Abtali mwerevu
JF-Expert Member
- May 5, 2013
- 637
- 432
Angalizo:
Nchi inayotajwa kama Nchi yetu, haina uhusiano wowote na nchi ya Tanzania.
Sehemu ya Kwanza
Komandoo Mako alikimbia akiwa kashika kidege kidogo kisichokuwa na rubani, baada ya umbali fulani, akakiachia nacho kikapaa peke yake. Pembeni alilala Komandoo Bwii, huyu alikuwa na kitu mfano wa runinga ndogo akikiangalia kile kidege kidogo na pengine yeye ndiye alikiongoza. Mbele kidogo, walilala Makomandoo wawili, Ado na Moli. Hawa walikuwa wadunguaji. Watu wengi hudhani kazi ya wadunguaji ni kulenga shabaha na kupiga pekee, si kweli, kazi kuu ya wadunguaji ni kufuatilia mienendo ya adui. Komandoo Ado na Moli walikesha usiku kucha wakifuatilia mienendo ya adui, akilala huyu anamwachia huyu, hata sasa mchana wa leo, kila kitu kilikuwa sawa.
Kidege kisicho na rubani kiliifikia kambi ya adui, kikadondosha mabomu pande zote, milipuko ikaitikisa kambi. Adui wengi wakafa, lakini wengine wakabaki. Waliobaki wakajiandaa kupambana, wamezishika vyema bunduki zao tena wamejaa taharuki.
Mako, Bwii, Ado na Moli walishapanda kifaru. Mako alikuwa kiongozi, pengine angetoa amri ya kufanya jambo fulani. Bwii alikuwa dereva wa kifaru hiki, Ado alikuwa mpigaji, ungeona kombora limerushwa, basi hiyo ilikuwa kazi ya Ado. Moli kazi yake ndani ya kifaru ilikuwa kuweka makombora mahali pake tayari kwa kupigwa.
Kifaru kilivurumusha makombora makali yaliyoiharibu kambi ya adui katika namna ya kutisha. Halafu walipofika eneo la kambi ambalo lilitimka vumbi, makomandoo wakashuka ndani ya kifaru. Komandoo Ado na Moli wakapanda juu ya paa katika namna ambayo sijawahi kuiona, huko wangewadungua adui waliosalia, pia wangewalinda wenzao waliokuwa chini. Bwii alitembea taratibu tena kwa tahadhari akiua kila adui aliyekutana naye. Maadui ni wagumu kufa, pamoja na milipuko ile, wapo ambao walisalia na walijaribu kupambana.
Makomando walisafisha kila hatua na sasa hapakuwa na dalili za adui kuwepo. Adui aliteketezwa yeye pamoja na kambi yake. Hakuna chochote cha maana kilichosalia.
Bwii aliwafanyia ishara Ado na Moli, nao wakamfanyia ishara fulani, halafu wakashuka. Wakasimama pembezoni mwa kifaru chao.
“Mwalimu yuko wapi?” aliuliza Bwii.
“Sijamwona… Wewe vipi?” alijibu Ado akimgeukia Moli ambaye hata hivyo alikataa kwa kupeleka kichwa kulia kisha kushoto.
“Huko juu mlikuwa mnafanya nini?” alihoji Bwii.
Mako walimuita Mwalimu. Ni yeye ndiye kawafundisha vijana hawa wakiwa katika kambi ya Makomandoo katika nchi yetu. Ado, Moli na Bwii walifanya mafunzo ya awali ya Uzalendo katika kambi moja, tena wamesoma shule moja ya sekondari walipoishia kidato cha nne na kuamua kuwa wazalendo. Wakiwa pamoja, wakafanya mafunzo ya Jeshi la Wanachi wa Nchi Yetu. Halafu hawakutosheka, wala hawakukaa kazini, wakaunganisha moja kwa moja katika kambi ya Makomandoo, huko wakakutana na Mwalimu wao Mako, tena Mako ndiyo lilikuwa darasa lake la kwanza kufundisha, akiwa kijana kama wao.
Komandoo Bwii alimpenda Mako, bila Mako pengine Bwii asingekuwa Komandoo. Kuna wakati wa mafunzo Bwii aliishiwa nguvu wakati wa zoezi la kutembea umbali mrefu wakiwa wamebeba boti vichwani, Mako alimbeba Bwii mpaka alipopata nguvu za kuendelea mwenyewe.
Kuna wakati Bwii alishindwa kusoma ramani na kuwapoteza wenzake. Wakubwa wakahoji kama Bwii alistahili kuwa hapo, Mako akamtetea kwa kutoa hoja kuwa, Bwii ana vipaji ambavyo ni yeye pekee anayeviona, akaomba apewe muda.
Wakati wa kuruka na parachuti, almanusura Bwii apoteze maisha akiwa angani, badala ya kubofya kitufe upande wa kulia, yeye alipapasa upande wa kushoto akisema, “Parachuti haina kitufeeeee… nakufaaa.” Mako aliruka na parachuti lake, akamfikia Bwii na kumweleza, “Kitufe kipo kulia Komandoo.” Bwii akapapasa upande wa kulia na kukiona kisha akakiminya na kuokoa maisha yake. Baada ya tukio hilo, Bwii akawa mtu jasiri, akafanya mafunzo kwa weredi mkubwa. Akawa jasiri asiyeogopa tena mwenye akili ya mapigano katika mazingira magumu kuliko mtu yeyote, halafu akaibuka kuwa na mwili mkubwa uliojaa misuli. Watu wote wakamuogopa Bwii. Kwa uwezo wake, endapo angebadilika kidogo, angetosha kuleta madhara makubwa.
“Mwalimu yuko wapi?” Bwii aliuliza tena, safari hii kakasirika.
“Hatujamuona,” walijibu Ado na Moli.
“Huko juu mlikuwa mnafanya nini?” aliuliza tena Bwii. Ado aliyechoshwa na swali lake akamdhihaki, “Tulikuwa tunalinda makalio yako yasipigwe risasi.”
Bwii akarusha ngumi. Ado akaikwepa. Moli akashangaa! Halafu Bwii akamkamata Ado, Moli akamkamata Bwii, makomandoo watatu wakasukumana mpaka katika kifaru, halafu Bwii kwa maguvu yake akawasukuma Ado na Moli wakadondoka chini kama furushi.
Haikuwa kizembe wala rahisi kiasi hicho, Ado na Moli wakanyanyuka, miguu yao ya kushoto imetangulia. Halafu Bwii akabeba kipande cha tofali, Ado akapaza sauti, “Bwii, achana na Systema, hapa tunapiga kung’fu… umejaa mwili unadhani tunakuogopa, mpumbavu wewe, raia!”
“Ndiyo, raia!” Moli akadakia. Bwii aliyekasirishwa na kuitwa raia, akatupa tofali chini, akarusha mateke matatu, mawili yakampata Ado, moja likamkosa Moli. Halafu Ado na Moli wakashambulia kwa pamoja, Bwii akarudi nyuma kujihami, vumbi likatimka!
Inaendelea...
Kuwa wa Kwanza Kupokea mwendelezo wa Riwaya hii Kwa kujiunga katika Group la bure WhatsApp. Kujiunga, Gusa Hapa
Tupate Wadhamini:
Soma: Jinsi ya Kuomba Chuo na Mkopo
Nchi inayotajwa kama Nchi yetu, haina uhusiano wowote na nchi ya Tanzania.
Sehemu ya Kwanza
Komandoo Mako alikimbia akiwa kashika kidege kidogo kisichokuwa na rubani, baada ya umbali fulani, akakiachia nacho kikapaa peke yake. Pembeni alilala Komandoo Bwii, huyu alikuwa na kitu mfano wa runinga ndogo akikiangalia kile kidege kidogo na pengine yeye ndiye alikiongoza. Mbele kidogo, walilala Makomandoo wawili, Ado na Moli. Hawa walikuwa wadunguaji. Watu wengi hudhani kazi ya wadunguaji ni kulenga shabaha na kupiga pekee, si kweli, kazi kuu ya wadunguaji ni kufuatilia mienendo ya adui. Komandoo Ado na Moli walikesha usiku kucha wakifuatilia mienendo ya adui, akilala huyu anamwachia huyu, hata sasa mchana wa leo, kila kitu kilikuwa sawa.
Kidege kisicho na rubani kiliifikia kambi ya adui, kikadondosha mabomu pande zote, milipuko ikaitikisa kambi. Adui wengi wakafa, lakini wengine wakabaki. Waliobaki wakajiandaa kupambana, wamezishika vyema bunduki zao tena wamejaa taharuki.
Mako, Bwii, Ado na Moli walishapanda kifaru. Mako alikuwa kiongozi, pengine angetoa amri ya kufanya jambo fulani. Bwii alikuwa dereva wa kifaru hiki, Ado alikuwa mpigaji, ungeona kombora limerushwa, basi hiyo ilikuwa kazi ya Ado. Moli kazi yake ndani ya kifaru ilikuwa kuweka makombora mahali pake tayari kwa kupigwa.
Kifaru kilivurumusha makombora makali yaliyoiharibu kambi ya adui katika namna ya kutisha. Halafu walipofika eneo la kambi ambalo lilitimka vumbi, makomandoo wakashuka ndani ya kifaru. Komandoo Ado na Moli wakapanda juu ya paa katika namna ambayo sijawahi kuiona, huko wangewadungua adui waliosalia, pia wangewalinda wenzao waliokuwa chini. Bwii alitembea taratibu tena kwa tahadhari akiua kila adui aliyekutana naye. Maadui ni wagumu kufa, pamoja na milipuko ile, wapo ambao walisalia na walijaribu kupambana.
Makomando walisafisha kila hatua na sasa hapakuwa na dalili za adui kuwepo. Adui aliteketezwa yeye pamoja na kambi yake. Hakuna chochote cha maana kilichosalia.
Bwii aliwafanyia ishara Ado na Moli, nao wakamfanyia ishara fulani, halafu wakashuka. Wakasimama pembezoni mwa kifaru chao.
“Mwalimu yuko wapi?” aliuliza Bwii.
“Sijamwona… Wewe vipi?” alijibu Ado akimgeukia Moli ambaye hata hivyo alikataa kwa kupeleka kichwa kulia kisha kushoto.
“Huko juu mlikuwa mnafanya nini?” alihoji Bwii.
Mako walimuita Mwalimu. Ni yeye ndiye kawafundisha vijana hawa wakiwa katika kambi ya Makomandoo katika nchi yetu. Ado, Moli na Bwii walifanya mafunzo ya awali ya Uzalendo katika kambi moja, tena wamesoma shule moja ya sekondari walipoishia kidato cha nne na kuamua kuwa wazalendo. Wakiwa pamoja, wakafanya mafunzo ya Jeshi la Wanachi wa Nchi Yetu. Halafu hawakutosheka, wala hawakukaa kazini, wakaunganisha moja kwa moja katika kambi ya Makomandoo, huko wakakutana na Mwalimu wao Mako, tena Mako ndiyo lilikuwa darasa lake la kwanza kufundisha, akiwa kijana kama wao.
Komandoo Bwii alimpenda Mako, bila Mako pengine Bwii asingekuwa Komandoo. Kuna wakati wa mafunzo Bwii aliishiwa nguvu wakati wa zoezi la kutembea umbali mrefu wakiwa wamebeba boti vichwani, Mako alimbeba Bwii mpaka alipopata nguvu za kuendelea mwenyewe.
Kuna wakati Bwii alishindwa kusoma ramani na kuwapoteza wenzake. Wakubwa wakahoji kama Bwii alistahili kuwa hapo, Mako akamtetea kwa kutoa hoja kuwa, Bwii ana vipaji ambavyo ni yeye pekee anayeviona, akaomba apewe muda.
Wakati wa kuruka na parachuti, almanusura Bwii apoteze maisha akiwa angani, badala ya kubofya kitufe upande wa kulia, yeye alipapasa upande wa kushoto akisema, “Parachuti haina kitufeeeee… nakufaaa.” Mako aliruka na parachuti lake, akamfikia Bwii na kumweleza, “Kitufe kipo kulia Komandoo.” Bwii akapapasa upande wa kulia na kukiona kisha akakiminya na kuokoa maisha yake. Baada ya tukio hilo, Bwii akawa mtu jasiri, akafanya mafunzo kwa weredi mkubwa. Akawa jasiri asiyeogopa tena mwenye akili ya mapigano katika mazingira magumu kuliko mtu yeyote, halafu akaibuka kuwa na mwili mkubwa uliojaa misuli. Watu wote wakamuogopa Bwii. Kwa uwezo wake, endapo angebadilika kidogo, angetosha kuleta madhara makubwa.
“Mwalimu yuko wapi?” Bwii aliuliza tena, safari hii kakasirika.
“Hatujamuona,” walijibu Ado na Moli.
“Huko juu mlikuwa mnafanya nini?” aliuliza tena Bwii. Ado aliyechoshwa na swali lake akamdhihaki, “Tulikuwa tunalinda makalio yako yasipigwe risasi.”
Bwii akarusha ngumi. Ado akaikwepa. Moli akashangaa! Halafu Bwii akamkamata Ado, Moli akamkamata Bwii, makomandoo watatu wakasukumana mpaka katika kifaru, halafu Bwii kwa maguvu yake akawasukuma Ado na Moli wakadondoka chini kama furushi.
Haikuwa kizembe wala rahisi kiasi hicho, Ado na Moli wakanyanyuka, miguu yao ya kushoto imetangulia. Halafu Bwii akabeba kipande cha tofali, Ado akapaza sauti, “Bwii, achana na Systema, hapa tunapiga kung’fu… umejaa mwili unadhani tunakuogopa, mpumbavu wewe, raia!”
“Ndiyo, raia!” Moli akadakia. Bwii aliyekasirishwa na kuitwa raia, akatupa tofali chini, akarusha mateke matatu, mawili yakampata Ado, moja likamkosa Moli. Halafu Ado na Moli wakashambulia kwa pamoja, Bwii akarudi nyuma kujihami, vumbi likatimka!
Inaendelea...
Kuwa wa Kwanza Kupokea mwendelezo wa Riwaya hii Kwa kujiunga katika Group la bure WhatsApp. Kujiunga, Gusa Hapa
Tupate Wadhamini:
Soma: Jinsi ya Kuomba Chuo na Mkopo