ila huu usambazaji umenichosha nimeacha riwaya nyingi sana kwa huu utaratibu



Sent using Jamii Forums mobile app
Sophoghani nliwahi kukwambia kua mimi sio mtunzi wa hizi riwaya, kuna sehemu nazitoa pia, na najitahidi kuziweka hapa jf ili ziwafkie wengi zaidi. Ukiona imekuchosha acha tuu kuifuatilia, sikumbuki kama nlishawahi kukulazimisha kuifuatilia. Kama unataka kusoma kwa mkupuo mwanzo mpaka mwisho nakushauri utafute vitabu. Tuliozea tutasonga nayo mpaka mwisho

the Legend☆
 
Sophoghani nliwahi kukwambia kua mimi sio mtunzi wa hizi riwaya, kuna sehemu nazitoa pia, na najitahidi kuziweka hapa jf ili ziwafkie wengi zaidi. Ukiona imekuchosha acha tuu kuifuatilia, sikumbuki kama nlishawahi kukulazimisha kuifuatilia. Kama unataka kusoma kwa mkupuo mwanzo mpaka mwisho nakushauri utafute vitabu. Tuliozea tutasonga nayo mpaka mwisho

the Legend☆
Tunapaje hivyo vitabu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA AROBAINI NA TISA

ENDELEA..................

Sarah akawa anarudi nyuma huku akiwa anajiuliza afanye kitu cha kushtukiza au akae kimya na kujifanya mjinga?

Sajenti Minja akaingia ndani na kufunga mlango, kipindi hicho chote Dokta Pendo alikuwa akiangalia tu,

"ebu Kaa hapa shoga yangu" Dokta Pendo aliongea huku akiwa anaoneshea eneo la jirani na alipo yeye, Sarah akasogea na kukaa pembeni ya Dokta Pendo, aliamua kutulia tu,

"mwenzako yupo wapi?" Sajenti Minja aliuliza huku akiwa bado amesimama,

"yule sio mwenzangu, hata mimi simjui" Sarah alijibu,

"aisee safari hii utaozea jela, yaani mnavamia kituo na kuua askari?" Sajenti Minja aliuliza,

"huyo mwenzako anayeuliziwa ni yupi?" Dokta Pendo aliuliza huku akimuangalia Sarah,

"eti Aisha" Sarah alijibu huku akiwa na hofu,

"sasa Sarah na Aisha wapi na wapi? Mbona unatuchanganyia habari wewe?" Dokta Pendo aliongea kwa mshangao huku akimuangalia Sajenti Minja,

"muulize mwenyewe aseme ni kweli alitoroshwa na huyo mwanamke au ametoroka mwenyewe?" Sajenti Minja aliuliza,

"ebu fungua mlango huo, kuna mtu anagonga mlango" Dokta Pendo alimwambia Sajenti Minja aliyekuwa amesimama mlangoni, kisha Sajenti Minja akageuka na kufungua mlango, alikutana na muhudumu aliyekuwa amebeba chakula,

"kilete hapa" Sarah aliongea huku akikaa vizuri, yule Muhudumu akaisogeza meza iliyokuwa pembeni na kumsogezea Sarah, kisha akaweka chakula juu ya meza, alafu akaondoka zake,

"kula shoga yangu, najua una njaa sana" Dokta Pendo aliongea huku akimpiga piga Sarah mgongoni,

"we Sarah si nimekuuliza? Kama yule mwanamke humjui ni kwa nini amekutorosha?" Sajenti Minja aliuliza huku akiuzuia mkono wa Sarah uliokuwa unapeleka chakula kinywani,

"khaa jamani!!!! kula ni ibada sasa kwa nini unasumbua mwenzio?" Dokta Pendo aliuliza kwa huruma,

"wewe unataka kujua nini?" Sarah aliuliza kwa hasira huku akikitupa kijiko cha chakula,

"yule mwanamke ni nani kwako?" Sajenti Minja aliuliza,

"yule mwanamke ndiye aliyemteka Dokta Pendo na kumvunja miguu, yule mwanamke ameshawahi kutaka kunichinja mara mbili, na yule mwanamke ndiye yule uliyeniokoa kule Vin hotel aliyetaka kunidhuru. Una jingine?" Sarah aliuliza kwa hasira,

"kwanini sasa amekuja kukuokoa?" Sajenti Minja aliuliza,

"hakuja kuniokoa kama unavyosema, alikuja kunichukua ili akanidhuru" Sarah alijibu na kumfanya Sajenti Minja acheke kwa dhihaka, yaani aliona anadanganywa,

"sasa mbona upo hapa ukiwa mzima na hujadhurika?" Sajenti Minja aliuliza baada ya kumaliza kucheka,

"hujasikia mlio wa bomu jirani na ofisi yenu?" Sarah aliuliza na kumfanya Sajenti Minja atege vizuri masikio yake,

"basi lile bomu lilitakiwa liniondoe mimi na yule mwanamke, yaani alitegewa yule mwanamke" Sarah aliongea,

"sasa kwanini akalipuka mtu mwingine?" Sajenti Minja aliuliza,

"yule ndiye aliyetega bomu, ila yule mwanamke aliyekuja pale polisi aligundua mapema ametegewa bomu, akatumia maarifa kumpachika lile lile bomu yule mtu aliyelipukiwa" Sarah aliongea na kumfanya Sajenti Minja apate mwanga,

"na kwanini watake kukuua wewe, una tatizo nao?" Sajenti Minja aliuliza,

"sina tatizo, labda wao wana tatizo na mimi" Sarah alijibu,

"maliza kula twende kituoni, utakuwa na mengi sana ya kunieleza" Sajenti Minja aliongea huku akikaa chini,

"wewe mtu vipi? Wewe unadhani kituoni kuzuri kule? wewe muhoji hapa hapa bwana" Dokta Pendo aliongea kwa ukali huku akimuangalia Sajenti Minja kwa jicho kali,

"wewe mbona unamtetea sana Sarah?" Sajenti Minja aliuliza kwa ukali,

"sioni kosa lake, mlimkamata kwa kudai ameniteka, mlivyonihoji nikakanusha hilo jambo, haya sasa hivi mnataka kumzushia kesi kubwa zaidi, eti ameshirikiana na mwenzie kumuua askari, hamna hata haya?" Dokta Pendo aliongea na kumfanya Sajenti Minja acheke,

"sasa wswe unatakaje?" Sajenti Minja aliuliza,

"Mimi huyu ni kama kijakazi wangu, ananiogesha na kunifanyia usafi wote unaohitajika, sasa ukimchukua huyu kwa kesi ya kumsingizia, utaniogesha wewe? Nikienda msalani utanisafisha?" Dokta Pendo aliuliza huku akiwa amemshikia kiuno Sajenti Minja,

"sawa yaishe, je mnaweza kunisaidia kumpata huyo Aisha?" Sajenti Minja aliuliza,

"tutampata wapi na sisi hatujui anapokaa" Dokta Pendo alijibu,

"Sarah nakuacha kwa sababu ya Dokta Pendo, sasa ninachokuomba usirudi kwako mpaka nikupe taharifa, maana ni lazima askari waende kukagua au kukuwinda maeneo ya kule kwako" Sajenti Minja aliongea huku akimuangalia Sarah,

"yaani nakosa uhuru kwa jambo ambalo sijalifanya?" Sarah aliuliza huku akisikitika,

"bwana wewe shukuru tu, bora uishi kwa kujificha kuliko kuishi mule selo" Dokta Pendo aliongea huku akijilaza,

"sasa mimi ninaondoka, nitarudi kesho kuwaambia kinachoendelea uko kituoni" Sajenti Minja aliongea huku akinyanyuka,

"sawa baba" Dokta Pendo alijibu,

"haya, mbaki Salama" Sajenti Minja aliongea huku akitoka nje,

"asante, na wewe pia" Dokta Pendo alijibu Wakati Sajenti Minja akifunga mlango.

"asante shoga, maana mmh" Sarah aliongea huku akiwa ahamini kama Sajenti Minja amemuacha,

"usijali shoga, tutaongea kesho, acha nilale maana nimechoka kweli" Dokta Pendo aliongea,

"sawa, mimi mwenyewe nikimaliza tu kula nalala" Sarah aliongea huku akiendelea kula.

**************************

.

Asubuhi hii bado Harry hakuweza kupata habari yoyote kuhusu Tekso, na kila alipojaribu kupiga namba yake ikawa hazipatikani. Harry akiwa ofisini kwake alishuhudia simu yake ikipokea ujumbe mfupi wa maneno, alipotazama jina la mtu aliyetuma huo ujumbe, kidogo ashtuke, aliona jina la Aisha, Harry akaichukua simu yake na kuufungua huo ujumbe,

"ulidhani nitakufa?" ujumbe uliandikwa hivyo na kumfanya sasa Harry achanganyikiwe, hakutegemea kabisa kusikia leo hii Aisha yupo hai. Harry akajaribu kupiga namba ya Aisha ili ampoze, ila siku iliita bila kupokelewa, akajaribu tena na tena ila hali ikawa ile ile, na mwisho kabisa simu ya Aisha ikawa haipatikani,

"huyu hajafa kweli au kuna mtu ananichezea?" Harry alijiuliza huku akirudia kuusoma ule ujumbe uliotumwa na Aisha, akajikuta anatabasamu mwenyewe.

Na muda huo huo akaingia Trigger, ujio haukuwa wa kawaida ule, aliingia akihema juu juu na kumfanya Harry amtolee macho,

"nina habari ya kushangaza sana" Trigger aliongea huku akikaa kwenye kiti,

"Mimi niliyonayo inashangaza zaidi" Harry aliongea kwa utulivu huku akimuangalia Trigger,

"wewe unayo ipi?" Trigger aliuliza,

"Aisha hajafa, yupo hai" Harry aliongea na kufanya Trigger amtumbulie macho,

"basi habari hiyo na habari yangu zinafanana" Trigger aliongea huku akijifuta jasho,

"wewe habari uliyonayo ni ipi?" Harry aliuliza,

"Tekso ndiye aliyelipuliwa bomu ile jana usiku" Trigger aliongea na kumfanya Harry ajishike mdomo,

"wewe nani kakwambia?" Harry aliuliza,

"angalia taharifa za habari, ile chini na saa anayovaa ndio vilivyokutwa baada ya kupekua eneo la mlipuko" Trigger aliongea na kumfanya Harry wasiwasi umuongezeke,

"mbona nakiona kifo changu" Harry aliongea kwa uoga huku akitetemeka,

"unasema?" Trigger alimuuliza baada ya kuhisi hamuelewi,

"hamna, Taita anaendeleaje?" Harry aliamua kubadili mada,

"ametolewa leo kwenye chumba cha watu mahututi, amepelekwa wodi ya kawaida" Trigger alijibu na kumfanya Harry ashtuke, maana muda wote wakati Taita yupo mahututi, Harry alikuwa anaomba Taita afe tu kwa maana alikuwa anamnyima amani,

"jambo jema, nitaenda baadae kumuona" Harry aliongea kinyoge huku mawazo yakiwa yamemtawala,

"sasa mimi naondoka, nilikuletea tu hiyo habari" Trigger aliongea huku akinyanyuka,

"na kuhusu Tekso tunafanyaje" Harry aliuliza,

"ndio naenda kufuatilia, then niwataharifu ndugu zake" Trigger alijibu,

"sawa, fanya hivyo" Harry aliongea na kumuacha Trigger akiondoka.

"sasa si bora nimuue Taita kwa mikono yangu mwenyewe, nitaishi vipi sasa, nataka kuwa huru" Harry aliongea huku akijikuna nywele zake,

"lazima niue, nimuue ninaemuweza, Aisha simuwezi, Sarah simuwezi, Taita nitajaribu" Harry aliongea peke yake huku akiinuka kwenye kiti.

*******************

Asubuhi sana Sarah aliwahi kudamka, akamuamsha na dokta Pendo,

"sasa acha mimi nyumbani mara moja, natakiwa nibadili nguo niende kazini, leo kuna mkataba itabidi niusaini mimi kama mkurugenzi mkuu wa kampuni" Sarah aliongea huku akimuangalia Dokta Pendo,

"sasa kwani lazima uende nyumbani? Nguo si unanunua mjini unabadilishia dukani?" Dokta Pendo aliuliza,

"yaani kwenda nyumbani lazima niende tu, kwanza nafuata kadi ya kutolea pesa, kwa maana hapa sina hela, pili kuna baadhi ya nyaraka natakiwa nizifuate, zipo nyumbani" Sarah aliongea,

"hapo siwezi kukuzuia, sasa usingetoka jana usiku, hiyo mikataba ingesainiwa na nani uko ofisini kwako?" Dokta Pendo aliuliza,

"lazima ningetoka, tayari nilikuwa na mipango yangu kichwani" Sarah aliongea huku akicheka,

"poa bwana, kuwa muangalifu, hutakiwi kujionesha sana mtaani, si unajua bado unatafutwa?" Dokta Pendo alimtahadharisha Sarah,

"usijali shoga yangu, nitawahi kurudi nije nikusaidie kukuogesha" Sarah aliongea huku akisimama,

"sawa shoga yangu" Dokta Pendo aliongea,

"haya, kwaheri" Sarah aliongea huku akimbusu Dokta Pendo kwenye paji la uso, kisha akatoka zake.

Alitembea mpaka nje ya jengo la hotel, akachukua bajaj iliyomfikisha nyumbani kwake, kisha akaingia ndani na kuchukua pesa, akamlipa dereva wa bajaji na kisha dereva wa bajaj akaondoka zake, Sarah akarudi ndani, akampita babu yake sebuleni, babu alikuwa akiangalia TV, ila alivyoomuona Sarah babu alipatwa na hofu, aliogopa.

Sarah akapitiliza chumbani kwake bila kuongea kitu, kisha akaingia bafuni kuoga.

Huku sebuleni babu akataka kutoka kukimbia, ila alipojaribu kufungua mlango ila mlango haukufunguka, babu hofu ikaongezeka, babu akachukua simu yake ili awapigie simu polisi, akakuta mtandao hamna, Sarah alizuia mawasiliano yote yanayoingia na kutoka ndani ya nyumba yake.

Babu yake Sarah akaona hali ngumu, akamkimbilia chumbani kwake na kujifungia, Sarah alikuwa anayoona yote kwenye runinga ndogo iliyopo bafuni kwake, alikuwa ametega camera kila sehemu ya nyumba yake.

Sarah alivyomaliza kuoga alitoka bafuni na kuvaa nguo zake, kisha akafungua kabati na kutoa nyaraka kadhaa, akazikagua na kuzirudisha kwenye bahasha ya kaki, kisha akatoka mpaka sebuleni na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye chumba cha babu yake, alitumia funguo kufungua na kumkuta babu yake akiwa amejikunyata kitandani,

"chukua hii, utatumia kwa ajili ya kununua chakula" Sarah aliongea huku akitupa noti mbili za elfu kumi kwenye sakafu, kisha Sarah akawa anatoka nje, alivyofungua tu geti ili atoe gari, alishtuka akikamatwa mkono,

"wewe ndio umeua askari na kutoroka kituoni?" Sauti iliongea huku akiivuta mikono ya Sarah, Sarah alipotupa jicho kumuangalia huyo mtu, akakuta ni askari wakiwa watano wakiwa wamemzunguka na mmoja ndiyo huyo alikuwa amemshika mkono.............................

***********ITAENDELEA************

the Legend☆
Nampenda Dr pendo mm
 
Sophoghani nliwahi kukwambia kua mimi sio mtunzi wa hizi riwaya, kuna sehemu nazitoa pia, na najitahidi kuziweka hapa jf ili ziwafkie wengi zaidi. Ukiona imekuchosha acha tuu kuifuatilia, sikumbuki kama nlishawahi kukulazimisha kuifuatilia. Kama unataka kusoma kwa mkupuo mwanzo mpaka mwisho nakushauri utafute vitabu. Tuliozea tutasonga nayo mpaka mwisho

the Legend☆
Watu kama hao usisumbuke kuwajibu
 
Sophoghani nliwahi kukwambia kua mimi sio mtunzi wa hizi riwaya, kuna sehemu nazitoa pia, na najitahidi kuziweka hapa jf ili ziwafkie wengi zaidi. Ukiona imekuchosha acha tuu kuifuatilia, sikumbuki kama nlishawahi kukulazimisha kuifuatilia. Kama unataka kusoma kwa mkupuo mwanzo mpaka mwisho nakushauri utafute vitabu. Tuliozea tutasonga nayo mpaka mwisho

the Legend☆
Mwambie aache ushanba kwanza kitu chenyewe tunapewa kwa hisani halafu unaleta ujuaji akwende zake huko
 
Haya Mambo ya kuwekeana vipande vipande yamenichosha, Sasa ivi nishajua na mute Kama wiki 2 ndio nakuja Soma ikiwa imekamilika mnanipandisha vibes af nianze subir kesho Tena mambo ya watchout part two, bongo movie...........

Kazi nzuri ila huu usambazaji umenichosha nimeacha riwaya nyingi sana kwa huu utaratibu



Sent using Jamii Forums mobile app
Ukuje wewe ushushe hizo bampa to bampa
 
Muelekeze chimbo akanunue Kama ataweza kulipia?
Watu wanapenda kitoga Bila ya kujali muda wa wenzao, anachotaka yeye utiririke tu mwanzo mwisho utafikiri huna majukumu mengine ya kufanya
Mkuu watu wa aina hiyo ni kuwasamehe na kuwapotezea tuu

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom