MPIGA ZEZE
JF-Expert Member
- May 16, 2011
- 2,539
- 2,296
Kuna utata gani kwenye tamko la Riz jamani kama si kumfanyia roho mbaya na wivu wa kike?. Kikwete anapokea watoto wa kambo nanyinyi mnaweza kuomba kuwa watoto wa kikwete ili muache wivu.
Hiyo singo ya 'wivu' tena 'wivu wa kike' imeishazoeleka sana katika masikio ya wabongo - magamba hayataki kukosolewa na hivyo kila anayejaribu kuwakosoa wanamchezea singo hiyo hiyo. Huyu kijana kama alivyo mzee wake wanapaswa kujitambua kuwa ni watu maarufu sana nchini, kwa hiyo hawana budi waache tabia za uswahili za kuzungumzia masuala mazito kwa kutumia mipasho. Tunawaheshimu sana na hivyo na wao wanahitajika kujiheshimu. Hili ni mojawapo ya fundisho - matumaini bwana mdogo ataanza kuwa mwangalifu kabla ya kufungua kinywa chake.