Willy Gamba 1
JF-Expert Member
- Jan 5, 2015
- 352
- 377
RIWAYA ;MKAKATI WA KUELEKEA IKULU
MTUNZI: HUSSEIN WAMAYYA
SEHEMU YA KWANZA.
Utangulizi
Wakati Baba wa Taifa anamlea Masurufu Hussein
Masurufu hakuwa anajua kuwa analea mtu ambaye
alikuwa amechoshwa na udhalili wanaoishi
wapigania uhuru.
Hakujua pia kuwa mzazi mwingine wa Masurufu
alikuwa mstaafu wa uliokuwa Muungano wa Afrika
Mashariki na ambaye licha ya kuutumikia
Muungano huo kwa nguvu na uwezo wake wote,
bado ameishia kudhalilika wakati akidai mafao
yake kiasi cha kufikia kuvua nguo hadharani.
Hakujua pia kuwa hizo ni sababu chache miongoni
mwa nyingi zilizomfanya Masurufu huyu aanze
kuhubiri utakatifu huku akifanya uhalifu baada ya
kupata nafasi na kuzitumia vyema fursa za Vita
vya Kagera, Uhujumu uchumi, Ubunge, Uwaziri na
baadae ubalozi wa Tanzania nje ya nchi.
Na sasa akishirikiana na Christopher MacDonald
Beberu wa G-8 Original, Masurufu anajiandaa
vyema kwenda Ikulu kwa lengo moja tu,
kuzinyonya rasilimali za Tanzania mpaka tone la
mwisho !
Ikoje hiyo safari yake?
SURA YA KWANZA
UHOLANZI - JANUARI 2005
Zilishapita siku za kutosha toka Dr. Masurufu na
watumushi wenzie katika Ubalozi wao kule
Uholanzi wafanye mkutano. Na ilishapita miaka
tisa toka Dr. Masurufu alipoteuliwa kuwa Balozi wa
Tanzania katika nchi hiyo. Asubuhi hii akiwa ndiyo
kwanza ametoka kuoga, mkewe akaingia ndani na
kumuuliza.
Habari za Asubuhi Baba Rose!
Nzuri tu, sijui za kwako Anajibu hali akijifuta maji
kwa taulo. Mkewe anafungua kabati na kumtolea
suti safi.
Zangu pia njema!
Ulikuwa wapi?
Nilikuwa namuhimiza Rose awahi shule. Mwenzie
Dan keshaondoka saa nyingi!
Oh!Vizuri! Masurufu akaanza kuvaa nguo.
Una habari mume wangu?
Habari gani?
Rais wa nchi yetu ya Tanzania anamaliza muda
wake mwaka huu. Nasikia chama tawala kitaanza
kugawa fomu mwezi ujao!
Sema haki ya Mungu!
Haki ya nani tena!
We habari hizi umezipata wapi? Sasa Dr.
Masurufu alikuwa akivaa viatu.
Redioni. Idhaa ya kiswahili ya BBC.
Zimetangazwa asubuhi wakati ulipokwenda kuoga!
Enhe! Dr. Masurufu akaacha kufunga kamba za
viatu na kumtazama mkewe kwa mshangao.
Wamesemaje?
Katibu Mkuu amesema fomu zitaanza kutolewa
mwezi ujao kwa watanzania wenye sifa. Gharama
yake itakuwa shilingi milioni mbili kwa kila fomu.
Kutoka hapo itakubidi uzunguke nchi nzima
kutafuta wadhamini kabla ya kurudisha fomu
mwezi unaofuata ambapo chama kitayapitia
majina ya wagombea safi na kuyapeleka kwa
wajumbe wa Kamati kuu kwa uamuzi wa mwisho!
Masurufu akamaliza kuvaa viatu, mkewe
akamuongoza mpaka eneo la kupatia chakula
ambako kulikuwa na chai ya nguvu. Akasema.
Kikao kilichopita nilitoa onyo kali kwa wale
watumishi wenzangu ambao walidhani wanaweza
kuniendesha kama yule Balozi aliyepelekwa
Singapore. Hiki ni chuma cha pua bwana
hawataniweza katu ha ha .haaah! Akacheka.
Mkewe akatabasamu tu. Dakika chache baadae
tabasamu lilizimika akarudi ndani ya tafakuri tena.
Mpenzi mke wangu! Dr. Masurufu akamwita
Kwa nini una majonzi mpenzi? Huonekani kuwa
mke wangu niliyekuzoea. Kulikoni?
Huu Uchaguzi laaziz!
Uchaguzi?!
Ndiyo!
Una nini ?
Huujali kabisa!
Siujali ndiyo!
Kwa nini huujali?
Unatuhusu nini? Ingawa sisi ni watanzania, tuko
maili nyingi nje ya Tanzania. Sidhani kama una
athari kwetu!
Kicheko cha uchungu kikamponyoka Glady mkewe!
Akamwambia Kwa taarifa yako, uchaguzi huu
unatuhusu sisi zaidi, kuliko unavyowahusu
watanzania wengine!
Kwa namna gani dia?
Swali zuri, sisi tunaitegemea Serikali iliyopo
madarakani kutuweka huku Ubalozini. Ikimaliza
muda wake na kuondoka hatutaipata tena fursa ya
kuishi kivulini hapa Uholanzi. Hatutaipata nafasi ya
kuishi katika kasri hili wala hatutapata wasaa wa
kutembelea magari haya ya kifahari. Hii ni pamoja
na watoto wetu kuacha kusoma shule za kimataifa
na kwenda kubanana na akina kajamba nani huko
uswahilini. Bado tu hujali?
Yakamuingia Dr. Masurufu. Akavua miwani na
kuisafisha Unajua kwa nini sijali? Akairudisha
miwani usoni.
Sijui!
Yupo mtu anayenifanya nisijali. Mtu ambaye
amechangia kwa asilimia kubwa mimi kuwa Balozi
wa Tanzania nchini Uholanzi. Mtu huyu ni Profesa
Zonga!
We ndiyo uko nyuma kweli kweli. Huyo Profesa
Zonga ndio atasababisha uteuliwe tena?
Ndiyo! Hata akiingia nani pale Ikulu, sisi
tutaendelea kuula tu. Watake tutaula, wasitake
tutaula!
Yaelekea unajiamini kupita kiasi baba Rose?!
Kwa nini nisijiamini mama watoto?! Dawa zake
ninatumia vizuri, masharti yake ninatimiza. Gari
nimemuachia. Nyumba nimemjengea. Kwa nini
nisijiamini?! Kwa nini?
Mkewe akashusha pumzi za kukata tamaa.
Lakini mume wangu, utakuwa Balozi mpaka lini?
Lini na sisi tutakuwa viongozi wa juu kabisa wa
Taifa letu la Tanzania, tukiandikwa na vyombo vya
habari kila tunapokohoa, tukilindwa kama miungu
wadogo, tukimiliki uchumi wote wa nchi?
Saini yako ikiamua juu ya kuishi au kufa kwa mtu
yeyote. Ukiwa Amiri Jeshi Mkuu unayeheshimika,
zulia jekundu likikulaki kila unapokuwa ziarani!
Kwa nini hutaki neema hii mume wangu?
Dr. Masurufu akavuta tafakuri kwa muda.
Akasema, Tatizo ni watu laaziz, watanikubali
kweli? Watu watanipa nafasi?!
Watu ndio kitu gani?
Una maana gani?
Labda ungezungumzia fedha. Kama huna fedha
kabisa, labda hicho kinaweza kuwa kikwazo. Lakini
watu?! Mbona ukiwa na fedha ni rahisi kupata
chochote unachotaka. Seuze watu! Na wewe fedha
unazo!
Lakini hazitoshi kufanya kampeni katika chama na
nchi nzima.
Zinatosha mume wangu. Zinatosha kabisa Dr.
Masurufu! Jiulize una rasilimali kiasi gani, una
marafiki wangapi wanaokuunga mkono ndani na
nje ya nchi. Hapa hapa Uholanzi wapo zaidi ya
kumi. Hao ni wale uliopata kunitambulisha na
kuwaleta nyumbani ambao kwa kinywa chako
umekiri kwamba ni wafanyabiashara wakubwa
ambao hawazungumzii milioni bali bilioni!
Hilo ni kweli! Masurufu akaafiki.
Bado hujanitambulisha wa nje ya hapo. Ambao
sina shaka unao wa kutosha!
Ni kweli ninao wa kutosha!
Unataka kuniambia wote hawa ukiwaendea
kuwaomba msaada na sio msaada hasa bali
wakuazime na ukishaukwaa urais tu
utawarudishia. Unataka kuniambia watakataa
wote?
Glady, unafahamu vizuri sana kama kitu hicho
hakiwezekani!
Kumbe kinachokufanya uhofie ni nini?
Hofu yangu iko kwenye kuanguka. Watu
wanaweza kula fedha zako halafu wakakunyima
kura!
Mawazo kama hayo mtafutaji hatakiwi kuwa nayo,
lakini pia huwajui watanzania vizuri. Watanzania
wana ukarimu uliopatiliza. Wanakumbuka hisani
kama sio fadhila hata katika hali inayokatisha
tamaa kabisa. Wakishakula fedha zako
hawatakuwa na zaidi ila kukupigia kura wakifika
katika sanduku la kura.
Kwa sasa ukiwazungukia marafiki zako wa ndani
na nje wakatupa walau bilioni mbili tu, hesabu
utakuwa umeshinda tayari. Niulize kwa nini!
Kwa nini?
Ukiwa na fedha hizo, ukaongezea na zako
haidhuru hata zikafikia bilioni nne au tano.
Unaweza kuanzisha gazeti lako ambalo si tu
litakuwa likikupigia debe kama mgombea safi,
mgombea chaguo, mgombea unayefaa na
kupendwa na wengi, usiye na kashfa na kadhalika
na kadhalika. Lakini pia, gazeti lako hilo litashiriki
kwa siri kuwachafua na kuwapaka matope
wagombea wengine kwa hila , wagombea ambao
watakuwa tishio kwako!
Enhe, nikingali nakusikiliza! Dr. Masurufu alianza
kusisimkwa.
Huo hautakuwa mwisho, utawanunua wahariri na
wamiliki wa vyombo vingine vya habari pamwe na
waandishi wao, ambao kazi yao itakuwa ni
kukufagilia mpaka chama kitakapokupitisha
ambapo hutalazimika kutumia nguvu katika
Uchaguzi Mkuu kwa vile chama na Serikali yake
vitakusaidia kwa nguvu zote, mpaka unaingia
Ikulu! Masurufu akakenua
Je, Mkewe akahitimisha kwa swali akitabasamu
Bado tu una hofu?
Hapana, sina hofu kabisa! Alijibu Masurufu kwa
moyo mweupe kabisa.
Kwa hiyo tunakwenda kupigana siyo? Kupigana
kwa ajili ya maslahi yetu, kupigana kwa ajili ya
urais wetu, kwa ajili ya kuiweka Tanzania ya sasa
na ijayo mikononi mwetu siyo!
Ndiyo mke wangu!
Ahadi?!
Ahadi!
Good! Glady akafurahi akitabasamu. Alikuwa
amefaulu kumfanya mumewe arudi katika reli.
Arudi kuyatazama maisha katka mwanga bora.
Mwanga ambao kama utawamulika vizuri
utawafanya waingie katika historia ya nchi na
kuishi kama sio kukumbukwa milele. Heshima iliyo
SURA YA PILI
KIGOMA - 1952
Wakati Tanganyika inapata uhuru mwaka 1961,
Masurufu Hussein Masurufu alikuwa na umri wa
miaka kumi na miwili akiwa darasa la pili katika
shule ya Mkoloni. Alikuwa kijana shababi na
umbile lake liliashiria kuwa atakuja kuwa jitu la
miraba mine baadae. Alijaaliwa sura jamali
iliyowavutia wengi ingawa mwenyewe hakulijua hilo
kwa wakati huo.
Baba yake Kepteni Hussein Masurufu alikuwa
katibu Mkuu wa TANU kanda ya magharibi kanda
iliyojumuisha mikoa ya Kigoma, Tabora na Rukwa.
Yeye akiishi Kigoma Mjini.
Akiwa miongoni mwa wazee wa awali wa
Tanganyika walioianzisha TAA na baadae
kumkaribisha Nyerere kabla hawajamchagua kuwa
Mwenyekiti wake, Hussein alikuwa ameshiriki kwa
kina katika harakati za kuisambaza TAA na baadae
TANU, na kupigania Uhuru mpaka hapo
ulipopatikana
Kuipenda kwake TAA hakukuja bure, alijikuta
akiipenda TAA kupita kiasi baada ya kuchoshwa na
utawala wa kibabe na wa kidhalimu wa wakoloni
wa Ujerumani na baadae Waingereza.
Awali alikuwa chini ya wajerumani Kapteni wa
meli, akiendesha meli za MV Lyemba na MV
Mwongozo zilizokuwa zikitoa huduma katika ziwa
Tanganyika kwenda katika nchi za Zambia, Burundi
na Zaire (sasa Congo), kupitia katika vijiji vilivyopo
katika mwambao wa Ziwa hilo lenye kina kirefu
kuliko yote Afrika. Katika Dunia likishika nafasi ya
pili baada ya lile la Bekari lililopo Urusi.
Alikuwa akilipwa mshahara mzuri wa wastani
uliomfanya awe na maisha mazuri tofauti na
wananchi wengi ambao walikuwa hawaishi
kuwatupia lawama wakoloni kuwa hawafai
hawafai.
Yeye akiwa na kisomo cha darasa la nane,
kilichomuwezesha kuzijua lugha za kingereza,
kijerumani, kigiriki na kiitaliano sawasawa, mke
mzuri, nyumba bora, mshahara wa kutakata na
mengine mengi, kamwe hakuona ubaya wa
wakoloni mpaka ilipofika siku ile.
Siku ambayo alikuwa anakabiliwa na safari ya
kwenda Zambia na baadae Zaire. Kama kawaida
alijilawa asubuhi na mapema na kuelekea bafuni.
Aliporudi mswaki ukingali mdomoni na taulo likiwa
mkononi ndipo mambo yalipoanza kuwa mambo.
Mkewe ambaye alikuwa mjamzito mwenye mimba
ya miezi nane na ushei alikuwa akigaa gaa huku
na huko kitandani mdomoni akiachia mayowe
yaliyoashiria kuwa alikuwa ndani ya Uchungu
uliopatiliza
Taulo likatupwa kushoto mswaki ukindondoka
mdomoni bila yeye kuwa na habari akakimbia
kimbia hovyo mle ndani akishika hiki na kile bila
uelekeo maalumu baadae akili zikamrejea,
akamjongelea mkewe na kumuuliza
Fatuma . Fatuma, vipi mpenzi?!
Na na . nahisi siku zimefika! Akasema kwa
taabu akishusha pumzi kwa nguvu. Maumivu
yakamzidi katika nyonga.
Kwani hujaenda kliniki tena?
Nilienda! Niitie gari Hussein
Madaktari walisemaje?
Gari Pliz, gari tafadhali
Bila kujua tatizo ita !
Hussein! Fatuma akabweka kwa nguvu machozi
yakimtoka kwa wingi. Hussein Masurufu
akashtuka, Naam! Akaitika kwa woga!
Unataka nife?
Oooh! No hapana . Hapana mahabuba wangu
nakupenda sana!
Basi ita gari Upesi!
Wakati anainuka akayaona majimaji mazito
yakichuruzika katika miguu ya mkewe. Akaogopa
zaidi umakini ukimpotea akaondoka upesi
akielekea sebuleni akajigonga katika mlango na
kuanguka chini.
Shit! Akaguta akiinuka na kuingia sebuleni.
Akaifikia simu ya mezani na kupiga hospitali
kuomba aletewe gari la wagonjwa. Baada ya
kuelekeza vya kutosha, alirudi tena sebuleni kwa
mkewe, akawa akiugulia pamoja nae. Ingawa huu
ulikuwa uzazi wake wa kwanza, na uchungu
ulikuwa ukimsumbua bado, lakini mafundisho
aliyoyapata kabla hajaolewa na Hussein Masurufu
yalikuwa yakingali mabichi kichwani mwa Fatuma.
Alimuagiza mumewe amuandalie kanga na pamba
za kutosha katika mkoba. Alimwambia pia
amchukulie kadi ya kliniki chupa la chai na vingine
vingi.
Kutahamaki gari lilishafika
Fatuma alichukuliwa mpaka katika hospitali ya
Maweni akapokelewa na kupewa kitanda. Manesi
wakimuakikishia Hussein kwamba mgonjwa wake
angejifungua baada ya muda mfupi.
Dakika kumi baadae akawa ndani ya Teksi no. 7
Peugeot 404 mali ya mzee Shaka wakieleka
Kasingirima Ujiji aliko mama mzazi wa Fatuma
Malilo. Ambako alifika anamzoa na kuja nae
hospitali.
Kichwa chake kikiwa hakitulii, Hussein Masurufu
alirandaranda hospitali nzima bila uelekeo
maalumu mpaka zilipokuja zile taarifa za faraja
masaa sita baadae, kwamba mkewe alikuwa
amejifungua mtoto wa kiume kwa operesheni
ndogo.
Furaha zilizomvaa hazikuwa na mfano, Nami
nitaitwa baba! Nimemzaa baba yangu! Mzee
Masurufu Laiti angelikuwepo! Aliendelea kufurahi
nusunusu mpaka waliporuhusiwa kuingia wodini na
yeye kukabidhiwa mtoto ambebe! Akambeba kwa
furaha na bashasha, tabasamu likiupamba uso
wake. Walifanana kama reale kwa ya pili
Waliporuhusiwa na kurejea nyumbani, ndipo akili
zilipomrejea Hussein kwamba alitakuwa kuwa
ndani ya meli ya Liemba muda huu akiwapeleka
abiria Zambia, Zaire na baadae Burundi. Ukweli
huu ukafanya akiliye iingiwe na ganzi.
Aliwafamu waajiri wake vizuri sana kosa dogo tu la
kutosafisha sakafu vizuri lingeweza kukugharimu
kibarua. Au wizi wa mali ya shirika wakati chombo
kikiwa safarini, hukumu yake ilikuwa kutoswa
baharini na kupoteza maisha yako.
Akajifikiria yeye!
Meli ilitakiwa kuondoa saa mbili kamili asubuhi.
Inapeleka abiria. Abiria waliolipa pesa zao, pesa
ambazo zinampa yeye mshahara. Mpaka muda
huu saa nane mchana yeye alikuwa hajatokea
bandarini
Masaa sita mbele!
Akajipeleka ofisini kama ambavyo mbwa hujipeleka
mbele ya chatu tayari kuliwa! Yeye akiamini
kwamba alikuwa na sababu ya msingi. Sababu ya
kuokoa maisha ya mkewe na maisha ya mwanae.
* * *
MTUNZI: HUSSEIN WAMAYYA
SEHEMU YA KWANZA.
Utangulizi
Wakati Baba wa Taifa anamlea Masurufu Hussein
Masurufu hakuwa anajua kuwa analea mtu ambaye
alikuwa amechoshwa na udhalili wanaoishi
wapigania uhuru.
Hakujua pia kuwa mzazi mwingine wa Masurufu
alikuwa mstaafu wa uliokuwa Muungano wa Afrika
Mashariki na ambaye licha ya kuutumikia
Muungano huo kwa nguvu na uwezo wake wote,
bado ameishia kudhalilika wakati akidai mafao
yake kiasi cha kufikia kuvua nguo hadharani.
Hakujua pia kuwa hizo ni sababu chache miongoni
mwa nyingi zilizomfanya Masurufu huyu aanze
kuhubiri utakatifu huku akifanya uhalifu baada ya
kupata nafasi na kuzitumia vyema fursa za Vita
vya Kagera, Uhujumu uchumi, Ubunge, Uwaziri na
baadae ubalozi wa Tanzania nje ya nchi.
Na sasa akishirikiana na Christopher MacDonald
Beberu wa G-8 Original, Masurufu anajiandaa
vyema kwenda Ikulu kwa lengo moja tu,
kuzinyonya rasilimali za Tanzania mpaka tone la
mwisho !
Ikoje hiyo safari yake?
SURA YA KWANZA
UHOLANZI - JANUARI 2005
Zilishapita siku za kutosha toka Dr. Masurufu na
watumushi wenzie katika Ubalozi wao kule
Uholanzi wafanye mkutano. Na ilishapita miaka
tisa toka Dr. Masurufu alipoteuliwa kuwa Balozi wa
Tanzania katika nchi hiyo. Asubuhi hii akiwa ndiyo
kwanza ametoka kuoga, mkewe akaingia ndani na
kumuuliza.
Habari za Asubuhi Baba Rose!
Nzuri tu, sijui za kwako Anajibu hali akijifuta maji
kwa taulo. Mkewe anafungua kabati na kumtolea
suti safi.
Zangu pia njema!
Ulikuwa wapi?
Nilikuwa namuhimiza Rose awahi shule. Mwenzie
Dan keshaondoka saa nyingi!
Oh!Vizuri! Masurufu akaanza kuvaa nguo.
Una habari mume wangu?
Habari gani?
Rais wa nchi yetu ya Tanzania anamaliza muda
wake mwaka huu. Nasikia chama tawala kitaanza
kugawa fomu mwezi ujao!
Sema haki ya Mungu!
Haki ya nani tena!
We habari hizi umezipata wapi? Sasa Dr.
Masurufu alikuwa akivaa viatu.
Redioni. Idhaa ya kiswahili ya BBC.
Zimetangazwa asubuhi wakati ulipokwenda kuoga!
Enhe! Dr. Masurufu akaacha kufunga kamba za
viatu na kumtazama mkewe kwa mshangao.
Wamesemaje?
Katibu Mkuu amesema fomu zitaanza kutolewa
mwezi ujao kwa watanzania wenye sifa. Gharama
yake itakuwa shilingi milioni mbili kwa kila fomu.
Kutoka hapo itakubidi uzunguke nchi nzima
kutafuta wadhamini kabla ya kurudisha fomu
mwezi unaofuata ambapo chama kitayapitia
majina ya wagombea safi na kuyapeleka kwa
wajumbe wa Kamati kuu kwa uamuzi wa mwisho!
Masurufu akamaliza kuvaa viatu, mkewe
akamuongoza mpaka eneo la kupatia chakula
ambako kulikuwa na chai ya nguvu. Akasema.
Kikao kilichopita nilitoa onyo kali kwa wale
watumishi wenzangu ambao walidhani wanaweza
kuniendesha kama yule Balozi aliyepelekwa
Singapore. Hiki ni chuma cha pua bwana
hawataniweza katu ha ha .haaah! Akacheka.
Mkewe akatabasamu tu. Dakika chache baadae
tabasamu lilizimika akarudi ndani ya tafakuri tena.
Mpenzi mke wangu! Dr. Masurufu akamwita
Kwa nini una majonzi mpenzi? Huonekani kuwa
mke wangu niliyekuzoea. Kulikoni?
Huu Uchaguzi laaziz!
Uchaguzi?!
Ndiyo!
Una nini ?
Huujali kabisa!
Siujali ndiyo!
Kwa nini huujali?
Unatuhusu nini? Ingawa sisi ni watanzania, tuko
maili nyingi nje ya Tanzania. Sidhani kama una
athari kwetu!
Kicheko cha uchungu kikamponyoka Glady mkewe!
Akamwambia Kwa taarifa yako, uchaguzi huu
unatuhusu sisi zaidi, kuliko unavyowahusu
watanzania wengine!
Kwa namna gani dia?
Swali zuri, sisi tunaitegemea Serikali iliyopo
madarakani kutuweka huku Ubalozini. Ikimaliza
muda wake na kuondoka hatutaipata tena fursa ya
kuishi kivulini hapa Uholanzi. Hatutaipata nafasi ya
kuishi katika kasri hili wala hatutapata wasaa wa
kutembelea magari haya ya kifahari. Hii ni pamoja
na watoto wetu kuacha kusoma shule za kimataifa
na kwenda kubanana na akina kajamba nani huko
uswahilini. Bado tu hujali?
Yakamuingia Dr. Masurufu. Akavua miwani na
kuisafisha Unajua kwa nini sijali? Akairudisha
miwani usoni.
Sijui!
Yupo mtu anayenifanya nisijali. Mtu ambaye
amechangia kwa asilimia kubwa mimi kuwa Balozi
wa Tanzania nchini Uholanzi. Mtu huyu ni Profesa
Zonga!
We ndiyo uko nyuma kweli kweli. Huyo Profesa
Zonga ndio atasababisha uteuliwe tena?
Ndiyo! Hata akiingia nani pale Ikulu, sisi
tutaendelea kuula tu. Watake tutaula, wasitake
tutaula!
Yaelekea unajiamini kupita kiasi baba Rose?!
Kwa nini nisijiamini mama watoto?! Dawa zake
ninatumia vizuri, masharti yake ninatimiza. Gari
nimemuachia. Nyumba nimemjengea. Kwa nini
nisijiamini?! Kwa nini?
Mkewe akashusha pumzi za kukata tamaa.
Lakini mume wangu, utakuwa Balozi mpaka lini?
Lini na sisi tutakuwa viongozi wa juu kabisa wa
Taifa letu la Tanzania, tukiandikwa na vyombo vya
habari kila tunapokohoa, tukilindwa kama miungu
wadogo, tukimiliki uchumi wote wa nchi?
Saini yako ikiamua juu ya kuishi au kufa kwa mtu
yeyote. Ukiwa Amiri Jeshi Mkuu unayeheshimika,
zulia jekundu likikulaki kila unapokuwa ziarani!
Kwa nini hutaki neema hii mume wangu?
Dr. Masurufu akavuta tafakuri kwa muda.
Akasema, Tatizo ni watu laaziz, watanikubali
kweli? Watu watanipa nafasi?!
Watu ndio kitu gani?
Una maana gani?
Labda ungezungumzia fedha. Kama huna fedha
kabisa, labda hicho kinaweza kuwa kikwazo. Lakini
watu?! Mbona ukiwa na fedha ni rahisi kupata
chochote unachotaka. Seuze watu! Na wewe fedha
unazo!
Lakini hazitoshi kufanya kampeni katika chama na
nchi nzima.
Zinatosha mume wangu. Zinatosha kabisa Dr.
Masurufu! Jiulize una rasilimali kiasi gani, una
marafiki wangapi wanaokuunga mkono ndani na
nje ya nchi. Hapa hapa Uholanzi wapo zaidi ya
kumi. Hao ni wale uliopata kunitambulisha na
kuwaleta nyumbani ambao kwa kinywa chako
umekiri kwamba ni wafanyabiashara wakubwa
ambao hawazungumzii milioni bali bilioni!
Hilo ni kweli! Masurufu akaafiki.
Bado hujanitambulisha wa nje ya hapo. Ambao
sina shaka unao wa kutosha!
Ni kweli ninao wa kutosha!
Unataka kuniambia wote hawa ukiwaendea
kuwaomba msaada na sio msaada hasa bali
wakuazime na ukishaukwaa urais tu
utawarudishia. Unataka kuniambia watakataa
wote?
Glady, unafahamu vizuri sana kama kitu hicho
hakiwezekani!
Kumbe kinachokufanya uhofie ni nini?
Hofu yangu iko kwenye kuanguka. Watu
wanaweza kula fedha zako halafu wakakunyima
kura!
Mawazo kama hayo mtafutaji hatakiwi kuwa nayo,
lakini pia huwajui watanzania vizuri. Watanzania
wana ukarimu uliopatiliza. Wanakumbuka hisani
kama sio fadhila hata katika hali inayokatisha
tamaa kabisa. Wakishakula fedha zako
hawatakuwa na zaidi ila kukupigia kura wakifika
katika sanduku la kura.
Kwa sasa ukiwazungukia marafiki zako wa ndani
na nje wakatupa walau bilioni mbili tu, hesabu
utakuwa umeshinda tayari. Niulize kwa nini!
Kwa nini?
Ukiwa na fedha hizo, ukaongezea na zako
haidhuru hata zikafikia bilioni nne au tano.
Unaweza kuanzisha gazeti lako ambalo si tu
litakuwa likikupigia debe kama mgombea safi,
mgombea chaguo, mgombea unayefaa na
kupendwa na wengi, usiye na kashfa na kadhalika
na kadhalika. Lakini pia, gazeti lako hilo litashiriki
kwa siri kuwachafua na kuwapaka matope
wagombea wengine kwa hila , wagombea ambao
watakuwa tishio kwako!
Enhe, nikingali nakusikiliza! Dr. Masurufu alianza
kusisimkwa.
Huo hautakuwa mwisho, utawanunua wahariri na
wamiliki wa vyombo vingine vya habari pamwe na
waandishi wao, ambao kazi yao itakuwa ni
kukufagilia mpaka chama kitakapokupitisha
ambapo hutalazimika kutumia nguvu katika
Uchaguzi Mkuu kwa vile chama na Serikali yake
vitakusaidia kwa nguvu zote, mpaka unaingia
Ikulu! Masurufu akakenua
Je, Mkewe akahitimisha kwa swali akitabasamu
Bado tu una hofu?
Hapana, sina hofu kabisa! Alijibu Masurufu kwa
moyo mweupe kabisa.
Kwa hiyo tunakwenda kupigana siyo? Kupigana
kwa ajili ya maslahi yetu, kupigana kwa ajili ya
urais wetu, kwa ajili ya kuiweka Tanzania ya sasa
na ijayo mikononi mwetu siyo!
Ndiyo mke wangu!
Ahadi?!
Ahadi!
Good! Glady akafurahi akitabasamu. Alikuwa
amefaulu kumfanya mumewe arudi katika reli.
Arudi kuyatazama maisha katka mwanga bora.
Mwanga ambao kama utawamulika vizuri
utawafanya waingie katika historia ya nchi na
kuishi kama sio kukumbukwa milele. Heshima iliyo
SURA YA PILI
KIGOMA - 1952
Wakati Tanganyika inapata uhuru mwaka 1961,
Masurufu Hussein Masurufu alikuwa na umri wa
miaka kumi na miwili akiwa darasa la pili katika
shule ya Mkoloni. Alikuwa kijana shababi na
umbile lake liliashiria kuwa atakuja kuwa jitu la
miraba mine baadae. Alijaaliwa sura jamali
iliyowavutia wengi ingawa mwenyewe hakulijua hilo
kwa wakati huo.
Baba yake Kepteni Hussein Masurufu alikuwa
katibu Mkuu wa TANU kanda ya magharibi kanda
iliyojumuisha mikoa ya Kigoma, Tabora na Rukwa.
Yeye akiishi Kigoma Mjini.
Akiwa miongoni mwa wazee wa awali wa
Tanganyika walioianzisha TAA na baadae
kumkaribisha Nyerere kabla hawajamchagua kuwa
Mwenyekiti wake, Hussein alikuwa ameshiriki kwa
kina katika harakati za kuisambaza TAA na baadae
TANU, na kupigania Uhuru mpaka hapo
ulipopatikana
Kuipenda kwake TAA hakukuja bure, alijikuta
akiipenda TAA kupita kiasi baada ya kuchoshwa na
utawala wa kibabe na wa kidhalimu wa wakoloni
wa Ujerumani na baadae Waingereza.
Awali alikuwa chini ya wajerumani Kapteni wa
meli, akiendesha meli za MV Lyemba na MV
Mwongozo zilizokuwa zikitoa huduma katika ziwa
Tanganyika kwenda katika nchi za Zambia, Burundi
na Zaire (sasa Congo), kupitia katika vijiji vilivyopo
katika mwambao wa Ziwa hilo lenye kina kirefu
kuliko yote Afrika. Katika Dunia likishika nafasi ya
pili baada ya lile la Bekari lililopo Urusi.
Alikuwa akilipwa mshahara mzuri wa wastani
uliomfanya awe na maisha mazuri tofauti na
wananchi wengi ambao walikuwa hawaishi
kuwatupia lawama wakoloni kuwa hawafai
hawafai.
Yeye akiwa na kisomo cha darasa la nane,
kilichomuwezesha kuzijua lugha za kingereza,
kijerumani, kigiriki na kiitaliano sawasawa, mke
mzuri, nyumba bora, mshahara wa kutakata na
mengine mengi, kamwe hakuona ubaya wa
wakoloni mpaka ilipofika siku ile.
Siku ambayo alikuwa anakabiliwa na safari ya
kwenda Zambia na baadae Zaire. Kama kawaida
alijilawa asubuhi na mapema na kuelekea bafuni.
Aliporudi mswaki ukingali mdomoni na taulo likiwa
mkononi ndipo mambo yalipoanza kuwa mambo.
Mkewe ambaye alikuwa mjamzito mwenye mimba
ya miezi nane na ushei alikuwa akigaa gaa huku
na huko kitandani mdomoni akiachia mayowe
yaliyoashiria kuwa alikuwa ndani ya Uchungu
uliopatiliza
Taulo likatupwa kushoto mswaki ukindondoka
mdomoni bila yeye kuwa na habari akakimbia
kimbia hovyo mle ndani akishika hiki na kile bila
uelekeo maalumu baadae akili zikamrejea,
akamjongelea mkewe na kumuuliza
Fatuma . Fatuma, vipi mpenzi?!
Na na . nahisi siku zimefika! Akasema kwa
taabu akishusha pumzi kwa nguvu. Maumivu
yakamzidi katika nyonga.
Kwani hujaenda kliniki tena?
Nilienda! Niitie gari Hussein
Madaktari walisemaje?
Gari Pliz, gari tafadhali
Bila kujua tatizo ita !
Hussein! Fatuma akabweka kwa nguvu machozi
yakimtoka kwa wingi. Hussein Masurufu
akashtuka, Naam! Akaitika kwa woga!
Unataka nife?
Oooh! No hapana . Hapana mahabuba wangu
nakupenda sana!
Basi ita gari Upesi!
Wakati anainuka akayaona majimaji mazito
yakichuruzika katika miguu ya mkewe. Akaogopa
zaidi umakini ukimpotea akaondoka upesi
akielekea sebuleni akajigonga katika mlango na
kuanguka chini.
Shit! Akaguta akiinuka na kuingia sebuleni.
Akaifikia simu ya mezani na kupiga hospitali
kuomba aletewe gari la wagonjwa. Baada ya
kuelekeza vya kutosha, alirudi tena sebuleni kwa
mkewe, akawa akiugulia pamoja nae. Ingawa huu
ulikuwa uzazi wake wa kwanza, na uchungu
ulikuwa ukimsumbua bado, lakini mafundisho
aliyoyapata kabla hajaolewa na Hussein Masurufu
yalikuwa yakingali mabichi kichwani mwa Fatuma.
Alimuagiza mumewe amuandalie kanga na pamba
za kutosha katika mkoba. Alimwambia pia
amchukulie kadi ya kliniki chupa la chai na vingine
vingi.
Kutahamaki gari lilishafika
Fatuma alichukuliwa mpaka katika hospitali ya
Maweni akapokelewa na kupewa kitanda. Manesi
wakimuakikishia Hussein kwamba mgonjwa wake
angejifungua baada ya muda mfupi.
Dakika kumi baadae akawa ndani ya Teksi no. 7
Peugeot 404 mali ya mzee Shaka wakieleka
Kasingirima Ujiji aliko mama mzazi wa Fatuma
Malilo. Ambako alifika anamzoa na kuja nae
hospitali.
Kichwa chake kikiwa hakitulii, Hussein Masurufu
alirandaranda hospitali nzima bila uelekeo
maalumu mpaka zilipokuja zile taarifa za faraja
masaa sita baadae, kwamba mkewe alikuwa
amejifungua mtoto wa kiume kwa operesheni
ndogo.
Furaha zilizomvaa hazikuwa na mfano, Nami
nitaitwa baba! Nimemzaa baba yangu! Mzee
Masurufu Laiti angelikuwepo! Aliendelea kufurahi
nusunusu mpaka waliporuhusiwa kuingia wodini na
yeye kukabidhiwa mtoto ambebe! Akambeba kwa
furaha na bashasha, tabasamu likiupamba uso
wake. Walifanana kama reale kwa ya pili
Waliporuhusiwa na kurejea nyumbani, ndipo akili
zilipomrejea Hussein kwamba alitakuwa kuwa
ndani ya meli ya Liemba muda huu akiwapeleka
abiria Zambia, Zaire na baadae Burundi. Ukweli
huu ukafanya akiliye iingiwe na ganzi.
Aliwafamu waajiri wake vizuri sana kosa dogo tu la
kutosafisha sakafu vizuri lingeweza kukugharimu
kibarua. Au wizi wa mali ya shirika wakati chombo
kikiwa safarini, hukumu yake ilikuwa kutoswa
baharini na kupoteza maisha yako.
Akajifikiria yeye!
Meli ilitakiwa kuondoa saa mbili kamili asubuhi.
Inapeleka abiria. Abiria waliolipa pesa zao, pesa
ambazo zinampa yeye mshahara. Mpaka muda
huu saa nane mchana yeye alikuwa hajatokea
bandarini
Masaa sita mbele!
Akajipeleka ofisini kama ambavyo mbwa hujipeleka
mbele ya chatu tayari kuliwa! Yeye akiamini
kwamba alikuwa na sababu ya msingi. Sababu ya
kuokoa maisha ya mkewe na maisha ya mwanae.
* * *