Abu Ubaidah Commando
JF-Expert Member
- Sep 8, 2016
- 7,590
- 6,956
MOSSAD wako vizuri lakini nadhani sehemu nyingine wanazidisha na kufanya propaganda ili kutishia watu hasa maadui zao (Psychological Warfare). Warusi na Wamarekani walikuwa wanatumia sana hii mbinu kipindi cha vita baridi. Mashirika ya kijasusi yakitoa taarifa usiziamini sana, nyingi huwa zimechakachuliwa au siyo za kweli.
Binafsi naamini CIA na MI6 zina mikono mirefu sana kuliko MOSSAD: Hata leo hii ukiwatoa CIA na MI6 sidhani kama Israeli inaweza kuwa salama hata kidogo. Edward Snowden anasema taarifa zote kutoka NSA vyombo vya ujasusi vya Israel hupewa bure bila kuchujwa.
Mfano mzuri kabisa, mikakati dhidi ya Iran nchi ya Israeli haiwezi kufanikisha yenyewe peke yake mpaka Marekani na Uingereza, kama angekuwa anaweza basi angekuwa keshamtwanga Iran mapema sana lakini huo uwezo hana.
Meir Dagan baada ya kustaafu alipohojiwa kuhusu Israel kuvamia Iran alisema "Iran is a big for Israel to fry alone" Akashauri kabisa Israel isijidanganye kuvamia Iran, madhara kwake yatakuwa makubwa sana.
CC: chige
Mkuu, wewe huwa nakubali hoja zako.penye ukweli unasema ukweli. Lakini kuna wengine humu ushabiki umewajaa na kukimbilia kukashifu imani za wengine.