ibra87
R I P
- Jul 22, 2015
- 5,614
- 5,338
MKE WA RAIS
SEHEMU YA 002
Mwanaume akageuka kumtazama mwanamke akashangaa kukutana na mdomo wa bastola, bastola ambayo ilikuwa mikononi kwa mwanamke Yule. Macho Yalikuwa mekundu kwa Hasira.. Bastola Ikakohoa mara Mbili Risasi mbele Zikapenya Katika Paji la Uso la Mwanaume Yule. Ubongo Ukaruka na Kusambaa Chumba Kizima. Mwanaume Akaanguka chini na Kutulia.. Alikuwa Tayari ni Maiti.
Mlio wa bastola Uliosikika kutoka ndani uliwashtua walinzi wake na kila mmoja akaupeleka mkono wake kiunoni wakaibuka na Silaha.. Hawakuta kuingia kwa Kupitia getini... Wote walichupa hewani na kudondokea ndani.. Wakauendea mlango wa ndani kwa Kasi Ya Ajabu.. Kazi ambayo haikuwahi kutokea.. Sekunde kumi baadae walikuwa ndani ya Jumba lile. Wakapigwa na butwaa baada ya kukuta kiza totoro.. Wakatazamana na Kupiga hatua kuelekea ndani Zaidi... Walipofika karibu na Mlango wa Kutokea Upande wa Pili wa Jengo lile.. Wote wakahisi kukanyaga kitu kama Maji.. Lakini Uzito wa kitu kile kikawafanya walinzi Wainame na Kugusa yale maji.. Kila mmoja Kengele Ya Hatari Ikalia kichwani mwake.. Wakajua mke wa Mheshimiwa Alikuwa Hatarini.. Hawakusubiri.. Mmoja Akarudi nyuma na Kuruka Flyng kick Na Kuingia na mlango mpaka ndani... Kufika ndani Walichupa tena kila Mmoja Akaangukia pembeni Huku Bastola Mkononi.. Chumba Kilikuwa giza na Hawakusikia Hata mkoromo wa Binadamu... Mmoja Alipoangukia Akachupa tena Mpaka Iliposwtch ya Kuwashia taa na Kuifyatua..
Chumba Kizima Kiliwaka taa.. Kitu cha kwanza kuonekana machoni kwa walinzi wale ilikuwa maiti, maiti ambayo ilikuwa imelala katikati ya dimbwi kubwa la damu. Ubongo ulikuwa umesambaa mule ndani... Wakahamisha macho Yao na Kuyapeleka Kitandani wakapigwa na Butwaa Baada Ya kumuona Mke Wa Rais akiwa na Bastola Ya Kirusi Mkononi Huku akionekana MachoZi Kumtoka na Kumlowanisha. Hawakutaka kusubiri... Wakamuinua pale na Kumkokota Mpaka nje.. Walipofika Nje Cha kwanza kukifanya Waliichukua Ile Bastola Mikononi mwake kisha wakamuingiza ndani Ya Gari na kuliondoa maeneo Yale kabla polisi Hawajafika Eneo lile.
Gari Ikatembea kwa Mwendo Wa kasi sana kuelekea Nyumbani kwa Mheshimiwa maeneo Ya Kinondoni... Gari ikafika na Moja kwa Moja Kuingia ndani.. Maafisa Usalama Waliokuwepo waliiona Hali Ile ya kuonyesha kuchanganyikiwa kwa Mke Wa Rais lakini kwa kuwa Alikuwa na Walinzi Wake maalum Walimuacha bila Ya Kumuuliza.
Baada ya kuingia pale na Kushuka kwenye gari Kisha kuingia Ndani, aliongoza moja kwa moja bafuni huku akionekana ni Mwenye huzuni na Majuto Usoni. Aliingia bafuni na kuyavua mavazi Yake... Akafungulia maji na kuyaacha yaendelee kushuka katika mwili wake. Tukio zima la kupigwa Picha Lilimuumiza sana.. Hakujua ni Watu gani waliofanya vile na Walifanya kwa Lengo lipi... Akaiona Heshima yake kama Mke wa Rais Ikianza Kushuka.. Akawaza kile ambacho alikuwa akikifanya kikimfikia Rais au Wananchi Wakiona Atakuwa katika Wakati Gani? Aliuona Mwisho Wake mbaya, alijiona Mjinga Kushawishika kufanya ujinga.. Je ni Wakina nani lakini? Na Walifanya kwa Lengo lipi na ni Upi mwisho wangu katika Kadhia hii? Hakuwa na Majibu kwa Muda ule.. Hakuwa na jibu la kumfanya Ajisikie Vizuri.. Akakata Tamaa na Kukaa Juu Ya Sinki La Kuogea.. Macho Yake yakitazama Paa la Jumba lile la Kifahari... Mawazo Juu ya Mumewe Yakawa yanapita Usoni Mwake... Akajilazimisha Kutabasamu Lakini Haikuwa Hivyo.. Hakukuwa na Tabasamu Wala Hakukuwa na Kicheko.... Yalikuwa machozi, machozi Na Majuto.. Akainuka pale na Kuchukua Vali lake Maaulum... Akajiangalia kisha Kwa Sauti Ya Kujiamini Akanena... NITAMUUA YOYOTE NITAKAE MUHISI.. kisha akatoka Mle Bafuni na Kuingia Chumbani Kwake... Alipoingiza Mguu wake Ndani akapokelewa na Mlio Kuonyesha Kulikuwa Sms Kwenye Simu Yake.... Moyo Ukampiga Paaa!! Kisha Mikono kumtetemeka. Hakujua kwanini lakini alijikuta Akiiogopa mpaka simu yake. Akapiga hatua kisha Akaichukua Simu na Kuusoma Ujumbe Ule... Alichokiona Kwenye Simu kilimfanya Aanguke Chini Kama Mzigo.....
UNADHANI AMEONA KITU GANI?
SEHEMU YA 002
Mwanaume akageuka kumtazama mwanamke akashangaa kukutana na mdomo wa bastola, bastola ambayo ilikuwa mikononi kwa mwanamke Yule. Macho Yalikuwa mekundu kwa Hasira.. Bastola Ikakohoa mara Mbili Risasi mbele Zikapenya Katika Paji la Uso la Mwanaume Yule. Ubongo Ukaruka na Kusambaa Chumba Kizima. Mwanaume Akaanguka chini na Kutulia.. Alikuwa Tayari ni Maiti.
Mlio wa bastola Uliosikika kutoka ndani uliwashtua walinzi wake na kila mmoja akaupeleka mkono wake kiunoni wakaibuka na Silaha.. Hawakuta kuingia kwa Kupitia getini... Wote walichupa hewani na kudondokea ndani.. Wakauendea mlango wa ndani kwa Kasi Ya Ajabu.. Kazi ambayo haikuwahi kutokea.. Sekunde kumi baadae walikuwa ndani ya Jumba lile. Wakapigwa na butwaa baada ya kukuta kiza totoro.. Wakatazamana na Kupiga hatua kuelekea ndani Zaidi... Walipofika karibu na Mlango wa Kutokea Upande wa Pili wa Jengo lile.. Wote wakahisi kukanyaga kitu kama Maji.. Lakini Uzito wa kitu kile kikawafanya walinzi Wainame na Kugusa yale maji.. Kila mmoja Kengele Ya Hatari Ikalia kichwani mwake.. Wakajua mke wa Mheshimiwa Alikuwa Hatarini.. Hawakusubiri.. Mmoja Akarudi nyuma na Kuruka Flyng kick Na Kuingia na mlango mpaka ndani... Kufika ndani Walichupa tena kila Mmoja Akaangukia pembeni Huku Bastola Mkononi.. Chumba Kilikuwa giza na Hawakusikia Hata mkoromo wa Binadamu... Mmoja Alipoangukia Akachupa tena Mpaka Iliposwtch ya Kuwashia taa na Kuifyatua..
Chumba Kizima Kiliwaka taa.. Kitu cha kwanza kuonekana machoni kwa walinzi wale ilikuwa maiti, maiti ambayo ilikuwa imelala katikati ya dimbwi kubwa la damu. Ubongo ulikuwa umesambaa mule ndani... Wakahamisha macho Yao na Kuyapeleka Kitandani wakapigwa na Butwaa Baada Ya kumuona Mke Wa Rais akiwa na Bastola Ya Kirusi Mkononi Huku akionekana MachoZi Kumtoka na Kumlowanisha. Hawakutaka kusubiri... Wakamuinua pale na Kumkokota Mpaka nje.. Walipofika Nje Cha kwanza kukifanya Waliichukua Ile Bastola Mikononi mwake kisha wakamuingiza ndani Ya Gari na kuliondoa maeneo Yale kabla polisi Hawajafika Eneo lile.
Gari Ikatembea kwa Mwendo Wa kasi sana kuelekea Nyumbani kwa Mheshimiwa maeneo Ya Kinondoni... Gari ikafika na Moja kwa Moja Kuingia ndani.. Maafisa Usalama Waliokuwepo waliiona Hali Ile ya kuonyesha kuchanganyikiwa kwa Mke Wa Rais lakini kwa kuwa Alikuwa na Walinzi Wake maalum Walimuacha bila Ya Kumuuliza.
Baada ya kuingia pale na Kushuka kwenye gari Kisha kuingia Ndani, aliongoza moja kwa moja bafuni huku akionekana ni Mwenye huzuni na Majuto Usoni. Aliingia bafuni na kuyavua mavazi Yake... Akafungulia maji na kuyaacha yaendelee kushuka katika mwili wake. Tukio zima la kupigwa Picha Lilimuumiza sana.. Hakujua ni Watu gani waliofanya vile na Walifanya kwa Lengo lipi... Akaiona Heshima yake kama Mke wa Rais Ikianza Kushuka.. Akawaza kile ambacho alikuwa akikifanya kikimfikia Rais au Wananchi Wakiona Atakuwa katika Wakati Gani? Aliuona Mwisho Wake mbaya, alijiona Mjinga Kushawishika kufanya ujinga.. Je ni Wakina nani lakini? Na Walifanya kwa Lengo lipi na ni Upi mwisho wangu katika Kadhia hii? Hakuwa na Majibu kwa Muda ule.. Hakuwa na jibu la kumfanya Ajisikie Vizuri.. Akakata Tamaa na Kukaa Juu Ya Sinki La Kuogea.. Macho Yake yakitazama Paa la Jumba lile la Kifahari... Mawazo Juu ya Mumewe Yakawa yanapita Usoni Mwake... Akajilazimisha Kutabasamu Lakini Haikuwa Hivyo.. Hakukuwa na Tabasamu Wala Hakukuwa na Kicheko.... Yalikuwa machozi, machozi Na Majuto.. Akainuka pale na Kuchukua Vali lake Maaulum... Akajiangalia kisha Kwa Sauti Ya Kujiamini Akanena... NITAMUUA YOYOTE NITAKAE MUHISI.. kisha akatoka Mle Bafuni na Kuingia Chumbani Kwake... Alipoingiza Mguu wake Ndani akapokelewa na Mlio Kuonyesha Kulikuwa Sms Kwenye Simu Yake.... Moyo Ukampiga Paaa!! Kisha Mikono kumtetemeka. Hakujua kwanini lakini alijikuta Akiiogopa mpaka simu yake. Akapiga hatua kisha Akaichukua Simu na Kuusoma Ujumbe Ule... Alichokiona Kwenye Simu kilimfanya Aanguke Chini Kama Mzigo.....
UNADHANI AMEONA KITU GANI?