Riwaya - Balaa

Nimeianza jana iko nzuri sana natamani ningesubiri iishe ndo nianze
 

Khaaa hao wambea wa vijiwen wametishaaa
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY.
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA SITINI NA TANO

Dokta Kilumba hakujibu, alikaa kimya.

"Tuyaache hayo Dokta, labda itakuwa unadharura kweli kila siku, naomba unijibu swali hili sasa, je una taarifa za kupotea maiti kumi na tano kila siku katika hospitali yako?"
"Taarifa hizo ninazo Mwandishi"
"Kwahiyo ndani ya siku saba, maiti ngapi zimepotea Dokta?"
"Maiti nyingi sana" Dokta Kilumba hakujishughulisha hata kuhesabu, alijibu tu.
"Kwa fikra zako unadhani maiti zinapotelea wapi?"
"Samahani Mwandishi, hilo swali siyo mahali sahihi hapa, mimi siyo mlinzi wa hospitali hii, mimi jukumu langu kuu ni kuhakikisha wagonjwa wanapona basi, wagonjwa wakifariki tu siyo jukumu langu tena, kwa bahati mbaya pia mimi sihusiki na chumba cha kuhifadhia maiti, kwa kifupi ninachoweza kukwambia, una maswali mazuri sana ndugu Mwandishi lakini umeyauliza kwa mtu asiye sahihi kabisa"
"Wewe ni mtu sahihi Dokta! Dokta Kilumba ni mganga mkuu wa hospitali hii. Una jukumu la kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa katika hospitali yako. Maiti zinapotea katika hospitali yako halafu unasema siyo jukumu lako, inaonesha kiasi gani usivyojua wajibu wako Dokta!"
"Sina maelezo zaidi, nikichotaka kukwambia nishakwambia, siongozi neno hapa wala sipunguzi, kupotea kwa maiti siyo jukumu langu, nukta!"
"Mbona kama hauoneshi kujari Dokta juu ya kupotea kwa maiti katika hospitali yako?"
"Kujari kuhusu nini Mwandishi, watu wanaiba maiti zao wenyewe ili kuitia doa hospitali halafu nd'o nijari?"
"Una uhakika na uyasemayo Dokta, inaingia akilini mtu kuiba maiti yake mwenyewe halafu alalamike kuibiwa?"
"Hilo sio swali langu, kawaulize wenyewe wanaoiba"
"Kama kuna mchezo mchafu wowote unaoendelea hapa hebu uacheni Dokta, unajua hamuwatendei haki wananchi"
"Nakuomba toka nje!"
"Hahaha Natoka ila nitarudi tena Dokta!"

Mwandishi wa habari, Gabriel Rondo alinyanyuka taratibu na kutoka nje. Alivyotoka nje tu, Dokta Kilumba alichukua simu yake na kumpigia Don Genge.

"Hallo Don kuna Mwandishi anaitwa Gabriel Rondo hapaswi kuliona jua la magharibi!"

ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757633010

SEHEMU YA SITINI NA SITA

"Analeta chokochoko huyo Mwandishi kama jina la gazeti lake?".
Kabisa Don, kumuacha hai ni kulitafuta balaa, huyu Mwandishi Inaonesha kuna vitu anajua kuhusu sisi"
"Usijari Dokta Kilumba, alasiri ataisikia kwenye bomba, kama ana fununu yoyote kuhusu sisi ataipeleka kuzimu"

Baada ya kukatwa simu kundi la Don Genge walifanya walichopaswa kufanya. Na walichofanya kilileta matunda mazuri kwao, maana ni kweli, saa kumi kamili jioni mwili wa Mwandishi wa habari, Gabriel Rondo uliokotwa katika ufukwe wa pwani ya Kilwa Kivinje. Mwili ulikuwa hauna macho, mwili uliojaa majeraha mengi sana, huku utumbo ukiwa unachungulia nje, ishara kuwa Gabriel Rondo alipitia mateso makali sana kabla ya kuuwawa! Nani angeweza kuutambua kuwa mwili ule ulikuwa wa Mwandishi Gabriel Rondo, hata ndugu zake wa karibu wasingeweza kuutambua. Ni kitambulisho kilichoning'inizwa kifuani kwake nd'o kilimtambulisha kuwa mwili ule ulikuwa wa Mwandishi Gabriel Rondo. Bila shaka kitambulisho hiko kiliwekwa makusudi na wauaji makatili wa Mwandishi huyo.

Jeshi la polisi la Kilwa Masoko likishirikiana na polisi wa Kilwa Masoko waliingia kazini kumsaka muuaji wa Mwandishi wa habari wa gazeti la Chokochoko Gabriel Rondo. Vyombo vya kutetea haki za binadamu vikapaza sauti zao, kupinga mauaji ya kikatili aliyofanyiwa Mwandishi wa habari. Chama cha waandishi wa habari nao walilaani kifo cha Mwandishi mwenzao na kutoa maadhimio mazito Kwa Serikali.
Tanzania nzima sasa ikageuzia jicho lake Kilwa, habari katika magazeti, televisheni zilihusu matukio ya ajabu yanayotokea Kilwa hasa katika hospitali ya wilaya ya Kilwa Kivinje.

Taarifa hizo ziliruka moja kwa moja mpaka katika hospitali ya misheni ya Ndanda, hospitali aliyokuwepo Dokta Yusha na wagonjwa wake. Dokta Yusha aliyasoma yote kwa umakini mkubwa sana, akijua sasa mambo yamekuwa mabaya zaidi huko Kilwa. Hakushangazwa sana na taarifa za kupotea maiti kumi na na tano kila siku, ila alishangazwa na kuuwawa bila hatia kwa Mwandishi wa habari wa gazeti la Chokocho, Gabriel Rondo.

"Lazima nirudi Kilwa kuuokoa jahazi"

ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA SITINI NA SABA

Wakati Dokta Yusha akiwa na mpango wa kurudi Kilwa. Kwenda kufichua uozo wa uongozi wa hospitali ya wilaya ya Kilwa, Kinyonga. Pamoja na kuweka hadharani ukatili wa kundi la Six killers.
Huko Kilwa Kivinje mambo yalikuwa magumu sana. Mambo yalikuwa magumu kwa kundi hatari la Six killers, mambo yalikuwa magumu kwa jeshi la Polisi la Kilwa na wananchi wa Kilwa kwa ujumla. Kifo cha Mwandishi wa habari wa gazeti la Chokochoko, Gabriel Rondo hakikuwarudisha nyuma kabisa waandishi wa habari wengine. Waandishi wa habari hawakuweka chini kalamu zao. Waandishi wa habari sasa walipamba moto. Wakiushutumu uongozi wa hospitali ya wilaya ya Kilwa, Kinyonga chini ya uongozi wa Dokta Zaidi Kilumba kwa balaa kubwa waliolileta. Ziliandikwa habari kuhusu udhaifu wa uongozi wa hospitali ya Kinyonga, yaliandikwa makala kuhusu unyama wa uongozi wa hospital ya Kinyonga. Na chini ya habari zote hawakusahau kuandika maneno haya 'upumzike salama Gabriel Rondo'

Taarifa za magazeti yale yalisambaa kwa kasi sana. Yalisambaa Tanzania yote, na baadhi ya nchi nje ya Tanzania. Kwa bahati au mzuri msambao wa habari hizo mbaya ukamfikia kijana mmoja..... Kijana shupavu sana, kijana mwerevu na mahiri katika sanaa ya mapambano.

Ilikuwa asubuhi tulivu sana na kijana huyo alikuwa amekaa katika sebuleni yake, katika nyumba ya kisasa iliyopo huko Mikocheni, Dar ea salaam. Asubuhi hiyo alikuwa anaangalia televesheni, ambapo kipindi cha kusoma magazeti kilimkuta akiwa ametulia kwenye sofa. Vichwa vingi sana vya habari vilisomwa katika magazeti hayo, lakini kichwa cha habari cha gazeti la Shupavu ndicho kilichomvutia zaidi.

"Kilwa kuna balaa !"

Kichwa cha habari hiko, kilichoandikwa kwa wino mwekundu, kuashiria uzito na uhatari wa habari hiyo, kilimnyanyua kijana huyo kutoka sofani, na miguu yake kumpeleka mtaani kutafuta gazeti la Shupavu ili aisome kwa makini habari hiyo. Hakupata shida sana kupata nakala ya gazeti la Shupavu. Baada ya dakika tano kijana huyo alirudi nyumbani kwake akiwa na gazeti la Shupavu mkononi. Alikaa tena palepale alipokaa awali, na kuanza kuisoma habari ile, 'Kilwa kuna balaa!"
Ilikuwa habari iliyoandikwa kwa umakini mkubwa sana, huku Mwandishi ikionekana alifanya utafiti wa kutosha kabla ya kushika kalamu yake na kuandika habari ile. Habari hiyo ilieleza kila kitu kuhusu Mpango wa utoaji mioyo ulivyo katika hospitali ya Kinyonga. Mwandishi pia akieleza uwepo wa kambi ya watoa mioyo huko porini, na kuweka hadharani udhaifu na ukatili wa uongozi wa hospitali ya wilaya Kilwa, Kinyonga...

ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA SITINI NA NANE

Habari ile ilimfanya yule kijana atafute jina la mwandishi wa habari ile. Hakukuwa na jina, maneno kutoka kwa 'Mwandishi wetu' yalisomeka juu ya habari ile. Yule kijana akapiga hatua nyingine mbele, alifunua kurasa za ndani, kutafuta namba ya mhariri, aliipata.
Aliziandika zile namba za mhariri katika kidaftari chake kidogo, kisha kuzinakili katika simu yake na kuzipiga. Simu iliita.
"Hallo, habari yako?" Upande wa pili uliongea na kusalimia.
"Bila shaka naongea na mhariri wa gazeti la Shupavu?"
"Ndiye mwenyewe, nani mwenzangu?"
"Naitwa Daniel Mwaseba"
"Ahaa Daniel. Vipi kaka yangu"
"Nina shida ndogo sana Mhariri naomba unisaidie"
"Shida gani hiyo Daniel?"
"Nataka unitajie jina la mwandishi wako mmoja na namba yake ya simu"
"Yupi huyo?"
"Aliyeandika habari yenye kichwa cha habari..... Kilwa kuna balaa"
"Hiyo habari tumetumiwa na msomaji wetu, tena ilikuwa katika mtindo wa makala lakini sisi tukaamua tuiandike katika mfumo huo wa habari"
"Mmeipataje sasa ile habari?"
"Jamaa katutumia kwa email, na hatuna contact zake kabisa, zaidi ya hiyo email ambayo nayo kama imetelekezwa, maana tunajaribu kumuuliza vitu hamna majibu yoyote"
"Sasa kwanini mmeiweka ile habari ilhali hamna hata uhakika nayo?"
"Ile habari ina ukweli kwa asilimia mia moja, nenda Kilwa Daniel utayagundua makubwa kuliko hayo aliyoyaandika huyo jamaa"
"Nataka mawasiliano na huyo jamaa kwanza, ndipo niende Kilwa, hatuishi kwa hisia"
"Tutajitahidi kukutafutia kaka"

Kwa wanaomjua Daniel Mwaseba hakuwa mtu wa kuombwa kuingia katika msako au misheni ya kuwasaka maadui wa nchi ya Tanzania. Alikuwa kashaingia rasmi katika kadhia hii tangu alivyoamua tu kwenda kununua lile gazeti. Daniel Mwaseba alitoka nje ya nyumba yake, akapanda gari lake na safari ya kuelekea Kilwa ilianza..

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
 
Cover ya Balaa itakavyokuwa
 

Attachments

  • 1427008236841.jpg
    56.5 KB · Views: 646
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA SITINI NA TISA

Ndani ya kambi ya Don Genge hali ilikuwa mbaya sana. Watu wote mle ndani walikuwa na nakala ya gazeti la Shupavu mkononi, wakisoma habari ile mbaya sana iliyoandikwa na Mwandishi wetu. Wote walikuwa wamejiinamia chini, wamekuwa wadogo mithili ya piriton. Gazeti la Shupavu lilianika kila kitu kuhusu wao na mipango yao.

"Kuna msaliti kati yetu" Moja wa six killers aliropoka kwa sauti kubwa.
Wengine wote walikaa kimya, kama hawakuisikia ile kauli toka kwa Moja. Kilipita kimya cha dakika kama tano, Tano ambaye sasa alikuwa amepata nafuu kile kidonda cha goti alivunja ukimya.
"Hakuna msaliti..."
"Ilaaa...." Moja alidakia kabla Tano hajamalizia alichotaka kusema.
"Mimi nina wasiwasi Sita ametekwa, na ni yeye ndiye aliyetoa siri zetu hizi" Tano aliongea kwa upole.
Don Genge alimwangalia Tano kwa jicho Kali huku akitetemeka mikono kwa hasira.
"Sasa kama Sita kakamatwa si muda wowote nasi tutakamatwa?" Dokta Sharifa aliuliza huku sauti yake ikionesha woga dhahiri.
"Hatuwezi kukamatwa. Hata huyo Sita hapajui mahala hapa kwa usahihi wake, kama usivyopajua wewe, ila tatizo hatutofanya kazi yetu tena, maana pale, hospitalini kutakuwa na ulinzi mkali sana baada ya taarifa hii" Don Genge alifafanua.
"Kipo tutakachofanya, jamaa wanataka mioyo ya maiti kumi na tano kila siku, hawajari maiti ya mtoto mdogo au mkubwa. Itabidi twende mashuleni, tunawateka watoto, tunawauwa na kisha tunawatoa mioyo, zoezi la kutoa mioyo tutalifanyia hapa" Moja hakukubali kushindwa, alitoa wazo ambalo kila mmoja alilikubali kwa kichwa. Don Genge sasa akaelewa, kwanini jamaa amepewa namba moja katika kundi la six killers, alikuwa katili sana. Alikuwa na akili sana.

Mpango wa kuwateka watoto wa shule ulibarikiwa na wote. Wakisubiri kesho yake waanze kuufanyia kazi mpango huo mpya...

ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…