RIWAYA: Msitu wa Solindo

RIWAYA: Msitu wa Solindo

The amazing universe, ni kama vile tunavo hisi katika milk way galaxy tupo alone lakin huenda kuna viumbe wengine wenye uwezo zaidi yetu...
 
The amazing universe, ni kama vile tunavo hisi katika milk way galaxy tupo alone lakin huenda kuna viumbe wengine wenye uwezo zaidi yetu...
Ni kweli na huenda pia kuwa, hakuna viumbe vingne vyenye uwezo zaidi yetu.....
Nawaza waza tu lakin😀😀
 
N
Yap, ni mawazo tuu ambayo baadae hujenga nguvu ya utafiti[emoji23][emoji23][emoji23]
Na vipi kama vipo na ikatokea vina nia ya kutuangamiza binadamu wote...
Na tena vinao uwezo mkubwa kulko sisi binadamu....
Hii inamaanisha vitatuangamiza na wanadamu tutatoweka wote juu ya uso wa nchi....

Na huenda usiku huu ndio vinapanga kutuangamiza!
Hahahaha hizi akili zangu bhna
Kama vipo na vina nia mbaya Mungu atuepushie mbali vishindwe!
 
N

Na vipi kama vipo na ikatokea vina nia ya kutuangamiza binadamu wote...
Na tena vinao uwezo mkubwa kulko sisi binadamu....
Hii inamaanisha vitatuangamiza na wanadamu tutatoweka wote juu ya uso wa nchi....

Na huenda usiku huu ndio vinapanga kutuangamiza!
Hahahaha hizi akili zangu bhna
Kama vipo na vina nia mbaya Mungu atuepushie mbali vishindwe!
Hahaha, ukisemacho ni fikirishi pia, mfano , vipi kama kuna viumbe wenye technology ya juu zaidi yetu katika umbali wa millions of miles katika upande mwingne wa universe?
.vipi kama wameshagundua uwepo wetu?


Hapa unajiuliza hivi ukiwa umeweka pembeni imani na mawazo kuwa mungu aliumba Dunia na vilivyomo, [emoji23][emoji23],
 
Hahaha, ukisemacho ni fikirishi pia, mfano , vipi kama kuna viumbe wenye technology ya juu zaidi yetu katika umbali wa millions of miles katika upande mwingne wa universe?
.vipi kama wameshagundua uwepo wetu?


Hapa unajiuliza hivi ukiwa umeweka pembeni imani na mawazo kuwa mungu aliumba Dunia na vilivyomo, [emoji23][emoji23],
Hahahaha noma sana!
Kwa assumptions km hizi ndio maana unakuta nchi zilizoendelea zinafanya tafiti kila leo nje ya dunia kujua nn kiko huko na kujidhatiti kiusalama... Ila bado swali linabaki km wapo viumbe wenye uwezo zaidi na huenda tunavyofanya hizi tafiti wanatuona, wanatukebehi na kutucheka tutawezaje kuifanya dunia kuwa sehemu salama kwetu?
Hatari sanaaa ukianza kuwaza hivi na ukajiona hauko salama na huna jibu la kujiweka salama unaweza ikimbia dunia!!
 
Hahahaha noma sana!
Kwa assumptions km hizi ndio maana unakuta nchi zilizoendelea zinafanya tafiti kila leo nje ya dunia kujua nn kiko huko na kujidhatiti kiusalama... Ila bado swali linabaki km wapo viumbe wenye uwezo zaidi na huenda tunavyofanya hizi tafiti wanatuona, wanatukebehi na kutucheka tutawezaje kuifanya dunia kuwa sehemu salama kwetu?
Hatari sanaaa ukianza kuwaza hivi na ukajiona hauko salama na huna jibu la kujiweka salama unaweza ikimbia dunia!!
[emoji23][emoji23][emoji23] eti uikimbie Dunia ? Haya mambo fikirishi ndyo yanawafanya wenzetu wapige hatua, Kama akina ELON MUSK ( Afanyavyo utafiti wa outer space). Ila Kwa sisi wengine tusiopenda kujisumbua na kuogopa kuishi Kwa hofu kama usemavyo acha tusifikiri kitofauti [emoji23][emoji23][emoji23] maana tusije tukakosa amani ya kuishi ha ha ha
 
[emoji23][emoji23][emoji23] eti uikimbie Dunia ? Haya mambo fikirishi ndyo yanawafanya wenzetu wapige hatua, Kama akina ELON MUSK ( Afanyavyo utafiti wa outer space). Ila Kwa sisi wengine tusiopenda kujisumbua na kuogopa kuishi Kwa hofu kama usemavyo acha tusifikiri kitofauti [emoji23][emoji23][emoji23] maana tusije tukakosa amani ya kuishi ha ha ha
Hahahaha ni bora kutulia tu ukiwaza sana unakuwa unajaza hofu ya kuogopa uvifikiriavyo pengine hata havipo na pengine hata ufanye nini huwezi vifikia kabisa!
 
MSITU WA SOLINDO

Mtunzi Richard Mwambe

Sehemu 10

Siku tatu baadae....
Ruperto Carola Cafe
Hellen na Stephan walionekana wenye furaha sana hasa kwa wazo lao lile
walilolipata maana walijua wazi kuwa pindi tu watapokamilisha zoezi hili watakuwa juu
sana kitaaluma, kiu yao ya kitafiti hasa juu ya mambo ya kale ilikuwa kubwa sana, lakini
bado hawakujua hasa ni nini wanachotaka kukifanya sasa, ni kitu cha hatari kiasi gani
wanachokifikiria, Hellen alijiuliza tu kama itakuwa safari kama ile ya Amazonia
iliyomchuku wiki tatu kuikamilisha akiishi na wa-Indios na wa-Amazonia ambako
alikutana na hatari ndogondogo tu, Stephan aliichukulia labda itakuwa safari kama ile
ambayo aliifanya huko Hamunatra katika jangwa la Misri ndani ya mapyramid
yaliyosadikiwa kuzikwa watawala wa nchi hiyo nyakati za kale kabisa, wote wawili
walijiona ni mashujaa sana kwa safari zao za utafiti walizozifanya katika maisha yao.
Stephan alishusha taratibu kikombe chake cha kahawa na kukiweka katika kijimeza
kidogo ndani ya mgahawa huo huku akiendelea na maongezi ya hapa na pale na Bi
Hellen. Binti mweusi alikuwa amekaa katika kimoja cha viti vitatu vilivyozunguka meza
hiyo akiwa na makaratasi machache mkononi mwake.
“Naitwa Saringo!” alijitambulisha kwa Hellen na Stephen, hili lilitukia mara baada ya
hawa wawili kujitambulisha kwake. Mazungumzo machache yalipita kati yao hasa ya
kufahamiana na kujuana zaidi, Stephen na Hellen walivutiwa na uchangamfu wa Saringo,
Saringo aliwaambia mambo mengi sana juu ya Africa hasa eneo ambalo yeye anatoka
Deutche Ost Africa, Stephen na Hellen walivutiwa sana na habari za huko na walipenda
kujua kama ni kweli au ni za kutunga tu za mababu wa kale. Saringo aliwasimulia mengi
sana hasa aliyosimuliwa na babu yake mzee Koloto, baada ya mazungumzo hayo saringo
aliwagusia juu ya stori ya babu yake alipokuwa askari wa wajerumani na alivyokuwa
akiongoza misafara ya wapagazi kuingia misituni na kuficha vitu visivyojulikana huko
kisha kuuawa, “No! Kwa nini waliwaua? Lazima kuna kitu” Hellen aliuliza kwa mshtuko
“Labda hawakutaka warudi tena huko, kuhofia kuchukua mali zao” Stephen alijibu
“ndiyo, ndiyo, hakika kabisa babu alinambia waliwaua ili wasiweze kurudi, lakini yeye
alinusurika na kufanikiwa kubaki hai” Saringo aliwaeleza na kutoa zile karatasi chache zenye michoro ya ajabu na maandishi ya kijerumani. Kwa Stephan haikuwa kitu kigeni
michoro ile kwani aliitumia sana alipokwenda huko Hamunatra, kwa haraka haraka
aliweza kuisoma na kutambua kilichofichwa katika michoro ile.
Stephen alitikisa kichwa kuashiria amegundua kitu, akanyanyua kikombe chake cha
kahawa na kunywa kidogo. “Vipi? Stephen!” Hellen aliuliza kwa shauku ya kutaka
kujua. Stephen alitikisa tena kichwa na kugeuza geuza mdomo wake, mara alionekana
kukunja uso, mara kutabasamu, akaiweka ile karatasi chakavumezani, na kunyanyua
kichwa kumwangalia Saringo. “Bingo!” Stephen alitamka neno hilo na kuamka alipokaa
akazungukazunguka huku akiwa amefungamanisha mikono yake kwa nyuma kisha
akarudi akaketi tena, “Saringo! Unajua Msitu wa Solondo?” Stephen alimrushia swali
Saringo, Saringo akaitikia kwa kutikisa kichwa, Stephen akaendelea “unajua Gereza
Saroge?” Saringo akaitikia tena kwa kutikisa kichwa, “good! We have to face a big
adventure!” .Stephen akachukua zile karatasi na kuzikunja vizuri kisha akampatia
Saringo “tunza, urithi ulioachiwa na babu yako” Saringo alizipokea na kuziweka
mkobani. “Kama tunaamua kufanya utafiti huu, basi na tujiandae vema sisi watatu ila
lazima tupate nguvu ya watu wa ziada kuukabili msitu wa Solondo.” Stephen aliwaeleza
akijua kwamba washaelewa kila kitu, “Stephen!” Hellen aliita “ tueleze kwanza kuna nini
ulichokiona kisha ndiyo tuone pamoja cha kufanya” Hellen alimueleza Stephan. “Ok!
Kadiri ya mchoro huu wakoloni wa kijerumani walipokuwa wanaitawala Deutch Ost
Africa walipata vitu vingi sana ikiwemo mali za aina mbalimbali, kwa hiyo
walichokifanya ni kuzificha ili vizazi na vizazi vyao vija kuchukua na kuupata utajiri huu
mnono, Babu yake Saringo aliifadhi kitu kikubwa asichokijua, huu ni urithi usiopimika
kwa mjukuu wake.” Stephen alimaliza maneno yake na kuwafumbua macho wadada
hawa wawili ambao walibaki kutazamana bila kujua wanachotazamania ni nini!
Walizungumza masuala machache na kukubaliana kuanza shughuli hii ya utafiti wa wapi
zilipo mali hizo, na jalada la utafiti huu wakaliita ‘Msitu wa Solondo’.
Saringo alizama kwenye mawazo mazito sana na daima alijaribu kuunganisha habari hii
aliyoisikia kwa Stephan na ile aliyoelezwa na babu yake mzee Koloto miaka mingi
nyuma, alijaribu kufikiria kama kuingia ndani ya msitu ule ni wazo linalowezekana au la,
kwa maana alishasikia mengi juu ya msitu ule, hakuwahi kufikiri kwenda huko hata siku
moja lakini sasa mawazo makubwa mawili yanagongana kichwani kwake moja likimtaka
aende na lingine likimzuia na kumuonesha hatari zote zinazomkabili, alifikiria juu ya
mali hiyo aliyoisema Stephen ambayo mpaka hapo hakuna alojua ni mali gani
iliyofichwa, Saringo alibaki hajui la kufanya.
Hellen kwa upande wake aliona wazo la kwenda huko ni zuri lakini alifikiria adha za
porini akilinganisha na zile alizopata akiwa huko Amazon, hakujua aamue nini, alifikiri
kuwa endapo watafanikiwa kufika mwisho wa safari yao salama atakuwa ni milionea wa
kutupwa mara alijiuliza itakuwaje endapo asirudi huko akaona kuwa maiti yake
haitaonekana hata kwa ndugu zake, alikata tamaa na kuona kuwa hilo ni wazo hasi kabisa
kwa wakati huo.
Stephen alikuwa na mambo mengi kichwani, alijua kama akifanikisha safari hiyo si tu
atakuwa kitaaluma lakini pia ataukwaa utajiri usokifani kutokana na mali hizo
zilizowekwa porini, alifurahi sana kwa ugunduzi huo hata siku hiyo maisha yake
yalibadilika na kuanza kuishi kama kibopa mmoja hivi, wanafunzi wake walimshangaa
sana alipoingia katika kipindi akiwa na furaha ya ajabu sana, alifundisha kiasi kwamba
muda wa kipindi chake ulikuwa hautoshi, kila saa aliangalia saa yake ile aliyoipenda sana.
Saringo aliona sasa ndoto zake zimetimia baada ya kujua kuwa amepata watu ambao
wameweza kugundua siri ile ambayo yeye hakuijua kirahisi, aliamua kwenda kusoma
katika chuo hicho ili naye apate kujua na kwa bahati mbaya au nzuri anakutana na watu
ambao wanafahamu na wameshafanya tafiti kama hizo. Saringo aliiona hiyo ni bahati
kubwa sana kwake na aliona kile alichokisubiri kwa miaka mingi kitendawili ambacho
hakukijua tatuzo lake sasa kimefika mwisho. Alishusha pumzi kwa nguvu na kujinyoosha
pale juu ya kitanda chake huku akitafakari hili na lile ‘nani wa kutupeleka msituni?’
alijiuliza lakini hakupata jibu, alikumbuka tu mahitaji aliyoambiwa na Stephen ‘mtu
anayejua misitu, mwenye nguvu na mkakamavu, nani! Cjui’ alijiuliza na kujijibu kwa
namna isiyosawa, Saringo alikuwa kama aliyechanganyikiwa katika kichwa chake,
hakujua anachofikiri wala anachokiwaza. Kila alipoamua kuingia ndani ya msitu ule akili
yake ilimtoa na kumuuliza maswali yasiyo na ukomo, alimkumbuka mjomba wake
Golam ambaye mara tatu alijaribu kuingia katika msitu huo wenye maajabu na kukutana
na vitu ambavyo havielezeki na hata mara ya mwisho aalikuwa kama mtu
aliyechanganyikiwa, bangi, gongo vurugu nyingi za mtaani ilikuwa ndiyo kawaida yake.
Lakini hakuna kitu kilichomsumbua sana saringo kama jinsi gani ya kupata sehemu ya
pili ya ramani ile maana ile ilkuwa ni nusu na nusu nyingine je ilikuwa wapi, hilo
lilikuwa swali ambalo halikupata jibu hata kidogo ‘hata kama tukienda msituni tutafikaje
kwenye maficho haya, hatuna sehemu ya pili ya mchoro huu, babu alinambia kipande
kingine kilibaki kwa yule askari wa kundi la pili, mh! Yuko wapi? Alikufa, mzima au
alikitupia wapi au kukificha wapi kipande kile, utata!!!’ Saringo alikosa jibu hata usingizi
ulimchukua.
7
Msituni Msituni
Kutoka juu ya kilima kile Hellen alinguka baada ya kuteleza vibaya alipokuwa katikati ya
msafara ule wa wale watu katili wasio na chembe ya huruma, alining’inia kwa kamba ile
iliyofungwa kiunoni mwake, akiwa amechoka na uso wake umesawajika vibaya kwa
matope, damu zilizoganda zilimfumba macho, njaa ya siku kadhaa haikupata tiba yake,
Hellen alibaki akining’inia kwenye korongo lile huku watesi wale wakimvuta kurudi juu,
msafara ulisimama kwa muda. Hellen alifikishwa juu na kujumuishwa na wengine na
msafara ule uliendelea, ‘Gwerino’ watu wanaokula nyama za watu daima walikuwa
wakifanya matambiko katika mawe na mapango makubwa yaliyopo katikati ya msitu wa
Solondo. Siku ya matambiko ilikuwa imefika na katika siku hii hutoa damu za watu na
kumwaga kwenye mawe yale ambayo wao waliamini Miungu yao ndimo inamoishi, siku
hiyo hawakula kabisa nyama za watu kwa kuwa zote walizipeleka Mzimuni. Msafara
ulizidi kuingia ndani kabisa ya msitu ule watu wapatao kama kumi na tano walifungwa
kamba viunoni na shingoni wakikokotwa huku wakipigwa sana. Hellen kati ya msafara
ule alikuwa amechoka sana hata alitamani afe na asifike anakopelekwa, wenzake
aliowakuta wamefungwa hakuwajua hata mmoja wao hakujuwa hata wametokea wapi,
hakuelewa lugha inayoongelewa na hawa Gwerino, kibaya zaidi alichokishuhudia ni jinsi
wanavyoua watu na kula nyama zao wengine wakinywa damu mbichi, Hellen aliona kuwa hii sio dunia aliyoijua kweli hili ni bara la giza, mara kadhaa amepoteza fahamu na
alipozinduka alijiuliza kwa nini alikuja kwenye safari mbaya kama hii. Msafara
uliendelea, watu walikuwa ni wengi sana wenye mienge mikononi, magongo makubwa,
mavazi yao yakutisha yaliyotengenezwa kawa ngozi wengine walivaa vidani ambavyo
vilikuwa ni mifupa ya vidole vya watu. Kila Hellen alipoona haya alihisi akili yake
kuchanganyika na ubongo, Hellen alichoka kabisa hakuweza kuendelea na safari ile
alianguka tena na sasa hali ilikuwa mbaya zaidi hakuweza kusogea hata kidogo. Msafara
ulisimama na yule kiongozi alishuka kutoka kwenye kiti kile cha enzi kilichobebwa na
wanaume wapatao nane hivi walioshiba kwelikweli. “Kusisi libiko?” yule kiongozi
aliwauliza waongoza msafara kwa sauti ya kutisha yenye kukwaruza akimaanisha
‘kumetokea nini’ huku akiwa anajongea taratibu na fimbo yake ambayo juu imepambwa
na fuvu la binadamu. “Libiko sinzota, kucholo londigo!” alijibiwa na kiongozi wa
msafara akimaanisha ‘hapa kuna kafara moja imechoka haiwezi kufika’ yule kiongozi
akatikisa kichwa kuashiria ameelewa alichoambiwa “Kucholo? Losa fo, libeso Kolilo, a
la to” aliongea kwa kufoka huku akizungukazunguka akimaanisha ‘imechoka, basi na
tuitoe sasa ili miungu ifurahi’ alimaliza na kuigonga chini fimbo yake kwa nguvu na
kupaaza sauti huku mkono wake mmoja ukiwa juu “I lee se?” na msafara wote ukajibu
“seeee!!!!” akimaanisha ‘ni sawa?’ msafara ukajibu ‘sawa’ . wale waliokuwa wakilinda
mateka wale wakamfungua kamba Hellen na kumnyanyua wakasonga nae mbele kidogo,
maana katika utaratibu wao kama kafara haiwezi kufika mzimuni basi mnaweza kutolea
popote na damu yake ndiyo mtayoipeleka mzimuni pamoja na moyo. Walifanya mduara
na wote walianza kugonga fimbo zao chini wakirudiarudia neno lile “Se, se, se, se”.
Hellen alifungwa mikono kwa nyuma na kupigishwa magoti kisha mtu mmoja lisimama
nyuma yake na kumuwekea mti wenye mfano wa kipago cha manati mgongoni na
kaamba moja iliyomzunguka shingoni ikavutwa nyuma mgongo wa Hellen ukapinda na
kifua chake kutangulizwa mbele tayari kwa kazi hiyo. Yule kiongozi alizunguka kwa
mbele na kukabidhiwa ule mti uliochongwa maalumu kwa kazi hiyo akaunyanyua juu na
alipotaka kuushusha kukipasua kifua cha Hellen alisita ghafla, akashusha mti ule taratibu,
watu wote walinyamaza kimya kabisa wakiwa hawajui nini kinachoendelea “Ifime, letose
seleke, ke la londigo, iso losabe?, bease keloya londigo” kiongozi yule aling’aka kwa
hasira akimaanisha ‘laana, hii sio kafara ni mwanamke huyu?, ivueni nguo hii kafara’
watumishi wa kiongozi yule mara moja walimfungua kamba Hellen na kumvua blauzi
yake iliyochakaa kwa uchafu wa aina tofauti, kiongozi yule akamwangalia Hellen na
kumeza funda kubwa la mate alipoona chuchu zile nyekundu zilivyosimama kama
mishale ya saa sita “seleke!” alitamka neno hilo huku akijipiga mkono wake wa kulia
kifuani mara kadhaa akimaanisha ‘laana’, katika utaratibu wao ilikuwa kafara lazima awe
binadamu wa kiume na si wa kike, muda wote walipomkamata Hellen hawakujua kama
ni mwanamke kwa jinsi alivyovaa suruali ile ya jeans, kilichomshtua kiongozi yule ni
jinsi alivyoona vitu vilivyotuna kifuani mwa Hellen ndipo alipofikiri kuwa huyu ni
mwanamke na walipomvua blauzi ile waligundua kuwa ni kweli. Wote walijipiga kifuani
kwa mkono wa kuume wakirudia neno lile ‘seleke’. Hellen aliondolewa kwenye kundi
lile la mateka wengine, akiwa bado amechoka sana alitembea kwa tabu, yule kiongozi
alimwita mmoja wa majemadari wake na kumnong’oneza kitu kisha alitoa ishara msafara
ule uendelee. Hellen aliingizwa kwenye kitu kama pango na kuwekwa pale huku akiwa
amefungwa kamba za miti ili asitoroke. Msafara uliendelea usiku ule na mateka wale sasa
walikuwa wamebaki kumi na nne.Akiwa mle pangoni, Hellen hakuwa na lolote la kufanya alitulia tu akisubiri mwisho
wake ufike, hakujua ni kwa nini alifungwa pale, macho yake yaliendelea kupambana na
giza nene lililotawala msitu ule, mbu na mbung’o walifurajhia kupata damu
wasiyoitarajia, hakika ilikuwa ni sherehe kwao usiku ule. Hellen alishuhudia mwanga ule
wa mienge ya watesi wake ukitokomea msituni, alitafakari sana lakini hakupata njia ya
kumtoa mahali pale, alibaki tu amejikalia huku machozi yakimtoka. Katika msitu ule ni
mivumo ya miti na upepo tu iliyosikika na milio ya ndege wasiyopendwa na binadamu,
bundi. Akiwa katika kutokujielewa Hellen allihisi vichaka vikitikisika aliogopa sana
akakza macho kuangali ni kitu gani kilichokuwa hapo, hakuweza kufanya lolote kwa
kuwa alikuwa amefungwa kwa kamba mikono na miguu yake, alibaki kuangali tu
kitachotokea, mara aliona kama mtu akitokea vichakani mle akinyata kuelekea pango lile,
Hellen alitulia akiangalia nyendo zote za kiumbe kile, mtu yule alizidi kunyata kana
kwamba kuna watu ambao hakupenda wamuone alisogea mpaka karibu kabisa na mlango
wa pango lile, akiwa anamulikwa kwa mbalamwezi hafifu iliyotoke nyuma yake Hellen
hakuweza kuona hata sura ya mtu huyu, alijua tu kwa vyovyote atakuwa ni mmoja wa
atesi wake ambaye labda amerudi kuja kujifaidia teka lile baada ya kujua kuwa alikuwa
ni mwanamke. Hellen alijibanza kwenye kiambaza cha pango lile akiwa kimya kabisa
bila hata kujitikisa alisubiri tu kuona mtu huyo atafanya nini kwake.
[emoji814][emoji814][emoji814]
Amata alipumzika vya kutosha katika kichaka kile ambacho alihifadhiwa na yule
nyani, alinyanyuka na kujinyoosha viungo na kujikuta yuko fiti kwani yule nyani
alimletea chakula pamoja na mizizi mbalimbali ili kumrudishia nguvu ambazo zilipotea
kwa mateso yale, Amata aligeuka huku na kule lakini hakumuona Kingusu eneo lile,
Amata alitoka ndani ya kichaka kile na kuangaza huku na huko akanyanyua mkono wake
na kubana vizuri midomo yake kisha akapiga mbinja kali ya kumuita Kingusu, alisubiri
kidogo lakini hakuona dalili ya Kingusu kuwa mahali pale, alipogeuka kurudi alipokaa
alikuta uta wake na podo viko pale akavichukua na kuvibeba tayari kwa safari lakini
aende wapi? Hata yeye hakujua. Alipiga hatua mbili tatu akasimama tena hakujua bado ni
nini anachotakiwa kufanya, baridi kali ilikuwa ikimpa taabu lakini alijitahidi kuivumilia
japo mara kwa mara alikuwa akitetemeka. Akiwa katika kutafakari hili na lile kwa mbali
aliona kitu kama moshi kikitokea katikati ya msitu ule, Amata aliangalia kwa makini sana
moshi ule na akagundua kuwa kule lazima kuna watu, lakini alibaki kujiuliza maswali
mengi ni watu wa namna gani hao, au ni vile viumbe vya ajabu ndivyo viishivyo huko
lakini hakupata jibu. Aliendelea kuuangalia moshi ule na akaamua kuelekea uko huko ili
akaone kulikoni ‘liwalo na liwe’ alipiga moyo konde na kuanza safari huku moyoni
akiwakumbuka wenzake wote ambao mpaka muda huo hakujua wapi walipo japo mmoja
wao tu, alijiona sasa kabaki peke yake na kilichobaki ni kufanya juu chini kutoka ndani
ya msitu ule na kurudi kijijini kwa kuwa hakujua hata aelekee wapi na upande gani, akili
yote ilikuwa ni kurudi alikotoka lakini sasa hakujua hata ni wapi alipo. Alitembea kwa
hadhari kubwa sana ndani ya msitu huo kuelekea kule alikoona moshi ule alidhamilia
kukabiliana na hatari iwayo yote atakayokutana nayo, mara kwa mara alitembea na
kuangalia nyuma maana alihisi kama kuna watu wanaomfuata lakini alipuuzia tu kwa
kuwa yeye alifahamu mambo mengi sana juu ya misitu. Amata alipita vichakani na
alipopata nafasi mara alikimbia na mara alitembea, alipoendelea mbele mara ghaflaalijikuta akitokea kwenye ukingo kama wa shimo kubwa alisimama na kuangaza macho
huku na huku hakuona mwisho wa bonde lile, bonge kubw lililofunikwa na miti mikubwa
iliyoshonana kwa namna ya ajabu, Amata alipigwa na bumbuwazi hakujua afanyeje
kuendelea na safari yake alipoangalia kule kulikokuwa kukitokea moshi ule aliona bado
unaendelea kufuka lakini mahali bado pakali mbali, alipoangalia bonde lile lilikuwa ni
kubwa na la ajabu hakuwahi kuona kitu kama hicho, Amata aliamua kushuka bondeni
kule kwa kutumia mizizi ya miti mikubwa iliyokuwa ikining’inia aliweka uta na podo
lake vizuri na kuanza kuteremka taratibu, kila mara aliangalia aendako na atokako lakini
aliona hafiki chini, mara ghafla mzizi ule ukakosa nguvu na kukatika Amata alipiga
ukelele na kuanguka kwa kasi kuelekea bondeni alijipiga kwenya baadhi ya miti na
kupata michubuko kadhaa mwilini aliendelea kupiga ukelele lakini hakukuwa na mtu
eneo hilo isipokuwa ndege wa mwituni, kasi ya kuporomoka chini iliongezeka kila nukta
Amata alijua sasa hata akifika chini asingepona, alijikuta anadondokea kwenye kitu kama
nyavu kubwa, hakuamini alichokiona uoto uliyojishonashona kama wavu ulimdaka
Amata naye alikuwa salama, aligeuka kuangali chini akaona sasa si mbali sana kumbe
angeweza hata kuteremka tu kwa kujirusha tu. Alijirusha mpaka chini na kutua kwenye
lundo la majani makavu akatulia dakika kadhaa lakini hakuona chochote, aliendelea
kutembea kwa hadhari kubwa sana na taratibu kuelekea kule alikoona moshi ule, katika
kutembea kule alisikia sauti ya mandege makubwa yakilialia Amata alijua popote penye
ndege wale lazima kuna mzoga, alisimama na kusikiliza kwa muda huku akijaribu na
kuvuta harufu kuona kama kuna harufu ya kitu chochote kilichooza, haikuwa hivyo.
Amata alichomoa moja ya mshale wake katika podo na kuupachika vizuri utani kauvuta
kwa mvuto wa wastani kisha taratibu alinyata kuelekea walikojaa ndege wale
alipokaribia eneo lile alitulia kimya kuangalia vizuri hakuelewa anachokiona kama ni
mzoga wa mtu au mnayama, Amata aliingiwa na woga kidogo aliushusha uta wake
uliokuwa tayari kwa kujeruhi na kuushika kwa mkono mmoja alipoangalia kwa makini
eneo lile hakukuwa na mzoga wowote Amata alisogea na kushuhudia tu madonge ya
damu nzito nzito yametapakaa eneo lile alipigwa na bumbuazi hakuelewa aliyepata
masaibu haya ni binadamu au mnyama aliiangalia damu ile kwa makini sana ilionekena
tukio hilo halikutokea muda mrefu, Amata alitazama huku na huku na kuona michirizi
mingine ya damu imeelekea porini aliifuata kwa hadhari kubwa huku uta wake ukiwa
umeshikwa tayari kwa kutoa pigo, akiangalia nyuma na mbele kwa haraka haraka
aliendelea kufuata damu zile, mbele kidogo alikuta damu zile zimepotea, alisimama na
kuangalia huku akijigeuza taratibu pande zote nne za dunia, akiwa pale chini alihisi kama
tone la maji limemdondokea, Amata akanyanyua kichwa chake kuona kulikoni,
hakuamini macho yake, mwili wa mwanadamu uliyoraluliwa vibaya ulikuwa kwenye
moja ya matawi ya mti ule ukining’inia, Amata aliuangalia mwili ule ukiwa pale juu,
machozi ya uchungu yalimdondoka nguvu zikamuisha na hasira ikaanza kuchukua nafasi
yake, alitamani amuone aliyefanya unyama ule kama ni mnyama au ni kiumbe wa aina
gani, Amata alikwea mti ule na kuuteremsha mwili ule mpaka chini akaulaza na
kuangalia vizuri ‘Stephan!’ alijisemea moyoni huku akilia aliugeuzageuza, akaweka
mkono wake shingoni mwa mwili ule labda angehisi joto lakini mwili ulishatawaliwa na
baridi, alijaribu kugusa kifuani kuona kama kuna dalili ya uhai ah wapi! Amata alijishika
kichwa na kukosa la kufanya ‘man down!’ alijisemea mwenyewe huku akibubujikwa na
machozi mwili wa Stephan ukiwa umelala bila uhai, aikuwa na majeraha ambayo
yalionesha kwa vyovyote kuwa ameuawa na mnyama mkali. Amata alibaki amekaakimya karibu kabisa na mwili ule, akiwa na maswali mengi kichwani mwake akijiuliza na
kujijibu ‘vipi wale wanawake wawili, bado wako hai au nao wamekufa?’
Amata akauchukua mwili ule na kufanya shimo la kumtosha Stephan ambaye kwa sasa
alishakuwa marehemu, akamsitili kwa heshima iliyomfaa, akafanya tuta mahali pale na
kuweka kitu kama msalaba, akasimama mbele ya kaburi lile na kutoa saluti ya heshima
“kwa heri kamanda, Hellen na ndugu zako hawatakuona tena”
Amata akachukua uta wake na kuanza kuondoka, mara akasita na kugeuka nyuma
alikumbuka karatasi zile ambazo Stephen daima alikuwa anazisoma ili kupata uelekeo
sahihi alitazama eneo lile hakuweza kuziona, taratibu aliamua kurudi kule michirizi ya
damu ilipotokea, Mungu si Athumani alizikuta japo zilipeperuka kwa upepo ila
hazikwenda mbali sana pamoja nazo aliokota na ile camera ndogo vyote akavitia kwenye
mfuko wake wa suruali ile ya jela na kuendelea na safari yake, poli kwa poli Amata
alitokea kwenye uwanda mkubwa ulioonekana kama umetadikwa zuria la kijani
aliangalia kwa makini akaokota kipande cha mti na kukirushia lol! Kumbe kuna maji,
akaendelea kuambaaambaa na ukingo wa bwawa hilo lakini lengo lake yeye ilikuwa ni
kuvuka na kuelekea upande wa pili lakini atavukaje ndiyo lilikuwa tatizo, aliendelea
kufuata ukingo ule mpaka alipokuta sehemu nyembamba ambayo aliona hapa angeweza
kuvuka kwa urahisi, alipokuwa akijiandaa mara akaona maji yale yakitikisika, akaangalia
kwa makini hakuona kitu, Amata akarudi nyuma kidogo mbali na mto ule ili kuona nini
kilichopo ndani yake, alikaza macho kutazama magugumaji yale yaliyotuama vizuri juu
ya maji ambapo kama huna subira basi unaweza kutumbukia ukijua ni ardhi kavu. Wazo
likamjia Amata akaingia porini na aliporudi alikuwa na digidigi mkononi akamrusha
majini, La haula! Mamba wakubwa walijinyanyua kugombania nyama ile ambayo hata
kwa vipi isingewatosha wote, Amata akapigwa na butwaa baada ya kuona jinsi
alivyogundua siri hiyo, akakaa chini akiwa hajui la kufanya lakini kichwani mwake
akiwa anafikiri jinsi gani angeweza vuka kwenda upande wa pili ambako lengo lake ni
kufika kule kunakofuka mosho akiamini kabisa lazima kuna binadamu wanaoishi huko
ila mara kwa mara alijiuliza itakuwaje kama watakuwa ni Gorino alijua kuwa huo
utakuwa ndiyo mwisho wake jinsi watakavyomtafuna.
Wazo likamjia, akaingia tena msituni na kufanya mawindo kidogo, akapata mnyama
mkubwa wa angalau, akamkatakata vipande vya kutosa kisha akasogea pale kwenye yale
maji, Amata akamwaga nyamazile kwa ustadi mkubwa na mamba wale walipokuwa
wakigombania yeye alitumia mwanya huo kupita juu ya migongo yao kwa kasi na
kufanikiwa kufika upande wa pili, alianguka kwenye majani kisha akaangalia kazi
aliyoifanya ilivyokuwa na mafanikio, mamba waliendelea kugombania nyama wakati
Amata alishafanikiwa lengo lake, aliamka na kujikung’uta majani yaliyoshikana na nguo
yake na kuendelea na safari kuelekea kule alikouona moshi ule, sasa Amata lijikuta
kwenye msitu wa upande wa pili, msitu wa kutisha wenye mawe mengi na makubwa,
yeye hakujali japo huku uoto mwingi ulikuwa wa miba, alihisi kupambana na hatari
nyingi kuliko alikotoka lakini alijipa moyo na kuendelea kutembea msituni mle japo kwa
taabu sana.
 
N

Na vipi kama vipo na ikatokea vina nia ya kutuangamiza binadamu wote...
Na tena vinao uwezo mkubwa kulko sisi binadamu....
Hii inamaanisha vitatuangamiza na wanadamu tutatoweka wote juu ya uso wa nchi....

Na huenda usiku huu ndio vinapanga kutuangamiza!
Hahahaha hizi akili zangu bhna
Kama vipo na vina nia mbaya Mungu atuepushie mbali vishindwe!
Tatizo Mungu huyo unayemtumainia hayupo
 
MSITU WA SOLINDO

Mtunzi Richard Mwambe

Sehemu 10

Siku tatu baadae....
Ruperto Carola Cafe
Hellen na Stephan walionekana wenye furaha sana hasa kwa wazo lao lile
walilolipata maana walijua wazi kuwa pindi tu watapokamilisha zoezi hili watakuwa juu
sana kitaaluma, kiu yao ya kitafiti hasa juu ya mambo ya kale ilikuwa kubwa sana, lakini
bado hawakujua hasa ni nini wanachotaka kukifanya sasa, ni kitu cha hatari kiasi gani
wanachokifikiria, Hellen alijiuliza tu kama itakuwa safari kama ile ya Amazonia
iliyomchuku wiki tatu kuikamilisha akiishi na wa-Indios na wa-Amazonia ambako
alikutana na hatari ndogondogo tu, Stephan aliichukulia labda itakuwa safari kama ile
ambayo aliifanya huko Hamunatra katika jangwa la Misri ndani ya mapyramid
yaliyosadikiwa kuzikwa watawala wa nchi hiyo nyakati za kale kabisa, wote wawili
walijiona ni mashujaa sana kwa safari zao za utafiti walizozifanya katika maisha yao.
Stephan alishusha taratibu kikombe chake cha kahawa na kukiweka katika kijimeza
kidogo ndani ya mgahawa huo huku akiendelea na maongezi ya hapa na pale na Bi
Hellen. Binti mweusi alikuwa amekaa katika kimoja cha viti vitatu vilivyozunguka meza
hiyo akiwa na makaratasi machache mkononi mwake.
“Naitwa Saringo!” alijitambulisha kwa Hellen na Stephen, hili lilitukia mara baada ya
hawa wawili kujitambulisha kwake. Mazungumzo machache yalipita kati yao hasa ya
kufahamiana na kujuana zaidi, Stephen na Hellen walivutiwa na uchangamfu wa Saringo,
Saringo aliwaambia mambo mengi sana juu ya Africa hasa eneo ambalo yeye anatoka
Deutche Ost Africa, Stephen na Hellen walivutiwa sana na habari za huko na walipenda
kujua kama ni kweli au ni za kutunga tu za mababu wa kale. Saringo aliwasimulia mengi
sana hasa aliyosimuliwa na babu yake mzee Koloto, baada ya mazungumzo hayo saringo
aliwagusia juu ya stori ya babu yake alipokuwa askari wa wajerumani na alivyokuwa
akiongoza misafara ya wapagazi kuingia misituni na kuficha vitu visivyojulikana huko
kisha kuuawa, “No! Kwa nini waliwaua? Lazima kuna kitu” Hellen aliuliza kwa mshtuko
“Labda hawakutaka warudi tena huko, kuhofia kuchukua mali zao” Stephen alijibu
“ndiyo, ndiyo, hakika kabisa babu alinambia waliwaua ili wasiweze kurudi, lakini yeye
alinusurika na kufanikiwa kubaki hai” Saringo aliwaeleza na kutoa zile karatasi chache zenye michoro ya ajabu na maandishi ya kijerumani. Kwa Stephan haikuwa kitu kigeni
michoro ile kwani aliitumia sana alipokwenda huko Hamunatra, kwa haraka haraka
aliweza kuisoma na kutambua kilichofichwa katika michoro ile.
Stephen alitikisa kichwa kuashiria amegundua kitu, akanyanyua kikombe chake cha
kahawa na kunywa kidogo. “Vipi? Stephen!” Hellen aliuliza kwa shauku ya kutaka
kujua. Stephen alitikisa tena kichwa na kugeuza geuza mdomo wake, mara alionekana
kukunja uso, mara kutabasamu, akaiweka ile karatasi chakavumezani, na kunyanyua
kichwa kumwangalia Saringo. “Bingo!” Stephen alitamka neno hilo na kuamka alipokaa
akazungukazunguka huku akiwa amefungamanisha mikono yake kwa nyuma kisha
akarudi akaketi tena, “Saringo! Unajua Msitu wa Solondo?” Stephen alimrushia swali
Saringo, Saringo akaitikia kwa kutikisa kichwa, Stephen akaendelea “unajua Gereza
Saroge?” Saringo akaitikia tena kwa kutikisa kichwa, “good! We have to face a big
adventure!” .Stephen akachukua zile karatasi na kuzikunja vizuri kisha akampatia
Saringo “tunza, urithi ulioachiwa na babu yako” Saringo alizipokea na kuziweka
mkobani. “Kama tunaamua kufanya utafiti huu, basi na tujiandae vema sisi watatu ila
lazima tupate nguvu ya watu wa ziada kuukabili msitu wa Solondo.” Stephen aliwaeleza
akijua kwamba washaelewa kila kitu, “Stephen!” Hellen aliita “ tueleze kwanza kuna nini
ulichokiona kisha ndiyo tuone pamoja cha kufanya” Hellen alimueleza Stephan. “Ok!
Kadiri ya mchoro huu wakoloni wa kijerumani walipokuwa wanaitawala Deutch Ost
Africa walipata vitu vingi sana ikiwemo mali za aina mbalimbali, kwa hiyo
walichokifanya ni kuzificha ili vizazi na vizazi vyao vija kuchukua na kuupata utajiri huu
mnono, Babu yake Saringo aliifadhi kitu kikubwa asichokijua, huu ni urithi usiopimika
kwa mjukuu wake.” Stephen alimaliza maneno yake na kuwafumbua macho wadada
hawa wawili ambao walibaki kutazamana bila kujua wanachotazamania ni nini!
Walizungumza masuala machache na kukubaliana kuanza shughuli hii ya utafiti wa wapi
zilipo mali hizo, na jalada la utafiti huu wakaliita ‘Msitu wa Solondo’.
Saringo alizama kwenye mawazo mazito sana na daima alijaribu kuunganisha habari hii
aliyoisikia kwa Stephan na ile aliyoelezwa na babu yake mzee Koloto miaka mingi
nyuma, alijaribu kufikiria kama kuingia ndani ya msitu ule ni wazo linalowezekana au la,
kwa maana alishasikia mengi juu ya msitu ule, hakuwahi kufikiri kwenda huko hata siku
moja lakini sasa mawazo makubwa mawili yanagongana kichwani kwake moja likimtaka
aende na lingine likimzuia na kumuonesha hatari zote zinazomkabili, alifikiria juu ya
mali hiyo aliyoisema Stephen ambayo mpaka hapo hakuna alojua ni mali gani
iliyofichwa, Saringo alibaki hajui la kufanya.
Hellen kwa upande wake aliona wazo la kwenda huko ni zuri lakini alifikiria adha za
porini akilinganisha na zile alizopata akiwa huko Amazon, hakujua aamue nini, alifikiri
kuwa endapo watafanikiwa kufika mwisho wa safari yao salama atakuwa ni milionea wa
kutupwa mara alijiuliza itakuwaje endapo asirudi huko akaona kuwa maiti yake
haitaonekana hata kwa ndugu zake, alikata tamaa na kuona kuwa hilo ni wazo hasi kabisa
kwa wakati huo.
Stephen alikuwa na mambo mengi kichwani, alijua kama akifanikisha safari hiyo si tu
atakuwa kitaaluma lakini pia ataukwaa utajiri usokifani kutokana na mali hizo
zilizowekwa porini, alifurahi sana kwa ugunduzi huo hata siku hiyo maisha yake
yalibadilika na kuanza kuishi kama kibopa mmoja hivi, wanafunzi wake walimshangaa
sana alipoingia katika kipindi akiwa na furaha ya ajabu sana, alifundisha kiasi kwamba
muda wa kipindi chake ulikuwa hautoshi, kila saa aliangalia saa yake ile aliyoipenda sana.
Saringo aliona sasa ndoto zake zimetimia baada ya kujua kuwa amepata watu ambao
wameweza kugundua siri ile ambayo yeye hakuijua kirahisi, aliamua kwenda kusoma
katika chuo hicho ili naye apate kujua na kwa bahati mbaya au nzuri anakutana na watu
ambao wanafahamu na wameshafanya tafiti kama hizo. Saringo aliiona hiyo ni bahati
kubwa sana kwake na aliona kile alichokisubiri kwa miaka mingi kitendawili ambacho
hakukijua tatuzo lake sasa kimefika mwisho. Alishusha pumzi kwa nguvu na kujinyoosha
pale juu ya kitanda chake huku akitafakari hili na lile ‘nani wa kutupeleka msituni?’
alijiuliza lakini hakupata jibu, alikumbuka tu mahitaji aliyoambiwa na Stephen ‘mtu
anayejua misitu, mwenye nguvu na mkakamavu, nani! Cjui’ alijiuliza na kujijibu kwa
namna isiyosawa, Saringo alikuwa kama aliyechanganyikiwa katika kichwa chake,
hakujua anachofikiri wala anachokiwaza. Kila alipoamua kuingia ndani ya msitu ule akili
yake ilimtoa na kumuuliza maswali yasiyo na ukomo, alimkumbuka mjomba wake
Golam ambaye mara tatu alijaribu kuingia katika msitu huo wenye maajabu na kukutana
na vitu ambavyo havielezeki na hata mara ya mwisho aalikuwa kama mtu
aliyechanganyikiwa, bangi, gongo vurugu nyingi za mtaani ilikuwa ndiyo kawaida yake.
Lakini hakuna kitu kilichomsumbua sana saringo kama jinsi gani ya kupata sehemu ya
pili ya ramani ile maana ile ilkuwa ni nusu na nusu nyingine je ilikuwa wapi, hilo
lilikuwa swali ambalo halikupata jibu hata kidogo ‘hata kama tukienda msituni tutafikaje
kwenye maficho haya, hatuna sehemu ya pili ya mchoro huu, babu alinambia kipande
kingine kilibaki kwa yule askari wa kundi la pili, mh! Yuko wapi? Alikufa, mzima au
alikitupia wapi au kukificha wapi kipande kile, utata!!!’ Saringo alikosa jibu hata usingizi
ulimchukua.
7
Msituni Msituni
Kutoka juu ya kilima kile Hellen alinguka baada ya kuteleza vibaya alipokuwa katikati ya
msafara ule wa wale watu katili wasio na chembe ya huruma, alining’inia kwa kamba ile
iliyofungwa kiunoni mwake, akiwa amechoka na uso wake umesawajika vibaya kwa
matope, damu zilizoganda zilimfumba macho, njaa ya siku kadhaa haikupata tiba yake,
Hellen alibaki akining’inia kwenye korongo lile huku watesi wale wakimvuta kurudi juu,
msafara ulisimama kwa muda. Hellen alifikishwa juu na kujumuishwa na wengine na
msafara ule uliendelea, ‘Gwerino’ watu wanaokula nyama za watu daima walikuwa
wakifanya matambiko katika mawe na mapango makubwa yaliyopo katikati ya msitu wa
Solondo. Siku ya matambiko ilikuwa imefika na katika siku hii hutoa damu za watu na
kumwaga kwenye mawe yale ambayo wao waliamini Miungu yao ndimo inamoishi, siku
hiyo hawakula kabisa nyama za watu kwa kuwa zote walizipeleka Mzimuni. Msafara
ulizidi kuingia ndani kabisa ya msitu ule watu wapatao kama kumi na tano walifungwa
kamba viunoni na shingoni wakikokotwa huku wakipigwa sana. Hellen kati ya msafara
ule alikuwa amechoka sana hata alitamani afe na asifike anakopelekwa, wenzake
aliowakuta wamefungwa hakuwajua hata mmoja wao hakujuwa hata wametokea wapi,
hakuelewa lugha inayoongelewa na hawa Gwerino, kibaya zaidi alichokishuhudia ni jinsi
wanavyoua watu na kula nyama zao wengine wakinywa damu mbichi, Hellen aliona kuwa hii sio dunia aliyoijua kweli hili ni bara la giza, mara kadhaa amepoteza fahamu na
alipozinduka alijiuliza kwa nini alikuja kwenye safari mbaya kama hii. Msafara
uliendelea, watu walikuwa ni wengi sana wenye mienge mikononi, magongo makubwa,
mavazi yao yakutisha yaliyotengenezwa kawa ngozi wengine walivaa vidani ambavyo
vilikuwa ni mifupa ya vidole vya watu. Kila Hellen alipoona haya alihisi akili yake
kuchanganyika na ubongo, Hellen alichoka kabisa hakuweza kuendelea na safari ile
alianguka tena na sasa hali ilikuwa mbaya zaidi hakuweza kusogea hata kidogo. Msafara
ulisimama na yule kiongozi alishuka kutoka kwenye kiti kile cha enzi kilichobebwa na
wanaume wapatao nane hivi walioshiba kwelikweli. “Kusisi libiko?” yule kiongozi
aliwauliza waongoza msafara kwa sauti ya kutisha yenye kukwaruza akimaanisha
‘kumetokea nini’ huku akiwa anajongea taratibu na fimbo yake ambayo juu imepambwa
na fuvu la binadamu. “Libiko sinzota, kucholo londigo!” alijibiwa na kiongozi wa
msafara akimaanisha ‘hapa kuna kafara moja imechoka haiwezi kufika’ yule kiongozi
akatikisa kichwa kuashiria ameelewa alichoambiwa “Kucholo? Losa fo, libeso Kolilo, a
la to” aliongea kwa kufoka huku akizungukazunguka akimaanisha ‘imechoka, basi na
tuitoe sasa ili miungu ifurahi’ alimaliza na kuigonga chini fimbo yake kwa nguvu na
kupaaza sauti huku mkono wake mmoja ukiwa juu “I lee se?” na msafara wote ukajibu
“seeee!!!!” akimaanisha ‘ni sawa?’ msafara ukajibu ‘sawa’ . wale waliokuwa wakilinda
mateka wale wakamfungua kamba Hellen na kumnyanyua wakasonga nae mbele kidogo,
maana katika utaratibu wao kama kafara haiwezi kufika mzimuni basi mnaweza kutolea
popote na damu yake ndiyo mtayoipeleka mzimuni pamoja na moyo. Walifanya mduara
na wote walianza kugonga fimbo zao chini wakirudiarudia neno lile “Se, se, se, se”.
Hellen alifungwa mikono kwa nyuma na kupigishwa magoti kisha mtu mmoja lisimama
nyuma yake na kumuwekea mti wenye mfano wa kipago cha manati mgongoni na
kaamba moja iliyomzunguka shingoni ikavutwa nyuma mgongo wa Hellen ukapinda na
kifua chake kutangulizwa mbele tayari kwa kazi hiyo. Yule kiongozi alizunguka kwa
mbele na kukabidhiwa ule mti uliochongwa maalumu kwa kazi hiyo akaunyanyua juu na
alipotaka kuushusha kukipasua kifua cha Hellen alisita ghafla, akashusha mti ule taratibu,
watu wote walinyamaza kimya kabisa wakiwa hawajui nini kinachoendelea “Ifime, letose
seleke, ke la londigo, iso losabe?, bease keloya londigo” kiongozi yule aling’aka kwa
hasira akimaanisha ‘laana, hii sio kafara ni mwanamke huyu?, ivueni nguo hii kafara’
watumishi wa kiongozi yule mara moja walimfungua kamba Hellen na kumvua blauzi
yake iliyochakaa kwa uchafu wa aina tofauti, kiongozi yule akamwangalia Hellen na
kumeza funda kubwa la mate alipoona chuchu zile nyekundu zilivyosimama kama
mishale ya saa sita “seleke!” alitamka neno hilo huku akijipiga mkono wake wa kulia
kifuani mara kadhaa akimaanisha ‘laana’, katika utaratibu wao ilikuwa kafara lazima awe
binadamu wa kiume na si wa kike, muda wote walipomkamata Hellen hawakujua kama
ni mwanamke kwa jinsi alivyovaa suruali ile ya jeans, kilichomshtua kiongozi yule ni
jinsi alivyoona vitu vilivyotuna kifuani mwa Hellen ndipo alipofikiri kuwa huyu ni
mwanamke na walipomvua blauzi ile waligundua kuwa ni kweli. Wote walijipiga kifuani
kwa mkono wa kuume wakirudia neno lile ‘seleke’. Hellen aliondolewa kwenye kundi
lile la mateka wengine, akiwa bado amechoka sana alitembea kwa tabu, yule kiongozi
alimwita mmoja wa majemadari wake na kumnong’oneza kitu kisha alitoa ishara msafara
ule uendelee. Hellen aliingizwa kwenye kitu kama pango na kuwekwa pale huku akiwa
amefungwa kamba za miti ili asitoroke. Msafara uliendelea usiku ule na mateka wale sasa
walikuwa wamebaki kumi na nne.Akiwa mle pangoni, Hellen hakuwa na lolote la kufanya alitulia tu akisubiri mwisho
wake ufike, hakujua ni kwa nini alifungwa pale, macho yake yaliendelea kupambana na
giza nene lililotawala msitu ule, mbu na mbung’o walifurajhia kupata damu
wasiyoitarajia, hakika ilikuwa ni sherehe kwao usiku ule. Hellen alishuhudia mwanga ule
wa mienge ya watesi wake ukitokomea msituni, alitafakari sana lakini hakupata njia ya
kumtoa mahali pale, alibaki tu amejikalia huku machozi yakimtoka. Katika msitu ule ni
mivumo ya miti na upepo tu iliyosikika na milio ya ndege wasiyopendwa na binadamu,
bundi. Akiwa katika kutokujielewa Hellen allihisi vichaka vikitikisika aliogopa sana
akakza macho kuangali ni kitu gani kilichokuwa hapo, hakuweza kufanya lolote kwa
kuwa alikuwa amefungwa kwa kamba mikono na miguu yake, alibaki kuangali tu
kitachotokea, mara aliona kama mtu akitokea vichakani mle akinyata kuelekea pango lile,
Hellen alitulia akiangalia nyendo zote za kiumbe kile, mtu yule alizidi kunyata kana
kwamba kuna watu ambao hakupenda wamuone alisogea mpaka karibu kabisa na mlango
wa pango lile, akiwa anamulikwa kwa mbalamwezi hafifu iliyotoke nyuma yake Hellen
hakuweza kuona hata sura ya mtu huyu, alijua tu kwa vyovyote atakuwa ni mmoja wa
atesi wake ambaye labda amerudi kuja kujifaidia teka lile baada ya kujua kuwa alikuwa
ni mwanamke. Hellen alijibanza kwenye kiambaza cha pango lile akiwa kimya kabisa
bila hata kujitikisa alisubiri tu kuona mtu huyo atafanya nini kwake.
[emoji814][emoji814][emoji814]
Amata alipumzika vya kutosha katika kichaka kile ambacho alihifadhiwa na yule
nyani, alinyanyuka na kujinyoosha viungo na kujikuta yuko fiti kwani yule nyani
alimletea chakula pamoja na mizizi mbalimbali ili kumrudishia nguvu ambazo zilipotea
kwa mateso yale, Amata aligeuka huku na kule lakini hakumuona Kingusu eneo lile,
Amata alitoka ndani ya kichaka kile na kuangaza huku na huko akanyanyua mkono wake
na kubana vizuri midomo yake kisha akapiga mbinja kali ya kumuita Kingusu, alisubiri
kidogo lakini hakuona dalili ya Kingusu kuwa mahali pale, alipogeuka kurudi alipokaa
alikuta uta wake na podo viko pale akavichukua na kuvibeba tayari kwa safari lakini
aende wapi? Hata yeye hakujua. Alipiga hatua mbili tatu akasimama tena hakujua bado ni
nini anachotakiwa kufanya, baridi kali ilikuwa ikimpa taabu lakini alijitahidi kuivumilia
japo mara kwa mara alikuwa akitetemeka. Akiwa katika kutafakari hili na lile kwa mbali
aliona kitu kama moshi kikitokea katikati ya msitu ule, Amata aliangalia kwa makini sana
moshi ule na akagundua kuwa kule lazima kuna watu, lakini alibaki kujiuliza maswali
mengi ni watu wa namna gani hao, au ni vile viumbe vya ajabu ndivyo viishivyo huko
lakini hakupata jibu. Aliendelea kuuangalia moshi ule na akaamua kuelekea uko huko ili
akaone kulikoni ‘liwalo na liwe’ alipiga moyo konde na kuanza safari huku moyoni
akiwakumbuka wenzake wote ambao mpaka muda huo hakujua wapi walipo japo mmoja
wao tu, alijiona sasa kabaki peke yake na kilichobaki ni kufanya juu chini kutoka ndani
ya msitu ule na kurudi kijijini kwa kuwa hakujua hata aelekee wapi na upande gani, akili
yote ilikuwa ni kurudi alikotoka lakini sasa hakujua hata ni wapi alipo. Alitembea kwa
hadhari kubwa sana ndani ya msitu huo kuelekea kule alikoona moshi ule alidhamilia
kukabiliana na hatari iwayo yote atakayokutana nayo, mara kwa mara alitembea na
kuangalia nyuma maana alihisi kama kuna watu wanaomfuata lakini alipuuzia tu kwa
kuwa yeye alifahamu mambo mengi sana juu ya misitu. Amata alipita vichakani na
alipopata nafasi mara alikimbia na mara alitembea, alipoendelea mbele mara ghaflaalijikuta akitokea kwenye ukingo kama wa shimo kubwa alisimama na kuangaza macho
huku na huku hakuona mwisho wa bonde lile, bonge kubw lililofunikwa na miti mikubwa
iliyoshonana kwa namna ya ajabu, Amata alipigwa na bumbuwazi hakujua afanyeje
kuendelea na safari yake alipoangalia kule kulikokuwa kukitokea moshi ule aliona bado
unaendelea kufuka lakini mahali bado pakali mbali, alipoangalia bonde lile lilikuwa ni
kubwa na la ajabu hakuwahi kuona kitu kama hicho, Amata aliamua kushuka bondeni
kule kwa kutumia mizizi ya miti mikubwa iliyokuwa ikining’inia aliweka uta na podo
lake vizuri na kuanza kuteremka taratibu, kila mara aliangalia aendako na atokako lakini
aliona hafiki chini, mara ghafla mzizi ule ukakosa nguvu na kukatika Amata alipiga
ukelele na kuanguka kwa kasi kuelekea bondeni alijipiga kwenya baadhi ya miti na
kupata michubuko kadhaa mwilini aliendelea kupiga ukelele lakini hakukuwa na mtu
eneo hilo isipokuwa ndege wa mwituni, kasi ya kuporomoka chini iliongezeka kila nukta
Amata alijua sasa hata akifika chini asingepona, alijikuta anadondokea kwenye kitu kama
nyavu kubwa, hakuamini alichokiona uoto uliyojishonashona kama wavu ulimdaka
Amata naye alikuwa salama, aligeuka kuangali chini akaona sasa si mbali sana kumbe
angeweza hata kuteremka tu kwa kujirusha tu. Alijirusha mpaka chini na kutua kwenye
lundo la majani makavu akatulia dakika kadhaa lakini hakuona chochote, aliendelea
kutembea kwa hadhari kubwa sana na taratibu kuelekea kule alikoona moshi ule, katika
kutembea kule alisikia sauti ya mandege makubwa yakilialia Amata alijua popote penye
ndege wale lazima kuna mzoga, alisimama na kusikiliza kwa muda huku akijaribu na
kuvuta harufu kuona kama kuna harufu ya kitu chochote kilichooza, haikuwa hivyo.
Amata alichomoa moja ya mshale wake katika podo na kuupachika vizuri utani kauvuta
kwa mvuto wa wastani kisha taratibu alinyata kuelekea walikojaa ndege wale
alipokaribia eneo lile alitulia kimya kuangalia vizuri hakuelewa anachokiona kama ni
mzoga wa mtu au mnayama, Amata aliingiwa na woga kidogo aliushusha uta wake
uliokuwa tayari kwa kujeruhi na kuushika kwa mkono mmoja alipoangalia kwa makini
eneo lile hakukuwa na mzoga wowote Amata alisogea na kushuhudia tu madonge ya
damu nzito nzito yametapakaa eneo lile alipigwa na bumbuazi hakuelewa aliyepata
masaibu haya ni binadamu au mnyama aliiangalia damu ile kwa makini sana ilionekena
tukio hilo halikutokea muda mrefu, Amata alitazama huku na huku na kuona michirizi
mingine ya damu imeelekea porini aliifuata kwa hadhari kubwa huku uta wake ukiwa
umeshikwa tayari kwa kutoa pigo, akiangalia nyuma na mbele kwa haraka haraka
aliendelea kufuata damu zile, mbele kidogo alikuta damu zile zimepotea, alisimama na
kuangalia huku akijigeuza taratibu pande zote nne za dunia, akiwa pale chini alihisi kama
tone la maji limemdondokea, Amata akanyanyua kichwa chake kuona kulikoni,
hakuamini macho yake, mwili wa mwanadamu uliyoraluliwa vibaya ulikuwa kwenye
moja ya matawi ya mti ule ukining’inia, Amata aliuangalia mwili ule ukiwa pale juu,
machozi ya uchungu yalimdondoka nguvu zikamuisha na hasira ikaanza kuchukua nafasi
yake, alitamani amuone aliyefanya unyama ule kama ni mnyama au ni kiumbe wa aina
gani, Amata alikwea mti ule na kuuteremsha mwili ule mpaka chini akaulaza na
kuangalia vizuri ‘Stephan!’ alijisemea moyoni huku akilia aliugeuzageuza, akaweka
mkono wake shingoni mwa mwili ule labda angehisi joto lakini mwili ulishatawaliwa na
baridi, alijaribu kugusa kifuani kuona kama kuna dalili ya uhai ah wapi! Amata alijishika
kichwa na kukosa la kufanya ‘man down!’ alijisemea mwenyewe huku akibubujikwa na
machozi mwili wa Stephan ukiwa umelala bila uhai, aikuwa na majeraha ambayo
yalionesha kwa vyovyote kuwa ameuawa na mnyama mkali. Amata alibaki amekaakimya karibu kabisa na mwili ule, akiwa na maswali mengi kichwani mwake akijiuliza na
kujijibu ‘vipi wale wanawake wawili, bado wako hai au nao wamekufa?’
Amata akauchukua mwili ule na kufanya shimo la kumtosha Stephan ambaye kwa sasa
alishakuwa marehemu, akamsitili kwa heshima iliyomfaa, akafanya tuta mahali pale na
kuweka kitu kama msalaba, akasimama mbele ya kaburi lile na kutoa saluti ya heshima
“kwa heri kamanda, Hellen na ndugu zako hawatakuona tena”
Amata akachukua uta wake na kuanza kuondoka, mara akasita na kugeuka nyuma
alikumbuka karatasi zile ambazo Stephen daima alikuwa anazisoma ili kupata uelekeo
sahihi alitazama eneo lile hakuweza kuziona, taratibu aliamua kurudi kule michirizi ya
damu ilipotokea, Mungu si Athumani alizikuta japo zilipeperuka kwa upepo ila
hazikwenda mbali sana pamoja nazo aliokota na ile camera ndogo vyote akavitia kwenye
mfuko wake wa suruali ile ya jela na kuendelea na safari yake, poli kwa poli Amata
alitokea kwenye uwanda mkubwa ulioonekana kama umetadikwa zuria la kijani
aliangalia kwa makini akaokota kipande cha mti na kukirushia lol! Kumbe kuna maji,
akaendelea kuambaaambaa na ukingo wa bwawa hilo lakini lengo lake yeye ilikuwa ni
kuvuka na kuelekea upande wa pili lakini atavukaje ndiyo lilikuwa tatizo, aliendelea
kufuata ukingo ule mpaka alipokuta sehemu nyembamba ambayo aliona hapa angeweza
kuvuka kwa urahisi, alipokuwa akijiandaa mara akaona maji yale yakitikisika, akaangalia
kwa makini hakuona kitu, Amata akarudi nyuma kidogo mbali na mto ule ili kuona nini
kilichopo ndani yake, alikaza macho kutazama magugumaji yale yaliyotuama vizuri juu
ya maji ambapo kama huna subira basi unaweza kutumbukia ukijua ni ardhi kavu. Wazo
likamjia Amata akaingia porini na aliporudi alikuwa na digidigi mkononi akamrusha
majini, La haula! Mamba wakubwa walijinyanyua kugombania nyama ile ambayo hata
kwa vipi isingewatosha wote, Amata akapigwa na butwaa baada ya kuona jinsi
alivyogundua siri hiyo, akakaa chini akiwa hajui la kufanya lakini kichwani mwake
akiwa anafikiri jinsi gani angeweza vuka kwenda upande wa pili ambako lengo lake ni
kufika kule kunakofuka mosho akiamini kabisa lazima kuna binadamu wanaoishi huko
ila mara kwa mara alijiuliza itakuwaje kama watakuwa ni Gorino alijua kuwa huo
utakuwa ndiyo mwisho wake jinsi watakavyomtafuna.
Wazo likamjia, akaingia tena msituni na kufanya mawindo kidogo, akapata mnyama
mkubwa wa angalau, akamkatakata vipande vya kutosa kisha akasogea pale kwenye yale
maji, Amata akamwaga nyamazile kwa ustadi mkubwa na mamba wale walipokuwa
wakigombania yeye alitumia mwanya huo kupita juu ya migongo yao kwa kasi na
kufanikiwa kufika upande wa pili, alianguka kwenye majani kisha akaangalia kazi
aliyoifanya ilivyokuwa na mafanikio, mamba waliendelea kugombania nyama wakati
Amata alishafanikiwa lengo lake, aliamka na kujikung’uta majani yaliyoshikana na nguo
yake na kuendelea na safari kuelekea kule alikouona moshi ule, sasa Amata lijikuta
kwenye msitu wa upande wa pili, msitu wa kutisha wenye mawe mengi na makubwa,
yeye hakujali japo huku uoto mwingi ulikuwa wa miba, alihisi kupambana na hatari
nyingi kuliko alikotoka lakini alijipa moyo na kuendelea kutembea msituni mle japo kwa
taabu sana.
Asanteh mzee wa site
 
MSITU WA SOLONDO

Mtunzi Richard Mwambe

Sehemu 11

Msafara wa Gorino ulitokomea katikati ya msitu, na kulipopambazuka ulikuwa
umefika mahali hasa palipokusudiwa, katika utaratibu wao walitakiwa kutoa kafara usiku
wa saba baada ya jua kupatwa na mwezi. Tukio hilo liliwafanya wao waamini kuwa
Mungu wao amekasirika hivyo inampasa kuombwa msamaha kwa kumwaga damu na
kula nyama, daima walimtoa yoyote kati yao ikiwa hawajapata binadamu wa kumtoa
kafala kutoka jamii nyingine. Safari hii waliamini kuwa Mungu wao ‘Kolilo’ atafurahi
kwa kupata damu nyingi hivyo kuwaondolea laana ‘seleke’ kwa kuwa walikamata
msafara wa waarabu waliokuwa wakipita huko Solondo katika pilikapilika za kutafuna
hazina ile ya kale, tamaa mbaya. Gorino waliwateka wote na kuwatesa sana, waliwaua na
kugawana nyama kwa ajili ya kitoweo, baada ya kuona kitendo kile cha jua kupatwa na
mwezi walijua Kolilo amechukia hivyo inabidi atolewe sadaka ya msamaha, ndipo
walipoazimi waliobaki wote wapelekwe mzimuni na watolewe kafara safi.
Katika pilikapilika za kulinda imaya yao ndipo walipomkuta Hellen kando ya mto akiwa
amekaa na hajui la kufanya. Hellen alipowaona akajua sasa amepata msaada kumbe
kaingia mikononi mwa Gorino ‘wala watu’. Binadamu hawa wa ajabu walifurahia kupata
windo bila jasho, Hellen aliongea lugha zote lakini wenzake wakabaki kucheka maana
hawakuelewa, walianza kumtomasatomasa wakitaka kugawana minofu ya kiumbe huyu
aliyenona sana na wengi wao walivutiwa na nyama ya matako na mapaja kwa kuwa
yalijaa hasa, lakini kabla hawajafikia azma yao ya kumcharangacharanga alitokea
mwenzao ambaye aliwaamuru windo lile lipelekwe kwa kiongozi wao kwanza halafu
yeye aamue ni nini cha kufanya.
Walimfunga kamba Hellen na kuenda nae katika ngome yao, moja kwa moja
walimfikisha kwa kiongozi wao aliyejulikana kama ‘Kelume’ kwa cheo chake, yeye
akaamua kuwa Hellen achanganywe na wale waarabu wengine ili asubiri zamu yake ya
kuliwa nyama, mpaka hapo hakuna aliyegundua kuwa huyu ni mwanamke. Hellen
hakujua la kufanya zaidi ya kupata mshtuko alipoona matukio yanayoendelea pale,
mauaji ya kinjyama huku ngoma ya ajabu ikichezwa na wanawake kwa wanaume ambao
kwa ujumla ni kama walikuwa uchi kwani walijifunika tu sehemu za siri. Ngoma hii
ilimkera sana Hellen kwa jinsi ilivyochezwa, kwake aliona watu hawa hawana hata
chembe ya adabu lakini wenzake kwao ilikuwa ni burudani na maisha ya kawaida, kwani
mara kadhaa alishuhudia wakifanya ngono bila kujali na wenzao wakishangilia, mara
waliletewa nyama kwenye vyungu vikubwa tu na kula wakifurahi, nyama ya watu.
Hellen alizimia alipoona jinsi Kelume anavyoua mmoja wa mateka na kumtoa moyo
kisha kushangilia sana na kuilamba damu iliyouzunguka moyo huo, wengine wakinya
damu katika bakuli. Hellen alihisi kufika dunia ya ajabu, alizidiwa na harufu mbaya ya
damu, ubongo wake ulichafuka lwa luona matukio yote yale, alizimia mara kwa mara.
Hata alipofungiwa katika lile pango kwake ilikuwa ni shida tu maana alijua wazi kuwa
wakimaliza kazi yao huko watarudi kwake, alitamani afe lakini haikuwezekana, akimbie
lakini alifungwa kamba, hakuna msaada.
“Lito, seki londigo Kolilo isom” amri ilitoka kwa kelume akimaanisha ‘simama, kafara
ya kolilo imefika’ msafara ulisimama alfajiri ile katika jiwe kubwa jeusi lililochongoka
juu kama kichuguu cha mchwa, hapa ndipo walipotolea kafara yao, nje yake kulikuwa na
mawe mengine mengi mengi yaliyojipanga katika mtindo tofauti. Msafara uliweka kambi
kusubiri giza liingie ili kalamu ya kafara itolewe, kwa kuwa kafara yao hutokewa tu
wakati wa mbalamwezi na si vinginevyo. Mateka wale walichukuliwa na kuwekwa
kwenye pango maalumu ndani ya jiwe lile ili kusubiri wakati, huku nje gorino wakiendelea na ibada zao kwa Kolilo
Missed article !!!!!
Amata alipiga ukelele baada ya kumuona swahiba wake Golama katika dimbwi la
mahaba na wasichana wale akataka kwenda katika chumba kile lakini alizuiwa na bibi
yule “huwezi fika walipo” bibi kizee alimwueleza Amata. “Nyie binadamu mnatusumbua
sana, kuna mambo mengi tunataka kwenu hasa hisia na akili” bibi kizee alimueleza
Amata huku akimuongoza kusikojulikana na nyuma yao kulifiatiwa na mabinti wale
warembo wenye nywele zinazoning’inia mpaka chini ya viuno vyao. Walifika eneo tulivu
sana lililojaa kila aina ya ufahari, Amata alikaribishwa kuketi katika jiwe moja kati ya
mengi yaliyokuwa hapo. Na mabinti wale waliowafuata waliwazunguka na kuketi chini,
Amata aliwatolea macho mabinti wale muda wote “Amata!” bibi kizee aliita “jambo
mnalolifanya ni jambo la hatari sana, sisi wenyewe na maarifa yetu yote ya nguvu ya
chini hatuwezi jaribu, tumeshashindwa muda mrefu” bibi kizee aliendelea kumueleza
Amata naye alisikiliza kwa makini “Gorino ni viumbe hatari, si binadamu wale hata sisi
wametuzidi uwezo” bibi kizee aliendelea kumuasa Amata, Amata alimsikiliza huku
akipepesa macho yake huku na kule. “Tamaa yenu binadamu ndiyo inawafikisha pabaya,
kwa nini hamridhiki?” bibi aliendelea kuongea na Amata ambaye kwa wakati huo akili
yake haikuwa hapo hata kidogo. “Bibi, naomba unisaidie, bila shaka wewe unajua
wenzangu wote walipo” Amata alimkatisha bibi kizee. Cheko la ajabu lilimtoka bibi yule
“Kijana nitakusaidia lakini kwa sharti moja, na wewe unisaidie” bibi alijibu na kutoa la
moyoni “sema bibi, nipo tayari kukusaidia” Amata alidakia na kujibu, “mimi nataka roho
hai ya Kelume” bibi alitoa ombi lake “Kelume! Ni nani huyo?” Amata kwa mshangao
aliuliza “ha ha ha ha ha! Kelume ni kiongozi wa Gorino, nataka roho yake hai” Bibi kizee
alimjibu Amata, Amata alifikiri sana juu ya ombi lile na alipoinua kichwa chake
kumtazama bibi yule alikutana uso kwa uso na Bundi mkubwa aliyesimama juu ya
kipande cha mti kilichopo mbele hapo, Amata alimtazama bundi yule mara bundi yule
aliruka na kutokomea mbali. Amata alinyanyuka pale alipoketi alipoangalia huku na huko
aligundua kuwa yuko mahali tofauti na alipokuwa mwanzo, alitulia kidogo na kuvuta
akili. Alivuta hatua chache mbele yake na kupanda juu ya jiwe kubwa lililopo hapo, na
alipofika juu alijilaza kifudifudi na kuangalia kwa makini pande zote, kwa mbali aliona
kitu kama mlima na chini yake aliona kama kusanyiko kubwa la watu, Amata hakuelewa
vizuri kama ni watu au ni nini, aliteremka kutoka katika jiwe lile na kusonga mbele
kupitia katika vichaka vyenye miiba na mawe ilimradi tu afike mahali ambapo angeina
kwa uzuri zaidi. Aliteremka bonde kubwa kwa taabu sana na alipofika chini aliendelea
kwenda kwa umakini zaidi kuelekea upande ule alipowaona wale watu, jua lilianza
kuchwea na kagiza mororo kalianza kuufukuza mwanga hafifu ulioujaza msitu huo,
Amata alijibanza katika jiwe mojawapo na kutulia akisubiri giza litawale ili ajue nini cha
kufanya.
[emoji814][emoji814][emoji814]
Hellen alitulia kimya akifuatilia nyendo za mtu huyo ambaye alikuwa akiingia pangoni mle kwa kunyata, akiwa bado na kamba miokononi na miguuni alijiegemeza
katika ukuta wa pango lile. Yule mtu aliendelea kusogea alipo Hellen, akanyoosha
mkono wake na kumshika mguu Hellen, Hellen hakuleta tabu yoyote alitulia tu kuona
nini kinaendelea, yule mtu alimburuza Hellen hadi nje ya pango, ‘Gorino’ Hellen
alishangaa na kuingiwa na woga, sasa alijaribu kujinasua lakini hakuweza kwa kuwa
alikuwa amefungwa kamba mikono na miguu, mtu yule alitoa tabasamu baya ambalo
Hellen alitema mate, kwa kitendo hiko alistukia kofi moja kali lililomrusha upande wa
pili, Hellen alilia kwa uchungu. Huku akijigalagaza kama mtoto. Lile pande la mtu
likamjia tena Hellen lilimwangalia kwa sura yake ya kutisha iliyopakwa vitu vya ajabu na
kuchanjwa chale nyingi, harufu yake ilimfanya Hellen kuhisi kichefuchefu, Hellen
aliliangali lile jitu ambalo lilionekana lina uchu wa kitu fulani toka kwa hellen, likaanza
kuongea lugha isiyojulikana, Hellen hakuelewa chochote kinachosemwa aliendelea
kulitazama lilipokuwa linamfuata pale alipo, Hellen alijaribu kujisogeza lakini hakuweza.
Lile jitu likamkamata Hellen kwa mkono wake wenye nguvu na kumuinua kutoka pale
alipokuwa amekaa, likamwangalia na kuanza kumshikashika matako na mapaja huku
mkono mmoja likiwa limemshika bega Hellen, Hellen alihisi maumivu makali sana
begani mwake na hakupenda hata kidogo jitu lile lilivyokuwa linamshikashika namna
hile lakini hakuweza kujinasua, lile jitu likaanza kumshika kiunoni taratibu likandisha
mkono wake kifuani na kuanza kuyaminya matiti, Helleni hakuvumilia hata kidogo
alijivuta nyuma kidogo na kuachia kichwa kilichompata kwenye mwamba wa pua, damu
nyingi zikaanza kuvuja kwenye pua ya jitu lile, hasira zikatawala, lile jitu likachukua mti
uliochongwa mbele ambao walitumia sana katika kutoa mioyo ya binadamu, liliunyanyua
na kumshambualia Hellen, Hellen alinyayua mikono yake kujikinga uso, mti ule ulipita
karibu na uso wa Hellen, Hellen aligeuka upande wa pili na kushudia mikono yake ikiwa
huru kumbe mti ule ulikata zile kamba, kazi! Hellen akiwa chini alijifungua kamba za
miguu kwa haraka na kusimama kulikabili jitu lile ambalo lilikuwa bado linajaribu kufuta
damu zile. Lile jitu lilipotahamaki lilimuona Hellen akianza kukimbia, lilitoa kamba
kiunoni na kuirusha miguuni kwa Hellen, Hellen aliruka samasoti moja na lipotua
aligeuka nyuma kuliangalia jitu lile lililokuwa likimfuata kwa kasi, Hellen aliruk teke
maridadi lililotua shavuni kwa jitu lile lakini halikuonekana kutetereke hata kidogo,
Hellen alipotu chini alipiga goti moja na kujizungusha kwa kasi na kumpa ngwara
maridadi lakini jitu lile halikuanguka. Hellen alijinyanyua na kurudi nyuma hatua chache
kupanga mashambulizi upya kabla hajajiweka sa alijikuta akipata gumi moja la shavu
lililompeleka chini, alijibiringisha na kunyanyuka haraka hakujali maumivu wala damu
zilizomtoka mdomoni, alipata gumi linigine nalo likampeleka chini sasa hakuweza
kunyanyuka mara moja alitambaa kama mtoto kuelekea kule kulikoangukia ule mti wa
yule gorino, jitu lile lilipoona mbinu ya Hellen likamfuata Hellen kwa kasi lakini
alichelewa Hellen alichukua ule mti na kujigeuza haraka na kuwa chali, jitu lile lilijirusha
kuchukua ule mti lakini badala ya kuuchukua lilijikuta likitua kwenye ncha ya jiti lile
ambalo lilididimia katikati ya kifua chake, lilitoa macho mpaka likakata roho, Hellen
alilisukuma kwa miguu yake na kulitupa pembeni. Hellen alinyanyuka na kuliangalia lile
jitu likiwa najiti lake kifuani ‘kumbe na mi naweza’ alijisemea moyoni, ndipo
alipogundua kuwa jino moja lilitoka mdomoni mwake na mawili yamelegea, alitema
mate yaliyochanganyika na damu, aliendelea kutema lakini aliona damu ile haiishi
aliondoka taratibu eneo lile na kuingiza ndani zaidi ya msitu ule, hakuwa hata na hamu ya
kutaka kujua nini kimejiri katika msafara ule. Alikimbia taratibu huku akipambana nanyasi ndefu miti yenye miba na mawe yaliyomfanya mara nyingi kupunguza mwendo
wake huo. Hellen alijikuta amechoka lakini hakukata tamaa huku akiwa anasali
kimoyomoyo aliendelea kukimbia na kuomba akutane na mmoja wao lakini haikuwa
hivyo aliendelea kukimbia na kuomba asikutane na wanyama au viumbe wabaya.
Giza lilianza kuitawala nuru, Hellen akawa amechoka sana akaanza kutembea taratibu na
kwa kuwa alikuwa anaogopa giza aliona njia pekee ni kujificha sehemu au kupanda juu
ya mti. Akiwa katika usingizi alisikia mlio wa ngoma kwa mbali kidogo, moyo
ulimlipuka na kwenda mbiyo maana aliitambua ngoma hiyo ‘Gorino’alijiwazia akijua
kuwa kumbe hawakwenda mbali na walipomuacha, ndiyo maana hata yule mmoja
alifanikiwa kurudi kirahisi. Hellen alijitahidi kupanda kwa shida kwenye mti mmojawapo
angalau ajiepushe na wanyama wapitao huko chini, na alipokuwa juu ndipo alipogundua
kuwa mti ule ulikuwa umebeba mtango uliotambaa vizuri na matango makubwamakubwa
yakining’inia “Thanks God!” Hellen alijikuta akiongea kwa sauti na kuanza
kuyashambulia matango yale kwa fujo, aliporidhika akapitiwa na usingizi akiwa
amekumbatia tawi la mti huo. Alipozinduka ulikuwa usiku mzito sana aliona kwa mbali
moto ukiwaka na ngoma zikirindima, Hellen aliangalia na kupata shauku ya kwenda japo
alijua ni Gorino waliopo huko kwa kuwa alishauzoea mdundo wa ngoma ile, alipiga
moyo konde akashuka kwa uangalifu wa hali ya juu, aliweka miguu chini taratibu na
kutazama huku na kule alipoona usalama upo alianza kutembea taratibu kulibili bonde
kubwa ambalo chini huko ndiko alikoona moto ule ‘itakuwaje wakinikamata’ alijiuliza
bila kupata jibu, lakini hakusita alisonga mbele kwa kujiamini lakini kila muda aligeuka
nyuma kutazama kama kuna yeyote anayemfuata, mara moja akiwa katika kugeuka
nyuma alijikuta akitereza na kuporomoka katika bonde refu, alijipiga katika miti na
mawe kadhaa yaliyopo katika poromoko.

[emoji814][emoji814][emoji814]
9
Saringo alinyata kwa ustadi sana akihakikisha hakuna anayeona hata unyasi ukitikisika,
punde si punde alitokea kwenye jiwe kubwa sana jeusi ambalo juu yake limebeba mawe
mengine yaliyokaa katika mitindo tofauti. Saringo hakuwa na woga hata kidogo akiamini
kabisa kuwa kama kufa ni kufa tu, aliendelea kunyata kulizunguka jiwe lile ambalo
lilichukua eneo kubwa sana, huku akisikia midundo ya ngoma na nyimbo asizozielewa
alijaribu kutafuta sehemu ambayo angeweza kuona ni nini kinaendelea, akiwa katika
kuzunguka alifika sehemu fulani na kuchuchumaa nyuma ya jiwe moja ambalo lilikuwa
na tundu katikati na kupitia hapo aliweza kuona ngoma ile japo kwa taabu kidogo. Ghafla
alihisi mkono wa mtu ukimshika bega, taratibu Saringo aligeuka kwa woga kwa kuwa
alikuwa hajui ni nani aliyemshika bega, moyo ulimlipuka na kwenda mbio baada ya
kuona gorino wawili wamesimama nyuma yake, alijinyanyua pale alipokuwa
amechuchumaa na kuegemea jiwe akitazamana na wale gorino walioonekana kuwa na
hasira kali.
Giza liliivamia nchi, sherehe ya kafara ya Gorino ilianza kwa kuwasha moto katia mienge
mingi waliokuwa nao, ngoma na nyimbo zilirindima katika msitu ule, huku na huku
katika mawe yale walionekana kuzunguka na kumwaga vitu fulani fulani. Saringo alitulia kimya kabisa katika moja ya jiwe alilohifadhiwa lakini aliweza kuona kila
kinachoendelea mahali pale. Mbele ya jiwe hilo aliweza kuona kitui kama shimo kubwa
linaloelekea chini na giza nene lilitawala ndani humo, Saringo alijiuliza kama hapo ndiyo
mahali pale alipoelezwa na babu yake au bado alikuwa hajafika, lakini hakuwa na la
kufanya kwa kuwa mpaka muda huo hakujua ni nani kafa au yuko hai katika kundi lao
zaidi ya Golam aliyepotea msituni.
Mbala mwezi ilianza kung’aa na sherehe ya kafara ilizidi kunoga, Saringo hakuwahi
kuona ngoma kama hiyo ya ajabu katika maisha yake, lakini jinsi ilivyochezwa ilimvutia
sana na hata wakati mwingine alicheka japo hakutoa sauti. Mara watu wawili wakaja hadi
pale alipo na kumfungua kisha kutoka nae moja kwa moja katikati ya ngoma ile, Saringo
alijaribu kujinasua lakini mikono ya gorino ilikuwa na nguvu za ajabu Saringo hakuweza
hata kutikisika alipiga kelele lakini hazikusaidia, alijikuta katikati ya gorino
waliomzunguka huku na huku, Saringo hakuwa na ujanja, hakuwa na lakufanya alibaki
kutazamana na Kerume aliyevimba kwa hasira maana katika utaratibu wa mwanamke
hakuruhusiwa kuwepo eneo la kafara. “Beliiiigo!!!” Kerume alitoa ukelele na ngoma ile
ilinyamaza kimya kikuu kikatawala “ Losa, losa, losa ilo seleke” akimaanisha “hii hii hii
ni laana” kwa hasira alizokuwa nazo Kerume hakuweza kujizuia alimsogelea saringo na
kumpiga makofi kadhaa ya nguvu yaliyompeleka chini Saringo, wafuasi wa Kerume
walimnyanyua mna kumsimamisha wima, Saringo alikuwa akitweta kwa uchungu na
hasira lakini hakuwa na cha kufanya. Kerume aliangalia huku na huku na kumyang’anya
mfuasi wake mmoja mti aliokuwa akiutumia katika ngoma ile na bila kuchelewa
aliunyanyua na kuuteremsha kwa pigo lisilo huruma kifuani mwa Saringo, Saringo
alipiga ukelele wa uchungu pale jiti lile lilipotua mwilini mwake, akapiga magoti na
kudondoka chini kifudifudi damu zikimmwagika. Kerume alinyoosha mikono yake juu
na kutoa ishara fulani, Mwili wa Saringo uliondolewa katika eneo lile na ngoma ile
ilianza upya. Ngoma ilipokolea mmoja wa mateka alitolewa pangoni akiwa na kamba
shingoni akivutwa kama mbuzi na kupandishwa juu ya jiwe mojawapo lililo katikati ya
kiwanja kile na kulazwa chali, Kerume alishuka kutoka alipokaa na mti wake maalumu
kwa kazi hiyo, aliunyanyua na kushusha pigo moja kifuani mwa mtu yule alipouchomoa
mti ule ulitoka na moyo, yowe la uchungu lilisikika na mtu yule uhai ukamtoka, wengine
walitega midomo yao kunywa damu iliyokuwa inaruka kwa kasi kutoka katika mwili ule.
Ngoma ilizidi kuchanganya, gorino wengine walionekana wakitoka katika pango lile na
mtu mwingine ambaye alikuwa ni mbishi sana na hakutaka kabisa kwenda, kipigo
alichopewa hakikuwa cha kawaida mpaka alipopoteza nguvu walimbeba na kumrusha
katika pango lingine kubwa zaidi. Joka kubwa lilimdaka kabla hajafika chini na
kumviringa kisha kupotea nae pangoni. Kelele za Gorino zilisikika kwa nguvu zaidi
wakishangilia kwa kuwa kafara yao ilipokelewa.
Damu nyingi ziliendelea kumtoka Saringo pale alipotupwa na Gorino ambao walikuwa
wakijiandaa kumchuna ngozi ili wapate nyama kama walivyoagizwa, kwa kuwa wao
hawakujuwa kama mtu yule amekufa au la, waliendelea kuchuna kamba na kunoa vitu
kama visu walivyotaka kutumia kwa kazi hiyo. Walimchukuwa Saringo na kuanza
kumfunga kamba mikononi ili wamning’inize tayari kuchuna ngozi ile, walipotaka
kumnyanyua ndipo mmoja alisukumwa na mkono wa Saringo kwa nguvu hafifu sana
akajua kumbe hajafa “soliti igola!” alimwambia mwenzake akimaanisa mbona hajafa.
Alichukua jiti lake na kutaka kumdidimiza Saringo moyoni lakini kabla hajatimiza azma yake alianguka chini na kurusharusha miguu na mikono huku na huku uhai ukimtoka.
Mwenzake aliangalia huku na huku hakuona mtu alipomwangalia mwenzake alikuta
mshale umemdidimia katika koromeo na macho yamemtoka pima, alitazama huku na
huku hakuona mtu tena aliweka mikono yake mdomoni akitaka kupiga mbinja
akachelewa kichwa chwake kilitawanywa na ubongo wote ukamwagika hakuweza hata
kufurukuta alirushwa na kuangukia upande wa pili, mwingine alikuwa mbali kidogo
akiandaa hiki na kile akashtushwa na kishindo kile akarudi na njiani akakuta kiwiliwili
cha mwenzake, alitazama vizuri na kugiuzageuza, akanyanyuka na kuelekea kule
walikokuwa wakitaka kumchuna Saringo, alipofika alikuta mwili usio na uhai wa
mwenzake nao umelala pale lakini hakuona ile nyama yao, alionekana wazi
kuchanganyikiwa hakujua afanye nini, katika kuzubaa huko kamba ilimnasa shingoni na
kumnyanyua juu alirusharusha miguu lakini taratibu sana roho iliacha mwili, mwili wa
marehemu yule ulianguka chini na kutulia kimya.
Hellen aliipachika bastola yake kiunoni, akisaidiana na Amata waliubeba mwili wa
Saringo aliyeonekana bado anpumua kwa mbali, Hellen alijitahidi kumpa tiba angalau
kuokoa damu iliyobaki na kufunga jeraha lile kwa kutumia blauzi yake, Hellen aliamua
kubaki na kanguo kepesi ka ndani tu baada ya kuichana blauzi yake ili kumsitiri Saringo,
Amata alileta maji na kumnywesha Saringo ambaye alionekana kupoteza nguvu nyingi
sana hasa kwa kutokwa na damu, kimvua chembamba kilinyesha usiku ule na hii ilikuwa
ni ahuweni kubwa kwa Saringo, Hellen aligundua kuwa pigo lile la Kerume kwa saringo
halikutua sawasawa moyoni kwake sipokuwa lilipiga chini kidogo na kuvunja mbavu
karibu mbili tatu za juu za upande wa kushoto. Amata aliingia porini nakuja na aina
fulani ya majani ambayo aliitafuna na kuweka katika jeraha lile na kufunga vizuri.
Walipohakikisha Saringo yupo salama wakaanza kupanga mikakati jinsi ya kuvamia eneo
lile, kundi lile la Gorino liliwatisha sana kila walipojiangalia silaha walizo nazo
zisingeweza kufanya chochote. Hellen aliifungua ile karatasi aliyopewa na Amata
akaangalia vizuri mchoro ule na maandishi yote yaliyoandikwa mle akagundua kuwa pale
katika lile jiwe ndiyo kuna pango la hazina. “Tuzunguke, ili tuwatokee kwa nyuma”
Hellen alimuambia Amata kwa kiswahili cha kubabaisha, Amata aliangalia vizuri eneo
lile ambalo kwa wakati huo halikuwa umbali wa kutisha waliweza kuona kila kitu
kinachoendelea, walimuacha Saringo pale baada ya kumuhifadhi vizuri na wao
kuteremka bondeni kisha kwa mwendo wa kunyata walilizunguka eneo lile na kutokea
kwa nyuma kama walivyopanga. Walitafuta eneo zuri ambalo wangejificha lakini pia
wangeweza kuona vizuri ili kujua nini wafanye, Amata na Hellen walijificha vizuri
katika kichaka kidogo lakini si mbali na eneo lile huku wakiwa makini kuona kama kuna
chochote cha kuwasumbua, alilivua podo lake na kuhesabu mishale ilobaki, si haba
ilikuwa kama ishirini na tano na alipotazama kundi lile alikuta kuna Gorino zaidi ya mia
moja Amata alichanganyikiwa akamtazama Hellen ambaye wakati huo naye alikuwa
akihesabu risasi alizonazo baada ya kupewa kikasha kile na Amata si haba zilikuwa kama
mia na ishirini akamnyoshea alama ya dole gumba Amata naye akajibu kwa mtindo uo
huo. “Subiri hapa mi nasogea mbele nione wanafanya nini!” Amata alimueleza Hellen
“Wapo kwenye kafara hata mimi nilikuwa kwenye msafara huo, wanaua watu, kuna watu
kama kumi na tano hivi” Hellen alimueleza Amata. Amata alijivuta taratibu mpaka
karibu na jiwe kubwa lakini hamad! Alijikuta amekutana na Gorino aliyeko katika ulinzi
wa eneo hilo, Amata alimtazama na kabla Gorino yule hajakaa vizuri alijikuta akipaa hewani kwa ngwala safi aliyopigwa na Amata, alitua kama mzigo na alipofika chini bisu
kubwa la Amata lilidimia kifuani mwa Gorino yule na kupoteza uhai. Amata alitazama
huku na huku kuhakikisha usalama kisha akaendelea kusogea upande wa pili kulizunguka
jiwe lile, kabla hajakata kona alimuona Gorino mwingine aliyekuwa kasimama akitazama
upande mwingine Amata alifikiri atumie mbinu gani kumuondoa lakini alikosa kwa kuwa
hakuwa tayari kutumia uta wake kwani alibakiwa na mishale michache, alifikiri kama
atumie mikono kumkabili lakini akaona inaweza kuwa mbinu mbaya endapo atazidiwa
nguvu, aliokota jiwe la kutosha na kulirusha kwa nguvu zote na kumpiga kisogoni,
Gorino yule aliyumba na alipokaa sawa aligeuka nyuma uso uso kwa uso na Amata,
Gorino alirusha jiti lake kwa Amata lakini Amata aliepa kwa ustadi na shabaha kukosa
uelekeo, Amata alidakwa koo hata akajikuta anakosa nguvu alijikusanya mna kupiga
kifuti kimoja kati maeneo nyeti ya Gorino yule, kutokana na maumivu yale alimuachia
Amata ambaye alichukua nafasi hiyo kumtandika mateke mawili ya usoni yaliyomfanya
anyanyuke kisha Amata akajirusha mzimamzima na kutua kwa miguu miwili kifuani
mwa Gorino yule ambaye aliyumba tena na kujipigiza kwenye jiwe, damu zilimtoka kwa
wingi kisogoni akajibwaga chini na uhai ukaambaa zake, maiti! Amata alipanda polepole
juu ya jiwe lile lakini kwa kuwa alikuwa haoni anakoelekea kumbe mmoja wa Gorino
ailikuwa kule juu, Hellen alimuona vizuri sana Gorino yule lakini alifikiria afanyeje
kama angetumia bastola yake basi ile kelele ingewashtua wengine, moyoni aliteseka
lakini hakujua afanye nini alibaki kutazama tu kitachotokea. Amata alishika vizuri jiwe la
juu ili ajivute lakini mara akahisi kitu kimemkanyaga, hakusita aliendelea kujivuta na
hapo alijikuta ameshikwa mikono yake na yote miwili na Gorino yule na kuvutiwa juu ya
jiwe lile, Amata alijinyanyua na lipo simama wima alimpiga kichwa Gorino yule na
kumsindikiza kwa makonde mfululizo, Gorino alipepesuka lakini Amata alimdaka na
kumgeuzia upande wa pili ambapo alimponyoka na kuanguka kutoka juu ya jiwe lile
kabla hajafika chini joka kubwa lilichomoza kutoka pangoni na kudaka juu kwa juu na
kuteremka nae chini mpaka pangoni Amata alibaki na bumbuwazi.
[emoji814][emoji814][emoji814]
Kule chini ngoma ya Gorino iliendelea na kafara ziliendelea kutolewa, tayari watu
karibu watano walikwishauawa kinyama na eneo lote lilikuwa likinuka damu lakini kwa
Gorino hiyo ilikuwa ni sherehe kubwa sana waliimba na kucheza wala hawakujua kama
kuna wenzao waliokwishapoteza maisha kati usiku huo. Kerume akiwa juu ya jiwe
lililochongwa kama kiti na wafuasi wake aliendelea kusherehekea karamu ile ya damu za
londigo, huku akitafuna nyama mbichi. Alitolewa mtu mwingine tayari kwa kafara
akapandishwa juu ya jiwe lile la kutolea kafara ambapo wakishamkata kichwa lazima
kidondokee pangoni na damu yake kutiririka kuelekea uko huko ambako wao waliamini
kuwa Kolilo ndimo anamoishi. Alikuwa ni kijana wa makamu aliyelekuwa akileta
upinzani wa hali ya juu ili asipelekwe katika jiwe lile, Gorino walimshika vizuri na
kumburuza kumpeleka jiweni walimpandisha na kumfunga panapotakiwa tayari kwa
kutoa kafara ya damu.
Hellen kutoka mbali aliweza kuona kila kinachoendelea na alipoona huyo kijana
akamkumbuka kwa kuwa alifungwa jirani yake wakiwa kama mateka kule msituni, alilia
kwa uchungu, akachukua bastola yake akaiweka sawa ‘liwalo na liwe’ akajisemea moyoni akaanza kuitafuta shabaha lakini hakujua nani hasa anayemlenga Kerume au
wafuasi wake ‘atakayenyanyua mkono wake tu ninaye’ alijisemea huku akiuma meno
aliweka bastora yake na domo la revolver lilikuwa tayari tayari kutekeleza
litakachoamriwa na mkono wa Hellen. Gorino walipiga kelele kama ishara ya kutekeleza
agizo la Kerume, Gorino mmuaji ambaye mwili wake wote ulichafuka damu ya
binadamu alinyayua juu lile jiti lake tayari kwa kazi, kabla hajashusha alipaishwa juu na
kujibwaga kama mzigo jeraha kubwa lililokuwa kifuani mwake lilimfanya ashindwe
kuyashinda mauti, bastola ya Hellen ilifuata maagizo sawasawa. Amata akiwa juu ya lile
jiwe alishtushwa n amlio ule na moja kwa moja alijuwa kuwa Hellen keshafyatua risasi
na kuwachokoza Gorino. Hali ya eneo lile ilivurugika gorino walitawanyika eneo lote
kutafuta adui wao wakiwa na munkari wa kuua yeyote watakeyemuona. Amata
alitegemea kwa hali ile wote wangeweza kumuacha Kerume ili amtoe uhai kama
alivyokubaliana na Bibi kizee lakini haikuwa hivyo gorino karibu ishirini walimzunguka
Kerume wakirukaruka huku na huko ingekuwa wamasai tungesema wamepandisha mori.
Gorino walizunguka wakiwa hawajui ni nani wananemtafuta sherehe imevurugika,
Amata alijikuta akinaswa kwa kamba mguuni ambayo ilimuangusha kutoka juu ya jiwe
lile mpaka chini na uta wake ukimtoka mkononi Gorino ailiyemvuta kwa kamba ile
alnyanyua jiti lake ili kumchoma lakini haikuwa hivyo wakati kajiziuka kuangalia juu
alijikuta kichwa chake kikifumuliwa kwa risasi kutoka kwa Hellen, Hellen alihama
haraka kutoka katika kichaka kile na kukimbilia nyuma ya mbuyu mkubwa uliopo mahali
hapo, sasa kwake ilikuwa ni kama kulipa kisasi kwa yote ambayo walimfanyia akiwa
mateka, hakutaka hata kidogo kumpoteza Amata katika machoyake, alibaki bado
anamwangalia pale alipoangukia, akiwa anajizoa zoa Gorino mmoja alikuwa akimjia kwa
kasi akifuatiwa na wengine nyuma yake huku wakipiga kelele yule wa mbele hakufika
kwani nae alipaishwa juu na kifua chake kilifumuliwa vibaya na risasi nyingine ya
Hellen, Amata kwa haraka alinyanyuka na kuokota uta wake lakini kabla hajajiweka
sawa alipata pigo moja la mgongoni alihisi kupigwa na kitu ka jiwe aligeuka kwa kasi na
kuchomoa jisu lake pigo moja la shingo lilirusu jisu lile kupenya Amata akalichomoa
wakati huo akimsindikiza na teke kali la nyuma gorino wa pili ambaye alipepesuka bila
uelekeo na kuangukia kando. Kerume alipagawa na kuchuka uta wake enye nguvu ya
ajabu aliweka mchale wake na kuuvuta shabaha kuelekea kwa Amata aliuachia na kasi
uliotoka nayo haikuwa rahisi binadamu wa kawaida kuuepa, Amata aliuona ukija usoni
kwake haraka alijigeuza na mhsle ule ulipita na kuondoa sehemu ya nywele zake za
kisogo na kumuishia gorino wa upande wa pili. Kazi ilikuwa ngumu kwa Amata
kujinasua kwani alikuwa tayari kazingirwa na Gorino wale, Hellen alijaza risasi zingine
kwenye magazini yake na ilipokuwa sawa kazi iliendelea Gorino mmoja baada ya
mwingine waliteremshwa kwa shabaha njema kabisa kutoka kwa mwanadada huyu uku
akihamahama ili kuwachanganya viumbe hawa katili wasio na chembe ya huruma.
Hellen alimuona mmoja wao akiweka mdomoni kitu kama tete la muhindi bila kuchelewa
aliijua vema silaha hiyo mbaya na ya sumu inayotumiwa sana huko Amazonia alihamisha
shabaha yake nakumfyatua yule kwanza ambaye alipoteza uhai apohapo.
Mapambano yalikuwa makubwa, Gorino walikuja na silaha nyingi iwezekanavyo, Amata
alishindwa kufurukuta alizingirwa huku na huku, Hellen ahakuweza kuwakabili wote
maana hakujua yupi awe wa kwanza na yupi afuate alibaki kuchanganyikiwa hasa
alipogeuka nyuma nakuwaona wengine wakimfuata, “Hellen!!! Kibuyuuuuuu” Amata
alipiga ukelele kumuelekeza Hellen, Hellen alipogeuka na kutazama huku na huku aliona
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom