Xav Emmanuel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2018
- 214
- 315
RIWAYA: LOVE SPEAR 01
MTUNZI; AUTHOR XAV
NAMBA; 0672493994
Email: xavemmanuel12@gmail.com
----------------------------
UTANGULIZI;
MAPENZI ni moja kati ya njia ambayo kila binadamu anapaswa apitie. Ni njia ambayo haina muonekano halisi ambao unajulikana. Kila mtu anaonja radha yake katika njia hii. Achana na wale wanaoyaona kuwa ni shubiri na hawa wengine wanasema mapenzi ni asali ya kujazia uhai. Kwamaana usipofanya chochote kuhusu mapenzi, unaweza kudhoofika kiuhai.
Hata mimi nimeshindwa kabisa kuyazungumzia mapenzi kwa mapana Zaidi. Kwa maana niliyopitia mimi si hayo tu nawe umepitia.. bali nawe unaweza ukawa na nyongeza au kunipa kitu kipya kabisa amabacho umekutana nacho kwenye njia hii ya Mapenzi pasi mwingine kupitia au kukiona.
ROYSON JOHNSON aliyapa mapenzi alama nyingi sana katika udanganyifu na kutoaaminika. Hatimaye anapata moja kati ya Spea ambayo inamfundisha nini maana ya Mapenzi. Anamfunza ni maana KUPENDA. Hatimaye REHMA AYOUB anakuwa Spea ya mapenzi kwa ROY. Anatoa vilivyoaribika na kudhorota na kuweka vifaa vipya kabisa.. njia hii inakuwa faida na hasara kwa pande zote mbili..
TIRIRIKA NAYO
-------------------------------
KIPANDE CHA 1;
CHUO KIKUU CHA ELIMU DAR ES SAALAM kilikuwa katika harakati zake za kila mhura wa masomo katika kuhakikisha wanakimbizana na muda kwa kumaliza kila kitu kinachohusu mtahara katika ufunzaji wa wanafunzi waalimu ambao wanatumika na wanaendelea kutumika katika Nyanja zote za elimu na taasisi duniani kote.
Pilikapilika zilikuwa moja kati ya vifungu vya sharia mama za chuo. Hakuna katiba wala kipande cha karatasi chochote ambacho kiliandika kuteseka au kusoma kupita maelezo katika chuo hiki. Sharia ya maangaiko ilipitishwa punde tu mara baada ya kupokelewa sifa za chuo kuwa kinadhalisha Uma wa waalimu ambao kwa takwimu ni bora katika utawala na ufundishaji kwa ujumla. Hivyo wanafunzi waalimu walizidi kuchilimika tu kutofuta uhalisia wa chuo hicho wa tangu na tangu.
Waliopishana katika kumbi za kusomea; walipishana. Waliopigana vikumbo kutoka na kuingia getini nao walifanya hivyo. Watu walikuwa wamezagaa kila kona ya chuo. Msururu wa wanafunzi walimu ulikuwa mkubwa mno kiasi cha wengi kukosa hata sehemu ya kukaa.
“Wazee.. njaa imekaza sana kwa upande wangu leo… mniache nipumue basi wakuu!.” Moja ya wanafunzi katika kundi alitoka nje ya mada katika mjadala na kuingiza uchosho kwa wenzake.
“Mwanangu! mi mwenyewe naona kuna wadudu wapo kando.. kwa kona hii wananibinya kinoma yani.. yani kama wanacheza Football tumboni” Mwenzake alidakia na kufanya kundi nzima kukenua meno yao. Walicheka kwa jitihada bila kuachiana nafasi. Wakajikuta wanafunika mada iliyowakusanyisha pale na wote kuikimbilia kwa hamu mada mpya ya njaa.
“Kud*d*ki..!, ko wajuba mnakazaa kuingiza madesa bila mlo?, mimi nilikuwa nawachora tu!. Hakuna nililoshika hata moja. Ukicheki mida inaruhusu kabisa kula..” Mwengine naye akajinyooshea njia kujipa faida. Wote walivamiana kwa kejeli. Walionyesha kufahamiana sana. Walikuwa jumla ya wanaume watano.
“Ohp!, afu ROY anazingua ujue. Toka afike hajaongea kabisa yani. Anatushangaa tu hapa. Haya mada yako ya njaa hiyoo imefika.. changia sasa.” Yule aliyeongea mwanzo akamgeuzia kibanzi mwenzake wa pembeni. Alikuwa naye karibu mkono wa kushoto.
“Brother! Njaa haina mwenyewe!. Kwani kuwasilisha swali si Alhamisi?.. tunakaza leoo da hahhahaha.. tutakutana bhana, kwani imebaki sehemu ndogo!.” Mwingine alimtetea Roy na kutoa ushauri uliofanya mmoja wao kufunga kitabu na kukikumbatia kifuani.
“Aaah!, semeni tu hivyo. Kikubwa kila mtu achukue pati yake hapa. Ngoma itakuwa rahisi Zaidi…”
“Poa,.. We KELVIN tutakutana Whatsapp. Tutachagua kulekule vipengele. Au sio..” alisema yule wa mwanzo na kunyanyuka pale. Alionekana mwongeaji sana.
ROY aliyekuwa kimya toka mazungumzo yanaanza, alichukua kitabu chake na kukifunua hadi katikati kama mtu anayehesabu pesa hivi. Alipofika kati alikomea hapo. Macho yake yakaangaza sehemu ya kitabu aliyofungua na kuipitia kwa macho yake.
“… If you bring us all this way for nothing I shall beat sense into you…. I have told you to let her alone.i know to deal with them, said Okagbue…” alisoma na kisha kutabasamu. Alionesha maneno hayo yamemgusa vilivyo. Akakifunga kitabu hicho na kusoma jina la jarada la kitabu.
“THINGS FALL APART” alihamasika sana baada ya kusoma maneno hayo ya lugha ya kiingeleza. Akayasoma tena kuhakiki kama atakuwa alipatia lakini mwishowe alijikuta anaachia tena tabasamu. Roy alikuwa anaongea na nafsi yake.
“It’s true!!. all things falling apart..” alijisema kimoyomoyo na kutabasamu tena. Alimalizia kusoma na jina la mwandishi wa kitabu hicho. Bado alikuwa anakitazama tu kitabu. Sio kwamba hakuwai kukiona kitabu hicho mwanzo, hapana. Ila ugeni wa kitu ambacho kipo moyoni kilimfanya kila kitu anachokiona kiwe kipya tena. Alikuwa anatabasamu tu mwenyewe akigeuza geuza kitabu hicho kilichoandikwa na Mbaba nguli wa Fasihi Afrika; Chinua Achebe.
“We taila, mbona unajichekesha chekesha sana!..” Kelvin alikuwa tayari kumkabili Roy ambaye alionekana kuwa na furaha ya aibu. Kwani mwanzo hakuionesha kabisa. Ila baada ya wenzao kutawanyika, Roy aliamua kujichekesha chekesha ovyo.
Roy akatazamana na rafiki yake huyo bila kupepesa macho. Roy alikuwa kama mtu ambaye amenyweshwa pombe inayonoga kwa masaa matatu ya nyuma, alikuwa na hali tofauti siku hiyo kwani baada ya kumjibu rafiki yake huyo alianza tena kutabasamu. Alikuwa kama kindele; yaani mtu aliyechukuliwa msukule na kurudishwa tena uraiani.
“Bro! usiniaminishe kama lile dili limetiki!!.. akii nitakupa heshima yako. Sio kazi rahisi kwa yule mtoto..” Kelvin alianza kutiwa shaka na mpango ambao waliapiana hapo mwanzo. Alihama upande na kumfuata Roy upande aliokaa.
“Enhe.. niambie kabla Tumbo halijatoboka hapa.. nina ubao kish*nzi sana yani..” alidadavua kutaka kujua kile walichoahidiana.
“Wooooooohps!... we unaongelea nini kwani!” Roy alimtoa maana mwenzake kwa kutoelewa kitu ambacho alikuwa anamuuliza.
“Mtoto Scola!... Umbwa wewe!. Unajichekesha tu hapa.. vipi ulimaliza jana hilehile au?” sasa alikuwa muwazi Kelvin.
“Hahahahaha!, we taila sana ujue!. Scola ndo kidudu gani. Bila shaka nilimaliza jana sa tatu tu. Sa tano nikamrudisha kwake. Hana jipya yule… hana tofauti na wengine. Hana makali, hana show, hana mbwembwe, hana lolote. Umbwa wewe… hahhahaha ulimsifia bure tu. We fala macho sio kigezo cha kuwa mzuri kitandani! Hahahahaha!..” alicheka Roy na kumwacha Kelven kwenye hali ya sintofahamu.
“Kwahiyo umepiga?” aliuliza tena kwa kutoamini.
“Ee, nimepiga na kukata.. hahahaha nilikuwa sina salio.. haha!” alijibu Roy na kucheka kwa sauti. Alisahau kabisa kama yupo chuo.
“Daah, we sio poa asee!. Ee kituo kinachofuata ni wapi sasa!”aliuliza Kelvin kumaanisha baada ya Scola nani anafuata.
“Aah!, Ebu achana na hawa watotowatoto.. nina kitu kipya.. bro… kipya!” aliongea Roy na sasa hakuonesha kucheka. Alikuwa muwazi katika sura yake na kuonesha kuwa alikuwa makini na anachokisema.
“Ee!” aliitika kwa utayari Kelvin na kumwacha Roy kuendelea.
“Bro.. naomba niwe serious kwa hili!.. sina utani kabisa.. hapa unaponiona viungo vyangu vya mwili vyote vimeseparate!. Vimetawanyika yani..” Aliongea Roy
“Vimetawanyika!,!” alishaangaa Kelvin na macho yake yakatua hadi kwenye sehemu ya uume wa Roy ambao umefichwa na kitambaa cha kaki. Alikuwa anahakikisha ni kiungo gani kilichotawanyika kwa Roy. Akaganda kutazama hapo.
“We kweli F*l*..!, Umbwa wewe, hahahaha..” alimshika kichwa Kelvin na kumuinua hadi kutazamana. Wote wakacheka. Walikuwa wanajuana kwa vilemba vyao.
“Brother!, nimetoka lecture leo ahsubui ile ya 1 hadi 2 kasoro 5 ile. Huwezi amini ile korido ya kwenda Room B... ule upande wa Wajawazito.. kuna mtoto nimemuona.. I Swear!. (naapa) sijawai kumwona mtu huyo katu… Bro nimeshindwa hata kupokea salamu yake. Nimejikuta namtazama tu hadi anapotea!.. aki! Kelv. DUCE hii sijawai penda kabisa… ila sasa naona kabisa ndio muda wangu huu!” aliongea kwa msisitizo.
“Nyooo!!!! wewe huyo? Hahhaha. We umbwa unaharibu tu watoto wa wenzako. Upende wapi wewe!!” alimshushua jamaake bila kumwonea aibu. Roy alitazama chini na kuwa mpole. Akainuka.
“Bro. ninachokuambia nakiamini kutoka moyoni. Nimempenda yule dada kwa asilimia zote za hapa duniani. Na nina hakika nitampata… kila gharama nitatumia.. nitampata tu, na nina hakika kuwa… yani Bro nakuhakikishia!. Nikimpata tu basi naacha umalaya. Natulia kaka aki tena” Roy leo alikuwa makini sana kwa aliyokuwa anaongea, hakuwa na utani hata kidogo. Hali hiyo ilimshitua kabisa rafiki yake na kushindwa kumwamini moja kwa moja.
“Sina hakika na ahadi yako. We mtafuta huyo mdada.. mchafue.. mwache.. mimi nishakuzoea mbona!” Bado Kelvin alikuwa mbishi kukubali. Roy alimtazama tu rafiki yake huyo na kutomjibu chochote. Alikusanya kila kilichochake na kuachana na rafiki yake huyo. Kila mtu akaendelea na majukumu yake..
INAENDELEA…..
MTUNZI; AUTHOR XAV
NAMBA; 0672493994
Email: xavemmanuel12@gmail.com
----------------------------
UTANGULIZI;
MAPENZI ni moja kati ya njia ambayo kila binadamu anapaswa apitie. Ni njia ambayo haina muonekano halisi ambao unajulikana. Kila mtu anaonja radha yake katika njia hii. Achana na wale wanaoyaona kuwa ni shubiri na hawa wengine wanasema mapenzi ni asali ya kujazia uhai. Kwamaana usipofanya chochote kuhusu mapenzi, unaweza kudhoofika kiuhai.
Hata mimi nimeshindwa kabisa kuyazungumzia mapenzi kwa mapana Zaidi. Kwa maana niliyopitia mimi si hayo tu nawe umepitia.. bali nawe unaweza ukawa na nyongeza au kunipa kitu kipya kabisa amabacho umekutana nacho kwenye njia hii ya Mapenzi pasi mwingine kupitia au kukiona.
ROYSON JOHNSON aliyapa mapenzi alama nyingi sana katika udanganyifu na kutoaaminika. Hatimaye anapata moja kati ya Spea ambayo inamfundisha nini maana ya Mapenzi. Anamfunza ni maana KUPENDA. Hatimaye REHMA AYOUB anakuwa Spea ya mapenzi kwa ROY. Anatoa vilivyoaribika na kudhorota na kuweka vifaa vipya kabisa.. njia hii inakuwa faida na hasara kwa pande zote mbili..
TIRIRIKA NAYO
-------------------------------
KIPANDE CHA 1;
CHUO KIKUU CHA ELIMU DAR ES SAALAM kilikuwa katika harakati zake za kila mhura wa masomo katika kuhakikisha wanakimbizana na muda kwa kumaliza kila kitu kinachohusu mtahara katika ufunzaji wa wanafunzi waalimu ambao wanatumika na wanaendelea kutumika katika Nyanja zote za elimu na taasisi duniani kote.
Pilikapilika zilikuwa moja kati ya vifungu vya sharia mama za chuo. Hakuna katiba wala kipande cha karatasi chochote ambacho kiliandika kuteseka au kusoma kupita maelezo katika chuo hiki. Sharia ya maangaiko ilipitishwa punde tu mara baada ya kupokelewa sifa za chuo kuwa kinadhalisha Uma wa waalimu ambao kwa takwimu ni bora katika utawala na ufundishaji kwa ujumla. Hivyo wanafunzi waalimu walizidi kuchilimika tu kutofuta uhalisia wa chuo hicho wa tangu na tangu.
Waliopishana katika kumbi za kusomea; walipishana. Waliopigana vikumbo kutoka na kuingia getini nao walifanya hivyo. Watu walikuwa wamezagaa kila kona ya chuo. Msururu wa wanafunzi walimu ulikuwa mkubwa mno kiasi cha wengi kukosa hata sehemu ya kukaa.
“Wazee.. njaa imekaza sana kwa upande wangu leo… mniache nipumue basi wakuu!.” Moja ya wanafunzi katika kundi alitoka nje ya mada katika mjadala na kuingiza uchosho kwa wenzake.
“Mwanangu! mi mwenyewe naona kuna wadudu wapo kando.. kwa kona hii wananibinya kinoma yani.. yani kama wanacheza Football tumboni” Mwenzake alidakia na kufanya kundi nzima kukenua meno yao. Walicheka kwa jitihada bila kuachiana nafasi. Wakajikuta wanafunika mada iliyowakusanyisha pale na wote kuikimbilia kwa hamu mada mpya ya njaa.
“Kud*d*ki..!, ko wajuba mnakazaa kuingiza madesa bila mlo?, mimi nilikuwa nawachora tu!. Hakuna nililoshika hata moja. Ukicheki mida inaruhusu kabisa kula..” Mwengine naye akajinyooshea njia kujipa faida. Wote walivamiana kwa kejeli. Walionyesha kufahamiana sana. Walikuwa jumla ya wanaume watano.
“Ohp!, afu ROY anazingua ujue. Toka afike hajaongea kabisa yani. Anatushangaa tu hapa. Haya mada yako ya njaa hiyoo imefika.. changia sasa.” Yule aliyeongea mwanzo akamgeuzia kibanzi mwenzake wa pembeni. Alikuwa naye karibu mkono wa kushoto.
“Brother! Njaa haina mwenyewe!. Kwani kuwasilisha swali si Alhamisi?.. tunakaza leoo da hahhahaha.. tutakutana bhana, kwani imebaki sehemu ndogo!.” Mwingine alimtetea Roy na kutoa ushauri uliofanya mmoja wao kufunga kitabu na kukikumbatia kifuani.
“Aaah!, semeni tu hivyo. Kikubwa kila mtu achukue pati yake hapa. Ngoma itakuwa rahisi Zaidi…”
“Poa,.. We KELVIN tutakutana Whatsapp. Tutachagua kulekule vipengele. Au sio..” alisema yule wa mwanzo na kunyanyuka pale. Alionekana mwongeaji sana.
ROY aliyekuwa kimya toka mazungumzo yanaanza, alichukua kitabu chake na kukifunua hadi katikati kama mtu anayehesabu pesa hivi. Alipofika kati alikomea hapo. Macho yake yakaangaza sehemu ya kitabu aliyofungua na kuipitia kwa macho yake.
“… If you bring us all this way for nothing I shall beat sense into you…. I have told you to let her alone.i know to deal with them, said Okagbue…” alisoma na kisha kutabasamu. Alionesha maneno hayo yamemgusa vilivyo. Akakifunga kitabu hicho na kusoma jina la jarada la kitabu.
“THINGS FALL APART” alihamasika sana baada ya kusoma maneno hayo ya lugha ya kiingeleza. Akayasoma tena kuhakiki kama atakuwa alipatia lakini mwishowe alijikuta anaachia tena tabasamu. Roy alikuwa anaongea na nafsi yake.
“It’s true!!. all things falling apart..” alijisema kimoyomoyo na kutabasamu tena. Alimalizia kusoma na jina la mwandishi wa kitabu hicho. Bado alikuwa anakitazama tu kitabu. Sio kwamba hakuwai kukiona kitabu hicho mwanzo, hapana. Ila ugeni wa kitu ambacho kipo moyoni kilimfanya kila kitu anachokiona kiwe kipya tena. Alikuwa anatabasamu tu mwenyewe akigeuza geuza kitabu hicho kilichoandikwa na Mbaba nguli wa Fasihi Afrika; Chinua Achebe.
“We taila, mbona unajichekesha chekesha sana!..” Kelvin alikuwa tayari kumkabili Roy ambaye alionekana kuwa na furaha ya aibu. Kwani mwanzo hakuionesha kabisa. Ila baada ya wenzao kutawanyika, Roy aliamua kujichekesha chekesha ovyo.
Roy akatazamana na rafiki yake huyo bila kupepesa macho. Roy alikuwa kama mtu ambaye amenyweshwa pombe inayonoga kwa masaa matatu ya nyuma, alikuwa na hali tofauti siku hiyo kwani baada ya kumjibu rafiki yake huyo alianza tena kutabasamu. Alikuwa kama kindele; yaani mtu aliyechukuliwa msukule na kurudishwa tena uraiani.
“Bro! usiniaminishe kama lile dili limetiki!!.. akii nitakupa heshima yako. Sio kazi rahisi kwa yule mtoto..” Kelvin alianza kutiwa shaka na mpango ambao waliapiana hapo mwanzo. Alihama upande na kumfuata Roy upande aliokaa.
“Enhe.. niambie kabla Tumbo halijatoboka hapa.. nina ubao kish*nzi sana yani..” alidadavua kutaka kujua kile walichoahidiana.
“Wooooooohps!... we unaongelea nini kwani!” Roy alimtoa maana mwenzake kwa kutoelewa kitu ambacho alikuwa anamuuliza.
“Mtoto Scola!... Umbwa wewe!. Unajichekesha tu hapa.. vipi ulimaliza jana hilehile au?” sasa alikuwa muwazi Kelvin.
“Hahahahaha!, we taila sana ujue!. Scola ndo kidudu gani. Bila shaka nilimaliza jana sa tatu tu. Sa tano nikamrudisha kwake. Hana jipya yule… hana tofauti na wengine. Hana makali, hana show, hana mbwembwe, hana lolote. Umbwa wewe… hahhahaha ulimsifia bure tu. We fala macho sio kigezo cha kuwa mzuri kitandani! Hahahahaha!..” alicheka Roy na kumwacha Kelven kwenye hali ya sintofahamu.
“Kwahiyo umepiga?” aliuliza tena kwa kutoamini.
“Ee, nimepiga na kukata.. hahahaha nilikuwa sina salio.. haha!” alijibu Roy na kucheka kwa sauti. Alisahau kabisa kama yupo chuo.
“Daah, we sio poa asee!. Ee kituo kinachofuata ni wapi sasa!”aliuliza Kelvin kumaanisha baada ya Scola nani anafuata.
“Aah!, Ebu achana na hawa watotowatoto.. nina kitu kipya.. bro… kipya!” aliongea Roy na sasa hakuonesha kucheka. Alikuwa muwazi katika sura yake na kuonesha kuwa alikuwa makini na anachokisema.
“Ee!” aliitika kwa utayari Kelvin na kumwacha Roy kuendelea.
“Bro.. naomba niwe serious kwa hili!.. sina utani kabisa.. hapa unaponiona viungo vyangu vya mwili vyote vimeseparate!. Vimetawanyika yani..” Aliongea Roy
“Vimetawanyika!,!” alishaangaa Kelvin na macho yake yakatua hadi kwenye sehemu ya uume wa Roy ambao umefichwa na kitambaa cha kaki. Alikuwa anahakikisha ni kiungo gani kilichotawanyika kwa Roy. Akaganda kutazama hapo.
“We kweli F*l*..!, Umbwa wewe, hahahaha..” alimshika kichwa Kelvin na kumuinua hadi kutazamana. Wote wakacheka. Walikuwa wanajuana kwa vilemba vyao.
“Brother!, nimetoka lecture leo ahsubui ile ya 1 hadi 2 kasoro 5 ile. Huwezi amini ile korido ya kwenda Room B... ule upande wa Wajawazito.. kuna mtoto nimemuona.. I Swear!. (naapa) sijawai kumwona mtu huyo katu… Bro nimeshindwa hata kupokea salamu yake. Nimejikuta namtazama tu hadi anapotea!.. aki! Kelv. DUCE hii sijawai penda kabisa… ila sasa naona kabisa ndio muda wangu huu!” aliongea kwa msisitizo.
“Nyooo!!!! wewe huyo? Hahhaha. We umbwa unaharibu tu watoto wa wenzako. Upende wapi wewe!!” alimshushua jamaake bila kumwonea aibu. Roy alitazama chini na kuwa mpole. Akainuka.
“Bro. ninachokuambia nakiamini kutoka moyoni. Nimempenda yule dada kwa asilimia zote za hapa duniani. Na nina hakika nitampata… kila gharama nitatumia.. nitampata tu, na nina hakika kuwa… yani Bro nakuhakikishia!. Nikimpata tu basi naacha umalaya. Natulia kaka aki tena” Roy leo alikuwa makini sana kwa aliyokuwa anaongea, hakuwa na utani hata kidogo. Hali hiyo ilimshitua kabisa rafiki yake na kushindwa kumwamini moja kwa moja.
“Sina hakika na ahadi yako. We mtafuta huyo mdada.. mchafue.. mwache.. mimi nishakuzoea mbona!” Bado Kelvin alikuwa mbishi kukubali. Roy alimtazama tu rafiki yake huyo na kutomjibu chochote. Alikusanya kila kilichochake na kuachana na rafiki yake huyo. Kila mtu akaendelea na majukumu yake..
INAENDELEA…..