RIWAYA: Msitu wa Solindo

RIWAYA: Msitu wa Solindo

MSITU WA SORONDO

Mtunzi Richard Mwambe

Simu 0754740668

Sehemu 5


Nini Amata?” Hellen alimuuliza
“Chatu! Nyoka mkubwa anayeweza kumeza mtu” Amata alijibu. Hellen akajificha
nyuma ya Amata, Saringo alikuwa akiangalia kwa makini lakini hakuweza kuona cha
kufanya alisubiri kuona nini Amata anataka kufanya, kwa upole Amata aliweka mshale
sawia katika uta wake na kuvuta kwa nguvu zake zote, mikono yake iliyojaa misuli ya
nguvu ilituna na kuonesha kiasi gani nguvu alizotumia kuvuta uta huo, huku akiongea
lugha isiyoeleweka akiwa ameuma meno bado hakuachia pigo lake, kilichoonekana ni
jinsi tu alivyoutembeza uta huo taratibu sana kutoka upande mmoja kwenda mwingine.
Kutoka ndani ya mitete ile nyoka mkubwa alifyatuka kwa spidi ya ajabu kuelekea mtoni
alipo Stephan, Amata aliachia uta wake na mchale uliondoka kwa spidi kali kukikabili
kichwa cha nyoka yule, hamad!!
“Stephannnnnnn!!!!!” Hellen alipiga kelele ya nguvu na Stephan alipogeuka alishuhudia
joka kubwa refu lililofungua domo lake likimuelekea, mara alishuhudia kitu kikipita kwa
kasi kati yake na joka lile, ulikuwa mshale wa Amata aliopigwa kwa ustadi lakini
kutokana na ukelele wa Hellen Joka lile liligeukia upande ulikotoka ukelele hivyo
kufanya shabaha ya Amata kuwa ya bure. Joka lile lilijivuta na kuburuzika chini
likijikunjakunja kuelekea walipo akina Amata, Amata alijinyanyua na kujirusha upande
wa pili akimvuta Saringo wakati huo Helleni alijiinua na kujikuta amechelewa, alipigwa
ngwala maridadi sana na joka lile na kupaishwa juu, kabla hajafika chini joka lili
lilimdaka kwa ustadi mkuwa na kujiviriga mwilini mwake, likiwa linadondoka kwa kwa
kasi, Amata alikuwa tayari kesha vuta uta wake na kuuwachia, shabaha ya ajabu! Mshale
ule ulipenya sawasawa karibu kabisa na kichwa cha joka lile, kutokana na maumivu yale
joka lile likamuachia Hellen na kudondoka chini Hellen nae akadondoka juu yake, Joka
lile likajivuta tena kumkimbiza Amata, amata hakukimbia mbali bali aliuzunguka mti ule
waliokuwa wamekaa huku akiweka vizuri mshale wake wa tatu alijikwaa na kuanguka
vibaya, joka lile likamtia mkononi likamviriga vizuri, bahati nzuri mkono mmoja wa
Amata ulikuwa nje ya mvirigo ule
“Amataaaaa....” Saringo aliita, na kumrushia kisu ambacho Amata alikidaka kwa ustadi
mkubwa na bila kuchelewa alididimiza kisu kile kwenye sehemu ya mwili wa joka hilo,
joka likajiinua juu likiwa bado halijamuachia Amata, Amata alisikia mvumo mkali na
alichokishuhudia ni damu iliyoruka kwa matone makubwa makubwa, joka lile halikuwa
na kichwa tena, likaanguka kwa mshindo mkuu, ilikuwa ni risasi kutoka AK 47
iliyopigwa kwa ustadi wa hali ya juu na Stephan na kukitawanya kichwa cha joka lile na
kukichanachana vibaya.
“Nice shot!!” Hellen alimsifu Stephan, wakakumbatiana na kubusiana kama ishara ya
kupongezana. Saringo alimfuata Amata pale alipolala na kumsaidia kujitoa katika joka
lile, haikuwa kazi rahisi kuukunjua mwili wa joka lile kubwa ambao kwa wakati huo
ulikuwa bado umejiviriga katika mwili wa Amata. Helen na Stephan nao waliungana na
Saringo katika kazi hiyo, mara wakafanikiwa na kumnasua Amata ambae uso wake
ulikuwa umechafuka kwa damu ya joka lile, wakamlaza vizuri na kumuosha uso wake.
Mikono laini ya Saringo ilipita usoni mwa Amata, Amata akajitikisa kidogo na kuushika
mkono wa Saringo
“Nini Amata?” saringo alimuuliza
“Mkono wako laini umenisisimua mwili...” Saringo akatabasamu aliposikia maneno hayo
ya Amata Usianze Amata!” Saringo akasisitiza. Amata aliketi na kutazama vizuri huku na huku,
akaokota uta na podo lake akaweka mgongoni... safari inaendelea!
Msitu ulizidi kuwa mnene mbele yao, lakini Stephan aliyekuwa na ramani ya wapi
wanakokwenda alisisitiza kuelekea upande huo hata kama haukuwa na njia, walisonga
mbele, panda milima, shuka, vuka mto pasua vichaka, mvua, jua vyote vilikuwa juu yao,
chakula kikubwa kilikuwa ni matunda ya porini ambayo kwayo walijitosheleza na
kujipatia vitamini za kutosha sio mpaka akuandikie daktari.
Jioni hiyo ya siku ya tatu mvua ilikuwa kubwa sana, radi zisizo na huruma zilipasua anga
lote na kulifanyia michoro ya kutisha, hapakuwa na pa kujikinga wala kujificha, wote
walitota miili hata nguo zao kugandamana na miili yao, walitetemeka kwa baridi kali ya
msituni hata miguu ilishindwa kutoa ushirikiano na mwili mara nyingi ilikataa kusonga
mbele, hakukua na lakufanya isipokuwa ni kujivuta hivyo hivyo, walitamani jua liwake
haikuwa hivyo, walipenda wakoke moto lakini kila kitu kililowana, safari ilizidi kuwa
ngumu kwani msitu wote ulifunikwa na ukungu mzito hata mwanga wa tochi haukufua
dafu. Amata alisimama na kugeuka nyuma akawaonea huruma wenzake maana walikuwa
wakitetemeka kupita maelezo. Saringo alimuendea Amata na kumkumbatia kwa nguvu
huku akitetemeka, vivyo hivyo kwa Hellen na Stephan, walivuta hatua fupifupi japo kwa
shida kujitafutia mahali pa kupumzika.
“Tukae humu mpenzi!” Amata alishtuka kidogo kusikia kauli hiyo toka kwa Saringo,
alibaki kujiulizauliza maana hajawahi kuitwa mpenzi katika maisha yake. Amata
alitazama na kuona pango pembezoni mwa mti kabla hajaamua cha kufanya Stephan na
Hellen wakawa tayari wamejitoma ndani ya pango hilo lenye kiza,
“Amata twende!” Saringo alisema huku akimvuta mkono kuelekea pangoni, Amata
alimvuta Saringo kwa nguvu na kumkumbatia kifuani mwake, akamkazia macho Saringo
alimtazama Amata usoni kwa hasira lakini hakuwa na la kusema alizungusha mikono
yake mgongoni kwa Amata na kuikutanisha kisha kuegemeza kichwa chake kifuani mwa
Amata. Amata alitulia kimya kwa muda akiangalia lile pango waliloingia akina Stephan
“Saringo! Unafikiri hilo ni pango? Isije kuwa mtego tu” Amata alimuuliza Saringo
“Wenzetu wameingia wewe hutaki, Amata una nini twende!” Saringo alisisitiza
“Saringo! Mbona hatumsikii Stephan au Hellen hata kutuita!? Nina wasiwasi hili si
pango la kawaida!” Amata aliposema maneno hayo Saringo akashtuka na kugundua
kuwa ni kweli hawa viumbe wawili wangeshawaita lakini kimya yapata dakika mbili
sasa, Saringo akamuachia Amata, akaokota kipande cha mti kilicho jirani hapo
akakirushia ndani ya pango lile lakini hakusikia chochote hata mdondoko wa kipande cha
mti, Saringo akajishika mdomo na kuanza kutoa machozi.
“Saringo! Hapa ni msituni, usilie, tulia, jikaze kama mwanamke. Kilichobaki hapa ni
kutafuta cha kufanya kwa kuwa sasa tumebaki wawili wenzetu tayari msitu umewameza”
Amata alimbembeleza Saringo
“Hatuna silaha za kutosha itakuwaje kupambana na maadui?” Saringo alimuuliza Amata.
Amata akatazama podo na uta wake akajikuta kabakiwa na takribani mishale kumi na
tano podoni, akatikisa kichwa akaingiza mkono kwa ndani ya suruali yake kama
anayetaka kutoa dhakari ili ajisaidie, Saringo akasogea pembeni kidogo kwa hofu maana
hakujua Amata anataka kufanya nini, alipotoa mkono ukatoka na bastola moja. Saringo
alishangaa
“Umeipata wapi?” Saringo alimuuliza Amata Alinipa Hellen nimuhifadhie” alimjibu Saringo na kumtupia swali
“unajua kuitumia?”
“Ndio!” Saringo akajibu huku akiichukua mikononi mwa Amata na kuigeuzageuza kisha
akatikisa kichwa kuashiria amekubali, akajaribu kama analenga kitu, Amata akampatia
kikasha kimoja cha risasi, Saringo akakipokea na kukihifadhi vizuri...
[emoji814][emoji814][emoji814]
Stephan na Hellen waliingia kwenye kitu kama pango lakini halikuwa pango la
kawaida bali ni kama shimo lakini halikuenda chini isipokuwa lilikuwa na mteremko
mkali sana, hawakuweza hata kufanya lolote bali waliporomoka ndani kwa kasi ya ajabu
na huku kulikuwa na giza nene kuliko giza lenyewe, waliendelea kuseleleka hakuna
aliyepiga kelele kwana kati yao kila mmoja alikuwa akitahamaki. Baada ya kama dakika
tano za mseleleko ule Hellen alijigonga kwenye kitu kama ukuta au jiwe na kupoteza
fahamu, Stephan hakujua afanye nini maana giza ni nene, huku akiwa anavuja damu
mkononi mwake kwa kuwa alichunika vibaya sehemu ya nyuma ya mkono wake, alitoa
kiberiti na kuwasha angalau apate mwanga kidogo, lakini mwanga ule bado haukufua
dafu kwa giza lile. Stephan aliegeme kitu kama ukuta lakini alihisi ulikuwa rafu sana
alijaribu kuvuta hisia na kutega sikio lake kwa makini labda atasikia chochote ama watu
kuongea au chochote, lakini hakusikia kitu, taratibu macho yalianza kupambana na giza
lile na kuanza kuona japo kidogo, akiwa bado katika kutambua kilichopo ndipo aliposikia
kwa mbali mtweto wa mtu anayehitaji msaada, mara moja akagundua kuwa bila shaka ni
Hellen lakini hakujua upande upi hasa yupo akajaribu kuita kwa upole, lakini bado
aliendelea kuusikia ule mtweto ambao kwa sasa ulikuwa wa taratibu lakini ulisikika
kutokana na ukimya wa mle shimoni, alijaribu kupanda taratibu haikuwa rahisi kwa kuwa
hapakuwa na pakujishikia ila tu alisaidiwa na vipande vya mawe vilivyochomoza huku
na huku, mara akamfikia Hellen ambaye alikuwa amenasa kwenye jiwe fulani kumbe
hakuwa mbali na pale alipoangukia Stephan, alijaribu kumnasua pale aliponasa na lile
jiwe likang’oka kumbe lilishikwa tu kwa udongo, wakaporomoka nalo mpaka pale chini.
Stephan alitoa mguno wa uchungu na kishindo kile kilimrudishia fahamu Hellen, Hellen
aliangalia huku na huku na kumgeukia Stephan
“Tuko wapi Stephan? Amata na Saringo wako wapi?” hellen aliuliza huku akionesha
kuweweseka. Stephan alimtuliza akiwa hajui nini cha kufanya zaidi kwa wakati ule
alitazama uku na huku na akagundua kuwa lile shimo lilikuwa linaendelea lakini sasa si
kwa kwenda chini bali tambarare ambapo unaweza kutembea ukiwa wima, bila kupoteza
muda alisimama na kumuinua Hellen, akiwa bado na bunduki yake mgongoni walianza
kutembea taratibu ndani ya shimo lile wakiwa hawajui wapi wanakoelekea,Hellen
alikuwa anamfuata tu akijua labda Stephan anajua chochote, waliendelea kwenda nusu
wakitembea na nusu wakikimbia ili mradi wafike wanakokwenda. Hellen alianza
kushikwa na woga aliushika mkono wa Stephan kwa nguvu zote akiwa anatweta kwa
nguvu, mara Stephan akasimama akainama na kushika magoti yake huku akitingisha
kichwa kwa masikitiko “...tumekwisha! Hellen, sijui hata tuendako”. Alichukua bunduki
yake nakufanya kama analenga kitu lakini hakuna alicholenga akafyatua binduki yake na
ukelele wa bunduki hile ulijirudia mara nyingi kabla hakujakua kimya tena, haja yake
asikie tu kama kuna mlio mwingine utakaosikika zaidi ya huo wa bunduki hiyo. Taratibu
waliendelea kutembea na kutembea mwisho walichoka na njaa iliwashika wakaketi chini
na kila mmoja alipitiwa na usingizi kwa muda wake
Safari ilikuwa ngumu kwa Amata na Saringo, chakula chao kikiwa ni matunda ya
mwituni na maji ya mtoni, waliendelea kwenda wakiwa hawajui hasa ni upande upi
ambao wanatakiwa kuelekea.
“Nahisi tunapotea !” Saringo alisimama na kusema huku kajishika kiuno
“Tufanyeje sasa! Tuendelee mbele labda tutajua la kufanya” Amata akamjibu huku
akimshika mkono akimaanisha safari iendelee. Saringo ambaye wakati huo alioneka uso
wote kusawajika kwa uchovu alijivuta kwa hatua za taratibu na kufuata kule
alikoongozwa na Amata.
“Twende mpaka tupate mahali pazuri pa kupumzika maana jioni nayo imeshakaribia”
Amata alimueleza Saringo huku wakiendelea na safari hiyo isiyo na mwisho bali yenye
hatari na misukosuko mingi. Baada ya kutembea kwa muda walifika eneo moja ambalo
liko wazi sana kama kiwanja cha mpira lakini ilikuwa ni katikati ya msitu, katika eneo
hilo kulikuwa na nyasi nzuri za kijani fupifupi lakini katikati kulikuwa na mbuyu
mkubwa sana mnene ambao juu yake aulionesha wazi kuwa kulikuwa na mibuyu
iliyoning’inia, Amata alisimama kabla ya kuingia katika uwanda ule akatafakari mawili
matatu, akamgeukia Saringo
“Umeona! Umeona mbuyu ule?” alimuuliza saringo ambaye kwa wakati huo alikuwa
kamuegemea Amata begani kwa upande wa mgongo.
“Huu ni uwanja au kitu gani?” Saringo naye alitupa swali kwa Amata,
“Hapana huu si uwanja hapa lazima kuna kitu, Stephan alitueleza kuhusu mbuyu siyo
ule?” Amata alimuuliza Saringo, kwa hamaki kubwa saringo aliutazama mbuyu ule,
kikapita kimya cha dharula. Akatikisa kichwa kwa ishara kuwa amekubaliana na Amata
“Yeah utakuwa ndio wenyewe! Alisema upo katikati ya uwanja, ndiyo nimekumbuka,
ndiyo utakuwa ni huu” saringo aliongea kwa upole sana katika hali ya kushangaa.
“Mbuyu wa Shetani!!!” Amata aliongezea kwa upole uleule
“Unasemeje Amata? Mbuyu wa Shetani?!” Saringo alimwangalia Amata usoni na
kumtupia swali lile.
“Ndiyo Saringo, ule ni mbuyu wa Shetani! Unaitwa Mbuyu Kolo... mbuyu wa maajabu,
babu yangu alinisimulia mengi sana juu ya mbuyu huu” Amata alimueleza Saringo huku
akiwekaweka manyasi vizuri kwa kukaa chini.
“Saringo!” Amata aliita taratibu na saringo alimgeukia “Bee, Amata unasemaje?” huku
akikaa katikati ya miguu ya Amata na kumlalia kimgongo kifuani.
“Ni nini mnakitafuta huku porini? Na akina Stephan?” Amata alimuuliza Saringo.
“Ni stori ndefu sana Amata, ndefu mno” Saringo akashusha pumzi ndefu na kumeza mate
kwa shida kutokana na ukavu wa midomo yake.
“Niambie tu, maana hapa tutalala ili kesho tujue cha kufanya, ila lazima tulale juu ya mti
kuepuka wanyama wakali wenye uchu na nyama tamu yenye chumvi ya Binadamu”
Amata alimueleza hayo saringo huku mikono yake akimzungushia saringo kwa mbele
kwa kuipitisha chini ya makwapa yake, alifikiri atapata upinzani kwa kitendo hicho lakini
la, Saringo aliivuta na kuikutanisha juu ya kifua chake kisha akainamisha kichwa kwa
nyuma na kumuangalia Amata kwa juu “nakupenda Amata!” alimwambia huku
akitabasamu, AmataAmata! Tukimaliza safari yetu tutakuwa matajiri sana, tunakwenda Solondo kuchukua
sanduku kubwa na ndani ya sanduku hilo kuna mali nyingi sana, dhahabu, almasi, yaspi,
lulu za aina mbalimbali, mawe ya thamani tofauti”. Saringo alimwambia Amata, Amata
alimkazia macho saringo
“Nani aliyekwambia Saringo?! Solondo ni msitu wa kifo, msitu unaokuwa hai na kumeza
kila aingiyae...”Amata alieleza lakini saringo alimkatisha “Hapana amata, hizo ni hadithi
za kale, si za kuamini, wazee wetu walitusimulia ili tuogope kabisa kuingia ndani ya
msitu huu lakini ukweli ni kuwa ndani ya msitu huu wajerumani wamehifadhi vitu vingi
sana na babu wa baba yangu alikuwa askari wao amekuja sana huku kuleta vitu
walivyokuwa wakivichimba huku na huko katika nchi yetu! Watu wengi waliuawa na
wajerumani ndio na hawakurudi tena vijijini mwao ndio maana hizo hadithi zenu
zikawepo” saringo aliongea kwa jazba
“...hadithi zenu !!! hadithi zenu!!!” Amata alijiwazia moyoni akijaribu kulinganisha
asemayo Saringo. Amata akashusha pumzi akibaki na maswali mengi kichwani akatoa
pera akaanza kutafuna huku akichezesha kichwa chake kama mtu anayefuatisha muziki
fulani. Wakiwa katika hali ya ukimya sana kila mtu alizama katika mawazo yake ambayo
hakuna mwingine aliyeyajua
“Dunia imekuharibu umesahau mila na desturi za nyumbani” aliropoka Amata
kumwambia Saringo, Saringo alihamaki kwa kauli ya Amata na kumtazama usoni sasa
sio kwa sura ile legevu bali yenye jazba na uchungu
“Unasemaje Amata?!.. wewe unaendekeza ujinga na upumbavu wa kijijini! Hujui hata
dunia upande wa pili inaendeleaje, lazima maisha yabadilike, mimi naishi mjini naelewa
lakini wewe umezaliwa na kukulia huku porini utajua nini, fuata nnayokwambia” saringo
alifoka.
“ Huwezi kuniamrisha kufuata unayonambia wewe ni mwanamke tu, kama mimi
nimekulia huku mshamba wa kizamani kwa nini mlinitafuata katika safari yenu hii isiyo
na miguu wala kichwa, na usomi wenu na maendeleo mliyonayo mngefika wapi?
Stephan yuko wapi , helen yuko wapi? Mbona wamepotea bila kujua, na we bado zamu
yako. Lazima udumishe mila na desturi, asili itabaki kuwa asili tu!” Amata alifoka pia.
“Asili itabaki kuwa asili tu” Maneno haya yalimchoma sana Saringo na yalimrudia mara
kwa mara. Saringo akanyanyuka na kusoge pembeni, akaketi na kuikunja miguu yake
kuelekea kidevuni huku akiwa kaizungushia mikono yake aliinama na kulia kwa
vikwifukwifu.
Giza liliufunika msitu taratibu, sauti za ndege na mbweha zilisikika huku na huko, macho
ya Amata yalikuwa yanapambana na usingizi uliokuwa unayasumbua huku wadudu nao
wakifurahia kuona kiumbe hiko katika makazi yao, hakuona njia nyingine zaidi ya
kutafuna matunda yake aliyoyahifadhi vyema katika mkoba suruali yake ile ya
kimagereza, huku akitumia nguvu nyingi kujaribu kuangazaangaza kuona kama kuna
hatari yoyote inayowakabili, alimwangalia Saringo na kugundua kuwa tayari alikuwa
amelala ‘wanawake bwana!’ alijisemea moyoni huku akitikisa kichwa chake kuonesha
kukata tamaa.
“We mbona unalala kibwege hivyo? Unafikiri uko kwenu hapa!” alimuamsha Saringo
kwa kumtikisa na kumwambia maneno hayo, saringo alinyanyua kichwa na kumtazama
Amata kwa sura yenye mikunjo ya usingizi na uchovu. Amata alitabasamu na
kukumbuka maneno aliyoambiwa na baba yake ‘ukitaka kuchagua mchumba mtazame
anapoamka’ hapo alihakikisha baada ya kuona sura ya Saringo alipotoka katika kipande akapotezea kimtindomtindo.
 
MSITU WA SOLONDO

Mtunzi Richard Mwambe


Sehemu 6


Amata! Tukimaliza safari yetu tutakuwa matajiri sana, tunakwenda Solondo kuchukua
sanduku kubwa na ndani ya sanduku hilo kuna mali nyingi sana, dhahabu, almasi, yaspi,
lulu za aina mbalimbali, mawe ya thamani tofauti”. Saringo alimwambia Amata, Amata
alimkazia macho saringo
“Nani aliyekwambia Saringo?! Solondo ni msitu wa kifo, msitu unaokuwa hai na kumeza
kila aingiyae...”Amata alieleza lakini saringo alimkatisha “Hapana amata, hizo ni hadithi
za kale, si za kuamini, wazee wetu walitusimulia ili tuogope kabisa kuingia ndani ya
msitu huu lakini ukweli ni kuwa ndani ya msitu huu wajerumani wamehifadhi vitu vingi
sana na babu wa baba yangu alikuwa askari wao amekuja sana huku kuleta vitu
walivyokuwa wakivichimba huku na huko katika nchi yetu! Watu wengi waliuawa na
wajerumani ndio na hawakurudi tena vijijini mwao ndio maana hizo hadithi zenu
zikawepo” saringo aliongea kwa jazba
“...hadithi zenu !!! hadithi zenu!!!” Amata alijiwazia moyoni akijaribu kulinganisha
asemayo Saringo. Amata akashusha pumzi akibaki na maswali mengi kichwani akatoa
pera akaanza kutafuna huku akichezesha kichwa chake kama mtu anayefuatisha muziki
fulani. Wakiwa katika hali ya ukimya sana kila mtu alizama katika mawazo yake ambayo
hakuna mwingine aliyeyajua
“Dunia imekuharibu umesahau mila na desturi za nyumbani” aliropoka Amata
kumwambia Saringo, Saringo alihamaki kwa kauli ya Amata na kumtazama usoni sasa
sio kwa sura ile legevu bali yenye jazba na uchungu
“Unasemaje Amata?!.. wewe unaendekeza ujinga na upumbavu wa kijijini! Hujui hata
dunia upande wa pili inaendeleaje, lazima maisha yabadilike, mimi naishi mjini naelewa
lakini wewe umezaliwa na kukulia huku porini utajua nini, fuata nnayokwambia” saringo
alifoka.
“ Huwezi kuniamrisha kufuata unayonambia wewe ni mwanamke tu, kama mimi
nimekulia huku mshamba wa kizamani kwa nini mlinitafuata katika safari yenu hii isiyo
na miguu wala kichwa, na usomi wenu na maendeleo mliyonayo mngefika wapi?
Stephan yuko wapi , helen yuko wapi? Mbona wamepotea bila kujua, na we bado zamu
yako. Lazima udumishe mila na desturi, asili itabaki kuwa asili tu!” Amata alifoka pia.
“Asili itabaki kuwa asili tu” Maneno haya yalimchoma sana Saringo na yalimrudia mara
kwa mara. Saringo akanyanyuka na kusoge pembeni, akaketi na kuikunja miguu yake
kuelekea kidevuni huku akiwa kaizungushia mikono yake aliinama na kulia kwa
vikwifukwifu.
Giza liliufunika msitu taratibu, sauti za ndege na mbweha zilisikika huku na huko, macho
ya Amata yalikuwa yanapambana na usingizi uliokuwa unayasumbua huku wadudu nao
wakifurahia kuona kiumbe hiko katika makazi yao, hakuona njia nyingine zaidi ya
kutafuna matunda yake aliyoyahifadhi vyema katika mkoba suruali yake ile ya
kimagereza, huku akitumia nguvu nyingi kujaribu kuangazaangaza kuona kama kuna
hatari yoyote inayowakabili, alimwangalia Saringo na kugundua kuwa tayari alikuwa
amelala ‘wanawake bwana!’ alijisemea moyoni huku akitikisa kichwa chake kuonesha
kukata tamaa.
“We mbona unalala kibwege hivyo? Unafikiri uko kwenu hapa!” alimuamsha Saringo
kwa kumtikisa na kumwambia maneno hayo, saringo alinyanyua kichwa na kumtazama
Amata kwa sura yenye mikunjo ya usingizi na uchovu. Amata alitabasamu na
kukumbuka maneno aliyoambiwa na baba yake ‘ukitaka kuchagua mchumba mtazame
anapoamka’ hapo alihakikisha baada ya kuona sura ya Saringo alipotoka katika kipande hicho cha usingizi, akarudi alipokaa na kusimama kwa muda kisha alimfuata Saringo,
kibaridi kilichukua nafasi yake msituni hapo na wakiwa wamejikunyata kila mmoja
kamshika mwenzie ili kupata kajoto wakapitiwa na usingizi uliowachukua kwenda
ulimwengu wa mbali.
[emoji814][emoji814][emoji814]
Saringo alibebwa juujuu na watu wa ajabu wenye mguu mmoja huku wakiimba
nyimbo zisizoeleweka, wakizunguka naye katika mduara mkubwa ambao katikati yake
kulikuwa na moto mkubwa sana, ngoma zilirindima, wengine walioketi pembeni
walionekana kunywa kitu kama pombe kwenye kata kubwakubwa huku wakifurahia na
kucheka kwa sauti za ajabu, Amata aliketi palepale akiangali huku akitetemeka kwa
woga wa ajabu, kijasho kilimtoka kila alipotaka kupiga kelele za kuomba msaada
alijikuta sauti haimtoki na wa le viumbe walimcheka sana, akijaribu kujitikisa
hakutikisika kabisa kumbe alikuwa amefungwa katika mti mkubwa uliopo katika uwanja
ule ambao ngoma hiyo ya ajabu ilipigwa na kuchezwa na hawa viumbe wa ajabu. Bado
wale wengine waliendelea kucheza huku wamembeba Saringo juu kwa juu wakipokezana
kwa furaha, mara wakamshusha na kumlaza katika jiwe kubwa lilichongwa kama
ngalawa lakini halikuwa na shimo katikati, akiwa kama alivyozaliwa juu ya lile jiwe
hakuweza hata kutikisika, Amata aliangalia kwa makini akitaka kujua wanataka
kumfanya nini lakini kila alipojitikisa hakutikisika na kila alipofanya hivyo alisikia sauti
za ajabu zikimcheka sana aliogopa na kutulia tuli kama maji ya mtungini.
Ilikuwa ni sherehe ya ajabu ambayo Amata hakupata kuiona tangu azaliwe katika dunia
hii, akiwa katika hali ya kutaharuki hakupenda kuona kinachoendelea, alifumba macho
yake kwa nguvu zote lakini bado akili na moyo wake vilitaka kuangalia kinachoendelea,
aliyafumbua macho yake na alichokiona kilimchanganya kwa kuwa hakuelewa ni nini na
kwa nini,wanawake saba waliokuwa watupu kabisa wakiwa wanatokea ndani ya kitu
kama pango ambalo liko chini ya mti mkubwa kichwani walijitwika vitu kama vyungu
wakiwa wanatembea kwa mwendo wa kurukaruka kwa kuwa walikuwa na mguu mmoja
kila mmoja, waliimba nyimbo zisizoeleweka na wa le wanaume waliombeba Saringo juu
juu na kumlaza pale katika jiwe waliendelea kucheza ngoma ile isiyoeleweka, Amata
alikuwa na woga mkuu akitetemeka mwili wote. Wanawake wale walilizunguka lile jiwe
na kutua vyungu vilivyokuwa kichwani mwao, mmoja wao aliyeonekana kama ndiye
kiongozi wao alitwaa chungu kimoja na kukinyanyua juu kama anayefanya sala fulani,
kisha akakishusha akakiweka pembeni ya miguu ya Saringo akaingiza mikono yake na
kuchota kitu kama mafuta ya kupikia na kuanza kumpaka Saringo akianzia miguuni
kisha na wenzake nao wakafanya hivyo, sasa walimpaka mwili mzima huku wakiongea
lugha ya ajabu ambayo Amata alijaribu kuisikiliza lakini hakuilewa ‘hawa viumbe
gani?!’ Amata alijiuliza bila majibu, aliendelea kutazama kwa woga. Wanawake wale
walipomaliza kazi hiyo walinyanyuka na kurudi kule walikotoka na kumuacha Saringo
akiwa kalala pale aking’aa kwa mafuta yale pindi akiangazwa na mwanga wa moto ule
akiwa kimya kabisa, Amata hakujua kama saringo alikuwa mzima au la maana
misukosuko yote yeye alikuwa kalala kama mfu hakujitikisa wala hakufanya lolote.
Mara wale wanaume wakaanza tena ngoma yao sasa kwa uchangamfu zaidi huku
wakipiga makelele ya ajabu na kurukaruka, ndipo Amata akagundua kuwa ule mguu
mmoja walionao kila mmoja wao huku chini ulikuwa na kanyagio kama la kuku, mara upepo mkali ukaanza kuvuma na wao wakiwa bado wanacheza ngoma yao sasa
wakionesha munkari na jazba zaidi, mara kutoka katika mti ule ambao waliingia wale
wanawake joka kubwa liliibuka kwa kasi ya ajabu,
“Ssss......” Amata alijaribu kumuita Saringo lakini sauti haikuweza kutoka hata kidogo,
joka lile lilijikunjua kwa kuzunguka likiwa hewani sasa likiwa linaelekea pale alipolazwa
Saringo, na liliposikia sauti hafifu ya Amata likageuka huku aliko na kutema mate kwa
kasi kumtemea Amata, mara Amata akazinduka kutoka usingizini, alikuwa akihema
kama mtu aliyekuwa akikimbizwa...
“Saringo, Saringo!” Aliita huku akiweweseka. Alipotulia alijikuta kaloa mwili mzima na
pembeni yake kuna kitu kama kata kubwa liliotelekezwa na ndani yake kulikuwa na maji
kidogo, ndipo alipogundua kuwa kamwagiwa maji na ndiyo yaliyomfanya akurupuke
kutoka katika usingizi wake, lakini nani alimwagia maji hakumjua wala hakumuona,
wala Saringo hakumuona eneo lile, alipoangalia vizuri aligundua kuwa hakuwa pale
ambapo alipitiwa na usingizi, hapa ni mahali pengine kabisa ambapo hakupajua kabisa,
aliangaza macho huku na kule lakini hakuona dalili ya mtu wala mnyama, palikuwa
patupu miti ikiwa imezunguka kwa mbali na katikati palikuwa wazi ni nyasi fupifupi tu
zilijaa katika eneo lile. Alijinyanyua kutoka pale alipokaa na kusimama wima, alivuta
ukimya kidogo kuona kama kuna kitachotokea awe mtu au mnyama lakini hali libaki
kuwa ileile ‘hapa ni wapi?’ Amata alijiuliza lakini hali ilikuwa ni ile ile, mara nyuma
yake akasikia sauti ikimwita kwa kunong’ona ikirudiarudia jina lake, amata alitulia na
kimya huku akiwa hajui cha kufanya, moyo ulimdunda kwa kasi akageuka taratibu kuona
ni nani aliyemuita, Amata alitahamaki, hakuamini macho yake alichokiona...
Bibi kizee aliyechoka, ngozi yake imekauka kwa kukosa vitamini, macho mekundu ya
kutisha, nywele zote nyeupe na unaweza kuzihesabu, miguu yenye vidole visivyo na
kucha, Amata alimwangalia kwa umakini ajuza yule lakini moyoni akijawa na hofu,
‘hakika ajuza huyu angekuwa kwenye mikoa ya upande fulani wa nchi mojawapo ya
Afrika Masahariki hakika asingekuwepo hii leo hasa kwa macho yake’ mawazo haya
yalipita haraka kichwani mwa Amata. Ajuza yule hakuwa hata anatikisika alisimama
vilevile huku akisaidiwa kwa mkongojo ule alioushika, alimkazia macho Amata, kwa
wakati huo Amata hakujua la kufanya, akimbie? Hapana, Amsalimie? Hakuna jibu, sasa
afanyeje hakika ulikuwa mtihani mkubwa sana kwake, “Amata...” bibi yule aliita tena
kwa sauti ya kukwaruza na mbaya huku akimwangalia Amata, Amata alimwangalia kwa
umakini na kuanza kurudi nyuma taratibu
“Usiogope Amata, sogea hapa!” yule bibi alimsihi Amata huku akimuonesha ishara ya
kumuita kwa mkono, Amata kwa woga alimsogelea bibi yule na alipomkaribia kabisa
mwili wake ulisisimka sana na damu yake kwenda mbio, yule bibi akanyanyua mkono
wake na kumpiga Amata kofi utosini, Amata aliona giza nene kisha hakuelewa chochote
kinachoendelea.
[emoji814][emoji814][emoji814]
Saringo aliendelea kutaabika na kuhangaika hakujua ni wapi alipo ila tu aligundua
kuwa yuko ndani ya kitu kikubwa cha mviringo, giza kila upande, joto na hewa nzito
alikuwa akipambana navyo wakati huo, akijaribu kunyanyuka alishindwa kabisa maana
alijigonga kwa juu alijaribu kupiga kelele lakini ilikuwa kazi bure hakuna aliyemsikia huko nje kama alikuwepo. Mara kwa mbali alisikia sauti za watu wakiongea alitega sikio
kwa utulivu mkubwa ili angalau asikie wanachokiongea lakini haikuwa hivyo kwani
lugha waliyoitumia hakuweza kuielewa hata kidogo ‘Gorino’ alijiwazia na mara hofu kuu
ilimjaa kijasho chembamba kikaanza kumwagika kwani alijua habari za viumbe hawa
ambao wanaishi katikati ya msitu huu wa Solondo na hupendelea kula moyo, utumbo,
maini na mapafu ya binadamu. Saringo aliona kuwa sasa aliyokuwa akisikia juu ya Msitu
wa Solondo yametimia, alijilaumu sana kwa nini na kwa vipi alijikuta akijihusisha na
safari hii ngumu na mbaya, alifumba macho yake na kukumbuka maneno ya babu yake
aliyokuwa akimsimulia alipokuwa mtoto juu ya safari ya Solondo, alijilaumu sana nafsi
yake na roho yake yenye uroho wa utajiri ‘nani aliniambia huku kuna
utajiri?alinidanganya! hapana, ni babu alinihakikishia kuwa wamezika mali nyingi
huku,ah no! Alinidanganya?’ Saringo alijiuliza na kujijibu, alijilaumu na kujipa moyo,
mawazo yake yakamrudisha nyuma sana na kumkumbuka babu yake Mzee Mapendo
siku walipokaa wakiota moto naye akamsimulia mengi ya wakati wa ukoloni na utawala
wao ambapo hapo ndipo alimsimulia juu hazina iliyofichwa na wajerumani huko
Solondo...
4
Miaka 20 nyuma Miaka 20 nyuma
Kijijini kwa akina Saring Kijijini kwa akina Saringo Kijijini kwa akina Saringo o
Mzee Koloto aliketi karibu kabisa na moto kwa kuwa yeye aliona baridi wakati
wenzake walikuwa wakiona joto kali, pembeni alikuwa na kiko yake na kikombe cha
maziwa, wajukuu walikuwa wamemzunguka kama unavyojua babu akaapo. Mzee huyu
aliyekula chumvi nyingi alikuwa na maneno mengi ingawaje sasa hakuwa na jino hata
moja kinywani mwake, alikuwa ahishiwi simulizi kwa wajukuu zake. Alipenda kujivuna
kuwa yeye ni askari imara wa mkoloni aliyeogopwa na kila mtu.
“Babu!” saringo aliita kwa sauti kijukuu, wakati huo akiwa na miaka nane darasa la
kwanza.
“Enhe niambie babu yangu!!!!!” Mzee Koloto alimuitikia kwa bashasha
“Babu vidole vyako vya miguu mbona sio vitano? Viko vitatu tu!” saringo alirusha swali
la uchokozi kwa babuye
“A aaa sasa mchumba umeanza udadisi wako! Nikwambie mara ngapi? Hivi vidole
vilikatika hukoooo porini huko tukiwa kazini zamani za mkoloni” alijibu kwa kirefu.
“Mmmm babu, kazini ndio ukatike vidole!”
“Eeeee mama, tulikuwa tunapambana na maadui, mimi nimekwenda vita ya kwanza ya
dunia na ya pili ya dunia, mimi askari mtiifu” aliongeza jibu na kuedelea “tulikuwa
tunatembea mwendo mrefu kutoka kule kilima cha Saroge kwa mguu wakati huo hakuna
mutuka hizi, tumetembea safari ndefu sana tunapanda milima na kushuka mabonde
mpaka kuleeee mlima wa Vegani, unaujua mlima Vegani wewe?” alimtupia swali
Saringo
“Mlima Vegani? Mi siujui babu” saringo alijibu
“Aaaaaah kweli huwezi kuujua wewe bado mdogo! Sasa kaa chini hapa nikusimulie!”
Mzee Koloto alimwambia Saringo. Saringo akakaa chini akimtazama babu yake kwa makini huku akifuta makamasi mara kwa mara kwa mikono yake na kufanya sehemu ya
kati ya mdomo na pua yake kung’aa kwa makamasi yaliyokauka.
Mzee Koloto akaanza simulizi yake “Tulipokuwa vijana sisi tulikuwa askari wa mkoloni,
tulikuwa tunakaa hukoooo Saroge ndiyo ilikuwa kambi ya Mjerumani miaka hiyoooo,
sisi tukiwa askari wakakamavu kabisa, tumefuga masharubu yetu tukisimama pale
kwenye gwaride aaaaaa mjukuu yaani upepo ukipuliza utasikia kama mtu anapiga
mbinja, hiyo ilikuwa ni moja ya sare yetu. Siku moja tukiwa kambini pale king’ola kililia
tukatoka ndani wote tukapanga mstari, tukatangaziwa kuwa kuna mgeni amekuja kutoka
Ujeremani huyu Bwana alikuwa anaitwa aaa nimemsahau kidogo oooh Karl Peter, huyu
Bwana alikuwa mrefu na mwenye tambo la kikakamavu haswa alikagua kikosi chetu na
aliporidhika tulichaguliwa askari hodari kama kumi hivi na mimi babu yako nilikuwepo.
Dhumuni ilikuwa ni kusafiri kwenda huko mlima Vegani alisema kuna mizigo ya
kuchukua kupeleka sehemu nyingine. Tulianza safari asubuhi sana kupitia katikati ya pori
kubwa, njiani wote tulikuwa kimya sana kila mtu akitafakari juu ya safari ile. Tulifika
Vegani baada ya siku mbili, pale mlimani tulikuta watu wengi sana nilishangaa kuona
mashimo makubwa makubwa na watu wakiingia na kutoka wamebeba maudongo mengi,
sikuelewa ni nini kinaendelea. Pale tukapokelewa na wajeremani wengine wakatupeleka
sehemu kupumzika kidogo, tukala halafu ndio tukaambiwa tunatakiwa kusindikiza
msafara wa mizigo kwenda Solondo. Asubuhi yake tukaenda katika lichumba limoja
kulikuwa na masanduku ya chuma mengi tu ndani yamejaa mavitu mazurimazuri, sisi
hata hatukujua ni vitu gani basi tulikuwa na wapagazi wakabeba pale yale masanduku
tukaanza safari ya kwenda huko Solondo” Mzee Koloto akakohoa kidogo, kisha
akaendelea “safari ile ilikuwa ndefu na ya hatari sana mjukuu wangu, tulipanda milima
mikali na kuvuka mito mikubwa yenye mamba wakubwa, tulikutana na nyoka wakubwa
wengine wana vichwa viwili tulipambana nao hivo hivo ndio kisa cha vidole vingine
kupotea uko huko.”
“Sa mlikuwa mnaenda api?” saringo aliuliza
“Aah mjukuu wangu, mbali huko kwenye msitu kulikuwa na jiwe kubwa sana chini lina
pango kubwa na shimo la ajabu humo ndio tukatengeneza eneo zuri tukachonga ngazi za
kupandia na kushuka, tukatengeneza vyumba vingi sana tukahifadhi hayo mamizigo yao,
kule wakaweka mamilango makubwa ya chuma na makufuli makubwa funguo wakabeba,
mimi mjukuu nikaona hii itakuwa ni mali sana kwa nini wafunge hivi!!!? Tukaongozwa
kutoka nje ya hilo pango... mjukuu wangu we hapo walianza kutugawanya makundi
makundi kurudi lakini walipanga kutuua sote ili tusije kurudi kule pangoni, muda fulani
niliona wanachukua karatasi fulani na kulisoma wakiongea kikwao na kuweka alama
fulanifulani kwenye ile karatasi na miti iliyo eneo hilo na mawe walituelekeza kuchonga
alama fulani fulani, kisha tukapanda mlima mmoja mkubwa na kusimika chuma kikubwa
kimoja kimesimama na kingine kimekatisha katikati yake, ule ndiyo uchawi wao mjukuu,
wakatuambia atakayekuja huku atakufa hatorudi tena duniani, tuliogopa sana lakini mimi
nikajua huu ni ujanja tu. Mjukuu! wale watu ni makatili bwana!! sisi tulikuwa wanne na
wao wawili, tukafika mtoni wakamwambia mmoja wetu avuke kwanza kumbe wanajua
kuna mamba alipoingia tu mtoni wale mamba wakamkamata wakamla, halafu wenyewe
wanacheka huku wanavuta kiko zao mdomoni, mimi! Mjukuu! nilikasirika sana sikujua
nifanye nini, wakatuambia tupite njia nyingine, tukaendelea na safari ile huku kila mmoja
wetu akiwa na mawazo mengi”
Mzee Koloto akaendelea kuchochea kuni zake katika ule moto huku akiendelea
 
MSITU WA SOLONDO

Mtunzi Richard Mwambe


Sehemu 6


Amata! Tukimaliza safari yetu tutakuwa matajiri sana, tunakwenda Solondo kuchukua
sanduku kubwa na ndani ya sanduku hilo kuna mali nyingi sana, dhahabu, almasi, yaspi,
lulu za aina mbalimbali, mawe ya thamani tofauti”. Saringo alimwambia Amata, Amata
alimkazia macho saringo
“Nani aliyekwambia Saringo?! Solondo ni msitu wa kifo, msitu unaokuwa hai na kumeza
kila aingiyae...”Amata alieleza lakini saringo alimkatisha “Hapana amata, hizo ni hadithi
za kale, si za kuamini, wazee wetu walitusimulia ili tuogope kabisa kuingia ndani ya
msitu huu lakini ukweli ni kuwa ndani ya msitu huu wajerumani wamehifadhi vitu vingi
sana na babu wa baba yangu alikuwa askari wao amekuja sana huku kuleta vitu
walivyokuwa wakivichimba huku na huko katika nchi yetu! Watu wengi waliuawa na
wajerumani ndio na hawakurudi tena vijijini mwao ndio maana hizo hadithi zenu
zikawepo” saringo aliongea kwa jazba
“...hadithi zenu !!! hadithi zenu!!!” Amata alijiwazia moyoni akijaribu kulinganisha
asemayo Saringo. Amata akashusha pumzi akibaki na maswali mengi kichwani akatoa
pera akaanza kutafuna huku akichezesha kichwa chake kama mtu anayefuatisha muziki
fulani. Wakiwa katika hali ya ukimya sana kila mtu alizama katika mawazo yake ambayo
hakuna mwingine aliyeyajua
“Dunia imekuharibu umesahau mila na desturi za nyumbani” aliropoka Amata
kumwambia Saringo, Saringo alihamaki kwa kauli ya Amata na kumtazama usoni sasa
sio kwa sura ile legevu bali yenye jazba na uchungu
“Unasemaje Amata?!.. wewe unaendekeza ujinga na upumbavu wa kijijini! Hujui hata
dunia upande wa pili inaendeleaje, lazima maisha yabadilike, mimi naishi mjini naelewa
lakini wewe umezaliwa na kukulia huku porini utajua nini, fuata nnayokwambia” saringo
alifoka.
“ Huwezi kuniamrisha kufuata unayonambia wewe ni mwanamke tu, kama mimi
nimekulia huku mshamba wa kizamani kwa nini mlinitafuata katika safari yenu hii isiyo
na miguu wala kichwa, na usomi wenu na maendeleo mliyonayo mngefika wapi?
Stephan yuko wapi , helen yuko wapi? Mbona wamepotea bila kujua, na we bado zamu
yako. Lazima udumishe mila na desturi, asili itabaki kuwa asili tu!” Amata alifoka pia.
“Asili itabaki kuwa asili tu” Maneno haya yalimchoma sana Saringo na yalimrudia mara
kwa mara. Saringo akanyanyuka na kusoge pembeni, akaketi na kuikunja miguu yake
kuelekea kidevuni huku akiwa kaizungushia mikono yake aliinama na kulia kwa
vikwifukwifu.
Giza liliufunika msitu taratibu, sauti za ndege na mbweha zilisikika huku na huko, macho
ya Amata yalikuwa yanapambana na usingizi uliokuwa unayasumbua huku wadudu nao
wakifurahia kuona kiumbe hiko katika makazi yao, hakuona njia nyingine zaidi ya
kutafuna matunda yake aliyoyahifadhi vyema katika mkoba suruali yake ile ya
kimagereza, huku akitumia nguvu nyingi kujaribu kuangazaangaza kuona kama kuna
hatari yoyote inayowakabili, alimwangalia Saringo na kugundua kuwa tayari alikuwa
amelala ‘wanawake bwana!’ alijisemea moyoni huku akitikisa kichwa chake kuonesha
kukata tamaa.
“We mbona unalala kibwege hivyo? Unafikiri uko kwenu hapa!” alimuamsha Saringo
kwa kumtikisa na kumwambia maneno hayo, saringo alinyanyua kichwa na kumtazama
Amata kwa sura yenye mikunjo ya usingizi na uchovu. Amata alitabasamu na
kukumbuka maneno aliyoambiwa na baba yake ‘ukitaka kuchagua mchumba mtazame
anapoamka’ hapo alihakikisha baada ya kuona sura ya Saringo alipotoka katika kipande hicho cha usingizi, akarudi alipokaa na kusimama kwa muda kisha alimfuata Saringo,
kibaridi kilichukua nafasi yake msituni hapo na wakiwa wamejikunyata kila mmoja
kamshika mwenzie ili kupata kajoto wakapitiwa na usingizi uliowachukua kwenda
ulimwengu wa mbali.
[emoji814][emoji814][emoji814]
Saringo alibebwa juujuu na watu wa ajabu wenye mguu mmoja huku wakiimba
nyimbo zisizoeleweka, wakizunguka naye katika mduara mkubwa ambao katikati yake
kulikuwa na moto mkubwa sana, ngoma zilirindima, wengine walioketi pembeni
walionekana kunywa kitu kama pombe kwenye kata kubwakubwa huku wakifurahia na
kucheka kwa sauti za ajabu, Amata aliketi palepale akiangali huku akitetemeka kwa
woga wa ajabu, kijasho kilimtoka kila alipotaka kupiga kelele za kuomba msaada
alijikuta sauti haimtoki na wa le viumbe walimcheka sana, akijaribu kujitikisa
hakutikisika kabisa kumbe alikuwa amefungwa katika mti mkubwa uliopo katika uwanja
ule ambao ngoma hiyo ya ajabu ilipigwa na kuchezwa na hawa viumbe wa ajabu. Bado
wale wengine waliendelea kucheza huku wamembeba Saringo juu kwa juu wakipokezana
kwa furaha, mara wakamshusha na kumlaza katika jiwe kubwa lilichongwa kama
ngalawa lakini halikuwa na shimo katikati, akiwa kama alivyozaliwa juu ya lile jiwe
hakuweza hata kutikisika, Amata aliangalia kwa makini akitaka kujua wanataka
kumfanya nini lakini kila alipojitikisa hakutikisika na kila alipofanya hivyo alisikia sauti
za ajabu zikimcheka sana aliogopa na kutulia tuli kama maji ya mtungini.
Ilikuwa ni sherehe ya ajabu ambayo Amata hakupata kuiona tangu azaliwe katika dunia
hii, akiwa katika hali ya kutaharuki hakupenda kuona kinachoendelea, alifumba macho
yake kwa nguvu zote lakini bado akili na moyo wake vilitaka kuangalia kinachoendelea,
aliyafumbua macho yake na alichokiona kilimchanganya kwa kuwa hakuelewa ni nini na
kwa nini,wanawake saba waliokuwa watupu kabisa wakiwa wanatokea ndani ya kitu
kama pango ambalo liko chini ya mti mkubwa kichwani walijitwika vitu kama vyungu
wakiwa wanatembea kwa mwendo wa kurukaruka kwa kuwa walikuwa na mguu mmoja
kila mmoja, waliimba nyimbo zisizoeleweka na wa le wanaume waliombeba Saringo juu
juu na kumlaza pale katika jiwe waliendelea kucheza ngoma ile isiyoeleweka, Amata
alikuwa na woga mkuu akitetemeka mwili wote. Wanawake wale walilizunguka lile jiwe
na kutua vyungu vilivyokuwa kichwani mwao, mmoja wao aliyeonekana kama ndiye
kiongozi wao alitwaa chungu kimoja na kukinyanyua juu kama anayefanya sala fulani,
kisha akakishusha akakiweka pembeni ya miguu ya Saringo akaingiza mikono yake na
kuchota kitu kama mafuta ya kupikia na kuanza kumpaka Saringo akianzia miguuni
kisha na wenzake nao wakafanya hivyo, sasa walimpaka mwili mzima huku wakiongea
lugha ya ajabu ambayo Amata alijaribu kuisikiliza lakini hakuilewa ‘hawa viumbe
gani?!’ Amata alijiuliza bila majibu, aliendelea kutazama kwa woga. Wanawake wale
walipomaliza kazi hiyo walinyanyuka na kurudi kule walikotoka na kumuacha Saringo
akiwa kalala pale aking’aa kwa mafuta yale pindi akiangazwa na mwanga wa moto ule
akiwa kimya kabisa, Amata hakujua kama saringo alikuwa mzima au la maana
misukosuko yote yeye alikuwa kalala kama mfu hakujitikisa wala hakufanya lolote.
Mara wale wanaume wakaanza tena ngoma yao sasa kwa uchangamfu zaidi huku
wakipiga makelele ya ajabu na kurukaruka, ndipo Amata akagundua kuwa ule mguu
mmoja walionao kila mmoja wao huku chini ulikuwa na kanyagio kama la kuku, mara upepo mkali ukaanza kuvuma na wao wakiwa bado wanacheza ngoma yao sasa
wakionesha munkari na jazba zaidi, mara kutoka katika mti ule ambao waliingia wale
wanawake joka kubwa liliibuka kwa kasi ya ajabu,
“Ssss......” Amata alijaribu kumuita Saringo lakini sauti haikuweza kutoka hata kidogo,
joka lile lilijikunjua kwa kuzunguka likiwa hewani sasa likiwa linaelekea pale alipolazwa
Saringo, na liliposikia sauti hafifu ya Amata likageuka huku aliko na kutema mate kwa
kasi kumtemea Amata, mara Amata akazinduka kutoka usingizini, alikuwa akihema
kama mtu aliyekuwa akikimbizwa...
“Saringo, Saringo!” Aliita huku akiweweseka. Alipotulia alijikuta kaloa mwili mzima na
pembeni yake kuna kitu kama kata kubwa liliotelekezwa na ndani yake kulikuwa na maji
kidogo, ndipo alipogundua kuwa kamwagiwa maji na ndiyo yaliyomfanya akurupuke
kutoka katika usingizi wake, lakini nani alimwagia maji hakumjua wala hakumuona,
wala Saringo hakumuona eneo lile, alipoangalia vizuri aligundua kuwa hakuwa pale
ambapo alipitiwa na usingizi, hapa ni mahali pengine kabisa ambapo hakupajua kabisa,
aliangaza macho huku na kule lakini hakuona dalili ya mtu wala mnyama, palikuwa
patupu miti ikiwa imezunguka kwa mbali na katikati palikuwa wazi ni nyasi fupifupi tu
zilijaa katika eneo lile. Alijinyanyua kutoka pale alipokaa na kusimama wima, alivuta
ukimya kidogo kuona kama kuna kitachotokea awe mtu au mnyama lakini hali libaki
kuwa ileile ‘hapa ni wapi?’ Amata alijiuliza lakini hali ilikuwa ni ile ile, mara nyuma
yake akasikia sauti ikimwita kwa kunong’ona ikirudiarudia jina lake, amata alitulia na
kimya huku akiwa hajui cha kufanya, moyo ulimdunda kwa kasi akageuka taratibu kuona
ni nani aliyemuita, Amata alitahamaki, hakuamini macho yake alichokiona...
Bibi kizee aliyechoka, ngozi yake imekauka kwa kukosa vitamini, macho mekundu ya
kutisha, nywele zote nyeupe na unaweza kuzihesabu, miguu yenye vidole visivyo na
kucha, Amata alimwangalia kwa umakini ajuza yule lakini moyoni akijawa na hofu,
‘hakika ajuza huyu angekuwa kwenye mikoa ya upande fulani wa nchi mojawapo ya
Afrika Masahariki hakika asingekuwepo hii leo hasa kwa macho yake’ mawazo haya
yalipita haraka kichwani mwa Amata. Ajuza yule hakuwa hata anatikisika alisimama
vilevile huku akisaidiwa kwa mkongojo ule alioushika, alimkazia macho Amata, kwa
wakati huo Amata hakujua la kufanya, akimbie? Hapana, Amsalimie? Hakuna jibu, sasa
afanyeje hakika ulikuwa mtihani mkubwa sana kwake, “Amata...” bibi yule aliita tena
kwa sauti ya kukwaruza na mbaya huku akimwangalia Amata, Amata alimwangalia kwa
umakini na kuanza kurudi nyuma taratibu
“Usiogope Amata, sogea hapa!” yule bibi alimsihi Amata huku akimuonesha ishara ya
kumuita kwa mkono, Amata kwa woga alimsogelea bibi yule na alipomkaribia kabisa
mwili wake ulisisimka sana na damu yake kwenda mbio, yule bibi akanyanyua mkono
wake na kumpiga Amata kofi utosini, Amata aliona giza nene kisha hakuelewa chochote
kinachoendelea.
[emoji814][emoji814][emoji814]
Saringo aliendelea kutaabika na kuhangaika hakujua ni wapi alipo ila tu aligundua
kuwa yuko ndani ya kitu kikubwa cha mviringo, giza kila upande, joto na hewa nzito
alikuwa akipambana navyo wakati huo, akijaribu kunyanyuka alishindwa kabisa maana
alijigonga kwa juu alijaribu kupiga kelele lakini ilikuwa kazi bure hakuna aliyemsikia huko nje kama alikuwepo. Mara kwa mbali alisikia sauti za watu wakiongea alitega sikio
kwa utulivu mkubwa ili angalau asikie wanachokiongea lakini haikuwa hivyo kwani
lugha waliyoitumia hakuweza kuielewa hata kidogo ‘Gorino’ alijiwazia na mara hofu kuu
ilimjaa kijasho chembamba kikaanza kumwagika kwani alijua habari za viumbe hawa
ambao wanaishi katikati ya msitu huu wa Solondo na hupendelea kula moyo, utumbo,
maini na mapafu ya binadamu. Saringo aliona kuwa sasa aliyokuwa akisikia juu ya Msitu
wa Solondo yametimia, alijilaumu sana kwa nini na kwa vipi alijikuta akijihusisha na
safari hii ngumu na mbaya, alifumba macho yake na kukumbuka maneno ya babu yake
aliyokuwa akimsimulia alipokuwa mtoto juu ya safari ya Solondo, alijilaumu sana nafsi
yake na roho yake yenye uroho wa utajiri ‘nani aliniambia huku kuna
utajiri?alinidanganya! hapana, ni babu alinihakikishia kuwa wamezika mali nyingi
huku,ah no! Alinidanganya?’ Saringo alijiuliza na kujijibu, alijilaumu na kujipa moyo,
mawazo yake yakamrudisha nyuma sana na kumkumbuka babu yake Mzee Mapendo
siku walipokaa wakiota moto naye akamsimulia mengi ya wakati wa ukoloni na utawala
wao ambapo hapo ndipo alimsimulia juu hazina iliyofichwa na wajerumani huko
Solondo...
4
Miaka 20 nyuma Miaka 20 nyuma
Kijijini kwa akina Saring Kijijini kwa akina Saringo Kijijini kwa akina Saringo o
Mzee Koloto aliketi karibu kabisa na moto kwa kuwa yeye aliona baridi wakati
wenzake walikuwa wakiona joto kali, pembeni alikuwa na kiko yake na kikombe cha
maziwa, wajukuu walikuwa wamemzunguka kama unavyojua babu akaapo. Mzee huyu
aliyekula chumvi nyingi alikuwa na maneno mengi ingawaje sasa hakuwa na jino hata
moja kinywani mwake, alikuwa ahishiwi simulizi kwa wajukuu zake. Alipenda kujivuna
kuwa yeye ni askari imara wa mkoloni aliyeogopwa na kila mtu.
“Babu!” saringo aliita kwa sauti kijukuu, wakati huo akiwa na miaka nane darasa la
kwanza.
“Enhe niambie babu yangu!!!!!” Mzee Koloto alimuitikia kwa bashasha
“Babu vidole vyako vya miguu mbona sio vitano? Viko vitatu tu!” saringo alirusha swali
la uchokozi kwa babuye
“A aaa sasa mchumba umeanza udadisi wako! Nikwambie mara ngapi? Hivi vidole
vilikatika hukoooo porini huko tukiwa kazini zamani za mkoloni” alijibu kwa kirefu.
“Mmmm babu, kazini ndio ukatike vidole!”
“Eeeee mama, tulikuwa tunapambana na maadui, mimi nimekwenda vita ya kwanza ya
dunia na ya pili ya dunia, mimi askari mtiifu” aliongeza jibu na kuedelea “tulikuwa
tunatembea mwendo mrefu kutoka kule kilima cha Saroge kwa mguu wakati huo hakuna
mutuka hizi, tumetembea safari ndefu sana tunapanda milima na kushuka mabonde
mpaka kuleeee mlima wa Vegani, unaujua mlima Vegani wewe?” alimtupia swali
Saringo
“Mlima Vegani? Mi siujui babu” saringo alijibu
“Aaaaaah kweli huwezi kuujua wewe bado mdogo! Sasa kaa chini hapa nikusimulie!”
Mzee Koloto alimwambia Saringo. Saringo akakaa chini akimtazama babu yake kwa makini huku akifuta makamasi mara kwa mara kwa mikono yake na kufanya sehemu ya
kati ya mdomo na pua yake kung’aa kwa makamasi yaliyokauka.
Mzee Koloto akaanza simulizi yake “Tulipokuwa vijana sisi tulikuwa askari wa mkoloni,
tulikuwa tunakaa hukoooo Saroge ndiyo ilikuwa kambi ya Mjerumani miaka hiyoooo,
sisi tukiwa askari wakakamavu kabisa, tumefuga masharubu yetu tukisimama pale
kwenye gwaride aaaaaa mjukuu yaani upepo ukipuliza utasikia kama mtu anapiga
mbinja, hiyo ilikuwa ni moja ya sare yetu. Siku moja tukiwa kambini pale king’ola kililia
tukatoka ndani wote tukapanga mstari, tukatangaziwa kuwa kuna mgeni amekuja kutoka
Ujeremani huyu Bwana alikuwa anaitwa aaa nimemsahau kidogo oooh Karl Peter, huyu
Bwana alikuwa mrefu na mwenye tambo la kikakamavu haswa alikagua kikosi chetu na
aliporidhika tulichaguliwa askari hodari kama kumi hivi na mimi babu yako nilikuwepo.
Dhumuni ilikuwa ni kusafiri kwenda huko mlima Vegani alisema kuna mizigo ya
kuchukua kupeleka sehemu nyingine. Tulianza safari asubuhi sana kupitia katikati ya pori
kubwa, njiani wote tulikuwa kimya sana kila mtu akitafakari juu ya safari ile. Tulifika
Vegani baada ya siku mbili, pale mlimani tulikuta watu wengi sana nilishangaa kuona
mashimo makubwa makubwa na watu wakiingia na kutoka wamebeba maudongo mengi,
sikuelewa ni nini kinaendelea. Pale tukapokelewa na wajeremani wengine wakatupeleka
sehemu kupumzika kidogo, tukala halafu ndio tukaambiwa tunatakiwa kusindikiza
msafara wa mizigo kwenda Solondo. Asubuhi yake tukaenda katika lichumba limoja
kulikuwa na masanduku ya chuma mengi tu ndani yamejaa mavitu mazurimazuri, sisi
hata hatukujua ni vitu gani basi tulikuwa na wapagazi wakabeba pale yale masanduku
tukaanza safari ya kwenda huko Solondo” Mzee Koloto akakohoa kidogo, kisha
akaendelea “safari ile ilikuwa ndefu na ya hatari sana mjukuu wangu, tulipanda milima
mikali na kuvuka mito mikubwa yenye mamba wakubwa, tulikutana na nyoka wakubwa
wengine wana vichwa viwili tulipambana nao hivo hivo ndio kisa cha vidole vingine
kupotea uko huko.”
“Sa mlikuwa mnaenda api?” saringo aliuliza
“Aah mjukuu wangu, mbali huko kwenye msitu kulikuwa na jiwe kubwa sana chini lina
pango kubwa na shimo la ajabu humo ndio tukatengeneza eneo zuri tukachonga ngazi za
kupandia na kushuka, tukatengeneza vyumba vingi sana tukahifadhi hayo mamizigo yao,
kule wakaweka mamilango makubwa ya chuma na makufuli makubwa funguo wakabeba,
mimi mjukuu nikaona hii itakuwa ni mali sana kwa nini wafunge hivi!!!? Tukaongozwa
kutoka nje ya hilo pango... mjukuu wangu we hapo walianza kutugawanya makundi
makundi kurudi lakini walipanga kutuua sote ili tusije kurudi kule pangoni, muda fulani
niliona wanachukua karatasi fulani na kulisoma wakiongea kikwao na kuweka alama
fulanifulani kwenye ile karatasi na miti iliyo eneo hilo na mawe walituelekeza kuchonga
alama fulani fulani, kisha tukapanda mlima mmoja mkubwa na kusimika chuma kikubwa
kimoja kimesimama na kingine kimekatisha katikati yake, ule ndiyo uchawi wao mjukuu,
wakatuambia atakayekuja huku atakufa hatorudi tena duniani, tuliogopa sana lakini mimi
nikajua huu ni ujanja tu. Mjukuu! wale watu ni makatili bwana!! sisi tulikuwa wanne na
wao wawili, tukafika mtoni wakamwambia mmoja wetu avuke kwanza kumbe wanajua
kuna mamba alipoingia tu mtoni wale mamba wakamkamata wakamla, halafu wenyewe
wanacheka huku wanavuta kiko zao mdomoni, mimi! Mjukuu! nilikasirika sana sikujua
nifanye nini, wakatuambia tupite njia nyingine, tukaendelea na safari ile huku kila mmoja
wetu akiwa na mawazo mengi”
Mzee Koloto akaendelea kuchochea kuni zake katika ule moto huku akiendelea
Asanteh mkuu
Usisahau kututupia cha kulalia sasa
 
MSITU WA SOLONDO

Mtunzi Richard Mwambe


Sehemu 6


Amata! Tukimaliza safari yetu tutakuwa matajiri sana, tunakwenda Solondo kuchukua
sanduku kubwa na ndani ya sanduku hilo kuna mali nyingi sana, dhahabu, almasi, yaspi,
lulu za aina mbalimbali, mawe ya thamani tofauti”. Saringo alimwambia Amata, Amata
alimkazia macho saringo
“Nani aliyekwambia Saringo?! Solondo ni msitu wa kifo, msitu unaokuwa hai na kumeza
kila aingiyae...”Amata alieleza lakini saringo alimkatisha “Hapana amata, hizo ni hadithi
za kale, si za kuamini, wazee wetu walitusimulia ili tuogope kabisa kuingia ndani ya
msitu huu lakini ukweli ni kuwa ndani ya msitu huu wajerumani wamehifadhi vitu vingi
sana na babu wa baba yangu alikuwa askari wao amekuja sana huku kuleta vitu
walivyokuwa wakivichimba huku na huko katika nchi yetu! Watu wengi waliuawa na
wajerumani ndio na hawakurudi tena vijijini mwao ndio maana hizo hadithi zenu
zikawepo” saringo aliongea kwa jazba
“...hadithi zenu !!! hadithi zenu!!!” Amata alijiwazia moyoni akijaribu kulinganisha
asemayo Saringo. Amata akashusha pumzi akibaki na maswali mengi kichwani akatoa
pera akaanza kutafuna huku akichezesha kichwa chake kama mtu anayefuatisha muziki
fulani. Wakiwa katika hali ya ukimya sana kila mtu alizama katika mawazo yake ambayo
hakuna mwingine aliyeyajua
“Dunia imekuharibu umesahau mila na desturi za nyumbani” aliropoka Amata
kumwambia Saringo, Saringo alihamaki kwa kauli ya Amata na kumtazama usoni sasa
sio kwa sura ile legevu bali yenye jazba na uchungu
“Unasemaje Amata?!.. wewe unaendekeza ujinga na upumbavu wa kijijini! Hujui hata
dunia upande wa pili inaendeleaje, lazima maisha yabadilike, mimi naishi mjini naelewa
lakini wewe umezaliwa na kukulia huku porini utajua nini, fuata nnayokwambia” saringo
alifoka.
“ Huwezi kuniamrisha kufuata unayonambia wewe ni mwanamke tu, kama mimi
nimekulia huku mshamba wa kizamani kwa nini mlinitafuata katika safari yenu hii isiyo
na miguu wala kichwa, na usomi wenu na maendeleo mliyonayo mngefika wapi?
Stephan yuko wapi , helen yuko wapi? Mbona wamepotea bila kujua, na we bado zamu
yako. Lazima udumishe mila na desturi, asili itabaki kuwa asili tu!” Amata alifoka pia.
“Asili itabaki kuwa asili tu” Maneno haya yalimchoma sana Saringo na yalimrudia mara
kwa mara. Saringo akanyanyuka na kusoge pembeni, akaketi na kuikunja miguu yake
kuelekea kidevuni huku akiwa kaizungushia mikono yake aliinama na kulia kwa
vikwifukwifu.
Giza liliufunika msitu taratibu, sauti za ndege na mbweha zilisikika huku na huko, macho
ya Amata yalikuwa yanapambana na usingizi uliokuwa unayasumbua huku wadudu nao
wakifurahia kuona kiumbe hiko katika makazi yao, hakuona njia nyingine zaidi ya
kutafuna matunda yake aliyoyahifadhi vyema katika mkoba suruali yake ile ya
kimagereza, huku akitumia nguvu nyingi kujaribu kuangazaangaza kuona kama kuna
hatari yoyote inayowakabili, alimwangalia Saringo na kugundua kuwa tayari alikuwa
amelala ‘wanawake bwana!’ alijisemea moyoni huku akitikisa kichwa chake kuonesha
kukata tamaa.
“We mbona unalala kibwege hivyo? Unafikiri uko kwenu hapa!” alimuamsha Saringo
kwa kumtikisa na kumwambia maneno hayo, saringo alinyanyua kichwa na kumtazama
Amata kwa sura yenye mikunjo ya usingizi na uchovu. Amata alitabasamu na
kukumbuka maneno aliyoambiwa na baba yake ‘ukitaka kuchagua mchumba mtazame
anapoamka’ hapo alihakikisha baada ya kuona sura ya Saringo alipotoka katika kipande hicho cha usingizi, akarudi alipokaa na kusimama kwa muda kisha alimfuata Saringo,
kibaridi kilichukua nafasi yake msituni hapo na wakiwa wamejikunyata kila mmoja
kamshika mwenzie ili kupata kajoto wakapitiwa na usingizi uliowachukua kwenda
ulimwengu wa mbali.
[emoji814][emoji814][emoji814]
Saringo alibebwa juujuu na watu wa ajabu wenye mguu mmoja huku wakiimba
nyimbo zisizoeleweka, wakizunguka naye katika mduara mkubwa ambao katikati yake
kulikuwa na moto mkubwa sana, ngoma zilirindima, wengine walioketi pembeni
walionekana kunywa kitu kama pombe kwenye kata kubwakubwa huku wakifurahia na
kucheka kwa sauti za ajabu, Amata aliketi palepale akiangali huku akitetemeka kwa
woga wa ajabu, kijasho kilimtoka kila alipotaka kupiga kelele za kuomba msaada
alijikuta sauti haimtoki na wa le viumbe walimcheka sana, akijaribu kujitikisa
hakutikisika kabisa kumbe alikuwa amefungwa katika mti mkubwa uliopo katika uwanja
ule ambao ngoma hiyo ya ajabu ilipigwa na kuchezwa na hawa viumbe wa ajabu. Bado
wale wengine waliendelea kucheza huku wamembeba Saringo juu kwa juu wakipokezana
kwa furaha, mara wakamshusha na kumlaza katika jiwe kubwa lilichongwa kama
ngalawa lakini halikuwa na shimo katikati, akiwa kama alivyozaliwa juu ya lile jiwe
hakuweza hata kutikisika, Amata aliangalia kwa makini akitaka kujua wanataka
kumfanya nini lakini kila alipojitikisa hakutikisika na kila alipofanya hivyo alisikia sauti
za ajabu zikimcheka sana aliogopa na kutulia tuli kama maji ya mtungini.
Ilikuwa ni sherehe ya ajabu ambayo Amata hakupata kuiona tangu azaliwe katika dunia
hii, akiwa katika hali ya kutaharuki hakupenda kuona kinachoendelea, alifumba macho
yake kwa nguvu zote lakini bado akili na moyo wake vilitaka kuangalia kinachoendelea,
aliyafumbua macho yake na alichokiona kilimchanganya kwa kuwa hakuelewa ni nini na
kwa nini,wanawake saba waliokuwa watupu kabisa wakiwa wanatokea ndani ya kitu
kama pango ambalo liko chini ya mti mkubwa kichwani walijitwika vitu kama vyungu
wakiwa wanatembea kwa mwendo wa kurukaruka kwa kuwa walikuwa na mguu mmoja
kila mmoja, waliimba nyimbo zisizoeleweka na wa le wanaume waliombeba Saringo juu
juu na kumlaza pale katika jiwe waliendelea kucheza ngoma ile isiyoeleweka, Amata
alikuwa na woga mkuu akitetemeka mwili wote. Wanawake wale walilizunguka lile jiwe
na kutua vyungu vilivyokuwa kichwani mwao, mmoja wao aliyeonekana kama ndiye
kiongozi wao alitwaa chungu kimoja na kukinyanyua juu kama anayefanya sala fulani,
kisha akakishusha akakiweka pembeni ya miguu ya Saringo akaingiza mikono yake na
kuchota kitu kama mafuta ya kupikia na kuanza kumpaka Saringo akianzia miguuni
kisha na wenzake nao wakafanya hivyo, sasa walimpaka mwili mzima huku wakiongea
lugha ya ajabu ambayo Amata alijaribu kuisikiliza lakini hakuilewa ‘hawa viumbe
gani?!’ Amata alijiuliza bila majibu, aliendelea kutazama kwa woga. Wanawake wale
walipomaliza kazi hiyo walinyanyuka na kurudi kule walikotoka na kumuacha Saringo
akiwa kalala pale aking’aa kwa mafuta yale pindi akiangazwa na mwanga wa moto ule
akiwa kimya kabisa, Amata hakujua kama saringo alikuwa mzima au la maana
misukosuko yote yeye alikuwa kalala kama mfu hakujitikisa wala hakufanya lolote.
Mara wale wanaume wakaanza tena ngoma yao sasa kwa uchangamfu zaidi huku
wakipiga makelele ya ajabu na kurukaruka, ndipo Amata akagundua kuwa ule mguu
mmoja walionao kila mmoja wao huku chini ulikuwa na kanyagio kama la kuku, mara upepo mkali ukaanza kuvuma na wao wakiwa bado wanacheza ngoma yao sasa
wakionesha munkari na jazba zaidi, mara kutoka katika mti ule ambao waliingia wale
wanawake joka kubwa liliibuka kwa kasi ya ajabu,
“Ssss......” Amata alijaribu kumuita Saringo lakini sauti haikuweza kutoka hata kidogo,
joka lile lilijikunjua kwa kuzunguka likiwa hewani sasa likiwa linaelekea pale alipolazwa
Saringo, na liliposikia sauti hafifu ya Amata likageuka huku aliko na kutema mate kwa
kasi kumtemea Amata, mara Amata akazinduka kutoka usingizini, alikuwa akihema
kama mtu aliyekuwa akikimbizwa...
“Saringo, Saringo!” Aliita huku akiweweseka. Alipotulia alijikuta kaloa mwili mzima na
pembeni yake kuna kitu kama kata kubwa liliotelekezwa na ndani yake kulikuwa na maji
kidogo, ndipo alipogundua kuwa kamwagiwa maji na ndiyo yaliyomfanya akurupuke
kutoka katika usingizi wake, lakini nani alimwagia maji hakumjua wala hakumuona,
wala Saringo hakumuona eneo lile, alipoangalia vizuri aligundua kuwa hakuwa pale
ambapo alipitiwa na usingizi, hapa ni mahali pengine kabisa ambapo hakupajua kabisa,
aliangaza macho huku na kule lakini hakuona dalili ya mtu wala mnyama, palikuwa
patupu miti ikiwa imezunguka kwa mbali na katikati palikuwa wazi ni nyasi fupifupi tu
zilijaa katika eneo lile. Alijinyanyua kutoka pale alipokaa na kusimama wima, alivuta
ukimya kidogo kuona kama kuna kitachotokea awe mtu au mnyama lakini hali libaki
kuwa ileile ‘hapa ni wapi?’ Amata alijiuliza lakini hali ilikuwa ni ile ile, mara nyuma
yake akasikia sauti ikimwita kwa kunong’ona ikirudiarudia jina lake, amata alitulia na
kimya huku akiwa hajui cha kufanya, moyo ulimdunda kwa kasi akageuka taratibu kuona
ni nani aliyemuita, Amata alitahamaki, hakuamini macho yake alichokiona...
Bibi kizee aliyechoka, ngozi yake imekauka kwa kukosa vitamini, macho mekundu ya
kutisha, nywele zote nyeupe na unaweza kuzihesabu, miguu yenye vidole visivyo na
kucha, Amata alimwangalia kwa umakini ajuza yule lakini moyoni akijawa na hofu,
‘hakika ajuza huyu angekuwa kwenye mikoa ya upande fulani wa nchi mojawapo ya
Afrika Masahariki hakika asingekuwepo hii leo hasa kwa macho yake’ mawazo haya
yalipita haraka kichwani mwa Amata. Ajuza yule hakuwa hata anatikisika alisimama
vilevile huku akisaidiwa kwa mkongojo ule alioushika, alimkazia macho Amata, kwa
wakati huo Amata hakujua la kufanya, akimbie? Hapana, Amsalimie? Hakuna jibu, sasa
afanyeje hakika ulikuwa mtihani mkubwa sana kwake, “Amata...” bibi yule aliita tena
kwa sauti ya kukwaruza na mbaya huku akimwangalia Amata, Amata alimwangalia kwa
umakini na kuanza kurudi nyuma taratibu
“Usiogope Amata, sogea hapa!” yule bibi alimsihi Amata huku akimuonesha ishara ya
kumuita kwa mkono, Amata kwa woga alimsogelea bibi yule na alipomkaribia kabisa
mwili wake ulisisimka sana na damu yake kwenda mbio, yule bibi akanyanyua mkono
wake na kumpiga Amata kofi utosini, Amata aliona giza nene kisha hakuelewa chochote
kinachoendelea.
[emoji814][emoji814][emoji814]
Saringo aliendelea kutaabika na kuhangaika hakujua ni wapi alipo ila tu aligundua
kuwa yuko ndani ya kitu kikubwa cha mviringo, giza kila upande, joto na hewa nzito
alikuwa akipambana navyo wakati huo, akijaribu kunyanyuka alishindwa kabisa maana
alijigonga kwa juu alijaribu kupiga kelele lakini ilikuwa kazi bure hakuna aliyemsikia huko nje kama alikuwepo. Mara kwa mbali alisikia sauti za watu wakiongea alitega sikio
kwa utulivu mkubwa ili angalau asikie wanachokiongea lakini haikuwa hivyo kwani
lugha waliyoitumia hakuweza kuielewa hata kidogo ‘Gorino’ alijiwazia na mara hofu kuu
ilimjaa kijasho chembamba kikaanza kumwagika kwani alijua habari za viumbe hawa
ambao wanaishi katikati ya msitu huu wa Solondo na hupendelea kula moyo, utumbo,
maini na mapafu ya binadamu. Saringo aliona kuwa sasa aliyokuwa akisikia juu ya Msitu
wa Solondo yametimia, alijilaumu sana kwa nini na kwa vipi alijikuta akijihusisha na
safari hii ngumu na mbaya, alifumba macho yake na kukumbuka maneno ya babu yake
aliyokuwa akimsimulia alipokuwa mtoto juu ya safari ya Solondo, alijilaumu sana nafsi
yake na roho yake yenye uroho wa utajiri ‘nani aliniambia huku kuna
utajiri?alinidanganya! hapana, ni babu alinihakikishia kuwa wamezika mali nyingi
huku,ah no! Alinidanganya?’ Saringo alijiuliza na kujijibu, alijilaumu na kujipa moyo,
mawazo yake yakamrudisha nyuma sana na kumkumbuka babu yake Mzee Mapendo
siku walipokaa wakiota moto naye akamsimulia mengi ya wakati wa ukoloni na utawala
wao ambapo hapo ndipo alimsimulia juu hazina iliyofichwa na wajerumani huko
Solondo...
4
Miaka 20 nyuma Miaka 20 nyuma
Kijijini kwa akina Saring Kijijini kwa akina Saringo Kijijini kwa akina Saringo o
Mzee Koloto aliketi karibu kabisa na moto kwa kuwa yeye aliona baridi wakati
wenzake walikuwa wakiona joto kali, pembeni alikuwa na kiko yake na kikombe cha
maziwa, wajukuu walikuwa wamemzunguka kama unavyojua babu akaapo. Mzee huyu
aliyekula chumvi nyingi alikuwa na maneno mengi ingawaje sasa hakuwa na jino hata
moja kinywani mwake, alikuwa ahishiwi simulizi kwa wajukuu zake. Alipenda kujivuna
kuwa yeye ni askari imara wa mkoloni aliyeogopwa na kila mtu.
“Babu!” saringo aliita kwa sauti kijukuu, wakati huo akiwa na miaka nane darasa la
kwanza.
“Enhe niambie babu yangu!!!!!” Mzee Koloto alimuitikia kwa bashasha
“Babu vidole vyako vya miguu mbona sio vitano? Viko vitatu tu!” saringo alirusha swali
la uchokozi kwa babuye
“A aaa sasa mchumba umeanza udadisi wako! Nikwambie mara ngapi? Hivi vidole
vilikatika hukoooo porini huko tukiwa kazini zamani za mkoloni” alijibu kwa kirefu.
“Mmmm babu, kazini ndio ukatike vidole!”
“Eeeee mama, tulikuwa tunapambana na maadui, mimi nimekwenda vita ya kwanza ya
dunia na ya pili ya dunia, mimi askari mtiifu” aliongeza jibu na kuedelea “tulikuwa
tunatembea mwendo mrefu kutoka kule kilima cha Saroge kwa mguu wakati huo hakuna
mutuka hizi, tumetembea safari ndefu sana tunapanda milima na kushuka mabonde
mpaka kuleeee mlima wa Vegani, unaujua mlima Vegani wewe?” alimtupia swali
Saringo
“Mlima Vegani? Mi siujui babu” saringo alijibu
“Aaaaaah kweli huwezi kuujua wewe bado mdogo! Sasa kaa chini hapa nikusimulie!”
Mzee Koloto alimwambia Saringo. Saringo akakaa chini akimtazama babu yake kwa makini huku akifuta makamasi mara kwa mara kwa mikono yake na kufanya sehemu ya
kati ya mdomo na pua yake kung’aa kwa makamasi yaliyokauka.
Mzee Koloto akaanza simulizi yake “Tulipokuwa vijana sisi tulikuwa askari wa mkoloni,
tulikuwa tunakaa hukoooo Saroge ndiyo ilikuwa kambi ya Mjerumani miaka hiyoooo,
sisi tukiwa askari wakakamavu kabisa, tumefuga masharubu yetu tukisimama pale
kwenye gwaride aaaaaa mjukuu yaani upepo ukipuliza utasikia kama mtu anapiga
mbinja, hiyo ilikuwa ni moja ya sare yetu. Siku moja tukiwa kambini pale king’ola kililia
tukatoka ndani wote tukapanga mstari, tukatangaziwa kuwa kuna mgeni amekuja kutoka
Ujeremani huyu Bwana alikuwa anaitwa aaa nimemsahau kidogo oooh Karl Peter, huyu
Bwana alikuwa mrefu na mwenye tambo la kikakamavu haswa alikagua kikosi chetu na
aliporidhika tulichaguliwa askari hodari kama kumi hivi na mimi babu yako nilikuwepo.
Dhumuni ilikuwa ni kusafiri kwenda huko mlima Vegani alisema kuna mizigo ya
kuchukua kupeleka sehemu nyingine. Tulianza safari asubuhi sana kupitia katikati ya pori
kubwa, njiani wote tulikuwa kimya sana kila mtu akitafakari juu ya safari ile. Tulifika
Vegani baada ya siku mbili, pale mlimani tulikuta watu wengi sana nilishangaa kuona
mashimo makubwa makubwa na watu wakiingia na kutoka wamebeba maudongo mengi,
sikuelewa ni nini kinaendelea. Pale tukapokelewa na wajeremani wengine wakatupeleka
sehemu kupumzika kidogo, tukala halafu ndio tukaambiwa tunatakiwa kusindikiza
msafara wa mizigo kwenda Solondo. Asubuhi yake tukaenda katika lichumba limoja
kulikuwa na masanduku ya chuma mengi tu ndani yamejaa mavitu mazurimazuri, sisi
hata hatukujua ni vitu gani basi tulikuwa na wapagazi wakabeba pale yale masanduku
tukaanza safari ya kwenda huko Solondo” Mzee Koloto akakohoa kidogo, kisha
akaendelea “safari ile ilikuwa ndefu na ya hatari sana mjukuu wangu, tulipanda milima
mikali na kuvuka mito mikubwa yenye mamba wakubwa, tulikutana na nyoka wakubwa
wengine wana vichwa viwili tulipambana nao hivo hivo ndio kisa cha vidole vingine
kupotea uko huko.”
“Sa mlikuwa mnaenda api?” saringo aliuliza
“Aah mjukuu wangu, mbali huko kwenye msitu kulikuwa na jiwe kubwa sana chini lina
pango kubwa na shimo la ajabu humo ndio tukatengeneza eneo zuri tukachonga ngazi za
kupandia na kushuka, tukatengeneza vyumba vingi sana tukahifadhi hayo mamizigo yao,
kule wakaweka mamilango makubwa ya chuma na makufuli makubwa funguo wakabeba,
mimi mjukuu nikaona hii itakuwa ni mali sana kwa nini wafunge hivi!!!? Tukaongozwa
kutoka nje ya hilo pango... mjukuu wangu we hapo walianza kutugawanya makundi
makundi kurudi lakini walipanga kutuua sote ili tusije kurudi kule pangoni, muda fulani
niliona wanachukua karatasi fulani na kulisoma wakiongea kikwao na kuweka alama
fulanifulani kwenye ile karatasi na miti iliyo eneo hilo na mawe walituelekeza kuchonga
alama fulani fulani, kisha tukapanda mlima mmoja mkubwa na kusimika chuma kikubwa
kimoja kimesimama na kingine kimekatisha katikati yake, ule ndiyo uchawi wao mjukuu,
wakatuambia atakayekuja huku atakufa hatorudi tena duniani, tuliogopa sana lakini mimi
nikajua huu ni ujanja tu. Mjukuu! wale watu ni makatili bwana!! sisi tulikuwa wanne na
wao wawili, tukafika mtoni wakamwambia mmoja wetu avuke kwanza kumbe wanajua
kuna mamba alipoingia tu mtoni wale mamba wakamkamata wakamla, halafu wenyewe
wanacheka huku wanavuta kiko zao mdomoni, mimi! Mjukuu! nilikasirika sana sikujua
nifanye nini, wakatuambia tupite njia nyingine, tukaendelea na safari ile huku kila mmoja
wetu akiwa na mawazo mengi”
Mzee Koloto akaendelea kuchochea kuni zake katika ule moto huku akiendelea
Asanteh mkuu
Usisahau kututupia cha kulalia sasa
 
MSITU WA SOLONDO

Mtunzi. Richard Mwambe

Sehemu 7

kumsimulia habari ile mjukuu wake, Saringo, kisha akaendelea... “Safari ile mjukuu
ilikuwa mbaya sana tulipita kwenye nyika kubwa, tukikutana na wanyama wakubwa
sana, sasa tulifika sehemu moja kulikuwa na kama kijiji hivi, hapo palikuwa na watu
wanaishi lakini watu hawa walikuwa wa ajabu sana, walipotuona walianza kufurahia na
kutuzunguka wakitaka kutukamata, walikuwa wanatisha kwa sura, nywele ndefu,
wamevaa ngozi, mbaya zaidi walikuwa wanakula watu. Mara tukajikuta katikati ya watu
hawa, yule askari mmoja wa kijerumani alianza kuwashambulia kwa risasi kwa kutumia
lile bunduki lake kubwa, walipoanza kuona wenzao wanaanguka ndipo walipopata hasira
na kutushambulia kwa nguvu, walimkamata mmoja wetu na kumkata kichwa kisha
niliona wengine wakinywa damu ile mbichi. Mimi nilifanikiwa kutoroka na mjerumani
mmoja tukawaacha wenzetu kule, kwa kweli sijui hata nini kiliwapata. Tulipofika porini
yule mjerumani akawa na hali mbaya maana alijeruhiwa sana hakuweza kutembea na
kuongea kwake kukawa kwa shida sana alikuwa akitokwa na damu nyingi mdomoni na
sehemu za kisogo chake, hakuchukua muda alikufa, nikabaki peke yangu msituni
niliogopa sana, nilipoangalia tulipotoka niliona tu moshi umetanda huko, mjukuu! Hivi
vidole vimekatika katika kujaribu kujiokoa na hao wagorino, hakuna nilichofanya
niliamua tu kujaribu bahati yangu, nikachukua yale makaratasi yule mjerumani alikuwa
nayo katika mkoba wake na lile libunduki lake, nikatembea msituni usiku na mchana,
mwisho nilifika kijijini baada ya siku kadhaa, ule mkoba mpaka leo ninao
nimeuning’iniza pale ukutani chumbani kwa bibi yako, ukiwa mkubwa uuchukue ule
utakuwa na mambo mengi sana sawa mjukuu ah! ah! ah!, mi ndiyo babu yako shujaa...”
alimaliza kwa kucheka huku akimpigapiga Saringo mgongoni.
Alipomaliza kusema hayo alikuta kumbe tayari mjukuu wake Saringo ameshapitiwa na
usingizi zamani sana na kwake hadithi hiyo ya kishujaa ilikuwa inajirudia kama ndoto
mbaya na ya kutisha.
[emoji814][emoji814][emoji814]
Amata alijikuta hana lakufanya baada ya kujikuta kafungwa kamba miguu yake na
kuning’inizwa kwenye kitu kama goli la mpira naye yupo kichwa chini miguu juu,
kichwa kilimuuma sana hata alikiona kizito, mara kwa mara alijikuta akiona giza na vitu
vyeupe vyeupe viking’aa sana vikimzunguka huku na huko. Alipogeuka kwa tabu huku
na huko hakuona mtu yeyote isipokuwa mandege makubwa tu yakizunguka na kutua
mahali fulani, Amata aliyatambua haraka haya mandege ambayo uyaonapo ujue kuwa
kuna mzoga eneo hilo, fahamu zilimrudi polepole Amata na kukikumbuka kile kizee
‘kigagula’ hakuna jirani wa kumuomba msaada, hakuna kiumbe cha kuelewa lugha yake,
aliona sasa hapa hana ujanja tena alipenda afe kabla hawa jamaa hawajamfikia akiogopa
kupambana na mateso makali bila yeye kujitetea. Inzi na wadudu warukao kwa jinsi zake
walikuwa wakimsumbua usoni kutokana na makamasi yaliyokuwa yanamvuja na
hakuweza kuyapangusa kwa kuwa mikono yake ilikuwa imefungwa kwa nyuma, alijaribu
kuitikisatikisa kuona labda kamba ile inaweza kuwa imelegea lakini haikuwa hivyo. Mara
ghafla aliona mti mkubwa uliopo hapo jirani ukitikisika matawi yake na alipoangalia
aligundua kuwa ni nyani mmoja mkubwa yuko hapo juu, alijaribu kutoa ishara kwa
kichwa labda nyani yule angeelewa kitu lakini haikuwa hivyo hata kidogo.
Kwa mbali sauti za viumbe hai zilisikika na kuongezeka zikiwa zinakaribia eneo lile,
mara akamuona yule nyani akikimbia tena juu zaidi ya mti na kupiga mruzi mmoja mkali, kumbe alikuwa na wenzake eneo lile wote wakapanda miti haraka na kukaa kimya
juu kana kwamba hakuna kiumbe hapo juu. Msafara mkubwa wa watu uliingia pale, watu
wakutisha wanaoonekena ni makatili kwelikweli wakiwa wamejichora marangi meupe
wamejichanja chale nyingi, kiunoni wamevaa tu kangozi ka kuwahifadhi maeneo yao.
Mbele yao wakiongozwa na mmoja wao mwenye tambo kubwa kwelikweli akiwa
amebeba lijiti lenye ncha kali linaloonekana kabisa kuwa limelowa damu, nyuma yake
walifuata watu kama kumi hivi wanne wakiwa wamebeba kitu kama nyama
kinachoning’inia kati ya miti miwili, wakafika pale kwenye kale kauwanja, wakasimama
na kushusha ule mzigo, yule kiongozi wao aliongea lugha fulani ya ajabu ambayo Amata
hakuielewa, mara wenzake waliitikia kwa kelele huku wakionyoosha juu majiti
waliyoyabeba ambayo yalkikuwa na ncha kali na yamelowa kwa damu. Wawili kati yao
walitoa ule mzigo, la haula !!! Amata hakuamini alichokiona mwili wa binadamu ambao
umetota kwa damu kiasi kwamba hauwezi kuuelewa ni umekumbwa na masaibu gani,
Amata alihisi mwili kusisimka na kuchoka kwa wakati mmoja, alitulia palepale
akiangalia nini kinaendelea, wakafunga kamba ule mwili kama alivyofungwa Amata na
kuja kuning’iniza kwa jinsi ile ile, Amata alijituliza na kufumba macho yake huku
akipumua kwa mbali ili wasijue kama ni mzima, walipomaliza kazi hiyo, yule kiongozi
wao akasogea kwa Amata na kumwangalia kwa makini sana akachukua kisu kikubwa na
kikali akakamkamata Amata upande wa kushoto wa bega lake kisha akacheka kwa sauti
ya ajabu na wenzake wakacheka kwa sauti hizo. Amata aliingiwa na hofu ‘mama moyo
wangu’ alihuzunika moyoni lakini alijua basi hakuna kitachosalimika. Yule jamaa
akainua bisu lake juu akashusha kwa kasi kuelekea kifua cha Amata, bila kutegemea
Amata alimuona lile jitu likiganda na kuanguka kama mzigo, wenzake wakashangaa na
kuangalia huku na huku na wasione mtu yeyote, walibaki kujiuliza imekuwaje kwa
mwenzao, kiongozi wao, walianza kupiga makelele wakikimbia huku na huku, Amata
akajua sasa amekwisha hata yeye hakuelewa kilichotokea alijigeuza kwa tabu kuangalia
pale alipoanguka yule mtu, kwa macho hafifu aligundua kuwa mgongoni kwa lile jitu
kunakitu kama mwiba wa mchongoma umemchoma, kwa haraka Amata aligundua kuwa
hiyo ni silaha hata ri ya ‘Amazonia’ alipata faraja kuwa huwenda kuna binadamu pale
aliyefanya kazi ile, kwa hiyo tumaini la maisha lilimjia tena, lakini hakuona dalili yamtu
isipokuwa viumbe vile vyenye hasira vikiruka huku na huko wengine wakiwa porini
kutafuta chochote, mara wakarudi na aina fulani ya majani wakayapondaponda huku
wakiongea lugha ile isiyoeleweka kicha wakamkamulia maji ya majani yale mdomoni
yule kiongozi wao baada ya muda kidogo akapiga chafya kama tani mfulululizo
akaamka. Amata lijua hapa kazi hii labda huyualiyefungwa hapo kaifanya lakini
alipomwangalia aliona ni kama mwili usio na uhai, matone ya damu yakiwa
yanadondoka taratibu kutoka mwili wa mtu yule. Amata alijaribu kuangalia kwa machale
mwili ule lkini hakuweza kugundua ni wa nani japo alihisi ni wa mmoja wao.
Lile jitu likaamka tena sasa likiwa na hasira na kukunja sura yake mbaya sasa halikuwa
na huruma hata kidogo, lilichukua lile jiti lake kubwa kuendelea na alichodhamiria.
Akiwa kainua tena jisu lake na huku kwa nyuma Amata kabanwa na mti wenye kipago na
mtu mwingine ili kuhakikisha lengo lao linatimia. Kabla hajashusha jisu lile mwili wa
Amata ulianguka chini, kamba iliyofungwa miguuni mwake ilikatwa kwa ustadi mkubwa
sana, Amata alisikia mvumo wa kasi ya kitu kichokata kamba ile, mara moja aligundua
kuwa ulikuwa mshale uliorushwa kwa uta wenye nguvu, na aina hii ya mishale ni
mishale iliyotengenezwa sana na marehemu baba yake, Amata aliduwaa pale chini hakuelewa nini kinatokea kabla hajapata akili sawasawa alishuhudia mshale mvumo wa
mshale mwingine ukielekea upande wake alijigeuza kifudifudi na mshsle ule ulipita
katikati ya fundo lililofunga mikono yake na kuchoma chini ardhini, sasa kamba ile
ilikuwa imefunguka, Amata alisikia mbinja ya ajabu akajiinua haraka aliposimama
akapata kizunguzungu cha ghafla kilichomrudisha chini lakini hiyo ilikuwa ni bahati
kwake kwani lile jitu lilifurusha jisu lake lililolenga shingo ya Amata lakini shabaha
ikakosa malengo, jitu lile lilimfuata Amata pale chini Amata kwa haraka akauchomoa ule
mshale pale ardhini na kuurusha kwa mrusho hafifu lakini mshale ule ulitua jichoni kwa
lile jitu, damu zikachuruzika kwa kasi, Amata alijiviringa upande wapi lina kulifikia lile
jisu alilinyakua na kupiga goti moja na kushindilia lile bisu mgongoni kwa lile jitu, lile
jitu likatoa mkoromo wa kutisha na kukata roho. Hali haikuwa shwari eneo lile, wale
wengine wakaanza kupiga kelele za ajabu na kuanza kumshambulia Amata kwa mapigo
ya kifo, kutokana na uchovu aliyonao Amata aliona hapa hata kukimbia hawezi alijitahidi
kufanya hiki na kile, mmoja wao alichumpa mbele ya Amata na kumkaba koo kwa
mikono yake yenye nguvu na mikavu inayokwaruza, lakini mara Amata alishuhudia
mshale mwingine ukizama shingoni kwa huyu mtu na kuanguka chini kama mzigo,
waliobaki walipoona hayo wakaamnza kutawanyika wakipiga kelele za sasa zilikuwa
tofauti na za mwanzo mara kutoka mbali aliona kundi lingine likija upande ule, Amata
alishindwa afanye nini, akauendea ule mwili ulioning’inizwa pale kuutazama vizuri.
Wale viumbe waliosalia waliendelea kutandikwa na mishale isiyojulikana wapi inatokea
na nani anaerusha. Amata alipigwa na butwaa alipouangalia mwili ule kwa nyuma...
hakuamini macho yake
“Ah!” alishangaa na kufikicha macho yake kama mtu ambaye haamini ni nini
alichokiona. Aligundua tu ni mwili wa binadamu wa kizungu kwa kuwa aliona baadhi ya
nywele ndefu ambazo zilisalia kichwani mwa mwili ule, sura yake haikujulikana vizuri
kwa jinsi ilivyogandamana na damu nyingi, Amata alijaribu kwa haraka labda angeona
angalau jinsia ya mwili huu ili ajue kuwa ni Hellen au Stephan, lakini kilichomshangaza
mwili ule haukuwa na alama yoyote ya jinsia. Watu wale walizidi kusogea wakiwa na
hari ya kufanya mashambulizi kwa adui zao, wale wenzao wote waliokuja na yule
kiongozi wao walikuwa wamelala kimya juu ya ardhi bila uhai baada ya kupigwa kwa
mishale isiyojulikana wapi inatoka, Amata alisikia mlio wa mbinja uliopigwa kutokea
kichakani, alijua maana ya mbinja ile kwani ni baba yake alikuwa akiipiga kumuashiria
kuwa hapo kuna hatari atoke haraka, Amata alishangaa maana hakujua ni nani
aliyeyafanya haya yote. Alihisi kitu kikimshika bega alipogeuka alikutana uso kwa uso
na nyani mkubwa mwenye kichwa cheupe, walitazamana kama sekunde kumi hivi, nyani
yule alimshika mkono Amata na kumvutia msituni, Amata alimwangalia nyani yule kwa
makini kule msituni ‘Kingusu’ Amata alijisemea moyoni, lakini alishangaa nyani huyu
amepata wapi ujasiri au amejuaje kuwa yeye yuko huku msituni! Kwa maana nyani huyu
alimuona zamani sana enzi za utoto wake, Amata alikaa chini ndani ya kichaka kile nyani
yule alimletea baadhi ya matunda, Amata alikula na kisha nyami yule akampa ishara ya
kuwa amfuate, Amata alinyanyuka na kumfuata nyani yule huku kichwani mwake
akijaribu kukumbuka juu ya kiumbe hiki cha ajabu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom