Riwaya: Mkono Wa Chuma

Riwaya: Mkono Wa Chuma

RIWAYA : MKONO WA CHUMA

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA ISHIRINI NANE.

________________
ENDELEA....
_________________

Sajenti Minja akapelekwa selo na kuwaacha wakubwa zake wakijadiliana, wote walionekana kutopendezwa na kitendo cha Sajenti Minja, na wote waliamini Sajenti Minja amemtorosha yule mwanamke, ila hawakujua sababu kwanini Sajenti Minja amtoroshe yule mwanamke?.

Baada ya majadiliano ya nusu saa, wale polisi walitawanyika, kila mtu akaelekea panapo muhusu, mkuu wa polisi alirudi ofisini kwake, hukutaka kuongea hata na waandishi wa habari, kichwa chake kilishavurugika kabisa, hakikukaa sawa kwa muda huo.

Mkuu wa polisi akaingia ndani ya ofisi yake, kisha akavua kofia na kuiweka juu ya meza, akaanza kufikiri huku akizunguka mule ndani ya ofisi yake, alifanya hivyo kama dakika kumi, kisha akachukua simu na kupiga namba anayoijua yeye,

"bado upo zamu?" Mkuu wa polisi aliuliza kwa mamlaka,.

"ndio mkuu" Sauti ya upande wa pili ilijibu kwa utii,

"mlete Sajenti Minja ofisini kwangu, sasa hivi" Mkuu wa polisi aliongea kisha akakata simu, alafu akavuta kiti na kukaa, kisha akanywa maji yaliyokuwa katika chupa, na kisha akavaa kofia yake, akatulia akimsubiri Sajenti Minja.

Baada ya dakika mbili mlango wa ofisi yake uligongwa, akaingia Askari mmoja aliyemtanguliza Sajenti Minja mbele huku mikononi akiwa na pingu,

"kwa hiyo hata alipokuwa selo hamkufungua pingu?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"ndio mkuu" Askari yule alijibu,

"na nyie mkaona sawa tu mtu kuwa na pingu ndani ya selo?" Mkuu wa polisi akaendelea kuongea na kumfanya yule Askari aliyemleta Sajenti Minja atoe funguo mfukoni ili amfungue Sajenti Minja,

"muache tu, sijasema umfungue " Mkuu wa polisi aliongea na kumfanya yule kijana arudishe funguo mfukoni,

"nipishe kidogo, kuna maswali nataka nimuhoji Minja" Mkuu wa polisi aliongea na kumfanya yule Askari apige saluti na kutoka nje ya ofisi ya mkuu wa polisi, ndani akabaki Sajenti Minja na mkuu wa polisi.

Mkuu wa polisi akamuangalia Sajenti Minja kwa muda, kisha akajikooza kusafisha koo,

"kwanini umemtorosha yule mwanamke?" Mkuu wa polisi aliuliza na kumtazama Sajenti Minja,

"sijamtorosha" Sajenti Minja alijibu kwa utulivu,

"acha upumbavu Minja, umeondoka nyumbani kwa Edward Sambo ukiwa wewe na mtuhumiwa tu, hukutaka kumpakia Askari mwenzako hata mmoja, alafu unafika peke yako kituoni na kusema mtuhumiwa ametoroka, ametorokaje?, yaani atoroke mikononi kwako? hapana, sio rahisi hivyo, ni lazima utakuwa umemtorosha tu" Mkuu wa polisi aliongea na kumfanya Sajenti Minja aangalie chini huku akitafakari.

"sijamtorosha mtuhumiwa" Sajenti Minja alijibu tena jibu lile lile,

"inasikitisha sana, Yaani bado unaendelea na msimamo wako ule ule?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"naomba unirudishe selo, maana kati sitobadili jibu langu, kwa sababu ndilo jibu la ukweli, na nyinyi hamuwezi kubadili msimamo wenu, kwa kuwa hamniamini tena" Sajenti Minja aliongea na kumuangalia mkuu wake,

"kabla sijakurudisha selo, ningependa kukufahamisha kuwa, hiki kitendo cha kipuuzi ulichokifanya cha kumtorosha yule mwanamke, kinaweza kupelekea mimi kufukuzwa kazi, pia kinaweza kupelekea wewe kufungwa na kukosa kazi" Mkuu wa polisi aliongea kwa uchungu,

"kama nitapoteza kazi na kufungwa kwa ajili ya ukweli wangu, ni sawa tu, ila siwezi kubadili kauli yangu" Sajenti Minja aliongea na kumfanya mkuu wake apige ngumi kwa hasira juu ya meza,

"afandee" Mkuu wa polisi aliita kwa sauti kubwa,

"naam afande" Askari aliyemleta Sajenti Minja aliitikia nje ya mlango huku akiingia ndani ya ofisi ya mkuu wa polisi,

"mrudishe selo huyu" Mkuu wa polisi aliongea na kisha yule Askari akamuinua Sajenti Minja na kumpeleka selo, Sajenti Minja akaingia selo na kwenda kukaa katika chumba kimoja kilichokuwa na harufu kali, kilikuwa jirani na choo, alikuwa akitafakari nini hatma yake, hasira ziliongezeka zaidi kila alipomfikiria BQ,

"nife mimi afe yeye, labda nisitoke humu" Sajenti Minja aliongea huku akiilalia mikono yake ambaye aliigemeza katika magoti, aliamua kulala huku akiwa amekaa.

Wakati Sajenti Minja akiwa katika hali hiyo, mkuu wa polisi yeye bado alikuwa na mawazo mengi, ikiwemo atazizuia vipi zile habari za Sajenti Minja kumtorosha mtuhumiwa zisifike kwa Rais, je zikifika yeye mkuu wa polisi kazi ndio itakuwa basi tena? au atashushwa cheo na kupelekwa mkoa mwingine?
Hayo ni baadhi ya maswali ambayo mkuu wa polisi alikuwa anajiuliza. Akajikuna kidevu, akakumbuka kuwa kati ya waandishi wa habari waliokuwepo pale usiku huu waliokuwa wakimsubiri Sajenti Minja na mtuhumiwa, alikuwepo muandishi wa habari mmoja maarufu sana wa moja kati ya vyombo vya habari vinavyoaminika sana nchini. Mkuu wa polisi akapanga kumtumia huyo muandishi wa habari, alichopanga ni kutoa hata rushwa ili mradi tu gazeti litalotoka siku inayofuata kutoa habari ambayo haitomchafua Sajenti Minja, alijua endapo Sajenti Minja angechafuliwa tu, wa kwanza kuwajibika atakuwa yeye mwenyewe mkuu wa polisi.

Mkuu wa polisi akawa anapeleka mkono wake ili aichukue simu yake mezani na kumpigia huyo muandishi wa habari, ila kabla mkono wake haujaishika simu, simu ilianza kuita, mkuu wa polisi akarusha mkono kwa mshtuko baada ya kuona jina la mpigaji, alikuwa ni Rais, mkuu wa polisi akahisi hofu kuu moyoni, jasho likaanza kumtoka ilihali ndani Kuna kiyoyozi cha kutosha.

Akaipokea ile simu kwa mashaka,

"ndio mkuu" Mkuu wa polisi aliongea mara baada ya kupokea simu,

"ulisema jina la kijana wako uliyempa kazi ya kuifuatilia hii kesi ya yule mwanamke muuaji, anaitwa Sajenti Minja?" Rais aliuliza kupitia simu,

"ndio mkuu" Mkuu wa polisi alijibu huku amepiga saluti, utadhani anayeongea nae katoka simu anamuona,

"huyo kijana wako imekuwaje tena amemtorosha muarifu?" Rais aliuliza na kusubiri jibu kutoka kwa mkuu wa polisi,

"hata mimi nimeshindwa kuelewa, ila huyu kijana tumemuweka selo" Mkuu wa polisi aliongea huku akitetemeka,

"huyo kijana namuhitaji hapa ikulu" Rais aliongea,

"sawa mkuu, namleta sasa hivi" Mkuu wa polisi aliongea,

"hapana, sihitaji umlete, nitatuma mtu aje amchukue" Rais aliongea,

"sawa mkuu" Mkuu wa polisi alijibu,

"wewe bado nakujadili, ila kaa ukijua umekalia kuti kavu" Rais aliongea,

"ila mheshimiwa, mimi sija..." Mkuu wa polisi alitaka kujitetea, ila simu ikakatwa, mkuu wa polisi akabaki akiitazama simu tu kwa hasira,

"nimekalia kuti kavu, kuti kavu?" Mkuu wa polisi alijiuliza huku akiangalia kiti alichokalia, kisha akainuka na kuzunguka zunguka mule ofisini kwake, akarudi akakaa, alimlaani sana Sajenti Minja kwa kumuharibia kazi, zaidi mkuu wa polisi akajuta kwa kumuamini Sajenti Minja na kumpa kazi ya kumtafuta mtuhumiwa.

Kufikia hapo alifuata wazo lake la kumpigia muandishi wa habari, maana tayari Rais alishapata taarifa ya Sajenti Minja kumtorosha mtuhumiwa.

**************

Asubuhi ya leo Rais alikuwa anajiandaa kwenda kuongea na waandishi wa habari, alisimama mbele ya kioo huku msichana mmoja akimpaka vipodozi usoni, na pembeni alikuwepo Ray Charles akifuatilia kila hatua.

Baada ya muda mchache maandalizi yalikuwa yameshakamilika, Rais akavaa koti lake la suti,

"wewe utanisubiri hapa" Rais alimwambia Ray Charles aliyekuwa amesimama,

"sawa" Ray Charles alijibu kisha Rais akatoka nje ya ofisi na yule msichana, wakawa wanaelekea katika chumba cha mikutano.

Rais alitembea mpaka katika mlango wa kuingilia, alimkuta bodyguard wake akimsubiri, wakaongozana mpaka katika chumba cha mikutano.

Rais alipoingia ndani ya chumba cha mikutano, watu wote wakasimama, Rais akaenda moja kwa moja katika sehemu ya kutolea hutuba na kusimama, ukapigwa wimbo wa Taifa.

Baada ya wimbo wa Taifa kuisha, Rais aliwasalimia wageni waalikwa, kisha akaendelea,

"Leo mnaweza kushangaaa na kuulizana vipi, mbona ametuita ikulu, kuna nini?, kifupi hakuna kitu kigeni sana msichokijua ambacho nitakieleza hapa.

Leo nimekuja na mambo mawili tu, kwa kuanza ningependa kuanza na jeshi letu la polisi. Jeshi letu la polisi limeoza, limeoza kabisa, hasa hasa hapa katika makao makuu ya polisi, inashangaza sana kuona mtu anaua viongozi wa serikali, alafu huyo mtu yupo hapa hapa mkoani na hakamatwi, ni upuuzi uliokithiri, au jeshi la polisi linashirikiana na waarifu? Sio polisi wote, ila Kuna baadhi wenye mamlaka watakuwa wanashirikiana na waarifu, yaliyotokea jana si mmeyasikia? Kijana mdogo tu wa polisi, mwenye cheo cha usajenti, ameenda katika nyumba ya mtu na akamkuta mtuhumiwa yule mwanamke muuaji, akamkamata vizuri tu, ila akataka kuondoka na mtuhumiwa akiwa yeye peke yake, akawatoa wenzake ndani ya gari, kwa kuwa wenzake hawana vyeo, wakakubali amri ya Sajenti wao. Sasa cha kushangaza huyo Sajenti akafika kituoni bila mtuhumiwa" Rais aliongea na kucheka,

"sio nacheka labda nafurahi, hapana, hii inasikitisha sana, yaani Sajenti wa polisi unashirikiana na mtuhumiwa? Huyo Sajenti amemtorosha mtuhumiwa, watu wakubwa na vyeo vyao walikuwa wanamsubiri Sajenti anampeleka mtuhumiwa, Sajenti akashuka peke yake, upumbavu wa kimataifa huu, yaani mtu anashuka kwa kujiamini na kusema mtuhumiwa ametoroka? Wakubwa zake wakamuweka ndani, ila sidhani kama kumuweka ndani inatosha, ni lazima achukuliwe hatua zaidi, maana huyo ni muhasi, hatufai, ni lazima awajibike kwa matendo yake ya kisaliti" Rais aliongea na kunywa maji kidogo, kisha akaendelea,

"jeshi la polisi nitalipa nafasi nyingine ya kurekebisha makosa yake, na wizara husika, yaani wizara ya ulinzi, nayo lazima ihusike na hii kashfa ya jeshi la polisi, kwa kuwa jeshi la polisi liko chini ya wizara, kwa hiyo basi, endapo endapo jeshi la polisi litashindwa kufanya kazi yake tena, nitaifumua wizara ya ulinzi mpaka jeshi lote la polisi makao makuu.
Hilo la kwanza nimemaliza. La pili ni kuhusu wizara yetu ya katiba na sheria, haina waziri kwa muda mrefu, nilikuwa najaribu kumtafuta mtu ambaye ataweza kuendana na wizara hiyo. Na nimeshampata, kwa leo nitampa ubunge wa kuteuliwa, naomba bwana Said Tambala asimame" Rais aliongea na kisha akasimama yule bwana waliyekuwa nae ikulu siku chache zilizopita,

"huyu bwana kuanzia sasa ni mbunge, ataenda kuapishwa bungeni, kisha nitampa uwaziri.

Nataka watu waende na kasi ninayoitaka mimi, sitaki kiongozi mzembe kabisa, viongozi wazembe mbadilike, maana fagio ninalokuja nalo sio la kawaida.
Sina mengi zaidi kwa leo, ni hayo tu" Rais alimaliza na kisha watu wakampigia makofi, Rais akatoka sehemu ya kutolea hutuba, na kwenda kuwapa mkono baadhi ya wageni na kupiga nao picha, kwa maana hiyo mkutano ulikuwa umemalizika rasmi.

*************

BQ hali ya kizunguzungu iliyomuanza siku chache zilizopita ilikuwa bado inamsumbua, ilizidi zaidi kiasi kwamba kwa siku alikuwa anazimia zaidi ya mara moja, hiyo ilikuwa ni hatari sana kwa ajili ya usalama wake.

Asubuhi ya leo aliamua kuingia katika maduka ya madawa kuitafuta dawa ambayo alitakiwa aitumie kwa muda huku akisubiri dawa nyingine kutoka urusi.

Asubuhi hiyo Askari walikuwa wamezagaa barabarani mara baada ya hutuba ya Rais, waliweka msako mkali ndani ya jiji, ila BQ alivaa Dela refu na miwani mipana, kichwani alifunga kiremba cha ki-nigeria, alibadilika muonekano, maana alipishana na Askari kadhaa na hawajamtilia shaka.

BQ akaingia katika duka kubwa la madawa ya binadamu, akaulizia dawa anayoitaka, akaambiwa ipo, akatajiwa na kiasi cha pesa, akatoa.

Wakati muhudumu akizitoa dawa katika shelves na kuziweka katika bahasha ndogo nyeupe, BQ alianza kuhisi kizunguzungu, kikazidi na akaanguka chini vibaya, akapoteza fahamu, wahudumu wa mule na wateja wakapata taharuki, mteja mmoja akatoka mbio kwenda nje kusogeza gari yake, Ile kasi aliyotoka nayo mteja ndio iliwashtua polisi wachache waliopo maeneo yale, polisi wawili wakaingia ndani ya lile duka la madawa, wakakuta baadhi ya watu wamemzunguka mwanamke akiwa amelala,

"Kuna nini?" Askari moja aliuliza huku akimsogelea yule mwanamke,

"ameanguka tu ghafla" Mhudumu mmoja alijibu, na kumfanya yule Askari asogee karibu zaidi ya BQ ambaye kiremba chake kilimvuka baada ya kuanguka, yule Askari akashtuka, akamuita mwenzie kwa ishara, yule Askari mwingine akasogea, kisha wakijadiliana kwa muda, mmoja kati yao akatoa simu na kuangalia picha kadhaa,

"ndio yeye" Askari mmoja aliongea, kisha wakapiga simu, baada ya dakika tano gari ya polisi ilisimama nje ya duka lile, wakambeba BQ na kutoka nae mpaka katika gari na kumlaza katika bodi ya gari, kisha mkono wake mmoja wakaufunga pingu na upande mwingine wa pingu wakaufunga katika chuma ya gari, gari ikaondolewa kwa kasi,

"tumefanikiwa kupata mkuu" Askari mmoja aliongea katika simu huky akitabasamu.

Ndani ya duka la madawa waliwaacha watu wakishangaa lile tukio huku wasijue kinachoendelea....

**********ITAENDELEA***********

the Legend☆
 
Sio kweli mkuu, tangu nijiunge jf mtu pekee kuwahi kumuita dear ni Shunie tuu, kama yupo mwingine mtaje hapa. Truth be told Shunie alikua so kind to me tangu siku zangu za kwanza kabisa hapa jf

the Legend☆
Pole mkuu ...

ila humu yumo umemwita dear... usikatae... ...hatusutani maana si vibaya...kumwita mtu dear... ita tu .

ila kwa mimi huu ni utani tu mkuu.. wala usiwaze yaani!

Lakini aste aste!

Hujakaribishwa vizuri na shunie peke yake humu...... ... ..

Na unalalamika kama unalia kisa kuambiwa unamwita shunie dear ..ili akuonee huruma au aniwakie..?

Weye vipi ..?

Mkuu The legend asante sana kwa riwaya... ..zinatufariji sana ...unajali furaha ya wenzio na hivyo ndo inavyo takiwa mkuu!

AMRI mpya tulipewa.. ... "tupendane "

Siku njema dear..ake na shuu..




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole mkuu ...

ila humu yumo umemwita dear... usikatae... ...hatusutani maana si vibaya...kumwita mtu dear... ita tu .

ila kwa mimi huu ni utani tu mkuu.. wala usiwaze yaani!

Lakini aste aste!

Hujakaribishwa vizuri na shunie peke yake humu...... ... ..

Na unalalamika kama unalia kisa kuambiwa unamwita shunie dear ..ili akuonee huruma au aniwakie..?

Weye vipi ..?

Mkuu The legend asante sana kwa riwaya... ..zinatufariji sana ...unajali furaha ya wenzio na hivyo ndo inavyo takiwa mkuu!

AMRI mpya tulipewa.. ... "tupendane "

Siku njema dear..ake na shuu..




Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahaa, kwamba ndo umeamua kushusha gazeti kabisa. Najua ni utani tuu mkuu Mine eyes.
Anyways, asante kwa kushkuru. Tuko pamoja as always...

the Legend☆
 
RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA.

____________________
TEMBEA NAYO...
____________________
Polisi waliendelesha gari kwa kasi sana, breki ya kwanza ilikuwa kituoni, wakashuka na wengine wakaizunguka gari, kisha mkuu wa polisi akatoka ndani na kwenda kushuhudia hilo tukio ambalo hajategemea, yaani mtuhumiwa kukamatwa kirahisi rahisi hivyo, eti amedondoka tu dukani alafu akakamatwa? Hiyo kwa mkuu wa polisi ilikuwa si tu habari ya kushangaza, ilikuwa ni habari ya kushangaza zaidi.

Mkuu wa polisi akajongea mpaka katika gari na kumshangaa mwanamke yule aliyekuwa amelala huku akiwa hana fahamu, mkuu wa polisi akatabasamu, kisha akapanda juu ya gari na kwenda kumgusa kabisa, maana kwa matukio aliyoyafanya yule dada, mkuu wa polisi hakuwahi kabisa kuamini kama huyu dada ni mtu, alihisi huenda ni jini.

"alaaaaah, kumbe ni mlemavu, hana mkono mmoja?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akikanyaga kanyaga kile kipisi cha mkono wa BQ,

"Sasa ndio ameanguka na kufa, na nyie mlivyo waoga mpaka maiti mkaifunga pingu" Mkuu wa polisi aliongea kwa ujasiri huku akiwacheka vijana wake,

"hajafa huyo, amezimia tu" Askari mmoja alijibu na kumfanya mkuu wa polisi arudi nyuma ghafla mpaka akapamia ukingo wa bodi ya gari na kuanguka kutoka juu ya gari mpaka chini, ila vijana wake walimuwahi na kumdaka, akawa anahema juu juu,

"Sasa mbona hamjaniambia tangu mwanzo kama kazimia, mmeniacha mpaka nimemsogelea, angeamka je?" Mkuu wa polisi aliuliza kwa hasira,

"amefungwa pingu, hasingeweza kufanya kitu" Askari mmoja alijibu,

"amezimia muda gani mpaka sasa?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"imeshapita dakika kumi" Askari alijibu,

"mpelekeni hospital, hapa anaweza akatufia" Mkuu wa polisi aliongea na kufanya vijana wake waingie katika gari,

"muweke ulinzi wa kutosha, mpigeni pingu kila sehemu" Mkuu wa polisi aliongea huku akiingia ndani kifua mbele, aliona tayari amemfurahisha Rais, mtuhumiwa ameshampata.

Gari ya polisi iliyombeba BQ, uliondoka na mwendo ule ule iliyokuja nao, tena safari hii na king'ora walipiga na kufanya magari mengine yakae pembeni.

Gari ilifika hospitali na kusimama, kisha wakamshusha BQ na kuingia ndani huku wakiwa wamembeba wenyewe. Walielekea mpaka eneo la mapokezi,

"mpelekeni wodi ya watu maalum, huyu ni mtu maalum" Askari aliongea bila hata kuwapa salamu,

"mmepita kwa daktari lakini, au mmeamua tu kusema apelekwe wodi maalum?" Dada wa mapokezi aliuliza,

"unatuuliza hata huoni sisi ni wakina nani?" Askari aliuliza kwa hasira,

"kila sehemu kuna utaratibu wake, hapa sio polisi, ni hospitali" Dada wa mapokezi alijibu huku nae akionekana hapendi dharau,

"Dada huyu ni mtuhumiwa hatari, hatakiwi kuwekwa wodi iliyo na watu wengine, anatakiwa kuwa katika wodi maalum ambayo Askari watakuwa na nafasi ya kukaa na kumlinda" Askari mwingine aliongea kistaharabu,

"sawa kaka yangu, ila hapa Kuna utaratibu wake, huyo anatakiwa kupimwa kwanza, alafu ndio apelekwe katika hiyo wodi mnayoitaka" Dada wa mapokezi aliongea huku akiwa ameshusha jazba kidogo,

"sawa, utaratibu ukoje?" Askari yule aliuliza,

"nendeni pale chumba cha vipimo, achekiwe kisha atapelekwa wodini, huyu mwanamke inaonekana ana hali mbaya, hamuwezi kumpeleka wodini tu, je akienda kufa uko?" Dada wa mapokezi aliuliza,

"kwa hiyo tumpeleke chumba cha vipimo?" Yule Askari aliuliza,

"mpelekeni tu, ila mlitakiwa muanzie kwa daktari" Dada wa mapokezi aliongea na kufanya Askari wote waliokuja pale hospital waanze kuelekea chumba cha vipimo,

"aisee nyie, sasa mnaendaje wote?" Dada wa mapokezi aliuliza kwa mshangao,

"inabidi twende wote, maana huyu dada ni hatari sana" Askari alijibu,

"jamani si amefungwa pingu huyo? Askari msijitie aibu kwa kweli, yaani wanaume karibia saba mnamlinda mwanamke mmoja aliyefungwa pingu?" Dada wa mapokezi aliuliza huku akishindwa kuzuia tabasamu lake KS dharau. Ikawabidi polisi wajadiliane kwa muda, na mwisho wote wakabaki mapokezi, katika chumba cha vipimo akaingia yule Askari mbishi kuliko wote.

BQ alilazwa kitandani na kisha daktari akaingia katika chumba kile cha vipimo, kwa haraka haraka tu, daktari aliweza kuliona lile jeraha la BQ la kichwani, alijua huenda hilo ndilo lililofanya dada huyo apoteze fahamu, lakini pia daktari alitaka kumfanyia vipimo vingine, kama vya presha na kisukari.

Daktari akavaa mipira mikononi, kisha akachukua kifaa cha kupimia presha,

"naomba usubiri hapo nje" Dokta alimwambia yule Askari aliyekuwa ndani,

"siwezi kuondoka na kumuacha mtuhumiwa" Askari alijibu,

"kaka, ethics zangu haziruhusu nichukue vipimo vya mgonjwa huku mtu hasiye na undugu au uhusiano wowote na mgonjwa akiwa ndani" Daktari aliongea huku akiwa anamuangalia yule polisi,

"hata mimi maadili yangu ya kazi hayaruhusu kukaa mbali na mtuhumiwa" Askari alijibu na kukaa katika kiti kidogo ndani ya chumba kile,

"ni bora nimuache mgonjwa, kuliko kumfanyia vipimo huku nikiwa nimesimamiwa" Daktari aliongea huku akivua mipira mkononi,

"maadili yangu ya kazi yananiruhusu kukukamata wewe endapo utakuwa kinyume na amri za polisi. Mpime au na wewe tukutie pingu" Askari aliongea huku akisimama,

"hiyo haiwezekani" Daktari aliongea kwa jeuri akitoka nje, Askari akasimama na kumzuia, mkwaruzano ukaanza ndani, Askari wa nje wakasikia, mmoja akaingia katika kile chumba,

"Kuna nini kwani?" Askari aliyeingia aliuliza,

"huyo mwenzio anataka kunifundisha kazi, wakati mimi nafanya kutokana na maadili ya kazi yangu" Daktari aliongea,

"huyu anataka nitoke nje ili amfanyie vipimo mtuhumiwa, sasa mimi nimegoma, ndio anataka kuondoka" Askari mbishi aliongea,

"sawa, ebu tutoke tumuache daktari afanye kazi yake, hapa tukibishana na wajuzi wa mambo, hakuna kitachoendelea, tutapoteza muda tu" Yule Askari aliyeingia alimshawishi mwenzake ambaye alikubali kukaa nje na kisha daktari akaendelea na vipimo.

Baada ya dakika ishirini, daktari aliwaita wauguzi na kumuweka BQ katika kitanda cha matairi, wakaanza kumsukuma kuelekea katika wodi maalum.
Askari walikuwa wanatembea nyuma ya kitanda kile kinachosukumwa na wauguzi. Walifika katika wodi na kumuweka kitandani BQ, kisha Askari yule mbishi akamfunga BQ pingu ya mkono akaambatanisha na chuma ya kitanda, kisha akaona haitoshi, akamfunga pingu ya mguu na kuambatanisha na chuma ya kitanda, kisha akatabasamu,

"mhhm jamani!! " Muuguzi mmoja aliguna baada ya kuona hicho kitendo,

"maadili yenu ya kazi yaishie uko uko katika vyumba vya vipimo, huku ni maadili ya kipolisi tu" Askari mbishi aliongea kwa ukali na kufanya wauguzi watoke mule wodini bila kuongeza neno.

******************

Rais anaonekana amekaa katika kiti akitazama mlango mmoja wa chuma, nyuma yake walikuwa vijana waliobeba machela, na Rais mkononi alikuwa akiangalia simu sehemu ya saa, yaani alikuwa akihesabu dakika, na muda huo ilikuwa sekunde ya hamsini na nne, mlango ukafunguka, akatoka Ray Charles, hapo Rais akatabasamu huku akipiga makofi,

"safi sana, leo umetumia dakika chache sana" Rais aliongea huku akitabasamu, lakini Ray Charles hakujibu kitu,

"hey nyie, nendeni mkatoe uchafu" Rais aliongea huku akiwatizama wale vijana waliokuwa nyuma yake, wale vijana haraka wakaingia katika kile chumba chenye mlango wa chuma na kutoka na pandikizi la baba waliolibeba katika machela, alikuwa ameshakufa na kichwa chake kilionekana kupondeka pondeka vibaya sana, kama kimetwangwa na chuma.

"Leo umetumia sekunde hamsini na nne tu, inaonesha umeimarika sana, tofauti na yule mtu wa mwisho, yule mtu wa mwisho ulitumia dakika moja na sekunde nne, safi sana Ray" Rais aliongea huku akimpiga piga mgongoni Ray Charles ambaye alikuwa kimya.

Kipindi hicho wale vijana wengine walikuwa wakiuweka ule mwili wa yule mtu katika kiroba, kisha wakakifunga vizuri,

"huyo mtamtoa usiku na mtaenda kumtupa baharini, kuna mwenzake mwingine atakuja huku kufa usiku, mtawajumuisha wote. Haya nendeni nje" Rais aliongea huku akisimama katika kiti chake na yeye akaelekea nje.

Hiyo ni tabia ya Rais, uwa anawatafuta wale watu shupavu au wenye uwezo wa kupambana na kisha uwaleta wapambane na Ray Charles ili kumuamrisha zaidi katika uwezo wa kupigana, kwa maana Ray bado alikuwa mzito mzito, kwa hiyo hapo alikuwa anamjengea kasi Ray Charles.

Vijana wengi waliokuwa wakipotea mitaani bila taarifa, mara nyingi waliokotwa asubuhi katika bahari huku wakiwa ndani ya magunia, hakuna aliyejua nani anayeua vijana hao, hiyo ilikuwa ni siri ya wachache tu.

Rais alivyotoka nje, aliwakuta wale vijana wakiwa pale,

"jioni ndio muda wa kazi, mnatakiwa mvamie na mumtoroshe yule bwana, nataka mission ionekane ya kutoroshwa, ili baadae watu wasiangaike kumtafuta, wajue amejificha" Rais aliongea huku akiwatazama vijana kwa zamu, ambao walitikisa kichwa kuonesha kukubaliana na Rais,

"kila kitu kinaenda kwa mipango, afe yule kibaraka, kisha tutamtafuta mwenzake" Rais aliongea na kuondoka, nyuma yake alikuwa Ray Charles.

*************

Mida ya saa kumi jioni, Sajenti Minja bado alikuwa yupo selo, hii ilikuwa ni siku ya tatu mfululizo, hakujua hatma yake. Hapo aliambiwa siku inayofuata atapelekwa magereza, kwa maana kukaa selo mwisho ni siku tatu, kitu kingine kilichomshangaza Sajenti Minja ni kuwa hakuna hata mtu aliyeenda kumuona, Iwe Sajenti Minja au Edward Sambo, hakujua sababu.
Sajenti Minja akiwa amekaa hapo chini na baadae ya watu wengine, alisikia kelele zikitokea nje, mule ndani ya selo wote wakapata taharuki mara baada ya kusikia milio ya risasi, watu wote selo wakakimbilia vyumbani, maana walihisi hali ya hatari.
Mara wakasikia mlango wa selo ukifunguliwa, kisha wakaingia watu wawili waliokuwa na silaha, na nyuso zao walizifunika kwa vitambaa vyeusi, waliacha wazi eneo la macho tu.

Wale watu wakaanza kuingia kila chumba na kukagua, kuna mtu walikuwa wanamtafuta. Walipofika katika chumba alichokuwepo Sajenti Minja, mmoja kati ya watu wale akamsogelea na kumkumbatia,

"tumekuja kukuokoa, maana leo ilikuwa siku yako ya kufa, tumetumwa na jeshi la ulinzi" Yule mtu aliongea na kumrushia Sajenti Minja bunduki, Sajenti Minja akaidaka, kisha wakaanza kutoka huku wale watuhumiwa wengine wa selo wakishangaa tu.

Sajenti Minja alitoka na wale watu mpaka nje, ambapo alikuta Askari kadhaa wakiwa chini ya ulinzi, Sajenti Minja alienda na kuingia ndani ya gari, kisha wale watu wengine wakaingia, na gari ikaondoka kwa kasi.

Baada ya gari kupotea kabisa katika eneo la polisi, wale vijana wakatoa vitambaa usoni, hakuna hata mmoja Sajenti Minja aliyemjua, wote walikuwa watu wageni kwake.

Gari iliendelea kutembea bila mtu yoyote kuongea, ubaya hata Sajenti Minja hakujua wanapoelekea, kwa maana alikaa upande wa nyuma wa gari na hakukuwa na vioo.

Baada ya muda mfupi gari ikasimama,

"tunakuomba tukuzibe macho boss, kwa maana hutakiwi kujua upo wapi mpaka baadae" Kijana mmoja aliongea jua heshima mbele ya Sajenti Minja,

"kwa hiyo mtaniziba macho mpaka kesho?" Sajenti Minja aliuliza kwa wasiwasi,

"hapana, ukishaingia ndani tu unafunguliwa kitambaa, usiogope mkuu kwa maana mwili wote tutakucha huru, ila macho ndio tutaziba" Kijana aliongea huku akitabasamu, Sajenti Minja akakubali. Sajenti Minja akafungwa kitambaa na kutelemka, alitembea kwa muda mchache mpaka akahisi ameingizwa katika chumba, akasikia mlango ukifungwa, kisha akafunguliwa kitambaa usoni, akajikuta yupo ndani ya chumba kizuri sana.

"nenda kaoge na ukitoka uko utakuta chakula safi" Yule kijana aliongea, kisha Sajenti Minja akaingia bafuni kuoga huku akijiuliza kwanini jeshi limsaidie, au limejua hana hatia? na kwanini aletwe katika chumba hicho kizuri, kwanini wasingempeleka kambini?.

Sajenti Minja alijiuliza huku akioga. Baada ya dakika kumi, Sajenti Minja alitoka bafuni na kukuta amewekewa kitandani suruali ya mazoezi na mezani Kuna chakula cha kutosha, akakimbilia mezani na kuanza kula, maana hakuwa amekula muda mrefu sana. Alikifakamia chakula kwa haraka. Alitumia muda mchache tu, kisha akaenda mlangoni na kufunga mlango, akarudi mezani akanywa maji, kisha akajitupia kitandani, usingizi ukampitia, akalala kama amekufa, maana ni muda mrefu aliukosa usingizi.

Sauti ya mlango kugongwa ndio ilimuondoa usingizini, akakurupuka na kuangalia saa, ilikuwa saa mbili na nusu usiku, akakumbuka alilala kwenye saa kumi na moja hivi.

Mlango ukagongwa kwa nguvu zaidi, Sajenti Minja akainuka na kuvaa suruali ile mpya aliyoletewa, kisha akainuka na kwenda kufungua mlango, atakutana na binti,

"unaitwa" Binti aliongea bila salamu, Sajenti Minja hakujali, akatoka huku akimfuata huyo binti, walitembea huku Sajenti Minja akiyaangalia mazingira ya eneo hilo, walitembea na kukatiza eneo moja, kutoka kwenye jengo moja na kwenda jengo lingine, Sajenti Minja akashtuka, alilijua vizuri hilo eneo, lilikuwa eneo la ikulu, ila hakusema kitu, akaendelea kumfuata yule dada.

Safari yao iliishia katika eneo kama ukumbi, na mbele kulikuwa na chumba kingine chenye mlango wa chuma, Sajenti Minja akaambiwa asubiri hapo.

Baada ya muda akaingia Rais, Sajenti Minja akashangaa zaidi, akajiuliza anataka kupandishwa cheo au anataka kupewa ulinzi wa Rais?
Raia akasogea na kukaa katika kiti ambacho kiliangalia ule mlango wa chuma, kisha akaitoa saa yake, wala hukutaka kuongea sana,

"fungueni mlango" Rais aliongea kwa sauti kisha vijana wanne wakaingia pale, Sajenti Minja aliwatambua, ni wale walioenda kumtorosha kituo cha polisi.

Vijana wakaingia na kwenda kuufungua kidogo ule mlango,

"ingia pale, ukitoka tutaongea" Rais alimwambia Sajenti Minja, kisha Sajenti Minja akawa anaelekea katika ule mlango huku akijiuliza Kuna nini?

Aliufikia mlango na kuingia, akastaajabu mara baada ya kumkuta Ray Charles ndani, Sajenti Minja akataka kutoka, ila mlango ukajifunga,

"unatakiwa upambane ili ujiokoe, wewe ni msaliti, unashirikiana na yule mwanamke muuaji na ndio maana ulimtorosha" Sauti ya Rais ilisikika kupitia spika za mule ndani ya chumba. Sajenti Minja sasa ndio akajua maisha yake yako hatarini zaidi kuliko alivyokuwa selo.

Wakati Sajenti Minja akiwaza hayo, Ray Charles alikuwa akimsogelea taratibu huku kichwa chake kikiwa kinataka kumaliza kazi haraka ili akapate sifa kwa Rais, sekunde kumi zilikuwa zimeshakatika tangu Sajenti Minja aingie mule ndani.

Rais alikuwa akihesabu huku akitabasamu, ilipofika sekunde ya thelathini, mlango ulifunguliwa, akatoka Ray Charles na nyuma yake alionekana Sajenti Minja akiwa amelala na mwili umepondwa pondwa vibaya, Damu zilienea chumba kizima.

"hii nzuri, umetumia muda mchache zaidi" Rais aliongea huku akitabasamu na kipindi hicho wale vijana wengine waliingia na kuuchukua mwili wa Sajenti Minja, wakautoa pale,

"ebu ngojeni, amekufa?" Rais aliuliza huku akiinuka,

"tayari mkuu" Kijana mmoja alijibu,

"malizia kabisa ili tupate uhakika" Rais aliongea kisha yule kijana akatoa bastola na kumpiga risasi nyingi Sajenti Minja,

"basi" Rais aliongea na kuelekea nje.

Ndani wale vijana waliuingiza mwili wa Sajenti Minja katika gunia, kisha wakautoa na ule mwili mwingine wa yule pandikizi la baba aliyeuawa mchana, wakaipeleka katika buti za gari, kisha wakaondoka na yale magari, miili wakaenda kuitupa baharini kwenye kina kirefu cha maji.

Habari ya Sajenti Minja ikaishia hapo....

**********ITAENDELEA************

the Legend☆
 
Wakuu hiyo episode ya 29 nliyoweka leo mtunzi aliitoa jana, that means hapa tulipofkia sasa ndo tunaenda sawa na mtunzi. Ntaendelea kushusha episodes kadri zitakavyoendelea kutolewa na mtunzi

the Legend☆
 
Pole mkuu ...

ila humu yumo umemwita dear... usikatae... ...hatusutani maana si vibaya...kumwita mtu dear... ita tu .

ila kwa mimi huu ni utani tu mkuu.. wala usiwaze yaani!

Lakini aste aste!

Hujakaribishwa vizuri na shunie peke yake humu...... ... ..

Na unalalamika kama unalia kisa kuambiwa unamwita shunie dear ..ili akuonee huruma au aniwakie..?

Weye vipi ..?

Mkuu The legend asante sana kwa riwaya... ..zinatufariji sana ...unajali furaha ya wenzio na hivyo ndo inavyo takiwa mkuu!

AMRI mpya tulipewa.. ... "tupendane "

Siku njema dear..ake na shuu..




Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom