Norami
Senior Member
- Feb 12, 2019
- 104
- 111
as
eseeh!🙂🙂🙂🙂huu utamu umekolea sana cjui uongezee uzii kidogo bishop maan naona keshoo mbaliiGereza la Kifo - 58
Mtunzi - HAMISI KIBARI
ILIPOISHIA
Happy aliondoa vyombo mezani huku Masunju akimpiga jicho la uchu kwa jinsi alivyokuwa anatamanisha usiku huo akiwa amevaa sketi yake fupi na blauzi fupi iliiyokuwa imeacha kitovu chake nje.
Msichana huyo mrembo alimkaribisha chumbani na kisha akamwambia anatoa vyombo nje kwa ajili ya kuvisafisha baadaye.
Masunju alibaki chaumbani na ndipo Happy akachepuka haraka haraka hadi kwenye dirisha la chumba walimokuwa akina Walari na dada yake Ramla kuwaambia kwamba waje kuvamia baada ya dakika zisizozidi kumi.
Wakati yule kijana aliyejifanya mchumba wa Happy hakuwa na wasiwasi wowote kuanza safari ya kwenda kumvamia Masunju, yule mpiga picha alianza kuogopa.
Endelea...
"Huyu mtu kweli hana bastola? Mimi naogopa bwana," akasema yule mpiga picha.
Wakati dakika kumi alizokuwa amewapa Happy zinaisha bado Ramla, Walari na Marare walikuwa wakimbembeleza yule mpiga picha asiogope lakini ilishindikana licha ya kumwongezea pesa kutoka sh. 40,000 walizokuwa wamemuahidi awali hadi sh. 60,000.
Ingawa Walari na Marare walipanga wawe wakishuhudia kwa mbali, lakini ilibidi sasa Marare aamue kuchukua kamera ya yule mpiga picha wa mtaani kwenda.
Yule kijana aliyepanga kujifanya mchumba wa Happy, akiwa hana wasiwasi alitangulia na alipofika akasukuma mlango wa kuingilia sebuleni na moja kwa moja akasukuma ule wa chumba walimokuwa Masunju na Happy. Happy alikuwa ameacha kuufunga kwa makusudi.
Masunju ambaye alikuwa uchi wa mnyama, huku akiwa amemkumbatia Happy ambaye alikuwa akijifanya yuko katika harakati za kuvua nguo, alishituka sana.
Happy alikurupuka na kwenda kupiga magoti akimwomba samahani yule 'mchumba' wake.
Masunju akiwa amechanganyikiwa alitaka kuchukua nguo zake alizokuwa amezitunduka ukutani haraka haraka, lakini yule 'mchumba' akaziwahi na kuzirusha nje ya chumba huku akimzuia kwa nguvu asitoke.
‘Mchumba’ huyo, akaanza kumhoji inakuwaje anafanya mapenzi na mchumba wake, wakati yeye yuko katika harakati za kufunga ndoa na msichana huyo na sasa walikuwa wanahesabu miezi tu.
Masunju, akiwa bado uchi alimuomba msamaha yule kijana huku akinyanyuka na kumuomba amuache achukue nguo zake na kwamba hilo suala wangelimaliza.
Yule kijana akiwa amekasirika 'sana' alitaka ampe maelezo ya kuridhisha kwa kitendo cha kumrubuni mchumba wake wakati yeye Masunju ana mke.
"Utakuwa mtu mshenzi sana wewe. Bila shaka wewe ni mpenzi wa shemeji Ramla na mimi nilishakuona unakuja hapa hapa mara kwa mara kwa dada yake huyu mchumba wangu. Huwa tunapishana tu. Sasa inakuwaje tena unamchukua mdogo wake ambaye ni mchumba wangu mimi?" Akawa anafoka kijana huyo aitwaye Bwire kwa hasira.
"Kijana samahani sana. Punguza hasira. Tutayamaliza tu kijana. Naomba sana unirudishie nguo zangu nivae," aliomba Masunju.
"Sikubali. Nimeshamhangaikia sana huyu binti. Unajua hasa aliyekuwa akimlipia karo ya shule ni nani? Si unajua hawa mabinti ni yatima?" Akazidi kufoka Bwire huku akina Walari waliokuwa nyuma ya dirisha wakisikia.
"Kijana tutayamaliza tu," akaomba Masunju huku sasa Happy akiwa amemgeukia kwa kumlaumu kwamba amemponza kuhusu mchumba wake na dada yake akipata habari hizo atamfukuza.
Masunju akazidi kumsihi Bwire ampe nguo zake, halafu wamalizane na sasa akamtaka atamke pesa anazotaka. Bwire huku akifunga mlango wa chumba kwa komeo alitoka kama vile anamleta nguo zake alizokuwa amezirusha sebuleni.
Alienda kumchukua Marare ili aje kumpiga picha Masunju. Marare alilazimika kuvaa kofia walioiazima haraka haraka ili kujaribu kuficha sura yake Masunju asimtambue.
Walipoingia mule chumbani ambako Masunju alikuwa bado ameketi kitandani akiwa uchi wa mnyama Marare ambaye alikuwa ameandaa tayari kamera akampiga haraka haraka picha.
Masunju aliposhituka kwamba anapigwa picha alisimama haraka haraka na kujaribu kuficha sura yake huku pia akifunika sehemu zake za siri kwa viganja. Baadaye akafanikiwa kuvuta shuka iliyokuwa kitandani lakini alikuwa ameshachelewa. Marare alikuwa keshampiga picha kadhaa na kutoka nje haraka, akimwacha Bwire akiendelea kuzozana na Masunju ambaye sasa alikua amechanganyikiwa.
Sasa Masunju alianza kugomba kuhusu suala la kupigwa picha, lakini Bwire akamjibu kwa jeuri kwamba ni lazima ampige ili kuweka ushahidi atakapokuwa anadai pesa zake nyingi ambazo ameshamgharimia Happy.
Masunju alizidi kumsihi kijana yule amsamehe, kisha ampe mkanda wa picha alizopigwa huku akiahidi kumpa gari dogo aina ya Toyota Carina pamoja pesa taslimu shilingi milioni moja.
"Mzee, mimi sasa ninakuruhusu uende zako, mambo ya pesa na gari tutaongea siku nyingine kadri tutakavyoafikiana na mchumba wangu kuhusu kadhia hii," akasema Bwire huku akitoka nje ya chumba ambako alichukua nguo za Masunju na kumrushia pale kitandani.
Mwanamume yule menene, Masunju alivaa haraka haraka, tena akiwa amesahau nguo ya ndani ambayo, Happy toka mapema, alikuwa amesukuma uvunguni mwa kitanda bila Masunju kufahamu.
Bwire, huku mawazoni akiingiwa na uchu wa gari, alizidi kumwambia Masunju kwa kiburi kwamba suala la kupeana pesa au gari wangelizungumzia siku nyingine ndipo ampe mkanda wa picha zake.
Masunju alizidi kubembeleza lakini Bwire alikataa na kutoka nje ambako kulikuwa na giza. Happy alikuwa amezima taa ya nje makusudi.
Masunju naye alitoka akizidi kumbembeleza Bwire ambaye alikuwa amesimama nje karibu na mlango. Akamsihi sana ampe mkanda wa picha aliyopigwa.
"Mzee, nimeshakwambia mkanda huupati leo. Kwanza mpiga picha mwenye ameshaondoka zake," akajibu Bwire.
"Kwenda wapi?"
"Kwenda kwake mzee. Wewe huoni huu ni usiku?"
Ghafla Masunju alichomoa bastola ambayo ilikuwa kwenye nguo zake na kumgusisha nayo Bwire kwenye paji la uso. Hicho ni kitu ambacho Bwire alikuwa hakukifikiria.
"Sasa kijana ninakuua ukileta masihara. Nimekupa kila ahadi hutaki kusikia. Mimi siondoki hapa bila kupata mkanda wa picha mlizopiga. Kwanza ninajiuliza huyu mpiga picha katokea wapi?" akafoka Masunju.
Bwire alivaa ujasiri na kumjibu kwamba yeye haogopi kifo wakati anapokuwa anafuatilia haki zake.
"Niue tu kama unataka. Lakini hili si suluhisho na utakuwa unajiweka katika matata zaidi. Niue kama unataka."
"Nyamaza. Mbwa wewe. Weka mikono juu la sivyo nitafumua ubongo wako sasa hivi," alifoka zaidi Masunju.
Bwire sasa alianza kuingiwa na wasi wasi huku akijilaumu ni kwa hakukagua bastola kwenye mifuko ya Masunju. Aliona yule mtu amekasirika kuzidi upeo wa kawaida na angeweza kumuua kweli.
"Sasa tuseme ndiyo unataka nikupe mkanda kwa nguvu halafu ahadi uliokuwa unainiambia ya pesa na gari ndiyo umefuta? Si ninakwambia kwamba hilo tutaliongelea siku nyingine?"
"Siwezi kuondoka hapa bila huo mkanda. Nikishaupata huo mkanda au kufuta hizo picha zote sasa tutazungumza," akasema Masunju akizidi kugandamiza mtutu wa bastola kwenye uso wake.
Bwire alizidi kuogopa.
"Naomba tuwasiliane kesho kwa sababu yule mpiga picha nilimbahatisha tu wakati nimetoka nje, lakini anakwenda kupiga picha katika ukumbi mmoja ambao kuna dansi usiku huu. Kwa hiyo ameshakwenda huko, si rahisi kumpata," akajibu Bwire.
"Bwana mdogo, usinifanye mimi mjinga. Hii inaonekana ni kitu cha kupanga. Inaonekana ulimuandaa huyo mpiga picha wako. Nipeleke kwa huyo mtu kabla sijachukua hatua mbaya kwako."
Muda wote wakiwa wanajibishana pale mlangoni, Happy alikuwa ameshakimbia baada ya kuona Masunju ametoa bastola. Akina Walari, Marare na Ramla walikua wamezunguka nyuma ya nyuma na kuchuchuma nyuma ya banda la kufugia kuku lililokuwa umbali mfupi kutoka mahala walikokuwa wamesimama Masunju na Bwire kiasi cha kusikia kila walichokuwa wakiongea.
Itaendelea...