Riba kwenye Mabenki ni Jipu kubwa sana

Riba kwenye Mabenki ni Jipu kubwa sana

Leo naomba ruhusa yenu nieleze kidogo kuhusu mkopo wa biashara.
U apotaka kuchukua mkopp wa biashara zingatia yafuatayo:
1.Uwe na biashara tayari
usikope ili kuanzisha biashara. Fanya biashara kwa mtaji wako kwa angalau mwaka mmoja bila mkopo. Hii itakusaidia kujua majira na misimu ya biashara. Lini onakuwa vizuri na lini inakuwa ovyo. Kwa biashara nyingi mwanzo wa mwaka na katikati ya mwaka huwa tofauti sana kimzunguko.
2. Usikope pesa nyingi kuliko mtaji wako. hii itakusaidia kurudisha pesa ya mkopo bila shida na hutaona mkopo kuwa ni mzigo.
3. Unapokopa hakikisha una uwezo wa kupata riba nje ya mtaji wako. Yaani itokane na faida ya biashara. Halafu ndio upambane kuizalisha ile hela ilo unapoirudisha isikuachie pengo kubwa.
4. Rejesho lisizidi nusu ya faida yako. Unapokopa hakikisha rejesho halizidi faida upatayo. ukifanikiwa katika hilo ni lazima upige hatua hadi watu washangae. Mf. manunuzi ni milioni 3 na mauzo ni milioni 4.8 Ukiwa na rejesho lisilozidi laki 9 utafurahia biashara yako ikiwa na mkopo. kila la heri!
 
Basi nawewe ukinunua mzigo elfu tano uza kwa elfu tano hiyohiyo kama ni mfanyabiashara...maana hujielewi
dah ishu inakuja kumuelekeza mtu ambaye hana akili ya kubadili msimamo wake lakin ngoja nijaribu hivi.....katika mabank wew ukienda kuweka 20.000 kwenye bank yoyote wao wanaenda kuifanyia biashara hiyo pesa yako na wew umeweka 20.000 yako ukiitaka utaenda kuichukua mda wowote. Pili kama ukikopa pesa bank mfano 5000 ukaenda kufanya biashara yako ya kuuza ice cream na baadae ukapata faida mda ukifika wa kurudisha hiyo 5000 uliyokopa urudishe kama ilivyo

umezungumzia mm nikinunua mzigo 5000 then nikauze hiyo hiyo elfu tano hapo utakua una maanisha hata kodi nisilipe ila inabd ujiongeze mwenyew ishu hapo ni riba dhulma kubwa na wizi mkubwa ambao watu wanaujua lakin hawataki kuuacha sio wanaodhulumiwa wala wanaodhulum na wanaishia kulalamika kwenye social media
by the way poleni safari bado ni ndefu sana
 
Kwa wale ambao wanahitaji mikopo au wanaofanya shughuli zao kwa kutegemea facilities za Mabenki kwa kweli hili jipu linahitajika kuangaliwa upya.

Kwa hapa nchini ukiangalia Prime Lending Rates kwa kweli zipo juu sana, zinafikia mpaka 30%. Ni watu wachache sana watakaoweza kufanya biashara na kupata faida.

Mikopo mingi hairejesheki, sijui ni kwa namna gani wataalam wa uchumi watasaidia katika hili,, ila maendeleo yatakua magumu kufikika kwa mwananchi wa kawaida, kama mwananchi huyo atakua hana uwezo wa kukopa na kufanya shughuli za maendeleo.

Wengi wa wakopaji unakuta dhamana zao zinaishia kutumika ili kurealize madeni yao kwa mabenki.

Magufuli ana mtihani mwingine kuhakikisha kweli hili linafanyiwa kazi maana ni jipu.
Tusilaumu mabenki tu bila kuangalia vigezo vinavyotumika kupanga riba.
Kigezo kikubwa ni gharama ya fedha i.e cost of fund.
Benki zinakopesha kutoka kwenye amana za wateja, lkn tz pesa zinazunguka nje ya mfumo wa fedha. Wenye bank accounts ni 15% ya wenye uwezo wa kuwa na akaunti. Kuzitoa fedha katika mfumo usio rasmi ni kazi na gharama kubwa.

Pili, Watz hawatambuliki kirahisi. Hatuna vitambulisho ambavyo ni tracable. Wafanyakazi wanakopeshwa kwa riba nafuu zaidi na bila dhamana kwa sababu ni tracable. Ukimkopesha mfanyabiashara ndogo manzese, unamtrace vp?. Hivyo riba lazma iwe kubwa kufidia risk hiyo kwani uwezekano wa kutompata baada ya kuchua pesa ni mkubwa.
 
Ni kweli kabisa lakini hatuna ujanja maana kupata mtaji kwa kilimo ni ngumu sana,duh nilikopa ACCESS Bank hadi namaliza mkopo nikiwa naongea peke yangu barabarani bora NMB na CRDB
Pole mkuu, suala la mikopo ya mabenki kwa nchi hii ni pasua kichwa, umakini mkubwa sana unatakiwa unaposogelea mikopo ya mabenki haya
 
Hahaha bora crdb wanakula nawewe kwenye mshahara angalau stress zinapungua kidogo ingawa hela za mkopo ni kama zina mashetani. Ili uzifanyie kazi vizuri inabidi ushetani wako uwe zaidi.
ahahahaaaa . . . . . . kweli apa unahitaji kuwa na ujanja hata zaidi ya ushetani huo maana duuh . . . .
 
Kuna siku nilimpa faka afisa mikopo wao baada ya kuanza kunipigia nikiwa kwenye sherehe nikamuuliza mbona siku mliyoniwekea mkopo uliingia saa 12jioni je muda huo nilizitoa na kuanza biashara. Mbona nyie siku moja tu mnachonga sana!! Aisee hadi alikata simu
ahahahahaaaa . . . .
 
Kwa wale ambao wanahitaji mikopo au wanaofanya shughuli zao kwa kutegemea facilities za Mabenki kwa kweli hili jipu linahitajika kuangaliwa upya.

Kwa hapa nchini ukiangalia Prime Lending Rates kwa kweli zipo juu sana, zinafikia mpaka 30%. Ni watu wachache sana watakaoweza kufanya biashara na kupata faida.

Mikopo mingi hairejesheki, sijui ni kwa namna gani wataalam wa uchumi watasaidia katika hili,, ila maendeleo yatakua magumu kufikika kwa mwananchi wa kawaida, kama mwananchi huyo atakua hana uwezo wa kukopa na kufanya shughuli za maendeleo.

Wengi wa wakopaji unakuta dhamana zao zinaishia kutumika ili kurealize madeni yao kwa mabenki.

Magufuli ana mtihani mwingine kuhakikisha kweli hili linafanyiwa kazi maana ni jipu.

When stroke talk sense, congratulation! Is anything improved since then Mh alipokabidhiwa nchi?!

Tupe Darasa la mikopo niyaje?
 
Nadhan ni uelewa mdogo wa wakopaji wengi... Angalieni benki za riba ndogo

Mbali ya kuangalia benki za riba kwa maana ya kufanya research kabla ya kukopa ni vizuri pia kujua/kupata maelezo kama:-

- Aina ya formula/ukokotozi wa marejesho ya mkopo (Reducing balance au Flat rate/Straitening balance method)
- Gharama nyinginezo zinazoendana na mkopo (Processing Fees / Insurance e.t.c)
- Kipindi cha mkopo/marejesho (Ni vizuri pale inapowezekana kipindi cha marejesho kiwe kifupi)
 
juzijuzi BOT wamepunguza riba kwa mabenki kwa sasa wanatakiwa riba kwa mteja lakini wao wanadai wanaenda kwa hatua ni benki moja tu ABC Bank ambayo imeshusha riba hadi asilimia 11% lakini nyingine bado zinakataa kushusha ndio maana nilifurahi serikali ilipochukua pesa zake kwenye mabenki na kurudisha bot angalau kiburi kitapungua
 
Tusilaumu mabenki tu bila kuangalia vigezo vinavyotumika kupanga riba.
Kigezo kikubwa ni gharama ya fedha i.e cost of fund.
Benki zinakopesha kutoka kwenye amana za wateja, lkn tz pesa zinazunguka nje ya mfumo wa fedha. Wenye bank accounts ni 15% ya wenye uwezo wa kuwa na akaunti. Kuzitoa fedha katika mfumo usio rasmi ni kazi na gharama kubwa.

Pili, Watz hawatambuliki kirahisi. Hatuna vitambulisho ambavyo ni tracable. Wafanyakazi wanakopeshwa kwa riba nafuu zaidi na bila dhamana kwa sababu ni tracable. Ukimkopesha mfanyabiashara ndogo manzese, unamtrace vp?. Hivyo riba lazma iwe kubwa kufidia risk hiyo kwani uwezekano wa kutompata baada ya kuchua pesa ni mkubwa.
bank haikupi mkopo hadi uwe imesecure huo mkopo acha kudanganya watu watumishi wa umma mikopo yao ni non secured
 
Kuna hiyo BancABC ni jipu kubwa. kuna mtumishi mwenzangu amekopa huko ni mwezi na nusu sasa hajapata huo mkopo na wameshaanza kumkata. Amefuatulia tawi la kariakoo hadi kwa meneja lkn hakuna jibu analopewa zaidi ya kuambiwa subiri tunaingiza sasa hv akicheki salio hamna kitu. Halafu riba wanadai ni 19% lakini uki calculate unakuta ni zaidi ya hiyo kuna ujanja unafanyika. Tuweni makini na haya mabenki.
 
Bongo hakuna Bank ya Riba ndogo zote mateso tu
Mi naona BancAbc wamezidi ni wababaishaji mno na Riba ni kubwa ajabu. wanakudanganya ni 19% ila uki calculate inazidi nadhaji ni 25% .Simshauri mtu kukopa huko aisee
 
Kwa mda gani
Abc Bank haifai ni kilio cha wengi.nina ushahidi kabisa mimi mwenyewe niliwahi kopa milioni tatu nimelipa milioni nne na laki nane kwa miaka miwili. Bado huyo mwenzangu anekopa ni mwezi na nusu sasa hela hajapewa na ameshaanza kukatwa riba. Abc Bank hawafai.
 
Kwa wale ambao wanahitaji mikopo au wanaofanya shughuli zao kwa kutegemea facilities za Mabenki kwa kweli hili jipu linahitajika kuangaliwa upya.

Kwa hapa nchini ukiangalia Prime Lending Rates kwa kweli zipo juu sana, zinafikia mpaka 30%. Ni watu wachache sana watakaoweza kufanya biashara na kupata faida.

Mikopo mingi hairejesheki, sijui ni kwa namna gani wataalam wa uchumi watasaidia katika hili,, ila maendeleo yatakua magumu kufikika kwa mwananchi wa kawaida, kama mwananchi huyo atakua hana uwezo wa kukopa na kufanya shughuli za maendeleo.

Wengi wa wakopaji unakuta dhamana zao zinaishia kutumika ili kurealize madeni yao kwa mabenki.

Magufuli ana mtihani mwingine kuhakikisha kweli hili linafanyiwa kazi maana ni jipu.
Heritage financing company limited ya haha Arusha riba ni 60%
 
Abc Bank haifai ni kilio cha wengi.nina ushahidi kabisa mimi mwenyewe niliwahi kopa milioni tatu nimelipa milioni nne na laki nane kwa miaka miwili. Bado huyo mwenzangu anekopa ni mwezi na nusu sasa hela hajapewa na ameshaanza kukatwa riba. Abc Bank hawafai.
ABC Bank riba ni 26%
 
Back
Top Bottom