Mdharuba
JF-Expert Member
- Oct 26, 2011
- 824
- 522
STORY: NITAKUFA NAE
MTUNZI: JK Mdharuba
+255 718 274 130
+250 726 023 140
mdharuba@gmail.com
SEHEMU YA KWANZA
★★★★★★★★★★★
"Sikiliza Jeff, pamoja na maneno yote uliyoongea, bado sijashawishika kuachana na Jk, sijui kanipa nini yule mwanaume, naomba mniache tu" Aliongea Merry huku machozi yakimbubujika wakati huu,, maneno haya aliyaongea huku kamasi zikimtoka. Jeff alishamthibitishia kuwa Jk hakuwa mkweli kwake, lakini bado alitamani saaana kuendelea kuwa na Jk, licha ya kuwa na uhakika wa asilimia mia kuwa Jk hakuwa mume bora.
Ila, Jeff alithibitisha haya yote kwa Merry akiwa na lake kichwani, ingawa Merry alimuona ni mtu mwema tu. Kusikia majibu haya, Jeff alianza kung'aka, na kuropoka, "Na tutaona mtafika wapi na huyo ms**ge wako Jk, unajifanya unajua kupeeendaa,, ila kitu ntakachomfanya hutaweza kuamini" Aliongea Jeff kwa hasira na kuondoka pale baa akimsukumia meza Merry bila kujali kama ataumia au laa...
Baada ya Jeffy kuondoka mahala pale, Merry alitoa simu yake iliyokuwa kwenye mkoba na kubofyabofya kisha akaweka sikioni, haikuhitaji PhD kujua kuwa alikua akimpgia Jk, mwanaume wa maisha yake, aliyempenda kwa moyo wake wote.
"Baby, uko wapi Laaziz wangu?" Aliongea kwa sauti laini bi Merry baada ya simu yake kupokelewa.
"Nipo hapa Kwa Aziz Ally ndo nasubiri daladala nielekee nyumbani"
"Mi natangulia basi baby huko nyumbani, maana kuna mtu kanitibua sana leo"
"Poa My love tutaongea vizuri nikifika huko, nakupenda sana"
"Nakupenda pia Jk wangu" Alisema Merry na kukata simu.
★★★★★★★★★★★★
Merry Hassan, binti wa kinyamwezi kutokea mkoani Tabora, anajikuta ghafla sana amezama kwenye penzi zito la Jumaa khatib maarufu kama ‘Jk' mtoto wa kitanga, kule Mahaba yalipozaliwa. Licha ya msimamo aliokua nao tangu anakua kuhusu wanaume, lakini alijikuta ghafla sana anazama katika penzi zito la kijana mmoja mtanashati ambaye alikua ni Mwalimu wa shule moja ya Sekondari Jijini Dar..
Wakware mbalimbali walikua wakimtolea macho Merry kutokana na jinsi Mungu alivyomtengeneza vizuri, lakini wala Merry hakujali akiamini wanaendeshwa tu na tamaa zao za kimwili..
Katika harakati zake za kila siku ndipo siku moja alikutana na kijana wa kitanga, mwenye umbo la wastani, mcheshi, akajikuta moja kwa moja anaukabidhi moyo wake kwake, tena mzimamzima..
Moja kati ya watu waliokua wasumbufu sana kwa Merry ni bwana Jeffy John, mfanyabiashara maarufu jijini Dar, alijaribu kutumia pesa zake kadri alivyoweza ili kumshawishi Merry aachane na Jk na awe na yeye lakini juhudi zake ziligonga mwamba. Licha ya kuwa na mkewe, Jeffy bado alionekana kuwa na hamu sana na penzi la Merry,, yeye akiamini Merry alimstahili mtu kama yeye kwa kuwa alikua na pesa na umaarufu!! Jambo ambalo Merry halikumuingia akilini, alimpenda Jk kwa moyo wake wote, licha ya kuwa Jk alikua na maisha ya kawaida saana..
Aliridhika kuwa nae, wakipata dagaa wanakula pamoja kwa amani, wanasikilizana, wanasaidiana kazi, na mambo mengi wakifanya pamoja kama watoto mapacha. Habari za kitandani ndo usiulize, kwani Merry alikua akipewa raha mpaka zinapitiliza, akiwa anatamani saa zote awe na Jk kitandani akiunyanyasa mwili wake..
"Jk, nakupenda saana, naomba usinisaliti, ntalia". Ni maneno ya kila siku yaliyokuwa yakisikika masikioni mwa Jk kutoka katika kinywa cha Merry..
★★★★★★★★★★★★
"Jk Mume wangu, yule Jeffy bado anaendelea sana kunisumbua, leo nilivyokwambia naenda kule Magomeni, basi mda ule wa mchana nilienda pale kwenye ile pub tunayokuwaga mara nyingi, akaja sijui katokea wapi akaanza kunambia eti ooh sijui ww una michepuko, sijui nini, basi akaongea weee mpaka mwisho nikamwmbia uniache tu na Jk wangu, akakasirika akanambia eti atanionyesha, na atakufanyia kitu kibaya" Alieleza Merry akiwa ameweka kichwa chake katika mapaja ya Jk huku mikono ya Jk ikishikashika uso wake laini, ilihali mikono ya Mwery ikiwa imezunguka kiuononi mwa Jk.
Baada ya maelezo haya Jk alitoa tabasamu pana, na kusema maneno machache "Watu wengine bana wana matatizo sana,, haya bana" kisha akaanza kuyatomasa matiti ya Merry yaliyokuwa yamefunikwa na khanga iliyokua imeishia kifuani hapo, taratiiib akaanza kuyapa tabu matiti yale huku mkono mmoja ukitambaa na mwili wa Merry taratiib, maisha ya usiku yakaendelea..
*********************
Asubuhi kabla Jk hajatoka kwenda kazini Merry aliamua kumuuliza Jk kuhusu jambo lile la Jeffy amelipokeaje..
"Jana ulikaa kimya baada ya kukueleza vile, sielewi ulichukuliaje mume wangu"
"Aaah achana nae huyo, hajielewi" Jk alijibu kifupi, akanywa chai kisha akatoka..
*******************************
"Wewe ukifika pale usiulize, fumua risasi moja ya kichwa akafie mbele bata yule" Jeffy alikua akimpanga kijana wake wa kazi kutekeleza agizo la kumuua Jk..hakuwa na huruma hata kidogo, alitaka Jk afe ili aone kama Merry ataendlea kuwa na maringo tena.
"Sawa mkuu nimekuelewa" Alisema kijana yule mwenye umri kati ya miaka 24 hadi 27 akionyesha kuyaelewa vizuri sana maelekezo ya Jeffy John..
*************************
Saa 7:30 mchana simu ya Merry iliita, ilikua ni namba ngeni, simu yake ilishaita kama mara 4 yeye akiwa jikoni, mara hii ya 5 ndo alipokua ameingia chumbani na kuskia simu yake ikiita, akapokea..
"Haloo, nadhani naongea na Merry mke wa Jk" ilisikika sauti ya upande wa pili..
"Ndio mimi, vipi kwema??" Aliuliza Merry akiwa anatetemeka, alishaanza kuhisi kuna ktu kibaya kimetokea sababu ya vile vitisho alivyopata kutoka kwa Jeffy juu ya mumewe Jk..
"Hapana, sio kwema, kuna tatizo.." Ilisema sauti upande wa pili na kumfanya Merry azidi kuchanganyikiwa..
★★★★★★★★★★★★★
Itaendelea....
MTUNZI: JK Mdharuba
+255 718 274 130
+250 726 023 140
mdharuba@gmail.com
SEHEMU YA KWANZA
★★★★★★★★★★★
"Sikiliza Jeff, pamoja na maneno yote uliyoongea, bado sijashawishika kuachana na Jk, sijui kanipa nini yule mwanaume, naomba mniache tu" Aliongea Merry huku machozi yakimbubujika wakati huu,, maneno haya aliyaongea huku kamasi zikimtoka. Jeff alishamthibitishia kuwa Jk hakuwa mkweli kwake, lakini bado alitamani saaana kuendelea kuwa na Jk, licha ya kuwa na uhakika wa asilimia mia kuwa Jk hakuwa mume bora.
Ila, Jeff alithibitisha haya yote kwa Merry akiwa na lake kichwani, ingawa Merry alimuona ni mtu mwema tu. Kusikia majibu haya, Jeff alianza kung'aka, na kuropoka, "Na tutaona mtafika wapi na huyo ms**ge wako Jk, unajifanya unajua kupeeendaa,, ila kitu ntakachomfanya hutaweza kuamini" Aliongea Jeff kwa hasira na kuondoka pale baa akimsukumia meza Merry bila kujali kama ataumia au laa...
Baada ya Jeffy kuondoka mahala pale, Merry alitoa simu yake iliyokuwa kwenye mkoba na kubofyabofya kisha akaweka sikioni, haikuhitaji PhD kujua kuwa alikua akimpgia Jk, mwanaume wa maisha yake, aliyempenda kwa moyo wake wote.
"Baby, uko wapi Laaziz wangu?" Aliongea kwa sauti laini bi Merry baada ya simu yake kupokelewa.
"Nipo hapa Kwa Aziz Ally ndo nasubiri daladala nielekee nyumbani"
"Mi natangulia basi baby huko nyumbani, maana kuna mtu kanitibua sana leo"
"Poa My love tutaongea vizuri nikifika huko, nakupenda sana"
"Nakupenda pia Jk wangu" Alisema Merry na kukata simu.
★★★★★★★★★★★★
Merry Hassan, binti wa kinyamwezi kutokea mkoani Tabora, anajikuta ghafla sana amezama kwenye penzi zito la Jumaa khatib maarufu kama ‘Jk' mtoto wa kitanga, kule Mahaba yalipozaliwa. Licha ya msimamo aliokua nao tangu anakua kuhusu wanaume, lakini alijikuta ghafla sana anazama katika penzi zito la kijana mmoja mtanashati ambaye alikua ni Mwalimu wa shule moja ya Sekondari Jijini Dar..
Wakware mbalimbali walikua wakimtolea macho Merry kutokana na jinsi Mungu alivyomtengeneza vizuri, lakini wala Merry hakujali akiamini wanaendeshwa tu na tamaa zao za kimwili..
Katika harakati zake za kila siku ndipo siku moja alikutana na kijana wa kitanga, mwenye umbo la wastani, mcheshi, akajikuta moja kwa moja anaukabidhi moyo wake kwake, tena mzimamzima..
Moja kati ya watu waliokua wasumbufu sana kwa Merry ni bwana Jeffy John, mfanyabiashara maarufu jijini Dar, alijaribu kutumia pesa zake kadri alivyoweza ili kumshawishi Merry aachane na Jk na awe na yeye lakini juhudi zake ziligonga mwamba. Licha ya kuwa na mkewe, Jeffy bado alionekana kuwa na hamu sana na penzi la Merry,, yeye akiamini Merry alimstahili mtu kama yeye kwa kuwa alikua na pesa na umaarufu!! Jambo ambalo Merry halikumuingia akilini, alimpenda Jk kwa moyo wake wote, licha ya kuwa Jk alikua na maisha ya kawaida saana..
Aliridhika kuwa nae, wakipata dagaa wanakula pamoja kwa amani, wanasikilizana, wanasaidiana kazi, na mambo mengi wakifanya pamoja kama watoto mapacha. Habari za kitandani ndo usiulize, kwani Merry alikua akipewa raha mpaka zinapitiliza, akiwa anatamani saa zote awe na Jk kitandani akiunyanyasa mwili wake..
"Jk, nakupenda saana, naomba usinisaliti, ntalia". Ni maneno ya kila siku yaliyokuwa yakisikika masikioni mwa Jk kutoka katika kinywa cha Merry..
★★★★★★★★★★★★
"Jk Mume wangu, yule Jeffy bado anaendelea sana kunisumbua, leo nilivyokwambia naenda kule Magomeni, basi mda ule wa mchana nilienda pale kwenye ile pub tunayokuwaga mara nyingi, akaja sijui katokea wapi akaanza kunambia eti ooh sijui ww una michepuko, sijui nini, basi akaongea weee mpaka mwisho nikamwmbia uniache tu na Jk wangu, akakasirika akanambia eti atanionyesha, na atakufanyia kitu kibaya" Alieleza Merry akiwa ameweka kichwa chake katika mapaja ya Jk huku mikono ya Jk ikishikashika uso wake laini, ilihali mikono ya Mwery ikiwa imezunguka kiuononi mwa Jk.
Baada ya maelezo haya Jk alitoa tabasamu pana, na kusema maneno machache "Watu wengine bana wana matatizo sana,, haya bana" kisha akaanza kuyatomasa matiti ya Merry yaliyokuwa yamefunikwa na khanga iliyokua imeishia kifuani hapo, taratiiib akaanza kuyapa tabu matiti yale huku mkono mmoja ukitambaa na mwili wa Merry taratiib, maisha ya usiku yakaendelea..
*********************
Asubuhi kabla Jk hajatoka kwenda kazini Merry aliamua kumuuliza Jk kuhusu jambo lile la Jeffy amelipokeaje..
"Jana ulikaa kimya baada ya kukueleza vile, sielewi ulichukuliaje mume wangu"
"Aaah achana nae huyo, hajielewi" Jk alijibu kifupi, akanywa chai kisha akatoka..
*******************************
"Wewe ukifika pale usiulize, fumua risasi moja ya kichwa akafie mbele bata yule" Jeffy alikua akimpanga kijana wake wa kazi kutekeleza agizo la kumuua Jk..hakuwa na huruma hata kidogo, alitaka Jk afe ili aone kama Merry ataendlea kuwa na maringo tena.
"Sawa mkuu nimekuelewa" Alisema kijana yule mwenye umri kati ya miaka 24 hadi 27 akionyesha kuyaelewa vizuri sana maelekezo ya Jeffy John..
*************************
Saa 7:30 mchana simu ya Merry iliita, ilikua ni namba ngeni, simu yake ilishaita kama mara 4 yeye akiwa jikoni, mara hii ya 5 ndo alipokua ameingia chumbani na kuskia simu yake ikiita, akapokea..
"Haloo, nadhani naongea na Merry mke wa Jk" ilisikika sauti ya upande wa pili..
"Ndio mimi, vipi kwema??" Aliuliza Merry akiwa anatetemeka, alishaanza kuhisi kuna ktu kibaya kimetokea sababu ya vile vitisho alivyopata kutoka kwa Jeffy juu ya mumewe Jk..
"Hapana, sio kwema, kuna tatizo.." Ilisema sauti upande wa pili na kumfanya Merry azidi kuchanganyikiwa..
★★★★★★★★★★★★★
Itaendelea....