Riwaya: Sala ya Sarah

Riwaya: Sala ya Sarah

RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA THELATHINI.

ILIPOISHIA..............

Muda wa saa tano usiku, Sarah akiwa amevaa kikazi aliegesha gari yake, kisha akashuka na kutembea mwendo wa dakika ishirini na kuingia kwenye jengo moja la ghorofa ambalo halijakamilika.

Alipanda mpaka juu ya ghorofa na kumkuta Trigger akiwa ameshika begi jeusi kubwa,

"naona umekuwa sasa" Trigger aliongea huku akimuangalia Sarah,

"nimefuata pesa, sihitaji habari nyingine" Sarah aliongea huku akiwa amesimama,

"chukua hizi hapa" Trigger aliongea na kumtupia Sarah lile begi, Sarah akalidaka na kuanza kuondoka. Wakati akiwa amepiga hatua tatu, mbele yake waliibuka vijana kama ishirini wote wakiwa na bastola, alipogeuka nyuma akakuta vijana wengine wengi wakiwa wamesimama na Trigger na wote wana bastola,

"wewe unadhani mjanja nani kati yetu na wewe?" Trigger aliuliza huku akiijaza bastola yake risasi............

**********ENDELEA************

"unafikiri unaweza kunifanya chochote?, jitathimini mtumwa mkubwa wa fikra wewe" Sarah aliongea huku akimtazama Trigger,

"mwachieni njia aondoke" Trigger aliongea huku akitabasamu kwa dharau, vijana wakaacha njia Sarah akapiga hatua tano mbele, kisha akamgeukia Trigger na kuichomoa bastola yake,

"nasikia unaweza kuchezea sana silaha, ipo siku nitakufundisha namna nzuri ya kucheza nazo" Sarah aliongea huku akiirusha rusha bastola yake na kipindi hicho Trigger alikuwa anatabasamu tu.

Sarah akageuza shingo yake na kuondoka, akakatiza pale pale katikati ya vijana wa Taita na kutelemka mpaka chini ya ghorofa.

"tumfuatilie?" Tekso alimuuliza Trigger,

"hapana, kufanya hivyo ni sawa na kumuua Taita" Trigger alijibu,

"si tutamfuatilia bila yeye kujua" Tekso aliongea,

"sio mjinga huyo, atakuwa ameweka mitego yake ili kujua tutafanyaje baada ya yeye kuondoka? Huoni hata alivyokuwa akijiamini?" Trigger aliuliza na kufanya wenzake wakubaliane nae.

"kwa hiyo tutegemee boss ataachiwa lini?" Strategic aliuliza,

"nadhani ni leo au kesho, lakini bado sina uhakika sana kwa sababu mwenye mamlaka ya kufanya hivyo ni Sarah mwenyewe" Trigger alizungumza,

"lakini hela si tumempa? Kwanini asimuachie sasa?" kijana mwingine aliuliza kwa jazba,

"hela ni nini kwani? Hapa tunazungumzia mamlaka na wala sio pesa" Trigger aliongea huku akimuangalia yule kijana,

"ila naamini hawezi kumdhuru" Tekso aliongea,

"kumdhuru kwa kweli hawezi, kwa sababu babu yake tunaye, ila bila hivyo huenda hata Taita angekuwa marehemu muda huu" Trigger alijibu huku akielekea kwenye ngazi za kushukia kwenye lile ghorofa ambalo halijakamilika na wenzake wakamfuata kwa nyuma.

"kwa hiyo sisi tunatakiwa tufanye nini kwa muda huu?" Tekso aliuliza,

"kukaa na kusubiri" Trigger alijibu huku akiwasha sigara yake.

****************

.
.

Sarah alipochukua pesa wala hakutaka kuhakikisha kama zipo sawa, alibeba begi akaondoka zake, hakwenda moja kwa moja kwenye gari lake, alichofanya aliingia katika kichochoro kimoja na kuangalia ni kipi vijana wa Taita watafanya?

Baada ya dakika kumi za Sarah kubana pale kichochoroni, aliweza kuwaona vijana wa Taita wakitoka ndani ya lile jengo bovu, akawashuhudia wakiingia kwenye gari na kuondoka, Sarah akaendelea kubana kwa dakika kumi nyingine huku akitazama usalama wake, alipojiridhisha yupo salama, alitoka kichochoroni huku akiwa na begi lake lililojaa pesa. Akatembea kwa mwendo wa nusu saa na kuikuta gari yake, akapanda na kutulia kwa dakika kumi nyingine kwa lengo lile lile la kuangalia usalama.

Alipoona pako sawa, akawasha gari yake na kuiondoa kwa mwendo wa taratibu, njiani alikuwa makini kuangalia vioo vya pembeni vya gari ili kuona kama kuna gari inamfuata, lakini hakufanikiwa kuona kitu.

Sarah aliingia kwake saa za usiku sana, alipofika aliingiza gari yake kwenye uzio wa nyumba yake, na kisha akaingia ndani, akapitiliza moja kwa moja chumbani na kutupia kitandani lile begi lililokuwa limejaa pesa, kisha akavua nguo zake za kazi na kujitupa kitandani, alipanga Kulala tu muda huo, mambo mengine alipanga kuyafanya siku inayofuata.

****************

Asubuhi ya leo Sajenti Minja aliamka na wazo la kwenda ofisini kwa Taita, maana yake siku iliyopita alimpigia sana simu Taita kwa namba aliyopewa kule Vin hotel, lakini simu ya Taita haikuwa ikipatikana.

Sajenti Minja aliamka na kujifanyia maandalizi ya mwili, kisha akaondoka zake mpaka kwenye jengo moja kubwa katikati ya mji lililokuwa na jina Dennis tower, kumbuka jina halisi la Taita ni Dennis, hilo Taita alipewa kutokana na pesa alizokuwa nazo.

Sajenti Minja aliegesha gari yake nje na kisha akaingia ndani ya lile jengo, akaelekea sehemu ya mapokezi na kueleza shida yake, akaambiwa apande mpaka ghorofa ya kumi na mbili ndipo zilipo ofisi za mkurugenzi wao, Sajenti Minja akapanda lift mpaka ghorofa ya kumi na mbili na kisha akaanza kusoma vibao vya juu vya kila ofisi, mpaka alipofika kwenye kibao kilichoandikwa "PRESIDENT" akatabasamu na kugonga mlango, mtu aliyekuwepo ndani akaitikia, Sajenti Minja akaingia ndani na kumkuta mtu wa makamo akiwa amekaa juu ya kiti ambacho mbele kulikuwa na meza, huyo mtu hakuwa Taita, maana Sajenti Minja anamfahamu vizuri Taita ingawa hawana na ukaribu. Sasa huyu aliyekuwepo mbele yake ni Harry, alikuwa yupo bize na computer,

"karibu ukae" Harry aliongea huku akiendelea kubofya,

"asante, nina shida na Taita, sasa sijui nimemkuta?" Sajenti Minja aliuliza,

"huo sio utaratibu kijana, utaratibu ni kujitambulisha kwanza, alafu ndio unasema shida yako" Harry aliongea huku akijitahidi kuonesha tabasamu,

"naitwa Joel Minja, ni askari kutoka kituo kikubwa cha polisi, nina shida na Taita" Sajenti Minja aliongea,

"shida ya kiofisi au binafsi? Kama shida ni ya kiofisi hata mimi naweza kukusaidia" Harry aliongea huku akapata uoga baada ya kujua huyo kijana anayeongea nae ni polisi,

"ni shida binafsi" Sajenti Minja aliongea na kufanya Harry wasiwasi umuongezeke zaidi,

"kama ni shida binafsi huyu bwana hayupo, amesafiri ameenda nje ya nchi" Harry alijibu kwa utulivu,

"atarudi lini?" Sajenti Minja aliuliza,

"kwa kweli hakuna anaejua, kwa sababu huyu bwana uwa hasemi siku atayorudi" Harry alijibu,
.

"sawa, nashukuru kiongozi, nadhani nitarudi tena siku nyingine" Sajenti Minja aliongea huku akinyanyuka kwenye kiti,

"sawa, karibu tena" Harry aliongea huku akimpa mkono Sajenti Minja, kisha Sajenti Minja akaondoka zake huku akiwa na imani kuwa ni kweli Taita amesafiri, kumbe yupo tu nchini ila ametekwa.

Hata baada ya Sajenti Minja kuondoka bado Harry hakuwa na amani kabisa, muda wote alikuwa anajutia maisha yake ambaye aliishi nyuma, alikuwa anaumiza kichwa sana ili aweze kujinasua kwenye kundi la Taita, lakini alishindwa kutokana vitisho alivyopewa na Taita, maana aliambiwa yoyote atakayeisaliti vita wanayoshindana na Sarah, ni lazima afe.

Baada ya muda mrefu wa kutafakari, Harry aliamua ni bora wote wafe, yaani Sarah na Taita, na aliona kwa kuwa Taita ametekwa muda huu na hajulikani alipo, ni bora aanze na Sarah.

Akaichukua simu yake na kupiga namba anayoijua,

"hey Aisha, habari yako?" Harry aliongea baada ya simu kupokelewa,

"poa, naongea na nani?" Aisha alijibu upande wa pili,

"ina maana namba yangu ulifuta?" Harry aliuliza,

"kuulizana ulizana ni kupoteza muda, sema wewe ni nani?" Aisha aliuliza huku akionekana hajapenda maswali,

"Mimi Harry, mwanasheria" Harry alijitambulisha,

"ooh kumbe wewe, leo umenikumbuka boss?" Aisha aliuliza huku akicheka,

"kuna mission nataka nikupe, upo wapi?" Harry aliuliza,

"nipo mjini, Wewe upo wapi?" Aisha aliuliza,

"nipo mjini, kama inawezekana tuonane muda huu?" Harry aliongea,

"njoo nipo hapa Rock restaurant, uje boss wangu" Aisha aliongea,

"poa, nakuja" Harry aliongea na kukata simu, kisha akainuka na kuelekea kwenye gari lake.

Aisha ni msichana ambaye historia yake hajulikani, ila walikutana na Harry katika mambo yao ya kazi haramu, huyu Aisha alikuwa ni mtu anaetumwa kufanya kazi za kuua, hukodiwa na watu tofauti wa mataifa mbalimbali kwa ajili ya kazi hiyo.

Harry alifika rock restaurant na kuangaza angaza akaweza kumuona Aisha Akiwa amekaa, akamfuata kisha wakakumbatiana kwa furaha,

"unakunywa nini?" Aisha aliuliza,

"maziwa fresh" Harry alijibu kisha Aisha akaenda kumuagizia na kurudi,

"najua umeniitia kazi, haya niambie" Aisha aliongea huku akitabasamu,

"Kuna mwanamke ananinyima raha, nataka ummalize" Harry aliongea,

"demu wako nini?" Aisha aliuliza huku akicheka,

"hapana, we fanya kazi tu, hupaswi kujua kingine" Harry alijibu,

"million hamsini ipo?" Aisha aliuliza,

"pesa sio kitu, mimi nataka furaha tu" Harry alijibu

"una picha yake?" Aisha aliuliza, Harry akatoa simu na kumuonesha picha ya Sarah,

"mrembo kabisa huyu, anapatikana wapi?" Aisha aliuliza,

"huo ndio mtihani, utatumia mbinu unazozijua wewe kumpata, kwa mimi sijui anapokaa" Harry alijibu,

"dah, poa, tanguliza malipo ya hawali, million thelathini, alafu nyingine utamalizia baada ya kazi " Aisha aliongea,

"Mimi nakupa pesa yote, sitaki kutoa nusu nusu" Harry aliongea,

"sawa boss, nitakutumia namba ya account yangu kwenye simu yako, Wewe unachotakiwa ufanye ni kunirushia hiyo picha ya huyo dada" Aisha aliongea,

"poa, tutawasiliana" Harry aliongea kisha akanyanyuka na kuondoka zake.

****************

Mishale ya mchana Aisha akiwa kwenye duka la silaha aliweza kumuona msichana akiingia hapo, alimpomtazama hakuwa mgeni kwake, ndipo alipotoa simu yake na kuiangalia, alikuwa ni Sarah, Aisha akatabasamu.

Sarah alielekea moja kwa moja kwa muuzaji na kumsabahi, kisha akaingiza mkono mfukoni na kutoka na risasi,

"risasi ya namna hii naweza kuipata hapa?" Sarah aliuliza,

"hiyo hamna dada yangu, hazipatikani kabisa" muuzaji alijibu kisha Sarah akaondoka zake, Aisha akaanza kumfuatilia kwa nyuma.

Sarah alipotoka hapo alielekea kwenye mgahawa wa jirani na hapo, akaagiza chakula na kula taratibu.

Muda huo Aisha nae aliingia ndani ya mgahawa huo na kuagiza juisi.

Sarah alipomaliza kula, akanyanyuka na kuelekea chooni, Aisha nae akamfuata.

Sarah akiwa chooni anajiangalia kwenye kioo, alishangaa mtu akisimama nyuma yake na kutabasamu, Sarah akageuka haraka na kumuangalia,

"hujambo mrembo?" Aisha aliongea huku akimsogelea Sarah, tena usogeleaji wa kishari. Sarah akaona bora aondoke, wakati akapiga hatua ili aondoke alikamatwa shingo na Aisha, Sarah akarusha ngumi ikadakwa kisha akapigwa pingu ya mkono mmoja, aliporusha ngumi ya pili ikadakwa na kuunganishwa katika pingu na mkono wa hawali, Sarah akakosa ujanja.

Alipojaribu kurusha teke, Aisha alimdhibiti kwa kumbana ukutani na kisha akatoa kisu chake mfukoni,

"wewe ndio unasumbua mabosi mjini?" Aisha aliuliza huku akitabasamu kisha kisu akakiweka shingoni kwa Sarah, akaanza kukikandamiza taratibu na damu ikaanza kumchuruzika Sarah, Sarah machozi yakaanza kumtoka na kuona ndoto yake ya kulipa kisasi ikimalizwa chooni, tena na mwanamke mwenzake ambaye hata hamjui.................

*********ITAENDELEA************

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA.

ILIPOISHIA......................

Sarah akiwa chooni anajiangalia kwenye kioo, alishangaa mtu akisimama nyuma yake na kutabasamu, Sarah akageuka haraka na kumuangalia,

"hujambo mrembo?" Aisha aliongea huku akimsogelea Sarah, tena usogeleaji wa kishari. Sarah akaona bora aondoke, wakati akapiga hatua ili aondoke alikamatwa shingo na Aisha, Sarah akarusha ngumi ikadakwa kisha akapigwa pingu ya mkono mmoja, aliporusha ngumi ya pili ikadakwa na kuunganishwa katika pingu na mkono wa hawali, Sarah akakosa ujanja.

Alipojaribu kurusha teke, Aisha alimdhibiti kwa kumbana ukutani na kisha akatoa kisu chake mfukoni,

"wewe ndio unasumbua mabosi mjini?" Aisha aliuliza huku akitabasamu kisha kisu akakiweka shingoni kwa Sarah, akaanza kukikandamiza taratibu na damu ikaanza kumchuruzika Sarah, Sarah machozi yakaanza kumtoka na kuona ndoto yake ya kulipa kisasi ikimalizwa chooni, tena na mwanamke mwenzake ambaye hata hamjui.................

************ENDELEA************

Ila kile kisu hakikuingia sana shingoni mwa Sarah, kiliingia kidogo na ndio maana kikasababisha ile damu shingoni mwa Sarah.

Aisha akakitoa kile kisu shingoni kwa Sarah na kisha akamuachia Sarah miguu yake, Aisha akaelekea moja kwa moja sehemu ambapo ziliwekwa toilet paper, akakata kipande kidogo na kisha akafutia damu iliyokuwepo kwenye kisu chake.

Muda wote Sarah alijitahidi kujishika shingoni na Mikono yake ingawa alifungwa pingu.

"bahati yako bado sijalipwa pesa yangu, maana siuagi mtu bila kukamilishiwa madai yangu ya hawali" Aisha aliongea huku akimfuata Sarah, alipomfikia alifungua pingu alizomfunga na kuziweka mahali pake, Aisha akawa anapiga hatua ili aondoke, Sarah akamuwahi na kumrushia teke, Aisha akamkwepa, Sarah akaona Kama amedharauliwa vile kwa kufanyiwa udhalilishaji ule na Aisha.

Sarah akarusha ngumi, Aisha akaikwepa tena na kufanya mkono wa Sarah uangukie mgongoni kwake, alichokifanya Aisha ni kukimata kichwa cha Sarah na kukibamiza kwenye kioo cha pale chooni, mpaka kile kioo kikapasuka,

"hao wapuuzi wanavyokusifia nilidhani labda unajua sana kupambana, kumbe fala tu" Aisha aliongea huku akijipangusa mikono yake kisha akawa anatoka zake kuelekea nje.

Sarah akajibandua pale kwenye kioo na kuona damu kidogo ikimchuruzika kwenye kichwa juu ya sikio, akatoa kitambaa chake na kujifuta, kisha nae akatoka nje, ndipo alipomshuhudia kwa mbali Aisha akiondoka kwa mwendo wa madaha huku baadhi ya wanaume wakwale wakimtupia jicho la matamanio kutokana na umbo lake la kike kumvaa vyema, Sarah akajikuta anawachukia wale wanaume bila ya sababu ya msingi,

"wangejua kuwa lile lijanamke ni likatili wala wasingethubu kuliangalia kwa matamanio hivyo" Sarah aliongea peke yake na kumalizia na sonyo la chini chini.

Sarah nae akaamua aelekee nje ili kumuwahi Aisha ili amfuatilie anapoelekea. Sarah akatembea kwa mwendo wa haraka mpaka nje ya mgahawa, akatupa jicho kushoto hakumuona Aisha, akatupa jicho kulia pia hakuona mtu, akasimama kwa muda huku akijilaumu kwa kuchelewa kutoka nje, mwisho nae akaamua aondoke zake, akaelekea sehemu alipoegesha gari lake, uwa anaegesha mbali sana na eneo ambalo huenda.

Sarah alivyopotea eneo lile ndio muda ambao aliibuka Aisha baada ya kujificha katika kichochoro kimoja eneo lile, Aisha uwa hatumiii gari pindi anapokuwa mjini, uwa anatumia njia za mkato sana, ni mwanamke ambaye amezoea sana maisha ya uswahilini na hata tabia zake ni za kiswahili tu.

Aisha alipotoka mafichoni, aliangalia uelekeo alioelekea Sarah kisha akatabasamu huku akitikisa kichwa, alafu mdogo mdogo akaingia zake kichochoni na safari ya kwenda anapopajua yeye ikaanza.

*****************

Sarah alipofika kwenye gari yake aliingia na kufungua eneo la mbele na kutoa dawa, akachukua pamba na kuanza kuipaka kwenye eneo la shingoni na kichwani juu ya sikio ambalo alijeruhiwa na Aisha.

Sarah alipomaliza kujipa huduma ya kwanza, aliwasha gari lake na kuondoka, alikuwa anarudi kwake,

"yule mwanamke ni nani?, alafu ametumwa na nani?" Sarah alijiuliza wakati akiendesha gari yake,

"hii vita inaanza kuwa nzito, maana wanaingizwa wapambanaji, tena wenye uwezo mkubwa" Sarah aliongea huku akimfikiria Aisha namna alivyomdhibiti kiurahisi.

Sarah aliingia nyumbani kwake huku akiwa na hasira, alipofika sebuleni hakutaka hata kupoteza muda, alivua viatu tu na kisha moja kwa moja na kuelekea kwenye chumba cha siri, huku mkononi akiwa amebeba chakula kwa ajili ya mjomba wake, bwana Taita.

Alifika ndani ya chumba na kuwasha taa, Taita alikuwa amelala sakafuni huku akiwa bado amefungwa kamba,

"Sarah hivi si uniachie tu, umetaka hela nimekupa, lakini huniachii, kwanini?" Taita aliuliza kwa upole,

"hela yako naweza kukurudishia, tatizo sio hela, suala la kukuachia ni mimi mwenyewe nikiamua na wala sio pesa yako" Sarah alijibu huku akimfungua Taita ili ale chakula alichomletea,

"basi kama tatizo sio pesa, niache nikafanye shughuli zangu, biashara zangu zinakwama uraiani" Taita aliongea kwa kulalamika,

"ngoja nikuulize kitu, hivi Katika kambi yenu kuna mwanamke hata mmoja?" Sarah alimuuliza Taita,

"mwanamke????? Hapana" Taita alijibu huku akifakamia chakula,

"kuna mwanamke alinivamia leo na kudai ametumwa, sasa ametekwa wapi huyo mwanamke?" Sarah alimuuliza Taita,

"Mimi sijui kwa kweli, kwani wewe unapambana na maadui wangapi?" Taita aliuliza,

"sina adui mimi" Sarah alijibu,

"sasa kama huna adui si uniachie" Taita aliongea,

"nitakuachia, ila siku ninayokuachia itabidi na babu yangu na mwanae wawe huru" Sarah aliongea,

"mbona baba mdogo alishaachiwa, ila babu yako ndio bado" Taita aliongea kwa kujiamini,

"sawa kama mmemuachia, ila mimi shida yangu ni babu" Sarah aliongea,

"nipe simu niwaambie wamuachie" Taita aliongea,

"hupaswi kuwa na haraka, hii shughuli ina utaratibu wake" Sarah aliongea huku akisimama,

"mama mbona unaondoka? Ina maana ndio na leo huniachii?" Taita alilalamika wakati Sarah akitoka, ila leo hakutaka kumfunga Taita Mikono, alimuacha huru tu.

Sarah akaenda sebuleni na kumpigia simu Harry,

"Sarah naongea" Sarah alijitambulisha baada ya Harry kupokea,

"nakusikilza" Harry alijibu huku akipata hofu,

"kesho kutwa naomba tuonane, kuna kitu nataka unisaidie" Sarah aliongea na kufanya Harry ajiulize ni kweli Sarah anahitaji msaada au mtego,

"sawa, tutaonana wapi?" Harry aliuliza,

"sema wewe, nitakuja popote kwa kuwa nina shida" Sarah aliongea kwa utulivu,

"ok, tutakutana Vin hotel, saa mbili usiku" Harry aliongea,

"na iwe hivyo, usiniangushe mwanasheria" Sarah aliongea,

"usijali" Harry aliongea kisha Sarah akakata simu, akatabasamu,

"wewe si ni mwanasheria? Utanisaidia kesi yangu sasa" Sarah aliongea peke yake kisha akatupa simu mezani.

*******************

Siku nyingine tena, Aisha alikutana na Harry katika mgahawa ule ule waliokutana hawali,

"nilikutana na msichana wako, nimemjaribu kabisa, ni mwepesi mno, basi tu sikutaka kumuua" Aisha aliongea huku akitabasamu,

"Sarah??" Harry aliuliza,

"ndio huyo huyo, hana lolote mpaka nikahisi pesa yako naila bure tu, maana hata kupambana hawezi" Aisha aliongea kwa dharau,

"huyo atakuwa sio yeye, ulipambana na mwingine" Harry aliongea huku akiwa haamini,

"kama huamini sawa, ngoja muda ufike tu" Aisha aliongea,

"sasa kwanini hujamuua?" Harry aliuliza,

"uwa siui mpaka malipo yakamilike" Aisha alijibu,

"ungeua tu, au hatuaminiani?" Harry aliuliza,

"kazi haramu hazihitaji kuaminiana" Aisha alijibu,

"sawa, ila sasa tayari nimeshakamilisha malipo yako, na kama utaweza leo usiku anza kazi, nitakutana mahala na Sarah, anadai anataka tuongee" Harry aliongea,

"haina shida, kwa kuwa malipo umekamilisha leo, basi na kazi itaisha leo" Aisha aliongea kwa kujiamini,

"basi sawa, saa mbili usiku nitakuwa nae Vin hotel, uje pale" Harry aliongea,

"nitakuja ila hatutaonana, nitaweka mitego yangu" Aisha aliongea,

"poa, basi baadae, acha niwahi kazini" Harry aliongea huku akisimama na Kuondoka zake, akamuacha Aisha akiendelea kupata juisi.

**************

Mishale ya saa mbili usiku, Sarah akiwa amevaa suruali nyeusi na koti la suti lenye rangi ya njano isiyokoa, alikuwa akiingia pale Vin hotel, alielekea moja kwa moja sehemu ambapo Harry alikuwa amekaa,

"shikamoo" Sarah alimsalimia Harry wakati akikaa,

"marhabaa, Harry aliitikia huku akikishangaa kisarah kilivyo kidogo alafu kinawaendesha,

"bila kupoteza muda, nimekuja kwa jambo moja hapa, nataka nifungue kesi ya mauaji dhidi ya Taita, naomba uwe wakili wangu" Sarah aliongea huku akimtazama Harry, hiyo kauli haikumshangaza tu Harry, ila ilimtisha kabisa, maana alijua kabisa yeye ni mtuhumiwa wa hiyo kesi pia,

"mauaji ya nani?" Harry alituliza akili kisha akauliza,

"vifo vya wazazi wangu" Sarah alijibu na kumuona namna Harry alivyoshtuka,

"hiyo haiwezekani, kama huna cha maana kilichokuleta bora uende tu" Harry aliongea kijeuri,

"kwa hiyo hilo sio la maana?" Sarah aliuliza huku akitabasamu,

"naona huna jipya, siku ukiwa na cha maana utaniita tena" Harry aliongea kijeuri huku akinyanyuka na kuondoka, alijiamini na pia aliamini Sarah hana muda mrefu wa kuishi.

Harry alitoka na kupanda gari yake, akaondoka. Baada ya dakika tano za kuondoka Harry, Sarah alitoka Vin hotel, siku hakuwa na gari, akawa anatembea huku akiamini anaweza kupata bajaj.

Alitembea mwenda mrefu bila kuona bajaj wala boda boda, na kumbuka Vin hotel ilijengwa nje ya mji. Sarah akiwa eneo ambalo kuna miti mingi, ndipo alipoweza kumuona mtu akija nyuma yake, kwa kuwa kulikuwa na giza basi ilikuwa ngumu kumtambua huyo mtu.

Yule mtu akazidi kupiga hatua mpaka akamsogelea Sarah,

"tumekutana tena kwa mara nyingine mrembo" Aisha aliongea na kufanya Sarah amkumbuke, Sarah alishtuka sana,

"ulikuwa unanitafuta, bado hujaridhika na ulichonifanyia?" Sarah alimuuliza,

"nilikuwa sijalipwa, ila leo nimelipwa na nimekuja kuhitimisha kazi" Aisha aliongea,

"hitimisha tu, ruksa" Sarah aliongea na kumfanya Aisha aanze kumsogelea kishari, kwa kujihami Sarah akamrushia ngumi za haraka haraka, Aisha akarudi nyuma, Sarah akamrukia na teke likamkuta Aisha kifuani, akadondoka na kunyanyuka, Sarah akarusha tena ngumi mfululizo, Aisha akarudi nyuma akajikuta ameingia kwenye miti, Sarah akamuendea kasi na kurusha ngumi nyingine, Aisha akamdaka na kuachia kifuti kilichomkuta Sarah tumboni, Sarah akagugumia kwa maumivu,

"wakati unarusha ngumi zako sio kwamba nilikuwa naziogopa, nilitaka nikuvutie huku porini ili nikumalize bila shida" Aisha aliongea kwa dharau, kisha akaachia ngumi mfululizo zilizomkuta Sarah shingoni, Sarah akaenda chini,

"nyanyuka tuendelee" Aisha aliongea huku akizitoa pingu zake mfukoni, Sarah akanyanyuka na kurusha teke kali, Aisha akaudaka mguu wa Sarah kisha akautupa kiufundi, Sarah akajikuta anazunguruka, Aisha akaudaka mkono wa Sarah na kuufunga pingu, Sarah akaona akilegea ataumia, akarusha ngumi kwa ule mkono wake uliobakia, Aisha akainama na kuushika, akautia pingu na ule mkono kisha akamvuta Sarah kwa nyuma na kumtia kabali, Sarah ujanja ukaisha,

"bado sana katika masuala ya kupambana, nenda kajifunzie kuzimu" Aisha aliongea huku akitabasamu na kuchomoa kisu chake, akakipeleka shingoni kwa Sarah, Sarah akataka hata kukurupuka, ila alishindwa, alibanwa kiufundi haswa, kwa mara ya kwanza machozi yakamtoka Sarah katika pambano, hakuwa na msaada ingawa aliuhitaji sana kwa muda huu...........

*********ITAENDELEA***********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA.

ILIPOISHIA......................

Sarah akiwa chooni anajiangalia kwenye kioo, alishangaa mtu akisimama nyuma yake na kutabasamu, Sarah akageuka haraka na kumuangalia,

"hujambo mrembo?" Aisha aliongea huku akimsogelea Sarah, tena usogeleaji wa kishari. Sarah akaona bora aondoke, wakati akapiga hatua ili aondoke alikamatwa shingo na Aisha, Sarah akarusha ngumi ikadakwa kisha akapigwa pingu ya mkono mmoja, aliporusha ngumi ya pili ikadakwa na kuunganishwa katika pingu na mkono wa hawali, Sarah akakosa ujanja.

Alipojaribu kurusha teke, Aisha alimdhibiti kwa kumbana ukutani na kisha akatoa kisu chake mfukoni,

"wewe ndio unasumbua mabosi mjini?" Aisha aliuliza huku akitabasamu kisha kisu akakiweka shingoni kwa Sarah, akaanza kukikandamiza taratibu na damu ikaanza kumchuruzika Sarah, Sarah machozi yakaanza kumtoka na kuona ndoto yake ya kulipa kisasi ikimalizwa chooni, tena na mwanamke mwenzake ambaye hata hamjui.................

************ENDELEA************

Ila kile kisu hakikuingia sana shingoni mwa Sarah, kiliingia kidogo na ndio maana kikasababisha ile damu shingoni mwa Sarah.

Aisha akakitoa kile kisu shingoni kwa Sarah na kisha akamuachia Sarah miguu yake, Aisha akaelekea moja kwa moja sehemu ambapo ziliwekwa toilet paper, akakata kipande kidogo na kisha akafutia damu iliyokuwepo kwenye kisu chake.

Muda wote Sarah alijitahidi kujishika shingoni na Mikono yake ingawa alifungwa pingu.

"bahati yako bado sijalipwa pesa yangu, maana siuagi mtu bila kukamilishiwa madai yangu ya hawali" Aisha aliongea huku akimfuata Sarah, alipomfikia alifungua pingu alizomfunga na kuziweka mahali pake, Aisha akawa anapiga hatua ili aondoke, Sarah akamuwahi na kumrushia teke, Aisha akamkwepa, Sarah akaona Kama amedharauliwa vile kwa kufanyiwa udhalilishaji ule na Aisha.

Sarah akarusha ngumi, Aisha akaikwepa tena na kufanya mkono wa Sarah uangukie mgongoni kwake, alichokifanya Aisha ni kukimata kichwa cha Sarah na kukibamiza kwenye kioo cha pale chooni, mpaka kile kioo kikapasuka,

"hao wapuuzi wanavyokusifia nilidhani labda unajua sana kupambana, kumbe fala tu" Aisha aliongea huku akijipangusa mikono yake kisha akawa anatoka zake kuelekea nje.

Sarah akajibandua pale kwenye kioo na kuona damu kidogo ikimchuruzika kwenye kichwa juu ya sikio, akatoa kitambaa chake na kujifuta, kisha nae akatoka nje, ndipo alipomshuhudia kwa mbali Aisha akiondoka kwa mwendo wa madaha huku baadhi ya wanaume wakwale wakimtupia jicho la matamanio kutokana na umbo lake la kike kumvaa vyema, Sarah akajikuta anawachukia wale wanaume bila ya sababu ya msingi,

"wangejua kuwa lile lijanamke ni likatili wala wasingethubu kuliangalia kwa matamanio hivyo" Sarah aliongea peke yake na kumalizia na sonyo la chini chini.

Sarah nae akaamua aelekee nje ili kumuwahi Aisha ili amfuatilie anapoelekea. Sarah akatembea kwa mwendo wa haraka mpaka nje ya mgahawa, akatupa jicho kushoto hakumuona Aisha, akatupa jicho kulia pia hakuona mtu, akasimama kwa muda huku akijilaumu kwa kuchelewa kutoka nje, mwisho nae akaamua aondoke zake, akaelekea sehemu alipoegesha gari lake, uwa anaegesha mbali sana na eneo ambalo huenda.

Sarah alivyopotea eneo lile ndio muda ambao aliibuka Aisha baada ya kujificha katika kichochoro kimoja eneo lile, Aisha uwa hatumiii gari pindi anapokuwa mjini, uwa anatumia njia za mkato sana, ni mwanamke ambaye amezoea sana maisha ya uswahilini na hata tabia zake ni za kiswahili tu.

Aisha alipotoka mafichoni, aliangalia uelekeo alioelekea Sarah kisha akatabasamu huku akitikisa kichwa, alafu mdogo mdogo akaingia zake kichochoni na safari ya kwenda anapopajua yeye ikaanza.

*****************

Sarah alipofika kwenye gari yake aliingia na kufungua eneo la mbele na kutoa dawa, akachukua pamba na kuanza kuipaka kwenye eneo la shingoni na kichwani juu ya sikio ambalo alijeruhiwa na Aisha.

Sarah alipomaliza kujipa huduma ya kwanza, aliwasha gari lake na kuondoka, alikuwa anarudi kwake,

"yule mwanamke ni nani?, alafu ametumwa na nani?" Sarah alijiuliza wakati akiendesha gari yake,

"hii vita inaanza kuwa nzito, maana wanaingizwa wapambanaji, tena wenye uwezo mkubwa" Sarah aliongea huku akimfikiria Aisha namna alivyomdhibiti kiurahisi.

Sarah aliingia nyumbani kwake huku akiwa na hasira, alipofika sebuleni hakutaka hata kupoteza muda, alivua viatu tu na kisha moja kwa moja na kuelekea kwenye chumba cha siri, huku mkononi akiwa amebeba chakula kwa ajili ya mjomba wake, bwana Taita.

Alifika ndani ya chumba na kuwasha taa, Taita alikuwa amelala sakafuni huku akiwa bado amefungwa kamba,

"Sarah hivi si uniachie tu, umetaka hela nimekupa, lakini huniachii, kwanini?" Taita aliuliza kwa upole,

"hela yako naweza kukurudishia, tatizo sio hela, suala la kukuachia ni mimi mwenyewe nikiamua na wala sio pesa yako" Sarah alijibu huku akimfungua Taita ili ale chakula alichomletea,

"basi kama tatizo sio pesa, niache nikafanye shughuli zangu, biashara zangu zinakwama uraiani" Taita aliongea kwa kulalamika,

"ngoja nikuulize kitu, hivi Katika kambi yenu kuna mwanamke hata mmoja?" Sarah alimuuliza Taita,

"mwanamke????? Hapana" Taita alijibu huku akifakamia chakula,

"kuna mwanamke alinivamia leo na kudai ametumwa, sasa ametekwa wapi huyo mwanamke?" Sarah alimuuliza Taita,

"Mimi sijui kwa kweli, kwani wewe unapambana na maadui wangapi?" Taita aliuliza,

"sina adui mimi" Sarah alijibu,

"sasa kama huna adui si uniachie" Taita aliongea,

"nitakuachia, ila siku ninayokuachia itabidi na babu yangu na mwanae wawe huru" Sarah aliongea,

"mbona baba mdogo alishaachiwa, ila babu yako ndio bado" Taita aliongea kwa kujiamini,

"sawa kama mmemuachia, ila mimi shida yangu ni babu" Sarah aliongea,

"nipe simu niwaambie wamuachie" Taita aliongea,

"hupaswi kuwa na haraka, hii shughuli ina utaratibu wake" Sarah aliongea huku akisimama,

"mama mbona unaondoka? Ina maana ndio na leo huniachii?" Taita alilalamika wakati Sarah akitoka, ila leo hakutaka kumfunga Taita Mikono, alimuacha huru tu.

Sarah akaenda sebuleni na kumpigia simu Harry,

"Sarah naongea" Sarah alijitambulisha baada ya Harry kupokea,

"nakusikilza" Harry alijibu huku akipata hofu,

"kesho kutwa naomba tuonane, kuna kitu nataka unisaidie" Sarah aliongea na kufanya Harry ajiulize ni kweli Sarah anahitaji msaada au mtego,

"sawa, tutaonana wapi?" Harry aliuliza,

"sema wewe, nitakuja popote kwa kuwa nina shida" Sarah aliongea kwa utulivu,

"ok, tutakutana Vin hotel, saa mbili usiku" Harry aliongea,

"na iwe hivyo, usiniangushe mwanasheria" Sarah aliongea,

"usijali" Harry aliongea kisha Sarah akakata simu, akatabasamu,

"wewe si ni mwanasheria? Utanisaidia kesi yangu sasa" Sarah aliongea peke yake kisha akatupa simu mezani.

*******************

Siku nyingine tena, Aisha alikutana na Harry katika mgahawa ule ule waliokutana hawali,

"nilikutana na msichana wako, nimemjaribu kabisa, ni mwepesi mno, basi tu sikutaka kumuua" Aisha aliongea huku akitabasamu,

"Sarah??" Harry aliuliza,

"ndio huyo huyo, hana lolote mpaka nikahisi pesa yako naila bure tu, maana hata kupambana hawezi" Aisha aliongea kwa dharau,

"huyo atakuwa sio yeye, ulipambana na mwingine" Harry aliongea huku akiwa haamini,

"kama huamini sawa, ngoja muda ufike tu" Aisha aliongea,

"sasa kwanini hujamuua?" Harry aliuliza,

"uwa siui mpaka malipo yakamilike" Aisha alijibu,

"ungeua tu, au hatuaminiani?" Harry aliuliza,

"kazi haramu hazihitaji kuaminiana" Aisha alijibu,

"sawa, ila sasa tayari nimeshakamilisha malipo yako, na kama utaweza leo usiku anza kazi, nitakutana mahala na Sarah, anadai anataka tuongee" Harry aliongea,

"haina shida, kwa kuwa malipo umekamilisha leo, basi na kazi itaisha leo" Aisha aliongea kwa kujiamini,

"basi sawa, saa mbili usiku nitakuwa nae Vin hotel, uje pale" Harry aliongea,

"nitakuja ila hatutaonana, nitaweka mitego yangu" Aisha aliongea,

"poa, basi baadae, acha niwahi kazini" Harry aliongea huku akisimama na Kuondoka zake, akamuacha Aisha akiendelea kupata juisi.

**************

Mishale ya saa mbili usiku, Sarah akiwa amevaa suruali nyeusi na koti la suti lenye rangi ya njano isiyokoa, alikuwa akiingia pale Vin hotel, alielekea moja kwa moja sehemu ambapo Harry alikuwa amekaa,

"shikamoo" Sarah alimsalimia Harry wakati akikaa,

"marhabaa, Harry aliitikia huku akikishangaa kisarah kilivyo kidogo alafu kinawaendesha,

"bila kupoteza muda, nimekuja kwa jambo moja hapa, nataka nifungue kesi ya mauaji dhidi ya Taita, naomba uwe wakili wangu" Sarah aliongea huku akimtazama Harry, hiyo kauli haikumshangaza tu Harry, ila ilimtisha kabisa, maana alijua kabisa yeye ni mtuhumiwa wa hiyo kesi pia,

"mauaji ya nani?" Harry alituliza akili kisha akauliza,

"vifo vya wazazi wangu" Sarah alijibu na kumuona namna Harry alivyoshtuka,

"hiyo haiwezekani, kama huna cha maana kilichokuleta bora uende tu" Harry aliongea kijeuri,

"kwa hiyo hilo sio la maana?" Sarah aliuliza huku akitabasamu,

"naona huna jipya, siku ukiwa na cha maana utaniita tena" Harry aliongea kijeuri huku akinyanyuka na kuondoka, alijiamini na pia aliamini Sarah hana muda mrefu wa kuishi.

Harry alitoka na kupanda gari yake, akaondoka. Baada ya dakika tano za kuondoka Harry, Sarah alitoka Vin hotel, siku hakuwa na gari, akawa anatembea huku akiamini anaweza kupata bajaj.

Alitembea mwenda mrefu bila kuona bajaj wala boda boda, na kumbuka Vin hotel ilijengwa nje ya mji. Sarah akiwa eneo ambalo kuna miti mingi, ndipo alipoweza kumuona mtu akija nyuma yake, kwa kuwa kulikuwa na giza basi ilikuwa ngumu kumtambua huyo mtu.

Yule mtu akazidi kupiga hatua mpaka akamsogelea Sarah,

"tumekutana tena kwa mara nyingine mrembo" Aisha aliongea na kufanya Sarah amkumbuke, Sarah alishtuka sana,

"ulikuwa unanitafuta, bado hujaridhika na ulichonifanyia?" Sarah alimuuliza,

"nilikuwa sijalipwa, ila leo nimelipwa na nimekuja kuhitimisha kazi" Aisha aliongea,

"hitimisha tu, ruksa" Sarah aliongea na kumfanya Aisha aanze kumsogelea kishari, kwa kujihami Sarah akamrushia ngumi za haraka haraka, Aisha akarudi nyuma, Sarah akamrukia na teke likamkuta Aisha kifuani, akadondoka na kunyanyuka, Sarah akarusha tena ngumi mfululizo, Aisha akarudi nyuma akajikuta ameingia kwenye miti, Sarah akamuendea kasi na kurusha ngumi nyingine, Aisha akamdaka na kuachia kifuti kilichomkuta Sarah tumboni, Sarah akagugumia kwa maumivu,

"wakati unarusha ngumi zako sio kwamba nilikuwa naziogopa, nilitaka nikuvutie huku porini ili nikumalize bila shida" Aisha aliongea kwa dharau, kisha akaachia ngumi mfululizo zilizomkuta Sarah shingoni, Sarah akaenda chini,

"nyanyuka tuendelee" Aisha aliongea huku akizitoa pingu zake mfukoni, Sarah akanyanyuka na kurusha teke kali, Aisha akaudaka mguu wa Sarah kisha akautupa kiufundi, Sarah akajikuta anazunguruka, Aisha akaudaka mkono wa Sarah na kuufunga pingu, Sarah akaona akilegea ataumia, akarusha ngumi kwa ule mkono wake uliobakia, Aisha akainama na kuushika, akautia pingu na ule mkono kisha akamvuta Sarah kwa nyuma na kumtia kabali, Sarah ujanja ukaisha,

"bado sana katika masuala ya kupambana, nenda kajifunzie kuzimu" Aisha aliongea huku akitabasamu na kuchomoa kisu chake, akakipeleka shingoni kwa Sarah, Sarah akataka hata kukurupuka, ila alishindwa, alibanwa kiufundi haswa, kwa mara ya kwanza machozi yakamtoka Sarah katika pambano, hakuwa na msaada ingawa aliuhitaji sana kwa muda huu...........

*********ITAENDELEA***********

the Legend☆
huyu shetani ametokea wapi jaman

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah nimetelekeza mambo mengi asee nkijua apa napitia episode kadhaa jamaa kumbe kamoja tu asee, ongeza ongeza mkuu tafadhali huu uraibu wa story zako ni taaabu mkula
 
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI

ILIPOISHIA....................

Yule mtu akazidi kupiga hatua mpaka akamsogelea Sarah,

"tumekutana tena kwa mara nyingine mrembo" Aisha aliongea na kufanya Sarah amkumbuke, Sarah alishtuka sana,

"ulikuwa unanitafuta, bado hujaridhika na ulichonifanyia?" Sarah alimuuliza,

"nilikuwa sijalipwa, ila leo nimelipwa na nimekuja kuhitimisha kazi" Aisha aliongea,

"hitimisha tu, ruksa" Sarah aliongea na kumfanya Aisha aanze kumsogelea kishari, kwa kujihami Sarah akamrushia ngumi za haraka haraka, Aisha akarudi nyuma, Sarah akamrukia na teke likamkuta Aisha kifuani, akadondoka na kunyanyuka, Sarah akarusha tena ngumi mfululizo, Aisha akarudi nyuma akajikuta ameingia kwenye miti, Sarah akamuendea kasi na kurusha ngumi nyingine, Aisha akamdaka na kuachia kifuti kilichomkuta Sarah tumboni, Sarah akagugumia kwa maumivu,

"wakati unarusha ngumi zako sio kwamba nilikuwa naziogopa, nilitaka nikuvutie huku porini ili nikumalize bila shida" Aisha aliongea kwa dharau, kisha akaachia ngumi mfululizo zilizomkuta Sarah shingoni, Sarah akaenda chini,

"nyanyuka tuendelee" Aisha aliongea huku akizitoa pingu zake mfukoni, Sarah akanyanyuka na kurusha teke kali, Aisha akaudaka mguu wa Sarah kisha akautupa kiufundi, Sarah akajikuta anazunguruka, Aisha akaudaka mkono wa Sarah na kuufunga pingu, Sarah akaona akilegea ataumia, akarusha ngumi kwa ule mkono wake uliobakia, Aisha akainama na kuushika, akautia pingu na ule mkono kisha akamvuta Sarah kwa nyuma na kumtia kabali, Sarah ujanja ukaisha,

"bado sana katika masuala ya kupambana, nenda kajifunzie kuzimu" Aisha aliongea huku akitabasamu na kuchomoa kisu chake, akakipeleka shingoni kwa Sarah, Sarah akataka hata kukurupuka, ila alishindwa, alibanwa kiufundi haswa, kwa mara ya kwanza machozi yakamtoka Sarah katika pambano, hakuwa na msaada ingawa aliuhitaji sana kwa muda huu...........

**********ENDELEA***********

Wakati Aisha akikipeleka kisu shingoni kwa Sarah, ulisikika mlio wa bastola, Aisha akageuka nyuma na kumuona mtu akiwaendea kwa kasi huku akiwa na bastola mkononi, Aisha akaona bora amalize kazi haraka kabla huyo mtu hajawafikia, Aisha akanyanyua kisu juu ili amchome nacho Sarah shingoni, wakati kisu kikiwa juu, kilipigwa na risasi na kile kisu kikadondoka chini, Aisha akatoa tusi la nguoni kumuelekea yule mtu aliyekuwa akizidi kuwasogelea,

"na wewe malaya sikuachi hivi hivi" Aisha aliongea huku akimgeukia Sarah kisha akaruka teke kali lililomkuta Sarah katika paji la uso na kisha kisogo cha Sarah kikagonga kwenye mti, Aisha alivyotua chini akaruka sarakasi ndogo kisha akaingia sehemu miti mingi zaidi ilipo, akakimbia huku akiwa na hasira za kushindwa kumuua Sarah wakati alimuhakikishia Harry kuwa ile kazi ingeisha usiku ule ule.

Yule bwana akafanikiwa kufika eneo lile, alikuwa ni Sajenti Minja, alifika na kumkuta msichana akiwa amefungwa pingu, Sajenti Minja akaingiza mkono mfukoni na kutoa funguo nyingi, akamfungua Sarah,

"ni nini kinaendelea?" Sajenti Minja aliuliza huku sura ya Sarah akihisi anaijua, na wakati huo Sarah nae akamtambua Sajenti Minja, mapigo ya moyo yakaongezeka,

"Mimi sijui, nilikuwa natoka hotelini naenda kutafuta usafiri, ndipo nikashangaa ananivamia na kunipiga" Sarah aliongea huku akijishika eneo la kisogoni ambapo kulikuwa na uvimbe,

"alafu wewe sura yako sio ngeni, hivi nimekuona wapi?" Sajenti Minja aliuliza,

"mhhhhhhh.....ndio tumeshawahi kuonana, kuna siku nilikuja polisi tukakutana pale nje, ulidahi umeifananisha gari yangu" Sarah aliongea huku akimuangalia Sajenti Minja,

"ooooh, nimekukumbuka. Sasa huyu aliyekushambulia unamjua?" Sajenti Minja aliuliza,

"simjui, alafu ni mwanamke" Sarah alijibu na kumfanya Sajenti Minja ashangae,

"huyo mwanamke huenda ni dada mmoja hivi hatari sana ambaye hata mimi ninamtafuta, ameshawahi kunishambulia mara mbili" Sajenti Minja aliongea huku akidhani Aisha ni Sarah na wakati huo Sarah alikuwa akimcheka Sajenti Minja chini chini.

"Mimi ni polisi, je naweza kukuchukua twende polisi ukafungue kesi?" Sajenti Minja aliuliza,

"hapana, mtu mwenyewe simjui, acha niende tu nyumbani" Sarah alijibu,

"naweza kukupeleka nyumbani?" Sajenti Minja aliuliza,

"hapana, nitaenda tu mwenyewe" Sarah alijibu,

"wewe kuwa na akili, huyo dada aliyekuvamia atakuwa bado anakuwinda, acha tu nikupeleke" Sajenti Minja alizidi kumshawishi Sarah,

"sawa nipeleke" Sarah aliitikia kisha wakatoka hapo kwenye miti na kuelekea moja kwa moja mpaka ilipo gari ya Sajenti Minja na wakaingia,

"au nikuachie uendeshe mwenyewe kwa sababu ndio unajua tuendapo" Sajenti Minja alimuuliza Sarah,

"hata hivyo ni sawa" Sarah aliitikia kisha Sajenti Minja akashuka na Sarah akaenda upande wa dereva, Sarah akawasha gari na kuiondoa.

"unakuja kula Vin hotel kwani huna mke?" Sarah alimuuliza Sajenti Minja,

"nani kakwambia nilikuja kula?" Sajenti Minja aliuliza huku akitabasamu,

"sasa ulienda kufanyaje?"Sarah alimuuliza,

"nilikuwa namtafuta mmiliki wa ile hotel" Sajenti Minja alijibu,

"ni ndugu yako?" Sarah alimuuliza,

"hapana, kuna maswali nataka kumuuliza" Sajenti Minja aliongea,

"ooh, nasikia ana pesa nyingi kweli" Sarah aliuliza kama kweli hamjui Taita,

"anazo, kwani wewe humjui Taita?" Sajenti Minja akamtupia swali Sarah,

"nitamjulia wapi mie" Sarah alijibu huku akiegesha gari nje ya uzio wa nyumba yake.

"nimefika, hapa ndipo naishi" Sarah aliongea,

"ni kwako au umepanga?" Sajenti Minja aliuliza,

"nimepanga" Sarah aliongea uongo huku akitabasamu,

"sasa niachie namba yako ya simu, ukihisi yule aliyekuvamia bado anakufuatilia, utanipigia" Sajenti Minja aliongea huku akiitoa simu yake, Sarah hakua na sababu ya kukataa, akampa namba Sajenti Minja.

"nilitaka kusahau, hapa unakaa peke yako au umeolewa?" Sajenti Minja aliuliza,

"nawe una maswali mengi, au kwa kuwa polisi? Mi naishi peke yangu bwana" Sarah alijibu huku akitelemka kwenye gari na pia alikuwa akitabasamu,

"kawaida kuuliza kwa mwanaume, au hupendi maswali?" Sajenti Minja aliuliza huku akiamia upande wa dereva,

"kwaheri bwana, nitakujibu siku nyingine" Sarah alijibu huku akifungua geti na kumuacha Sajenti Minja akimtupia jicho la wizi. Sarah akamuona kisha akarudi nyuma,

"nilitaka kusahau, asante kwa msaada wako" Sarah aliongea,

"usijali, ila hujaniambia jina lako" Sajenti Minja aliongea,

"naitwa Sarah" Sarah alijibu,

"haya Sarah, usiku mwema" Sajenti Minja aliaga,

"na kwako pia afisa" Sarah aliongea huku akitabasamu na kuingia ndani na kumuacha Sajenti Minja akiondoka zake.

Hiyo ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa Sarah kumruhusu mtu apajue anapoishi, hakutaka iwe hivyo, ila ilitokea tu baada ya kuhisi uoga wa kufuatiliwa na Aisha, huyu mwanamke alianza kumuogopa kutokana na aina ya upambanaji wake, alikuwa anapambana kirahisi tu, ila alikuwa ni ngumu kumshinda. Sarah hakutaka kujiamini tena mbele ya Aisha kwa muda huu.

************,

Siku mpya iliwakuta Harry, Trigger na Aisha wakiwa ndani ya ofisi ya Taita wakijadiliana.

"Trigger, huyu ni Aisha nimemuongeza kwa ajili ya kazi ya kumkabili Sarah" Harry alimtambulisha Aisha kwa Trigger,

"sawa, mimi naitwa Trigger" Trigger aliongea huku akimpa mkono Aisha,

"nimefurahi kukufahamu" Aisha aliongea huku akipeana mkono na Trigger,

"sasa tujadiliane namna ya kumpata Sarah, Aisha amepata nafasi ameshindwa kuitumia" Harry aliongea,

"na wewe si nilikuambia kuna mtu alikuja na bunduki kuja kumsaidia, vinginevyo ningemuua "

"huyo aliyekuja kumuokoa ni mwenzake?" Trigger aliuliza,

"hakuna anaejua" Harry alijibu kwa ufupi,

"eti Trigger, una mbinu gani rahisi ya kumpata Sarah?" Aisha aliuliza,

"sina, aisee, labda tukambane Dokta Pendo" Trigger alijibu,

"yes, hiyo ni akili" Harry alionesha kukubaliana na Trigger, kisha wakapanga namna ya kwenda kumbana Dokta Pendo, walikubaliana kwenda usiku wa hiyo siku.

***********************

Siku hii mpya Sarah aliitumia kufuatilia masuala ya kampuni yake mpya anayotaka kuifungua na pia aliitumia kufanya manunuzi ya vitu mbalimbali vya nyumbani kwake.

Sarah aliporudi kwake nyakati za usiku, aliingia ndani ya nyumba yake na kupitia kwenye friji ambapo alichukua juisi na kwenda moja kwa moja mpaka katika chumba chake cha siri na kuingia,

"chukua juisi upoze njaa" Sarah aliongea huku akimtupia Taita box la juisi, lakini Taita hakujibu kitu wala hakuonekana kutingishika, Sarah akahisi huenda Taita anamfanyia ujanja ili amzidi akili, Sarah akatoa bastola yake,

"nyanyuka unywe juisi mbwa wewe, au nikufumue hilo litumbo lake?" Sarah aliongea kwa ukali lakini Taita hakutingishika, Sarah akamsukuma kwa mguu na kuufanya mwili wa Taita ugeuke, macho yalikuwa wazi kazi amekufa na pia damu zilikuwa zikimtoka kwenye matundu ya pua zake zote mbili, Sarah akashtuka, akaweka bastola chini na kumsogelea Taita, akapeleka mkono kifuani kuangalia mapigo ya moyo, yalikuwa kwa mbali sana, Sarah akachanganyikiwa huku asijue ni kitu gani kimemkuta Taita.

*****************

Usiku huu Dokta Pendo akiwa amevaa nguo zake za kulalia huku akiwa yupo sebuleni akitazama filamu, alisikia mlango wa sebuleni kwake ukigongwa,

"shoga amenikumbuka leo?" Dokta Pendo alijiuliza huku akihisi huyo mtu anaegonga mlango ni Sarah.

Dokta Pendo akaenda mpaka mlangoni na kufungua mlango ' yarabi toba" macho yake yalikutana hana kwa hana na mdomo wa bastola,

"habari" Aisha aliongea huku akimsogelea Dokta Pendo na kumfanya Dokta Pendo arudi nyuma bila kuongea kitu. Aisha aliingia huku akiwa ameambatana na Trigger na Harry,

"hatujaja kukuua hapa, ila ukitaka kufa tutakuua, tunataka utusaidie shida moja" Trigger aliongea huku akimuangalia Dokta Pendo lakini Dokta Pendo hakuwa na uwezo wa kujibu, alikuwa akitetemeka tu.

"mpigie Sarah na umwambie aje hapa una shida naye" Trigger alimpa maelekezo Dokta Pendo,

"namba yake sina" Dokta Pendo alijikaza na kujibu,

"nasikia ni shoga yako? Kwanini huna namba yake?" Aisha aliuliza huku akitabasamu,

"sio shoga yangu, aliniteka tu" Dokta Pendo alijijitea,

"huyu tuondoke nae, maana atatusumbua tu" Harry aliongea,

"Mimi ngoja nibakie hapa kama tulivyopanga, huenda yule mrembo anaweza kuja" Aisha aliongea,

"wewe baki, tutawasiliana" Harry aliongea huku akitoka nje ya nyumba na kumfanya Trigger amvute Dokta Pendo ili atoke,

"niache, mimi siendi popote" Dokta Pendo alilalama huku akijichomoa mikononi mwa Trigger,

"sipendagi kusumbuliwa na mabinti" Trigger aliongea kisha akamkata ngumi kali ya kichwa Dokta Pendo na kuzimia pale pale,

"khaa, wewe unampiga ngumi nzito mwanamke kama unampiga mwanaume mwenzako?" Aisha na ukatili wake wote aliogopa namna Trigger alivyomfanya Dokta Pendo,

"ukimchekea ataharibu kazi" Trigger aliongea huku akimuweka Dokta Pendo mabegani, kisha akatoka nae nje na ndani akabaki Aisha akiangaza angaza mandhari ya sebule ile.

*******************

Baada ya Sarah kuona hali ya Taita inazidi kuwa mbaya, maana hata kupumua alikuwa akipumua kwa tabu, Sarah alienda mpaka katika vifaa vyake vya matibabu na kuja na mipira ya oxygen ambayo alimuwekea Taita eneo la puani na mdomoni kisha akamtoa shati lake,

"nadhani Dokta Pendo anaweza kuwa msaada" Sarah aliongea kisha akatoka katika chumba chake cha siri na kuelekea sebuleni, akakaa koti sweta na kuelekea moja kwa moja kwenye gari, kisha akaliwasha na kuliondoa ndani ya geti kisha akaondoka kwa kasi kuelekea kwa Dokta Pendo.

Kwa jinsi alivyokuwa na haraka, gari lake hakuegesha mbali kama anavyofanyaga, leo aliiegesha pale pale mlangoni kwa Dokta Pendo.

Sarah akatelemka na kwenda kugonga mlango,

"hodi Shoga" Sarah aliita huku akigonga mlango, lakini hakujibiwa

"shoga" Sarah aliita kwa sauti kubwa zaidi huku akiendelea kugonga mlango,

"Ngoja, nakuja shoga" Sauti kutoka ndani ilimjibu, lakini haikuwa sauti ya Dokta Pendo, Sarah akapata wasiwasi, akawa anajiandaa kutoa bastola ili avamie, lakini kabla Hajaichomoa bastola yake mlango ulifunguliwa kwa kasi na Sarah akavutwa ndani, bastola ya yake ikadondoka miguuni kwa Aisha.

Sarah alipomuona Aisha alijikuta akikiasirika, haikuwa hasira ya kuvutwa au kupigwa, ilikuwa ni hasira ya kujilaumu kwanini amekuja kwa Dokta Pendo na kukutana na huyu mwanamke mbaya, Sarah hakuwa alikosa kujiamini kabisa mbele ya Aisha, uoga ukamjaa. Na wakati huo Aisha alifunga mlango kwa ndani kisha akaiokota bastola ya Sarah na kumuelekezea Sarah,

"hii ya leo haina kuremba, ni kumaliza kazi na kupotea" Aisha aliongea na kuikoki bastola huku akiwa hana tabasamu lake kama tulivyomzoea, alikuwa yupo makini kiasi kwamba ndita zilionekana vyema kwenye paji lake la uso.........

**********ITAENDELEA************

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom