Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,266
- 33,039
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova.
Ripoti ya timu iliyoundwa na Jeshi la Polisi nchini kuchunguza mauaji ya raia Octavian Kashita, ambaye alipigwa risasi na polisi wa kituo cha Oysterbay, inatarajiwa kuwekwa hadharani kesho.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema taarifa hizo ni pamoja na timu mbalimbali walizowahi kuziunda ambazo zilikuwa zikichunguza matukio ya mauaji ya raia yaliyofanywa na askari wake jijini Dar es Salaam.
"Ripoti za matukio hayo zilikuwa zimekamilika lakini tulikuwa hatujaziweka wazi kwenye jamii," alifafanua.
Kamanda Kova alisema kwa sasa timu inayochunguza mauaji ya Kashita inaendelea na kazi ya kuchunguza taarifa mbalimbali walizozipokea kutoka kwa wananchi.
Aidha, aliwataka mtu yeyote mwenye taarifa, apige simu namba 0715 748333.
Mauaji ya raia huyo yalitokea Jumapili ya wiki iliyopita baada ya askari watano wa kituo cha polisi Oysterbay kupata taarifa za kuwepo kwa watekaji eneo la Victoria karibu na nyumba za viongozi wa serikali.
Askari hao ni Koplo Ahmad, Detective Cyprian, PC Kombo, PC Kasa na PC Charles ambao kwa sasa wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi.
CHANZO: NIPASHE