iddy eba
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 575
- 1,169
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA ISHIRINI
ILIPOISHIA
Inspekta Kobo yu matatani, ana kwa ana na mtutu wa bunduki. Hesabu zake zimeenda ndivyo sivyo na sasa kivumbi kimemgeukia.
ENDELEA!!
Kama alivyoona ndivyo ilivyotokea, yule bwana akafyatua risasi.
Kobo hakutarajia kama angepata nafasi ya kusikia risasi ile ikivuma pembezoni mwa sikio lake.
Lakini hivyo ndivyo ilivyokuwa.
Shabaha iliyumba malikiti.
Kobo akapata muda wa kufumbua ili atazame kama ataweza kubiringita tena ili akwepe kwa mara nyingine tena.
Akayahimiza macho yake kutazama....
Macho yakakutana na kitu cha kutisha, haikuwa risasi ya kawaida... hii ya sasa asingeweza kuikwepa asilani.
Ilikuwa pana sana, hata kama angebiringita kwa kasi kuu bado asingeweza kujinasua.
Inspekta Kobo akasalimu amri kwa kuitanguliza mikono yake kukabiliana na kitu kile kikubwa.
Kilipomkaribia zaidi akayafumba macho yake.
Kikatua juu yake, upepo ukakata!
Kobo akarejea katika ulimwengu wa waliopoteza fahamu wasijue namna ya kuzitafuta.
__________
MIILI miwili ilikuwa imebebana bila kukusudia, yote isiyojiweza na bila budi kujibweteka mwili mmoja juu ya mwingine.
Miili hii ilitazamwa kutokea mbali na vikundi viwili visivyokuwa na majina rasmi ya kuvitambulisha.
Kukosa majina hakukumaanisha ule uwepo ni batili.
"Unahisi bado anapumua yule?" Sauti dadisi ya Zubeda ilimuuliza Nguzu.
"Uhakika pekee ninaoweza kuuthibitisha ni kwamba yule bazazi nimemfyatua barabara katika chembe ya moyo wake..." Alijibu huku akiwa bado na umakini wa hali ya juu.
Kundi la pili lilikuwa katika mfadhaiko, wakati likiamini kuwa limeunyakua ushindi na kilichosalia ni kuvikwa taji mara shambulizi linatoka wasipopajua na kumsambaratisha mwenzao aliyekuwa anangojewa waweze kuondoka eneo lile.
Makundi yote mawili yalibaki katika tahadhari hakuna aliyekuwa tayari kwenda kuwatenganisha wawili wale waliolaliana.
Mmoja akiwa ni mwili na mwenza wake akiwa ni mwili na roho pamoja na fahamu zilizokwenda likizo isiyokuwa na muda maalumu.
"Martin.... bila kujalisha kama mzee Kobo atainuka ama la, bila kujali kama tutabaki hai ama la. Naomba unisamehe mimi kwa yote yaliyotokea" Sauti tulivu ya Zubeda ilipenya katika masikio ya Martin Nguzu.
Hakuitoa silaha yake katika lindo lake katika watu wale wawili waliolaliana mmoja akiwa ni Inspekta Kobo.
"Unavyozungumzia kuwa hai ama la kana kwamba ni pipi ambayo unaweza ukaamua kuimung'unga ama la na isikupunguzie lolote. Uhai unayo thamani kubwa sana usiuongelee kijuu juu hivyo" Akamjibu kwa kumnanga.
Koplo Zubeda akabaki kimya huku hatia ikimsulubu na kujiona yu mkosaji mkubwa sana.
Hakukumbuka kujiuliza ni lipi basi kosa lake?
KUTOKEA upande wa pili, tumaini la ghafla katika pori la mfadhaiko liliibuka, aliyeshuhudia akawasihi na wenzake nao waone.
"Oya...yupo hai aisee... namuona anatikisika" Alisema na kuwavuta wenzake kutazama kwa makini, kweli mwenzao alikuwa anajitikisa.
Ile hulka ya wanadamu waonapo jambo wasilolitarajia hujikuta wakiisahau misingi yao yote na kujikuta katika mkumbo wa liwalo na liwe, haikuwa upande huu badala yake ilikuwa upande wa pili.
Zubeda anayesukumwa na hatia ya kupendwa kwa dhati kisha kuja kumsaliti Inspekta Kobo na hatimaye kumweka katika kitanzi kile ilikuwa inamponza.
Konstebo Nguzu naye alihitaji sana kujua ni nini hatma ya Kobo pamoja na makundi yanayoshambulia yana nia gani.
Hakuamini hata kidogo kuwa yawezekana kabisa kuwa eti chanzo ni yeye tu hadi haya yote yanatokea.
Kama ni yeye kwanini wahukumiwe hata wasiokuwa watu wa ukoo wake?
Wakati akiwaza na kuwazua akaikumbuka sura tulivu ya Kobo iliyojaa hekima na busara siku aliyomuita na kumsihi aachane na Zubeda wake!
Huruma kuu ikamvamia.
Hali hizi ziliwafanya wasisimke walipoona ile miili pale chini ikijitikisa.
Nguzu akamuhakikishia Zubeda kuwa aliyejitikisa ni Kobo si yule hayawani aliyejaribu kumfyatua.
Zubeda hakuamini upesi, Nguzu akajitoa muhanga kwenda kumwokoa Kobo, huku nyuma shughuli ya kulinda usalama wake akaiacha mikononi mwa Zubeda.
"Kiumbe yeyote atakayejaribu kunidhuru, fyatua usifikirie mara mbilimbili. Ule muda utakaotumia kufikiri nd'o muda ambao macho yako yatakishuhudia kifo changu. Hiki cha sasa kitakuwa kifo taslimu." Nguzu alimweleza Zubeda.
Kisha akamkumbatia kwa nguvu sana, akamtazama machoni na kuzungumza kwa sauti tulivu.
"Naitwa Martin Ngengekuzenza Nguzu. Jina langu lina maana kubwa kulikoni uhai wangu... kwa lolote lile nikianguka naomba nifukiwe kwa jina hilo." Akamaliza na kumbusu Zubeda katika papi za midomo yake.
Akaondoka akimwacha Zubeda akipambana machozi yasiyazibe macho yake.
Alihisi lile ni busu na kumbatizi la mwisho kutoka kwa kijana yule machachari.
Umakini ukarejea baada ya Konstebo Nguzu kuingia ukumbi wa vita, Zubeda askari mkakamavu akaishikilia vyema silaha yake, akavuta pumzi na kushusha akajiandaa kukabili kwa lolote kama alivyoelekezwa.
Umbali wa kutoka mlangoni hadi ulipokuwa mwili wa Kobo haukuwa mita nyingi sana, lakini ilikuwa ni zaidi ya kilometa kadhaa kwa Nguzu kutokana na kutokuwa na uhakika ni wapi anaweza kuwepo adui awezaye kuitoa roho yake mara moja.
Akapiga hatua huku uoga ukishamiri katika moyo wake, alijitia ujasiri kwa maneno aliyoelezwa na mzee Majenga kuwa hatakufa kwa sababu mzimu wa babu yake unaishi naye mpaka atakapoitimiza azma yake.
Hatua takribani kama tano kabla hajaufikia ule mzoga juu ya mwili. Kilio kikubwa kikasikika kutokea katika dirisha ambalo alibaki Zubeda kama mlinzi wake wakati akielekea kumkomboa Kobo.
Upesi Nguzu akaiweka vyema silaha yake lakini hakujua ni wapi afyatue kabla hajaisikia sauti kali nyuma yake ikimwamuru kutulia kama alivyo.
Nguzu alikuwa mikononi mwa watu wabaya!
Nini kimejiri kwa Zubeda?? alibaki akijiuliza wakati huu ambapo alimuhitaji sana mwanamama yule ili kuweza kumkomboa.
Kimya! hapakuwa na shambulizi lolote la kumkomboa.
"Taratibu kabisa angusha silaha yako chini, bila kuinama walau sentimita moja" Sauti ikachimba mkwara zaidi.
Nguzu hakusubiri onyo la pili akaiachia bastola yake itue chini naye abaki na Mungu pekee kama mlinzi wake wa haja.
"Wananiua wapuuzi!" alijisemea
"Sogea mbele kwa hatua za taratibu kabisa. Bila shaka sina haja ya kukumbusha kuwa ukifanya upuuzi wowote ule hautakumbuka chanzo cha kifo chako...." sauti ile tulivu inayojiamini iloiendelea kumwongoza Nguzu.
Nguzu akatii!
Alikuwa kama hayawani ama zuzu asiyejua 'a' wala 'ba'. Kifo pekee nd'o kitu ambacho aliwaza kwa wakati huo.
"Shusha mbuyu mwamba...." Sauti tofauti na ile iliyokuwa inamwongoza ilizungumza kwa kukaripia na kuonyesha uharaka.
Mbuyu? Nguzu akajiuliza asijue ni kitu gani kimemaanishwa katika kauli ile tata.
Hakuwa tayari kuuwawa namna ile bila kuimaliza kazi yake, lakini pia hakuwa walau na akili ya ziada ya kujiokoa.
Utajiokoa vipi ungali jirani na mdomo wa bunduki usiokuwa na huruma ukifunguliwa?
"Mpigie tajiri..." Sauti iliyokuwa ya kwanza kumtetemesha Nguzu ilizungumza.
Baada ya sekunde chache, mazungumzo yalisikika upande uliosikika zaidi ulikuwa upande wa kwanza huku aliyepigiwa simu akisikika kwa mbali sana.
Simu haikukatwa iliachwa hewani na hapo Nguzu akarushiwa swali.
"Unaitwa nani? na upo hapa kwa shughuli gani?"
Nguzu akafikiria kuhusu kuongopa kuhusu jina lake, lakini akachagua kucheza karata nyingine.
"Naitwa Martin, nipo hapa kwa ...."
"Martin nani?" Swali lilitupwa, hadi sasa alikuwa hajaziona nyuso za maadui zake.
"Martin Nguzu!" Akamalizia.
"Acha upuuzi, hatuna muda wa kupoteza," alijibu kwa hasira kisha akarejea katika simu yake, "Tajiri... huyu mjinga anasema anaitwa Martin Nguzu. Hana faida kwetu..."
"Naitwa Martin, Konstebo Martin Nguzu. Sijawahi kufa lakini nakijua kifo. Jaribuni kuniua mara ya pili huenda nikakijua kifo" Nguzu akapigilia hofu na utata mwingine. Alikuwa ameupata ujasiri wa hali ya juu sana.
Wale mabwana wawili hawakuelewa ni kipi anachojiamini angali hana silaha na wakiamua ni sekunde moja tu wanammaliza.
Mazungumzo katika simu yakaendelea huku akibaini sasa kuwa mpiga simu alimuhitaji akiwa hai. Lakini hilo si pekee lililomjengea ujasiri.
Kuna jambo la ziada ambalo lilihesabika kwa sekunde kadhaa kabla halijabadilika na kuwa kindumbwendumbwe!
Ilikuwa ghafla sana, Nguzu akaruka upande wa kushoto bila wale watu kumtarajia kama atafanya hivyo.
Palepale milipuko miwili ya risasi ikasikika.
Mayowe ya hofu na maumivu yakasikika.
"Usithubutu walau kujitikisa, maana nitafyatua jicho lako badala ya bega!" Sauti iliyoongea kwa tabu kabisa ilitoa maelekezo.
Bwana aliyekuwa anazungumza na simu akabaki kutulia tuli asiamini kilichokuwa kinatokea.
Inspekta Kobo kutoka katika usingizi wa kifo alikuwa amechota medali zake za ushujaa palepale chini.
Nguzu pekee ndiye aliyeutambua uhai wake, na aliamua kumuamini walipozungumza kwa ishara za macho.
Ishara ambazo ni wao pekee wangeweza kuelewana kwa sababu wamepitia mafunzo ya kijeshi.
Nguzu akajitokeza na kuiwahi ile silaha ambayo ilimponyoka yule aliyesambaratis
hwa na Kobo kwa shabaha moja iliyojikita katika kifua chake moja kwa moja.
"Nahitaji ujibu swali uliloniuliza hapo kabla. Ni nini unafanya hapa na unafanya kwa manufaa ya nani? Niko tofauti kidogo na wewe... sichimbi mkwara huwa natenda. Ukichelewa kunijibu nakuvunja miguu....." Nguzu akiwa anatazama na bwana yule aliyepagawa alizungumza.
Yule bwana akapagawa asiamini anaonana ana kwa ana na Kontebo Martin Nguzu ambaye wanaamini kuwa walimteketeza ndani ya nyumba.
Hakuwa na budi kujieleza vyema kabisa.
Nguzu akashtuka jina la muhusika wa haya lilipotajwa.
Lilikuwa jina refu lakini ubini wa 'KAZEZE' ukamwacha katika namna ya kupigwa butwaa.
Jina ambalo lipo katika kitabu cha babu yake, mzee Florian Ngengekuzenza Nguzu, jina lililosheheni chuki, visasi na unyanyasaji.
Jina hili linasikika tena katika maisha yake.
"Ina maana Joseph Kazeze alikiacha kisasi chake kirithiwe na watoto wake ama?" Nguzu alijikuta akiuliza kwa sauti, lakini asipate mtu sahihi wa kumjibu.
"Zu...Zubeda yupo wapi" Inspekta Kobo akiwa ameketi chini aliuliza kwa sauti ya chini sana, bila shaka alikuwa katika maumivu bado.
Swali lile likamshtua sana Nguzu, alikuwa amesahau kabisa kuwa kuna mlipuko ulikuwa umesikika kabla hajadhibitiwa na mabwana wale waliodai kuwa walikuwa wameagizwa na mkuu wa majeshi mstaafu, Jeremiah Stamford Kazeze.
Kukosa kule utulivu kukaondoka na umakini wake.
Yule mtumwa akamvamia Nguzu upesi na teke kali ambalo liliiondoa silaha yake mkononi.
Akarusha teke la pili ambalo lilielekea kupasua fuvu la kichwa cha Nguzu. Nguzu akawahi kuinama.
Wakati anajiandaa kumkabili akajikuta akikabiliana na madonge ya damu.
Kobo alikuwa amejipima tena umakini wake kama upo sawa.
"Usingemuua Inspekta..."
"Angekuua wewe.... amepitia mafunzo ambayo wewe hujawahi hata kuyaona kwenye luninga.... hata hivyo sijamuua labda aamue kufa mwenyewe tu..."
Hatimaye Inspekta alisimama kwa tabu, wakati huo Nguzu alikuwa ametangulia kwenda kuitambua hali ya afya ya Zubeda ambaye bila shaka alishambuliwa.
Hakika alikuwa amepoteza fahamu, risasi ilikuwa imemkwangua begani na kumtupa ukutani.
Halikuwa jeraha kubwa sana, hata alivyoshtuliwa kwa kumwagiwa maji ilikuwa rahisi kwake kusimama na kutambua kila kilichokuwa kinaendelea.
Kigiza kilikuwa kinaanza kuingia wakati watatu hawa wakiwa wamepata fursa ya kuwa mbali na ile nyumba na walikuwa wameweza kujadili kwa ufupi sana juu ya kisa hiki.
Hakuna aliyegusia suala la mapenzi ya kuchangia, walitazama zaidi uhai na amani yao.
Inspekta akashauri wafanye mchakato wa kuwasiliana na IGP waweze kuupata msaada wa upesi sana dhidi ya Kazeze IGP mstaafu waliyeamini fika kuwa yupo nyuma ya yote haya.
Wakati wao wanafikiria namna ya kuwasiliana na IGP.... ni wakati huohuo IGP mstaafu Kazeze alikuwa yu njiani kuelekea nyumbani kwa IGP.
_________
ILIPOISHIA
Inspekta Kobo yu matatani, ana kwa ana na mtutu wa bunduki. Hesabu zake zimeenda ndivyo sivyo na sasa kivumbi kimemgeukia.
ENDELEA!!
Kama alivyoona ndivyo ilivyotokea, yule bwana akafyatua risasi.
Kobo hakutarajia kama angepata nafasi ya kusikia risasi ile ikivuma pembezoni mwa sikio lake.
Lakini hivyo ndivyo ilivyokuwa.
Shabaha iliyumba malikiti.
Kobo akapata muda wa kufumbua ili atazame kama ataweza kubiringita tena ili akwepe kwa mara nyingine tena.
Akayahimiza macho yake kutazama....
Macho yakakutana na kitu cha kutisha, haikuwa risasi ya kawaida... hii ya sasa asingeweza kuikwepa asilani.
Ilikuwa pana sana, hata kama angebiringita kwa kasi kuu bado asingeweza kujinasua.
Inspekta Kobo akasalimu amri kwa kuitanguliza mikono yake kukabiliana na kitu kile kikubwa.
Kilipomkaribia zaidi akayafumba macho yake.
Kikatua juu yake, upepo ukakata!
Kobo akarejea katika ulimwengu wa waliopoteza fahamu wasijue namna ya kuzitafuta.
__________
MIILI miwili ilikuwa imebebana bila kukusudia, yote isiyojiweza na bila budi kujibweteka mwili mmoja juu ya mwingine.
Miili hii ilitazamwa kutokea mbali na vikundi viwili visivyokuwa na majina rasmi ya kuvitambulisha.
Kukosa majina hakukumaanisha ule uwepo ni batili.
"Unahisi bado anapumua yule?" Sauti dadisi ya Zubeda ilimuuliza Nguzu.
"Uhakika pekee ninaoweza kuuthibitisha ni kwamba yule bazazi nimemfyatua barabara katika chembe ya moyo wake..." Alijibu huku akiwa bado na umakini wa hali ya juu.
Kundi la pili lilikuwa katika mfadhaiko, wakati likiamini kuwa limeunyakua ushindi na kilichosalia ni kuvikwa taji mara shambulizi linatoka wasipopajua na kumsambaratisha mwenzao aliyekuwa anangojewa waweze kuondoka eneo lile.
Makundi yote mawili yalibaki katika tahadhari hakuna aliyekuwa tayari kwenda kuwatenganisha wawili wale waliolaliana.
Mmoja akiwa ni mwili na mwenza wake akiwa ni mwili na roho pamoja na fahamu zilizokwenda likizo isiyokuwa na muda maalumu.
"Martin.... bila kujalisha kama mzee Kobo atainuka ama la, bila kujali kama tutabaki hai ama la. Naomba unisamehe mimi kwa yote yaliyotokea" Sauti tulivu ya Zubeda ilipenya katika masikio ya Martin Nguzu.
Hakuitoa silaha yake katika lindo lake katika watu wale wawili waliolaliana mmoja akiwa ni Inspekta Kobo.
"Unavyozungumzia kuwa hai ama la kana kwamba ni pipi ambayo unaweza ukaamua kuimung'unga ama la na isikupunguzie lolote. Uhai unayo thamani kubwa sana usiuongelee kijuu juu hivyo" Akamjibu kwa kumnanga.
Koplo Zubeda akabaki kimya huku hatia ikimsulubu na kujiona yu mkosaji mkubwa sana.
Hakukumbuka kujiuliza ni lipi basi kosa lake?
KUTOKEA upande wa pili, tumaini la ghafla katika pori la mfadhaiko liliibuka, aliyeshuhudia akawasihi na wenzake nao waone.
"Oya...yupo hai aisee... namuona anatikisika" Alisema na kuwavuta wenzake kutazama kwa makini, kweli mwenzao alikuwa anajitikisa.
Ile hulka ya wanadamu waonapo jambo wasilolitarajia hujikuta wakiisahau misingi yao yote na kujikuta katika mkumbo wa liwalo na liwe, haikuwa upande huu badala yake ilikuwa upande wa pili.
Zubeda anayesukumwa na hatia ya kupendwa kwa dhati kisha kuja kumsaliti Inspekta Kobo na hatimaye kumweka katika kitanzi kile ilikuwa inamponza.
Konstebo Nguzu naye alihitaji sana kujua ni nini hatma ya Kobo pamoja na makundi yanayoshambulia yana nia gani.
Hakuamini hata kidogo kuwa yawezekana kabisa kuwa eti chanzo ni yeye tu hadi haya yote yanatokea.
Kama ni yeye kwanini wahukumiwe hata wasiokuwa watu wa ukoo wake?
Wakati akiwaza na kuwazua akaikumbuka sura tulivu ya Kobo iliyojaa hekima na busara siku aliyomuita na kumsihi aachane na Zubeda wake!
Huruma kuu ikamvamia.
Hali hizi ziliwafanya wasisimke walipoona ile miili pale chini ikijitikisa.
Nguzu akamuhakikishia Zubeda kuwa aliyejitikisa ni Kobo si yule hayawani aliyejaribu kumfyatua.
Zubeda hakuamini upesi, Nguzu akajitoa muhanga kwenda kumwokoa Kobo, huku nyuma shughuli ya kulinda usalama wake akaiacha mikononi mwa Zubeda.
"Kiumbe yeyote atakayejaribu kunidhuru, fyatua usifikirie mara mbilimbili. Ule muda utakaotumia kufikiri nd'o muda ambao macho yako yatakishuhudia kifo changu. Hiki cha sasa kitakuwa kifo taslimu." Nguzu alimweleza Zubeda.
Kisha akamkumbatia kwa nguvu sana, akamtazama machoni na kuzungumza kwa sauti tulivu.
"Naitwa Martin Ngengekuzenza Nguzu. Jina langu lina maana kubwa kulikoni uhai wangu... kwa lolote lile nikianguka naomba nifukiwe kwa jina hilo." Akamaliza na kumbusu Zubeda katika papi za midomo yake.
Akaondoka akimwacha Zubeda akipambana machozi yasiyazibe macho yake.
Alihisi lile ni busu na kumbatizi la mwisho kutoka kwa kijana yule machachari.
Umakini ukarejea baada ya Konstebo Nguzu kuingia ukumbi wa vita, Zubeda askari mkakamavu akaishikilia vyema silaha yake, akavuta pumzi na kushusha akajiandaa kukabili kwa lolote kama alivyoelekezwa.
Umbali wa kutoka mlangoni hadi ulipokuwa mwili wa Kobo haukuwa mita nyingi sana, lakini ilikuwa ni zaidi ya kilometa kadhaa kwa Nguzu kutokana na kutokuwa na uhakika ni wapi anaweza kuwepo adui awezaye kuitoa roho yake mara moja.
Akapiga hatua huku uoga ukishamiri katika moyo wake, alijitia ujasiri kwa maneno aliyoelezwa na mzee Majenga kuwa hatakufa kwa sababu mzimu wa babu yake unaishi naye mpaka atakapoitimiza azma yake.
Hatua takribani kama tano kabla hajaufikia ule mzoga juu ya mwili. Kilio kikubwa kikasikika kutokea katika dirisha ambalo alibaki Zubeda kama mlinzi wake wakati akielekea kumkomboa Kobo.
Upesi Nguzu akaiweka vyema silaha yake lakini hakujua ni wapi afyatue kabla hajaisikia sauti kali nyuma yake ikimwamuru kutulia kama alivyo.
Nguzu alikuwa mikononi mwa watu wabaya!
Nini kimejiri kwa Zubeda?? alibaki akijiuliza wakati huu ambapo alimuhitaji sana mwanamama yule ili kuweza kumkomboa.
Kimya! hapakuwa na shambulizi lolote la kumkomboa.
"Taratibu kabisa angusha silaha yako chini, bila kuinama walau sentimita moja" Sauti ikachimba mkwara zaidi.
Nguzu hakusubiri onyo la pili akaiachia bastola yake itue chini naye abaki na Mungu pekee kama mlinzi wake wa haja.
"Wananiua wapuuzi!" alijisemea
"Sogea mbele kwa hatua za taratibu kabisa. Bila shaka sina haja ya kukumbusha kuwa ukifanya upuuzi wowote ule hautakumbuka chanzo cha kifo chako...." sauti ile tulivu inayojiamini iloiendelea kumwongoza Nguzu.
Nguzu akatii!
Alikuwa kama hayawani ama zuzu asiyejua 'a' wala 'ba'. Kifo pekee nd'o kitu ambacho aliwaza kwa wakati huo.
"Shusha mbuyu mwamba...." Sauti tofauti na ile iliyokuwa inamwongoza ilizungumza kwa kukaripia na kuonyesha uharaka.
Mbuyu? Nguzu akajiuliza asijue ni kitu gani kimemaanishwa katika kauli ile tata.
Hakuwa tayari kuuwawa namna ile bila kuimaliza kazi yake, lakini pia hakuwa walau na akili ya ziada ya kujiokoa.
Utajiokoa vipi ungali jirani na mdomo wa bunduki usiokuwa na huruma ukifunguliwa?
"Mpigie tajiri..." Sauti iliyokuwa ya kwanza kumtetemesha Nguzu ilizungumza.
Baada ya sekunde chache, mazungumzo yalisikika upande uliosikika zaidi ulikuwa upande wa kwanza huku aliyepigiwa simu akisikika kwa mbali sana.
Simu haikukatwa iliachwa hewani na hapo Nguzu akarushiwa swali.
"Unaitwa nani? na upo hapa kwa shughuli gani?"
Nguzu akafikiria kuhusu kuongopa kuhusu jina lake, lakini akachagua kucheza karata nyingine.
"Naitwa Martin, nipo hapa kwa ...."
"Martin nani?" Swali lilitupwa, hadi sasa alikuwa hajaziona nyuso za maadui zake.
"Martin Nguzu!" Akamalizia.
"Acha upuuzi, hatuna muda wa kupoteza," alijibu kwa hasira kisha akarejea katika simu yake, "Tajiri... huyu mjinga anasema anaitwa Martin Nguzu. Hana faida kwetu..."
"Naitwa Martin, Konstebo Martin Nguzu. Sijawahi kufa lakini nakijua kifo. Jaribuni kuniua mara ya pili huenda nikakijua kifo" Nguzu akapigilia hofu na utata mwingine. Alikuwa ameupata ujasiri wa hali ya juu sana.
Wale mabwana wawili hawakuelewa ni kipi anachojiamini angali hana silaha na wakiamua ni sekunde moja tu wanammaliza.
Mazungumzo katika simu yakaendelea huku akibaini sasa kuwa mpiga simu alimuhitaji akiwa hai. Lakini hilo si pekee lililomjengea ujasiri.
Kuna jambo la ziada ambalo lilihesabika kwa sekunde kadhaa kabla halijabadilika na kuwa kindumbwendumbwe!
Ilikuwa ghafla sana, Nguzu akaruka upande wa kushoto bila wale watu kumtarajia kama atafanya hivyo.
Palepale milipuko miwili ya risasi ikasikika.
Mayowe ya hofu na maumivu yakasikika.
"Usithubutu walau kujitikisa, maana nitafyatua jicho lako badala ya bega!" Sauti iliyoongea kwa tabu kabisa ilitoa maelekezo.
Bwana aliyekuwa anazungumza na simu akabaki kutulia tuli asiamini kilichokuwa kinatokea.
Inspekta Kobo kutoka katika usingizi wa kifo alikuwa amechota medali zake za ushujaa palepale chini.
Nguzu pekee ndiye aliyeutambua uhai wake, na aliamua kumuamini walipozungumza kwa ishara za macho.
Ishara ambazo ni wao pekee wangeweza kuelewana kwa sababu wamepitia mafunzo ya kijeshi.
Nguzu akajitokeza na kuiwahi ile silaha ambayo ilimponyoka yule aliyesambaratis
hwa na Kobo kwa shabaha moja iliyojikita katika kifua chake moja kwa moja.
"Nahitaji ujibu swali uliloniuliza hapo kabla. Ni nini unafanya hapa na unafanya kwa manufaa ya nani? Niko tofauti kidogo na wewe... sichimbi mkwara huwa natenda. Ukichelewa kunijibu nakuvunja miguu....." Nguzu akiwa anatazama na bwana yule aliyepagawa alizungumza.
Yule bwana akapagawa asiamini anaonana ana kwa ana na Kontebo Martin Nguzu ambaye wanaamini kuwa walimteketeza ndani ya nyumba.
Hakuwa na budi kujieleza vyema kabisa.
Nguzu akashtuka jina la muhusika wa haya lilipotajwa.
Lilikuwa jina refu lakini ubini wa 'KAZEZE' ukamwacha katika namna ya kupigwa butwaa.
Jina ambalo lipo katika kitabu cha babu yake, mzee Florian Ngengekuzenza Nguzu, jina lililosheheni chuki, visasi na unyanyasaji.
Jina hili linasikika tena katika maisha yake.
"Ina maana Joseph Kazeze alikiacha kisasi chake kirithiwe na watoto wake ama?" Nguzu alijikuta akiuliza kwa sauti, lakini asipate mtu sahihi wa kumjibu.
"Zu...Zubeda yupo wapi" Inspekta Kobo akiwa ameketi chini aliuliza kwa sauti ya chini sana, bila shaka alikuwa katika maumivu bado.
Swali lile likamshtua sana Nguzu, alikuwa amesahau kabisa kuwa kuna mlipuko ulikuwa umesikika kabla hajadhibitiwa na mabwana wale waliodai kuwa walikuwa wameagizwa na mkuu wa majeshi mstaafu, Jeremiah Stamford Kazeze.
Kukosa kule utulivu kukaondoka na umakini wake.
Yule mtumwa akamvamia Nguzu upesi na teke kali ambalo liliiondoa silaha yake mkononi.
Akarusha teke la pili ambalo lilielekea kupasua fuvu la kichwa cha Nguzu. Nguzu akawahi kuinama.
Wakati anajiandaa kumkabili akajikuta akikabiliana na madonge ya damu.
Kobo alikuwa amejipima tena umakini wake kama upo sawa.
"Usingemuua Inspekta..."
"Angekuua wewe.... amepitia mafunzo ambayo wewe hujawahi hata kuyaona kwenye luninga.... hata hivyo sijamuua labda aamue kufa mwenyewe tu..."
Hatimaye Inspekta alisimama kwa tabu, wakati huo Nguzu alikuwa ametangulia kwenda kuitambua hali ya afya ya Zubeda ambaye bila shaka alishambuliwa.
Hakika alikuwa amepoteza fahamu, risasi ilikuwa imemkwangua begani na kumtupa ukutani.
Halikuwa jeraha kubwa sana, hata alivyoshtuliwa kwa kumwagiwa maji ilikuwa rahisi kwake kusimama na kutambua kila kilichokuwa kinaendelea.
Kigiza kilikuwa kinaanza kuingia wakati watatu hawa wakiwa wamepata fursa ya kuwa mbali na ile nyumba na walikuwa wameweza kujadili kwa ufupi sana juu ya kisa hiki.
Hakuna aliyegusia suala la mapenzi ya kuchangia, walitazama zaidi uhai na amani yao.
Inspekta akashauri wafanye mchakato wa kuwasiliana na IGP waweze kuupata msaada wa upesi sana dhidi ya Kazeze IGP mstaafu waliyeamini fika kuwa yupo nyuma ya yote haya.
Wakati wao wanafikiria namna ya kuwasiliana na IGP.... ni wakati huohuo IGP mstaafu Kazeze alikuwa yu njiani kuelekea nyumbani kwa IGP.
_________