the_legend
JF-Expert Member
- Jan 14, 2019
- 1,612
- 7,110
- Thread starter
- #201
RIWAYA : MKONO WA CHUMA
MTUNZI : ALEX KILEO
SEHEMU YA ISHIRINI NANE.
________________
ENDELEA....
_________________
Sajenti Minja akapelekwa selo na kuwaacha wakubwa zake wakijadiliana, wote walionekana kutopendezwa na kitendo cha Sajenti Minja, na wote waliamini Sajenti Minja amemtorosha yule mwanamke, ila hawakujua sababu kwanini Sajenti Minja amtoroshe yule mwanamke?.
Baada ya majadiliano ya nusu saa, wale polisi walitawanyika, kila mtu akaelekea panapo muhusu, mkuu wa polisi alirudi ofisini kwake, hukutaka kuongea hata na waandishi wa habari, kichwa chake kilishavurugika kabisa, hakikukaa sawa kwa muda huo.
Mkuu wa polisi akaingia ndani ya ofisi yake, kisha akavua kofia na kuiweka juu ya meza, akaanza kufikiri huku akizunguka mule ndani ya ofisi yake, alifanya hivyo kama dakika kumi, kisha akachukua simu na kupiga namba anayoijua yeye,
"bado upo zamu?" Mkuu wa polisi aliuliza kwa mamlaka,.
"ndio mkuu" Sauti ya upande wa pili ilijibu kwa utii,
"mlete Sajenti Minja ofisini kwangu, sasa hivi" Mkuu wa polisi aliongea kisha akakata simu, alafu akavuta kiti na kukaa, kisha akanywa maji yaliyokuwa katika chupa, na kisha akavaa kofia yake, akatulia akimsubiri Sajenti Minja.
Baada ya dakika mbili mlango wa ofisi yake uligongwa, akaingia Askari mmoja aliyemtanguliza Sajenti Minja mbele huku mikononi akiwa na pingu,
"kwa hiyo hata alipokuwa selo hamkufungua pingu?" Mkuu wa polisi aliuliza,
"ndio mkuu" Askari yule alijibu,
"na nyie mkaona sawa tu mtu kuwa na pingu ndani ya selo?" Mkuu wa polisi akaendelea kuongea na kumfanya yule Askari aliyemleta Sajenti Minja atoe funguo mfukoni ili amfungue Sajenti Minja,
"muache tu, sijasema umfungue " Mkuu wa polisi aliongea na kumfanya yule kijana arudishe funguo mfukoni,
"nipishe kidogo, kuna maswali nataka nimuhoji Minja" Mkuu wa polisi aliongea na kumfanya yule Askari apige saluti na kutoka nje ya ofisi ya mkuu wa polisi, ndani akabaki Sajenti Minja na mkuu wa polisi.
Mkuu wa polisi akamuangalia Sajenti Minja kwa muda, kisha akajikooza kusafisha koo,
"kwanini umemtorosha yule mwanamke?" Mkuu wa polisi aliuliza na kumtazama Sajenti Minja,
"sijamtorosha" Sajenti Minja alijibu kwa utulivu,
"acha upumbavu Minja, umeondoka nyumbani kwa Edward Sambo ukiwa wewe na mtuhumiwa tu, hukutaka kumpakia Askari mwenzako hata mmoja, alafu unafika peke yako kituoni na kusema mtuhumiwa ametoroka, ametorokaje?, yaani atoroke mikononi kwako? hapana, sio rahisi hivyo, ni lazima utakuwa umemtorosha tu" Mkuu wa polisi aliongea na kumfanya Sajenti Minja aangalie chini huku akitafakari.
"sijamtorosha mtuhumiwa" Sajenti Minja alijibu tena jibu lile lile,
"inasikitisha sana, Yaani bado unaendelea na msimamo wako ule ule?" Mkuu wa polisi aliuliza,
"naomba unirudishe selo, maana kati sitobadili jibu langu, kwa sababu ndilo jibu la ukweli, na nyinyi hamuwezi kubadili msimamo wenu, kwa kuwa hamniamini tena" Sajenti Minja aliongea na kumuangalia mkuu wake,
"kabla sijakurudisha selo, ningependa kukufahamisha kuwa, hiki kitendo cha kipuuzi ulichokifanya cha kumtorosha yule mwanamke, kinaweza kupelekea mimi kufukuzwa kazi, pia kinaweza kupelekea wewe kufungwa na kukosa kazi" Mkuu wa polisi aliongea kwa uchungu,
"kama nitapoteza kazi na kufungwa kwa ajili ya ukweli wangu, ni sawa tu, ila siwezi kubadili kauli yangu" Sajenti Minja aliongea na kumfanya mkuu wake apige ngumi kwa hasira juu ya meza,
"afandee" Mkuu wa polisi aliita kwa sauti kubwa,
"naam afande" Askari aliyemleta Sajenti Minja aliitikia nje ya mlango huku akiingia ndani ya ofisi ya mkuu wa polisi,
"mrudishe selo huyu" Mkuu wa polisi aliongea na kisha yule Askari akamuinua Sajenti Minja na kumpeleka selo, Sajenti Minja akaingia selo na kwenda kukaa katika chumba kimoja kilichokuwa na harufu kali, kilikuwa jirani na choo, alikuwa akitafakari nini hatma yake, hasira ziliongezeka zaidi kila alipomfikiria BQ,
"nife mimi afe yeye, labda nisitoke humu" Sajenti Minja aliongea huku akiilalia mikono yake ambaye aliigemeza katika magoti, aliamua kulala huku akiwa amekaa.
Wakati Sajenti Minja akiwa katika hali hiyo, mkuu wa polisi yeye bado alikuwa na mawazo mengi, ikiwemo atazizuia vipi zile habari za Sajenti Minja kumtorosha mtuhumiwa zisifike kwa Rais, je zikifika yeye mkuu wa polisi kazi ndio itakuwa basi tena? au atashushwa cheo na kupelekwa mkoa mwingine?
Hayo ni baadhi ya maswali ambayo mkuu wa polisi alikuwa anajiuliza. Akajikuna kidevu, akakumbuka kuwa kati ya waandishi wa habari waliokuwepo pale usiku huu waliokuwa wakimsubiri Sajenti Minja na mtuhumiwa, alikuwepo muandishi wa habari mmoja maarufu sana wa moja kati ya vyombo vya habari vinavyoaminika sana nchini. Mkuu wa polisi akapanga kumtumia huyo muandishi wa habari, alichopanga ni kutoa hata rushwa ili mradi tu gazeti litalotoka siku inayofuata kutoa habari ambayo haitomchafua Sajenti Minja, alijua endapo Sajenti Minja angechafuliwa tu, wa kwanza kuwajibika atakuwa yeye mwenyewe mkuu wa polisi.
Mkuu wa polisi akawa anapeleka mkono wake ili aichukue simu yake mezani na kumpigia huyo muandishi wa habari, ila kabla mkono wake haujaishika simu, simu ilianza kuita, mkuu wa polisi akarusha mkono kwa mshtuko baada ya kuona jina la mpigaji, alikuwa ni Rais, mkuu wa polisi akahisi hofu kuu moyoni, jasho likaanza kumtoka ilihali ndani Kuna kiyoyozi cha kutosha.
Akaipokea ile simu kwa mashaka,
"ndio mkuu" Mkuu wa polisi aliongea mara baada ya kupokea simu,
"ulisema jina la kijana wako uliyempa kazi ya kuifuatilia hii kesi ya yule mwanamke muuaji, anaitwa Sajenti Minja?" Rais aliuliza kupitia simu,
"ndio mkuu" Mkuu wa polisi alijibu huku amepiga saluti, utadhani anayeongea nae katoka simu anamuona,
"huyo kijana wako imekuwaje tena amemtorosha muarifu?" Rais aliuliza na kusubiri jibu kutoka kwa mkuu wa polisi,
"hata mimi nimeshindwa kuelewa, ila huyu kijana tumemuweka selo" Mkuu wa polisi aliongea huku akitetemeka,
"huyo kijana namuhitaji hapa ikulu" Rais aliongea,
"sawa mkuu, namleta sasa hivi" Mkuu wa polisi aliongea,
"hapana, sihitaji umlete, nitatuma mtu aje amchukue" Rais aliongea,
"sawa mkuu" Mkuu wa polisi alijibu,
"wewe bado nakujadili, ila kaa ukijua umekalia kuti kavu" Rais aliongea,
"ila mheshimiwa, mimi sija..." Mkuu wa polisi alitaka kujitetea, ila simu ikakatwa, mkuu wa polisi akabaki akiitazama simu tu kwa hasira,
"nimekalia kuti kavu, kuti kavu?" Mkuu wa polisi alijiuliza huku akiangalia kiti alichokalia, kisha akainuka na kuzunguka zunguka mule ofisini kwake, akarudi akakaa, alimlaani sana Sajenti Minja kwa kumuharibia kazi, zaidi mkuu wa polisi akajuta kwa kumuamini Sajenti Minja na kumpa kazi ya kumtafuta mtuhumiwa.
Kufikia hapo alifuata wazo lake la kumpigia muandishi wa habari, maana tayari Rais alishapata taarifa ya Sajenti Minja kumtorosha mtuhumiwa.
**************
Asubuhi ya leo Rais alikuwa anajiandaa kwenda kuongea na waandishi wa habari, alisimama mbele ya kioo huku msichana mmoja akimpaka vipodozi usoni, na pembeni alikuwepo Ray Charles akifuatilia kila hatua.
Baada ya muda mchache maandalizi yalikuwa yameshakamilika, Rais akavaa koti lake la suti,
"wewe utanisubiri hapa" Rais alimwambia Ray Charles aliyekuwa amesimama,
"sawa" Ray Charles alijibu kisha Rais akatoka nje ya ofisi na yule msichana, wakawa wanaelekea katika chumba cha mikutano.
Rais alitembea mpaka katika mlango wa kuingilia, alimkuta bodyguard wake akimsubiri, wakaongozana mpaka katika chumba cha mikutano.
Rais alipoingia ndani ya chumba cha mikutano, watu wote wakasimama, Rais akaenda moja kwa moja katika sehemu ya kutolea hutuba na kusimama, ukapigwa wimbo wa Taifa.
Baada ya wimbo wa Taifa kuisha, Rais aliwasalimia wageni waalikwa, kisha akaendelea,
"Leo mnaweza kushangaaa na kuulizana vipi, mbona ametuita ikulu, kuna nini?, kifupi hakuna kitu kigeni sana msichokijua ambacho nitakieleza hapa.
Leo nimekuja na mambo mawili tu, kwa kuanza ningependa kuanza na jeshi letu la polisi. Jeshi letu la polisi limeoza, limeoza kabisa, hasa hasa hapa katika makao makuu ya polisi, inashangaza sana kuona mtu anaua viongozi wa serikali, alafu huyo mtu yupo hapa hapa mkoani na hakamatwi, ni upuuzi uliokithiri, au jeshi la polisi linashirikiana na waarifu? Sio polisi wote, ila Kuna baadhi wenye mamlaka watakuwa wanashirikiana na waarifu, yaliyotokea jana si mmeyasikia? Kijana mdogo tu wa polisi, mwenye cheo cha usajenti, ameenda katika nyumba ya mtu na akamkuta mtuhumiwa yule mwanamke muuaji, akamkamata vizuri tu, ila akataka kuondoka na mtuhumiwa akiwa yeye peke yake, akawatoa wenzake ndani ya gari, kwa kuwa wenzake hawana vyeo, wakakubali amri ya Sajenti wao. Sasa cha kushangaza huyo Sajenti akafika kituoni bila mtuhumiwa" Rais aliongea na kucheka,
"sio nacheka labda nafurahi, hapana, hii inasikitisha sana, yaani Sajenti wa polisi unashirikiana na mtuhumiwa? Huyo Sajenti amemtorosha mtuhumiwa, watu wakubwa na vyeo vyao walikuwa wanamsubiri Sajenti anampeleka mtuhumiwa, Sajenti akashuka peke yake, upumbavu wa kimataifa huu, yaani mtu anashuka kwa kujiamini na kusema mtuhumiwa ametoroka? Wakubwa zake wakamuweka ndani, ila sidhani kama kumuweka ndani inatosha, ni lazima achukuliwe hatua zaidi, maana huyo ni muhasi, hatufai, ni lazima awajibike kwa matendo yake ya kisaliti" Rais aliongea na kunywa maji kidogo, kisha akaendelea,
"jeshi la polisi nitalipa nafasi nyingine ya kurekebisha makosa yake, na wizara husika, yaani wizara ya ulinzi, nayo lazima ihusike na hii kashfa ya jeshi la polisi, kwa kuwa jeshi la polisi liko chini ya wizara, kwa hiyo basi, endapo endapo jeshi la polisi litashindwa kufanya kazi yake tena, nitaifumua wizara ya ulinzi mpaka jeshi lote la polisi makao makuu.
Hilo la kwanza nimemaliza. La pili ni kuhusu wizara yetu ya katiba na sheria, haina waziri kwa muda mrefu, nilikuwa najaribu kumtafuta mtu ambaye ataweza kuendana na wizara hiyo. Na nimeshampata, kwa leo nitampa ubunge wa kuteuliwa, naomba bwana Said Tambala asimame" Rais aliongea na kisha akasimama yule bwana waliyekuwa nae ikulu siku chache zilizopita,
"huyu bwana kuanzia sasa ni mbunge, ataenda kuapishwa bungeni, kisha nitampa uwaziri.
Nataka watu waende na kasi ninayoitaka mimi, sitaki kiongozi mzembe kabisa, viongozi wazembe mbadilike, maana fagio ninalokuja nalo sio la kawaida.
Sina mengi zaidi kwa leo, ni hayo tu" Rais alimaliza na kisha watu wakampigia makofi, Rais akatoka sehemu ya kutolea hutuba, na kwenda kuwapa mkono baadhi ya wageni na kupiga nao picha, kwa maana hiyo mkutano ulikuwa umemalizika rasmi.
*************
BQ hali ya kizunguzungu iliyomuanza siku chache zilizopita ilikuwa bado inamsumbua, ilizidi zaidi kiasi kwamba kwa siku alikuwa anazimia zaidi ya mara moja, hiyo ilikuwa ni hatari sana kwa ajili ya usalama wake.
Asubuhi ya leo aliamua kuingia katika maduka ya madawa kuitafuta dawa ambayo alitakiwa aitumie kwa muda huku akisubiri dawa nyingine kutoka urusi.
Asubuhi hiyo Askari walikuwa wamezagaa barabarani mara baada ya hutuba ya Rais, waliweka msako mkali ndani ya jiji, ila BQ alivaa Dela refu na miwani mipana, kichwani alifunga kiremba cha ki-nigeria, alibadilika muonekano, maana alipishana na Askari kadhaa na hawajamtilia shaka.
BQ akaingia katika duka kubwa la madawa ya binadamu, akaulizia dawa anayoitaka, akaambiwa ipo, akatajiwa na kiasi cha pesa, akatoa.
Wakati muhudumu akizitoa dawa katika shelves na kuziweka katika bahasha ndogo nyeupe, BQ alianza kuhisi kizunguzungu, kikazidi na akaanguka chini vibaya, akapoteza fahamu, wahudumu wa mule na wateja wakapata taharuki, mteja mmoja akatoka mbio kwenda nje kusogeza gari yake, Ile kasi aliyotoka nayo mteja ndio iliwashtua polisi wachache waliopo maeneo yale, polisi wawili wakaingia ndani ya lile duka la madawa, wakakuta baadhi ya watu wamemzunguka mwanamke akiwa amelala,
"Kuna nini?" Askari moja aliuliza huku akimsogelea yule mwanamke,
"ameanguka tu ghafla" Mhudumu mmoja alijibu, na kumfanya yule Askari asogee karibu zaidi ya BQ ambaye kiremba chake kilimvuka baada ya kuanguka, yule Askari akashtuka, akamuita mwenzie kwa ishara, yule Askari mwingine akasogea, kisha wakijadiliana kwa muda, mmoja kati yao akatoa simu na kuangalia picha kadhaa,
"ndio yeye" Askari mmoja aliongea, kisha wakapiga simu, baada ya dakika tano gari ya polisi ilisimama nje ya duka lile, wakambeba BQ na kutoka nae mpaka katika gari na kumlaza katika bodi ya gari, kisha mkono wake mmoja wakaufunga pingu na upande mwingine wa pingu wakaufunga katika chuma ya gari, gari ikaondolewa kwa kasi,
"tumefanikiwa kupata mkuu" Askari mmoja aliongea katika simu huky akitabasamu.
Ndani ya duka la madawa waliwaacha watu wakishangaa lile tukio huku wasijue kinachoendelea....
**********ITAENDELEA***********
the Legend☆
MTUNZI : ALEX KILEO
SEHEMU YA ISHIRINI NANE.
________________
ENDELEA....
_________________
Sajenti Minja akapelekwa selo na kuwaacha wakubwa zake wakijadiliana, wote walionekana kutopendezwa na kitendo cha Sajenti Minja, na wote waliamini Sajenti Minja amemtorosha yule mwanamke, ila hawakujua sababu kwanini Sajenti Minja amtoroshe yule mwanamke?.
Baada ya majadiliano ya nusu saa, wale polisi walitawanyika, kila mtu akaelekea panapo muhusu, mkuu wa polisi alirudi ofisini kwake, hukutaka kuongea hata na waandishi wa habari, kichwa chake kilishavurugika kabisa, hakikukaa sawa kwa muda huo.
Mkuu wa polisi akaingia ndani ya ofisi yake, kisha akavua kofia na kuiweka juu ya meza, akaanza kufikiri huku akizunguka mule ndani ya ofisi yake, alifanya hivyo kama dakika kumi, kisha akachukua simu na kupiga namba anayoijua yeye,
"bado upo zamu?" Mkuu wa polisi aliuliza kwa mamlaka,.
"ndio mkuu" Sauti ya upande wa pili ilijibu kwa utii,
"mlete Sajenti Minja ofisini kwangu, sasa hivi" Mkuu wa polisi aliongea kisha akakata simu, alafu akavuta kiti na kukaa, kisha akanywa maji yaliyokuwa katika chupa, na kisha akavaa kofia yake, akatulia akimsubiri Sajenti Minja.
Baada ya dakika mbili mlango wa ofisi yake uligongwa, akaingia Askari mmoja aliyemtanguliza Sajenti Minja mbele huku mikononi akiwa na pingu,
"kwa hiyo hata alipokuwa selo hamkufungua pingu?" Mkuu wa polisi aliuliza,
"ndio mkuu" Askari yule alijibu,
"na nyie mkaona sawa tu mtu kuwa na pingu ndani ya selo?" Mkuu wa polisi akaendelea kuongea na kumfanya yule Askari aliyemleta Sajenti Minja atoe funguo mfukoni ili amfungue Sajenti Minja,
"muache tu, sijasema umfungue " Mkuu wa polisi aliongea na kumfanya yule kijana arudishe funguo mfukoni,
"nipishe kidogo, kuna maswali nataka nimuhoji Minja" Mkuu wa polisi aliongea na kumfanya yule Askari apige saluti na kutoka nje ya ofisi ya mkuu wa polisi, ndani akabaki Sajenti Minja na mkuu wa polisi.
Mkuu wa polisi akamuangalia Sajenti Minja kwa muda, kisha akajikooza kusafisha koo,
"kwanini umemtorosha yule mwanamke?" Mkuu wa polisi aliuliza na kumtazama Sajenti Minja,
"sijamtorosha" Sajenti Minja alijibu kwa utulivu,
"acha upumbavu Minja, umeondoka nyumbani kwa Edward Sambo ukiwa wewe na mtuhumiwa tu, hukutaka kumpakia Askari mwenzako hata mmoja, alafu unafika peke yako kituoni na kusema mtuhumiwa ametoroka, ametorokaje?, yaani atoroke mikononi kwako? hapana, sio rahisi hivyo, ni lazima utakuwa umemtorosha tu" Mkuu wa polisi aliongea na kumfanya Sajenti Minja aangalie chini huku akitafakari.
"sijamtorosha mtuhumiwa" Sajenti Minja alijibu tena jibu lile lile,
"inasikitisha sana, Yaani bado unaendelea na msimamo wako ule ule?" Mkuu wa polisi aliuliza,
"naomba unirudishe selo, maana kati sitobadili jibu langu, kwa sababu ndilo jibu la ukweli, na nyinyi hamuwezi kubadili msimamo wenu, kwa kuwa hamniamini tena" Sajenti Minja aliongea na kumuangalia mkuu wake,
"kabla sijakurudisha selo, ningependa kukufahamisha kuwa, hiki kitendo cha kipuuzi ulichokifanya cha kumtorosha yule mwanamke, kinaweza kupelekea mimi kufukuzwa kazi, pia kinaweza kupelekea wewe kufungwa na kukosa kazi" Mkuu wa polisi aliongea kwa uchungu,
"kama nitapoteza kazi na kufungwa kwa ajili ya ukweli wangu, ni sawa tu, ila siwezi kubadili kauli yangu" Sajenti Minja aliongea na kumfanya mkuu wake apige ngumi kwa hasira juu ya meza,
"afandee" Mkuu wa polisi aliita kwa sauti kubwa,
"naam afande" Askari aliyemleta Sajenti Minja aliitikia nje ya mlango huku akiingia ndani ya ofisi ya mkuu wa polisi,
"mrudishe selo huyu" Mkuu wa polisi aliongea na kisha yule Askari akamuinua Sajenti Minja na kumpeleka selo, Sajenti Minja akaingia selo na kwenda kukaa katika chumba kimoja kilichokuwa na harufu kali, kilikuwa jirani na choo, alikuwa akitafakari nini hatma yake, hasira ziliongezeka zaidi kila alipomfikiria BQ,
"nife mimi afe yeye, labda nisitoke humu" Sajenti Minja aliongea huku akiilalia mikono yake ambaye aliigemeza katika magoti, aliamua kulala huku akiwa amekaa.
Wakati Sajenti Minja akiwa katika hali hiyo, mkuu wa polisi yeye bado alikuwa na mawazo mengi, ikiwemo atazizuia vipi zile habari za Sajenti Minja kumtorosha mtuhumiwa zisifike kwa Rais, je zikifika yeye mkuu wa polisi kazi ndio itakuwa basi tena? au atashushwa cheo na kupelekwa mkoa mwingine?
Hayo ni baadhi ya maswali ambayo mkuu wa polisi alikuwa anajiuliza. Akajikuna kidevu, akakumbuka kuwa kati ya waandishi wa habari waliokuwepo pale usiku huu waliokuwa wakimsubiri Sajenti Minja na mtuhumiwa, alikuwepo muandishi wa habari mmoja maarufu sana wa moja kati ya vyombo vya habari vinavyoaminika sana nchini. Mkuu wa polisi akapanga kumtumia huyo muandishi wa habari, alichopanga ni kutoa hata rushwa ili mradi tu gazeti litalotoka siku inayofuata kutoa habari ambayo haitomchafua Sajenti Minja, alijua endapo Sajenti Minja angechafuliwa tu, wa kwanza kuwajibika atakuwa yeye mwenyewe mkuu wa polisi.
Mkuu wa polisi akawa anapeleka mkono wake ili aichukue simu yake mezani na kumpigia huyo muandishi wa habari, ila kabla mkono wake haujaishika simu, simu ilianza kuita, mkuu wa polisi akarusha mkono kwa mshtuko baada ya kuona jina la mpigaji, alikuwa ni Rais, mkuu wa polisi akahisi hofu kuu moyoni, jasho likaanza kumtoka ilihali ndani Kuna kiyoyozi cha kutosha.
Akaipokea ile simu kwa mashaka,
"ndio mkuu" Mkuu wa polisi aliongea mara baada ya kupokea simu,
"ulisema jina la kijana wako uliyempa kazi ya kuifuatilia hii kesi ya yule mwanamke muuaji, anaitwa Sajenti Minja?" Rais aliuliza kupitia simu,
"ndio mkuu" Mkuu wa polisi alijibu huku amepiga saluti, utadhani anayeongea nae katoka simu anamuona,
"huyo kijana wako imekuwaje tena amemtorosha muarifu?" Rais aliuliza na kusubiri jibu kutoka kwa mkuu wa polisi,
"hata mimi nimeshindwa kuelewa, ila huyu kijana tumemuweka selo" Mkuu wa polisi aliongea huku akitetemeka,
"huyo kijana namuhitaji hapa ikulu" Rais aliongea,
"sawa mkuu, namleta sasa hivi" Mkuu wa polisi aliongea,
"hapana, sihitaji umlete, nitatuma mtu aje amchukue" Rais aliongea,
"sawa mkuu" Mkuu wa polisi alijibu,
"wewe bado nakujadili, ila kaa ukijua umekalia kuti kavu" Rais aliongea,
"ila mheshimiwa, mimi sija..." Mkuu wa polisi alitaka kujitetea, ila simu ikakatwa, mkuu wa polisi akabaki akiitazama simu tu kwa hasira,
"nimekalia kuti kavu, kuti kavu?" Mkuu wa polisi alijiuliza huku akiangalia kiti alichokalia, kisha akainuka na kuzunguka zunguka mule ofisini kwake, akarudi akakaa, alimlaani sana Sajenti Minja kwa kumuharibia kazi, zaidi mkuu wa polisi akajuta kwa kumuamini Sajenti Minja na kumpa kazi ya kumtafuta mtuhumiwa.
Kufikia hapo alifuata wazo lake la kumpigia muandishi wa habari, maana tayari Rais alishapata taarifa ya Sajenti Minja kumtorosha mtuhumiwa.
**************
Asubuhi ya leo Rais alikuwa anajiandaa kwenda kuongea na waandishi wa habari, alisimama mbele ya kioo huku msichana mmoja akimpaka vipodozi usoni, na pembeni alikuwepo Ray Charles akifuatilia kila hatua.
Baada ya muda mchache maandalizi yalikuwa yameshakamilika, Rais akavaa koti lake la suti,
"wewe utanisubiri hapa" Rais alimwambia Ray Charles aliyekuwa amesimama,
"sawa" Ray Charles alijibu kisha Rais akatoka nje ya ofisi na yule msichana, wakawa wanaelekea katika chumba cha mikutano.
Rais alitembea mpaka katika mlango wa kuingilia, alimkuta bodyguard wake akimsubiri, wakaongozana mpaka katika chumba cha mikutano.
Rais alipoingia ndani ya chumba cha mikutano, watu wote wakasimama, Rais akaenda moja kwa moja katika sehemu ya kutolea hutuba na kusimama, ukapigwa wimbo wa Taifa.
Baada ya wimbo wa Taifa kuisha, Rais aliwasalimia wageni waalikwa, kisha akaendelea,
"Leo mnaweza kushangaaa na kuulizana vipi, mbona ametuita ikulu, kuna nini?, kifupi hakuna kitu kigeni sana msichokijua ambacho nitakieleza hapa.
Leo nimekuja na mambo mawili tu, kwa kuanza ningependa kuanza na jeshi letu la polisi. Jeshi letu la polisi limeoza, limeoza kabisa, hasa hasa hapa katika makao makuu ya polisi, inashangaza sana kuona mtu anaua viongozi wa serikali, alafu huyo mtu yupo hapa hapa mkoani na hakamatwi, ni upuuzi uliokithiri, au jeshi la polisi linashirikiana na waarifu? Sio polisi wote, ila Kuna baadhi wenye mamlaka watakuwa wanashirikiana na waarifu, yaliyotokea jana si mmeyasikia? Kijana mdogo tu wa polisi, mwenye cheo cha usajenti, ameenda katika nyumba ya mtu na akamkuta mtuhumiwa yule mwanamke muuaji, akamkamata vizuri tu, ila akataka kuondoka na mtuhumiwa akiwa yeye peke yake, akawatoa wenzake ndani ya gari, kwa kuwa wenzake hawana vyeo, wakakubali amri ya Sajenti wao. Sasa cha kushangaza huyo Sajenti akafika kituoni bila mtuhumiwa" Rais aliongea na kucheka,
"sio nacheka labda nafurahi, hapana, hii inasikitisha sana, yaani Sajenti wa polisi unashirikiana na mtuhumiwa? Huyo Sajenti amemtorosha mtuhumiwa, watu wakubwa na vyeo vyao walikuwa wanamsubiri Sajenti anampeleka mtuhumiwa, Sajenti akashuka peke yake, upumbavu wa kimataifa huu, yaani mtu anashuka kwa kujiamini na kusema mtuhumiwa ametoroka? Wakubwa zake wakamuweka ndani, ila sidhani kama kumuweka ndani inatosha, ni lazima achukuliwe hatua zaidi, maana huyo ni muhasi, hatufai, ni lazima awajibike kwa matendo yake ya kisaliti" Rais aliongea na kunywa maji kidogo, kisha akaendelea,
"jeshi la polisi nitalipa nafasi nyingine ya kurekebisha makosa yake, na wizara husika, yaani wizara ya ulinzi, nayo lazima ihusike na hii kashfa ya jeshi la polisi, kwa kuwa jeshi la polisi liko chini ya wizara, kwa hiyo basi, endapo endapo jeshi la polisi litashindwa kufanya kazi yake tena, nitaifumua wizara ya ulinzi mpaka jeshi lote la polisi makao makuu.
Hilo la kwanza nimemaliza. La pili ni kuhusu wizara yetu ya katiba na sheria, haina waziri kwa muda mrefu, nilikuwa najaribu kumtafuta mtu ambaye ataweza kuendana na wizara hiyo. Na nimeshampata, kwa leo nitampa ubunge wa kuteuliwa, naomba bwana Said Tambala asimame" Rais aliongea na kisha akasimama yule bwana waliyekuwa nae ikulu siku chache zilizopita,
"huyu bwana kuanzia sasa ni mbunge, ataenda kuapishwa bungeni, kisha nitampa uwaziri.
Nataka watu waende na kasi ninayoitaka mimi, sitaki kiongozi mzembe kabisa, viongozi wazembe mbadilike, maana fagio ninalokuja nalo sio la kawaida.
Sina mengi zaidi kwa leo, ni hayo tu" Rais alimaliza na kisha watu wakampigia makofi, Rais akatoka sehemu ya kutolea hutuba, na kwenda kuwapa mkono baadhi ya wageni na kupiga nao picha, kwa maana hiyo mkutano ulikuwa umemalizika rasmi.
*************
BQ hali ya kizunguzungu iliyomuanza siku chache zilizopita ilikuwa bado inamsumbua, ilizidi zaidi kiasi kwamba kwa siku alikuwa anazimia zaidi ya mara moja, hiyo ilikuwa ni hatari sana kwa ajili ya usalama wake.
Asubuhi ya leo aliamua kuingia katika maduka ya madawa kuitafuta dawa ambayo alitakiwa aitumie kwa muda huku akisubiri dawa nyingine kutoka urusi.
Asubuhi hiyo Askari walikuwa wamezagaa barabarani mara baada ya hutuba ya Rais, waliweka msako mkali ndani ya jiji, ila BQ alivaa Dela refu na miwani mipana, kichwani alifunga kiremba cha ki-nigeria, alibadilika muonekano, maana alipishana na Askari kadhaa na hawajamtilia shaka.
BQ akaingia katika duka kubwa la madawa ya binadamu, akaulizia dawa anayoitaka, akaambiwa ipo, akatajiwa na kiasi cha pesa, akatoa.
Wakati muhudumu akizitoa dawa katika shelves na kuziweka katika bahasha ndogo nyeupe, BQ alianza kuhisi kizunguzungu, kikazidi na akaanguka chini vibaya, akapoteza fahamu, wahudumu wa mule na wateja wakapata taharuki, mteja mmoja akatoka mbio kwenda nje kusogeza gari yake, Ile kasi aliyotoka nayo mteja ndio iliwashtua polisi wachache waliopo maeneo yale, polisi wawili wakaingia ndani ya lile duka la madawa, wakakuta baadhi ya watu wamemzunguka mwanamke akiwa amelala,
"Kuna nini?" Askari moja aliuliza huku akimsogelea yule mwanamke,
"ameanguka tu ghafla" Mhudumu mmoja alijibu, na kumfanya yule Askari asogee karibu zaidi ya BQ ambaye kiremba chake kilimvuka baada ya kuanguka, yule Askari akashtuka, akamuita mwenzie kwa ishara, yule Askari mwingine akasogea, kisha wakijadiliana kwa muda, mmoja kati yao akatoa simu na kuangalia picha kadhaa,
"ndio yeye" Askari mmoja aliongea, kisha wakapiga simu, baada ya dakika tano gari ya polisi ilisimama nje ya duka lile, wakambeba BQ na kutoka nae mpaka katika gari na kumlaza katika bodi ya gari, kisha mkono wake mmoja wakaufunga pingu na upande mwingine wa pingu wakaufunga katika chuma ya gari, gari ikaondolewa kwa kasi,
"tumefanikiwa kupata mkuu" Askari mmoja aliongea katika simu huky akitabasamu.
Ndani ya duka la madawa waliwaacha watu wakishangaa lile tukio huku wasijue kinachoendelea....
**********ITAENDELEA***********
the Legend☆
