Riwaya: 'Njama'

Mimi nimesoma haya mavitabu ya hadithi mpaka basi. Kina Ben Mtobwa, sss Simbamwene, Hammie Rajabu Musiba mwenyewe vote vi4....lakini vyooote kilichonishika ni Sofia wa Gongo la mboto. Pili pilipili na pumbazo la moyo....dah kitambo kweli

Una nakala yoyote unisaidie nami nisome.????
 
Ayaaa,rusheni nondo moja moja jama,mtatuchanganya,tufatilie kikomo,kisha mwenye kufa n's kupona,kijasho chembamba,hofu na uchu waturushie kimoja kimoja!dah,hii ni zaidi ya utamu
 
Kuna mdau kajitokeza kule jukwaa la Sports and entertainment specifically entertainment ameanza kuweka riwaya ya HOFU
Cc. MAPIKIPIKI pono

Ahsante mkuu,ngoja nijikumbushe hofu,kisha utumwagie KK yaani kikosi cha kisasi,halafu ulee uhondo wa wizi wa almas mwadui(Elungata),mkuu katika novel zote za willy gamba,sijasoma novel moja ya kijasho chembamba,chonde chonde mwenye hiyo novel atumwagie humu,
 
Last edited by a moderator:
 
Gamba kwa kujipendelea!hofu alikuwa na nyaso,njama na veronica amadu toto la freetown alipouawa akahamia kwa zawadi kikosi cha kisasi akawa na tete kisha uchu akawa na bibiana vyote vinono.
 
Gamba kwa kujipendelea!hofu alikuwa na nyaso,njama na veronica amadu toto la freetown alipouawa akahamia kwa zawadi kikosi cha kisasi akawa na tete kisha uchu akawa na bibiana vyote vinono.
Good observation. Njama anasema hapendi kupika kwenye Hofu huko Rwanda anasema anapenda kupika........!
 
[QUOTE="kidi kudi, post: 11543553vitaburvya huyo]Riwaya; 'NJAMA' Mtunzi; A.E MUSIBA (Willy Gamba) NAONANA NA CHIFU Ndege ilitua kwenye uwanja wa ndege wa mjini Dar es Salaam kiasi cha saa moja na nusu asubuhi. Nilipita harakaharaka katika sehemu za afya, uhamiaji na ushuru wa forodha, kisha nikachukua teksi iliyonipeleka moja kwa moja katika ofisi yangu ya 'Afrika International Agencies', iliyoko mtaa wa Independence karibu na ofisi kuu za shirika la Bima la Taifa. "Hallo bosi, umerudi!", Rose mfanyakazi wetu sehemu ya mapokezi alisema. "Naam nimepata ujumbe wa teleksi kutoka kwa Marcelina kuwa mama anakufa". "Na kweli nenda ofisi kwako mwandishi wako mahususi alikuwa na wasi wasi maana huko juu wanakuulizia kila baada ya dakika kumi.

Ama kweli huko juu kuna kitu kikubwa kinawawasha". Nilielekea ofisini kwangu, nilipofika nikafungua mlango wa mwandishi wangu mahsusi, Linda. Oh, Mungu wangu, afadhali umefika, kidogo nipate wazimu maana huko juu hawanipi nafasi hata ya kupumua. Naulizwa kila wakati kwanini hujafika, utafikiri mimi ndiye nakufuga". "Poa sasa nimefika mwenyewe.

Vipi shughuli hapa?". "Mambo shwali, isipokuwa toka juzi kuna jambo limeharibika, maana jana nzima ofisi inawaka moto. Chifu huko juu ametingwa na mambo. Na afadhali uende sasa hivi, mimi nawajulisha kuwa uko kwenye lifti unaelekea ofisini kwake". "Yaa fanya hivyo". Niliacha mzigo wangu kwa Linda, nikaelekea ofisini kwa Chifu ambaye ofisi yake ilikuwa orofa ya tatu, na sisi tulikuwa chini katika jengo hilo hilo.

Nilifungua mlango bila kubisha hodi. Nikaingia ndani ya ofisi ya mwandishi mahsusi wa Chifu. "Ooh, Mungu wangu! Afadhali umekuja!", Maselina alisema kwa moyo wa furaha. "Hujambo lakini?". "Sijambo ila wasiwasi ni juu yako tu. Pole sana, nafikiri tumekukatishia likizo murua kabisa". "Wacha kusema. Tayari nilikuwa nimeshapata kipande cha msichana.

Nilipopata ujumbe wako kidogo nipate ugonjwa wa moyo. Je kuna nini huku kinacholeta wasiwasi hivi?". "Atakueleza mwenyewe kinachompandisha damu yake. Nakwambia amekuwa anakuhitaji kwa haraka sana, hata hivi anaona umechelewa. hivi sasa nilikuwa nataka kutuma teleksi nyingine". "Mama yangu mzazi! mtafikiri nina roketi yangu mwenyewe!". "Ngoja nimwambie kwamba umefika. Akifungua mlango kisha atukute tunapga soga sijui atafanya nini. Huenda atapasuka!". "Mwache apasuke! Mnafikiri kunikatisha likizo yangu nilijisikiaje.

Utadhani moyo wangu umetengenezwa kwa chuma, na wake kwa udongo". "Kamwambie mwenyewe hayo huko ndani", Maselina alijibu akimwemwesa huku akiinua simu. Huyu Maselina tumefanya kazi pamoja kwa muda mrefu kiasi ya kwamba uelewano wetu hauwezi kuelezeka kwa maneno. Huenda siku moja nitapata maneno ya kueleza, ila tu kwa leo naweza kusema ni rafiki yangu mkubwa. "Chifu, namba moja yuko hapa", Maselina alitamka katika simu. Nambari moja, ndivyo nilikuwa najulikana kikazi.

Katika kazi yetu sisi hutumia namba, mimi nilikuwa namba moja hivyo unaweza mwenyewe kuchekecha ukajuwa kwa nini. Mimi Willy si mtu wa majivuno. Watu wengi, hasa wakubwa wa serikali walinijua kwa hii namba yangu. Wengi walikuwa hawajui namba moja ni Willy Gamba, ila kwa watu wachache sana. Hii ilinipa fursa hata nyumbani Dar es Salaam nijulikane kama mfanyabiashara wa kawaida tu, na si Willy Gamba ambaye ni namba moja katika Idara ya Usalama, Tanzania. Maselina aliweka simu chini. "Nenda ndani mara moja". Nilifungua mlango, na nikamkuta Chifu akitembea toka kona moja ya chumba hadi kona nyingine.

Kwa mtu ninayemfahamu nikajua hapo alipo alikuwa na matatizo makubwa sana yaliyomsakama rohoni mwake. "Kaa chini namba moja', Chifu aliamru. Chifu anaponiita kwa namba yangu ya kazi ujue kuna jambo kubwa. nilivuta kiti nikaa, yeye akazidi kutembea kona hadi kona nyingine, hatimaye akasimama nyuma ya kiti chake. "Nashukuru kwa kufika kwako mapema, namba moja ndio sababu nakutegemea sana". "Asante", nilijibu halafu nikaendelea. "Mbona hivi, nini kinakuwasha?". Alichukuwa mtemba uliokuwa mezani, akafungua mkebe wa tumbaku akaijaza, kisha akawasha na kuanza kupuliza.

Alipuliza mara mbili, halafu akazungusha kiti chake ambacho kinazunguka kwenye tendegu, akaketi. "Kina jambo kubwa limetokea!". Aliweka mtemba wake mezani na kuweka mikono yake kwenye mezani. Akaniangalia machoni, huku macho yake yakionesha ukali wake. Akili yangu ikiwa tayari kusikiliza jambo hili huku moyo ukinidunda.

Utanisikiliza, utauliza maswali baadaye". Sawa". "Nafikiri nitaanza toka mwanzo. Ingawaje mambo mengine unayajua, nitayarudia tu kwa ajili ya umuhimu wa habari yenyewe ilivyo, unaonaje?". "Utakavyoona wewe Chifu". "Unajua nchi yetu inalea vyama vingi vya wapigania uhuru. Kama vile vyama vya wapigania uhuru toka Zimbabwe, Afrika Kusini n.k. Pamoja n a kulea vyama hivi tunawapatia vijana wao ya kijeshi. Kwa vile mafunzo mengi yanapatikana hapa na makao makuu ya vyama hivi yapo hapa, basi silaha zao vile vile zinapitia hapa na sisi tunazipokea toka nchi rafiki na kuwapa wanaohusika. "Hapa tuna vyama viwili vya wapigania uhuru katika Afrika kusini.

Vyama hivi ni 'The Peoples liberetion Front, of South Afrika (PLF)" kinachoongozwa na Ndugu Cecil Chimalamo na South Afrika National Party (SANP) kinachoongozwa na Ndugu Ray Simbuche. Miezi sita iliyopita Ndugu Cecil Chimalamo wa PLF alikwenda Urusi ambako alioba msaada wa silaha na akaahidiwa kupewa silaha hizo ambazo zingepelekwa Dar es Salaam mnamo muda wa miezi sita. "Wiki iliyopita Ubalozi wa Urusi wa hapa mjini ulipata karatasi za maelezo ya silaha hizi ambazo tayari zilikuwa zimeshapakiwa kwenye meli siku nyingi na zilikuwa njiani kuwasili Dar es Salaam.

Na makaratasi haya yalisema meli hiyo itawasili mjini hapa mnamo wiki hii'. "Basi yalipofika, ubalozi uliyashughulikia kikamilifu kwa upande wake, kisha ukayapitisha kwenye kamati ya ukombozi ya Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), maana kamati hii ndiyo inashughulikia mambo haya kama unavyofahamu. Kamati nayo ilianza kuzishughulikia karatasi hizi mpaka zikawa tayari, wakawa sasa wanangoja meli kufika.

Habari kutoka kwenye Wakala wa Meli zilieleza kuwa meli hiyo itaingia bandarini Dar es Salaam tarehe tatu mwezi huu ambayo ilikuwa juzi ile". "Baada ya kupata habari hizi kamati ilipanga pamoja na ofisi ya mambo ya silaha za wapigania uhuru pia na maofisa wa bandari wanaohusika kuwa mizigo hiyo ipakuliwe usiku wa tarehe nne yaani juzi kuamkia jana. Kwa sababu karatasi zote zilikuwa zimekamilika na sehemu zote zikiwa na habari kamili, pande zote zilikaa zikisubiri silaha hizo mnamo siku hiyo kama ulivyopangwa".

Chifu alichukua mtemba wake tena akavuta kidogo kisha akauweka juu ya meza. "Nafikiri umenielewa mpaka hapo?". "Wakati huo mpango hii yote ya kupakua mizigo hii, ofisi ya PLF ilikuwa ikishirikishwa?", niliuliza. "Ndio, kwa sababu huwa wanaelezwa mambo yote yanavyokwenda, hivyo huwa wana habari kamili ya mambo yote.

Naweza kuendelea?". "Unaweza". "Sasa jambo la kushangaza likatokea juzi. Maofisa wa ofisi ya jshi la ulinzi inayoshughulikia silaha za wapigania uhuru walikwenda kwenye ofisi ya kamati ya ukombozi juzi mnamo saa nne ili kuchukua karatasi hizo za mizigo, wapate kijitayarisha kwa upakuaji wa mizigo hiyo wakati wa usiku.

Walipofika kwenye ofisi hii wakakuta ofisa anayehusika hajafika kazini. Ikabidi wamwone ofisa wa juu katika ofisi hiyo kumweleza umuhimu uliopo wa kuandaa kupakua silaha hizo usiku. "Huyu ofisa wa juu katika ofisi hii ya kamati naye alisema kuwa alikuwa ameshangazwa kwanini ofisa huyo alikuwa hajafika kazini. Hivyo wote kwa ujumla wakaondoka kuelekea nyumbani kwa ofisa huyo kuona kama anaumwa aweze kuwaelekeza wapi walipoziweka karatasi hizo. Huyu ofisa alikuwa akikaa sehemu za Upanga, Barabara ya Umoja wa mataifa, nyumba namba 1168". "Walipofika nyumbani kwa ofisa huyo walimkuta mfanyakazi wake akiwa nje. Walipomuuliza kama wenye nyumba wapo aliwajibu kuwa yeye hakai hapo ila huwa anakuja kila asubuhi lakini alipofika asubuhi hii alikuta milango yote ya kuingilia ndani ya nyumba imefungwa.

Hivyo mpaka muda huo alikuwa anasubiri kwani alifikiri wametoka. Ofisa huyo alikuwa anakaa yeye pamoja na mke wake na walikuwa bado hawajapata watoto. Ofisa mmoja wa jeshi alikwenda kuangalia gereji akakuta gari la ofisa huyu lipo na lilikuwa bado halijatoka. Kitu hiki kilimtia mashaka akawaeleza wenzake na akashauri wajaribu kuingia ndani ya nyumba huenda walikuwa bado wamo ndani.

Kwani kama kutoka wangekuwa wametoka na gari lao, walikubaliane wavunje mlango wa kuingilia ndani". Chifu alinyamaza kidogo akainua macho yake kuniangalia. "Walishtushwa kwa kumkuta ofisa huyu amepigwa risasi amekufa sebuleni, huku akiwa amevalia vizuri kabisa kuonyesha kuwa alikuwa anatoka matembezini.

Halafu ukumbini walimkuta mke wa ofisa huyo naye amepigwa risasi amekufa huku akiwa amevalia nguo za kulia. Haapo hapo wakanyanyua simu na kutoa ripoti ya vifo hivi kituo cha polisi Oysterbay ambacho hakikuchelewa kutuma maofisa wao kwenye nyumba hiyo. Baada ya polisi kufika, maofisa hao wa jeshi na ofisa kutoka kamati ya ukombozi ilibidi warudi upesi kwenye ofisi ya kamati, maana vifo hivi vilileta wasiwasi". Wakati wote huu akieleza, mimi nilikuwa kimya kabisa na akili yangu ilichemka niliposikia habari hizi za mauaji. "Halafu ikawaje?". "Walirudi ofisi za kamati upesi upesi, na kuanza kutafuta makaratasi haya ya mizigo kila mahali ofisini hapa, lakini hawakuona kitu.

Hapo ndipo jasho lilipowatoka. Jambo hili liliwapa wasiwasi zaidi ikabidi wakimbilie bandarini kutoa habari kwa maofisa wa bandari kuwa karatasi zimepotea". Chifu macho yake yaliwaka nikajua karibu anasema kitu cha kustua. "Walipofika katika ofisi za bandari, ofisa anayehusika na habari hizi, walipomweleza kuwa makaratasi yamepotea, alishangaa sana, ndipo mwishoni akawaeleza kuwa silaha zilikuwa zimeisha chukuliwa usiku uliokuwa umepita na wanajeshi waliovalia nguo za jeshi la ulinzi na wakiwa na karatasi zote za kuchukulia silaha, zikiwa kamili kabisa. Walikuwa wamefika na magari ya jeshi la wananchi, hata akawatolea namba za magari.

Kundi hili lililochukua silaha liliongozwa na mtui aliyevalia nguo za cheo cha meja. Kusikia hivi kundi lote lililofika kwenye ofisi ya bandari lilichoka kabisa. "Lakini si walikuwa wamekubaliana na ofisi ya bandari kuwa watapakua usiku wa juzi kuamkia jana, ilikuwaje yeye akaruhusu mizigo ipakuliwe usiku wa juzi ile kuamkia juzi?". "Huko ndiko nakuja kufafanua. Ofisa wa bandari alieleza kuwa mnamo terehe tatu mwezi huu ambayo ni juzi ile kiasi cha saa kumi alipata simu toka ofisi ya Kamati ya Ukombozi.
 
Nilikisoma hiki kitabu miaka zamani sana wakati huko hata Dar sijui vzr nilikuwa nakuja likizo tuu, lkn Leo nimeirudia na kujua sehemu zoote zilizotajwa Asante kwa kunirudisha shule ya msingi na sekondari.
 
Nilikisoma hiki kitabu miaka zamani sana wakati huko hata Dar sijui vzr nilikuwa nakuja likizo tuu, lkn Leo nimeirudia na kujua sehemu zoote zilizotajwa Asante kwa kunirudisha shule ya msingi na sekondari.
Hata mn nilikisoma nikiwa mdogo dar siifahamu hivyo leo nime enjoy sana . Hv New Africa hotel ndo ipo pale posta jirani na NBC Corporate eeh? Kumbe zamani ilikuwa Bank ya Nyumba daaah.
 
Hata mn nilikisoma nikiwa mdogo dar siifahamu hivyo leo nime enjoy sana . Hv New Africa hotel ndo ipo pale posta jirani na NBC Corporate eeh? Kumbe zamani ilikuwa Bank ya Nyumba daaah.
Hawa watunzi noma sana imebidi veronica afe ili amwachie Zabibu nafasi ya kutafunwa na Gamba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…