ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,064
- 49,749
Mawaziri dizaini ya Hawa wanakuwa wamevimbiwa madaraka,Kuna mtumishi wa Umma Huwa anaenda Dodoma kujifurahisha?
Ukiona hivyo ujue mambo ni pending na ya muda mrefu kiasi huyo Afisa Utumishi anakosa jawabu la Moja kwa Moja.
Kabla ya kutoa Kauli za ajabu ajabu muwe mnatafakari kwanza.
---
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amepiga marufuku tabia ya baadhi ya maofisa utumishi kutoa vibali vya safari kwa watumishi kwenda Dodoma, kufuatilia masuala binafsi ya kiutumishi.
Kwa mujibu wa Naibu Waziri huyo, hiyo ni kazi ya maofisa utumishi hao, kwani wengi wa watumishi wanaokwenda Dodoma, hufuatilia masuala yahusuyo kupandishwa madaraja, kubadilishiwa miundo na kada, au kudai malimbikizo ya mshahara.
"Vitendo kama hivi, vinawanyima wananchi haki yao na fursa ya kuhudumiwa na watumishi hao ambao hulazimika kusafiri na hivyo kuwa nje ya vituo vyao vya kazi," amesema.
Ridhiwani ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ikiwa ni siku yake ya tatu ya ziara anayoendelea kufanya mkoani Mara, ambapo amewataka maofisa hao kuleta matumaini kwa wenzao.
"Acheni ile tabia ya kuonekana miungu watu, tatueni matatizo ya watumishi," amesema.
Pia amewaagiza maofisa utumishi wa halmashauri zote nchini kuacha tabia ya kukaa ofisini badala yake watembelee ofisi zilizopo katika kata na vijiji ili kutatua changamoto za watumishi walioko huko.
Ukiona hivyo ujue mambo ni pending na ya muda mrefu kiasi huyo Afisa Utumishi anakosa jawabu la Moja kwa Moja.
Kabla ya kutoa Kauli za ajabu ajabu muwe mnatafakari kwanza.
---
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amepiga marufuku tabia ya baadhi ya maofisa utumishi kutoa vibali vya safari kwa watumishi kwenda Dodoma, kufuatilia masuala binafsi ya kiutumishi.
Kwa mujibu wa Naibu Waziri huyo, hiyo ni kazi ya maofisa utumishi hao, kwani wengi wa watumishi wanaokwenda Dodoma, hufuatilia masuala yahusuyo kupandishwa madaraja, kubadilishiwa miundo na kada, au kudai malimbikizo ya mshahara.
"Vitendo kama hivi, vinawanyima wananchi haki yao na fursa ya kuhudumiwa na watumishi hao ambao hulazimika kusafiri na hivyo kuwa nje ya vituo vyao vya kazi," amesema.
Ridhiwani ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ikiwa ni siku yake ya tatu ya ziara anayoendelea kufanya mkoani Mara, ambapo amewataka maofisa hao kuleta matumaini kwa wenzao.
"Acheni ile tabia ya kuonekana miungu watu, tatueni matatizo ya watumishi," amesema.
Pia amewaagiza maofisa utumishi wa halmashauri zote nchini kuacha tabia ya kukaa ofisini badala yake watembelee ofisi zilizopo katika kata na vijiji ili kutatua changamoto za watumishi walioko huko.