Songa Heri
JF-Expert Member
- Feb 6, 2016
- 1,723
- 1,872
RIWAYA; ANGAMIZO
MWANDISHI; HALFANI SUDY
Simu 0674 395733
Sehemu Ya Kwanza
Kumekucha Arusha. Jiji lilipo kaskazini mwa nchi ya Tanzania. Siku ilianza kwa manyunyu ya mvua na radi kidogo katika jiji la Arusha. Kutokana na manyunyu hayo ya mvua, hali ya ubaridi iliongezeka katika jiji la Arusha. Baridi iliyowafanya watu wengi kuyakumbuka makoti yao na kuyatia mwilini.
Siku hiyo ilikuwa ya furaha sana kwa Abdul Washiro. Ilikuwa siku ambayo alikuwa anatimiza ndoto kubwa sana katika maisha yake. Alichaguliwa kujiunga na chuo cha uhasibu Arusha. Jumatatu hiyo ndio Ilikuwa siku yake ya kuripoti pale chuoni.
Abdul alikuwa na furaha sana. Hata ile hali ya baridi haikumchukiza kabisa. Hakuwa anaihisi baridi kabisa. Mawazo yake yote yalikuwa juu ya kutimiza ndoto hiyo kubwa sana katika maisha yake. Wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza walikusanyika katika ukumbi wa chuo kwa ajili ya usajili. Walikuwa wanafunzi wengi sana kutoka mikoa mbali mbali Tanzania, waliokwenda jijini Arusha kuisaka elimu.
Baada ya maelezo ya awali ya utambulisho toka uongozi wa chuo pale ukumbini sasa ulifika muda wa kupanga foleni ili usajili uanze.
Kila mtu alikuwa anagombea nafasi ya kukaa mbele ili angalau asisote sana kwenye foleni. Ilikuwa ni fujo sana . Abdul alikaa kwenye kiti cha plastiki akiangalia vurugu zile.
Hakuwa na wasiwasi wowote, alijua maadamu amechaguliwa kujiunga na chuo kile, basi atasajiriwa tu.
Baada ya fujo kutulia, Abdul naye alienda kujiunga kwenye foleni. Alikuwa mtu wa mwisho katika foleni ile ya usajili. Alikaa kwenye foleni huku akiwaza safari yake ya elimu ilipotokea.
***
Abdul aliwaza jinsi alivyosoma kwa shida shule ya Sekondari Bagamoyo. Wazazi wake hawakuwa na uwezo wa kumsomesha. Hivyo alipata shida sana kupata mtu mwenye moyo wa kumsomesha. Ilibidi mchana asome sana, ili jioni afanye biashara ndogondogo ya kuuza karanga ili aweze kupata hela ya mahitaji madogomadogo ya shule. Baba yake Abdul alikuwa mvuvi . Lakini pesa akizopata kutokana na kazi yake ya uvuvi zilitosha kuilisha familia yake tu. Hii ilitokana na Mzee Washiro kuwa na familia kubwa ya watoto saba. Mama yake hakuwa na kazi zaidi ya kuchuuza samaki mtaani, samaki wa mumewe. Inamaana ilikuwa sawa na kusema, baba na mama yake Abdul walikuwa wanafanya biashara moja. Baba anavua samaki, tena kwa zana dhaifu za uvuvi na mama anawauza kwa kuwachuuza mtaani.
Katika watoto wote saba wa baba na mama Abdul. Abdul pekee ndio alikuwa anasoma shule. Wengine wote hawakutaka hata kusikia neno shule. Hawakuona umuhimu wa shule. Waliona kaka yao akivyoteseka kwa ajili ya kusoma. Kupata sare, madaftari na michango midogomidogo ilikuwa shida. Nduguze Abdul wote walikuwa wanashinda pwani wakijitafutia ridhiki. Hata hivyo hawakuwa wanapata ridhiki ya kutosha. Pamoja na shida zote hizo, Abdul alijitahidi sana katika masomo ili afanikiwe, na kuisaidia familia yake iliyotopea katika dimbwi la umaskini. Ukweli ni kwamba alikuwa anafanya vizuri sana darasani. Siku zote alikuwa anaamini elimu ndio mkombozi wake. Elimu ndio silaha pekee ya kuishika kwa maskini kama yeye. Na aliishika kweli elimu. Mungu hamtupi mja wake, alifanikiwa kumaliza kidato cha nne pale shule ya Sekondari Bagamoyo, na kufaulu vizuri sana. Abdul alichaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano katika shule ya Sekondari Ndanda. Pamoja na kuijua thamani ya elimu, lakini alipofaulu kwenda Ndanda, Abdul pia aliitambua thamani ya pesa. Alijua kwamba kumbe pesa na elimu vilikuwa vinaenda sambamba. Abdul hakuwa na pesa kabisa ya kuweza kumpeleka shule. Kwanza nauli kutoka Bagamoyo hadi Mtwara, mkoa iliyopo shule hiyo Ilikuwa mtihani. Hapo hujajumlisha pesa ya ada pamoja na vitu vingine vya shule. Ndoto yake ya kusoma Abdul ilikomea hapo. Alihisi hawezi tena kuendelea na kusoma. Hata wazazi wake walimwambia hivyo. Baba yake alikuwa na jukumu zito la kuhakikisha familia inakula, familia inatibiwa, familia inavaa pia . Hakuwa na kipato cha kutosha kumuwezesha Abdul kwenda Mtwara kusoma. Abdul alikuwa na akiba ya shilingi elfu kumi iliyotokana na biashara zake za kuuza karanga jioni. Kumbuka Abdul ndiye alikuwa mkubwa katika familia hii. Alikuwa na ndugu sita nyuma yake, wote wakimwangalia yeye. Aliamua kuzifuta kabisa fikra za kukata tamaa. Aliamini kukata tamaa ni dhambi kubwa sana katika maisha. Aliyakumbuka vizuri maneno ya Mwalimu wake wa Kiswahili wakati anasoma pale Bagamoyo sekondari.
"Usipende kukata tamaa ukiwa bado unaishi. Pambana hadi pumzi yako ya mwisho. Hakuna linaloshindakana chini ya jua". Maneno hayo ya mwalimu wake yalijirudia katika kichwa chake. Aliapa lazima asome kwa njia yoyote ile. Alikuwa anajiona mwenye wajibu wa baadae kuwasaidia wazazi wake. Kusaidia ndugu zake pia.
"Lazima nisome" Alihisi maneno hayo anayesema polepole maneno hayo. Haikuwa hivyo, yalisikiwa na mtu aliyekuwa mbele yake katika foleni ile ndefu ya usajili.
"Unaonekana una mawazo sana kaka" Sauti nyororo ya dada aliyekuwa mbele ya Abdul ilipenya kwenye masikio yake.
"Hapana, sina mawazo dada"
"Mbona unaongea peke yako sasa ?" Abdul hakujibu.
"Naitwa Mayasa"
"Naitwa Abdul"
"Tunaweza kuonana baadae sehemu tofauti na hapa?"
"Bila shaka"
Walibadilishana namba zao za simu palepale kwenye foleni. Zoezi la usajili lilichukuwa saa zipatazo tano. Hatimaye Abdul akasajiriwa kama mwanafunzi wa chuo cha uhasibu.
Baada ya kusajiriwa, Abdul alienda katika hosteli za chuo kupumzika. Alijilaza kitandani huku akikumbuka misukosuko ya safari yake ya kusaka elimu. Alikumbuka alivyoteseka kipindi kile anatafuta hela ya ada pamoja na ya matumizi ili aende kusoma shule ya Sekondari Ndanda. Alienda kuomba serikalini lakini hawakumuelewa. Alienda kuomba kwa Mbunge wake naye hakumuelewa . Hakupata hela ya ada, hakupata hela ya nauli. Bado alikuwa na elfu kumi ndani, chini ya mto wake wa kulalia.
Ilikuwa bado wiki moja ili shule ifunguliwe. Na Abdul akaanze kidato cha tano. Sasa ndoto yake ilikuwa inaanza kuyeyuka. Hakuwa na njia ya mkato ya kumpeleka shule.
" Si ruhusa kukata tamaa katika maisha ukiwa bado unaishi.." Kauli ya mwalimu wake ilijirudia tena katika kichwa chake.
"Sasa kwanini mimi naruhusu kukata tamaa nikiwa bado ninaishi. Tena na afya tele. Haiwezekani!
"Lazima niende Mtwara nikasome"
Usiku wa siku ile alipata wazo. Wazo ambalo lilipewa baraka na kichwa chake. Aliamua kwenda Mtwara kwa miguu. Alikuwa ameamua hivyo.
Usiku ule ule aliweka vitu vyake vyote sawa. Tayari kwa safari. Asubuhi aliwaambia wazazi wake.
"Baba na Mama mimi leo naenda shule "
"Umepata ada mwanangu ?" Mama yake alimuuliza kwa sauti yake ya upole.
" Hapana"
"Sasa utaenda vipi shule ?" Baba yake alimuuliiza nae.
" Kwa miguu"
"Miguu ?"
"Ndio wazazi wangu. Lazima niende Mtwara kusoma. Na nimeamua kwenda Mtwara kwa miguu !" Alisema akiwa anajiamini sana.
"Hivi Abdul unaujua umbali wa Mtwara kutoka hapa ?"
"Siujui, lakini nitafika "
"Ni mbali sana Mtwara, huwezi kwenda kwa miguu Abdul " Mama yake alimwambia kwa sauti yake ya upole.
"Nimeshafunga kila kitu changu. Ilibaki kuwaaga nyinyi na ndugu zangu. Nakubali Mtwara ni mbali. Lakini bila elimu safari yetu ya kuelekea kwenye mafanikio inazidi kuwa mbali. Bora niumie kwa kutembea kwa miguu kuisaka elimu. Kuliko kuumia kwa umaskini huu uliotukuka. Umaskini umeweka kambi nyumbani kwetu. Hautaki kutuacha hata kidogo. Na kitu pekee kinachoweza kuufukuza umaskini huu kipo Mtwara. Lazima niende Mtwara "
"Tufanye utaenda Mtwara kwa miguu. Je hela ya ada utaitoa wapi ?" Baba alimtupia swali zito. Alifikiria kidogo akajibu.
"Nitajua huko huko Mtwara. Lakini lazima nifike Mtwara kwanza. Mambo mengine yatajijibu huko huko."
Wazazi wake hawakuwa na jinsi. Walimruhusu aende Mtwara . Mama yake alikuwa analia machozi kwa kumuonea huruma Abdul. Baba yake alikuwa anamhurumia pia. Abdul alikuwa jasiri na imara katika msimamo wake. Alidhamiria kwenda kusoma Mtwara kwa njia yoyote ile . Baba aliwaita ndugu zake wote. Akawaambia juu ya safari ya Abdul ya kwenda shuleni Mtwara, tena kwa miguu. Ndugu zake wote walisikitika sana. Kila mmoja aliingia ndani na kutoa akiba aliyojiwekea na kumpa. Abdul alianza safari yake ya kutoka Bagamoyo kwenda Mtwara akiwa na elfu ishirini tu. Familia nzima aliiacha kwenye majonzi makuu. Hakujari. Hakusikitika. Alidhamiria kwenda kusoma. Alidhamiria kweli kwenda Mtwara kwa miguu.
Inaitwa Angamizo!! Kwanini Angamizo? Tuwe wote mwanzo mwisho katika riwaya hii kali.
Wale wanaohitaji Mkanda wa Siri season 2 tuchekiane WhatsApp 0674 395733 ni 2000 tu. Shukrani sana kwa wote walioniunga mkono. Sina cha kusema zaidi ya AHSANTE SANA!
MWANDISHI; HALFANI SUDY
Simu 0674 395733
Sehemu Ya Kwanza
Kumekucha Arusha. Jiji lilipo kaskazini mwa nchi ya Tanzania. Siku ilianza kwa manyunyu ya mvua na radi kidogo katika jiji la Arusha. Kutokana na manyunyu hayo ya mvua, hali ya ubaridi iliongezeka katika jiji la Arusha. Baridi iliyowafanya watu wengi kuyakumbuka makoti yao na kuyatia mwilini.
Siku hiyo ilikuwa ya furaha sana kwa Abdul Washiro. Ilikuwa siku ambayo alikuwa anatimiza ndoto kubwa sana katika maisha yake. Alichaguliwa kujiunga na chuo cha uhasibu Arusha. Jumatatu hiyo ndio Ilikuwa siku yake ya kuripoti pale chuoni.
Abdul alikuwa na furaha sana. Hata ile hali ya baridi haikumchukiza kabisa. Hakuwa anaihisi baridi kabisa. Mawazo yake yote yalikuwa juu ya kutimiza ndoto hiyo kubwa sana katika maisha yake. Wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza walikusanyika katika ukumbi wa chuo kwa ajili ya usajili. Walikuwa wanafunzi wengi sana kutoka mikoa mbali mbali Tanzania, waliokwenda jijini Arusha kuisaka elimu.
Baada ya maelezo ya awali ya utambulisho toka uongozi wa chuo pale ukumbini sasa ulifika muda wa kupanga foleni ili usajili uanze.
Kila mtu alikuwa anagombea nafasi ya kukaa mbele ili angalau asisote sana kwenye foleni. Ilikuwa ni fujo sana . Abdul alikaa kwenye kiti cha plastiki akiangalia vurugu zile.
Hakuwa na wasiwasi wowote, alijua maadamu amechaguliwa kujiunga na chuo kile, basi atasajiriwa tu.
Baada ya fujo kutulia, Abdul naye alienda kujiunga kwenye foleni. Alikuwa mtu wa mwisho katika foleni ile ya usajili. Alikaa kwenye foleni huku akiwaza safari yake ya elimu ilipotokea.
***
Abdul aliwaza jinsi alivyosoma kwa shida shule ya Sekondari Bagamoyo. Wazazi wake hawakuwa na uwezo wa kumsomesha. Hivyo alipata shida sana kupata mtu mwenye moyo wa kumsomesha. Ilibidi mchana asome sana, ili jioni afanye biashara ndogondogo ya kuuza karanga ili aweze kupata hela ya mahitaji madogomadogo ya shule. Baba yake Abdul alikuwa mvuvi . Lakini pesa akizopata kutokana na kazi yake ya uvuvi zilitosha kuilisha familia yake tu. Hii ilitokana na Mzee Washiro kuwa na familia kubwa ya watoto saba. Mama yake hakuwa na kazi zaidi ya kuchuuza samaki mtaani, samaki wa mumewe. Inamaana ilikuwa sawa na kusema, baba na mama yake Abdul walikuwa wanafanya biashara moja. Baba anavua samaki, tena kwa zana dhaifu za uvuvi na mama anawauza kwa kuwachuuza mtaani.
Katika watoto wote saba wa baba na mama Abdul. Abdul pekee ndio alikuwa anasoma shule. Wengine wote hawakutaka hata kusikia neno shule. Hawakuona umuhimu wa shule. Waliona kaka yao akivyoteseka kwa ajili ya kusoma. Kupata sare, madaftari na michango midogomidogo ilikuwa shida. Nduguze Abdul wote walikuwa wanashinda pwani wakijitafutia ridhiki. Hata hivyo hawakuwa wanapata ridhiki ya kutosha. Pamoja na shida zote hizo, Abdul alijitahidi sana katika masomo ili afanikiwe, na kuisaidia familia yake iliyotopea katika dimbwi la umaskini. Ukweli ni kwamba alikuwa anafanya vizuri sana darasani. Siku zote alikuwa anaamini elimu ndio mkombozi wake. Elimu ndio silaha pekee ya kuishika kwa maskini kama yeye. Na aliishika kweli elimu. Mungu hamtupi mja wake, alifanikiwa kumaliza kidato cha nne pale shule ya Sekondari Bagamoyo, na kufaulu vizuri sana. Abdul alichaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano katika shule ya Sekondari Ndanda. Pamoja na kuijua thamani ya elimu, lakini alipofaulu kwenda Ndanda, Abdul pia aliitambua thamani ya pesa. Alijua kwamba kumbe pesa na elimu vilikuwa vinaenda sambamba. Abdul hakuwa na pesa kabisa ya kuweza kumpeleka shule. Kwanza nauli kutoka Bagamoyo hadi Mtwara, mkoa iliyopo shule hiyo Ilikuwa mtihani. Hapo hujajumlisha pesa ya ada pamoja na vitu vingine vya shule. Ndoto yake ya kusoma Abdul ilikomea hapo. Alihisi hawezi tena kuendelea na kusoma. Hata wazazi wake walimwambia hivyo. Baba yake alikuwa na jukumu zito la kuhakikisha familia inakula, familia inatibiwa, familia inavaa pia . Hakuwa na kipato cha kutosha kumuwezesha Abdul kwenda Mtwara kusoma. Abdul alikuwa na akiba ya shilingi elfu kumi iliyotokana na biashara zake za kuuza karanga jioni. Kumbuka Abdul ndiye alikuwa mkubwa katika familia hii. Alikuwa na ndugu sita nyuma yake, wote wakimwangalia yeye. Aliamua kuzifuta kabisa fikra za kukata tamaa. Aliamini kukata tamaa ni dhambi kubwa sana katika maisha. Aliyakumbuka vizuri maneno ya Mwalimu wake wa Kiswahili wakati anasoma pale Bagamoyo sekondari.
"Usipende kukata tamaa ukiwa bado unaishi. Pambana hadi pumzi yako ya mwisho. Hakuna linaloshindakana chini ya jua". Maneno hayo ya mwalimu wake yalijirudia katika kichwa chake. Aliapa lazima asome kwa njia yoyote ile. Alikuwa anajiona mwenye wajibu wa baadae kuwasaidia wazazi wake. Kusaidia ndugu zake pia.
"Lazima nisome" Alihisi maneno hayo anayesema polepole maneno hayo. Haikuwa hivyo, yalisikiwa na mtu aliyekuwa mbele yake katika foleni ile ndefu ya usajili.
"Unaonekana una mawazo sana kaka" Sauti nyororo ya dada aliyekuwa mbele ya Abdul ilipenya kwenye masikio yake.
"Hapana, sina mawazo dada"
"Mbona unaongea peke yako sasa ?" Abdul hakujibu.
"Naitwa Mayasa"
"Naitwa Abdul"
"Tunaweza kuonana baadae sehemu tofauti na hapa?"
"Bila shaka"
Walibadilishana namba zao za simu palepale kwenye foleni. Zoezi la usajili lilichukuwa saa zipatazo tano. Hatimaye Abdul akasajiriwa kama mwanafunzi wa chuo cha uhasibu.
Baada ya kusajiriwa, Abdul alienda katika hosteli za chuo kupumzika. Alijilaza kitandani huku akikumbuka misukosuko ya safari yake ya kusaka elimu. Alikumbuka alivyoteseka kipindi kile anatafuta hela ya ada pamoja na ya matumizi ili aende kusoma shule ya Sekondari Ndanda. Alienda kuomba serikalini lakini hawakumuelewa. Alienda kuomba kwa Mbunge wake naye hakumuelewa . Hakupata hela ya ada, hakupata hela ya nauli. Bado alikuwa na elfu kumi ndani, chini ya mto wake wa kulalia.
Ilikuwa bado wiki moja ili shule ifunguliwe. Na Abdul akaanze kidato cha tano. Sasa ndoto yake ilikuwa inaanza kuyeyuka. Hakuwa na njia ya mkato ya kumpeleka shule.
" Si ruhusa kukata tamaa katika maisha ukiwa bado unaishi.." Kauli ya mwalimu wake ilijirudia tena katika kichwa chake.
"Sasa kwanini mimi naruhusu kukata tamaa nikiwa bado ninaishi. Tena na afya tele. Haiwezekani!
"Lazima niende Mtwara nikasome"
Usiku wa siku ile alipata wazo. Wazo ambalo lilipewa baraka na kichwa chake. Aliamua kwenda Mtwara kwa miguu. Alikuwa ameamua hivyo.
Usiku ule ule aliweka vitu vyake vyote sawa. Tayari kwa safari. Asubuhi aliwaambia wazazi wake.
"Baba na Mama mimi leo naenda shule "
"Umepata ada mwanangu ?" Mama yake alimuuliza kwa sauti yake ya upole.
" Hapana"
"Sasa utaenda vipi shule ?" Baba yake alimuuliiza nae.
" Kwa miguu"
"Miguu ?"
"Ndio wazazi wangu. Lazima niende Mtwara kusoma. Na nimeamua kwenda Mtwara kwa miguu !" Alisema akiwa anajiamini sana.
"Hivi Abdul unaujua umbali wa Mtwara kutoka hapa ?"
"Siujui, lakini nitafika "
"Ni mbali sana Mtwara, huwezi kwenda kwa miguu Abdul " Mama yake alimwambia kwa sauti yake ya upole.
"Nimeshafunga kila kitu changu. Ilibaki kuwaaga nyinyi na ndugu zangu. Nakubali Mtwara ni mbali. Lakini bila elimu safari yetu ya kuelekea kwenye mafanikio inazidi kuwa mbali. Bora niumie kwa kutembea kwa miguu kuisaka elimu. Kuliko kuumia kwa umaskini huu uliotukuka. Umaskini umeweka kambi nyumbani kwetu. Hautaki kutuacha hata kidogo. Na kitu pekee kinachoweza kuufukuza umaskini huu kipo Mtwara. Lazima niende Mtwara "
"Tufanye utaenda Mtwara kwa miguu. Je hela ya ada utaitoa wapi ?" Baba alimtupia swali zito. Alifikiria kidogo akajibu.
"Nitajua huko huko Mtwara. Lakini lazima nifike Mtwara kwanza. Mambo mengine yatajijibu huko huko."
Wazazi wake hawakuwa na jinsi. Walimruhusu aende Mtwara . Mama yake alikuwa analia machozi kwa kumuonea huruma Abdul. Baba yake alikuwa anamhurumia pia. Abdul alikuwa jasiri na imara katika msimamo wake. Alidhamiria kwenda kusoma Mtwara kwa njia yoyote ile . Baba aliwaita ndugu zake wote. Akawaambia juu ya safari ya Abdul ya kwenda shuleni Mtwara, tena kwa miguu. Ndugu zake wote walisikitika sana. Kila mmoja aliingia ndani na kutoa akiba aliyojiwekea na kumpa. Abdul alianza safari yake ya kutoka Bagamoyo kwenda Mtwara akiwa na elfu ishirini tu. Familia nzima aliiacha kwenye majonzi makuu. Hakujari. Hakusikitika. Alidhamiria kwenda kusoma. Alidhamiria kweli kwenda Mtwara kwa miguu.
Inaitwa Angamizo!! Kwanini Angamizo? Tuwe wote mwanzo mwisho katika riwaya hii kali.
Wale wanaohitaji Mkanda wa Siri season 2 tuchekiane WhatsApp 0674 395733 ni 2000 tu. Shukrani sana kwa wote walioniunga mkono. Sina cha kusema zaidi ya AHSANTE SANA!