- Thread starter
-
- #21
SEHEMU YA SABA
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya
MAWASILIANO: 0655 727325
SEHEMU YA SABA
"Her name is Fridah! I need her right now!" (Anaitwa Frida, namuhitaji hapa sasa hivi!) alikoroma mzungu!
Mkuu wa kituo akatoka nje akiwa anatetemeka!!
Ndio. Lazima atetemeke maana kwa namna yoyote Frida lazima atamtaja kuwa yeye ndiye muhusika wa mimba ile!! Kibarua kitaota majani!!
Hofu ikatanda sana!! Hadi anafika nje hakujua afanye nini!!!
Wakati mnyanyasaji huyu akiwa katika hofu kuu. Frida alikuwa katika mawazo ya ataweza vipi kuzungumza na yule mzungu mwenye upendo wa hakli ya juu. Alihitaji kutoa shtaka lake dhidi ya mkuu wa kituo. Uamuzi huu hakumshirikisha Mwanaidi. Aliuhifadhi moyoni.
Mara akiwa katika mawazo hayo mazito. Akasikia akiitwa jina lake kwa mbali. Akageuka!! Alikuwa mkuu wa kituo!!
Moyo ukamwenda mbio Frida. Na ilikuwa kawaida kila alipomuona mwanaume huyu alimchukulia kama mnyama mkali.
*****
Hakuna kitu kinachokera nakuumiza kichwa kama kutafuta kazi na hakuna kingine kibaya kama kuipoteza kazi uliyoitafuta kwa kutumia nguvu nyingi.
Ni fedheha hii ilimkumba msimamizi mkuu wa kituo. Ni kweli alifurahia kujistarehesha na Frida kwa kutumia mamlaka aliyokuwa nayo lakini hakutaka huyo Frida awe chanzo cha yeye kupoteza kazi yake.
Akiwa amehamaki sana huku akiwa ameogofyeka na ukali wa mzungu yule. Mwanaume huyu katili asiyekuwa na upendo hata kidogo alitoka nje. Alipoagizwa kumuita Frida
Akazurura huku na huko! Akamuona aliyetaka kumuona. Frida!
Akamuita! Hakutegemea kama tukio hilo linaweza kutokea. Aligeuka mtu asiyemtegemea japo huyo ndiye aliyehitajika.
"Sio wewe!" alimwambia kwa sauti ya kuamuru!!
"Frida!" aliita tena, sasa yule aliyemtaka akageuka. Akapunga mkono kuashiria amfuate.
Alipomfikia akamtaka amfuate anapoelekea. Yule binti mrefu mwembamba akamfuata akinyata kama hataki. Hawakuzungumza lolote wakaingia katika kile chumba alichokuwa mzungu.
Binti akaendelea kusimama wima, nywele zake ndefu kiasi fulani zikiwa zimemziba jicho moja. Akazirusha nyuma na kushindwa kutoa salamu kwa mzungu kwa sababu ya kutojua lugha.
Mzungu hakuwa na papara. Na aliujua ujanjaujanja wa wa afrika. Hakumuaga mtu pale chumbani akatoka na kurejea baada ya dakika chache akiwa ameongozana na muhusika mwingine wa kile kituo.
"I want you to translate! (Nahitaji ufanye tafsiri)" aliamuru huku uso wake ukiwa umeiva kwa hasira.
"What's you are real name! (Jina lako halisi ni nani)"
"Winifrida…" alijibu bila wasiwasi.
"Famous name! (Jina maarufu)"
"Frida.." akatoa jibu ambalo mkuu wa kituo alikuwa analingojea kwa hamu.
Mahojiano yakaendelea kwa hatua ndogondogo. Hadi wakaifikia nia yao. Mimba!
Hapo huyu binti akaruka maili mia. Akakataa katakata.
Mzungu akabadili tena mtu wa kumtafasiria. Alifanya hivyo ili kuepukana na wabongo hawa waliomzunguka wasije kucheza dili ili kumdanganya.
Hali ikawa ile ile.
"Tunaweza kukupima tena??" aliulizwa. Hakungoja kujifikiria akakubali kuwa yu tayari tena mbele ya watu wote.
Vipimo vikafanywa tena, majibu yakatoka. Hayakuwekwa hadharani. Wakapima tena. Frida hakuwa na mimba!!!
Hapa sasa madaktari walioaminiwa na yule mzungu aibu ikawa juu yao. Mzungu akahamishia hasira zake kwao. Hawakuwa na cha kujibu. Heshima kwa mkuu wa kituo ikarejea maradufu. Akamwomba msamaha kwa lugha za ukali alizotumia dhidi yake.
Maskini bwana huyu hakujua kuwa mkuu wa kituo ni mbongo halisi, tayari alikuwa amemchezea mchezo. Aliyeletwa mbele yake alikuwa ni mtu mwingine kabisa. Huyu alikuwa ni Winifrida na wala sio Frida yule chokoraa kutoka gerezani.
Mzungu akiwa na hasira tele, kipara chake kikitokwa jasho. Hakutaka tena kuzungumza na mtu na hata mtoto mnene kiasi, mwenye sura inayotangaza msiba huku macho yake yakiwa mekundu. Alimkimbilia. Alikuwa ana haja ya kuonana naye kwaajili ya kumueleza kitu kizito sana.
Alimfikia akamkumbatia. Mzungu akamkumbatiakisha akawaambia waliokuwa pembeni yake, "Tell her that I will be back (Mwambie nitarejea).
"Yuko bize siku nyingine" mbongo akafanya tafsiri anayojua yeye.
Huyu binti alikuwa ni Frida Gereza. Akawa ameikosa nafasi ya kuzungumza na mzungu huyo.
Kwa pona pona aliyoipata mkuu wa kituo. Hakutaka tena kucheza karata hizi mbovu. Hata kabla huyo mzungu hajarudi tena tayari alikuwa ameweka mambo sawa. Mwanaidi na Frida walikuwa maeneo ya Posta wakitafuta mahali pa kulala. Makazi ya usiku ya chokoraa!!
Walikuwa wamefukuzwa kimyakimya!!
Mkuu wa kituo akabaki na tabasamu usoni huku akijisifu kuwa yu mshindi katika vita kuu. Hakuiwaza tena mimba ya Frida.
Dada mkuu yule w zamani katika shule ya msingi alikuwa na akili ya kuzaliwa. Kitendo cha wawaili hawa kufukuzwa mapema baada tu ya mzungu kuwatembelea na kuwapima mimba kilimtia mashaka. Uhusiano wa Winifrida kuitwa na kutuhumiwa kuwa ana ujauzito kisha kupimwa na kukutwa salama pia kulimshtua. Hakutaka kumweleza Frida mapema. Lakini baada ya muda kidogo alifanya maamuzi. Kwa senti chache alizokuwanazo alinunu Pregnant Tester (PT). Hiki ni kifaa binafsi cha kupimia ujauzito kwa njia ya mkojo.
Frida akaamriwa kukikojolea. Akafanya hivyo.
Machale na hisia sahihi kabisa. Frida alikuwa ana mimba!!!
Msichana huyu alichanganyikiwa kusikia hivyo. Lakini bado Mwanaidi alikuwa jasiri. Alimshauri kuwa kuamua kubaki nayo ni kujiua kwa mateso kabla ya wakati.
"Kwa hiyo nitafanyaje mimi."
"Usijali!! Lala hapa nakuja."
Mwanaidi akatoweka tena na kutafuta duka la madawa lililokuwa wazi usioku ule. Akanunua madawa aliyoyajua yeye. Akafanikiwa kupata na maji ya kunywa ya bei chee. Frida akapewa sharti akatii. Akanywa yale madawa. Kisha akalala.
Mambo yakaanza kubadilika baada ya masaa machache. Ule usiku ukageuka kuwa usiku wa uchungu mtakatifu.
Tumbo likamsokota Frida. Mwanzoni alijikaza lakini uvumilivu ukamshinda akaanza kupiga kelele. Akalia sana Mwanaidi kazi yake kumbembeleza.
Damu ikaanza kumtoka. Hatimaye uchungu uliopitiliza ukaondoka na fahamu zake. Alipoamka alfajiri hakuwa mjamzito tena.
Mungu alikuwa pamoja naye! Njia hii hatarishi ingeweza kuondoka na uhai wake.
****
Hakuna kipindi watoto wa mitaani wananyanyasika kama kipindi cha masika. Mvua hizi za masika huvuruga kabisa makazi yao ya kulala. Watoto hukesha kama popo. Sehemu zao za kulala zote huwa majimaji na magunia yao ambayo ni vitandavyenye thamani huwa chepechepe.
Usiku huu ulikuwa usiku wa namna yake kwa Mwanaidi na Frida. Hawakuitegemea hali hii lakini sasa ilikuwa imewakumba. Walizurura huku na huko bila kuupata muafaka wa watalala vipi. Baridi kali iliwapuliza na manyunyu yaliyoambatana na upepo mkali yaliilowanisha miili yao.
Baada ya kuzurura sana!! Mwanaidi akaanza kupunguza mwendo na hatimaye akasimama. Frida aliyekuwa ametangulia akageuza na kurudi nyuma kutazama nini kimemsibu rafiki yake.
"Frida…" Mwanaidi aliita huku midomo yake ikichezacheza na meno yakigongana mdomoni.
"Naumwa!! Naumwa sana" Mwanaidi alimweleza. Kifua kilikuwa kinambana. Frida alibaki anashangaa, mtu ambaye anamtegemea. Sasa anaumwa. Na ni yeye aliyekuwa mwalimu wake mtaani.
"Kaninunulie dawa. Dawa ya kupuliza naanza kukosa hewa." Alizidi kujieleza Mwanaidi huku sasa akiwa amekaa chini.
Hali tete!! Hakika palikuwa na tatizo.
"Inaitwaje…na hela sasa." Aliuliza Frida huku akiwa na hofu kubwa.
"Nenda watakuelewa waambie siwezi kupumua. Nitakufa Fri…Fri…" Sauti ikazidi kupotea.
Ilikuwa saa tatu usiku. Mitaa ya posta haikuwa imejikita vyema katika akili ya Frida. Alijaribu kukata huku na kule. Hatimaye akalipata duka.
Akawaeleza kama Mwanaidi alivyomuelezea. Akawalilia akalia sana chokoraa huyu. Hatimaye akaeleweka.
Akapewa bure dawa ile ambayo hata aliyempa aliamini kuwa hawezi kuwa na nia mbaya na dawa ile ya kupuliza ambayo hutumiwa hasahasa na wagonjwa wa pumu.
Frida akatimua mbio aweze kumuwahi Mwanaidi.
Unapajua Posta unapasikia?
Hilo swali alilijibu Frida kwa vitendo. Mtaa huu na mtaa ule inafanana. Jingo hili na lile la awali yanalingana urefu. Kila mahali panafanana na ikulu ya Tanzania. Frida akwa amepotea.
Alijaribu kuituliza akili yake. Akapunguza mwendo aweze kuwa makini lakini bado hali ikawa ileile.
Alitaka kuwauliza watu lakini hakujua atawauliza wamuelekeze wapi maana hata pahali alipokuwa awali na Mwanaidi hakupajua vizuri.
Frida akaanza kulia. Mvua kubwa ikayatwaa machozi yake na kuyasafirisha mbali. Nguo zikanata katika mwili.
Sasa Frida alikuwa anaomboleza kana kwamba Mwanaidi amekufa tayari. Usiku huu ukapita. Asubuhi anakuja kugundua alilala nyuma ya jingo ambalo Mwanaidi alikuwa akimngojea. Dawa yake mkononi ndiyo ilimgutusha akamkumbuka. Mwanaidi.
Akaangalia sehemu zote hapakuwa na kiumbe anayeishi!
Mwanaidi alikuwa ametoweka!
Kilio kikaanza upya kwa yatima huyu. Aliugulia maumivu sana.
Ile hali ya kumfikiria Mwanaidi kuwa amekufa kwa kusombwa na maji ikamfanya ajisikie kitu kama chuki kikitambaa katika mtima wake. Chuki dhidi ya wanaume. Akamuweka katika orodha mkuu wa kituo kama muhusika namba moja wa kifo cha Mwanaidi.
Waarabu wa pemba hujuana kwa vilemba. Na hata yatima na machokoraa hujuana kwa vilio vyao. Chokoraa mmoja akafahamu kuwa Frida alikuwa katika majonzi. Kwanza alimgawia kipande cha muhogo alichokuwa anatafuna. Frida akapokea.
"Unaonekana mgeni maeneo haya. We ni wa kempu ipi?"
"Kempu ni nini?" aliuliza Frida.
Yule msichana aliyejitambulisha kwa jina la Isha akatabasamu. Hakuendelea kuuliza maswali. Frida akajiumauma akaelezea juu ya kupotea kwa Mwanaidi.
"Hiyo ni kawaida, wengine hubakwa na wengine huchunwa ngozi. Sijui watakuwa wameenda naye wapi." Alijibiwa kwa tahadhari.
"Mama yangu alichukuliwa mikononi mwangu. Mimi wakanibaka yeye aliondoka nao moja kwa moja hadi leo. Majangili na wanyang'anyi ni watu wabaya."
Isha aliongozana na Frida. Wakaelekea feri. Huko wakapanda pantoni. Iliyowavusha ng'ambo ya pili. Isha akiwa kiongozi wa Frida walizifikia nyumba nyingi walizokuwa wanaishi wanafunzi wa chuo kikuu cha IFM.
"Huwa tunawafulia nguo. Nifuate!"
Walianzia mlango wa kwanza. Wenyewe hawakuwepo. Mlango wa pili hawakuhitaji huduma. Mlango wa tatu bahati ikawa upande wao. Kijana mnene aliyenukia raha, akawakabidhi lundo la nguo.
"Jinsi mia tatu, suruali na shati mia mbili, soksi na fulana huwa tunafanya mia mia." Isha alimtajia bei.
Yule kijana akawapatia ndoo na sabuni. Akawaelekeza bomba lilipo. Wakaanza kufua. Frida alikuwa mwepesi zaidi kuliko Isha na hakuonekana kuchoka. Isha hakuitegemea hali hiyo.
Mchana wakapokea ujira wao na kuondoka.
Urafiki wao ukaanzia hapa. Mwanaidi akaanza kusahaulika ili kutimiza ule usemi usemao ‘mavi ya kale hayanuki!'
Kila mwisho wa juma walikuja na kutafuta kibarua cha kufua nguo za wanafunzi. Kwa siku za kawaida waliokota makopo tupu ya maji na soda na kuyauza kwa kilo katika viwanda vya wahindi na waarabu.
Maisha yakaendelea!!
Ni huku Kigamboni ambapo Frida alikutana na maajabu!!
***MAAJABU gani FRIDA anakutana nayo Kigamboni!!
***MWANAIDI na ugonjwa wake wa PUMU….ameishia wapi.
**JE MKUU WA KITUO ataishi milele na roho yake mbaya.
mbalu amina mabata
RIWAYA: CHOKORAA
MTUNZI: George Iron Mosenya
MAWASILIANO: 0655 727325
SEHEMU YA SABA
"Her name is Fridah! I need her right now!" (Anaitwa Frida, namuhitaji hapa sasa hivi!) alikoroma mzungu!
Mkuu wa kituo akatoka nje akiwa anatetemeka!!
Ndio. Lazima atetemeke maana kwa namna yoyote Frida lazima atamtaja kuwa yeye ndiye muhusika wa mimba ile!! Kibarua kitaota majani!!
Hofu ikatanda sana!! Hadi anafika nje hakujua afanye nini!!!
Wakati mnyanyasaji huyu akiwa katika hofu kuu. Frida alikuwa katika mawazo ya ataweza vipi kuzungumza na yule mzungu mwenye upendo wa hakli ya juu. Alihitaji kutoa shtaka lake dhidi ya mkuu wa kituo. Uamuzi huu hakumshirikisha Mwanaidi. Aliuhifadhi moyoni.
Mara akiwa katika mawazo hayo mazito. Akasikia akiitwa jina lake kwa mbali. Akageuka!! Alikuwa mkuu wa kituo!!
Moyo ukamwenda mbio Frida. Na ilikuwa kawaida kila alipomuona mwanaume huyu alimchukulia kama mnyama mkali.
*****
Hakuna kitu kinachokera nakuumiza kichwa kama kutafuta kazi na hakuna kingine kibaya kama kuipoteza kazi uliyoitafuta kwa kutumia nguvu nyingi.
Ni fedheha hii ilimkumba msimamizi mkuu wa kituo. Ni kweli alifurahia kujistarehesha na Frida kwa kutumia mamlaka aliyokuwa nayo lakini hakutaka huyo Frida awe chanzo cha yeye kupoteza kazi yake.
Akiwa amehamaki sana huku akiwa ameogofyeka na ukali wa mzungu yule. Mwanaume huyu katili asiyekuwa na upendo hata kidogo alitoka nje. Alipoagizwa kumuita Frida
Akazurura huku na huko! Akamuona aliyetaka kumuona. Frida!
Akamuita! Hakutegemea kama tukio hilo linaweza kutokea. Aligeuka mtu asiyemtegemea japo huyo ndiye aliyehitajika.
"Sio wewe!" alimwambia kwa sauti ya kuamuru!!
"Frida!" aliita tena, sasa yule aliyemtaka akageuka. Akapunga mkono kuashiria amfuate.
Alipomfikia akamtaka amfuate anapoelekea. Yule binti mrefu mwembamba akamfuata akinyata kama hataki. Hawakuzungumza lolote wakaingia katika kile chumba alichokuwa mzungu.
Binti akaendelea kusimama wima, nywele zake ndefu kiasi fulani zikiwa zimemziba jicho moja. Akazirusha nyuma na kushindwa kutoa salamu kwa mzungu kwa sababu ya kutojua lugha.
Mzungu hakuwa na papara. Na aliujua ujanjaujanja wa wa afrika. Hakumuaga mtu pale chumbani akatoka na kurejea baada ya dakika chache akiwa ameongozana na muhusika mwingine wa kile kituo.
"I want you to translate! (Nahitaji ufanye tafsiri)" aliamuru huku uso wake ukiwa umeiva kwa hasira.
"What's you are real name! (Jina lako halisi ni nani)"
"Winifrida…" alijibu bila wasiwasi.
"Famous name! (Jina maarufu)"
"Frida.." akatoa jibu ambalo mkuu wa kituo alikuwa analingojea kwa hamu.
Mahojiano yakaendelea kwa hatua ndogondogo. Hadi wakaifikia nia yao. Mimba!
Hapo huyu binti akaruka maili mia. Akakataa katakata.
Mzungu akabadili tena mtu wa kumtafasiria. Alifanya hivyo ili kuepukana na wabongo hawa waliomzunguka wasije kucheza dili ili kumdanganya.
Hali ikawa ile ile.
"Tunaweza kukupima tena??" aliulizwa. Hakungoja kujifikiria akakubali kuwa yu tayari tena mbele ya watu wote.
Vipimo vikafanywa tena, majibu yakatoka. Hayakuwekwa hadharani. Wakapima tena. Frida hakuwa na mimba!!!
Hapa sasa madaktari walioaminiwa na yule mzungu aibu ikawa juu yao. Mzungu akahamishia hasira zake kwao. Hawakuwa na cha kujibu. Heshima kwa mkuu wa kituo ikarejea maradufu. Akamwomba msamaha kwa lugha za ukali alizotumia dhidi yake.
Maskini bwana huyu hakujua kuwa mkuu wa kituo ni mbongo halisi, tayari alikuwa amemchezea mchezo. Aliyeletwa mbele yake alikuwa ni mtu mwingine kabisa. Huyu alikuwa ni Winifrida na wala sio Frida yule chokoraa kutoka gerezani.
Mzungu akiwa na hasira tele, kipara chake kikitokwa jasho. Hakutaka tena kuzungumza na mtu na hata mtoto mnene kiasi, mwenye sura inayotangaza msiba huku macho yake yakiwa mekundu. Alimkimbilia. Alikuwa ana haja ya kuonana naye kwaajili ya kumueleza kitu kizito sana.
Alimfikia akamkumbatia. Mzungu akamkumbatiakisha akawaambia waliokuwa pembeni yake, "Tell her that I will be back (Mwambie nitarejea).
"Yuko bize siku nyingine" mbongo akafanya tafsiri anayojua yeye.
Huyu binti alikuwa ni Frida Gereza. Akawa ameikosa nafasi ya kuzungumza na mzungu huyo.
Kwa pona pona aliyoipata mkuu wa kituo. Hakutaka tena kucheza karata hizi mbovu. Hata kabla huyo mzungu hajarudi tena tayari alikuwa ameweka mambo sawa. Mwanaidi na Frida walikuwa maeneo ya Posta wakitafuta mahali pa kulala. Makazi ya usiku ya chokoraa!!
Walikuwa wamefukuzwa kimyakimya!!
Mkuu wa kituo akabaki na tabasamu usoni huku akijisifu kuwa yu mshindi katika vita kuu. Hakuiwaza tena mimba ya Frida.
Dada mkuu yule w zamani katika shule ya msingi alikuwa na akili ya kuzaliwa. Kitendo cha wawaili hawa kufukuzwa mapema baada tu ya mzungu kuwatembelea na kuwapima mimba kilimtia mashaka. Uhusiano wa Winifrida kuitwa na kutuhumiwa kuwa ana ujauzito kisha kupimwa na kukutwa salama pia kulimshtua. Hakutaka kumweleza Frida mapema. Lakini baada ya muda kidogo alifanya maamuzi. Kwa senti chache alizokuwanazo alinunu Pregnant Tester (PT). Hiki ni kifaa binafsi cha kupimia ujauzito kwa njia ya mkojo.
Frida akaamriwa kukikojolea. Akafanya hivyo.
Machale na hisia sahihi kabisa. Frida alikuwa ana mimba!!!
Msichana huyu alichanganyikiwa kusikia hivyo. Lakini bado Mwanaidi alikuwa jasiri. Alimshauri kuwa kuamua kubaki nayo ni kujiua kwa mateso kabla ya wakati.
"Kwa hiyo nitafanyaje mimi."
"Usijali!! Lala hapa nakuja."
Mwanaidi akatoweka tena na kutafuta duka la madawa lililokuwa wazi usioku ule. Akanunua madawa aliyoyajua yeye. Akafanikiwa kupata na maji ya kunywa ya bei chee. Frida akapewa sharti akatii. Akanywa yale madawa. Kisha akalala.
Mambo yakaanza kubadilika baada ya masaa machache. Ule usiku ukageuka kuwa usiku wa uchungu mtakatifu.
Tumbo likamsokota Frida. Mwanzoni alijikaza lakini uvumilivu ukamshinda akaanza kupiga kelele. Akalia sana Mwanaidi kazi yake kumbembeleza.
Damu ikaanza kumtoka. Hatimaye uchungu uliopitiliza ukaondoka na fahamu zake. Alipoamka alfajiri hakuwa mjamzito tena.
Mungu alikuwa pamoja naye! Njia hii hatarishi ingeweza kuondoka na uhai wake.
****
Hakuna kipindi watoto wa mitaani wananyanyasika kama kipindi cha masika. Mvua hizi za masika huvuruga kabisa makazi yao ya kulala. Watoto hukesha kama popo. Sehemu zao za kulala zote huwa majimaji na magunia yao ambayo ni vitandavyenye thamani huwa chepechepe.
Usiku huu ulikuwa usiku wa namna yake kwa Mwanaidi na Frida. Hawakuitegemea hali hii lakini sasa ilikuwa imewakumba. Walizurura huku na huko bila kuupata muafaka wa watalala vipi. Baridi kali iliwapuliza na manyunyu yaliyoambatana na upepo mkali yaliilowanisha miili yao.
Baada ya kuzurura sana!! Mwanaidi akaanza kupunguza mwendo na hatimaye akasimama. Frida aliyekuwa ametangulia akageuza na kurudi nyuma kutazama nini kimemsibu rafiki yake.
"Frida…" Mwanaidi aliita huku midomo yake ikichezacheza na meno yakigongana mdomoni.
"Naumwa!! Naumwa sana" Mwanaidi alimweleza. Kifua kilikuwa kinambana. Frida alibaki anashangaa, mtu ambaye anamtegemea. Sasa anaumwa. Na ni yeye aliyekuwa mwalimu wake mtaani.
"Kaninunulie dawa. Dawa ya kupuliza naanza kukosa hewa." Alizidi kujieleza Mwanaidi huku sasa akiwa amekaa chini.
Hali tete!! Hakika palikuwa na tatizo.
"Inaitwaje…na hela sasa." Aliuliza Frida huku akiwa na hofu kubwa.
"Nenda watakuelewa waambie siwezi kupumua. Nitakufa Fri…Fri…" Sauti ikazidi kupotea.
Ilikuwa saa tatu usiku. Mitaa ya posta haikuwa imejikita vyema katika akili ya Frida. Alijaribu kukata huku na kule. Hatimaye akalipata duka.
Akawaeleza kama Mwanaidi alivyomuelezea. Akawalilia akalia sana chokoraa huyu. Hatimaye akaeleweka.
Akapewa bure dawa ile ambayo hata aliyempa aliamini kuwa hawezi kuwa na nia mbaya na dawa ile ya kupuliza ambayo hutumiwa hasahasa na wagonjwa wa pumu.
Frida akatimua mbio aweze kumuwahi Mwanaidi.
Unapajua Posta unapasikia?
Hilo swali alilijibu Frida kwa vitendo. Mtaa huu na mtaa ule inafanana. Jingo hili na lile la awali yanalingana urefu. Kila mahali panafanana na ikulu ya Tanzania. Frida akwa amepotea.
Alijaribu kuituliza akili yake. Akapunguza mwendo aweze kuwa makini lakini bado hali ikawa ileile.
Alitaka kuwauliza watu lakini hakujua atawauliza wamuelekeze wapi maana hata pahali alipokuwa awali na Mwanaidi hakupajua vizuri.
Frida akaanza kulia. Mvua kubwa ikayatwaa machozi yake na kuyasafirisha mbali. Nguo zikanata katika mwili.
Sasa Frida alikuwa anaomboleza kana kwamba Mwanaidi amekufa tayari. Usiku huu ukapita. Asubuhi anakuja kugundua alilala nyuma ya jingo ambalo Mwanaidi alikuwa akimngojea. Dawa yake mkononi ndiyo ilimgutusha akamkumbuka. Mwanaidi.
Akaangalia sehemu zote hapakuwa na kiumbe anayeishi!
Mwanaidi alikuwa ametoweka!
Kilio kikaanza upya kwa yatima huyu. Aliugulia maumivu sana.
Ile hali ya kumfikiria Mwanaidi kuwa amekufa kwa kusombwa na maji ikamfanya ajisikie kitu kama chuki kikitambaa katika mtima wake. Chuki dhidi ya wanaume. Akamuweka katika orodha mkuu wa kituo kama muhusika namba moja wa kifo cha Mwanaidi.
Waarabu wa pemba hujuana kwa vilemba. Na hata yatima na machokoraa hujuana kwa vilio vyao. Chokoraa mmoja akafahamu kuwa Frida alikuwa katika majonzi. Kwanza alimgawia kipande cha muhogo alichokuwa anatafuna. Frida akapokea.
"Unaonekana mgeni maeneo haya. We ni wa kempu ipi?"
"Kempu ni nini?" aliuliza Frida.
Yule msichana aliyejitambulisha kwa jina la Isha akatabasamu. Hakuendelea kuuliza maswali. Frida akajiumauma akaelezea juu ya kupotea kwa Mwanaidi.
"Hiyo ni kawaida, wengine hubakwa na wengine huchunwa ngozi. Sijui watakuwa wameenda naye wapi." Alijibiwa kwa tahadhari.
"Mama yangu alichukuliwa mikononi mwangu. Mimi wakanibaka yeye aliondoka nao moja kwa moja hadi leo. Majangili na wanyang'anyi ni watu wabaya."
Isha aliongozana na Frida. Wakaelekea feri. Huko wakapanda pantoni. Iliyowavusha ng'ambo ya pili. Isha akiwa kiongozi wa Frida walizifikia nyumba nyingi walizokuwa wanaishi wanafunzi wa chuo kikuu cha IFM.
"Huwa tunawafulia nguo. Nifuate!"
Walianzia mlango wa kwanza. Wenyewe hawakuwepo. Mlango wa pili hawakuhitaji huduma. Mlango wa tatu bahati ikawa upande wao. Kijana mnene aliyenukia raha, akawakabidhi lundo la nguo.
"Jinsi mia tatu, suruali na shati mia mbili, soksi na fulana huwa tunafanya mia mia." Isha alimtajia bei.
Yule kijana akawapatia ndoo na sabuni. Akawaelekeza bomba lilipo. Wakaanza kufua. Frida alikuwa mwepesi zaidi kuliko Isha na hakuonekana kuchoka. Isha hakuitegemea hali hiyo.
Mchana wakapokea ujira wao na kuondoka.
Urafiki wao ukaanzia hapa. Mwanaidi akaanza kusahaulika ili kutimiza ule usemi usemao ‘mavi ya kale hayanuki!'
Kila mwisho wa juma walikuja na kutafuta kibarua cha kufua nguo za wanafunzi. Kwa siku za kawaida waliokota makopo tupu ya maji na soda na kuyauza kwa kilo katika viwanda vya wahindi na waarabu.
Maisha yakaendelea!!
Ni huku Kigamboni ambapo Frida alikutana na maajabu!!
***MAAJABU gani FRIDA anakutana nayo Kigamboni!!
***MWANAIDI na ugonjwa wake wa PUMU….ameishia wapi.
**JE MKUU WA KITUO ataishi milele na roho yake mbaya.
mbalu amina mabata
Last edited by a moderator: