Risasi zarindima mtaa wa swahili

Risasi zarindima mtaa wa swahili

kisale

Senior Member
Joined
Mar 3, 2009
Posts
111
Reaction score
1
HABARI TOKA MTAA WA MSIMBAZI JIJINI DAR SASA HIVI ZINASEMA KUNA MAPAMBANO MAKALI KATI YA POLISI NA WATU WANAOSADIKIWA KUWA NI MAJAMBAZI.
wadau mliopo karibu na maeneo hayo tunaomba ripoti.
 
Taarifa za hivi Punde zinadai mapambano yamemalizika na Polisi wamefanikiwa kuyatia nguvuni majambazi matano.matatu yamejeruhiwa vibaya sana.
 
HABARI TOKA MTAA WA MSIMBAZI JIJINI DAR SASA HIVI ZINASEMA KUNA MAPAMBANO MAKALI KATI YA POLISI NA WATU WANAOSADIKIWA KUWA NI MAJAMBAZI.
wadau mliopo karibu na maeneo hayo tunaomba ripoti.

jamani, wizi asubuhi asubuhi namna hii, Mungu tu ajalie wasiuliwe raia wasio na hatia kwani msongamano uliopo kariakoo mhh..
 
Jamani mbona kuna mdau amenipigia simu sasa hivi anasema mitaa yote ya kuingia kkoo imefungwa??? Sijui kama ka mradi kangu kamepona pale mtaa wa Nyarung'ombe!! Najaribu kuwatafuta wasaidizi wangu pale kkoo siwapati!!
 
tetesi zasema majambazi hawa walijaribu kupora Bereau de change moja karibu na nbc msimbazi. Polisi wamejitahidi sana kuwadhibiti na wamekamatwa.

Lets wait for more updates.
 
Mbona hizi taarifa zinakuja in pieces? hakuna mtu mwenye data zilizokamilika wakuu......?
 
Next Level
Si unajua tena, breaking news lazima ziji break into pieces? Natania tu
Ila Tanzania tukicheza mambo yatakuwa mabaya zaidi, majambazi yanajijenga upya kwa ari, kasi na nguvu mpya
 
inabidi tuombee majeruhi wapone waweze kubana wawataje wenzao ktk mtandao...
 
Polisi wakiamua kufanya kazi ya ukweli na ya kuaminika wanaifanya bila shida...
Ishu kama hiyo imo ndani kabisa ya uwezo wao..... Tunawaaminia na kuwasupport.

Taarifa kuja into pieces usiogope bwana NEXT LEVEL... kAMA ulivyosoma hapo, Kova atatupa full scandal badae.....Tulia
 
Tuwapongeze vijana wetu polisi waliokuwa doria huko na kufanya kweli. Pia msamaria mwema aliyetia taarifa hizi maana mipango kama hiyo huwa inapangwa kwa muda, hivyo pia tumshukuru aliyezivujisha habari za mipango hiyo. Pia hii ni changamoto kwa Jeshi lote la polisi maana ujambazi umeanza kuibuka tena kwa kasi baada ya kutulia kwa kiasi mpaka wengine tumepata usingizi majumbani mwetu. Usingizi wetu huu usiwakumbe jeshi la polisi maana kila kukicha majambazi wanapanga mbinu mpya za ujambazi!! Kova please, jitahidi!! na tuko nyuma yako.

Kwa sasa ujambazi umeanza kwa kasi Dar na Arusha!!
 
Polisi wakiamua kufanya kazi ya ukweli na ya kuaminika wanaifanya bila shida...
Ishu kama hiyo imo ndani kabisa ya uwezo wao..... Tunawaaminia na kuwasupport.

Taarifa kuja into pieces usiogope bwana NEXT LEVEL... kAMA ulivyosoma hapo, Kova atatupa full scandal badae.....Tulia

Ni kweli polisi wakiamua kazi wanaifanya vizuri hasa pale majambazi hao wanafanikiwa mara ya kwanza na badala ya kukata fungu kama walivyoahidiana wanayeyusha na kusema hawakupiga nyingi. Next time polisi wanakuwa na kisasi nao na kuamua kulipiza kisasi cha kunyimwa mgao wa mwanzo.

Walininikamata hawa wenye difenda one day, na kutaka niwape laki tano kwa bahati nzuri akapita afande mmoja ananijua, akaniambia hao jamaa ni wabaya wanavisasi niwape hata hela ya soda vinginevyo wanaweza hata kunishambulia siku ingine kwa risasi wakiniita jambazi. Yaani hakuna kosa lolote zaidi ya kuendeshwa na mtu aliye na leseni changa gari ikatuzimikia barabarani si unajua manual, wakang'ang'ani tunafudishana, hawakutaka kuona leseni wala nini, ukawa ubishi mkubwa ila sikuwapa hata shillingi maana ilibidi watupeleke kituoni.

Credit kwa baadhi:
kuna baadhi ya polisi wazuri na wachapa kazi hasa na waaminifu ila wanavunjwa nguvu na wenzao wachache na maslahi duni wanayolipwa wakati wakiwaona wenzao wasio waaminifu wanajenga mahekalu na kununua magari ya kifahari kwa kushirikiana na majambazi.
 
HABARI TOKA MTAA WA MSIMBAZI JIJINI DAR SASA HIVI ZINASEMA KUNA MAPAMBANO MAKALI KATI YA POLISI NA WATU WANAOSADIKIWA KUWA NI MAJAMBAZI.
wadau mliopo karibu na maeneo hayo tunaomba ripoti.

Ni mambo ya kawaida hayo Hapa jijini DAr
 
Wamesema kova atatoa taarifa baadaye leo mchana

Hizi tetesi bwana.....
Ngoja nisubiri taarifa kamili maana unaweza kuta sio majambazi yakawa kama mambo yanayomuandama Zombe!
 
Raia mwema mmoja aliyeiacha chai yake kwenda kuangalia risasi ameambulia hali ya u nusu mauti baada ya kuchabangwa risasi ya mbavuni.
Amekimbizwa muhimbili ili kujaribu kuiunganisha roho yake na mwili, maana inaweeza kukatika kutoka mwilini muda wowote maana alikuwa ana breed sana.
 
Raia mwema mmoja aliyeiacha chai yake kwenda kuangalia risasi ameambulia hali ya u nusu mauti baada ya kuchabangwa risasi ya mbavuni.
Amekimbizwa muhimbili ili kujaribu kuiunganisha roho yake na mwili, maana inaweeza kukatika kutoka mwilini muda wowote maana alikuwa ana breed sana.

Mkuu zingatia matumizi ya r na l vinginevyo neno linapoteza maana halisi.
Breed=Bleed?!
 
Inajulikana wazi kuwa Kova ana usongo na majambazi na aliahidi mwanzoni kuwa ama zao ama zake na ndio tunaona juhudi zake kuwa,kila wanapokutana face to face watamkamata japo mmoja.
 
Back
Top Bottom