Rished Bade kumsaidia Kitillya TRA





Tafakari.........................
 
Hii benki ya Baclays Bank managing director wake ni Rished Bade ambaye anatoka Arusha na wana undugu na Idrisa Rashid managing director wa Tanesco.Huyu Rashid Bade walikuwa wote benki kuu ya Tanzania wakati Idrisa Rashid akiwa gavana wa Benki kuu.Hivyo kama mikopo ilichukuliwa Baclays twaweza unganisha dots.Pia ile mipesa ya EPA na Richmond iliyopitia CRDB kwa managing director Kimei haikuwa bahati mbaya.Kimei alikuwa ni mkurugenzi benki kuu wakati Idrisa Rashid alipokuwa gavana wa benki kuu.Kwa hiyo Idrisa Rashid,Rished Bade na Kimei wanafahamiana sana tu na kwa karibu wakiwa benki kuu na baada ya kutoka benki kuu inaelekea wameendeleza mtandao fulani wa kuliza nchi.

Kiufupi twaweza kusema unapoongelea ufisadi na connection na benki kuu Rished bade,Idrisa na Kimei wako connected Kiuhalifu unaohusu ndani na nje ya benki kuu kupitia EPA,Richmond,Dowans.Maana mapesa yaliibwa benki kuu yakaenda CRDB mengine yakaibwa kupitia Richmond yakaenda CRDB na mengine yakakopwa Baclays sijui yalienda wapi kama mmiliki anakana kuwa hakukopa labda yalifanyiwa money laundering kupitia benki fulani yakayeyukia kule kunakofanana na wanakoficha pesa akina chenge na wengineo.
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/25556-new-revelation-dowans-in-huge-debt-5.html
 

Mkatoliki safi
 
uteuzi wowote wa d.haifu huwa nina mashaka nao maana jamaa hateui bila maslahi binafsi..poor tanzania rais anateua kila mtu,alibakisha kuteua wake za wateule wake tu
 
Jamani huyu c ndo ameua Barclay Bank (T)?? alikuwa anatoa mikopo kwa marafiki zake tuu mpk ikapata hasara ndo akaja mkenya??? Kweli tanzania hii kuwa uyaone...Kila kitu ni kujuana na si utendaji.....Hakika huko TRA marafiki zake hatalipa tena kodi
 
Kikubwa usiminye wafanya biashara wadogo wadogo waliopo vyama vya upinzani kwa manufaa ya ccm
 
Rished Bade ni kichwa kweli kwa akili za darasani,kuhusu utendaji sifahamu! Lakini nadhani uteuzi huu utakua na mkono wa Dr. I. Rashid ambaye ni mtu wake wa karibu sana.
 
Kaka yake Bashir msomali, MD wa Stambic Tanzania.
Hawa wote washikaji wa JK na ndo financial supporters wa CCM wakati wa uchaguzi kwa influence zao.
Jk group: Marsha, Othman, Bashir, Ray, Magai, Ishengoma, Mujurizi, Rukaza na huyu bwana mteule.
 
Kama anaweza poa@ Ila hizi post Kubwa kubwa tuhakikishe Tunawapa Wazawa asije Kuwa Msomali Huyo!!
 

Ana CV nzuri ya banking & Finance, nafikiri ni mtu mzuri anaejua kutumia human resources zake ndio maana anaonekana amekuwa na achievement katika sehemu nyingi alizopita, binafsi namtakia kila la kheri katika kazi yake hiyo mpya.
 
Kiutendaji alipokuwa Barclays Bank alitaka kufanya Rapid Expansion ya Bank hiyo Tanzania kwa bahati mbaya sana mpango wake ulikumbwa na wizi mkubwa sana. Si unakumbuka kipindi cha wafanyakazi wa benki kuipiga barclays Bank. Yaani kulikuwa na fraud sana ambazo zilifanywa na wafanyakazi wa chini. Kwaiyo yeye anaweza kulaumiwa kwa kushindwa kuweka strict control mechanism za kufanya benki isiibiwe sana kwa kiasi kile,otherwise anajitahidi. Lakini wapo wengi wazuri ambao wangeweza kushika nafasi hiyo si mnajua tena mambo ya nchi hizi nani anakujua matters zaidi kuliko uwezo ulionao.Ilitakiwa nafasi hii itangazwe kwa watanzania wote na watu waombe kisha interview ifanyike mwenye uwezo apate. Nchini Uganda katika URA nafasi huwa zinatangazwa na watu wanaomba interview inafanyika kisha aliyeshinda anatangazwa na Board Ya URA kama mshindi. Na nafasi kama hizi kwa UGANDA ni za Mkataba kwa maana ukishindwa ku perform unaondolewa. Kwa mtazamo wangu huyu mtu anauzoefu zaidi wa mambo ya mabenki kwaiyo angeweza kufaa zaidi BOT. kWA TRA itabidi ajifunze zaidi kwani issue hapa siyo mortgage finance au banking business bali ni Collections ya Taxes.
 
Niliwai kusema kua Tajiri anazidi kupewa utajiri na masikini anazidi kuelemewa na umasikini..Rished Bade alikua bosi wangu pale Barclays Bank..ivi hii Serikali yetu ikoje lakini au ndio Nguvu mpya na kujinufaisha na utajiri hivi hakuna wasomi kuliko yeye??????????????? au ndio analipwa fadhila baada ya kutoa mahela yake kipindi JK akiomba kura???
 

Umeunganisha vizuri dots za mahusiano sema umekuja kuharibu na habari zako za Dowans na EPA.

Hadi DR Rashidi anaondoka BOT bado mambo ya kula hela za EPA hayajaanza, just for your info!
 
Ilo jina sasa khaa pande za wapi Tanganyika ya mwalimu maana limekaa mahadhi ya kiarabu kama sio kisomali
Wanaomjua pls
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…