Riwaya: Sala ya Sarah

Riwaya: Sala ya Sarah

RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA AROBAINI NA NANE.

ENDELEA..................

Baada ya hapo, Harry na Trigger wakiwa ndani ya gari wakimsubiri Tekso, walikaa muda kidogo bila Tekso kutokea,

"atakuwa ameondoka nini?" Trigger aliuliza baada ya kusubiri kwa muda,

"na kwanini aondoke bila kutupa taharifa?" Harry aliuliza,

"si mlikuwa mnawasiliana lakini, muulize" Trigger aliongea,

"baada ya mlipuko mawasiliano yalikatika" Harry alijibu,

"tunapotezeana muda tu hapa" Trigger aliongea huku akiwasha gari,

"pita njia ya kule darajani tukashuhudie miili ya mabinti" Harry alimwambia Trigger,

"tutasikia kwenye taharifa ya habari" Trigger alijibu huku akigeuza gari, hakupita njia ya darajani, alipita njia tofauti kabisa na ile aliyoitaka Harry.

**************

Aisha na Sarah walivyotoka kituoni kwa polisi, walikimbilia mpaka darajani kwa chini, walivyofika Aisha akaangalia kwenye jengo moja refu, kisha akawa anavua kile kikoti alichopewa na Tekso, cha ajabu kile kikoti hakikuwa na kifungo cha juu kile kikubwa, wakati akivua kile kikoti Tekso alimuona kupitia darubini, alichofanya Tekso ni kubonyeza remote ya kulipua bomu kabla, baada ya hapo kikasikika kishindo kikubwa,

"suicide mission" Aisha aliongea huku akitazama juu ya jengo ambapo alikuwepo Tekso, kulikuwa kunawaka moto, kwa maana hiyo Tekso alijilipua mwenyewe, Sarah alikuwa akishangaa tu namna Aisha alivyokuwa anatabasamu,

"Hilo bomu ulitega wewe?" Sarah alimuuliza Aisha,

"wale washenzi walinitegea mimi kwenye kifungo kimoja cha hili koti, ila wakati tupo ndani ya gari nilikitoa kifungo bila wao kujua na kukipachika kwenye nywele ndefu za Tekso, sasa amejilipua yeye huku akijua ananilipua mimi" Aisha aliongea huku akiendelea kutabasamu,

"ni wenzako lakini, kwanini watake kukuua?" Sarah aliuliza,

"sio wenzangu, walinikodi tu nikuue wewe, sasa walivyoona nachelewa wakajua labda mimi na wewe ni kitu kimoja, wakanitegea bomu ili nikiwa na wewe ndio walipue" Aisha aliongea huku akikaa juu ya jiwe,

"kwanini wasingetulipua ndani ya kituo cha polisi!?" Sarah aliuliza,

"hawakutaka watu wengi wafe" Aisha alijibu,

"sasa pale bomu lilipolipukia si ni hotelini, sasa ndio wamekufa watu wengi zaidi?" Sarah aliuliza,

"sio kosa langu" Aisha alijibu,

"nyie wote wapuuzi, hamjui mnachokifanya, mmeua watu wengi kwa ajili ya ujinga wenu" Sarah aliongea kwa hasira huku akiondoka,

"sema asante sasa kwa kukutoa polisi na kukuepusha na mlipuko wa bomu" Aisha aliongea huku akicheka akimuangalia Sarah anavyoondoka,

"hata usingenitoa polisi, ningetoka mwenyewe katika muda niliotaka" Sarah aliongea huku akisimama na kumgeukia Aisha,

"nitakufumua malaya wewe" Aisha aliongea kwa utani huku akimnyooshea bunduki Sarah,

"piga, nimeshapigwa risasi nyingi tu" Sarah aliongea kwa jeuri kisha akageuka na kuondoka na kumuacha Aisha akitabasamu huku akitingisha kichwa chake.

Baada ya hapo Aisha alinyanyuka na kuondoka zake, alikuwa na hasira sana juu ya Harry, na wala hakutaka kumpigia simu ili amwambie bado yupo hai, alichofanya Aisha alielekea moja kwa moja nyumbani kwake, alipofika aliingia ndani na kuelekea moja kwa moja bafuni, akaondoa nguo zote na kuingia ndani ya sink, akafunga macho,

"Harry sitaki vita na wewe, ila ikinibidi nitafanya utakavyo, very easy kudili na wewe, huna mbinu hujui kupambana na wala hajui lolote kuhusu technology, unachojua ni sheria tu" Aisha aliongea huku povu la jakuzi likiwa limemmeza na kumuacha kichwa tu, tena sehemu ya uso.

*********************

Sajenti Minja akiwa amefungwa kamba na akiwa anamuangalia mwenzake ambaye alikuwa tayari marehemu tayari baada ya kupigwa risasi na Aisha.

Sajenti Minja akiwa anaangalia namna ya kujiokoa alishuhudia mtu akiingia ndani, alikuwa askari,

"hii hatari, pole kiongozi" Askari aliyeingia aliongea huku akimfungua Sajenti Minja,

"asante, uko nje kuko salama?" Sajenti Minja aliuliza,

"hakuna usalama kwa kweli, kuna askari wamepigwa, wengine wapo kwenye hali mbaya" Askari alijibu,

"mshike huyu miguuni mimi nimshike mikononi tumbebe tumpele hospitali" Sajenti Minja aliongea huku akiishika mikono ya yule askari ambaye alikuwa amekufa. Wakambeba mpaka nje, koridoni alipishana na askari kadhaa wakiwa na majeraha na wengine wakipeana pole, wengine waliangua kilio baada ya kuuona mwili wa mwenzao ukibebwa na kupelekwa kwenye gari.

Sajenti Minja wakati akiendelea kuwasaidia kuwabeba majeruhi wengine, alipigiwa simu na mkubwa wake,

"upo wapi?" Mkuu wa polisi aliuliza baada ya Sajenti Minja kupokea simu,

"nipo kituoni, tulivamiwa" Sajenti Minja alijibu kwa utulivu,

"mmevamiwa? na nani?" Mkuu wa polisi aliuliza kwa mshangao,

"kuna mwanamke alituvamia na kumchukua yule mtuhumiwa tuliyekuwa tumemkamata kwa kesi ya kumteka na kumtorosha mgonjwa hospitali" Sajenti Minja alijibu,

"kuna uharibifu wowote umefanyika?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"ameua mtu askari mmoja na wengine kama nane wamejeruhiwa" Sajenti Minja aliongea,

"waandishi wa habari wamefika?" Mkuu wa polisi aliuliza kwa wasiwasi,

"hapana" Sajenti Minja alijibu,

"hakikisheni hakuna mtu yoyote tofauti na nyie atakayejua hilo tukio, msimwambie mtu yoyote" Mkuu wa polisi aliongea kwa mamlaka,

"hakuna shida mkuu" Sajenti Minja aliongea kinyenyekevu,

"ila hicho sio nilichokupigia, sababu ya mimi kukupigia simu ni kutaka uende hoteli ya Rock Hill, kuna mlipuko umetokea muda sio mrefu" Mkuu wa polisi aliongea,

"sawa mkuu, naenda sasa hivi" Sajenti Minja aliongea,

"sawa, mimi nakuja hapo kituoni muda sio mrefu" Mkuu wa polisi aliongea kisha akakata simu.

"huu usiku wa leo wa ajabu sana" Sajenti Minja aliongea kisha akachukua gari yake na kuondoka kwenda kwenye hotel ya Rock Hill, haikuwa mbali na kituo cha polisi, ilikuwa ni jirani tu.

Baada ya muda mfupi Sajenti Minja aliweza kufika kwenye jengo la hotel na kukuta kikosi cha zima moto kikiwajibika katika kufanya kazi husika, bahati nzuri alikuta zimamoto wako kwenye hatua za mwisho za kuzima moto huo, Sajenti Minja akasogelea kundi la watu ambao walikuwa wamevaa Sare, alihisi ni wafanyakazi wa hotel ile,

"nyie ni wahusika?" Sajenti Minja aliuliza baada ya salamu,

"ndio" walijibu,

"Mimi ni askari, nani alikuwa zamu leo?" Sajenti Minja aliuliza,

"wote unaotuona hapa tulikuwa zamu leo" msichana mmoja alijibu,

"aliyekuwa msimamizi mkuu ni yupi?" Sajenti Minja aliuliza,

"ni mimi" Yule msichana akajibu tena,

"nifuate" Sajenti Minja aliongea kisha yule binti akamfuata, safari yao ikaishia mbele ya watu wa kikosi cha zima moto, wakasalimiana na Sajenti Minja, ni mtu ambaye wanamfahamu,

"sasa naombeni mtupeleke kule juu kwa kutumia winch lenu, kuna ukaguzi nataka kuufanya" Sajenti Minja aliongea kisha wale mabwana wa kikosi cha zimamoto wakafanya kama Sajenti Minja alivyotoka.

Wakafika mpaka eneo la juu kabisa ambapo sehemu ndogo ilikuwa imeharibika vibaya, walipofika juu waliweza kukuta mwili wa mtu ukiwa umeungua vibaya na mbaya zaidi baadhi ya vipande vya mwili wa huyo mtu vilikuwa vimetawanywa vibaya, yule binti ambaye ndiye msimamizi wa ile hotel ilimbidi aanze kulia kwa maana hajawahi kukutana na tukio la kutisha namna ile, ilibidi vijana kadhaa wa kikosi cha zima moto wamfariji.

Sajenti Minja katika kukagua kagua mwili ule, aliweza kuokota mkufu wa shaba uliokuwa na kidani kilichokuwa na herufi "S", Sajenti Minja akachukua kama ushahidi na kuweka ndani ya mfuko wa nylon, kisha akamgeukia yule binti ambaye ndiye msimamizi wa ile hotel,

"hiki chumba alipanga nani?" Sajenti Minja aliuliza,

"ni kijana mmoja, aliingia usiku huu" binti yule alijibu,

"jina lake nani?" Sajenti Minja aliuliza,

"jina tulikuwa bado hatujaandika kwa maana alitaka kwanza aangalie kama hiki chumba kitamfaa" Binti alijibu na kumfanya Sajenti Minja akunje uso kwa mshangao,

"huo utaratibu gani mnampa chumba mtu alafu jina mnamuandika baadae?" Sajenti Minja aliuliza,

"hotel yetu ina utaratibu huo" Binti alijibu, kisha Sajenti Minja akainama chini na kuokota kitu, ilikuwa ni saa,

"tushusheni chini, nimemaliza" Sajenti Minja aliongea na kisha wale vijana wa zimamoto wakatekeleza agizo la Sajenti Minja, wakamshusha chini akiwa pamoja na yule binti.

Walipofika chini, Sajenti Minja alikutana na waandishi habari ambao walimuhoji maswali machache na kisha akayajibu kwa namna anavyojua yeye, kisha akaingia kwenye gari yake na kuiwasha,

"leo mambo hayajaenda nitakavyo, ngoja nikamuone Dokta Pendo" Sajenti Minja aliongea huku akiwa ameegemea staring ya gari lake, kisha akanyanyua sura yake na kuondoa gari, ilikuwa safari ya kwenda hotelini, kwenda kumuona Dokta Pendo.

**********************

Baada ya Sarah kuachana na Aisha, Sarah hakuwaza kitu kingine, alichowaza muda huo ni hali ya Dokta Pendo, wala hakutaka kuwaza kuwa Dokta Pendo alijibu nini alipokuwa akihojiwa, aliamini tu kuwa Dokta Pendo ni mtu mwema kwake, kwa sababu ameshamsaidia kwenye hali nyingi tete.

Sarah akatembea mpaka kwenye eneo moja lililokuwa na watu wengi wakifanya shughuli mbalimbali usiku ule, alienda moja kwa moja kwenye duka dogo ambalo lilionekana likifanya biashara ya kuchajisha simu, aligundua kutokana na tangazo lililokuwa limebandikwa nje.

"naweza kupata huduma ya kupiga simu?" Sarah aliongea baada ya kumsalimia muuzaji,

"hapana, hatuna huduma hiyo" Muuzaji alijibu na kumfanya Sarah ashike kichwa kwa mawazo,

"naomba unisaidie, nitanunua vocha" Sarah aliongea kwa huruma,

"inaelekea una shida sana, tumia, ongea haraka maana salio linakata muda sio mrefu, nna sekunde ishirini tu" Muuzaji aliongea huku akimpa Sarah simu,

"sekunde ishirini ni nyingi sana" Sarah aliongea huku akiipokea ile simu, kisha akaandika namba ya Dokta Pendo, aliihifadhi kichwani, baada ya kuandika akapiga, simu ikaanza kuita,

"hallow" Dokta Pendo alipokea,

"Mimi Sarah, upo wapi?" Sarah aliuliza,

"nipo hotelini, njoo shoga yangu" Dokta Pendo aliongea kwa furaha,

"hotel gani shoga" Sarah aliuliza kisha Dokta Pendo akamuelekeza, Sarah akairudisha simu ya watu na kushukuru, kisha akaanza kutembea mdogo mdogo kwenda kwenye hiyo hotel aliyoelekezwa na dokta Pendo, hakuwa na pesa muda huo, pesa yote aliiacha kaunta ya polisi.

Sarah alifanikiwa kufika sehemu ya mapokezi ya hotel na kumuulizia mwenyeji wake, akapelekwa mpaka chumba alichopo Dokta Pendo, alipofika wakakumbatiana kwa furaha,

"kaoge kwanza shoga" Dokta Pendo alimwambia mwenzake,

"kwani ninanuka shoga?" Sarah aliuliza huku akicheka,

"kukaa selo ni mkosi, nenda kaoge na uzitupe hizo nguo" Dokta Pendo aliongea,

"nikizitupa nitavaa nini shoga?" Sarah aliuliza huku akielekea bafuni,

"tutajua baadae" Dokta Pendo aliongea wakati Sarah akiingia bafuni.

Baada ya dakika kumi na tano Sarah alikuwa amemaliza kuoga na alikuwa yupo kitandani amekaa na dokta Pendo,

"umetokaje polisi? Sajenti Minja amekuachia?" Dokta Pendo aliuliza,

"nina njaa kwanza, natakiwa nile alafu tutaongea baadae" Sarah aliongea,

"ngoja niwapige simu wahudumu, utakula chakula gani?" Dokta Pendo aliuliza,

"chai, alafu wali na samaki" Sarah alijibu,

"shoga unapenda chai wewe" Dokta Pendo aliongea huku akitabasamu kisha akachukua simu na kuwapigia wahudumu, akawaagiza wampelekee chakula.

"wakati tukiwa tunasubiri chakula, haya niambie umetokaje polisi?" Dokta Pendo aliuliza,

"Aisha, yule mwanamke wa kikosi cha Taita ndio aliyekuja kunitorosha" Sarah aliongea na kumfanya Dokta Pendo ashangae,

"kwanini Aisha, kwani mnajuana?" Dokta Pendo aliuliza kwa mshangao,

"sijui kitu shoga yangu, mimi mwenyewe bado najiuliza ingawa alinipa sababu" Sarah alijibu,

"sababu gani?" Dokta Pendo aliuliza,

"eti Aisha alitegewa bomu bila yeye kujua, wakataka aje kunitorosha, alafu ndio wamlipue tukiwa nae" Sarah alijibu na kipindi hicho mlango ulikuwa ukigongwa,

"chakula hicho kimekuja, kamfungulie" Dokta Pendo aliongea na kisha Sarah akainuka, akaenda mpaka mlangoni na kufungua mlango, mlango ulivyofunguka kidogo akimbie, alikutana na Sajenti Minja ambaye alikuja kumuangalia Dokta Pendo,

"wewe mpumbavu kumbe umekimbilia huku?" Sajenti Minja aliuliza huku akiwa amesimama mlangoni anamuangalia Sarah.........

**********ITAENDELEA**********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA AROBAINI NA TISA

ENDELEA..................

Sarah akawa anarudi nyuma huku akiwa anajiuliza afanye kitu cha kushtukiza au akae kimya na kujifanya mjinga?

Sajenti Minja akaingia ndani na kufunga mlango, kipindi hicho chote Dokta Pendo alikuwa akiangalia tu,

"ebu Kaa hapa shoga yangu" Dokta Pendo aliongea huku akiwa anaoneshea eneo la jirani na alipo yeye, Sarah akasogea na kukaa pembeni ya Dokta Pendo, aliamua kutulia tu,

"mwenzako yupo wapi?" Sajenti Minja aliuliza huku akiwa bado amesimama,

"yule sio mwenzangu, hata mimi simjui" Sarah alijibu,

"aisee safari hii utaozea jela, yaani mnavamia kituo na kuua askari?" Sajenti Minja aliuliza,

"huyo mwenzako anayeuliziwa ni yupi?" Dokta Pendo aliuliza huku akimuangalia Sarah,

"eti Aisha" Sarah alijibu huku akiwa na hofu,

"sasa Sarah na Aisha wapi na wapi? Mbona unatuchanganyia habari wewe?" Dokta Pendo aliongea kwa mshangao huku akimuangalia Sajenti Minja,

"muulize mwenyewe aseme ni kweli alitoroshwa na huyo mwanamke au ametoroka mwenyewe?" Sajenti Minja aliuliza,

"ebu fungua mlango huo, kuna mtu anagonga mlango" Dokta Pendo alimwambia Sajenti Minja aliyekuwa amesimama mlangoni, kisha Sajenti Minja akageuka na kufungua mlango, alikutana na muhudumu aliyekuwa amebeba chakula,

"kilete hapa" Sarah aliongea huku akikaa vizuri, yule Muhudumu akaisogeza meza iliyokuwa pembeni na kumsogezea Sarah, kisha akaweka chakula juu ya meza, alafu akaondoka zake,

"kula shoga yangu, najua una njaa sana" Dokta Pendo aliongea huku akimpiga piga Sarah mgongoni,

"we Sarah si nimekuuliza? Kama yule mwanamke humjui ni kwa nini amekutorosha?" Sajenti Minja aliuliza huku akiuzuia mkono wa Sarah uliokuwa unapeleka chakula kinywani,

"khaa jamani!!!! kula ni ibada sasa kwa nini unasumbua mwenzio?" Dokta Pendo aliuliza kwa huruma,

"wewe unataka kujua nini?" Sarah aliuliza kwa hasira huku akikitupa kijiko cha chakula,

"yule mwanamke ni nani kwako?" Sajenti Minja aliuliza,

"yule mwanamke ndiye aliyemteka Dokta Pendo na kumvunja miguu, yule mwanamke ameshawahi kutaka kunichinja mara mbili, na yule mwanamke ndiye yule uliyeniokoa kule Vin hotel aliyetaka kunidhuru. Una jingine?" Sarah aliuliza kwa hasira,

"kwanini sasa amekuja kukuokoa?" Sajenti Minja aliuliza,

"hakuja kuniokoa kama unavyosema, alikuja kunichukua ili akanidhuru" Sarah alijibu na kumfanya Sajenti Minja acheke kwa dhihaka, yaani aliona anadanganywa,

"sasa mbona upo hapa ukiwa mzima na hujadhurika?" Sajenti Minja aliuliza baada ya kumaliza kucheka,

"hujasikia mlio wa bomu jirani na ofisi yenu?" Sarah aliuliza na kumfanya Sajenti Minja atege vizuri masikio yake,

"basi lile bomu lilitakiwa liniondoe mimi na yule mwanamke, yaani alitegewa yule mwanamke" Sarah aliongea,

"sasa kwanini akalipuka mtu mwingine?" Sajenti Minja aliuliza,

"yule ndiye aliyetega bomu, ila yule mwanamke aliyekuja pale polisi aligundua mapema ametegewa bomu, akatumia maarifa kumpachika lile lile bomu yule mtu aliyelipukiwa" Sarah aliongea na kumfanya Sajenti Minja apate mwanga,

"na kwanini watake kukuua wewe, una tatizo nao?" Sajenti Minja aliuliza,

"sina tatizo, labda wao wana tatizo na mimi" Sarah alijibu,

"maliza kula twende kituoni, utakuwa na mengi sana ya kunieleza" Sajenti Minja aliongea huku akikaa chini,

"wewe mtu vipi? Wewe unadhani kituoni kuzuri kule? wewe muhoji hapa hapa bwana" Dokta Pendo aliongea kwa ukali huku akimuangalia Sajenti Minja kwa jicho kali,

"wewe mbona unamtetea sana Sarah?" Sajenti Minja aliuliza kwa ukali,

"sioni kosa lake, mlimkamata kwa kudai ameniteka, mlivyonihoji nikakanusha hilo jambo, haya sasa hivi mnataka kumzushia kesi kubwa zaidi, eti ameshirikiana na mwenzie kumuua askari, hamna hata haya?" Dokta Pendo aliongea na kumfanya Sajenti Minja acheke,

"sasa wswe unatakaje?" Sajenti Minja aliuliza,

"Mimi huyu ni kama kijakazi wangu, ananiogesha na kunifanyia usafi wote unaohitajika, sasa ukimchukua huyu kwa kesi ya kumsingizia, utaniogesha wewe? Nikienda msalani utanisafisha?" Dokta Pendo aliuliza huku akiwa amemshikia kiuno Sajenti Minja,

"sawa yaishe, je mnaweza kunisaidia kumpata huyo Aisha?" Sajenti Minja aliuliza,

"tutampata wapi na sisi hatujui anapokaa" Dokta Pendo alijibu,

"Sarah nakuacha kwa sababu ya Dokta Pendo, sasa ninachokuomba usirudi kwako mpaka nikupe taharifa, maana ni lazima askari waende kukagua au kukuwinda maeneo ya kule kwako" Sajenti Minja aliongea huku akimuangalia Sarah,

"yaani nakosa uhuru kwa jambo ambalo sijalifanya?" Sarah aliuliza huku akisikitika,

"bwana wewe shukuru tu, bora uishi kwa kujificha kuliko kuishi mule selo" Dokta Pendo aliongea huku akijilaza,

"sasa mimi ninaondoka, nitarudi kesho kuwaambia kinachoendelea uko kituoni" Sajenti Minja aliongea huku akinyanyuka,

"sawa baba" Dokta Pendo alijibu,

"haya, mbaki Salama" Sajenti Minja aliongea huku akitoka nje,

"asante, na wewe pia" Dokta Pendo alijibu Wakati Sajenti Minja akifunga mlango.

"asante shoga, maana mmh" Sarah aliongea huku akiwa ahamini kama Sajenti Minja amemuacha,

"usijali shoga, tutaongea kesho, acha nilale maana nimechoka kweli" Dokta Pendo aliongea,

"sawa, mimi mwenyewe nikimaliza tu kula nalala" Sarah aliongea huku akiendelea kula.

**************************

.

Asubuhi hii bado Harry hakuweza kupata habari yoyote kuhusu Tekso, na kila alipojaribu kupiga namba yake ikawa hazipatikani. Harry akiwa ofisini kwake alishuhudia simu yake ikipokea ujumbe mfupi wa maneno, alipotazama jina la mtu aliyetuma huo ujumbe, kidogo ashtuke, aliona jina la Aisha, Harry akaichukua simu yake na kuufungua huo ujumbe,

"ulidhani nitakufa?" ujumbe uliandikwa hivyo na kumfanya sasa Harry achanganyikiwe, hakutegemea kabisa kusikia leo hii Aisha yupo hai. Harry akajaribu kupiga namba ya Aisha ili ampoze, ila siku iliita bila kupokelewa, akajaribu tena na tena ila hali ikawa ile ile, na mwisho kabisa simu ya Aisha ikawa haipatikani,

"huyu hajafa kweli au kuna mtu ananichezea?" Harry alijiuliza huku akirudia kuusoma ule ujumbe uliotumwa na Aisha, akajikuta anatabasamu mwenyewe.

Na muda huo huo akaingia Trigger, ujio haukuwa wa kawaida ule, aliingia akihema juu juu na kumfanya Harry amtolee macho,

"nina habari ya kushangaza sana" Trigger aliongea huku akikaa kwenye kiti,

"Mimi niliyonayo inashangaza zaidi" Harry aliongea kwa utulivu huku akimuangalia Trigger,

"wewe unayo ipi?" Trigger aliuliza,

"Aisha hajafa, yupo hai" Harry aliongea na kufanya Trigger amtumbulie macho,

"basi habari hiyo na habari yangu zinafanana" Trigger aliongea huku akijifuta jasho,

"wewe habari uliyonayo ni ipi?" Harry aliuliza,

"Tekso ndiye aliyelipuliwa bomu ile jana usiku" Trigger aliongea na kumfanya Harry ajishike mdomo,

"wewe nani kakwambia?" Harry aliuliza,

"angalia taharifa za habari, ile chini na saa anayovaa ndio vilivyokutwa baada ya kupekua eneo la mlipuko" Trigger aliongea na kumfanya Harry wasiwasi umuongezeke,

"mbona nakiona kifo changu" Harry aliongea kwa uoga huku akitetemeka,

"unasema?" Trigger alimuuliza baada ya kuhisi hamuelewi,

"hamna, Taita anaendeleaje?" Harry aliamua kubadili mada,

"ametolewa leo kwenye chumba cha watu mahututi, amepelekwa wodi ya kawaida" Trigger alijibu na kumfanya Harry ashtuke, maana muda wote wakati Taita yupo mahututi, Harry alikuwa anaomba Taita afe tu kwa maana alikuwa anamnyima amani,

"jambo jema, nitaenda baadae kumuona" Harry aliongea kinyoge huku mawazo yakiwa yamemtawala,

"sasa mimi naondoka, nilikuletea tu hiyo habari" Trigger aliongea huku akinyanyuka,

"na kuhusu Tekso tunafanyaje" Harry aliuliza,

"ndio naenda kufuatilia, then niwataharifu ndugu zake" Trigger alijibu,

"sawa, fanya hivyo" Harry aliongea na kumuacha Trigger akiondoka.

"sasa si bora nimuue Taita kwa mikono yangu mwenyewe, nitaishi vipi sasa, nataka kuwa huru" Harry aliongea huku akijikuna nywele zake,

"lazima niue, nimuue ninaemuweza, Aisha simuwezi, Sarah simuwezi, Taita nitajaribu" Harry aliongea peke yake huku akiinuka kwenye kiti.

*******************

Asubuhi sana Sarah aliwahi kudamka, akamuamsha na dokta Pendo,

"sasa acha mimi nyumbani mara moja, natakiwa nibadili nguo niende kazini, leo kuna mkataba itabidi niusaini mimi kama mkurugenzi mkuu wa kampuni" Sarah aliongea huku akimuangalia Dokta Pendo,

"sasa kwani lazima uende nyumbani? Nguo si unanunua mjini unabadilishia dukani?" Dokta Pendo aliuliza,

"yaani kwenda nyumbani lazima niende tu, kwanza nafuata kadi ya kutolea pesa, kwa maana hapa sina hela, pili kuna baadhi ya nyaraka natakiwa nizifuate, zipo nyumbani" Sarah aliongea,

"hapo siwezi kukuzuia, sasa usingetoka jana usiku, hiyo mikataba ingesainiwa na nani uko ofisini kwako?" Dokta Pendo aliuliza,

"lazima ningetoka, tayari nilikuwa na mipango yangu kichwani" Sarah aliongea huku akicheka,

"poa bwana, kuwa muangalifu, hutakiwi kujionesha sana mtaani, si unajua bado unatafutwa?" Dokta Pendo alimtahadharisha Sarah,

"usijali shoga yangu, nitawahi kurudi nije nikusaidie kukuogesha" Sarah aliongea huku akisimama,

"sawa shoga yangu" Dokta Pendo aliongea,

"haya, kwaheri" Sarah aliongea huku akimbusu Dokta Pendo kwenye paji la uso, kisha akatoka zake.

Alitembea mpaka nje ya jengo la hotel, akachukua bajaj iliyomfikisha nyumbani kwake, kisha akaingia ndani na kuchukua pesa, akamlipa dereva wa bajaji na kisha dereva wa bajaj akaondoka zake, Sarah akarudi ndani, akampita babu yake sebuleni, babu alikuwa akiangalia TV, ila alivyoomuona Sarah babu alipatwa na hofu, aliogopa.

Sarah akapitiliza chumbani kwake bila kuongea kitu, kisha akaingia bafuni kuoga.

Huku sebuleni babu akataka kutoka kukimbia, ila alipojaribu kufungua mlango ila mlango haukufunguka, babu hofu ikaongezeka, babu akachukua simu yake ili awapigie simu polisi, akakuta mtandao hamna, Sarah alizuia mawasiliano yote yanayoingia na kutoka ndani ya nyumba yake.

Babu yake Sarah akaona hali ngumu, akamkimbilia chumbani kwake na kujifungia, Sarah alikuwa anayoona yote kwenye runinga ndogo iliyopo bafuni kwake, alikuwa ametega camera kila sehemu ya nyumba yake.

Sarah alivyomaliza kuoga alitoka bafuni na kuvaa nguo zake, kisha akafungua kabati na kutoa nyaraka kadhaa, akazikagua na kuzirudisha kwenye bahasha ya kaki, kisha akatoka mpaka sebuleni na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye chumba cha babu yake, alitumia funguo kufungua na kumkuta babu yake akiwa amejikunyata kitandani,

"chukua hii, utatumia kwa ajili ya kununua chakula" Sarah aliongea huku akitupa noti mbili za elfu kumi kwenye sakafu, kisha Sarah akawa anatoka nje, alivyofungua tu geti ili atoe gari, alishtuka akikamatwa mkono,

"wewe ndio umeua askari na kutoroka kituoni?" Sauti iliongea huku akiivuta mikono ya Sarah, Sarah alipotupa jicho kumuangalia huyo mtu, akakuta ni askari wakiwa watano wakiwa wamemzunguka na mmoja ndiyo huyo alikuwa amemshika mkono.............................

***********ITAENDELEA************

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA HAMSINI

ENDELEA..................

Sarah akaona sasa kama akifanya uzembe anaweza kukosa kusaini mikataba ya kampuni yake,

"nitaenda mwenyewe, usinifunge pingu" Sarah aliongea huku akiivuta mikono yake kutoka kwa askari yule aliyemshika,

"wewe mwanamke usitupangie cha kufanya, usitufundishe kazi wewe" Askari yule aliongea huku akiivuta mikono ya Sarah na kutaka kuifunga pingu,

"usimfunge pingu, pingu ya nini wakati tupo sita hapa, alafu tumuhofie mwanamke mmoja tu?" Askari mwingine Aliuliza na kumfanya mwenzake asitishe zoezi la kumfunga Sarah pingu, na hicho ndicho kitu Sarah alikihitaji,

"songa mbele" Yule askari aliyetaka kumfunga Sarah pingu aliongea huku akimsukuma Sarah mgongoni, Sarah hakukasirika, badala yake alifurahi, alitembea hatua ndogo ndogo huku akiivuta sketi yake juu taratibu huku akizidi kuisogelea gari ya polisi, Sarah akainama na kuishika sketi eneo la mpasuo na kuvuta kidogo na kufanya mpasuo kuongezeka kidogo, kisha Sarah akatumia mwanya wa askari kushangaa anachofanya, Sarah akamvuta askari wa nyuma na kumpiga ngumi ya koromeo, yule askari akaangukia chini na kuanza kugala gala chini huku amejishika koo, askari mmoja akatoa bastola haraka, Sarah alikuwa na kasi zaidi ya haraka ya huyo askari, Sarah akaruka juu na kutua mbele ya askari yule, kisha akaudaka mkono wa yule askari na kisha akaupiga ngumi kwenye kiwiko, mkono wa yule askari ukastuka na kuiacha ile bastola, Sarah akaidaka na kisha akaachia teke lililompeleka yule askari chini, wale askari wengine wakataka na wao kutoa bastola,

"mi nawaua, mtu akichomoa tu silaha mi ninammaliza" Sarah aliongea huku akiwaelekezea bastola, wale askari wakawa wamesimama huku mikono yao ikiwa inataka kuelekea kwenye silaha zao.

Askari mmoja akataka kupuuza agizo la Sarah, akachomoa bastola yake, Sarah akamfyatulia risasi ya mkono iliyoondoka na kidole chake, yule askari akapiga ukelele wa maumivu huku akiwa ahamini kitendo kilichotokea,

"tupeni bastola chini" Sarah aliongea huku akiwaangalia, askari wakatii agizo na kuzirusha zile silaha mbele ya Sarah, Sarah akaziokota na kuziweka kwenye mkoba wake, kisha akapiga risasi tairi za mbele za gari waliyokuja nayo polisi, kisha akaingia kwenye gari yake na kuiwasha,

"nitakuja mwenyewe kituoni" Sarah aliongea huku akiwatizama polisi kisha akawasha gari na kuliondoa kwa kasi na kumuacha babu yake akichungulia getini huku akiwa anashangaa kitendo wanachofanyiwa polisi.

****************

Sajenti Minja alikuwa na dokta Pendo, alienda kumjulia hali na pia alienda kumjulisha Sarah kuwa kuna askari wataenda kwake asubuhi,

"Sarah yupo wapi?" Sajenti Minja aliuliza,

"Sarah ameenda kwake, anadai anatakiwa aende kazini kuna kazi muhimu" Dokta Pendo alijibu,

"aisee, atakuwa ameshakamatwa, kuna askari wametumwa kwenda kumkamata" Sajenti Minja aliongea huku akiwa hana tumaini,

"nenda basi kamsaidie" Dokta Pendo aliongea huku akiwa anataka kulia,

"Mimi nitamsaidiaje sasa?" Sajenti Minja aliuliza,

"nenda, au ngoja nimpigie simu" Dokta Pendo aliongea huku akibonyeza simu yake,

"simu yake ipo polisi, au ana namba nyingine?" Sajenti Minja aliuliza huku akimuangalia Dokta Pendo,

"dah, sasa tunafanyaje?" Dokta Pendo aliuliza huku akiwa amekata tamaa, na kipindi hicho simu ya Sajenti Minja ilikuwa ikiita,

"bosi huyo ananipigia, sijui kuna nini?" Sajenti Minja aliuliza huku akiiangalia simu yake,

"naam mkuu" Sajenti Minja aliongea baada ya kupokea simu,

"upo wapi?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"nipo njiani naelekea kituoni" Sajenti Minja alijibu,

"unapajua kwa yule dada aliyetoroshwa jana kituoni?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"ndio napajua" Sajenti Minja alijibu,

"nenda haraka" Mkuu wa polisi alitoa amri na Sajenti Minja hakutaka kuhoji zaidi, alijua lazima kuna tukio limetokea ambalo ni tofauti.

"Sarah kuna kitu kimetokea nyumbani kwake" Sajenti Minja aliongea huku akinyanyuka,

"atakuwa amekamatwa eee?" Dokta Pendo aliuliza kwa wasiwasi,

"sijajua, nimeambiwa tu niende" Sajenti Minja aliongea,

"ebu nenda, alafu unijulishe" Dokta Pendo aliongea huku akiwa bado na wasiwasi.

Sajenti Minja akatoka na kuelekea nje, kisha akaingia kwenye gari na akashika uelekeo unaenda nyumbani kwa Sarah, njia yote alikuwa anawaza kuna tukio gani gani limetokea uko.

Sajenti Minja ilimchukua dakika chache kufika nyumbani kwa Sarah, alikuta hali ya kushangaza sana, alikuta askari wakiwa wamekaa na kila mtu akionekana mwenye maumivu, ila mwenye maumivu zaidi alikuwa ni yule aloyetolewa kidole kwa ajili ya risasi,

"ingieni kwenye gari" Sajenti aliongea huku akiwaangalia wale askari ambao baadhi yao walijitahidi kumpigia saluti ila hakutaka kujali.

Baada ya wale askari kuingia ndani, Sajenti Minja akili yake ikamwambia ashuke ili aingie ndani kwa Sarah, alitelemka katika gari na kwenda mpaka ndani kwa Sarah, akamkuta babu yake Sarah akiwa sebuleni akiangaika kupiga simu bila mafanikio,

"mzee kuna usalama?" Sajenti Minja aliuliza,

"usalama utoke wapi? Rafiki yako amewapiga askari hapo nje" Babu yake Sarah aliongea na kumfanya Sajenti Minja ashtuke,

"rafiki yangu? Rafiki yangu gani?" Sajenti Minja aliuliza,

"Sarah" Babu yake Sarah alijibu,

"Sarah ndio amewapiga wanaume watano? Na mwingine kampiga risasi?" Sajenti Minja aliuliza huku akiwa ahamini,

"unashangaa nini? Yule si mwanamke wa kawaida, hafai kabisa" Babu yake Sarah alizidi kutoa maelezo yaliyozidi kumvuruga Sajenti Minja,

"twende kituoni ukanieleze vizuri" Sajenti Minja aliongea,

"kituoni tena? Maelezo si ninakupa hapa hapa?" babu yake Sarah aliongea,

"si unajua kuna wagonjwa ndani ya gari? Twende ili niwapitishe wagonjwa hospitali alafu niwaache hapo, alafu mimi na wewe tunaenda polisi" Sajenti Minja aliongea,

"sawa, twende" Babu yake Sarah aliongea na kisha akawa anaelekea nje huku Sajenti Minja akija kwa nyuma.

Wakatoka mpaka nje na kuingia ndani ya gari, kisha Sajenti Minja akawasha gari na kuliondoa huku wagonjwa wakiwa nyuma wakiugulia maumivu.

*******************

Harry aliamua kuelekea hospitali, alichukua gari yake na safari ikaishia kwenye geti la hospitali, akaegesha gari na kuingia mpaka ndani, akamkuta Vin akiwa na Taita wakiongea huku Vin akiwa na furaha,

"oooh Harry, vipi ndugu yangu" Taita aliongea kwa furaha alipomuona Harry,

"safi, aisee Mungu mkubwa, leo hii unaongea vizuri hivyo?" Harry aliongea huku akijilazimisha kuwa na furaha,

"yule malaya alitaka kuniua, ila ameshindwa, sasa mimi naenda kummaliza" Taita aliongea na kufanya Vin atege vizuri masikio,

"tuachane nae, mimi nadhani tusimfuatilie tena" Harry aliongea,

"Harry bado unao uoga? Mimi nilidhani kwa kilichonikuta utapata hasira na kupanga mashambulizi, kumbe mwenzangu unarudi nyuma?" Taita aliuliza kwa mshangao,

"Mimi nahisi natakiwa nitoke ili familia yangu iwe salama" Harry aliongea kwa utulivu,

"narudia tena Harry, endapo utasaliti hii safari tuliyoianza, ni lazima nikuue, sihitaji tena maelezo" Taita aliongea kwa ukali,

"kwani baba, huyo binti una tatizo nae gani?" Vin aliuliza huku akimuangalia Taita,

"ni mtu mbaya sana, hafai kabisa, nitakueleza baadae" Taita aliongea huku akimshika mkono Vin,

"aisee, nitarudi baadae" Harry aliongea huku akipiga hatua za kuondoka, hakuwa na raha kabisa,

"umekasirika kwa nilichokwambia? Hakuna budi mzee, pambana, ulishachagua kuwa upande wangu tangu tunaanza kazi hii, leo hii unataka kukimbia kwa kuwa yule mjusi wa kipindi kile amekuwa mamba?" Taita aliongea na kucheka, Harry hakutaka kujibu, badala yake aliendelea kutembea kuelekea nje.

"Baba ebu kuwa, muwazi, Sarah na wewe ugomvi wenu chanzo chake nini?" Vin aliuliza,

"nitakwambia mwanangu, ila kwa sasa unachotakiwa kufanya ni kunilinda mpaka nitoke hospitali" Taita aliongea Kwa upendo na mwanae,

"utaniambia lini sasa?" Vin aliuliza kwa ghadhabu,

"si unaona bado nipo hospitali? Nikitoka hospitali nitakusimulia kila kitu tukiwa nyumbani" Taita aliongea kwa kubembeleza huku akiwa na mwanae huyo,

"sawa bwana" Vin alijibu kinyonge huku akikaa pembeni ya baba yake huyo ambaye ni baba feki.

*******************

Nyakati za usiku Harry alifika hospitali na hakukuta mtu zaidi ya Taita, Harry akamsalimia Taita kisha akavuta kiti na kukaa,

"unaendeleaje?" Harry alimuuliza Taita,

"naendelea vizuri, ila nguvu ndio bado hazijarejea vyema" Taita alijibu,

"sasa, unajua tangu umepoteza fahamu kuna mambo mengi yametokea ikiwemo kumpoteza mtu wetu wa technology, Tekso, na tulipofikia inaelekea hakuna atayebaki, njia ya kumzuia Sarah ni kwenda kumfungulia kesi tu" Harry aliongea kwa utulivu na kumfanya Taita acheke,

"sasa hivi ndio mwisho wake, na vin ndio atakayemaliza huu mchezo, nataka amuue dada yake" Taita aliongea kwa kujiamini,

"Vin tayari kishawahi kumpiga risasi mbili na Sarah hakufa" Harry aliongea na kumfanya Taita ashtuke,

"kumbe wameshakutana?" Taita aliuliza,

"ndio, niliwakutanisha" Harry alijibu,

"umewaambia wao ni ndugu?" Taita aliuliza,

"hapana" Harry alijibu,

"safi sana, ngoja nitoke hapa tukaendeleze mapambano" Taita aliongea,

"Mimi hayo mapambano sitoendeleza, bora nikimbie niwaache" Harry aliongea,

"kukimbia huwezi, lazima nitakukamata na kukuua tu Harry, labda kama una njia nyingine ya kuniepuka" Taita aliongea kwa jeuri,

"njia ipo" Harry alijibu,

"ipi?" Taita aliuliza,

"lazima mmoja wenu afe, kati yako au Sarah" Harry aliongea huku akiangalia chini,

"hilo ndio jibu, najua kuniua mimi huwezi, sasa ni lazima umuue Sarah" Taita aliongea,

"kumuua Sarah nimeshindwa ingawa nimejaribu sana, sasa kwa kuwa nimeshindwa kumuua Sarah, ni bora nimuue wewe" Harry aliongea huku akiitoa bastola yake na kumuelekezea Taita,

"ni kweli au unanitania?" Taita aliuliza huku akijivuta ili akae vizuri kitandani,

"nipo hapa kwa ajili ya kutetea uhuru wangu na familia yangu, nimechoka kuishi kama mtumwa" Harry aliongea huku machozi yakimtoka,

"sasa endapo utaniua mimi, ndio Sarah atakusamehe?" Taita aliuliza huku akimtazama akimuangalia Harry,

"hatonisamehe ila nitaweza kukimbia na kwenda kujificha popote duniani" Harry aliongea kwa uchungu,

"sawa, niue" Taita aliongea na ghafla akashtukia akipigwa risasi ya kifuani na kutoa jicho kumuangalia Harry huku akiwa ahamini kama kweli amepigwa risasi na kipindi hicho Harry nae akiwa anashangaa ni wapi hiyo risasi maana yeye hakufyatua hiyo risasi,

"yaani nyani niliyemuokota porini na kumpa matunzo bora mpaka akawa mtu, leo hii unaniua?" Taita aliuliza huku akimuangalia Harry na kipindi hicho mkono wa Taita ulikuwa kifuani kwake akijishika jeraha la risasi na damu zilianza kuenea, kitu ambacho Taita hakujua ni kwamba ile risasi haikufyatuliwa na Harry,

"ila mimi...... " Harry alitaka ajitetee na kueleza kuwa hajampiga yeye, ila kabla hajaanza kumuelewesha Taita, mlango wa wodi ulifunguliwa na Vin akaingia na kumkuta Harry akiwa amemuelekezea bastola Taita, Vin akastuka na kipindi hicho risasi nyingine ikapigwa na kupiga bega la Taita, Vin akachukia sasa, akajua ni Harry amedhamiria kumuua baba yake na kipindi hicho Harry mshangao ukaongezeka na asijue ni nani anayefyatua hizo risasi.....................

**********ITAENDELEA***********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA HAMSINI NA MOJA.

ENDELEA..................

"unataka kumuua baba yangu?" Vin aliuliza huku akimfuata Harry kwa hasira, Harry kuona hivyo kwa haraka sana akamgeuzia bastola Vin, Vin hakujali, akawa anazidi kumsogelea Harry, ghafla pasipo kutegemea, Vin alipigwa risasi ya bega, haikuingia ila ilimpalaza tu, ingawa ilimpalaza ila maumivu yalimpata, Vin akaanguka chini na kujishika bega lake kwa maumivu aliyoyapata, Harry kuona hivyo akazidi kushangaa iweje watu wanapigwa risasi wakati yeye hajafyatua risasi hata moja? Wakati akijiuliza hivyo, akili nyingine ilimwambia akimbie eneo hilo kwa kuwa sio eneo salama kwake, Harry akamtupia macho Vin na kumuona akinyanyuka, Harry akatumia mwanya huo kukimbilia nje, Vin kuona hivyo nae akakurupuka na kutoka zake nje mbio kwenda kuona kama atamuwahi Harry, lakini hakumpata, ikambidi apige kelele na baadhi ya watu wakamzunguka,

"msaada, Dokta anaitajika aende wodi namba Saba, kuna mgonjwa amevamiwa" Vin aliongea na kufanya watu watoe taharifa kwa madaktari, daktari mmoja akakimbilia wodi namba saba, Vin nae akawa anamfuata kwa nyuma,

"subiri hapo hapo" Daktari mwingine alimzuia Vin kuingia wodini, ikambidi asubiri pale nje ya mlango, baada ya dakika moja mlango ulifunguliwa na wakatoka madaktari wawili wakiwa wanakisukuma kitanda cha Taita,

"mnampeleka wapi?" Vin aliuliza huku akitaka kuzuia kitanda,

"usijali Vin, nipo salama, naenda theater kutolewa risasi" Taita aliongea huku akitabasamu,

"sawa baba, nitangoja hapa hapa" Vin aliongea,

"Dokta, mchukueni huyu mkamtibie hapo begani, hamuoni akivuja damu" Taita alimwambia madaktari na hapo Vin akagundua kuwa nae amejeruhiwa,

"nae amepigwa risasi?" Daktari aliuliza,

""imenipalaza tu" Vin alijibu,

"twende na wewe ukawekewe dawa na kufungwa bandeji hapo begani" Daktari aliongea na kumfanya Vin awafuate kwa nyuma huku akiwa amejishika bega lake.

*******************

Kwenye ghorofa ndefu pembeni ya hospitali, kulikuwa na mwanamke mrembo akiiweka bunduki yake kwenye begi refu mfano wa begi la gitaa. Bunduki yake ilikuwa ndefu na nyuma iliandikwa M24, rifle. Ni bunduki maalum za wadunguaji zinazotumiwa sana na wanajeshi wa marekani na Israel.

Mwanamke yule baada ya kuiweka bunduki yake kwenye begi, alibeba begi na kulivaa mgongoni, akaitoa miwani yake machoni na kutoa leso kisha akafuta jasho, alikuwa ni Aisha.

"mission complete, tunaenda kupanga mission ya pili sasa" Aisha aliongea peke yake huku akitelemka kwenye ngazi ya lile ghorofa ambalo halijakamilika.

Aisha huyu ndiye aliyempiga risasi Taita na vin, Aisha alikuwa na lengo la kumtengenezea uadui Harry dhidi ya Taita. Aisha alijua kabisa kuwa Harry anataka kumuua Taita, kitu alichokuwa akikifamya Aisha ni kumfuatilia Harry kila aendapo hospitali, aliamini ipo siku Harry atatoa bastola kwa lengo la kutisha Taita, ila hakuwa na imani kama Harry anaweza kumfyatulia mtu risasi, aliijua roho ya Harry haina ujasiri, alijua roho ya Harry imejaa uoga, wasiwasi na hofu kubwa pindi inapokabiliwa na jambo zito. Ndio maana alipoona Harry amemshikia Taita, aliona hiyo ndiyo njia bora ya kumuharibia Harry. Na hata Aisha alipomlenga Taita, alijua anamlenga sehemu gani, alipiga zile sehemu ambazo alijua haziwezi kumletea matatizo ya kupoteza maisha, alipiga sehemu ambazo hazina madhara zaidi ya vidonda tu vya muda mfupi.

Baada ya tukio hilo, Aisha alitelemka mpaka chini ya ghorofa na kuingia kwenye vichochoro kadhaa na kupotelea mitaani, ndivyo alivyo binti huyu, uwa hapendi kabisa kupanda magari, uwa anaamini anapotembea kwa miguu, uwa anaona vitu vingi tofauti mtaani ambavyo humpatia elimu tofauti.

********************

Sajenti Minja aliwapitisha wagonjwa Hospital na kisha akaelekea moja kwa moja hotelini alipo Dokta Pendo, hakwenda kituo cha polisi kama alivyomuahidi babu yake Sarah,

"sasa huku ndio kituoni?" Babu yake Sarah aliuliza,

"shuka mzee, twende tukamuone Dokta Pendo, yupo hapa" Sajenti Minja aliongea huku akimfungulia mlango babu yake Sarah, mzee akashuka na kisha akaanza kumfuata Sajenti Minja ambaye alikuwa akielekea kwenye lift kwa ajili ya kupanda ghorofa za juu.

Walifika mpaka kwenye mlango wa Dokta Pendo, wakagonga hodi, Dokta Pendo akaitikia kutoka ndani, Sajenti Minja akasukuma mlango na kuingia mpaka ndani huku akiwa ameongozana na babu yake Sarah,

"wewe mzee ndio punguani kabisa, yaani wewe kumbe uliyemchongea Sarah polisi, wewe unadhani polisi ni sehemu nzuri?" Dokta Pendo alibwata mara tu baada ya kumuona babu yake Sarah, na kumfanya mzee yule apate mshangao wa kushambuliwa kwa maneno namna ile,

"acha upumbavu binti, nimekusaidia alafu unanigombeza?'" Babu yake Sarah aliuliza kwa mshangao,

"sijatekwa mimi, ningekuwa nimetekwa si ningekuwa naomba watu msaada kipindi tulipokuwa tunaenda kufanya mazoezi?" Dokta Pendo aliuliza kwa ukali,

"kijana eee, twende kituoni kama tulivyokubaliana, kunileta hapa ni kosa kisheria, ni sawa na kuniteka" Babu yake Sarah aliongea kwa kujiamini,

"Kaa hapo, hata hapa ni polisi pia" Sajenti Minja aliongea huku akimtazama babu,

"guest unapaita polisi, huoni unadhalilisha jeshi?" Babu yake Sarah aliuliza,

"mzee una wasiwasi gani wakati hapa kuna camera kila sehemu, moja, mbili, ya tatu ile pale mlangoni" Sajenti Minja aliongea huku akizihesabu camera zilizokuwa ndani ya kile chumba na kumfanya mzee atulie kidogo,

"haya, unasemaje sasa, sitaki huyu binti aingilie lakini, hapa ni mimi na wewe tu" Babu yake Sarah aliongea huku akikaa katika kiti kilichopo ndani ya chumba kile,

"sawa, je wewe na Sarah mmejuana vipi?" Sajenti Minja alimuuliza babu yake Sarah,

"yule mpumbavu tulikutana nae kwenye chumba kimoja hivi, mimi nilikuwa nimetekwa, na yeye pia alikuwa ametekwa na alipigwa usiku kucha, ilipofika kesho yake, mimi nilimuonea huruma, kwa kuwa mimi nilifungiwa ndani ya Chemba moja mule mule kwenye chumba alichofungiwa huyu mpumbavu, mimi nilikuwa na uwezo wa kutoka kwenye hiyo chemba na kurudi bila mtu yoyote kujua, sasa ndipo nilipomsaidia kwa kumfungua kamba" Babu yake Sarah aliongea,

"Alafu ikawaje?" Sajenti Minja akauliza,

"huwezi amini, baada ya kumfungua, tulikaa masaa mawili ndani ya chumba kile, kuna kijana akaingia kutuletea chakula, bwana wee, yule mwanamke alimpiga yule kijana, baada ya hapo tulitoka nje, na kila tuliyekutana nae alipigwa vibaya, tena na wengine nahisi walikufa kabisa, ndio akanipeleka kwake, na nakumbuka siku ile tunaingia kwake tu, ndio tukakutana na wewe ukitaka kuingia chumbani kwake" Babu alitoa maelezo na kumfanya Sajenti Minja aikumbuke hiyo siku,

"wewe kwanini ulitekwa?" Sajenti Minja aliuliza,

"Mimi sijui, walikuja nyumbani kwangu usiku na kuniteka mimi na mwanangu, baada ya hapo walinipiga risasi nikapoteza fahamu, nilipozinduka nilijikuta nipo sehemu hata siijui na nilikuwa na bandeji kwenye majeraha, baadae sana nikasikia na nyumba yangu ilichomwa moto na waarifu" Babu yake Sarah aliongea na kufanya Sajenti Minja akuimbuke ile kesi ya mzee kutekwa na nyumba ya huyo mzee ikachomwa moto, akakumbuka kuwa siku ya kwanza kwenda kwenye hiyo nyumba iliyoungua moto, alikutana na mwanamke ambaye walipambana nae na kisha huyo mwanamke akakimbia.

Wakati Sajenti Minja aliwaza hayo, ndio wakati huo Dokta Pendo akakumbuka kuwa ni kweli kuwa kipindi anatekwa kwa mara ya kwanza na Trigger, alipelekwa kumtibia huyo mzee, na akakumbuka kuwa Sarah alishawahi kumwambia kuwa yule mzee ni babu yake,

"wewe mzee kweli humjui huyu mwanamke aliyekusaidia kukuokoa ulipotekwa?" Dokta Pendo aliuliza kwa mshangao huku akimuangalia yule mzee,

"simjui kabisa, ningekuwa namjua si ningesema?" Babu yake Sarah aliuliza,

"wewe mzee nimekukumbuka? Na mimi hunijui?" Dokta Pendo aliuliza huku akiwa amemkazia macho babu yake Sarah,.

"sikujui" Babu yake alijibu,

"mzee unawafahamu kwa sura watu waliokuteka?" Sajenti Minja aliuliza,

"ndio, nawafahamu, yupo mwanaume mmoja katili sana, amejichora chora mwili mzima, alafu yupo mwanamke mmoja katika hilo kundi ambaye anakujaga mara moja moja, mara ya mwisho kushuhudia ni siku moja ambapo kuna binti mmoja alitekwa na kupigwa vibaya, alivunjwa miguu yote na kisha akafa, ndipo wakashauriana wakamtupe" Babu yake Sarah aliongea na kufanya Dokta Pendo ajue ni yeye ndiye aliyetekwa na kupigwa vibaya,

"mwambie mzee atupishe, kuna kitu nataka tuongee" Dokta Pendo alimwambia Sajenti Minja,

"ongea tu, unamuogopa mzee?" Sajenti Minja aliuliza,.

"mwambie aondoke, kuna kitu nataka kukuambia kuhusu Sarah" Dokta Pendo aliongea na kumfanya Sajenti Minja ashtuke,

"mzee chukua nauli, nenda nyumbani, nitakuja baadae" Sajenti Minja aliongea huku akimpatia pesa babu yake Sarah,

"huyu anamjua vizuri tu, ila anamfichia madhambi yake tu" Babu yake Sarah aliongea huku akielekea nje.

"haya niambie, ni kipi unakijua kuhusu Sarah?" Sajenti Minja aliuliza,

"huyu mzee unaemuona, ni babu yake Sarah kabisa, yaani ni baba wa baba yake na Sarah" Dokta Pendo alitoa taharifa iliyomshtua Sajenti Minja,

"sasa mbona huyu mzee haoneshi kumjua Sarah?" Sajenti Minja aliuliza,

"sikia, mara ya kwanza wakati mimi nimetekwa, nilitekwa kwa ajili ya kumtibu mtu aliyepigwa risasi, sura niliyoikuta ya huyo mtu ni hii ya huyu mzee, ila pia mara ya kwanza nakutana na Sarah, alinifuata nyumbani kwangu, alijua mimi na wale watekaji tunashirikiana kwa kuwa alimfuatilia mtekaji mmoja na akamuona akiwa na mimi, tena siku hiyo huyo mtekaji alikuwa akinitoa kumtibu huyo babu na kunirudisha hospitali. Sasa usiku ndipo Sarah alinivamia na kunieleza kila kitu kuhusu huyu mzee, aliniambia maneno mengi tu kuhusu huyu mzee na pia akisema huyu mzee ndio mtu pekee anayemthamini aliyebaki duniani. Basi mimi nilimsaidia kwa kumuingiza ndani ya ngome ya watekaji, ila hakufanikiwa kumuokoa babu yake" Dokta Pendo aliongea na kumfanya Sajenti Minja aunganishe matukio, Sajenti Minja akawaza na kugundua kuwa, kama huyu mzee ni babu yake Sarah, basi ile nyumba iliyoungua zamani ambayo ni ya mtoto wa huyo mzee, basi huyo mtoto ndiye baba yake Sarah, na huyo baba yake Sarah ndiye alimuoa dada yake Taita.

"kwa hiyo Sarah na Taita ni mtu na mjomba wake?" Sajenti Minja aliuliza huku akimuangalia Dokta Pendo na kumfanya Dokta Pendo ashangae,

"kivipi?" Dokta Pendo aliuliza huku moyoni mwake akijua fika kuwa Sarah na Taita ni mtu na adui yake.

"Sarah ana kitu cha kunieleza, kuna kitu anaficha" Sajenti Minja aliongea huku akiinuka kwenye kiti,

"Sarah na Taita? aisee unanivuruga wakati tulikuwa tunaongea vizuri" Dokta Pendo aliongea huku akiwa kweli amevurugwa baada ya kuambiwa kuwa Sarah na Taita ni ndugu,

"tangu umemjua Sarah ameshawahi kukuonesha ndugu yake mwingine tofauti na huyu mzee?" Sajenti Minja aliuliza,

"hapana, mbona hata mimi hawajui ndugu zangu?" Dokta Pendo aliuliza,

"Sarah unajua anafanya kazi gani?" Sajenti Minja aliuliza,

"ana kampuni inayosafirisha mzigo inayoingia na kutoka nchini" Dokta Pendo alijibu,

"alishawahi kukusimulia makuzi yake, au habari za wazazi wake?" Sajenti Minja aliendelea kuuliza,

"hapana, ila alisema atanisimulia akipata muda kwa maana sio hadithi ya kuvutia" Dokta Pendo alijibu,

"nitarudi baadae" Sajenti Minja aliongea huku akiondoka,

"njoo unieleweshe basi" Dokta Pendo aliongea wakati Sajenti Minja akiondoka, lakini Sajenti Minja alipuuza na kuondoka zake huku kichwa chake kikianza kupata mwanga fulani juu ya kesi anayoifuatilia...........

**********ITAENDELEA************

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA HAMSINI NA MBILI.

ENDELEA..................

Sajenti Minja aliamua kumrudia babu yake Sarah, aliona kupitia huyo mzee anaweza kupata kitu kingine cha ziada, Sajenti Minja alitelemka mpaka chini ya jengo na kuingia kwenye gari lake, akawasha na kutaka kuliondoa, ila alisikia mtu akigonga kioo cha upande wa pili, akamtupia jicho na kukuta ni yule mzee, babu yake Sarah,

"ingia ndani ya gari, nilikuwa nakufuata" Sajenti Minja aliongea huku akishusha kioo cha gari, Babu yake Sarah akafungua mlango na kuingia ndani ya gari,

"kuna nini tena? Mbona unanistua?" Babu yake Sarah aliuliza huku akirudishia mlango wa gari,

"kuna maswali nilisahau kukuuliza" Sajenti Minja aliongea huku akizima gari, aliamua amuulizie hapo hapo,

"uliza, tena hapa nitakujibu vizuri kwa kuwa kule juu yule mwanamke alikuwa anaingilia sana mahojiano" Babu yake Sarah aliongea,

"mzee uliposema kwamba ulitekwa na nyumba yako ikachomwa moto, kuna kesi kama hiyo ilitokea miaka kumi na tisa iliyopita, kuna bwana mmoja anaitwa Isack, aliteketezwa yeye na familia yake, na walikufa wote akabaki mtoto mmoja mdogo wa kike,. Je huyo mtu una uhusiano nae gani?" Sajenti Minja aliongea na kumfanya babu yake Sarah apoe kidogo, akatulia kwa sekunde kadhaa,

"huyo mtu unayemzungumzia ni mwanangu, alichomwa akiwa ndani ya nyumba, aliteketezwa yeye na familia yake" Babu yake Sarah aliongea kwa upole,

"hujawahi kufuatilia kituo cha polisi na kuhoji juu ya upelelezi wa hiyo kesi unaendelea au lah!? Au ulishakubaliana na matokeo?" Sajenti Minja aliuliza,

"kipindi cha mwanzo baada ya tukio, kulikuwa na polisi ambaye alikuwa akifuatilia na alikuwa anajitahidi sana kuniambia kila hatua anayopiga, ila kwa bahati mbaya, yule polisi nae alikufa baadae hospitali wakati akijitahidi kumlinda huyo binti wa mwanangu ambaye alikuwa amesalimika" Babu yake Sarah alijibu,

"huyo binti yupo wapi sasa hivi?" Sajenti Minja aliuliza,

"yupo uingereza, aliondoka akiwa mdogo sana na sasa hivi ni muajiriwa wa uko, nadhani hata uraia amechukua wa uko" Babu yake Sarah alijibu,

"mara ya mwisho kuwasiliana nae ilikuwa lini?" Sajenti Minja aliuliza,

"muda kidogo, kabla sijatekwa" Babu yake Sarah alijibu,

"jina lake unalikumbuka?" Sajenti Minja aliuliza,

"nitalisahau vipi wakati alipewa jina la marehemu mke wangu. Binti anaitwa Sarah, Sarah isack" Babu alijibu na kumfanya Sajenti Minja akubaliane na hisia zake, sasa Sajenti Minja alishajua kuwa Sarah mwenyewe anaezungumziwa ni huyo Sarah ambaye babu anamponda kila siku na kumuita mtekaji,

"huyo Sarah ukimuona utamjua?" Sajenti Minja aliuliza,

"hapana, ni muda sana sijamuona, miaka kumi na tisa ni mingi sana" Babu yake Sarah alijibu na kufanya Sajenti Minja ajiulize kwanini Sarah anamficha ukweli babu yake?,

"na Taita Unamjua?" Sajenti Minja aliuliza,

"namjua vizuri, mwanangu ambaye ni baba yake Sarah alimuoa mdogo wake Taita" Babu yake Sarah alijibu,

"je, kulikuwa na ugomvi wowote kati ya Taita na Dada yake?" Sajenti Minja aliuliza swali lililomfanya babu ashangae,

"Mimi nitajuaje sasa? Hayo ni mambo yao" Babu yake Sarah alijibu kwa mshangao,

"sawa mzee, nashukuru kwa majibu yako" Sajenti Minja aliongea,

"sasa nipeleke basi nyumbani" Babu yake Sarah aliongea,

"nyumba yako si imeungua mzee?" Sajenti Minja aliuliza kwa hamaki,

"kwa yule mtekaji ndio nyumbani, maana sina sehemu nyingine" Babu yake Sarah aliongea na kumfanya Sajenti Minja acheke,

"wewe mzee ni mtu wa ajabu sana, yaani mtu anakuifadhi lakini bado unamchongea polisi?" Sajenti Minja aliuliza huku akiwa bado anacheka,

"sasa unataka nifiche maovu?" Babu yake Sarah aliuliza,

"endelea kufichua, ila kuwa muangalifu" Sajenti Minja aliongea huku akiindoa gari yake na kuiingiza barabarani.

**********************

Vin alikuwa pembeni ya kitanda cha baba yake, hali ya baba yake haikuwa mbaya kwa maana Aisha alipiga sehemu ambazo hazina madhara sana.

"mzee samahani, ningependa unipe habari za Sarah, maana haiwezekani Harry amuogope kiasi hicho mpaka atake kukuua" Vin aliongea huku akimtazama Taita,

"unataka kujua ukweli kuhusu Sarah?" Taita aliuliza huku akitabasamu,

"ndio, atakuwa ana sababu ya kufanya hivyo, sio mwendawazimu yule kiasi kwamba atake kuua watu hovyo" Vin aliongea kwa kujiamini,

"Sarah ni mtu anayenituhumu kuwa nimemuulia wazazi wake, sasa anataka kulipa kisasi" Taita aliongea na kumfanya Vin ashangae,

"ni kweli uliua wazazi wake?" Vin aliuliza,

"hapana, hata mimi sijui ni kitu gani kiliwaua, ila mama yake ni ndugu yangu, alikuwa ni mtoto wa baba yangu mdogo" Taita aliongea na kumzidishia maswali Vin,

"sasa si bora ufanye mpango wa kumfikisha mahakamani?" Vin aliuliza,

"mahakamani? Haiwezekani, ukae ukijua kuwa mama yako aliuliwa na Sarah, hicho ndicho kinachofanya nishindwe kumpeleka mahakamani, nataka na mimi nilipe kisasi" Taita aliamua kumdanganya Vin ili amtie hasira, na kweli Vin alipata hasira baada ya kusikia kuwa mama yake aliuliwa na Sarah,

"sasa kama ni hivyo, basi naomba hiyo kazi ya kumuua Sarah niifanye mimi" Vin aliongea kwa hasira huku akiwa amekunja ngumi, Taita akageukia upande wa pili na kucheka, aliamini kuwa ameshaanza kumjaza chuki dhidi ya dada yake,

"ukifanya hivyo, hakika hata nikifa, nitakufa kifo cha amani, nilikuwa nampenda sana mke wangu" Taita aliongea kwa huzuni na kufanya Vin azidi kupata uchungu, na kipindi hicho Trigger alikuwa akiingia ndani ya wodi,

"salama hapa?" Trigger aliuliza huku akiwatizama kwa zamu,

"uzima haupo, mwenzako amefanya kitu cha ajabu sana, amenipiga risasi mbili na kisha akampiga Vin risasi moja ya bega" Taita alijibu kwa ukali,

"nani aliyefanya hivyo!?" Trigger aliuliza huku akishangaa,

"Harry, namuhitaji Harry, fanya kila uwezacho kumleta Harry hapa, nahitaji akiwa mzima ili nimuue mwenyewe" Taita aliongea kwa hasira na kumfanya Trigger ashangae zaidi, hakuamini anachokisikia,

"Harry huyu huyu?" Trigger aliuliza kwa mshangao

"fanya nilichokugiza, maswali tutaulizana ukishamleta" Taita aliongea na kufanya Trigger atii amri, Trigger akapiga hatua za kuanza kuondoka, ila ghafla akageuka,

"umesema nimlete hapa? Utamuua hapa hapa?" Trigger aliuliza huku akimuangalia Taita,

"Trigger umri umeenda ujue, acha bangi mdogo wangu, sasa hapa nitamuuaje? Mpeleke kule kambini" Taita aliongea na kumfanya Trigger aondoke zake huku akitabasamu,

"Harry umenyea shuka kipindi cha baridi" Trigger aliongea peke yake huku akitabasamu na pia akitingisha kichwa chake kwa masikitiko.

********************

Sarah alivyotoka kazini, aliamua kupitia katika hotel aliyokuwepo Dokta Pendo, aliingia moja kwa moja mpaka chumbani na kumkuta Dokta Pendo akiwa ameinamia kitandani akiwa na mawazo sana,

"shoga vipi, unamuwaza nani?" Sarah alimuuliza huku akitabasamu, Dokta Pendo akainua kichwa chake na kumkuta Sarah akimuangalia,

"umeingia muda gani?" Dokta Pendo aliuliza huku akijilazimisha kutabasamu,

"sasa hivi tu, vipi umekula?" Sarah aliuliza,

"tayari, nasikia umewapiga polisi asubuhi, Minja alikuwa anakutafuta" Dokta Pendo aliongea kwa utulivu,

"nitaenda kujisalimisha baadae, sasa wangenikamata si ningeshindwa kusaini mikataba, alafu ningeonekana mswahili" Sarah alijitetea,

"umekula lakini?" Dokta Pendo aliuliza,

"bado, nikifika nyumbani nitapika" Sarah alijibu,

"hivi shoga, kumbe Taita ni mjomba wako?" Dokta Pendo aliuliza swali la ghafla lililomstua Sarah,

"nani amekuambia?" Sarah aliuliza kwa mshtuko,

"Minja, Minja alikuja na babu yako, alikuwa akimuhoji na mwisho wa mahojiano tukagundua yule mzee ni babu yako, na pia Taita ni mjomba wako, je ni kweli?" Dokta Pendo aliuliza, ila Sarah hakujibu na badala yake aliinamisha tu kichwa chini bila kujibu,

"na yule mzee amenijua mimi ni nani?" Sarah alimuuliza Dokta Pendo,

"hapana, mzee hajakujua bado" Dokta Pendo aliuliza,

"nadhani wakati umefika, nahitajika kuvua gamba na kubaki na ngozi yangu halisi" Sarah aliongea kwa sauti ya chini ila iliyomfikia vyema Dokta Pendo,

"unamaanisha nini!?" Dokta Pendo aliuliza na kumfanya Sarah ashtuke, maana hakutegemea kama sauti yake ingemfikia Dokta Pendo,

"tunaweza kwenda nyumbani mara moja?" Sarah aliuliza,

"kufanya nini?" Dokta Pendo aliuliza,

"nahitaji kujitambulisha mbele yako na yule mzee, sihitaji kujificha tena" Sarah aliongea kwa sauti tulivu,

"sawa, twende" Dokta Pendo aliongea baada ya yeye mwenyewe kupata shahuku ya kutaka kumjua vizuri Sarah.

Sarah akamsaidia Dokta Pendo na kutelemka nae mpaka chini na wakaingia ndani ya gari, Sarah akawasha gari yake na safari ya kuelekea kwake ikaanza.

Baada ya muda mfupi waliweza kufika nyumbani kwa Sarah, Sarah akatelemka na kufungua geti, kisha akarudi kwenye gari na kuliingiza ndani ya geti, akarudi na kurudishia geti, kisha akamshusha Dokta Pendo na kumuingiza ndani, walimkuta mzee akiwa amekaa sebuleni kifua wazi akitazama runinga, Sarah akamkalisha Dokta Pendo kwenye kiti, kisha yeye akaelekea chumbani kwake, hawakumsemesha kabisa mzee.

Mzee akanyanyuka taratibu na kuelekea nje, alivyofika nje ya geti, mzee akatoa simu na kupiga, alikuwa anawapigia polisi, tena hakupanga kabisa kumpigia Sajenti Minja, aliona hawezi kumkamata Sarah.

Baada ya kumaliza kupiga simu polisi na kuwafahamisha kuwa Sarah yupo pale muda huo, mzee alirudi ndani na kujitupa juu ya kochi bila kumsemesha neno lolote Dokta Pendo.

Baada ya muda Sarah alirudi sebuleni akitokea chumbani, mkononi alikuwa na picha chache za zamani. Sarah akajitupa juu ya kochi na kumsalimia babu yake, kisha akamtupia zile picha mbele yake juu ya meza, mzee akamuangalia Sarah,

"chukua hizo picha uziangalie, labda kuna mtu unaweza kumfahamu" Sarah aliongea huku akimuangalia babu yake, mzee akaokota zile picha na kuanza kuziangalia, akawa anastuka kila anapoangalia picha moja, aliziangalia zote mpaka akazimaliza,

""hizi picha umezitoa wapi?" Babu yake Sarah aliuliza,

"ni za kwangu, na hiyo ndiyo familia yangu, yaani baba yangu, mama yangu na mdogo wangu" Sarah aliongea na kumfanya mzee ashtuke zaidi,

"wewe binti wewe?" Babu yake aliongea huku akitetemeka,

"naitwa Sarah, Sarah Isack" Sarah aliongea na kujitambulisha rasmi kwa babu yake, babu yake akapigwa na bumbuwazi, akainuka kama mshale na kwenda sehemu alipokaa Sarah, akaushika mkono wa Sarah na kugeuza kwa nyuma, akaangalia kwa sekunde kadhaa kisha akamkumbatia Sarah,

"ni kweli, wewe ni Sarah mjukuu wangu, kwa nini ulikaa kimya muda wote huo? Umesababisha nakuchukulia kama muharifu" Babu yake Sarah aliongea kwa huzuni huku akiwa bado amemkumbata Sarah na kipindi hicho akiwa anajiuliza ni kipi babu yake alichokiangalia nyuma ya mkono,

"mzee mbona umemuangalia nyuma ya mkono, kuna nini?!" Dokta Pendo aliuliza,

"kwenye ukoo wetu uwa tunawapaka dawa za asili ambazo uwa zinakuwa kama doa jeusi juu ya kiwiko, wa kwanza anawekwa doa moja na wa pili anawekwa madoa mawili, yaani madoa yanawekwa kwa idadi" Babu yake Sarah aliongea na kumfanya Sarah agundue hicho kitu, maana hilo doa alikuwa analionaga ila alijua limetokea lenyewe tu.

"sasa babu kuna kitu nataka nikuambie, familia yangu haikuungua kwa bahati mbaya, ni Taita ndiye aliyechoma moto nyumba yetu huku baba na mama wakiwa wamefungwa kamba, mimi na sebastian(vin) tulitolewa nje ila baadae nilirudidhwa ndani na kuachwa kisha moto ukawashwa, Sebastian aliondoka na taita. Na mimi nilipona kwenye moto kwa sababu mfanyakazi wa ndani aliniokoa ila yeye alikufa" Sarah aliongea huku akilia na kipindi hicho sasa babu yake na dokta Pendo wakabaki midomo wazi baada ya kusikia kuwa muhusika mkuu ni Taita, na hapo Dokta Pendo ndiye akaelewa ni kwanini Sarah anadili na Taita tu.

"kumbe Taita ndiye muuaji?" Babu yake Sarah aliuliza,

"ila hili jambo msimwambie mtu yoyote, nataka kulimaliza mwenyewe" Sarah aliongea na kumfanya babu yake ashangae,

"na hata ulivyotekwa na kuchomewa nyumba yako, walikuwa wakinitafuta mimi, walidhani wakikuteka wewe, basi watanipata kwa urahisi" Sarah aliongea huku akiwa anatoka machozi na kipindi hicho polisi zaidi ya hamsini walikuwa wameizunguka nyumba ya Sarah baada ya kuarifiwa na babu yake Sarah.

"wote mliopo ndani tunaomba mjisalimishe, msipofanya hivyo itatubidi tutumie nguvu kubwa kuwashurutisha" Sauti ya tangazo kutoka nje ilisikika, walikuwa ni polisi. Sarah akanyanyuka haraka na kuchungulia dirishani na kuona askari kibao, akikimbilia upande wa nyuma napo akakuta askari wengi wakiwa wameizunguka nyumba, Sarah akarudi sebuleni na kujitupa kwenye kochi, alikuwa amekata tamaa, hakuwa na uwezo wa kupambana na askari zaidi ya hamsini. Kipindi hicho babu machozi yalikuwa yakimtoka na kujiona ana hatia,

"ni kosa langu, mimi ndiye niliyeita polisi" Babu yake Sarah aliongea huku akilia na kujilaumu mwenyewe, na wakati huo polisi wapatao kumi wakiwa na silaha mkononi walikuwa wameshavuka geti na walikuwa wakiuendea mlango wa kuingilia sebuleni kwa sarah, sura zao zilionesha kuwa na hasira nyingi sana juu ya mtu wanayemtafuta kwa maana alihaibisha jeshi la polisi kwa kuwapiga na kuwajeruhi askari wenzao kadhaa nyakati za asubuhi..............

**********ITAENDELEA***********

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom