Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,014
- 9,883
UTATU WA G RECORDS
DJ Gulu Ramadhan Nnanji " G LOVER" alifungua studio yake, G RECORDS na kumpatia mikoba yote ya production, Roy Bukuku.
Kazi nyingi zilipikwa pale huku utambulisho wa kazi alizozitengeneza Roy ukiwa ni uzito wa midundo yake.
Mara kukawa na G2 (G mbili au G Square), kisha akaibuka KGT na baadaye, Roy akafariki na kubadili taswira nzima ya G RECORDS.
Nazileta kazi 20 zilizopikwa na "wamba" hawa wawili kutoka nyumba kubwa, G RECORDS
NGOMA KUMI ZA ROY
1. HAWAPENDI - JOH MAKINI
2. ICE CREAM- NOORAH FT SUMA LEE
3. USIKU HUU - DAZ BABA FT BLUE
4. CHUNGWA - SUMA LEE
5. MAPOZI - MR BLUE
6. SAFARI NI NDEFU - BWANA MISOSI FT SUMA LEE
7. USITOE - BIG MAN IZ FT ENIKAH
8. NIMEKUBAMBA - ENIKAH
9. SIAMINI - MATONYA
10. DAKIKA MOJA - NGWEA FT NOORAH
NGOMA KUMI ZA KGT
1. NIACHE NITEMBEE - BABY J FT CHID BENZ
2. HASIRA ZA NINI - CHID BENZ FT ALI KIBA
3. CINDERELLA - ALI KIBA
4. NI SOO - PASHA
5. NIDANGANYE - SHETTA FT DIAMOND
6. MAPENZI MATAMU - HAKEEM 5
7. MOYO - ABBY SKILLS FT KIBA
8. I'M IN LOVE - ALI COM FT KGT
9. ABIRIA CHUNGA MZIGO WAKO - MATONYA FT BLUE
10. ANASOMA - PICO FT FA
Roy ndiye aliyemtoa Blue. Baada ya kifo chake, Blue alipata shida sana maana alikiri kuwa Roy alimuwezea sana na baada ya kutuliza akili sana, akaona akomae na Man Walter, Sei na Dunga kwa kiasi kikubwa.
Roy alifanya kazi nyingi za Suma Lee, Abby Skills, na Mr Blue.
20% anasimulia kuwa kipindi analibishia hodi game hili aliibuka kwa Roy mpaka akachoka.
Siku moja Blue akagonga na kuwaacha akina 20 wakiwa WAMEKAA benchi. Roy akiwa ndani akauliza, nani anagonga, Blue akajibu, "Blue hapa" Roy akamwambia apite.
Siku ya pili, 20 akaona usintanie, akagonga na Roy alipouliza nani?? 20 akajibu "Blue hapa" Roy akaruhusu aingie, wakatoana nishai huko ndani.
Baada ya Wameiba pombe na Vijimambo kufanya vizuri, Roy akamchek Noorah na kumwambia kama ana ngoma nyingine aibuke watoe kitu, Noorah akafunua daftari lake la mistari na kwenda na vocals zote mpaka chorus lakini Roy akaivua Ile chorus na kumpa msanii wake afanye maunyama, ndiyo namwongelea Ismail "Suma Lee"
Roy aliacha pigo kubwa kwa WAPENDA MUZIKI lakini pia kwa mdogo wake wa damu aliyefanya naye kazi nyingi aitwaye ENIKAH.
Gulu aliwahi kulalamikiwa kuwa aliwapendelea Wazanzibar wenzake na wasanii wake wengi walidaiwa kuwa waislam, akawapa jibu jepesi tu kuwa mbona producer wake mkuu Roy alikuwa Mkristo.
KGT yeye aliendelea na Abby Skills, na Ali Kiba lakini akatuibulia Pasha na kufanya kazi nyingi na Picco Kikongwe.
Msanii gani mwingine au ngoma gani nyingine zilipikwa G2 na zimesahaulika?
Una kumbukumbu gani nyingine kuhusu G RECORDS?
LUAH
110523.
DJ Gulu Ramadhan Nnanji " G LOVER" alifungua studio yake, G RECORDS na kumpatia mikoba yote ya production, Roy Bukuku.
Kazi nyingi zilipikwa pale huku utambulisho wa kazi alizozitengeneza Roy ukiwa ni uzito wa midundo yake.
Mara kukawa na G2 (G mbili au G Square), kisha akaibuka KGT na baadaye, Roy akafariki na kubadili taswira nzima ya G RECORDS.
Nazileta kazi 20 zilizopikwa na "wamba" hawa wawili kutoka nyumba kubwa, G RECORDS
NGOMA KUMI ZA ROY
1. HAWAPENDI - JOH MAKINI
2. ICE CREAM- NOORAH FT SUMA LEE
3. USIKU HUU - DAZ BABA FT BLUE
4. CHUNGWA - SUMA LEE
5. MAPOZI - MR BLUE
6. SAFARI NI NDEFU - BWANA MISOSI FT SUMA LEE
7. USITOE - BIG MAN IZ FT ENIKAH
8. NIMEKUBAMBA - ENIKAH
9. SIAMINI - MATONYA
10. DAKIKA MOJA - NGWEA FT NOORAH
NGOMA KUMI ZA KGT
1. NIACHE NITEMBEE - BABY J FT CHID BENZ
2. HASIRA ZA NINI - CHID BENZ FT ALI KIBA
3. CINDERELLA - ALI KIBA
4. NI SOO - PASHA
5. NIDANGANYE - SHETTA FT DIAMOND
6. MAPENZI MATAMU - HAKEEM 5
7. MOYO - ABBY SKILLS FT KIBA
8. I'M IN LOVE - ALI COM FT KGT
9. ABIRIA CHUNGA MZIGO WAKO - MATONYA FT BLUE
10. ANASOMA - PICO FT FA
Roy ndiye aliyemtoa Blue. Baada ya kifo chake, Blue alipata shida sana maana alikiri kuwa Roy alimuwezea sana na baada ya kutuliza akili sana, akaona akomae na Man Walter, Sei na Dunga kwa kiasi kikubwa.
Roy alifanya kazi nyingi za Suma Lee, Abby Skills, na Mr Blue.
20% anasimulia kuwa kipindi analibishia hodi game hili aliibuka kwa Roy mpaka akachoka.
Siku moja Blue akagonga na kuwaacha akina 20 wakiwa WAMEKAA benchi. Roy akiwa ndani akauliza, nani anagonga, Blue akajibu, "Blue hapa" Roy akamwambia apite.
Siku ya pili, 20 akaona usintanie, akagonga na Roy alipouliza nani?? 20 akajibu "Blue hapa" Roy akaruhusu aingie, wakatoana nishai huko ndani.
Baada ya Wameiba pombe na Vijimambo kufanya vizuri, Roy akamchek Noorah na kumwambia kama ana ngoma nyingine aibuke watoe kitu, Noorah akafunua daftari lake la mistari na kwenda na vocals zote mpaka chorus lakini Roy akaivua Ile chorus na kumpa msanii wake afanye maunyama, ndiyo namwongelea Ismail "Suma Lee"
Roy aliacha pigo kubwa kwa WAPENDA MUZIKI lakini pia kwa mdogo wake wa damu aliyefanya naye kazi nyingi aitwaye ENIKAH.
Gulu aliwahi kulalamikiwa kuwa aliwapendelea Wazanzibar wenzake na wasanii wake wengi walidaiwa kuwa waislam, akawapa jibu jepesi tu kuwa mbona producer wake mkuu Roy alikuwa Mkristo.
KGT yeye aliendelea na Abby Skills, na Ali Kiba lakini akatuibulia Pasha na kufanya kazi nyingi na Picco Kikongwe.
Msanii gani mwingine au ngoma gani nyingine zilipikwa G2 na zimesahaulika?
Una kumbukumbu gani nyingine kuhusu G RECORDS?
LUAH
110523.