HaMachiach
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 3,450
- 6,211
MSITU WA SORONDO
Mtunzi Richard Mwambe
Simu 0754740668
1
Chau cafe Chau cafe
Amata Ga Imba aliendelea kunywa kahawa yake polepole kana kwamba hana
shughuli nyingine ya kufanya kwa siku hiyo, kichwani akiwa na mawazo mengi sana
akipanga na kupangua juu ya maisha yake ya sasa na baadae, alipotahamaki hata kashata
alizokuwa akila zilikwisha moyoni akajiuliza kama aliagiza kashata au ameshazila
zimekwisha! Hilo nalo likawa jambo jingine ambalo lilikosa jibu kabisa.
“Chausiku!!” aliita kwa nguvu kana kwamba aliyekuwa anamuita alikuwa umbali wa
kilomita kadhaa lakini kumbe wote walikuwa hapo jirani tu.
Watu walishtuka kwa sauti hiyo hata wengine walidiriki kumtupia maneno yasiyostahili
“Samahani waheshimiwa!” aliomba msamaha
“Samahani nini mjinga wewe!” mmoja alitamka kwa hasira
“Wengine tuna BP utatuuwa bure sura ka Sokwe!” mwingine aliongeza
Amata aliumia sana moyoni kwa tukio lile, akainamia mezani, akatikisa kichwa kisha
akasimama kwa hasira na kuelekea eneo la kunawia mikono, akajitazama kwenye kioo,
akatabasamu, kisha akageuka na kurudi alipoketi kwanza.
Kabla hajaketi alisikia sauti nyuma yake
“Umejiona ee? Ka sokwe, tena wa Gombe!” mmoja alimkejeli, wengine wakaangua
kicheko cha dharau na kupiga miluzi.
Hasira za ghafla zikamrudia Amata, akageuka na kuelekea upande ambao sauti ile
imesikika
“Nani aliyesema vile?” aliuliza kwa kung’aka, wakacheka tena
“Ukimuona utamfanya nini? Fala wewe mtoto wa porini!!” mwingine alisema na
wengine wakaangua kicheko. Amata alipiga hatua mbili mbele na kumkunja shati yule
aliyesema maneno hayo akamuinua kwa nguvu akamrusha chini, huyo akaanguka chini
mzimamzima kama gunia, jamaa akanyanyuka kwa hasia na kumvamia Amata, Amata
akamdaka na kupiga vichwa vitatu vya nguvu akamsukuma kidogo na kumrushia
makonde kama mvua, kijana yule alichanganyikiwa hata hakuweza kujibu mashambulizi
alianguka chini mara ya pili.
“Ameua! Ameua! Ameua!” kelele za watu zilijaza mgahawa ule mara watu wakajaa
wanataka kumshika Amata. Yule kijana bado alikuwa chini hajitambui kwa kipondo cha
ghafla alichokipata. Amata aliruka kutoka aliposimama akatua juu ya meza na kutaka
kutoroka kwa kupitia dirishani, watu walimgombania kwa kumshika shatia wengine
suruali, masikini Amata shati lake lilichanika vibaya akabaki na fulana ya ndani na
kuwaachia shati wananchi wenye hasira, alliruka kupitia dirisha la mgahawa huo na
kudondokea kwenye lundo la mawe kwa kutanguliza mkono, alihisi maumivu makali ya
mkono lakini alipogeuka aliona watu wale wanakuja pale alipo, akanyanyuka na kutimua
mbio
“Huyo huyo! Kamata muuaji huyo!!” kelele za wananchi wale zilikuwa kama kichocheo
kwa kijana Amata kuongeza spidi. Mara kwa mbele aligongana na pande la mtu na
kuangushwa mbali, alinyanyuka na kuanza kukimbia tena, watu walitoka majumbani na
kumuunganishia kama kawaida ya wananchi. Mbio ziliendelea na wananchi nao
hawakuchoka, alitokea kwenye wigo wa nyumba la! Hapakuwa na njia aliruka na kupanda ukuta kisha akatokea upande wapili na kupanda tena alitua chini kwa miguu
yake mikakamavu na kutimua mbio lakini la haula! Alipokuwa akijaribu kuvuka kichaka
kidogo katika eneo hilo alijikwaa vibaya na kuanguka chini, mchezo umekwisha. Watu
wakamkamata na kuanza kumpiga hata kumuumiza vibaya, Mungu si Athumani polisi
waliwahi kumuokoa kutoka kwenye mikono ya watu wenye hasira.
“Tuachie huyo tummalize! Muuaji huyo!” watu walipiga kelele na wengine bado
walidiriki kurusha hata mawe ambayo baadhi yaliwapata askari wale. Askari mmoja
akafyatua risasi hewani na watu wale wakatawanyika kwa woga wakikimbia uku na huku
wengine wakianguka na kukanyagana vibaya. Amata alichukuliwa mpaka kituo kidogo
cha polisi akiwa hatamaniki kwa jinsi alivyolowa damu hata fulana yake aliyobaki nayo
baada ya kuwaachia shati watu wale haikujulikana kama ni nyeupe au nyekundu, juu ya
jicho lake la kushoto jeraha kubwa lilikuwa bado linavuja damu, mkono wake umevimba,
kucha ya kidole gumba cha mguu wa kushoto haikujulikana hata imeng’okea wapi.
Askari wale walimpiga Tanganyika jeki bila huruma wala kujali kuwa mwenzao
ameumia namna ile wallimkokota tena na makofi juu mpaka kituo kidogo cha polisi na
kumlundika selo.
Ndani ya chumba kidogo cha selo katika kituo cha polisi cha kijiji wahalifu walijazana
mpaka hewa haikutosha kabisa, walichoka na hata wengine kukosa nguvu, kupoteza
fahamu kwa kukosa hewa ya kutosha. Amata aliingia kwenye selo hiyo katika hali ile
aliyokuwanayo, akakaribishwa na joto na harufu mbaya haja kubwa na ndogo
zilizochanganyika, mwanga hafifu uliopita katika kadirisha kadogo kenye ukubwa wa
mlango wa banda la njiwa ndio pekee kalikokuwa kanatoa faraja kwa binadamu hawa
waliokuwa na makazi ya muda ndani ya chumba hiki, wote walikuwa na sura za kutisha
ambazo bila kuuliza utajua kuwa sasa nimeingia kuzimu.
Ucku huo ulikuwa mrefu sana kwa Amata, mawazo mengi yalitawala kichwa chake,
maumivu makali yaliusumbua mwili wake, alijituliza kimya kwenye moja ya kona za
kijichumba hiko huku akisikia kichefuchefu kama mama mjamzito kila mara alitamani
kutema mate lakini atatemea wapi watu wamejazana hata wengine wamekaa kwa
kupakatana mh! Mawazo yaliendelea kumsonga hata usingizi mwepesi
uliokatishwakatishwa kwa nyimbo za kuchukiza za mbu masikioni mwake ulikuja na
kuondoka, aliwaza jinsi anavyoishi kwa tabu bila Baba wala Mama wa kumtetea, japo
aliachiwa shamba kubwa na kibanda cha kuishi lakini hakuujua uelekeo wa maisha yake,
“alikuwa analinga na Baba yake, ataona sasa” wengi walisema hivyo, Amata aliona ama
jamii yote haimtaki, dunia imemchukia au ulimwengu unampa adhabu?
“Kwa nini mimi?” alijiuliza uliza moyoni mara kwa mara hasa alipokuwa kwenye
kibanda chake huko shambani kwao ambako alipitisha maisha yake ya ujana tangu
wazazi wake walipofariki yeye akiwa na umri wa miaka michache nyuma, mama yake
aliuawa na Simba alipokwenda kuchota maji nje kidogo ya shamba lao ijapokuwa Baba
yake alijaribu kumtetea dhidi ya Simba hao wakali wenye uchu wa nyama lakini hakufua
dafu ‘kidole kimoja hakivunji Chawa’ alipiga kelele za msaada lakini hakuna aliyekuja.
Lakini Baba yake alikufa baada ya kuugua kwa muda mfupi miaka michache baadae.
Kila aliporudiwa na picha hizi alilia sana na kujiona kuwa yeye ni binadamu mwenye
mkosi, akuwahi kuwa na kaka wala dada isipokuwa ndugu tu ambao pia hawakuwa na
msaada nae kabisa. Amata!!!” aligutushwa na sauti kali ya askari iliyotokea kwenye kadirisha ka mlango wa
selo hiyo.
“Afande!” aliitikia kwa uchovu na kujaribu kujiinua kutoa alipokuwepo lakini alijikuta
anapata kizunguzungu na kuwaangukia wenzake waliokuwa hapo. Alifika mlangoni pale
kwa shida mbele yake alimuona msichana mrembo sana kasimama, mrefu wa wastani
maji ya kunde, alivalia vizuri suruali yake ya kitambaa nyeusi na blauzi yake nyeupe
huku shingoni kafunga skafu yenye mchanganyiko wa rangi, nywele zake fupi
zilizokatwa kiumahili na vinyozi wanaojua kazi yao, kiatu chake kirefu kilimfanya
aonekane kuwa ni mrembo anayetunzwa na pedeshee fulani. Dada yule alijivuta taratibu
mpaka kwenye dirisha lile. Amata alipokea pumzi safi iliyonukia na kuvutia kutoka kwa
mrembo huyo, hakuamini anachokiona ni malaika au binadamu, aliduwaa, akapigwa na
bumbuwazi, mikono yake ikiwa imeshika nondo mbili zenye kutu alijikuta anaishiwa
nguvu. Mrembo yule alishika nondo zile kwa kubana mikono ya Amata akaiangalia sura
ya Amata iliyochoka na kukaukiwa na damu..
“Saringo! Naitwa Saringo” almwambia Amata kwa sauti ya chini
“Hunijui, ila utanijua punde tu” aliendelea “Haujaua ila umeumiza vibaya, sasa unastahili
zawadi kwa kazi uliyoifanya bila kujua, na zawadi hiyo utaipata ukimaliza kazi yako”
Saringo alishusha pumzi na kumwangalia Amata usoni na kumuona jinsi
alivyochanganyikiwa, akaendelea kumwambia mashairi yake yasiyoeleweka kwa mtu
mwenye akili timamu, sasa kwa kukunja sura akamwambia Amata “ Lazima ufungwe,
uishie jela!” akageuka nakuondoka zake. Amata akazidi kulowa jasho, maswali yasiyo na
majibu yalimzunguka tena ‘nilijua malaika mwema kaja kuniokoa kumbe malaika mbaya
wa mauti kanitembelea’ alijiwazia na kuanza kulia. Amata hakupata jibu mwanamke yule
ni nani, na anataka nini, utata. Asubuhi ile kalandinga liliwachukua mpaka mahakama ya
kijiji, jalada la Amata lilikuwa la tatu kuitwa, taratibu akiwa na pingu mikononi
aliingizwa katika chumba cha hakimu na kusomewa mashitaka ya kudhuru mwili,
alijikuta hana cha kukana isipokuwa kukubali, kesi ikahairishwa mpaka baada ya siku
kumi na nne. Walipokuwa wanarudi kwenye kalandinga alimuona binti yuleyule akiwa
amesimama katika kundi la watu waliokuja mahakamani hapo, muonekano wake ulikuwa
tofauti na wote pale kwani ndiye aliyevaa nadhifu kuliko wote ‘huyu ni nani?’ Amata
alijiuliza hakupata jibu, moyoni alimlaani kuliko anavyomlaani shetani walipogongana
macho Amata alitema mate chini na kumuonesha kidole cha kati. Mara alijikuta
anatandikwa kofi la kisogoni au vijana huita ‘mbata’
“Panda juu unatuchelewesha!” sauti kali ya askari ilisikika. Amata na wengine
wakapanda na lori lile kuondoka kwa kasi.
[emoji814][emoji814][emoji814]
“Una mpenzi mzuri sana, mtoto kaumbika kama Malaika, he he he mbona wewe na yeye
hamuendani kabisa au wewe ni mchunga ng’ombe wao!” mmoja wa mahabusu
alimuuliza Amata kwa sauti mbaya ya kukwaruza isitoshe inatisha. Amata aligeuka na
kumwangalia akatabasamu kwa sura iliyochoka
“Simjui hata anatoka wapi” alimjibu
“Kwangu ni kama shetani tu yule, anataka kuniua, kunifunga, hilo ndilo limemleta hapa”
aliendelea kumueleza yule mahabusuKwa nini aje kukuona asubuhi yote ile? Au kuna uhusiano wowote na kesi yako?”
aliendelea kudadisi mahabusu yule,
“Sijui chochote! Mbona maswali mengi umempenda? Mfwate basi, mi nshakwambia
smjui! Yule ni shetani tu” Amata alijibu kwa hasira kidogo na mahabusu yule
hakuendelea na maswali yake.
Kesi ilitajwa tena baada ya siku kumi na nne, Amata na wenzake wakiwa na pingu
mikononi waliingizwa katika chumba maalumu cha mahabusu mahakamani hapo, Amata
alisimama karibu na mlango, mara ghafla alipata mshtuko mkubwa, hakuamini
alichokiona nje ya jingo hilo, akakaza macho kutazama kwa makini akayafikicha kidogo
aone labda alikuwa ndotoni lakini hapana alichokiona ni sahihi na macho
hayakumdanganya. Hakutaka kupoteza hata sekunde katika lile alilokuwa anliona lakini
bahati mbaya hakuweza kusikia kinachozungumzwa. ‘Yule sio Chausiku?’ alijiuliza
moyoni lakini pia hakutaka kuyaamini macho yake.
Chausiki Binti Saidi, msichana mfupi mwenye afya njema kibonge, mmiliki wa mgahawa
unaojulikana kwa jina la Chau Café, msichana huyu ambaye amekuwa pamoja na Amata,
wamesoma shule moja ya msingi kijijini hapo na kucheza michezo mingi ya utoto
pamoja, yeye alifanikiwa kufika japo darasa la saba wakati Amata alifukuzwa shule
akiwa darasa la tano kwa kisa cha kumpiga mawe mwalimu wake wa darasa. Maisha
yalimwendea kombo Amata kielimu japo alijitahidi sana katika rasilimali alizoachiwa na
marehemu baba yake Chausiku alimpenda kutokana na bidii yake katika kazi. Watu
walimbeza sana Chausiku kwa jinsi alivyoonesha upendo kwa Amata hii ikapelekea
Chausiku kutokuwa karibu sana na kijana huyu ambaye japo aliugusa moyo wake,
pamoja na ukorofi lakini hakuweza kumtoa moyoni mwake, moyoni mwa Chausiku
Amata alikuwa kama maji yatuliavyo mtungini yasipoguswa. Vijana wengi walipenda
kwenda mgahawani kwake japo tu roho zao zisuhuzike kwa kumuona binti huyu, wapo
waliomdanganya kwa pesa na vitu mbalimbali lakini msimamo wake thabiti
haukumfanya ayumbishwe na vitu vyote hivyo bali aliuacha moyo wake utue kama
kipepeo atuavyo katika ua alilolichagua.
Chausiku aliumizwa sana na kisa kilichomkuta Amata, alijua kuwa Amata kwa hali
aliyonayo asingeweza kupata msaada wowote wa kisheria au utetezi katika kesi yake,
alijitahidi kufanya kila awezalo ili tu amsaidie Amata katika hili.
Jalada la Amata liliitwa, polisi walimtoa katika chumba kile akiwa chini ya ulinzi na
kupelekwa katika chumba cha mahakama, akiwa anapita katika kikorido kidogo cha
jengo hilo alisikia sauti nyembamba tamu ikipenya masikioni mwake, ilikuwa si ya
mwingine bali Chausiku ambaye alikuwa akilia kwa machozi mazito “Mnyezi Mungu
akusaidie” ni maneno aliyomwambia, Amata aligeuka kwa kuiba, alifarijika kuona
kumbe wapo katika binadamu awa hawa wanaompenda, kidogo alijisikia mtu kati ya
watu.
Kesi ya Amata ilikwisha alihukumiwa kifungo cha miaka miwili na miezi sita jela.
Waliondolewa mahakamani na Amata alianza kutumikia kifungo chake huko gereza la
kilimo Sogera, gereza lenye kazi ngumu, kulima, kupanda, kuvuna, muda wote mkiwa
katika matope, maji machafu, mnakula chakula huku mnanyeshewa na mvua, mateso!.
Mtunzi Richard Mwambe
Simu 0754740668
1
Chau cafe Chau cafe
Amata Ga Imba aliendelea kunywa kahawa yake polepole kana kwamba hana
shughuli nyingine ya kufanya kwa siku hiyo, kichwani akiwa na mawazo mengi sana
akipanga na kupangua juu ya maisha yake ya sasa na baadae, alipotahamaki hata kashata
alizokuwa akila zilikwisha moyoni akajiuliza kama aliagiza kashata au ameshazila
zimekwisha! Hilo nalo likawa jambo jingine ambalo lilikosa jibu kabisa.
“Chausiku!!” aliita kwa nguvu kana kwamba aliyekuwa anamuita alikuwa umbali wa
kilomita kadhaa lakini kumbe wote walikuwa hapo jirani tu.
Watu walishtuka kwa sauti hiyo hata wengine walidiriki kumtupia maneno yasiyostahili
“Samahani waheshimiwa!” aliomba msamaha
“Samahani nini mjinga wewe!” mmoja alitamka kwa hasira
“Wengine tuna BP utatuuwa bure sura ka Sokwe!” mwingine aliongeza
Amata aliumia sana moyoni kwa tukio lile, akainamia mezani, akatikisa kichwa kisha
akasimama kwa hasira na kuelekea eneo la kunawia mikono, akajitazama kwenye kioo,
akatabasamu, kisha akageuka na kurudi alipoketi kwanza.
Kabla hajaketi alisikia sauti nyuma yake
“Umejiona ee? Ka sokwe, tena wa Gombe!” mmoja alimkejeli, wengine wakaangua
kicheko cha dharau na kupiga miluzi.
Hasira za ghafla zikamrudia Amata, akageuka na kuelekea upande ambao sauti ile
imesikika
“Nani aliyesema vile?” aliuliza kwa kung’aka, wakacheka tena
“Ukimuona utamfanya nini? Fala wewe mtoto wa porini!!” mwingine alisema na
wengine wakaangua kicheko. Amata alipiga hatua mbili mbele na kumkunja shati yule
aliyesema maneno hayo akamuinua kwa nguvu akamrusha chini, huyo akaanguka chini
mzimamzima kama gunia, jamaa akanyanyuka kwa hasia na kumvamia Amata, Amata
akamdaka na kupiga vichwa vitatu vya nguvu akamsukuma kidogo na kumrushia
makonde kama mvua, kijana yule alichanganyikiwa hata hakuweza kujibu mashambulizi
alianguka chini mara ya pili.
“Ameua! Ameua! Ameua!” kelele za watu zilijaza mgahawa ule mara watu wakajaa
wanataka kumshika Amata. Yule kijana bado alikuwa chini hajitambui kwa kipondo cha
ghafla alichokipata. Amata aliruka kutoka aliposimama akatua juu ya meza na kutaka
kutoroka kwa kupitia dirishani, watu walimgombania kwa kumshika shatia wengine
suruali, masikini Amata shati lake lilichanika vibaya akabaki na fulana ya ndani na
kuwaachia shati wananchi wenye hasira, alliruka kupitia dirisha la mgahawa huo na
kudondokea kwenye lundo la mawe kwa kutanguliza mkono, alihisi maumivu makali ya
mkono lakini alipogeuka aliona watu wale wanakuja pale alipo, akanyanyuka na kutimua
mbio
“Huyo huyo! Kamata muuaji huyo!!” kelele za wananchi wale zilikuwa kama kichocheo
kwa kijana Amata kuongeza spidi. Mara kwa mbele aligongana na pande la mtu na
kuangushwa mbali, alinyanyuka na kuanza kukimbia tena, watu walitoka majumbani na
kumuunganishia kama kawaida ya wananchi. Mbio ziliendelea na wananchi nao
hawakuchoka, alitokea kwenye wigo wa nyumba la! Hapakuwa na njia aliruka na kupanda ukuta kisha akatokea upande wapili na kupanda tena alitua chini kwa miguu
yake mikakamavu na kutimua mbio lakini la haula! Alipokuwa akijaribu kuvuka kichaka
kidogo katika eneo hilo alijikwaa vibaya na kuanguka chini, mchezo umekwisha. Watu
wakamkamata na kuanza kumpiga hata kumuumiza vibaya, Mungu si Athumani polisi
waliwahi kumuokoa kutoka kwenye mikono ya watu wenye hasira.
“Tuachie huyo tummalize! Muuaji huyo!” watu walipiga kelele na wengine bado
walidiriki kurusha hata mawe ambayo baadhi yaliwapata askari wale. Askari mmoja
akafyatua risasi hewani na watu wale wakatawanyika kwa woga wakikimbia uku na huku
wengine wakianguka na kukanyagana vibaya. Amata alichukuliwa mpaka kituo kidogo
cha polisi akiwa hatamaniki kwa jinsi alivyolowa damu hata fulana yake aliyobaki nayo
baada ya kuwaachia shati watu wale haikujulikana kama ni nyeupe au nyekundu, juu ya
jicho lake la kushoto jeraha kubwa lilikuwa bado linavuja damu, mkono wake umevimba,
kucha ya kidole gumba cha mguu wa kushoto haikujulikana hata imeng’okea wapi.
Askari wale walimpiga Tanganyika jeki bila huruma wala kujali kuwa mwenzao
ameumia namna ile wallimkokota tena na makofi juu mpaka kituo kidogo cha polisi na
kumlundika selo.
Ndani ya chumba kidogo cha selo katika kituo cha polisi cha kijiji wahalifu walijazana
mpaka hewa haikutosha kabisa, walichoka na hata wengine kukosa nguvu, kupoteza
fahamu kwa kukosa hewa ya kutosha. Amata aliingia kwenye selo hiyo katika hali ile
aliyokuwanayo, akakaribishwa na joto na harufu mbaya haja kubwa na ndogo
zilizochanganyika, mwanga hafifu uliopita katika kadirisha kadogo kenye ukubwa wa
mlango wa banda la njiwa ndio pekee kalikokuwa kanatoa faraja kwa binadamu hawa
waliokuwa na makazi ya muda ndani ya chumba hiki, wote walikuwa na sura za kutisha
ambazo bila kuuliza utajua kuwa sasa nimeingia kuzimu.
Ucku huo ulikuwa mrefu sana kwa Amata, mawazo mengi yalitawala kichwa chake,
maumivu makali yaliusumbua mwili wake, alijituliza kimya kwenye moja ya kona za
kijichumba hiko huku akisikia kichefuchefu kama mama mjamzito kila mara alitamani
kutema mate lakini atatemea wapi watu wamejazana hata wengine wamekaa kwa
kupakatana mh! Mawazo yaliendelea kumsonga hata usingizi mwepesi
uliokatishwakatishwa kwa nyimbo za kuchukiza za mbu masikioni mwake ulikuja na
kuondoka, aliwaza jinsi anavyoishi kwa tabu bila Baba wala Mama wa kumtetea, japo
aliachiwa shamba kubwa na kibanda cha kuishi lakini hakuujua uelekeo wa maisha yake,
“alikuwa analinga na Baba yake, ataona sasa” wengi walisema hivyo, Amata aliona ama
jamii yote haimtaki, dunia imemchukia au ulimwengu unampa adhabu?
“Kwa nini mimi?” alijiuliza uliza moyoni mara kwa mara hasa alipokuwa kwenye
kibanda chake huko shambani kwao ambako alipitisha maisha yake ya ujana tangu
wazazi wake walipofariki yeye akiwa na umri wa miaka michache nyuma, mama yake
aliuawa na Simba alipokwenda kuchota maji nje kidogo ya shamba lao ijapokuwa Baba
yake alijaribu kumtetea dhidi ya Simba hao wakali wenye uchu wa nyama lakini hakufua
dafu ‘kidole kimoja hakivunji Chawa’ alipiga kelele za msaada lakini hakuna aliyekuja.
Lakini Baba yake alikufa baada ya kuugua kwa muda mfupi miaka michache baadae.
Kila aliporudiwa na picha hizi alilia sana na kujiona kuwa yeye ni binadamu mwenye
mkosi, akuwahi kuwa na kaka wala dada isipokuwa ndugu tu ambao pia hawakuwa na
msaada nae kabisa. Amata!!!” aligutushwa na sauti kali ya askari iliyotokea kwenye kadirisha ka mlango wa
selo hiyo.
“Afande!” aliitikia kwa uchovu na kujaribu kujiinua kutoa alipokuwepo lakini alijikuta
anapata kizunguzungu na kuwaangukia wenzake waliokuwa hapo. Alifika mlangoni pale
kwa shida mbele yake alimuona msichana mrembo sana kasimama, mrefu wa wastani
maji ya kunde, alivalia vizuri suruali yake ya kitambaa nyeusi na blauzi yake nyeupe
huku shingoni kafunga skafu yenye mchanganyiko wa rangi, nywele zake fupi
zilizokatwa kiumahili na vinyozi wanaojua kazi yao, kiatu chake kirefu kilimfanya
aonekane kuwa ni mrembo anayetunzwa na pedeshee fulani. Dada yule alijivuta taratibu
mpaka kwenye dirisha lile. Amata alipokea pumzi safi iliyonukia na kuvutia kutoka kwa
mrembo huyo, hakuamini anachokiona ni malaika au binadamu, aliduwaa, akapigwa na
bumbuwazi, mikono yake ikiwa imeshika nondo mbili zenye kutu alijikuta anaishiwa
nguvu. Mrembo yule alishika nondo zile kwa kubana mikono ya Amata akaiangalia sura
ya Amata iliyochoka na kukaukiwa na damu..
“Saringo! Naitwa Saringo” almwambia Amata kwa sauti ya chini
“Hunijui, ila utanijua punde tu” aliendelea “Haujaua ila umeumiza vibaya, sasa unastahili
zawadi kwa kazi uliyoifanya bila kujua, na zawadi hiyo utaipata ukimaliza kazi yako”
Saringo alishusha pumzi na kumwangalia Amata usoni na kumuona jinsi
alivyochanganyikiwa, akaendelea kumwambia mashairi yake yasiyoeleweka kwa mtu
mwenye akili timamu, sasa kwa kukunja sura akamwambia Amata “ Lazima ufungwe,
uishie jela!” akageuka nakuondoka zake. Amata akazidi kulowa jasho, maswali yasiyo na
majibu yalimzunguka tena ‘nilijua malaika mwema kaja kuniokoa kumbe malaika mbaya
wa mauti kanitembelea’ alijiwazia na kuanza kulia. Amata hakupata jibu mwanamke yule
ni nani, na anataka nini, utata. Asubuhi ile kalandinga liliwachukua mpaka mahakama ya
kijiji, jalada la Amata lilikuwa la tatu kuitwa, taratibu akiwa na pingu mikononi
aliingizwa katika chumba cha hakimu na kusomewa mashitaka ya kudhuru mwili,
alijikuta hana cha kukana isipokuwa kukubali, kesi ikahairishwa mpaka baada ya siku
kumi na nne. Walipokuwa wanarudi kwenye kalandinga alimuona binti yuleyule akiwa
amesimama katika kundi la watu waliokuja mahakamani hapo, muonekano wake ulikuwa
tofauti na wote pale kwani ndiye aliyevaa nadhifu kuliko wote ‘huyu ni nani?’ Amata
alijiuliza hakupata jibu, moyoni alimlaani kuliko anavyomlaani shetani walipogongana
macho Amata alitema mate chini na kumuonesha kidole cha kati. Mara alijikuta
anatandikwa kofi la kisogoni au vijana huita ‘mbata’
“Panda juu unatuchelewesha!” sauti kali ya askari ilisikika. Amata na wengine
wakapanda na lori lile kuondoka kwa kasi.
[emoji814][emoji814][emoji814]
“Una mpenzi mzuri sana, mtoto kaumbika kama Malaika, he he he mbona wewe na yeye
hamuendani kabisa au wewe ni mchunga ng’ombe wao!” mmoja wa mahabusu
alimuuliza Amata kwa sauti mbaya ya kukwaruza isitoshe inatisha. Amata aligeuka na
kumwangalia akatabasamu kwa sura iliyochoka
“Simjui hata anatoka wapi” alimjibu
“Kwangu ni kama shetani tu yule, anataka kuniua, kunifunga, hilo ndilo limemleta hapa”
aliendelea kumueleza yule mahabusuKwa nini aje kukuona asubuhi yote ile? Au kuna uhusiano wowote na kesi yako?”
aliendelea kudadisi mahabusu yule,
“Sijui chochote! Mbona maswali mengi umempenda? Mfwate basi, mi nshakwambia
smjui! Yule ni shetani tu” Amata alijibu kwa hasira kidogo na mahabusu yule
hakuendelea na maswali yake.
Kesi ilitajwa tena baada ya siku kumi na nne, Amata na wenzake wakiwa na pingu
mikononi waliingizwa katika chumba maalumu cha mahabusu mahakamani hapo, Amata
alisimama karibu na mlango, mara ghafla alipata mshtuko mkubwa, hakuamini
alichokiona nje ya jingo hilo, akakaza macho kutazama kwa makini akayafikicha kidogo
aone labda alikuwa ndotoni lakini hapana alichokiona ni sahihi na macho
hayakumdanganya. Hakutaka kupoteza hata sekunde katika lile alilokuwa anliona lakini
bahati mbaya hakuweza kusikia kinachozungumzwa. ‘Yule sio Chausiku?’ alijiuliza
moyoni lakini pia hakutaka kuyaamini macho yake.
Chausiki Binti Saidi, msichana mfupi mwenye afya njema kibonge, mmiliki wa mgahawa
unaojulikana kwa jina la Chau Café, msichana huyu ambaye amekuwa pamoja na Amata,
wamesoma shule moja ya msingi kijijini hapo na kucheza michezo mingi ya utoto
pamoja, yeye alifanikiwa kufika japo darasa la saba wakati Amata alifukuzwa shule
akiwa darasa la tano kwa kisa cha kumpiga mawe mwalimu wake wa darasa. Maisha
yalimwendea kombo Amata kielimu japo alijitahidi sana katika rasilimali alizoachiwa na
marehemu baba yake Chausiku alimpenda kutokana na bidii yake katika kazi. Watu
walimbeza sana Chausiku kwa jinsi alivyoonesha upendo kwa Amata hii ikapelekea
Chausiku kutokuwa karibu sana na kijana huyu ambaye japo aliugusa moyo wake,
pamoja na ukorofi lakini hakuweza kumtoa moyoni mwake, moyoni mwa Chausiku
Amata alikuwa kama maji yatuliavyo mtungini yasipoguswa. Vijana wengi walipenda
kwenda mgahawani kwake japo tu roho zao zisuhuzike kwa kumuona binti huyu, wapo
waliomdanganya kwa pesa na vitu mbalimbali lakini msimamo wake thabiti
haukumfanya ayumbishwe na vitu vyote hivyo bali aliuacha moyo wake utue kama
kipepeo atuavyo katika ua alilolichagua.
Chausiku aliumizwa sana na kisa kilichomkuta Amata, alijua kuwa Amata kwa hali
aliyonayo asingeweza kupata msaada wowote wa kisheria au utetezi katika kesi yake,
alijitahidi kufanya kila awezalo ili tu amsaidie Amata katika hili.
Jalada la Amata liliitwa, polisi walimtoa katika chumba kile akiwa chini ya ulinzi na
kupelekwa katika chumba cha mahakama, akiwa anapita katika kikorido kidogo cha
jengo hilo alisikia sauti nyembamba tamu ikipenya masikioni mwake, ilikuwa si ya
mwingine bali Chausiku ambaye alikuwa akilia kwa machozi mazito “Mnyezi Mungu
akusaidie” ni maneno aliyomwambia, Amata aligeuka kwa kuiba, alifarijika kuona
kumbe wapo katika binadamu awa hawa wanaompenda, kidogo alijisikia mtu kati ya
watu.
Kesi ya Amata ilikwisha alihukumiwa kifungo cha miaka miwili na miezi sita jela.
Waliondolewa mahakamani na Amata alianza kutumikia kifungo chake huko gereza la
kilimo Sogera, gereza lenye kazi ngumu, kulima, kupanda, kuvuna, muda wote mkiwa
katika matope, maji machafu, mnakula chakula huku mnanyeshewa na mvua, mateso!.