Ripoti ya mauaji ya raia Dar sasa kesho

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,266
33,039
Kova%2811%29.jpg

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova.



Ripoti ya timu iliyoundwa na Jeshi la Polisi nchini kuchunguza mauaji ya raia Octavian Kashita, ambaye alipigwa risasi na polisi wa kituo cha Oysterbay, inatarajiwa kuwekwa hadharani kesho.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema taarifa hizo ni pamoja na timu mbalimbali walizowahi kuziunda ambazo zilikuwa zikichunguza matukio ya mauaji ya raia yaliyofanywa na askari wake jijini Dar es Salaam.
"Ripoti za matukio hayo zilikuwa zimekamilika lakini tulikuwa hatujaziweka wazi kwenye jamii," alifafanua.
Kamanda Kova alisema kwa sasa timu inayochunguza mauaji ya Kashita inaendelea na kazi ya kuchunguza taarifa mbalimbali walizozipokea kutoka kwa wananchi.
Aidha, aliwataka mtu yeyote mwenye taarifa, apige simu namba 0715 748333.
Mauaji ya raia huyo yalitokea Jumapili ya wiki iliyopita baada ya askari watano wa kituo cha polisi Oysterbay kupata taarifa za kuwepo kwa watekaji eneo la Victoria karibu na nyumba za viongozi wa serikali.
Askari hao ni Koplo Ahmad, Detective Cyprian, PC Kombo, PC Kasa na PC Charles ambao kwa sasa wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi.



CHANZO: NIPASHE
 
blaaaah,blaaaaaaaaaah,blaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaha,blaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaablllllllllllllllaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.hili zee jitu la wapi hili???natamani ningekua prezidaa nikalikata makofi mawili matatu na hizi taarifa zake za kifala huku linaripoti kifo cha mtu,watu wanasikitika mtu katutoka we unaKUJA NA MLOLONGO WA TAARIFA YA UCHUNGUZI WA POLISI WAKATI POLISI NDIO KAUA?NONSENSE.katika watu watakufa vibaya wewe kova wa kwanza maana una-cover habari ya kifo kama vile unasimulia mwali alivyoolewa kwa mbwembwe.:angry:
 
Kova%2811%29.jpg

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova.



Ripoti ya timu iliyoundwa na Jeshi la Polisi nchini kuchunguza mauaji ya raia Octavian Kashita, ambaye alipigwa risasi na polisi wa kituo cha Oysterbay, inatarajiwa kuwekwa hadharani kesho.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema taarifa hizo ni pamoja na timu mbalimbali walizowahi kuziunda ambazo zilikuwa zikichunguza matukio ya mauaji ya raia yaliyofanywa na askari wake jijini Dar es Salaam.
"Ripoti za matukio hayo zilikuwa zimekamilika lakini tulikuwa hatujaziweka wazi kwenye jamii," alifafanua.
Kamanda Kova alisema kwa sasa timu inayochunguza mauaji ya Kashita inaendelea na kazi ya kuchunguza taarifa mbalimbali walizozipokea kutoka kwa wananchi.

Aidha, aliwataka mtu yeyote mwenye taarifa, apige simu namba 0715 748333.
Mauaji ya raia huyo yalitokea Jumapili ya wiki iliyopita baada ya askari watano wa kituo cha polisi Oysterbay kupata taarifa za kuwepo kwa watekaji eneo la Victoria karibu na nyumba za viongozi wa serikali.
Askari hao ni Koplo Ahmad, Detective Cyprian, PC Kombo, PC Kasa na PC Charles ambao kwa sasa wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi.



CHANZO: NIPASHE

Wahenga walisema tomorrow never comes, kamanda Kova kesho uliyoisema ni ya terehe 20 may 2010 au ya siku utakayoulizwa, hata kama ni mwaka kesho?????

Jamani kama hiyo ripoti imetolewa na mtu anayo sio mbaya akiweka jamvini.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom