Dam55
JF-Expert Member
- Oct 8, 2015
- 5,592
- 11,831
RIWAYA: MAUAJI YA KASISI
MTUNZI: richard MWAMBE
Simu: +255 766 974865
UTANGULIZI
MAUAJI YA KASISI
© Richard Richard Mwambe
Ni kizaazaa katika jiji la Nairobi, Kasisi wa kanisa katoliki anauawa katika lango kuu la kuingilia kanisani hapo mapema alfajiri. Sajini Maria na wasaidizi wake wanaingia kazini kuwasaka wauaji.
Nyuma ya pazia la mauaji hayo, jasusi linalotafutwa na idara mbalimbali za usalama duniani ikiwemo ile ya Tanzania (TSA), Bill Van Getgand, anahusishwa na mauaji hayo kwa kuwakodi majambazi ambao anawalipa pesa nyingi kumuua kasisi huyo na kisha kuiba monstrance iliyotoka makao makuu ya kanisa hilo, Vatican, kwa ajili ya adhimisho la jubilee ya miaka 100 ya Ukristo nchini Kenya.
Idara mbalimbali za usalama duniani ikiwemo ile ya Tanzania zinatambua uwepo wa jasusi huyo, hivyo msako unaanza ndani ya jiji la Nairobi na viunga vyake.
Kamanda Amata anajikuta tena katika sakata hili gumu ambalo linaihatarisha kazi yake na maisha yake kwa ujumla. Anarudishwa Tanzania akiwa hoi, hajitambui. Anapopata fahamu anaamua kumrudia jasusi huyo ili kumfunza adabu wakati huo akiwa hatambuliki na idara yake ya usalama.
Bill anatoroka baada ya kuipata ile monstrance na kuwaua walio jirani nae ili wasije kutoa siri endapo watajikuta mikononi mwa polisi. Baada ya kazi nzuri ya Kamanda Amata mpaka kugundua ni wapi jasusi huyo yupo, idara yake inamrudisha kazini na kumtuma ama kumkamata au kumuua kabisa jasusi huyo anayesumbua dunia.
Ndani ya mji wa Aachen, Ujerumani Kamanda Amata anafanya kazi ngumu akipata vikwazo kutoka shirika la upelelezi la USA…. Nini kilijiri huko Ujerumani?
Soma riwaya hii tamu MAUAJI YA KASISI na mwenyewe utasema hakika hii ni riwaya kali kuliko zote…
*****************************************************
SEHEMU YA KWANZA
1
HOLY FAMILY BASILICA
NAIROBI – saa 01:00 asubuhi
HAKUNA mtu aliyeamini anachokiona mbele yake, kila aliyepita njia alitikisa kichwa na wengine kuangusha machozi. Polisi kutoka kituo cha kati cha Nairobi walikuwa hapo mbele ya kanisa hilo kubwa wakifanya uchunguzi wa hili na lile. Mwili usio na uhai ulikuwa umelala chini na majeraha makubwa kifuani yakiwa yameganda damu nzito. Hakuna asiyejua mwili ule ni wa nani, kila aliyepita alisikitika, wengine hata walighairisha safari zao za kazini, vilio vilitawala eneo lile. Kila mtu alionekana kuguswa kwa namna moja au nyingine na mauaji ya Kasisi huyu wa kanisa la Roman Catholic, Rev Fr Frederick Gichuru, hakuna aliyejua kwa nini na ni nani aliyetekeleza mauaji haya ya kinyama. Baada ya kumsachi hakuna cha ziada walichokikuta katika kanzu ya kasisi huyo zaidi ya rozari iliyokuwa mkononi mwake.
“Bila shaka alikuwa katika sala zake za asubuhi” sauti ya kukwaruza kutoka kwa koplo Otholong’ong’o ilipenya sikioni mwa sajenti Maria Kariuki ambaye kwa muda huo alikuwa bado amepigwa na butwaa. Sajenti Maria alisikitika na kujutia nafsi yake, alijiona kama mwenye makosa mbele ya Mungu kwa kifo hicho.
“Ndiyo, afande, daima asubuhi kabla ya misa makasisi wa kikatoliki huwa na wajibu wa kusali kwanza wao weyewe” Sajenti Maria alimjibu koplo Otholong’ong’o huku ukungu mzito ukimtoka kinywani mwake kuashiria baridi kali ya mwezi wa sita hapo Nairobi. Bado sajenti Maria alikuwa kajiinamia jirani kabisa na mwili ule akiuangalia kwa makini jinsi ulivyoharibiwa kwa risasi, maganda saba ya Colt 45 yalikuwa mkononi mwake, huku akiyarusharusha alijinyanyua taratibu na kuamuru mwili ule uondolewe na kupelekwa chumba cha maiti cha hospitali ya rufaa.
§§§§§
Inspekta Simon Saitoti alimkazia macho sajenti Maria aliyekuwa ameketi mbele yake akiwa na jalada moja la khaki lililoandikwa juu ‘MAUAJI YA KASISI’, alionekana kama mtu ambaye haelewi anachoelezwa, alilivuta jalada lile na kuliperuzi kurasa zake chache kwa dakika kadhaa, kisha akainua macho yake kutazama ukutani ambako kulipambwa kwa picha ya muasisi wa taifa hilo, hayati Jomo Kenyatta.
“Umesema paroko wa kanisa hilo hamjamkuta, sivyo?” Inspekta Saitoti alimtwanga swali sajenti Maria.
“Ndiyo afande, na tulipowauliza masista walisema kuwa kawaida wanakuwa na zamu ya kufanya misa za asubuhi vigangoni, hivyo paroko alikuwa amekwenda kigangoni” Maria alijibu kwa ukakamavu wa kipolisi.
“Ok, mauaji kama haya hayajawahi kutokea hapa kwetu hii ni mara ya kwanza, na naomba sana iwe mara ya mwisho, endelea kufanya uchunguzi wa tukio hili kwa kina ukishirikiana na koplo Otholong’ong’o na mnipe taarifa za kina, ili tuwatie mbaroni wauaji.”
“Sawa afande” sajenti Maria alisimama na kurudi nyuma hatua mbili na kupiga saluti ikiwa ni kitendo cha kuonesha heshima kwa mkubwa wake kadiri ya nidhamu za kipolisi.
§§§§§
Kijua cha haja kililing’aza jiji kubwa la Nairobi, jiji lenye pilikapilika za kila aina katika ukanda wa Afrika ya Mashariki. Watu walionekana wakitembea na kuvuka barabara kwa haraka haraka kuashiria kuwa ukichelewa tu matatu itakugonga. Bado hali ya ubaridi ilikuwa ikiendelea na kila mtu alionekana kujidhatiti kwa hali hiyo.
Kwenye kituo kimoja cha basi, mwanaume mmoja mrefu alikua amesimama akisubiri matatu, mara tu matatu moja ikafika na muziki mkubwa ndani yake, akaikaribia na kupanda ndani yake, mkononi alikuwa na mfuko wa plastiki ulioandikwa UCHUMI, bila shaka alikuwa akitoka supermarket, safari yake kwa matatu hiyo iliishia katika kitongoji cha Uthiru Kenoo barabara kuu ya kwenda Uganda. Kwa mwendo wa wastani alivuka kwa kupitia daraja kubwa na kufika upande wa pili wa barabara hiyo ambapo kuna biashara nyingi, aliliendea gari aina ya Hammer lililokuwa limepaki hapo, ndani yake hakukuonesha dalili yoyote ya kuwapo mtu, alifungua mlango kwa kidubwasha maalum na kuuweka ule mfuko katika kiti cha mbele kisha akatokomea kusikojulikana.
Takribani nusu saa hakuna aliyeisogelea gari ile, mara akaja mtu mwingine mnene wa haja pamoja na mwanamke mmoja mrefu na mwenye mwii ulioumbika vizuri, wakaingia ndani ya gari ile na kujifungia milango.
“Shit, washakosea tena” alisikika Yule mtu mnene akimwambia Yule mwanamke
“Nini tena?”
“Hawako makini na kazi yao, tunawalipa pesa nyingi lakini hawajui nini cha kufanya, nguruwe wakubwa hawa”
“Kwani nini?” Yule mwanamke alizidi kudadisi
“Ah, we yaache tu, hutakiwi kujua”
“Aaa jamani, yani umelala na mimi umenambia vingapi mpaka hili usinambie?”
“Mambo ya kazi haya, achana nayo”.
Ile gari ilitiwa moto na kurudi mjini, hakuna ambaye angekaa bila kulitupia macho gari hilo kwa jinsi lilivyo na uzuri wa aina yake na gharama yake ndiyo iliyotia kiwewe.
Moja kwa moja gari ile ilisimama karibu kabisa na mtaa wa Koinange, mtaa unaosifika kwa machangudoa hapo Nairobi.
“Nitakucheki usiku twende club” mtu mnene mwenye asili ya kihindi alimwambia Yule mwananmke na kumpa noti za shilingi elfu moja moja tano za Kikenya.
§§§§§
Askofu mkuu wa jimbo kuu la Nairobi, Mhashamu Gregory Julius Maina, akiwa ofisini kwake alishikwa na huzuni kubwa kwa habari ya mauaji ya Fr Gichuru, alimlilia na kumuombea lakini hakujua ni nini hasa chanzo cha kifo hicho. Alitafakari na kuumiza kichwa, kisha akainua macho yake na kutazama jopo lile la makasisi lililokuwa mbele yake, kila mmoja alikuwa ama akiangusha au akijifuta machozi, ukumbi wa parokia ya Maria Consolatha katika eneo la Westland ulikuwa umetulia kimya kabisa kana kwamba hakukuwa na watu ndani yake.
“Nawasalimu katika jina la Bwana” Askofu aliwasalimu makasisi wale wapatao kama mia mbili weupe kwa weusi.
“Amen” waliitikia.
“Nina masikitiko moyoni, kuwatangazia rasmi kifo cha kasisi mwenzetu padre Frederick Gichuru, paroko msaidizi wa parokia ya Familia Takatifu, kilichotokea leo alfajiri kwa kupigwa risasi tatu kifuani na kupoteza uhai papo hapo” alifuta machozi na kukaa kimya kidogo, kisha akaendelea “Tunalaani vikali kabisa mauaji haya yasiyo na sababu inayoeleweka, hatuna cha kusema zaidi ila sisi kama kanisa tunaiomba serikali na vyombo vyake vya dola vifanye kazi ya kuwatia nguvuni wote wanaohusika, na tunawaomba raia wema wanaojua tetesi yoyote ya kifo hiki kutoa taarifa polisi au hata kwetu ili kusaidia katika kupambana na kadhia hii. Zaidi ya yote Bwana awasamehe kwa maana hawajui watendalo. Ibada ya mazishi itafanyika keshokutwa katika Basilica la Familia Takatifu” alimaliza Askofu kutoa tamko kwa niaba ya kanisa, kisha kuwapatia Baraka na wote wakatawanyika.
“Baba, pole kwa msiba” Kasisi mmoja alimsalimu paroko wa Basilica la Familia Takatifu ambaye msaidizi wake ndiye aliyeuawa asubuhi hiyo.
“Tumeshapoa, Mungu mwenyewe anajua”
Mara gari ya polisi aina ya Land Cruiser iliingia katika viwanja vya kanisa hilo la Consolata, sajenti Maria alikuwa wa kwanza kuteremka, akiwa ndani ya suruali yake ya buluu na shati la buluu bahari alipendeza kwelikweli. Alifanya juu chini kumpata Padre Joe Smith, raia wa Marekani ambaye ni paroko wa Basilica lililotokea mauaji, alipompata alimuomba kuongea naye machache na wote wakaelekea katika ofisi ya parokia hapo Consolatha.
“Pole sana baba kwa msiba, naitwa sajenti Maria kutoka kituo cha polisi cha kati Nairobi”
“Asante, tumeshapoa” alijibu Fr Joe Smith kwa Kiswahili chake kinachopendwa na wengi hasa anapotoa mahubiri.
“Wakati tukio linatokea, wewe ulikuwa wapi asubuhi hiyo?”
“Mimi nilikuwa nimekwenda kufanya misa ya asubuhi kigangoni”
“Siku hiyo ni wewe ulitakiwa uende kigangoni?”
“Hapana, kadiri ya ratiba siku hiyo haikuwa zamu yangu”
“Enhe sasa ilikuwaje ukaenda?”
“Fr Gichuru, usiku wa jana alinambia kuwa yeye hajisikii vizuri, hivyo angependa kubaki parokiani” alimjibu sajenti Maria ambaye alionekana kuandika vitu Fulani kwenye kitabu chake.
“Je unafahamu lolote kama marehemu alikuwa na ugomvi na mtu, au hali yoyote tofauti iliyokuwa katika maeneo yenu kama wachungaji?”
“Kwa kweli katika siku hizi, kumekuwa na mambo ya ajabu kabisa, kuna watu walikuwa wanakuja sana pale parokiani na kuuliza mambo mengi kwa watoto watumishi, wakati Fulani tulimkuta mtu anapekua Sacristia, walipomuuliza akawachapa makofi.”
“Mlichukua hatua gani?”
“Niwaulize ninyi polisi, mimi nilipiga simu polisi na mkaahidi kuja kufanyia uchunguzi lakini bho! Sikuwaona”
“Sawa, msaidizi wako alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtu yeyote awe sista au mwingine yeyote?”
Fr Joe alishtuka kidogo kwa swali hilo. Sajenti Maria akatoa tabasamu lake lisilo nahisia hata kidogo mbele ya watu.
“Mbona umeshtuka baba?”
“Eh nikikuuliza wewe kama una mahusiano na kasisi hautashtuka?” wote wakacheka kisha Joe akaendelea “Hakuna kitu kama hicho, kama kipo basi mimi sijui”
“Haya, asante sana baba, kama nikikuhitaji nitakutafuta” wakapeana mikono na kuagana.
Sista Rose alikuwa akibubujikwa na machozi mbele ya sajenti Maria.
“Usilie Sista, ni maswali machache tu nataka kukuuliza”
“Sawa afande”
“Wakati mauaji yanatokea wewe ulikuwa wapi?”
“Muda huo mimi nilikuwa natoka nyumbani kwetu naenda kuandaa misa kanisani…
Ilivyokuwa
…Ilikuwa yapata saa kumi na moja na nusu alfajiri, sista Rose alikuwa na zamu ya kwenda kuandaa misa, aliamka na kujiandaa, kisha akiwa ndani ya mavazi ya kitawa alitoka nje ya nyumba ‘coventi’ yao na kwa mwendo wa taribu na rozari yake mkononi alikatisha kauwanja kanakotenganisha nyumba yao na kanisa, mara alisimama ghafla moyo wake ulifanya paaah! Hakujua kwa nini, kwa mbali alimuona Fr Gichuru akiingia kwenye uwanja wa kanisa hilo akiwa kwenye vazi lake jeusi na kofia nyeusi yenye nyoya katikati, alivaa kikasisi hasa na si mara nyingi kuonekana katika mavazi haya. Alikuwa akitembea taratibu na mara walikutana na sista Rose katikati ya uwanja, wakasalimiana kwa ishara lakini Fr Gichuru alibaki kasimama akimwangalia sista Rose, akamuonesha ishara ya kuwa ainamishe kichwa chake, sista Rose akafanya hivyo na Fr Gichuru akamuwekea mikono kichwani kumbariki, mara mwanga wa taa za gari ukawamulika kutoka getini, hakuna liyejua ni gari ya nani, Fr Gichuru akamuacha Sr Rose aendelee na shughuli yake yeye akaliendea geti…
Sista Rose alikuwa kajibanza kwenye ua kubwa lililo karibu kabisa na mlango wa kuingilia sakristia, akiangalia kinachoendelea, baada ya mabishano mafupi kati ya Fr Gichuru na wale jamaa waliokuja na ile gari mara alishuhudia kasisi yule akianguka chini kwa kishindo na sauti ya kike iliamuru wengine kupanda garini na kuondoka kwa kasi. Sista Rose alibaki akitetemeka huku machozi yakimwagika na si kumbubujika, alishindwa afanye nini, awaamshe wenzake au aende kumsaidia Fr Gichuru, alikuwa njia panda hakujua afanye nini. Gari ile ilipoondoka alirudi nyumbani kwao akilia na kuwapa taarifa wenzake ambao wote waliamka na kwenda kuona tukio hilo kisha kupiga simu polisi na kwa paroko ambaye alikuwa ameenda kigangoni kwa misa ya alfajiri…
“Poleni kwa msiba huo mzito” sajenti Maria alitoa pole akiwa na macho makavu kabisa, “Labda sista niambie, unaweza kukumbuka aina ya gari walilokuja nalo?”
“Kwa kweli ni shida kulikumbuka kwa kuwa kulikuwa na giza na mi nilikuwa mbali kidogo” sista alijibu.
“Kipi cha pekee unachokumbuka katika tukio hilo?”
“Sauti ya mwanamke iliyokuwa ikimhimiza mwenzake kumaliza kazi, nilisikia wakitamka jina ‘Black Cheetah’” alimaliza na kutungua kilio.
“Ok waweza kwenda tutakapokuhitaji tutakupa taarifa.
§§§§§
Black Cheetah, jambazi sugu linalotafutwa na polisi ukanda wote wa Africa Mashariki, linajikuta katika sakata jipya, sakata la mauaji ya kasisi. Kila mtu aliamini kuwa jambazi hilo si bure tu bali linatumia hata nguvu za giza kwa jinsi linavyoweza kuwatoroka polisi katika mazingira ya kutatanisha hata wenyewe kushindwa kujielewa inakuwakuwaje. Hakuna aliyekuwa halijui jina hili, si mtoto wala mtu mzima, jina la Black Cheetah halikuisha midomoni mwao.
Sajenti Maria alishtushwa kusikia jina hilo likitajwa na sista Rose kuwa aliisikia sauti ya kike ikilitamka katika tukio hilo. Alitafakari akaona kibarua hicho si cha kitoto ni kucheza na mtu au watu waliokomaa kwenye taaluma.
Black Cheetah, kama anavyojiita ni kijana mtukutu, mkakamavu, muasi aliyetoroka katika kundi lao la M23 huko mashariki mwa Congo, aliyetokea kuwa jambazi sugu na tishio katika ukanda wote wa Afrika ya mashariki, alikuwa akikodiwa na matajiri wakubwa kutekeleza mauaji au wizi wa kutumia silaha. Mara kadhaa ameshahusishwa na wizi wa benki uliotokea Dar es salaam Tanzania miaka michache iliyopita, mlipuko wa bomu uliotokea Kampala wakati watu wakiangalia mpira na matukio mengi yaliyotukia huko Kenya ambayo hata hatuwezi kuyaainisha hapa, kwa ujumla alikuwa gaidi.
Mwezi mmoja uliopita
Ngong Hills Hotel-Nairobi
GARI AINA ya Hammer nyeusi ilisogea taratibu katika maegesho ya hoteli ya Ngong Hills, watu watatu, wanaume, wakashuka wakiwa ndani ya suti nyeusi zilizotanguliwa na shati nyeupe, mmoja kati yao mwenye mwili mnene alikuwa akitembea kwa msaada wa fimbo maalum, taratibu waliingia hotelini hapo na moja kwa moja wakaelekea sehemu ya chakula na kuchukua meza yenye viti vine na kuketi, kiti kimoja kilibaki wazi wakaagiza vyakula na vinywaji na kuanza maongezi yao. Maongezi yaliendelea na baada ya muda kidogo kijana mmoja aliingia mahali pale akiwa kavalia koti kubwa la bluu nyeusi akiwa na kofia kubwa aina ya pama, kwa hatua za maringo aliijongea meza hiyo, kila mtu alimuangalia kwa mwendo wake hususan camera za usalama. Alifika katika meza ile na kuvuta kiti kimoja kilichobaki kikimsubiri yeye, akaketi na kuiweka bilauri yake vizuri kabla ya kuimiminia kinywaji kilichokuwa hapo.
“Yes, Cheetah…” yule bwana anaetembea kwa msaada wa fimbo alimkaribisha
“Nimeitika wito wako, bwana Bill” Cheetah alijibu.
“Vizuri, hawa ni wadau wenzangu ambao sote tumekuita ili tukupe kazi maalum” aliendelea
“Nawasikiliza”
“Kuna kazi ndogo tunataka utufanyie” alizungumza bwana Wambugu, akajikohoza na kuendelea “Tunataka kitu kinachoitwa Monstrance, kimehifadhiwa katika kanisa kuu la Familia Takatifu hapa Nairobi, of course ni kazi ndogo tu”
“Hakuna kazi ndogo kama itahitaji kumwaga damu, hasa damu ya watu wasio na hatia” Cheetah alimjibu Wambugu
“No! hatumwagi damu, ni kujua ilipo na kuichukua basi”
“Unafikiri tutaipata kwa urahisi kama unavyofikiria? Maana ingekuwa hivyo basi hata wewe ungeenda pale na kuichukua, lakini kama umeniita mimi maana yake ni kwamba hiyo si kazi ndogo kwa vyovyote lazima vyuma vitaongea” Cheetah alimaliza kauli yake na kuinua bilauri iliyojaa kilevi na kujimiminia kinywani mwake baada ya kulishuighulikia pande la nyama lililokuwa ndani ya sahani hiyo.
“Hilo nalo neno bwana Cheetah. By the way wewe utajua la kufanya, sisi tunachotaka ni Monstrance basi” alimaliza bwana Wambugu.
“Ok, tusipoteze muda, mimi nitaunda kikosi kazi kitakachoweza kufanikisha kazi hiyo, lakini mjue kule ni kanisani, wale makasisi wana mazindiko yao, hivyo lazima mnipatie fedha iliyotakata”
“Ha ha ha ha ha hilo usitie shaka bwanaaa bwana Cheetah” cheko la kivivu lilimtoka yule bwana anyetembea kwa fimbo, kisha akainua simu yake na kubofya namba kadhaa, punde tu vijana wawili waliingia pamwe na briefcase ndogo mkononi, ikawekwa mezani, kwa ishara ya mkono ya mkono yule bwana alimuomba Wambugu kuifungua, baada ya kuzungusha vijinamba Fulani mara yenyewe ilifyatuka kuashiria kuwa kilichopo kiljaa ndani yake kwa kukandamizwa hasa. Naam manoti yenye sura za Moi na Kenyatta yalipangwa na kubanwa katika mabandali kibao, Black Cheetah macho yalimtoka pima.
“Ukifanikisha kazi basi hata briefcase hii ni mali yako” yule bwana alizungumza kivivu.
Black Cheetah alitikisa kichwa juu chini juu chini kuashiria amekubaliana nao. Kwa kuanzia alipewa mabandali kadhaa katika mfuko wa plastiki. Waliagana wane hao na Cheetah akaondoka zake akiwaacha wao wakiendelea kutumbua mavyakula yaliyojaa mezani hapo.
Katika maegesho ya magari, Cheetah aliisogelea gari yake na kusimama kidogo kisha akaangalia uku na huku, hakuona yeyote wala chochote cha kushuku, akaingia na kukaa nyuma ya usukani, milango ikafungwa na vyoo vyote vikabaki juu. Aliufungu ule mfuko wa karatasi na kuhesabu burungutu zile, si haba takribani laki mbili za Kenya, alikenua kwa furaha na kulazimisha tabasamu ambalo halikuendani na uso wake khasilan. Alitia gia na kuyaacha maegesho, baada ya kulivuka geti moja kwa moja aliningia barabara ya Ngong na kurudi katikati ya jiji la Nairobi.
“Hivi unafikiri tutafanikiwa kuipata?”Wambugu alimwuliza yule bwana anyetembelea fimbo
“Ha ha ha ha Wambugu unanichekesha sana, kazi iko kwa Cheetah lazima atararua mpaka tuipate, na tukishaitia mkononi yule Don kule Ujerumani atatukatisha kwa pesa nyingi, si ya kitoto” aliongea kwa sauti yake ya kivivu huku mdomoni akitafuna vyakula aina aina.
“Don!” Wambugu alishangaa
“Yeah, Don, anaitwa Don Fredrick Schurmann, ni tajiri sana katika mji wa Achen, yeye ndiye anayetaka hiyo Monstrance, amesema tukiifikisha mikononi mwake tutapata pesa nyingi sana, ha ha ha ha !” alimaliza kwa kucheka na kunyanyua bilauri yake iliyojaa mnvinyo wa Sant Raphael.
§§§§§
Katika bar kubwa ya Dagoreti Corner super pub, watu walijaa sana wakiburudika kwa vinywaji, nyama choma huku muziki laini wa The Mushroom ukisikika kutoka katika spika kubwa zilizozunguka eneo hilo. Hakuna aliyefikiria kesho kila mmoja alijiachia kwa starehe zake alizoziona kuwa zinamfaa, ilimradi siku ilipita katika mtindo huo. Katika kona moja ya pub hiyo watu watatu waliketi katika mtindo wa mzunguko mmoja wao alikuwa mwanamke walionekana kana kwamba wana mazungumzo mazito sana, hivyo hakuna mtu ambaye alisogelea eneo lile zaidi ya mhudumu wa pub hiyo, naye alikuja tu kuleta alichoagizwa na kuondoka zake.
“Ndiyo vijana, kuna kazi ya kuifanya haraka iwezekanavyo” Cheetah alianzisha mazungumzo.
“Tunakusikia mkuu” sauti pekee ya kike iliiitikia kauli hiyo.
“Tunatakiwa kuchukua mzigo pale Holy Family Basilica”
“Mapesa mangapi tukachukue?” aliuliza kijana mwingine aliyeketi hapo.
“Siyo pesa Bwana Gichui, kuna kitu kinaitwa Monstrance, mnakijua?” Cheetah aliwauliza na wote wakatazamana.
“Monstrance!?” Mellina Wanjiku alishtuka na kujishika kifua kwa mshangao.
“Unashtuka nini, unaijua?” Cheetah aliuliza, na yeye alionekana kushtuka kidogo na kuanza kujiuliza kama kapokea mbuzi kwenye gunia safari hii.
“Naijua Monstrance, ni chombo kitakatifu sana, kukishika kwa hila inaweza kuwa matatizo kwetu” Mellina alijibu kwa upole sana, akatulia kidogo kisha akaendelea “Pamoja na ujambazi ninaoufanya sikuwa kufikiri kuligeukia kanisa, kuna nini kwenye Monstrance hiyo?” aliuliza Mellina
“Ah vile vitu vya wakatoliki huwa vinatengenezwa kwa dhahabu tu, itakuwa ndiyo wanayoitaka” alijibu Gichui.
Black Cheetah alijikuta kwenye mtihani mgumu, kama kuna vitu aliviogopa ni miujiza ya Kimungu ambayo mara nyingi aliisoma kati vitabu vitakatifu, mtihani mkubwa! Alijiona amefanya ujinga kutokuuliza nini kilichomo katika monstrance hiyo, je kama wakizikuta nyingi ni ipi ya kuichukua, utata!
“Cheetah!” aliita Mellina.
Black Cheetah alishtushwa na wito huo kutoka katika lindi la mawazo, akawatazama wanakikundi wenzake ambao yeye aliona wangefaa kwa kazi hiyo lakini sasa walimfanya hata yeye kushikwa na wasiwasi.
“Ok, tunafanya kazi au hatufanyi tuchague moja” aliwapa mtego. Baada ya kutafakari mara mbili mara tatu wote waliamua kuingia kazini kuisaka hiyo monstrance.
ITAENDELEA...
MTUNZI: richard MWAMBE
Simu: +255 766 974865
UTANGULIZI
MAUAJI YA KASISI
© Richard Richard Mwambe
Ni kizaazaa katika jiji la Nairobi, Kasisi wa kanisa katoliki anauawa katika lango kuu la kuingilia kanisani hapo mapema alfajiri. Sajini Maria na wasaidizi wake wanaingia kazini kuwasaka wauaji.
Nyuma ya pazia la mauaji hayo, jasusi linalotafutwa na idara mbalimbali za usalama duniani ikiwemo ile ya Tanzania (TSA), Bill Van Getgand, anahusishwa na mauaji hayo kwa kuwakodi majambazi ambao anawalipa pesa nyingi kumuua kasisi huyo na kisha kuiba monstrance iliyotoka makao makuu ya kanisa hilo, Vatican, kwa ajili ya adhimisho la jubilee ya miaka 100 ya Ukristo nchini Kenya.
Idara mbalimbali za usalama duniani ikiwemo ile ya Tanzania zinatambua uwepo wa jasusi huyo, hivyo msako unaanza ndani ya jiji la Nairobi na viunga vyake.
Kamanda Amata anajikuta tena katika sakata hili gumu ambalo linaihatarisha kazi yake na maisha yake kwa ujumla. Anarudishwa Tanzania akiwa hoi, hajitambui. Anapopata fahamu anaamua kumrudia jasusi huyo ili kumfunza adabu wakati huo akiwa hatambuliki na idara yake ya usalama.
Bill anatoroka baada ya kuipata ile monstrance na kuwaua walio jirani nae ili wasije kutoa siri endapo watajikuta mikononi mwa polisi. Baada ya kazi nzuri ya Kamanda Amata mpaka kugundua ni wapi jasusi huyo yupo, idara yake inamrudisha kazini na kumtuma ama kumkamata au kumuua kabisa jasusi huyo anayesumbua dunia.
Ndani ya mji wa Aachen, Ujerumani Kamanda Amata anafanya kazi ngumu akipata vikwazo kutoka shirika la upelelezi la USA…. Nini kilijiri huko Ujerumani?
Soma riwaya hii tamu MAUAJI YA KASISI na mwenyewe utasema hakika hii ni riwaya kali kuliko zote…
*****************************************************
SEHEMU YA KWANZA
1
HOLY FAMILY BASILICA
NAIROBI – saa 01:00 asubuhi
HAKUNA mtu aliyeamini anachokiona mbele yake, kila aliyepita njia alitikisa kichwa na wengine kuangusha machozi. Polisi kutoka kituo cha kati cha Nairobi walikuwa hapo mbele ya kanisa hilo kubwa wakifanya uchunguzi wa hili na lile. Mwili usio na uhai ulikuwa umelala chini na majeraha makubwa kifuani yakiwa yameganda damu nzito. Hakuna asiyejua mwili ule ni wa nani, kila aliyepita alisikitika, wengine hata walighairisha safari zao za kazini, vilio vilitawala eneo lile. Kila mtu alionekana kuguswa kwa namna moja au nyingine na mauaji ya Kasisi huyu wa kanisa la Roman Catholic, Rev Fr Frederick Gichuru, hakuna aliyejua kwa nini na ni nani aliyetekeleza mauaji haya ya kinyama. Baada ya kumsachi hakuna cha ziada walichokikuta katika kanzu ya kasisi huyo zaidi ya rozari iliyokuwa mkononi mwake.
“Bila shaka alikuwa katika sala zake za asubuhi” sauti ya kukwaruza kutoka kwa koplo Otholong’ong’o ilipenya sikioni mwa sajenti Maria Kariuki ambaye kwa muda huo alikuwa bado amepigwa na butwaa. Sajenti Maria alisikitika na kujutia nafsi yake, alijiona kama mwenye makosa mbele ya Mungu kwa kifo hicho.
“Ndiyo, afande, daima asubuhi kabla ya misa makasisi wa kikatoliki huwa na wajibu wa kusali kwanza wao weyewe” Sajenti Maria alimjibu koplo Otholong’ong’o huku ukungu mzito ukimtoka kinywani mwake kuashiria baridi kali ya mwezi wa sita hapo Nairobi. Bado sajenti Maria alikuwa kajiinamia jirani kabisa na mwili ule akiuangalia kwa makini jinsi ulivyoharibiwa kwa risasi, maganda saba ya Colt 45 yalikuwa mkononi mwake, huku akiyarusharusha alijinyanyua taratibu na kuamuru mwili ule uondolewe na kupelekwa chumba cha maiti cha hospitali ya rufaa.
§§§§§
Inspekta Simon Saitoti alimkazia macho sajenti Maria aliyekuwa ameketi mbele yake akiwa na jalada moja la khaki lililoandikwa juu ‘MAUAJI YA KASISI’, alionekana kama mtu ambaye haelewi anachoelezwa, alilivuta jalada lile na kuliperuzi kurasa zake chache kwa dakika kadhaa, kisha akainua macho yake kutazama ukutani ambako kulipambwa kwa picha ya muasisi wa taifa hilo, hayati Jomo Kenyatta.
“Umesema paroko wa kanisa hilo hamjamkuta, sivyo?” Inspekta Saitoti alimtwanga swali sajenti Maria.
“Ndiyo afande, na tulipowauliza masista walisema kuwa kawaida wanakuwa na zamu ya kufanya misa za asubuhi vigangoni, hivyo paroko alikuwa amekwenda kigangoni” Maria alijibu kwa ukakamavu wa kipolisi.
“Ok, mauaji kama haya hayajawahi kutokea hapa kwetu hii ni mara ya kwanza, na naomba sana iwe mara ya mwisho, endelea kufanya uchunguzi wa tukio hili kwa kina ukishirikiana na koplo Otholong’ong’o na mnipe taarifa za kina, ili tuwatie mbaroni wauaji.”
“Sawa afande” sajenti Maria alisimama na kurudi nyuma hatua mbili na kupiga saluti ikiwa ni kitendo cha kuonesha heshima kwa mkubwa wake kadiri ya nidhamu za kipolisi.
§§§§§
Kijua cha haja kililing’aza jiji kubwa la Nairobi, jiji lenye pilikapilika za kila aina katika ukanda wa Afrika ya Mashariki. Watu walionekana wakitembea na kuvuka barabara kwa haraka haraka kuashiria kuwa ukichelewa tu matatu itakugonga. Bado hali ya ubaridi ilikuwa ikiendelea na kila mtu alionekana kujidhatiti kwa hali hiyo.
Kwenye kituo kimoja cha basi, mwanaume mmoja mrefu alikua amesimama akisubiri matatu, mara tu matatu moja ikafika na muziki mkubwa ndani yake, akaikaribia na kupanda ndani yake, mkononi alikuwa na mfuko wa plastiki ulioandikwa UCHUMI, bila shaka alikuwa akitoka supermarket, safari yake kwa matatu hiyo iliishia katika kitongoji cha Uthiru Kenoo barabara kuu ya kwenda Uganda. Kwa mwendo wa wastani alivuka kwa kupitia daraja kubwa na kufika upande wa pili wa barabara hiyo ambapo kuna biashara nyingi, aliliendea gari aina ya Hammer lililokuwa limepaki hapo, ndani yake hakukuonesha dalili yoyote ya kuwapo mtu, alifungua mlango kwa kidubwasha maalum na kuuweka ule mfuko katika kiti cha mbele kisha akatokomea kusikojulikana.
Takribani nusu saa hakuna aliyeisogelea gari ile, mara akaja mtu mwingine mnene wa haja pamoja na mwanamke mmoja mrefu na mwenye mwii ulioumbika vizuri, wakaingia ndani ya gari ile na kujifungia milango.
“Shit, washakosea tena” alisikika Yule mtu mnene akimwambia Yule mwanamke
“Nini tena?”
“Hawako makini na kazi yao, tunawalipa pesa nyingi lakini hawajui nini cha kufanya, nguruwe wakubwa hawa”
“Kwani nini?” Yule mwanamke alizidi kudadisi
“Ah, we yaache tu, hutakiwi kujua”
“Aaa jamani, yani umelala na mimi umenambia vingapi mpaka hili usinambie?”
“Mambo ya kazi haya, achana nayo”.
Ile gari ilitiwa moto na kurudi mjini, hakuna ambaye angekaa bila kulitupia macho gari hilo kwa jinsi lilivyo na uzuri wa aina yake na gharama yake ndiyo iliyotia kiwewe.
Moja kwa moja gari ile ilisimama karibu kabisa na mtaa wa Koinange, mtaa unaosifika kwa machangudoa hapo Nairobi.
“Nitakucheki usiku twende club” mtu mnene mwenye asili ya kihindi alimwambia Yule mwananmke na kumpa noti za shilingi elfu moja moja tano za Kikenya.
§§§§§
Askofu mkuu wa jimbo kuu la Nairobi, Mhashamu Gregory Julius Maina, akiwa ofisini kwake alishikwa na huzuni kubwa kwa habari ya mauaji ya Fr Gichuru, alimlilia na kumuombea lakini hakujua ni nini hasa chanzo cha kifo hicho. Alitafakari na kuumiza kichwa, kisha akainua macho yake na kutazama jopo lile la makasisi lililokuwa mbele yake, kila mmoja alikuwa ama akiangusha au akijifuta machozi, ukumbi wa parokia ya Maria Consolatha katika eneo la Westland ulikuwa umetulia kimya kabisa kana kwamba hakukuwa na watu ndani yake.
“Nawasalimu katika jina la Bwana” Askofu aliwasalimu makasisi wale wapatao kama mia mbili weupe kwa weusi.
“Amen” waliitikia.
“Nina masikitiko moyoni, kuwatangazia rasmi kifo cha kasisi mwenzetu padre Frederick Gichuru, paroko msaidizi wa parokia ya Familia Takatifu, kilichotokea leo alfajiri kwa kupigwa risasi tatu kifuani na kupoteza uhai papo hapo” alifuta machozi na kukaa kimya kidogo, kisha akaendelea “Tunalaani vikali kabisa mauaji haya yasiyo na sababu inayoeleweka, hatuna cha kusema zaidi ila sisi kama kanisa tunaiomba serikali na vyombo vyake vya dola vifanye kazi ya kuwatia nguvuni wote wanaohusika, na tunawaomba raia wema wanaojua tetesi yoyote ya kifo hiki kutoa taarifa polisi au hata kwetu ili kusaidia katika kupambana na kadhia hii. Zaidi ya yote Bwana awasamehe kwa maana hawajui watendalo. Ibada ya mazishi itafanyika keshokutwa katika Basilica la Familia Takatifu” alimaliza Askofu kutoa tamko kwa niaba ya kanisa, kisha kuwapatia Baraka na wote wakatawanyika.
“Baba, pole kwa msiba” Kasisi mmoja alimsalimu paroko wa Basilica la Familia Takatifu ambaye msaidizi wake ndiye aliyeuawa asubuhi hiyo.
“Tumeshapoa, Mungu mwenyewe anajua”
Mara gari ya polisi aina ya Land Cruiser iliingia katika viwanja vya kanisa hilo la Consolata, sajenti Maria alikuwa wa kwanza kuteremka, akiwa ndani ya suruali yake ya buluu na shati la buluu bahari alipendeza kwelikweli. Alifanya juu chini kumpata Padre Joe Smith, raia wa Marekani ambaye ni paroko wa Basilica lililotokea mauaji, alipompata alimuomba kuongea naye machache na wote wakaelekea katika ofisi ya parokia hapo Consolatha.
“Pole sana baba kwa msiba, naitwa sajenti Maria kutoka kituo cha polisi cha kati Nairobi”
“Asante, tumeshapoa” alijibu Fr Joe Smith kwa Kiswahili chake kinachopendwa na wengi hasa anapotoa mahubiri.
“Wakati tukio linatokea, wewe ulikuwa wapi asubuhi hiyo?”
“Mimi nilikuwa nimekwenda kufanya misa ya asubuhi kigangoni”
“Siku hiyo ni wewe ulitakiwa uende kigangoni?”
“Hapana, kadiri ya ratiba siku hiyo haikuwa zamu yangu”
“Enhe sasa ilikuwaje ukaenda?”
“Fr Gichuru, usiku wa jana alinambia kuwa yeye hajisikii vizuri, hivyo angependa kubaki parokiani” alimjibu sajenti Maria ambaye alionekana kuandika vitu Fulani kwenye kitabu chake.
“Je unafahamu lolote kama marehemu alikuwa na ugomvi na mtu, au hali yoyote tofauti iliyokuwa katika maeneo yenu kama wachungaji?”
“Kwa kweli katika siku hizi, kumekuwa na mambo ya ajabu kabisa, kuna watu walikuwa wanakuja sana pale parokiani na kuuliza mambo mengi kwa watoto watumishi, wakati Fulani tulimkuta mtu anapekua Sacristia, walipomuuliza akawachapa makofi.”
“Mlichukua hatua gani?”
“Niwaulize ninyi polisi, mimi nilipiga simu polisi na mkaahidi kuja kufanyia uchunguzi lakini bho! Sikuwaona”
“Sawa, msaidizi wako alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtu yeyote awe sista au mwingine yeyote?”
Fr Joe alishtuka kidogo kwa swali hilo. Sajenti Maria akatoa tabasamu lake lisilo nahisia hata kidogo mbele ya watu.
“Mbona umeshtuka baba?”
“Eh nikikuuliza wewe kama una mahusiano na kasisi hautashtuka?” wote wakacheka kisha Joe akaendelea “Hakuna kitu kama hicho, kama kipo basi mimi sijui”
“Haya, asante sana baba, kama nikikuhitaji nitakutafuta” wakapeana mikono na kuagana.
Sista Rose alikuwa akibubujikwa na machozi mbele ya sajenti Maria.
“Usilie Sista, ni maswali machache tu nataka kukuuliza”
“Sawa afande”
“Wakati mauaji yanatokea wewe ulikuwa wapi?”
“Muda huo mimi nilikuwa natoka nyumbani kwetu naenda kuandaa misa kanisani…
Ilivyokuwa
…Ilikuwa yapata saa kumi na moja na nusu alfajiri, sista Rose alikuwa na zamu ya kwenda kuandaa misa, aliamka na kujiandaa, kisha akiwa ndani ya mavazi ya kitawa alitoka nje ya nyumba ‘coventi’ yao na kwa mwendo wa taribu na rozari yake mkononi alikatisha kauwanja kanakotenganisha nyumba yao na kanisa, mara alisimama ghafla moyo wake ulifanya paaah! Hakujua kwa nini, kwa mbali alimuona Fr Gichuru akiingia kwenye uwanja wa kanisa hilo akiwa kwenye vazi lake jeusi na kofia nyeusi yenye nyoya katikati, alivaa kikasisi hasa na si mara nyingi kuonekana katika mavazi haya. Alikuwa akitembea taratibu na mara walikutana na sista Rose katikati ya uwanja, wakasalimiana kwa ishara lakini Fr Gichuru alibaki kasimama akimwangalia sista Rose, akamuonesha ishara ya kuwa ainamishe kichwa chake, sista Rose akafanya hivyo na Fr Gichuru akamuwekea mikono kichwani kumbariki, mara mwanga wa taa za gari ukawamulika kutoka getini, hakuna liyejua ni gari ya nani, Fr Gichuru akamuacha Sr Rose aendelee na shughuli yake yeye akaliendea geti…
Sista Rose alikuwa kajibanza kwenye ua kubwa lililo karibu kabisa na mlango wa kuingilia sakristia, akiangalia kinachoendelea, baada ya mabishano mafupi kati ya Fr Gichuru na wale jamaa waliokuja na ile gari mara alishuhudia kasisi yule akianguka chini kwa kishindo na sauti ya kike iliamuru wengine kupanda garini na kuondoka kwa kasi. Sista Rose alibaki akitetemeka huku machozi yakimwagika na si kumbubujika, alishindwa afanye nini, awaamshe wenzake au aende kumsaidia Fr Gichuru, alikuwa njia panda hakujua afanye nini. Gari ile ilipoondoka alirudi nyumbani kwao akilia na kuwapa taarifa wenzake ambao wote waliamka na kwenda kuona tukio hilo kisha kupiga simu polisi na kwa paroko ambaye alikuwa ameenda kigangoni kwa misa ya alfajiri…
“Poleni kwa msiba huo mzito” sajenti Maria alitoa pole akiwa na macho makavu kabisa, “Labda sista niambie, unaweza kukumbuka aina ya gari walilokuja nalo?”
“Kwa kweli ni shida kulikumbuka kwa kuwa kulikuwa na giza na mi nilikuwa mbali kidogo” sista alijibu.
“Kipi cha pekee unachokumbuka katika tukio hilo?”
“Sauti ya mwanamke iliyokuwa ikimhimiza mwenzake kumaliza kazi, nilisikia wakitamka jina ‘Black Cheetah’” alimaliza na kutungua kilio.
“Ok waweza kwenda tutakapokuhitaji tutakupa taarifa.
§§§§§
Black Cheetah, jambazi sugu linalotafutwa na polisi ukanda wote wa Africa Mashariki, linajikuta katika sakata jipya, sakata la mauaji ya kasisi. Kila mtu aliamini kuwa jambazi hilo si bure tu bali linatumia hata nguvu za giza kwa jinsi linavyoweza kuwatoroka polisi katika mazingira ya kutatanisha hata wenyewe kushindwa kujielewa inakuwakuwaje. Hakuna aliyekuwa halijui jina hili, si mtoto wala mtu mzima, jina la Black Cheetah halikuisha midomoni mwao.
Sajenti Maria alishtushwa kusikia jina hilo likitajwa na sista Rose kuwa aliisikia sauti ya kike ikilitamka katika tukio hilo. Alitafakari akaona kibarua hicho si cha kitoto ni kucheza na mtu au watu waliokomaa kwenye taaluma.
Black Cheetah, kama anavyojiita ni kijana mtukutu, mkakamavu, muasi aliyetoroka katika kundi lao la M23 huko mashariki mwa Congo, aliyetokea kuwa jambazi sugu na tishio katika ukanda wote wa Afrika ya mashariki, alikuwa akikodiwa na matajiri wakubwa kutekeleza mauaji au wizi wa kutumia silaha. Mara kadhaa ameshahusishwa na wizi wa benki uliotokea Dar es salaam Tanzania miaka michache iliyopita, mlipuko wa bomu uliotokea Kampala wakati watu wakiangalia mpira na matukio mengi yaliyotukia huko Kenya ambayo hata hatuwezi kuyaainisha hapa, kwa ujumla alikuwa gaidi.
Mwezi mmoja uliopita
Ngong Hills Hotel-Nairobi
GARI AINA ya Hammer nyeusi ilisogea taratibu katika maegesho ya hoteli ya Ngong Hills, watu watatu, wanaume, wakashuka wakiwa ndani ya suti nyeusi zilizotanguliwa na shati nyeupe, mmoja kati yao mwenye mwili mnene alikuwa akitembea kwa msaada wa fimbo maalum, taratibu waliingia hotelini hapo na moja kwa moja wakaelekea sehemu ya chakula na kuchukua meza yenye viti vine na kuketi, kiti kimoja kilibaki wazi wakaagiza vyakula na vinywaji na kuanza maongezi yao. Maongezi yaliendelea na baada ya muda kidogo kijana mmoja aliingia mahali pale akiwa kavalia koti kubwa la bluu nyeusi akiwa na kofia kubwa aina ya pama, kwa hatua za maringo aliijongea meza hiyo, kila mtu alimuangalia kwa mwendo wake hususan camera za usalama. Alifika katika meza ile na kuvuta kiti kimoja kilichobaki kikimsubiri yeye, akaketi na kuiweka bilauri yake vizuri kabla ya kuimiminia kinywaji kilichokuwa hapo.
“Yes, Cheetah…” yule bwana anaetembea kwa msaada wa fimbo alimkaribisha
“Nimeitika wito wako, bwana Bill” Cheetah alijibu.
“Vizuri, hawa ni wadau wenzangu ambao sote tumekuita ili tukupe kazi maalum” aliendelea
“Nawasikiliza”
“Kuna kazi ndogo tunataka utufanyie” alizungumza bwana Wambugu, akajikohoza na kuendelea “Tunataka kitu kinachoitwa Monstrance, kimehifadhiwa katika kanisa kuu la Familia Takatifu hapa Nairobi, of course ni kazi ndogo tu”
“Hakuna kazi ndogo kama itahitaji kumwaga damu, hasa damu ya watu wasio na hatia” Cheetah alimjibu Wambugu
“No! hatumwagi damu, ni kujua ilipo na kuichukua basi”
“Unafikiri tutaipata kwa urahisi kama unavyofikiria? Maana ingekuwa hivyo basi hata wewe ungeenda pale na kuichukua, lakini kama umeniita mimi maana yake ni kwamba hiyo si kazi ndogo kwa vyovyote lazima vyuma vitaongea” Cheetah alimaliza kauli yake na kuinua bilauri iliyojaa kilevi na kujimiminia kinywani mwake baada ya kulishuighulikia pande la nyama lililokuwa ndani ya sahani hiyo.
“Hilo nalo neno bwana Cheetah. By the way wewe utajua la kufanya, sisi tunachotaka ni Monstrance basi” alimaliza bwana Wambugu.
“Ok, tusipoteze muda, mimi nitaunda kikosi kazi kitakachoweza kufanikisha kazi hiyo, lakini mjue kule ni kanisani, wale makasisi wana mazindiko yao, hivyo lazima mnipatie fedha iliyotakata”
“Ha ha ha ha ha hilo usitie shaka bwanaaa bwana Cheetah” cheko la kivivu lilimtoka yule bwana anyetembea kwa fimbo, kisha akainua simu yake na kubofya namba kadhaa, punde tu vijana wawili waliingia pamwe na briefcase ndogo mkononi, ikawekwa mezani, kwa ishara ya mkono ya mkono yule bwana alimuomba Wambugu kuifungua, baada ya kuzungusha vijinamba Fulani mara yenyewe ilifyatuka kuashiria kuwa kilichopo kiljaa ndani yake kwa kukandamizwa hasa. Naam manoti yenye sura za Moi na Kenyatta yalipangwa na kubanwa katika mabandali kibao, Black Cheetah macho yalimtoka pima.
“Ukifanikisha kazi basi hata briefcase hii ni mali yako” yule bwana alizungumza kivivu.
Black Cheetah alitikisa kichwa juu chini juu chini kuashiria amekubaliana nao. Kwa kuanzia alipewa mabandali kadhaa katika mfuko wa plastiki. Waliagana wane hao na Cheetah akaondoka zake akiwaacha wao wakiendelea kutumbua mavyakula yaliyojaa mezani hapo.
Katika maegesho ya magari, Cheetah aliisogelea gari yake na kusimama kidogo kisha akaangalia uku na huku, hakuona yeyote wala chochote cha kushuku, akaingia na kukaa nyuma ya usukani, milango ikafungwa na vyoo vyote vikabaki juu. Aliufungu ule mfuko wa karatasi na kuhesabu burungutu zile, si haba takribani laki mbili za Kenya, alikenua kwa furaha na kulazimisha tabasamu ambalo halikuendani na uso wake khasilan. Alitia gia na kuyaacha maegesho, baada ya kulivuka geti moja kwa moja aliningia barabara ya Ngong na kurudi katikati ya jiji la Nairobi.
“Hivi unafikiri tutafanikiwa kuipata?”Wambugu alimwuliza yule bwana anyetembelea fimbo
“Ha ha ha ha Wambugu unanichekesha sana, kazi iko kwa Cheetah lazima atararua mpaka tuipate, na tukishaitia mkononi yule Don kule Ujerumani atatukatisha kwa pesa nyingi, si ya kitoto” aliongea kwa sauti yake ya kivivu huku mdomoni akitafuna vyakula aina aina.
“Don!” Wambugu alishangaa
“Yeah, Don, anaitwa Don Fredrick Schurmann, ni tajiri sana katika mji wa Achen, yeye ndiye anayetaka hiyo Monstrance, amesema tukiifikisha mikononi mwake tutapata pesa nyingi sana, ha ha ha ha !” alimaliza kwa kucheka na kunyanyua bilauri yake iliyojaa mnvinyo wa Sant Raphael.
§§§§§
Katika bar kubwa ya Dagoreti Corner super pub, watu walijaa sana wakiburudika kwa vinywaji, nyama choma huku muziki laini wa The Mushroom ukisikika kutoka katika spika kubwa zilizozunguka eneo hilo. Hakuna aliyefikiria kesho kila mmoja alijiachia kwa starehe zake alizoziona kuwa zinamfaa, ilimradi siku ilipita katika mtindo huo. Katika kona moja ya pub hiyo watu watatu waliketi katika mtindo wa mzunguko mmoja wao alikuwa mwanamke walionekana kana kwamba wana mazungumzo mazito sana, hivyo hakuna mtu ambaye alisogelea eneo lile zaidi ya mhudumu wa pub hiyo, naye alikuja tu kuleta alichoagizwa na kuondoka zake.
“Ndiyo vijana, kuna kazi ya kuifanya haraka iwezekanavyo” Cheetah alianzisha mazungumzo.
“Tunakusikia mkuu” sauti pekee ya kike iliiitikia kauli hiyo.
“Tunatakiwa kuchukua mzigo pale Holy Family Basilica”
“Mapesa mangapi tukachukue?” aliuliza kijana mwingine aliyeketi hapo.
“Siyo pesa Bwana Gichui, kuna kitu kinaitwa Monstrance, mnakijua?” Cheetah aliwauliza na wote wakatazamana.
“Monstrance!?” Mellina Wanjiku alishtuka na kujishika kifua kwa mshangao.
“Unashtuka nini, unaijua?” Cheetah aliuliza, na yeye alionekana kushtuka kidogo na kuanza kujiuliza kama kapokea mbuzi kwenye gunia safari hii.
“Naijua Monstrance, ni chombo kitakatifu sana, kukishika kwa hila inaweza kuwa matatizo kwetu” Mellina alijibu kwa upole sana, akatulia kidogo kisha akaendelea “Pamoja na ujambazi ninaoufanya sikuwa kufikiri kuligeukia kanisa, kuna nini kwenye Monstrance hiyo?” aliuliza Mellina
“Ah vile vitu vya wakatoliki huwa vinatengenezwa kwa dhahabu tu, itakuwa ndiyo wanayoitaka” alijibu Gichui.
Black Cheetah alijikuta kwenye mtihani mgumu, kama kuna vitu aliviogopa ni miujiza ya Kimungu ambayo mara nyingi aliisoma kati vitabu vitakatifu, mtihani mkubwa! Alijiona amefanya ujinga kutokuuliza nini kilichomo katika monstrance hiyo, je kama wakizikuta nyingi ni ipi ya kuichukua, utata!
“Cheetah!” aliita Mellina.
Black Cheetah alishtushwa na wito huo kutoka katika lindi la mawazo, akawatazama wanakikundi wenzake ambao yeye aliona wangefaa kwa kazi hiyo lakini sasa walimfanya hata yeye kushikwa na wasiwasi.
“Ok, tunafanya kazi au hatufanyi tuchague moja” aliwapa mtego. Baada ya kutafakari mara mbili mara tatu wote waliamua kuingia kazini kuisaka hiyo monstrance.
ITAENDELEA...